Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Kuna siku zimepita kidogo, nilipatwa na ghathabu na sikuchangia kwa adabu, Yaliyotokea nilisikia aibu sana. Mchangiaji mmoja aka nikanya kwa kuniambia wazi Mzee wa Mmbaga hapa unapitiliza na napeleka salamu hizi Mvaa. Nakajua anafahamu anapotoka Baba yangu na mama yangu. NILISIKIA AIBU SANA. Ni kujitafakari yuu.
Barikiwa sana sana, nimekuelewa ndugu yangu
 
Chadema, we are tired of your bulshit. If you can't call for mass action, then trust me we are trashing your membership cards. We are fed up
 
Matusi ya nini sasa jamani?
povu la nn sasa, kwa we mwenyewe sio sperms? Laiti baba yako angejua siku ya kuingiza mimba yako ungezaliwa mtoto mwenye mitusi namna hii bora angepiga nyeto amwage chooni tu.
 
Nianze Kwanza kwa Kutoa Pole zangu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe, Familia yake, Wapiga Kura wake, Wanachama wake wa CHADEMA, Wanasiasa mbalimbali, Wabunge na Sisi Watanzania wa kawaida tusioegemea upande wowote ule (Mzukulu) nikiwemo kwa kilichotokea. Naamini Mwenyezi Mungu ataupigania Uhai wake ila kwa waliohusika Maulana / Mola atawajibu kwa Adhabu Kali kabisa.

Jana nilipoziona tu zile Nondo Kali na zenye Mashiko za Mheshimiwa Tundu Lissu nilihisi kabisa kuwa ili kuwapoteza Watu na Kuyahamisha Mawazo yao katika Kukijadili au Kuyajadili yale aliyoyaandika ambayo yote ni mazuri basi ni lazima tu Spinning ya Hatari ingefanyika. Kilichofanyika ni kutaka Kufunika alichokifanya Lissu jana kuanzia leo Watanzania wote tujikite zaidi katika Kuzungumzia hili lililomkuta Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Na Kiutaalam zaidi ili kuonyesha kuwa hawa Wahuni wanaolelewa vibaya na walijipanga ni kwamba itakuwa walijipanga tokea pale Taarifa za Mheshimiwa Tundu Lissu aliposema kuwa atazungumza na Watanzania hivyo hata Wao walishajipanga na walipoona Jana Mheshimiwa Tundu Lissu katoa Nondo ile Kabambe basi na Wao wakaamua Kulitekeleza hilo walilolitekeleza.

Kuna Mmoja namuheshimu sana humu ila sasa nitaanza Kumdharau amesema kuwa Mheshimiwa Mbowe Kavamiwa na Majambazi akiwa na Kimada aliyemnunua. Ameshindwa kujua ya kwamba Siku zote Mbinu za Kijasusi huwa zinaratibiwa vyema na Kimkakati zaidi kwa kuwahusisha Magenge ya Wahuni ili hata likija Kufanikiwa basi hao Majasusi wasijulikane moja kwa moja kama ni Wao.

Kwa hali ilivyo na kwa uelewa wangu mdogo sana wa Masuala ya Usalama ( Ujasusi ) ila wale wanaojua zaidi yangu hapa JF watanisaidia ni kwamba kwa Nyakati tuliopo na kwa Hofu ya Wapinzani na Agenda zao, na kwa Uchungu wa Kulikosa Jimbo la Hai ambalo wanalitaka na kwa kutaka Kuleta Hofu na Vitisho nitakuwa wa mwisho Kuamini kama katika hili Tukio la Mbowe hayo Mapanga hayakuwa na Sumu za Kijasusi.

Namalizia tu kwa kusema kama Tanzania ya sasa imefikia hapa ambapo Wanasiasa wanafanyiwa mambo haya mabaya halafu nchi ina Kiongozi Mkuu na ina Idara yake ya Usalama na mambo (matukio) haya yanatokea kila Kukicha ila wanayanyamazia basi huenda kwa Mwaka huu Tanzania ikawa na Vifo vingi vya Wanasiasa (hasa wa Upinzani) na Wanaharakati kuliko wale ambao labda CORONA ingewauwa au imewauwa.

Nawaombea LAANA mbaya sana na Kali mno kwa Mwenyezi Mungu hawa Wote wanaoyafanya haya na hasa huyo Mkubwa wao anayewatuma.
 
Kwani amewaumiza wangapi ndani ya Chama?
Naunga Mkono hoja, ni wakati wake sasa kulipa.
Unalala na wake za watu, kila girlfriend wa mwenzio unamtamani, hutaki mtu akuguse.
Anawaonngoza viongozi wenzake kama watoto wa shule. Anawafukuza kwenye chama kihuni. Anatumia pesa ya chama apendavyo. Je, hajajenga uadui wa kutosha dhidi yake? Na bado anatetewa? Je, hao wanao mtetea wakiitwa "wapumbavu na malofa" nao watakasirika!
 


View attachment 1472626
View attachment 1472650

Salaam,

Taarifa nilizozipata hivi punde toka chanzo changu kinanihabarisha kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman A. Mbowe amevamiwa na kikundi cha watu wasiojulikana akielekea nyumbani kwake usiku huu na kupigwa na wamemuumiza.

Tukio hili limetokea majira ya saa 6-7 usiku.

Mhe. Mbowe amekimbizwa Hospitali ya Ntyuka iliyopo jijini Dodoma.

Kamanda Muroto amesema wamepata taarifa kuwa kavunjwa mguu wa kulia na amelazwa Wodi namba 4 hospitalini hapo. Amesema taarifa zaidi zitafuata

UPDATES
FREEMAN MBOWE AHAMISHIWA DAR KUTOKEA DODOMA


Kiongozi huyo wa Kambi rasmi ya Upinzani, ametolewa katika hospitali ya DCMC jijini Dodoma na kusafirishwa kwenda jijini Dar kwa matibabu zaidi

Mnadhimu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, Esther Bulaya amesema wataeleza baadaye ni hospitali gani anakwenda kutibiwa Mbowe, akifika jijini Dar

Daktari anayemtibu amesema hali ya Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai inaendela vizuri ila ni maumivu bado yupo nayo kutokana na kuvunjika kwa mfupa wa mguu wa kulia


MAONI YANGU:
Mhe. Mbowe kuvamiwa na kupigwa eneo la Area D, jijini Dodoma, Mtaa wa Sengia; linalotajwa kuwa na ulinzi wa kutosha, kama ilivyotokea kwa Lissu kunaacha maswali mengi, je, hili linaweza kuwa limechochewa na Lissu kutangaza nia ya kugombea Urais wa JMT October 2020? Ni hasira au kitu gani? No one knows.

Bado najiuliza; hivi kama Taifa kwa tabia hizi za kihuni tunaelekea wapi? Hawa wanaojichukulia sheria mikononi kila siku wanafanya hivyo kwa kutumwa na nani? Matendo haya yataendelea kwa viongozi wa upinzani mpaka lini?

We need to wake up, better late than never.

Get well soon Mh Mbowe,hawa wamepagawa na wapo stressed and they are obsessed.Hawa wasiojulikana ni kina nani hasa hapa nchini?Hawa wanaowatuma wanaamini kwa mbinu kama hizi wanadhani ndiyo watapendwa na Wananchi?Kwa nini wanaendelea kutokujulina?Uimara wa vyombo vyetu vya ulinzi upo kwa kiwango gani?
Hivi kama viongozi wanashambuliwa katika maeneo rasmi yenye uangalizi/ulinzi 24/7 nani yupo salama nchi hii?Je,ni rahisi kiasi gani kumvamia Mbowe ambaye ni KUB,anatembea kwa gari muda mwingi inakuwaje kuvamiwa na vibaka?Alitekwa?Mambo ni mengi ila muda in finyu.
 
Kwa mara nyingine tena, wale wale wanaohubiri amani, umoja na ushirikiano ndio hao hao wanaoongoza kwa maneno ya kejeli, dhihaka na dharau dhidi ya Mbowe. Niwakumbushe tu Mbowe ana familia, ana ndugu, ana wafuasi na kiongozi. Mbowe si mhalifu, Mbowe si jambazi, kumsemea maneno ya kejeli na dhihaka hivi sidhani kama ni sahihi.

Tanzania si mali ya CCM wala ya mtu binafsi, nashindwa kuelewa kama tukio hili lingetokea upande wa CCM na Pro Chadema wakasema chochote kile, wangejitokeza watu hapa na kudai kuwa Mwenyekiti anadharauliw ana blah blahblah kibao.

Niwashauri tu, kwa kile ambacho hamko tayari kufanyiwa basi msiwafanyie wenzenu, muda ni mwamuzi mwaminifu asiye na upendeleo.
Binafsi nachukia mtu kama wewe kufanya CCM jalala la takataka za CHADEMA. Kutokaa naxmatukio ya kunyanyasana CHADEMA, hakuna shaka kuna migogoro ya ndani kwa ndani ya chama ambayo ninyi hamko jasiri kuizungumzia mkapata suluhisho la kudumu.

Nawahakikiushia umakini wa Serikali iliyoko madarakani, shambulio dhidi ya Mbowe, litaweka hadharani uchafu na uozo uliyoko CHADEMA, once and for all, ili viongozi na wafuasi wao wasiendelee kuumwaga CCM. Hakuna jiwe litaachwa kufunuliwa.
 
Sitajali nani amesema nini kwenye uzi huu, nitatoa mchango wangu Kwa uelewa wangu na utashi wangu. Mtoa Uzi/taarifa alianza vizuri Sana Kwa maana ya kutupasha habari isipokua akachagua upande kwenye ubeti wa tatu (3).

Kama ni kweli mtu huyo kashambuliwa, kwa sababu zozote, siungi mkono jambo hilo ns pia siungi mkono endapo jambo hili ni la "kupika"

'Ambele Daniel Mwasuka'
Eeenh, "---jambo hili ni la 'kupika'".

Great Thinkers of JF, mbele kwa mbele!
 
Nionyeshe au nitajie popote pale mwana chadema yoyote yule aliyetukana, nipe mfano wowote ule. Ndugu Tanzania ni yetu sote, siasa za kishenzi namna hii hazijengi, tukosoane kwa heshima. Wote tuna maumivu sawa, leo hii Mbowe yuko kitandani, wewe inakusaidia nini? inakuongezea nini? Tukeindelea kushabikia huu ushenzi watoto wetu na ndugu zetu watarithi nini? Chuki? CCM, CCM, CCM MUNGU anawaona.

Tayari wewe mwenyewe umeonesha ushabiki na chuki dhahiri pale unaposema CCM, CCM, CCM MUNGU anawaona
 
Dodoma sio salama tena, Mji mdogo mambo mengi.
Itakuwaje salama wakati inasadikika wahusika ni wakutumwa na waliostahili kuwalinda wahanga?Usalama wa miji yetu ni mdogo na hatuna vyombo imara vya ulinzi.
Kila kitu ni siasa hadi inakera.Hebu tubadili utawala tuone wengine watakavyokabiliana na hizi changamoto.
Dodoma hapo hapo kina kiongozi alishambuliwa mchana na bado leo wahalifu wanaitwa wasiojulikana.Vyombo vyetu vya uchunguzi ni efficient? Hata hili kabla ya uchunguzi unaambiwa ni vibaka,wahuni, na hakuna LA maana.Vibaka wa Dodoma?
 
Unajua watanzania tunasahau kirahisi sana. Kumbukeni ule ujumbe wa Gwajima kwa wana-ukoo wake kuhusu kumlinda rais kwa hali na mali mtaelewa nini kinaendelea. Nchi imeharibiwa sana na hawa watu...
Inawezekana ukawa umeweka kidole penye tatizo mkuu 'fazili'; ila sikumbuki alichowambia Gwajima wanajamii wake ni nini ..., unaweza kudokeza kidogo hapa nasi tujue?
 
Unajua watanzania tunasahau kirahisi sana. Kumbukeni ule ujumbe wa Gwajima kwa wana-ukoo wake kuhusu kumlinda rais kwa hali na mali mtaelewa nini kinaendelea. Nchi imeharibiwa sana na hawa watu...
Ndio maana chdm wanamhusish nabii mashimo
 
Unajua watanzania tunasahau kirahisi sana. Kumbukeni ule ujumbe wa Gwajima kwa wana-ukoo wake kuhusu kumlinda rais kwa hali na mali mtaelewa nini kinaendelea. Nchi imeharibiwa sana na hawa watu...
Umemsikia Lijua likali wewe! Kumbe Hasira zetu tumezijenga kwenye vitu vya uongo buana! Eti ni pombe na badala ya kusema ni pombe, inasingiziwa sirikali

Sijui ni kweli, mi simo
 
Acha ujinga wako, toa mifano, pia nimekuuliza, kwahio kwakua walifanya hvyo (ambayo najua ni uongo pia) na wewe ndio ufanye hivyo? Ndio akili zenu zinawatuma hivyo?
Wewe na wenye mawazo kama yako humu JF hamjui kinachozungumzwa, kupangwa na kutekelezwa na Kamati ya Kamati Kuu ya CHADEMA.

Kutenda kosa siyo kosa lakini kurudia kosa ni kosa, wahenga walinena. Makosa ndani ya CHADEMA yamekuwa mengi (Chacha Wangwe, Ben Saanane, Lissu) kiasi cha kujiuliza kulikoni. Sasa kaguswa Mbowe, M/Kiti na KUB, ambaye ana ulinzi saa 24, hata akiwa anatoa hotuba sehemu yoyote, ni dhahiri kosa hili alisameheki tena. Ukweli zamu hii utafichuliwa.
 
Yaani kama ndio siasa hizi, hii chuki inayopandikizwa itatughalimu siku moja.
Hiyo chuki ni tafsiri yako, wa Tz wengi wapo busy na maisha yao na wana siasa wapo busy na Maisha yao, in fact unaweza kukuta hili tukio likawa exit plan ya victim , kisingizio kapigwa wakati kesha vuna vyakutosha
 
Wewe na wenye mawazo kama yako humu JF hamjui kinachozungumzwa, kupangwa na kutekelezwa na Kamati ya Kamati Kuu ya CHADEMA.

Kutenda kosa siyo kosa lakini kurudia kosa ni kosa, wahenga walinena. Makosa ndani ya CHADEMA yamekuwa mengi (Chacha Wangwe, Ben Saanane, Lissu) kiasi cha kujiuliza kulikoni. Sasa kaguswa Mbowe, M/Kiti na KUB, ambaye ana ulinzi saa 24, hata akiwa anatoa hotuba sehemu yoyote, ni dhahiri kosa hili alisameheki tena. Ukweli zamu hii utafichuliwa.
Wewe unayekijua kiseme! Poor you! Acheni ramli chonganishi, na ya kwenu yanajulikaña pia
 
Moods wameondoa post yangu ambayo ilielezea kile ambacho Lijualikali amekisema bungeni muda mfupi uliopita ambacho kwa mtazamo wangu kingewarahisishia Polisi katika uchaguzi wao

Lijualikali anasema Mbowe ameanguka sababu ya ulevi

Anadai maelezo ya Msigwa kwamba walikuwa ote hadi saa moja jioni kisha wakaachana inathibitisha kwamba walienda kulewa

Amepigiwa makofi mengi na wabunge ila picha ya Waziri Mkuu ambayo Star Tv wamezoom akisikiliza ni "kama" moyoni alikuwa anasikitika maneno yanayomtoka Lijualikali

Baada ya kumaliza, Spika amesimama nakutoa kauli tata kwamba ndiomaana hawataki kusema

Spika amesema hata wao wanajiuliza kwanini Mbowe alipelekwa kituo cha Afya cha binafsi badala ya hospital?

Binafsi sijui Lijualikali anauhakika gani na maneno aliyoyasema ila kam Taifa bado tunasafari ndefu hasa kwa huu ulevi wa siasa wa kutojua useme nini na wakati gani

Nadhani Polisi sasa kazi yao itakamilika leo jioni, hata kama ameongelea Bungeni mi naona kistaarabu tu akahojiwe athibishe kauli yake la sivyo aombe radhi maana kipimo cha ulevi sidhani Kama alikuwa nacho kumpima
 
Back
Top Bottom