DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

Bado tu tunaendelea kujadili habari ya kajibwa ka kizungu TL? Jamani hebu tuje na plan za maendeleo 2019
Maendeleo ya kupanga kuwaua wenzako siyo maendeleo, maendeleo halisi hayajengwe kwenye misingi ya kumwaga damu.
 
JPM mtuhumiwa namba moja!!, Bado unatarajia uchunguzi kweli???
 
Wanafahamika, wanafahamika sana! Wasiojulikana sasa wanajulikana. Ethiopia is putting to task former secutity boses for the atrocities commited in the past regime!
Ethiopia PM: Security agencies committed 'terrorist acts'
Abiy Ahmed said security institutions tortured citizens in order for government to remain in power.
 
Kile kitendo kilikuwa kimesukwa kimepangwa na watu wa wazito na wenye mamlaka.

Shambulio lenyewe lilikuwa ni shabuliizi la karibu huku wakijua hata marehemu LISSU akiwajua sura zao haidhuru atakuwa marehemu asiweza kuongea.

Kwa bahati nzuri na matakwa ya mungu hawakufanikiwa,na yote waliokua wakisema wakati wa shambulizi hilo la kinyama na baada ya shambulizi Lissu na mwenzake waliyasikia

Hii issue ni kama ya Jamal Kashogi lazima Imuondoe magufuli na serikali yake madarakani
 
Heri umununue MTU kama ana kukera, mkaribishe mezani mpe teuzi,kuliko kumuuwa huo ni msalaba unao hadi utakapoondoka duniani pia ni laana ya kukwamisha kila ufanyalo,pia roho ya marehemu huwa haiondoki duniani hadi ilipe kisasi kwa wahusika wote,ndo uondoka duniani.
 
Sitakufa Bali nitaishi, ni maneno ya kiimani yanayoonyesha kwamba Mwenyenzi Mungu haziakiwi na Wala hakuna mwanadamu anayebaki salama baada ya kumwaga damu. Kama ulikuwa kiongozi wa juu lazima watakushusha na kila utakapotazama jamii utahisi Kama wamaelewa dhambi uliyoitenda.

Hata ungekuwa na Mali nyingi kiasi gani au cheo kikubwa kiasi gani bado kila kuitwapo Leo damu ya mwanadamu Italia juu yako.

Kwa waajiriwa yaani waliotumwa kuua ndo mwisho wa mafanikio yako, utabaki kuwa mlevi, mvutaji na mzinifu kuitafuta amani lakini kila utakapotulia mwenyewe na kuona picha ya ulipanga kumua lazima dishi licheze tu.

Naandika haya kuwakumbusha waliompiga Lisu Risasi na waliopanga na kuelekeza apigwe Risasi popote mlipo hayo maumivu na mikosi mnayopitia usiku na mchana ni kwa sababu ya damu isiyo na hatia mliyomwaga na milele damu hiyo itaambatana nanyi pamoja na vizazi vyenu.

Tundu Lisu kama kiumbe unayestahiki kuishi nakutakia afya njema na usisite kuomba na kumwachia Mungu.

Visasi si juu yetu bali ni juu ya mtoa pumzi.....uliumizwa Dodoma ila tambua waliokuumiza watateseka milele wawapo Dodoma au nje Dodoma.
 
Nakubaliana na wewe. Sema tatizo Mungu hafanyi kazi kwa formula zetu sisi binadam, hebu fikiria Idd Amini, Mobutu Seseko etc walivyokuja kufa vifo bila mateso yoyote ukilinganisha na waliyoyafanya ktk tawala zao.

Pia Mzee wetu wa Zimbabwe check anavyomalizia pension pamoja na aliyomfanyia Morgan Tchagarai!!. World's not fair na haitakuja kuwa.
 
Na iwe,watesi wa lissu waendelee kuteseka,wapate magonjwa makubwa makubwa yasiyoambukiza.....hasa cancer
 
Mungu hayupo, ni hadithi tu imetungwa.

Ukielewa hilo, hayo mengine huwezi kushangaa.
 
Tundu Lisu kama kiumbe unayestahiki kuishi nakutakia afya njema na usisite kuomba na kumwachia Mungu.

Jambo linalowaumiza mno ni kumwona Mh Tundu Lissu akitabasamu.

Hakuna adhabu kubwa kuliko hiyo kwa mtu aliyetaka kumwondoa Lissu ambaye licha ya maumivu ya kimwili, anaonekana kama tukio liliompata haikuwa kitu chochote kwake.

Ingesaidia kidogo, pamoja na kunusurika kwake, kama angeonekana mtu mwenye hasira, mwenye tabia iliyobadilika na kuwa mtu mwenye malalamiko na mengine mengi ya kuwaonyesha watesi kuwa angalao waliambulia kupata hali hizo mbaya kwa mtu waliyetaka kumwondoa uhai.

Badala yake imekuwa kama ni kinyume cha waliyoyatarajia. Lazima hali hii itakuwa inawatesa, inawaumiza sana fikra zao.
 
Mbona husemi walioua askari wetu wanane nk.huko kibiti au wale hawakustahili kuishi mheshimiwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…