Sina hakika if this is coicindence ama vipi.....
Ikulu kulikuwa na usanii uleule tuliouzoea kila wakati wa serikali hii wa kupokea wanachokiita taarifa za uchunguzi wa wizi wa madini ya almasi na tanzanite toka kwa wawekezaji ambao walisainishwa mikataba na hawahawa CCM wanaojifanya kulia lia leo .....
At the same time mtu ambaye ni kama ndiye kama kiongozi wetu ktk kutuamusha na kutushtua kuwa tunaendelea kufanyiwa usanii Tundu Lissu, anapigwa risasi ktk jaribio la kutaka kumuua.....!!!
Wamejaribu kumpakazia kila aina ya vijikesi vya kijinga jinga ili wamfunge jela kama njia ya kumnyamazisha, wameshindwa. Sasa the best option walioona inafaa kuendelea kuficha madhambi yao ni kumuua kabisa huyu ndugu yetu....!!
Kwa namna yoyote hili halikubaliki na tunalilaani tukio hili la kijinga kwa nguvu zoote....
Tushindaneni kwa nguvu za hoja na si kuanza kutoana uhai...
Hili kwa kweli ni hapana, halikubaliki hata Kidogo!!!
Tundu Lissu, kamanda wetu, Mungu wa mbinguni muumba wa mbingu na nchi akusaidie na kukuokoa kutoka ktk mauti ya kutengenezwa na wakola hawa....!!!
Utapona kamanda na mapambano yataendelea hadi wakoloni hawa weusi chini ya Chama Cha Makinikia - CCM watakaponyoosha mikono yao juu ku - surrender...!!