Mara nyingi huwa tunaangalia matokeo ya vitu ba kuacha kuangalia mizizi.
Kabla ya kufika kwa aliyepiga risasi, rais wa Tanzania kwa kauli zake mbovu za kuhalalisha wapinzani waandamwe, amechangia kuwepo kwa hali hii.
Kabla ya rais kuwa rais, chama tawala kilichomuwezesha huyu rais kuwa rais, kimetuangusha.
Wazee wa Chama tawala waliompendekeza huyu rais kuwa rais wametuangusha.
Wapiga kura waliotupa huyu bungeni wametuangusha.
Marais waliomteua ubunge wametuangusha.
Bunge lenyewe ambalo amekaa bungeni miaka yote bila kujifunza mengi, limetuangusha.
Vyuo vya elimu ya juu na shule za elimu ya awali vimetuangusha.
Kanisa lililomlea limetuangusha.
Familia iliyomlea imetuangusha.
Jamii nzima ya Tanzania iliyoshiriki kutufikisha hapa imetuangusha.