Dodoma: Waziri Mkuu aagiza Mwanajeshi, maarufu kama HK akamatwe kwa udhalilishaji

Dodoma: Waziri Mkuu aagiza Mwanajeshi, maarufu kama HK akamatwe kwa udhalilishaji

katafute state ya kwako. wananchi kutoa malalamiko yao kwa viongozi wao wa kitaifa ni jambo la kawaida halijaanza leo wala jana lilikuwepo na litaendelea. we ndio failing person. Ktu kidogo tu mtu anakimbilia kuisema vibaya serikali. we ndio umefeli umejaa frustrations.

Wewe unayetetea habari za wananchi kutoa malalamiko yao ya kuibiana simu na TV, kupigana, kwa viongozi wa taifa hujui hata hesabu kuna wananchi wangapi, malalamiko mangapi kama hayo, na viongozi wa kitaifa wangapi. Utakubali mpaka kesi ya mtu kuibiwa kuku imsubiri rais na waziri mkuu, wakati kuna polisi na mahakama.

Halafu huelewi kwamba, jambo kuwa la kawaida haimaanishi ni zuri. Jambo linaweza kuwa ni baya na la kawaida, watu wamelizoea. Kulizoea hakufanyi lisiwe baya.

Serikali itasemwa vibaya tu, hiyo ni haki ya watu ya kikatiba. Ukinilalamikia kwa kuisema serikali vibaya, unanionesha huna elimu ya uraia na hujui haki za kikatiba ni zipi.

Zaidi, umeshindwa kujibu hoja, unanishambulia mimi mtoa hoja kwa ad hominem attacks, hii ni ishara ya mtu asiye na hoja.
 
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana alipokuwa akizungumza na wananchi wa Nzuguni katika maadhimisho ya miradi iliyozinduliwa katika kilele cha sherehe za miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kikiwamo kituo cha Zimamoto na Uokoaji.

Kijana huyo alitoa tuhuma hizo, baada ya Waziri Mkuu kutoa nafasi kwa wananchi kuzungumza kero zinazowakabili ili waweze kupata msaada.

Alipopata nafasi hiyo, alidai mwanajeshi huyo aliyemtaja kwa jina maarufu la HK, kunyanyasa vijana wa eneo hilo na yeye akiwamo kwa kuchukuliwa TV yake kwa madai kuwa kuna mtu amemuambia kuwa amemuona na simu ya mke wake.

“Alikuja nyumbani kupekua vitu vya nyumbani kwangu zikiwamo nguo za ndani za mke wangu kwa kuziinua huku akizinyanyapaa, alipokosa simu aliamua kubeba TV na kuondoka nayo na jana amenipigia simu kuniambia kuwa kero yangu hata nikipeleka kwa Rais Samia haitatatulika…naomba Waziri Mkuu nisaidiwe afuatiliwe,” alilalamika.

Waziri Mkuu alimuagiza Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Martin Otieno, kumsaidia kijana huyo na kumtafuta mwanajeshi huyo ili akamatwe.

“Pia nitazungumza na CDF (Mkuu wa Majeshi) kama anavyoeleza kijana huyu kama ndivyo kamanda yeyote wa jeshi lolote hapaswi kuwafanya hivyo Watanzania, jeshi lipo kwa ajili ya kuwalinda wao, maisha yao, vifaa vyao na mali zao zinakuwa salama sio kwenda kuchukua mali zao,” alionya.

“Huyo kijana apatikane na kama atakataa tutapata taarifa zake kwenye kikosi alipo na tutamtafuta CDF atatupa mawasiliano ili tujue kwanini amechukua TV ya huyu kijana. Huyu kijana apewe ushirikiano anaweza kupata matatizo na huyo kamanda akisikia ametamkwa hadharani, huyu kijana alindwe asipate madhara.”

Alisema taarifa ya kijana hiyo ichukuliwe kama taarifa kamili na ifanyiwe kazi ili apate haki yake ya msingi.

Chanzo: Nipashe
“Alikuja nyumbani kupekua vitu vya nyumbani kwangu zikiwamo nguo za ndani za mke wangu kwa kuziinua huku akizinyanyapaa,

[emoji1787]
 
Hii habari ni ishara ya a failing state.

Ukishaona kiongozi wa kitaifa anaingilia kazi za polisi na mahakama, kesi za nani kaiba simu na TV ya nani, huyu kampiga yule, ujue this is a failing state. Maybe not quite a failed state, but a failing state.

Yani hata huyo Waziri Mkuu hajui kazi yake ni nini.
Kaletewa malaliko tena wazi ulitaka afanyeje? polisi kumkamata mjeda ni ngumu sana
 
Kaletewa malaliko tena wazi ulitaka afanyeje? polisi kumkamata mjeda ni ngumu sana
Mpaka Waziri Mkuu kuletewa malalamiko haya ndiyo tayari nchi ishakuwa failing state, kwa sababu kuna ngazi kibao chini yake zinaonekana zimeshindwa kushughuikia hili.

Sasa mnapoangalia hili kwa sababu limeletwa kwa Waziri Mkuu na limepata coverage, mnashindwa kujiuliza haya yapo mangapi kila siku ambayo hayamfikii Waziri Mkuu kwa sababu tunaye mmoja tu na kesi kama hizi zipo maelfu na maelfu?

Tunakuwaje nchi ya kutegemea Waziri Mkuu atatue kesi za polisi, jeshi na mahakama?
 
Hii habari ni ishara ya a failing state.

Ukishaona kiongozi wa kitaifa anaingilia kazi za polisi na mahakama, kesi za nani kaiba simu na TV ya nani, huyu kampiga yule, ujue this is a failing state. Maybe not quite a failed state, but a failing state.

Yani hata huyo Waziri Mkuu hajui kazi yake ni nini.
Hakika, ila vilaza wanashangilia sana hili kila kona ya nchi!
 
katafute state ya kwako. wananchi kutoa malalamiko yao kwa viongozi wao wa kitaifa ni jambo la kawaida halijaanza leo wala jana lilikuwepo na litaendelea. we ndio failing person. Ktu kidogo tu mtu anakimbilia kuisema vibaya serikali. we ndio umefeli umejaa frustrations.
Unaelewa wakuu wa mikoa, wilaya, mtendaji wa kata na mwenyekiti wa kijiji/mtaa wamewekwa kwa sababu zipi??
 
We wanajeshi unawajua vizuli?
Nikisema nawajua au siwajui itakusaidia nini?

Mimi siongozwi na mhemko na chuki dhidi ya kundi fulani katika jamii.

Ila jua tuhuma ni tuhuma tu kama hakuna ushahidi usio na shaka, tukiruhusu hili ni hatari kwa mustakabari wa Taifa letu.

Kesho wewe 25000q utasema IFAC kisa Mhasibu wa Shirika X kaja kunivamia nyumbani kwangu na kubagua kuku wangu.
Ndio itoke hukumu tu? Kisa mnyonge 25000q kasema kwa kiongozi Fulani wa kisiasa?
Ndio nchi inavyopaswa kuendeshwa?
Ndio huo utawala wa kisheria inavyopaswa kuwa?
 
Uanajeshi wa kizamani na kutaka madeal na maraia ndio inkuwaga hivi .

USSR
Jambo usilo lijua ni sawa na usiku wa kiza, usije toa hukumu kwa kusikiliza upande mmoja.
Nasakia KIUHALISIA mambo hayako hivyo kama alivyo sema. Kama ni kweli utaona kwenye TV na mitandaoni kesi ikiendelea.
Hata kama una watoto hapo kwako au ndugu wapo chini yako usije jaribu tena narudia usije jaribu kutoa huku kwa kusikiliza upande mmoja tu.
 
Makosa yanarudiwa tena hivi kweli kero zote zinapelekwa Kwa MH.PM !! Inamaana Ngazi zote hazina uwezo wa kutatua tatizo hilo!!? Twafwaaa
 
Hii habari ni ishara ya a failing state.

Ukishaona kiongozi wa kitaifa anaingilia kazi za polisi na mahakama, kesi za nani kaiba simu na TV ya nani, huyu kampiga yule, ujue this is a failing state. Maybe not quite a failed state, but a failing state.

Yani hata huyo Waziri Mkuu hajui kazi yake ni nini.
Wewe ni mpumbavu sana sasa ukitaka afanyaje
 
Mpaka Waziri Mkuu kuletewa malalamiko haya ndiyo tayari nchi ishakuwa failing state, kwa sababu kuna ngazi kibao chini yake zinaonekana zimeshindwa kushughuikia hili.

Sasa mnapoangalia hili kwa sababu limeletwa kwa Waziri Mkuu na limepata coverage, mnashindwa kujiuliza haya yapo mangapi kila siku ambayo hayamfikii Waziri Mkuu kwa sababu tunaye mmoja tu na kesi kama hizi zipo maelfu na maelfu?

Tunakuwaje nchi ya kutegemea Waziri Mkuu atatue kesi za polisi, jeshi na mahakama?
Kipindi cha MAGUFULI mbona watu wengi tu walikuwa wanamlilia Magu awasaidie haikuwa failed State?
 
Hii habari ni ishara ya a failing state.

Ukishaona kiongozi wa kitaifa anaingilia kazi za polisi na mahakama, kesi za nani kaiba simu na TV ya nani, huyu kampiga yule, ujue this is a failing state. Maybe not quite a failed state, but a failing state.

Yani hata huyo Waziri Mkuu hajui kazi yake ni nini.
Kuna tofauti kati ya kazi na shughuli. Bwana majaliwa anafanya shughuli siyo kazi.
 
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana alipokuwa akizungumza na wananchi wa Nzuguni katika maadhimisho ya miradi iliyozinduliwa katika kilele cha sherehe za miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kikiwamo kituo cha Zimamoto na Uokoaji.

Kijana huyo alitoa tuhuma hizo, baada ya Waziri Mkuu kutoa nafasi kwa wananchi kuzungumza kero zinazowakabili ili waweze kupata msaada.

Alipopata nafasi hiyo, alidai mwanajeshi huyo aliyemtaja kwa jina maarufu la HK, kunyanyasa vijana wa eneo hilo na yeye akiwamo kwa kuchukuliwa TV yake kwa madai kuwa kuna mtu amemuambia kuwa amemuona na simu ya mke wake.

“Alikuja nyumbani kupekua vitu vya nyumbani kwangu zikiwamo nguo za ndani za mke wangu kwa kuziinua huku akizinyanyapaa, alipokosa simu aliamua kubeba TV na kuondoka nayo na jana amenipigia simu kuniambia kuwa kero yangu hata nikipeleka kwa Rais Samia haitatatulika…naomba Waziri Mkuu nisaidiwe afuatiliwe,” alilalamika.

Waziri Mkuu alimuagiza Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Martin Otieno, kumsaidia kijana huyo na kumtafuta mwanajeshi huyo ili akamatwe.

“Pia nitazungumza na CDF (Mkuu wa Majeshi) kama anavyoeleza kijana huyu kama ndivyo kamanda yeyote wa jeshi lolote hapaswi kuwafanya hivyo Watanzania, jeshi lipo kwa ajili ya kuwalinda wao, maisha yao, vifaa vyao na mali zao zinakuwa salama sio kwenda kuchukua mali zao,” alionya.

“Huyo kijana apatikane na kama atakataa tutapata taarifa zake kwenye kikosi alipo na tutamtafuta CDF atatupa mawasiliano ili tujue kwanini amechukua TV ya huyu kijana. Huyu kijana apewe ushirikiano anaweza kupata matatizo na huyo kamanda akisikia ametamkwa hadharani, huyu kijana alindwe asipate madhara.”

Alisema taarifa ya kijana hiyo ichukuliwe kama taarifa kamili na ifanyiwe kazi ili apate haki yake ya msingi.

Chanzo: Nipashe
Pumbavu
 
Back
Top Bottom