Earthmover
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 24,977
- 23,799
Mambo ni mambo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Vipi umati uliomlaki Airport Dar ulisababisha vurugu popoteKila la heri ila msiingize JINAI kwenye hayo maandamano kama kuzuia shughuli za kawaida za watu wengine , kusababisha foleni zisizokuwa za lazima n.k. Kwa ushauri tu, si angekwenda na watu wachache NEC, achukue fomu na kisha arudi kwenye ofisi za CHADEMA na kuzungumza na wanachama wao. Huu ni ushauri tu ili kuepusha figisu figisu na vyombo vya dola. Nasema tena ni ushauri tu na kwa nia njema kwa mustakabali wa Umoja wa nchi yetu.
Tulia nyumbani tu huku Dunia ikifuatilia kinachoendelea keshoKesho jumamosi hiyo ofisi ipo wazi? Kama iko wazi ni mpaka saa ngapi? Hatutaki kusikia alifika akakuta ofisi imefungwa wakati amekuwa na wiki nzima ya kufuata hiyo fomu.
Lazima tuwe serious, au kama ni maigizo , pia tuambiane tusipotezeane muda.
Wazo zuriAkumbuke tu huo ndo mji ulioweka historia ya uhai wake, ikibidi atembelee eneo la tukio kutoa sadaka na aende hospitaliya mkoa kuwashukuru madaktari na manesi, zaidi ya yote awe MAKINI.
Usishangae kumuona kny majukwaa akimnadi mteuleHivi yule Mzee Yuko wapi siku hizi?
Kesho tutakaza macho kuona itifaki, taratibu, kanuni, sheria na mazowea ya Tume ya Uchaguzi yatakuwa yaleyale kwa CHADEMA mjini Dodoma kama ilivyokuwa kwa mwenyekiti wa CCM ambaye ni mtia nia Urais aliyowasili ktk Ofisi ya Tume kuchukua fomu
Tujikumbushe jinsi Tume ya Uchaguzi walichofanya kwa Magufuli jana :
Vipi online TV's zitarusha mubashara Hilo tukio.?Vipi umati uliomlaki Airport Dar ulisababisha vurugu popote
Mie nimetoa angalizo hilo pia, nikaambiwa nitulie nyumbani. Inawezekana wanajua walichokiapanga.Hivi kesho ni siku ya kazi au chadema wanatafuta ugomvi ?
Haraka sana wahi hospital ..itakuwa dish limekucheza weweLissu hawezi kushinda na kamwe hatakuwa rais wa Tanzania labda jua libadili uelekeo,kwa lipi lissu kaifanyia Tanzania na watanzania hadi wampe heshima ya kiongoza nchi yetu?
Lissu ni mtu hatari sana kwa mstakabari wa taifa letu kwani ni selfish person, ni mtu mwenye jazba,hana nidhamu,amejaaa chuki,na anatumika na nchi za magharibi ili kuvuruga mstakari na umoja wa taifa letu,huyu bwana hafai lazima apingwe kwa kila namna .
Harafu mtu anaposema lissu atakuwa rais ni kujidanganya sana,ataongoza serikali ipi ikiwa chama chake hakina uhakika wa kupata japo wabunge watano,hii ni ndoto
Mwambie lissu kuwa amejidanganya na kama anamatumaini ya kuiongoza Tanzania basi kapotea,
Eti mtetezi wa wanyonge,wanyonge wepi hao anaowatetea ?
Wewe ni daktari ?Haraka sana wahi hospital ..itakuwa dish limekucheza wewe
Afanye hivi kama jinsi ulivyo shauri hilo litachangia kuinua hamasa ya watanzania litasaidia kuwakumbusha machungu watanzania wote wanaompenda ..pia litachangia kuwafanya watu wazidi kuwa na motisha ya kukiondoa chama tawala madarakani ..naimani hilo tukio likitokea kesho kuna watu watamwaga machozi ya huzuni na furahaSina hakika kama Lissu ameshafika Dodoma tangu arudi kutoka kwenye matibabu; ila cha kwanza, kabla ya kwenda sijui kuchukua fomu au kufanya kitu kingine chochote, afike pale alipomiminiwa risasi, ainame abusu mahali pale amshukuru Mungu kwa kumuokoa na mauti ya wazi maana ardhi ile ilimnenea mema. Na ijulikane hakika yuko Mungu aponyaye. Baada ya hapo aendelee na mishe zake kwenda kuchukua fomu na mengineyo yaendelee.
NdioWewe ni daktari ?
kwani hata wakienda kwa kumsindikiza mtu wao wanakua wameenda kuiba viti vya tume ? why wafumuliwe na kwa sababu zipi na je wewe unaetaka vyombo vya ulinzi vifumue wananchi kweli unalitakia taifa ili mema kweli acheni izo ustarabu wa kueshim uhuru wa mtu ali hali hajavunja sheria ndo utatuvusha salama uchaguzi huu , na nimatumain yangu vyombo vyetu vya ulinzi viko makini katika kushauri vizuri ili kila kitu kiende sawa tuliona ya dar ya mapokezi mambo yalikua safi hakuna hata mende alie dhulika na kweli walifanya kazi nzuri ,na kwa mwendo huo nimatumaini yangu kila kitu kitaenda sawa mpaka 28 octoTume ya Taifa ya Uchaguzi imeishatoa utaratibu wa wagombea kuchukua fomu sasa kama mnajitia vichwa maji jaribu muende kwa maandamano, muone mtakavyofumuliwa.
Ungesema mkoa mwingine, Dodoma hawana maana hata kidogo watakaojaa ni wanafunzi wa vyuo na wapenda matukio, kwenye uchaguzi watakuwa makwao, na itabaki kijani kwa asilimia kubwa.
Basi sawaKwa mjibu wa Lisu Tanzania kuna Corona na watu wanakufa, hivyo sitarajii shamra shamra kama za mwenzake anayeamini Corona imekwisha.
Mie bado sijaona kibaya anachoongea Lissu, tumekaa kwa utulivu wa kinyonge kwa miaka karibu mitatu mpaka akili zimesinyaa, tunaona Lissu anaongea hovyo.hivi kati ya TL na Jiwe ambaye ni Rais, anayetaka kuwapanua watu na kumuoza mama ake kwa zawadi ya jogoo nani mropokaji?
Hata mie nashangaa, kesho ni siku ya sherehe za wakulima iweje ofisi za NEC ziwe wazi.Je, CHADEMA wameshajiridhisha na Tume ya Uchaguzi ( NEC ) kuwa Kesho watakuwepo? Aliyeipanga hii tarehe alikosea na naomba niishie hapa.
Afadhali Lissu anaweza kufundwa, wa kwako ukimshauri ndio unaharibu kabisa.October 2020 uchaguzi lakini mpaka sasa wanyanyembe hamjajipanga kwenye kitengo cha habari?
Mgombea wenu Lissu mpaka sasa hajajua aelekee wapi mpaka afundwe?
Hata ratiba za sikuu hamzijui?
Nyinyi hamna umakinifu hamuwezi kupewa nchi.
Basi kaa na kura yako nyumbani kwako, sisi tunataka taifa linaloongozwa kwa sheria na katiba na Lissu ndio tumaini la kutupeleka huko.Ni vizuri mgombea aache miemuko ajitofautishe na aliyepo, atambue kula ni za makundi yote kuna watu ukiwa na miemuko unawatisha zaidi utapata kula za vijana ambao mara nyingi si wapiga kura wazee na wanawake watakukwepa maana wataofia machafuko wao hawana pa kukimbilia achunge na adhibiti mdomo wake, maneno madogo tu yanaeza mpunguzia kula. 2015 nilimchagua Lowassa ila mwaka huu naona kama wagombea wenye nguvu wanafanana tabia ya kutoambilika