Uchaguzi 2020 Dodoma yazizima kwa Maandalizi ya Lissu kuchukua fomu 8.8.2020

Uchaguzi 2020 Dodoma yazizima kwa Maandalizi ya Lissu kuchukua fomu 8.8.2020

hivi kati ya TL na Jiwe ambaye ni Rais, anayetaka kuwapanua watu na kumuoza mama ake kwa zawadi ya jogoo nani mropokaji?
Em nawe tumia hata akili ya chekechea bc mkuu, kwa akili yako yote unadhani aliloongea litafanyika hivyo.? Bc mzungumzie na yule mama aliyesema amemuandikia barua rais ya kimapenzi
 
Mtoa mada na nyie wengine mnaodhani huyo mtu wenu atashinda endeleeni kujazana upumbavu kichwani
 
Akumbuke tu huo ndo mji ulioweka historia ya uhai wake, ikibidi atembelee eneo la tukio kutoa sadaka na aende hospitaliya mkoa kuwashukuru madaktari na manesi, zaidi ya yote awe MAKINI.

CHADEMA muwe makini mno kama mdau anavyosema hapa. Yasije yakatumika yale yaliyomdhuru Mwakyembe (hamtashtukia haraka).. kwenye watu wengi kuna mengi. Lissu alindwe sana sana, asijiamini sana. Muhimu tufike kwenye campaign salama.
 
Kwa nini mtengeneze mazingira ya uwepo wa nguvu ya umma?.Mgombea wa ACt-Wazalendo kachukua Fomu kwa utulivu ule ule wa jana.Fanyeni masihara,mtajikuta mnawaangalia Magufuli na Membe wakipishana kwenye majimbo huku nyie mkiwa watazamaji.

Mbona nyinyi mlitoa kabisa taarifa ya Mwenyekiti wenu mkihitaji wanachama wenu na watu walienda nae kuchukua form?! Baada ya hapo mkafanya na campaign kabisaa. Hapa mnateseka nini?!
 
Tayari tunakaribia mji ule, kwa mbali kwenye giza hili totoro tumeanza kuona utitiri wa taa za mji na huo mji ni Dodoma ili kuweza kutekeleza takwa la kisheria.

Kesho ni siku muhimu kwa kambi ya upinzani kupitia CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu wa tarehe 28 October 2020.
 
Ww ni msemaji wa tume? Sio vibaya pia Molemo akitolea ufafanuzi kama wamehakikishiwa kukuta ofisi ikiwa wazi.
wanataka kupata kisingizio sababu hata Membe alitakiwa kwenda kesho lakini imebidi aende leo. Hii tabia ya Chadema ya kutengeneza matukio haitawasaidia chochote
 
wanataka kupata kisingizio sababu hata Membe alitakiwa kwenda kesho lakini imebidi aende leo. Hii tabia ya Chadema ya kutengeneza matukio haitawasaidia chochote

Kwani tume wanaona shida gani kusema kama leo hawatakuwepo ili wasiwape cdm hayo matukio? Sehemu zote kwenye watu au taasisi zenye nia njema, huwataarifu wadau wao kuwa siku fulani hawatafungua ofisi, na huweka sababu ya kutofungua ofisi. Unaposema Membe alienda jana, kwani cdm wanafanya mambo yao kwa kuwaiga ACT?
 
WanaJF

Dodoma Inazizima.Ndivyo tunavyoweza kusema kwa Sasa.

Mapokezi kabambe yanamsubiri mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia Chadema Tundu Antipass Lissu ambaye atachukua rasmi fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kesho siku ya Nane Nane.

Inatarajiwa mgombea huyo kusindikizwa na umati mkubwa wa wakazi wa jiji la Dodoma katika kile kinachoonyesha Imani kubwa waliyo nayo kwa kiongozi huyo.

Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu ametoa wito rasmi kwa wakazi wa jiji la Dodoma na mikoa jirani kumsindikiza mgombea huyo Safari itakayoanzia makao makuu ya Chadema Kanda ya Kati Area C Mtaa wa Makongoro.

Katika mahojiano na wakaazi kadhaa wa jiji Hilo wameonyesha shauku kubwa ya kutaka kumuona Tundu Lissu ikiwa ni miaka mitatu alipoondolewa katika jiji Hilo akiwa nusu mfu baada ya kupigwa risasi kumi na sita na watu wasiojulikana na Sasa anarejea jiji Hilo Hilo akiwa mzima wa afya na akitembea kwa miguu yake miwili huku wabaya wake waliotaka kumuua wakifichama kusikojulikana.

Hapo Jana wanafunzi wa vyuo vikuu vya UDOM, CBE na Mipango walikuwa katika vikao vya namna ya kumsindikiza Lissu ambaye walimwita shujaa wao.

Tundu Lissu amejizolea uungwaji mkono na umaarufu mkubwa kutokana na sera yake ya kuwapa watu Uhuru wa kusema na kutoa maoni yao bila kuingiliwa na vyombo vya Dola endapo atachaguliwa kuwa Rais.Na pia kuruhusu vyama vya siasa. NGO's na vyombo vya Habari kufanya kazi zake kwa Uhuru Kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Chadema leo inatarajiwa kutoa ratiba njia atakazopita mtetezi huyo wa wanyonge na Msemaji wa wasio na sauti ili walau watu kujipanga manjiani kumsalimia na kumsindikiza.

#NiYeye2020
Lissu aliutangazia ulimwengu kuwa Tanzania kuna Corona na Serikali haisemi ukweli na haichukui tahadhari ya kujilinda. Yeye amejipanga vipi kuhusu social distancing, kunawa maji tiririka na kuvaa barakoa? Au ATAMUIGA Rais Magufuli kutovaa barakoa kwa kuwa HAKUNA Corona!?
 
CCM imeshindwa kuboresha maslahi ya wafanyakazi na kutoa ajira kwa vijana.
 
Back
Top Bottom