Dondoo za hatifungani za leo - 20yrs Bond 15.49%

Dondoo za hatifungani za leo - 20yrs Bond 15.49%

Nilivo elewa ni kwamba mfano nimewekeza 20M hatifungani kwa mwaka napata faida 3098000 hii ina maana kwamba ni sawa na 258166.66 kwa mwezi
Ninaweza kwenda bank mfano crdb bank nikachukua mkopo wa 15M,labda marejesho ni 250000 monthly,naweza ongea na bank niwe nalipa kwa mwaka yaani kuponi kama alivoeleza mtoa mada,ile kuponi ninayopokea inakatwa kulipa mkopo wangu hivyo baada ya miaka 7 ntakuwa nimemaliza mkopo na mtaji wangu bado upo pale pale hii ndo faida ya kuwekeza kwenye hatifungani,unatumia faida unayopokea kulipa deni la mkopo

Faida nyingine kama sitoi hiyo koponi basi baada ya miaka 20 ntakuwa na faida ya jumla (3098000 ×20= 61,960,000) hii ni faida tu
Mtaji 20M + faida 61960000= jumla 81,960,000/= ni sawa na mafao ya mtumishi
Kama ndivyo ni uwekezaji mzuri sana


Nadhani mtoa mada atatuelewesha zaidi
Kuna kitu watu wengi hamuangalii na ndio mnapigwa hapo.
Hiyo fedha unayowekeza baada ya miaka miwili itakua imeshuka thamani kiasi gani kutokana na mfumuko wa bei?
Ingekuwa tanaruhusiwa kuweka kwa stable currency kama USD matajiri wasingefanya tena biashara zaidi ya kununua hati fungani.

Mwaka jana nilikuwa na mradi wa nyumba za kupanga ulinigharimu kama 140m pamoja na kiwanja.
Mshikaji mmoja katika story akaniambia nimefeli bora ningewekeza katika hati fungani ningepiga hela ndefu bila usumbufu.
Nikamuuliza baada ya miaka kumi ile M140 kwenye hati fungani itakuwa na thamani ya kununua hata kiwanja chenye thamani ya M20 leo?
Na hizi nyumba baada ya miaka hiyo 10 zitakuwa na thamani ile ile ya 140m?
 
Mungekua flexible tuweke hizo hatifungani kwa US dollor na tulipwe kwa dollor baada ya miaka 20, apo ningeuza my assets ili ni wekeze ila kwa Tz shilling hixi karatasi zinazo shuka kwa kasi, mtu moja anamiliki 7nb nyumbani kwake ziko nje ya mfumo rasimi inflation haikwepeki.......boresheni hata mueweke kwenye Gold standarnd.
💯
 
Kuna kitu watu wengi hamuangalii na ndio mnapigwa hapo.
Hiyo fedha unayowekeza baada ya miaka miwili itakua imeshuka thamani kiasi gani kutokana na mfumuko wa bei?
Ingekuwa tanaruhusiwa kuweka kwa stable currency kama USD matajiri wasingefanya tena biashara zaidi ya kununua hati fungani.

Mwaka jana nilikuwa na mradi wa nyumba za kupanga ulinigharimu kama 140m pamoja na kiwanja.
Mshikaji mmoja katika story akaniambia nimefeli bora ningewekeza katika hati fungani ningepiga hela ndefu bila usumbufu.
Nikamuuliza baada ya miaka kumi ile M140 kwenye hati fungani itakuwa na thamani ya kununua hata kiwanja chenye thamani ya M20 leo?
Na hizi nyumba baada ya miaka hiyo 10 zitakuwa na thamani ile ile ya 140m?
Watanzania wengi hawana financial literacy, hususani kwenye finance market, inflation rate yetu haikuruhusu kufaidi hiyo pesa, kabisa ni kupoteza mda nikupe mfano 2004, 1US $ = 900 up to 970 Tanzanian shilling miaka 20 kwa sasa 2024 1US$ =2400 up to 2600,.....kama uliwekeza 100m miaka 20 iliopita sasa hivi wakukurudishia hiyo pesa haina value tena, kama ni dollor unapata $45,000 kwa sasa lakini miaka 20 ilio pita hiyo pesa ungepata $110 000. Hapo kuna faida kweli hapana..........

Kama unataka kufaidi finance market neenda UK au US kanunue hizo bonds wana wapa hata foreiners fursa hiyo ya kununua, wekeza dollor $50,000, rudi Tanzania kalale hutakuja kufa masikini maishani yako, utakua unakula tu exchange rate tu ya unstable currency yetu inao panda kila ukicha, kwa mwezi huwezi kukosa 10 to 15m, na pesa inawekwa tu kwenye your local account hamna haja ya kupigia customer care.
 
Kuna kuponi ya kwanza na kuponi ya pili manaake hiyo 15% imegawanywa mala mbili, manaake huenda unalipwa kila baada ya 10yrs ila sioni kila mwaka hapo kwenye jadweli.
Kuna vitu nikisoma huku una nakataa kabisa jf sio home of great thinkers

Mkuu kabla ya hii post, hukuwahi kujua chochote kuhusu government bonds? Tufanye hukujua, lakini mbona post imeeleza vizuri tena kwa urahisi sana
Sasa umeshindwa vipi kuelewa na hapo wameweka mchanganuo vizuri kabisa hadi mfano wa pesa utayoweka na utavyolipwa kila baada ya miezi 6
 
Mungekua flexible tuweke hizo hatifungani kwa US dollor na tulipwe kwa dollor baada ya miaka 20, apo ningeuza my assets ili ni wekeze ila kwa Tz shilling hixi karatasi zinazo shuka kwa kasi, mtu moja anamiliki 7nb shilling nyumbani kwake, ziko pesa zote ziko nje ya mfumo rasimi hyper inflation haikwepeki.......boresheni au mueweke kwenye Gold standarnd.
Mkuu sio dollor ni dollar
 
Matokeo ya mnada uliofanyika Leo tarehe 31 Julai 2024
IMG-20240731-WA0009.jpg
 
Leo jumatano ya tarehe 31 Julai 2024, ni siku ya mnada wa Hatifungani ya miaka 20 yenye riba ya 15.49% kwa mwaka.

Kwa watakao shinda katika mnada huu watakuwa na dhamana ya miaka 20 kama nilivyosema hapo awali. Dhamana hii itakuja na kuponi mbili kwa mwaka, yaani kila baada ya miezi sita (06)

Ninaposema kuponi namaanisha utalipwa nusu ya riba ndani ya miezi sita na nusu nyengine utalipwa baada ya miezi sita tena ili kukamilisha mwaka.

Hatifungani hii itadumu Kwa muda wa miaka 20 hivyo baada ya miaka 20 utalipwa pesa uliyowekeza (principal amount). Mfano huo hapo kwenye picha
View attachment 3057276

FAIDA ZA HATIFUNGANI HII

:-Kama zilivyo hatifungani zengine itakupa faida zifuatazo zitakazodumu kwa muda wa miaka 20

📚 Hatifungani ni dhamana (collateral) hivyo una uwezo wa kukopa Benki kupitia hatifungani hii, uwezo wa kukopa utatofautiana kulingana na fedha ulizowekeza.

📚Kuwa na uhakika wa malengo ya muda mrefu. Mfano, ada ya mtoto. Kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu Mtanzania hutumia miaka 17 shuleni. Hivyo unaweza kuwekeza pesa ambayo kuponi zake zitatumika kama ada ya mwanao.

📚 Hatifungani ni uwekezaji wenye hatari ndogo. Hatifungani za serikalli zinasimamiwa na serikalli kupitia Benki kuu ya Tanzania (B.O.T) hivyo uwezekano wa wewe kupata hasara ni mdogo mno.

NOTE: Faida zipo nyingi sana hizo ni baadhi tu, kujifunza mengi kuhusu Hatifungani, karibu uwanja wa email @geminifinaces808@gmail.com

Kila la kheri🙏🇹🇿

Hi
Hii rate ya 15.47% imepanda lini? Mwaka 2022 mwanzoni ilishushwa sana na kuwa 12%. Je imepandishwa Tena? Na imepanda lini?

Huwa kuna vitu naulizaga lakinj kwenye majinu watu huingia mitini, vinawekwa Ila majibu yanakua hakuna. Ni either mtu anakua hajui hiko kitu au anajua lakini hawezi kutoa maelezo yaliyonyooka, au na yeye kasikia tu sehemu
 
Capital gain na Interest zinakatwa kodi ya zuio (Withholding Tax)
Du. Kwa hiyo hayo malipo mwanzisha thread aliyoweka ya mara mbili kwa mwaka bado yanapigwa tena panga la kodi. Unaweza kutupa mfano wa kiwango cha kodi kama unafahamu?
 
Back
Top Bottom