Dondoo za hatifungani za leo - 20yrs Bond 15.49%

Dondoo za hatifungani za leo - 20yrs Bond 15.49%

Leo jumatano ya tarehe 31 Julai 2024, ni siku ya mnada wa Hatifungani ya miaka 20 yenye riba ya 15.49% kwa mwaka.

Kwa watakao shinda katika mnada huu watakuwa na dhamana ya miaka 20 kama nilivyosema hapo awali. Dhamana hii itakuja na kuponi mbili kwa mwaka, yaani kila baada ya miezi sita (06)

Ninaposema kuponi namaanisha utalipwa nusu ya riba ndani ya miezi sita na nusu nyengine utalipwa baada ya miezi sita tena ili kukamilisha mwaka.

Hatifungani hii itadumu Kwa muda wa miaka 20 hivyo baada ya miaka 20 utalipwa pesa uliyowekeza (principal amount). Mfano huo hapo kwenye picha
View attachment 3057276

FAIDA ZA HATIFUNGANI HII

:-Kama zilivyo hatifungani zengine itakupa faida zifuatazo zitakazodumu kwa muda wa miaka 20

📚 Hatifungani ni dhamana (collateral) hivyo una uwezo wa kukopa Benki kupitia hatifungani hii, uwezo wa kukopa utatofautiana kulingana na fedha ulizowekeza.

📚Kuwa na uhakika wa malengo ya muda mrefu. Mfano, ada ya mtoto. Kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu Mtanzania hutumia miaka 17 shuleni. Hivyo unaweza kuwekeza pesa ambayo kuponi zake zitatumika kama ada ya mwanao.

📚 Hatifungani ni uwekezaji wenye hatari ndogo. Hatifungani za serikalli zinasimamiwa na serikalli kupitia Benki kuu ya Tanzania (B.O.T) hivyo uwezekano wa wewe kupata hasara ni mdogo mno.

NOTE: Faida zipo nyingi sana hizo ni baadhi tu, kujifunza mengi kuhusu Hatifungani, karibu uwanja wa email @geminifinaces808@gmail.com

Kila la kheri🙏🇹🇿

Hi
Mkuu hizi hesabu haziko sahihi depending na t-bonds ambazo umezungumzia,sababu hujaconsider vitu kama face value,bidding price,yearly coupon,etc ambazo mwisho wa siku zitatupa total gain.
 
Hii rate ya 15.47% imepanda lini? Mwaka 2022 mwanzoni ilishushwa sana na kuwa 12%. Je imepandishwa Tena? Na imepanda lini?

Huwa kuna vitu naulizaga lakinj kwenye majinu watu huingia mitini, vinawekwa Ila majibu yanakua hakuna. Ni either mtu anakua hajui hiko kitu au anajua lakini hawezi kutoa maelezo yaliyonyooka, au na yeye kasikia tu sehemu
Kama ni kweli interest rate ni above 15% annually basi ni uwekezaji mzuri at least unapunguza hatari ya kupoteza mtaji wako.
 
Kama ni kweli interest rate ni above 15% annually basi ni uwekezaji mzuri at least unapunguza hatari ya kupoteza mtaji wako.
Inategemea tu malengo yako. Mimi nimeweka mzigo wa 20m kwa ajili ya dogo wa 10yrs kama ada nikiwa sipo kazini. Sasa hapo kipi bora, ifanye biashara ipotee yote au ipoe BOT baada ya 10 years achukue plus 15% interest?
 
Kuna kitu watu wengi hamuangalii na ndio mnapigwa hapo.
Hiyo fedha unayowekeza baada ya miaka miwili itakua imeshuka thamani kiasi gani kutokana na mfumuko wa bei?
Ingekuwa tanaruhusiwa kuweka kwa stable currency kama USD matajiri wasingefanya tena biashara zaidi ya kununua hati fungani.

Mwaka jana nilikuwa na mradi wa nyumba za kupanga ulinigharimu kama 140m pamoja na kiwanja.
Mshikaji mmoja katika story akaniambia nimefeli bora ningewekeza katika hati fungani ningepiga hela ndefu bila usumbufu.
Nikamuuliza baada ya miaka kumi ile M140 kwenye hati fungani itakuwa na thamani ya kununua hata kiwanja chenye thamani ya M20 leo?
Na hizi nyumba baada ya miaka hiyo 10 zitakuwa na thamani ile ile ya 140m?
Mkuu nadhani na wao siyo wajinga. Wanajua kwamba currency yetu siyo stable. Ndo maana wanatoa % kubwa ya returns. Bond za US na nchi nyingine zilizoendelea, sidhani kama interest inazidi 2%. au 3%. Wakati kwetu ni 15%+.

Kwa mtu asiye na uchumi mkubwa, au mwenye matamanio ya biashara, hati fungani ni investment nzuri sana. After all, kibongo kibongo, kipato cha mwajiriwa hakijawahi kuendana na inflation.

Ukiwa na bonds, hata ukitangulia mbele ya haki, una matumaini kwamba madogo hawatakosa karo na matumizi mengine ya kila siku.
 
Inategemea tu malengo yako. Mimi nimeweka mzigo wa 20m kwa ajili ya dogo wa 10yrs kama ada nikiwa sipo kazini. Sasa hapo kipi bora, ifanye biashara ipotee yote au ipoe BOT baada ya 10 years achukue plus 15% interest?
Umefanya powa sana.
 
Watanzania wengi hawana financial literacy, hususani kwenye finance market, inflation rate yetu haikuruhusu kufaidi hiyo pesa, kabisa ni kupoteza mda nikupe mfano 2004, 1US $ = 900 up to 970 Tanzanian shilling miaka 20 kwa sasa 2024 1US$ =2400 up to 2600,.....kama uliwekeza 100m miaka 20 iliopita sasa hivi wakukurudishia hiyo pesa haina value tena, kama ni dollor unapata $45,000 kwa sasa lakini miaka 20 ilio pita hiyo pesa ungepata $110 000. Hapo kuna faida kweli hapana..........

Kama unataka kufaidi finance market neenda UK au US kanunue hizo bonds wana wapa hata foreiners fursa hiyo ya kununua, wekeza dollor $50,000, rudi Tanzania kalale hutakuja kufa masikini maishani yako, utakua unakula tu exchange rate tu ya unstable currency yetu inao panda kila ukicha, kwa mwezi huwezi kukosa 10 to 15m, na pesa inawekwa tu kwenye your local account hamna haja ya kupigia customer care.

Mkuu Covax , tupe tips na elimu zaidi kuhusu Bonds za US na UK for foreigners.

Financial literacy ni muhimu sana kwa maisha ya sasa.

Cc: Masanja

-Kaveli-
 
Milioni 15 kwa mwaka zidisha kwa 20 jibu ni milioni 300 duuh mbona faida nene
Hapa nipo wanapofactor in infation.Ina maana kwamba baada ya miaka 20 milioni mia 300 inaweza kuwa sawa na milioni 100 ya sasa.Yaani kituna unachonunu kwa 1000 sasa hivi kitauzwa 3000.Unachonunua kwa 10,000 kitauzwa 30,000...
 
Mkuu Covax , tupe tips na elimu zaidi kuhusu Bonds za US na UK for foreigners.

Financial literacy ni muhimu sana kwa maisha ya sasa.

Cc: Masanja

-Kaveli-
Kama una pesa wewe nunua bonds tuu. Hati fungani ni kama insurance. Ni rahisi kushauriwa kwamba uweke pesa kwenye biashara. Ila biashara pia ni kamari. Mifumo yetu ya kibongo ni wizi wizi tuu. Ukiwa na million 100, Million 50 weka Bond na 50M weka kwenye biashara. Usiweke mayai yote kwenye kikapu kimoja.

Naona siku hizi pia kuna uwezekano wa kununua bonds kwenye nchi za SADC. KIKUBWA JIONGEZE. Angalia nchi yenye uchumi imara kama Botswana au Namibia au SA. Nunua huko.

Kwa maisha yetu ya kibongo kibongo, ukiwategemea akina Mwigulu ambao na wenyewe wanapambana kujikomboa kwa jasho la walalahoi..ni ngumu kuchomoka.
 
Kuna kitu watu wengi hamuangalii na ndio mnapigwa hapo.
Hiyo fedha unayowekeza baada ya miaka miwili itakua imeshuka thamani kiasi gani kutokana na mfumuko wa bei?
Ingekuwa tanaruhusiwa kuweka kwa stable currency kama USD matajiri wasingefanya tena biashara zaidi ya kununua hati fungani.

Mwaka jana nilikuwa na mradi wa nyumba za kupanga ulinigharimu kama 140m pamoja na kiwanja.
Mshikaji mmoja katika story akaniambia nimefeli bora ningewekeza katika hati fungani ningepiga hela ndefu bila usumbufu.
Nikamuuliza baada ya miaka kumi ile M140 kwenye hati fungani itakuwa na thamani ya kununua hata kiwanja chenye thamani ya M20 leo?
Na hizi nyumba baada ya miaka hiyo 10 zitakuwa na thamani ile ile ya 140m?
Mim naungana na wewe mkuu, ni bora sana narudia tena ni hora sana milioni 100 kuiwekeza kwenye nyumba ya kupangisha ambayo inaweza kukupa hiyo milioni 15 kwa mwaka na bado unaweza kutumia hiyo nyumba kama collateral kuomba mkopo na ukaweza kujenga nyumba nyingine ambapo ukiwa na mahesabu mazuri ndani ya miaka 10 huwez kukusa nyumba walau 3. Nyumba inapanda thamani kila kukicha ila shilingi yetu inaporomoka sana thamani yake kila siku
 
Hapa nipo wanapofactor in infation.Ina maana kwamba baada ya miaka 20 milioni mia 300 inaweza kuwa sawa na milioni 100 ya sasa.Yaani kituna unachonunu kwa 1000 sasa hivi kitauzwa 3000.Unachonunua kwa 10,000 kitauzwa 30,000...
Ni kweli kabisa ila wengi hawaliangalie mwaka 2004 tulikua tunapanda daladala kutoka ubugo mpaka kkoo kwa sh 150, mwaka 2024 ubungo mpaka kkoo ni sh 600, manaake sh 150 ya 2004 ni sawa sawa na sh 600 ya leo ni mara 4 yake, hiyo ndo inaoitya hyper inflation.
 
Umefanya vyema mkuu baada ya miaka 10,mtaji pamoja na faida utakuwa na 50m+
Hii elimu wengi wetu hatuna ndio maana tunaangaika
Inategemea tu malengo yako. Mimi nimeweka mzigo wa 20m kwa ajili ya dogo wa 10yrs kama ada nikiwa sipo kazini. Sasa hapo kipi bora, ifanye biashara ipotee yote au ipoe BOT baada ya 10 years achukue plus 15% interest?
 
Ni kweli kabisa ila wengi hawaliangalie mwaka 2004 tulikua tunapanda daladala kutoka ubugo mpaka kkoo kwa sh 150, mwaka 2024 ubungo mpaka kkoo ni sh 600, manaake sh 150 ya 2004 ni sawa sawa na sh 600 ya leo ni mara 4 yake, hiyo ndo inaoitya hyper inflation.
Lakini mkuu ata kwenye bond pesa inaongezeka hiyo 15% inaifanya pesa yako uliyoiweka isiwe ile ile ya mwaka 2004 itakuwa ni kubwa leo 2024
Watu mnaongea mambl mengi as if haizai
Kuweka kwenye bond ni tofauti na kusave bank
 
Lakini mkuu ata kwenye bond pesa inaongezeka hiyo 15% inaifanya pesa yako uliyoiweka isiwe ile ile ya mwaka 2004 itakuwa ni kubwa leo 2024
Watu mnaongea mambl mengi as if haizai
Kuweka kwenye bond ni tofauti na kusave bank
And people think like…..life is static. Hapana. Hali yetu 2004 na leo ni tofauti sana.
 
Mungekua flexible tuweke hizo hatifungani kwa US dollor na tulipwe kwa dollor baada ya miaka 20, apo ningeuza my assets ili ni wekeze ila kwa Tz shilling hixi karatasi zinazo shuka kwa kasi, mtu moja anamiliki 7nb shilling nyumbani kwake, ziko pesa zote ziko nje ya mfumo rasimi hyper inflation haikwepeki.......boresheni au mueweke kwenye Gold standarnd.
Tuwekeze kwa gold value Wala sio hata iyo dollar yako pia huwa inashuka ingawa sio Kama tzs Ila bucks ,fiber ,lira,Aussie,loonie and kiwi zinashuka pia
 
Tuwekeze kwa gold value Wala sio hata iyo dollar yako pia huwa inashuka ingawa sio Kama tzs Ila bucks ,fiber ,lira,Aussie,loonie and kiwi zinashuka pia
Mbona hata dhahabu inashuka pia, wewe umeshindwa kujua inflation na depreciation vyote vinamanisha kushuka ila havifanani, pesa ya bongo ina hyper infñation sio kushuka kwa kawaida depreciation.....dollar in depreciate sio ku-inflate.
 
Back
Top Bottom