Dotto Biteko: Tumezima mtambo wa bwawa la Mwl Nyerere
Sasa kipi ni kipi?

Maji yawe mengi tupate umeme ama maji yawe kidogo?

Excuses za Tanesco zimekuwa za hovyo kweli. Na zote kisingizio ni maji.

Kiangazi, wanalalamika maji ni kidogo. Yamepungua kina. Sawa, mvua zimenyesha kunabadilika kuwa mvua zimekuwa nyingi, tunayapunguza. WTF!.

Walijenga bwawa kubwa kama lile bila ya kuweka viashiria kama litajaa kama litajaa kabla ya wakati?
 
Najiuliza shina ni nini? hatuna weledi, hatuna teknolojia, poor decision making au poor political will au Bwegez wamejaa kwenye hiyo Taasisi? Inasikitisha sana! kujenga bwawa tabu!! hata uratibu wa bwawa nao tabu. sijui kipi tunaweza sasa. Au tunahitaji tuletewe tena SAP part II
Shule za kusomea ujinga:

 
Kwani hayo maji ya ziada hayawezi kuhifadhiwa sehemu halafu muda ukifika wa kuyahitaji wanayatumia?
 
Nafikiri aliekufa alikufa na mradi wake.. lakini sitaki kuamini hili maana sio kwamba wanashindwa ni kujiendekeza na ni upuuzi tupu,ifike hatua muone aibu kila siku porojo yule mzee aliona mbali alijua miaka michache ijayo kutakuwa na upungufu wa umeme maana nchi inakuwa hii, na ndio maana akaleta hilo bwawa..

Ukweli ni kwamba umeme ulikuwa hautoshi na ndio maana mgao ulikuwa ni mkali wala siswala la mvua. sasa kinachotokea ni kwasababu ya walafi fulani tu ili wafanye biashara zao za mafuta na majenereta hovyo kabisa,nina chuki na watu wa hovyohovyo ujinga tupu.
 
Nadhani concept ni moja.

Kuna mashine 9, inayofanya kazi ni moja. Bwawa linatakiwa kuhifadhi maji ya mashine 9.

Sasa kama mashine moja kati ya 9 ndio inafanya kazi, maji mengine hayana sababu ya kuwepo pale, lazima yafunguliwe yaondoke.

Iwapo mashine zote 9 zingekua zinafanya kazi basi hayo maji bado yasingetosha.

Ni serikali kuhakikisha mashine zote zinawashwa kwa wakati mmoja tu ama vinginevyo yale maji yote yatapotea bure.
Hawana hela ya kuleta mitambo mingine? Mbona ma v8 yanaletwa bila kujiuliza? Nashauri viongozi wapigwe mnada fedha ipatikane ya mitambo. Mvua zinawataka waharakishe wao wanajizungusha tu
 
Kwani hayo maji ya ziada hayawezi kuhifadhiwa sehemu halafu muda ukifika wa kuyahitaji wanayatumia?
Hapo ni kama unawaambia wachimbe bwawa lingine. Cha msingi kama mitambo ni michache waongeze mingind na wauze umeme kama wanaona nchini hauhitajiki. Na kama unahitajika bei ya umeme ipunguzwe wananchi wafurahie matunda ya viongozi walio jikana nafsi kuanzisha mradi
 
St
Sasa wakishayapunguza maji kipindi cha kiangazi watasema maji ni machache mno. Shenzi taipu zao hao wawashe mashine zote watengeneze storage facility za umeme ili utumike kipindi maji yakiwa machache kipindi cha kiangazi ndio wazime baadhi ya mashine.
Storage facilities za umeme wa megawatt 200 mpaka 1000 ni kama zipi? Mabetry 1000,000 ya gari yatumike kutunza charge? Kuna vifaa gani special?

Kila mwenye betri la la gari asiye na kazi nalo,tunaliomba
 
JPM alikurupuka kujenga bwawa kwa kutumia ramani za miaka ya sabini, akaambiwa, akajifanya chizi, hakufanya hata environmental impact assessment, maji yakiachiwa yanaenda katika mashamba ya wananchi na nyumba zao hapo rufiji, soon tutasikia habari ya mafuriko hapo rufiji.

Hata kipande cha reli alichojenga JPM ndicho kina kelele za kimazingira, pale Morogoro lile tuta linafanya maji yasiwr na njia, kwa hiyo yanarudi kwa wananchi na kusababisha mafuriko. Natamani wale wakazi wa maeneo yanayopata mafuriko kutokana na kutofanywa kwa Environmental Impact Assessment wafungue kesi dhidi ya serikali.

Ni muhimu serikali ikawa na msimamo kwenye mambo ya kitaalamu kuliko kukimbizana na presha za kisiasa
 
AFRIKA tuna shida jamani. Sasa inabidi tumwombe Mungu apunguze mvua.

Mitambo inazama majini. Serikali imeshtuka baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kutangaza mvua itanyesha kali. Wakati wana dizaini bwawa hawakujua kuna siku mvua zitapiga kali. Hakuna provision ya kuchepusha maji yanapozidi....

MWANANCHI ONLINE
APRIL 1st 2024

Mashine yazimwa Julius Nyerere

View attachment 2951205
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dr. Dotto Biteko, akikagua mitambo ya kufua umeme


Biteko amesema kutokana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA) kutangaza uwepo wa mvua kubwa kwenye maeneo mengi, wizara hiyo itaendelea kuchukua kila hatua ya tahadhari

“Mfano Kituo cha Julius Nyerere ipo mashine moja ya kuzalisha umeme, lakini maji yanayozalishwa pale ni mengi sana kinyume kabisa na mipango tuliyokuwa nayo"

Maana tulikuwa tunajua kwamba Julius nyerere ingeweza kujaa bwawa lile mwezi wa 12 mwaka 2026, lakini yamejaa ndani ya msimu huu tu mmoja na yale maji yanavyojaa yanakuja mengi kwa wakati mmoja,” amesema.

Amesema baada ya kuona wingi walitoa tahadhari Machi kwa watu wote walioko upande wa chini wa bwawa, kwamba wangeachia maji maana uwezo wa kuendelea kuyashikilia haupo.

“Ukianza kufungulia yale maji, Julius Nyerere lazima uizime, maana yanayotoka juu ni mengi zaidi kuliko yanayotoka kwenye teresi, hivyo ninavyozungumza mtambo wa Julius Nyerere tumeuzima, tunapunguza maji ili tupate umeme," amesema Dk Biteko
Du members wa Jamii forums,NI wataalam wa kila kutu,Wana ponda na kulaumu hata vitu cya kitaalamu,shida Sana.
 
Si ajabu hiyo turbinę yenyewe waliyokuwa wanaitumia washaikongoloa huko kupunguza maji ni kisingizio tu.

Juzi wamemwaga maji mpaka maeneo ya jirani kufurika hata week mbili hazijapita maji yamejaa tena.

Shida ni ujuaji waliotengeneza mashine wameshauri testing ifanyike taratibu mpaka mwezi wa sita ndio waanze kuitumia mitambo at full capacity (its for good monitoring reasons kwa upande wa manufacturer) serikali ya Tanzania inajua zaidi kuliko waliotengeneza hizo turbinę wamelazimisha matumizi ya full capacity washakongoloa mtambo hakuna warranty cover kutengeneza lipa.

Very useless and predictable people
 
Hiv Biteko ni Dr. wa taaluma gani?
images - 2024-03-10T190459.157.jpeg
 
Makadirio yao yalikuwa bwawa lijae 2026 lakini limejaa ndani ya msimu mmoja tu 2023/24.... Hivi haya yalikuwa makadirio ya aina gani?

Hapo waseme tu walikuwa wanataka kuwapiga watanzania dana dana hadi 2026 lakini walivyoona kelele zimezidi ndo wakawasha kamtambo kamoja.

Hako kamtambo kamoja kati ya 9 iliyopo ndo kanawapa shida hivi, je zikiwashwa zote 9 wataweza kuzimanage kweli?

Majii yakijaa shida, yakipungua shida. Sitashangaa wakitangaza mgao wa umeme sababu maji yamejaa na yakipungua tena watatangaza mgao na kutuhimiza tuombee mvua zinyeshe bwawa lijae.... Hii nchi ni kama wote tupo chekechea.
Tanzania kuna shida kubwa sana
 
Nadhani concept ni moja.

Kuna mashine 9, inayofanya kazi ni moja. Bwawa linatakiwa kuhifadhi maji ya mashine 9.

Sasa kama mashine moja kati ya 9 ndio inafanya kazi, maji mengine hayana sababu ya kuwepo pale, lazima yafunguliwe yaondoke.

Iwapo mashine zote 9 zingekua zinafanya kazi basi hayo maji bado yasingetosha.

Ni serikali kuhakikisha mashine zote zinawashwa kwa wakati mmoja tu ama vinginevyo yale maji yote yatapotea bure.
Maelezo ya Kitapeli tu haya. Tuliwambia ccm imezeeka haiwezi tena kuleta mabdiliko ndani Nchi.

Wanachojua wao ni ufisadi, wizi wa mali za umma, kuteua na kupeana vyeo tu.
 
Storage facilities za umeme wa megawatt 200 mpaka 1000 ni kama zipi? Mabetry 1000,000 ya gari yatumike kutunza charge? Kuna vifaa gani special?

Kila mwenye betri la la gari asiye na kazi nalo,tunaliomba
Pekeni huo umeme unaozidi hata Malawi au Zambia au kenya bure au wauzieni kwa bei ndogo mbona akili hamna nyie
 
Hayo yote hawakuwa wameyaona awali?

Hakukuwepo na contingency plans zozote zile kuhusu maji kuwa mengi?
Walijua kwasababu maneno haya ''Saddle dam' niliyapata wakati wa kufuatilia ujenzi
Ukiangalia clip za awali za ujenzi kuna 'saddle dam' mbili zimejengwa kwasababu ya kudhibiti maji yakizidi

Sasa tunaposikia haya kwakweli lazima tukubali kwamba Waafrika hatuwezi kujitawala
Kwamba umeme hakuna kwasababu maji yamejaa! Kama si upuuzi ni ujinga wa hali ya juu sana

Anayesema hayo bila aibu si yule fundi wa VETA ni Naibu Waziri mkuu!

JokaKuu
 
Back
Top Bottom