DP World anapewa kazi ya kupakua na kupakia Makontena tu, sio Bandari yote ya Dar wala si nje ya Dar

DP World anapewa kazi ya kupakua na kupakia Makontena tu, sio Bandari yote ya Dar wala si nje ya Dar

Wewe ni mjinga na hujui chochote zaidi ya uchawa! Na ndio maana unaita " Bandali"!

Huwezi ku- run Bandari bila storage! Kuna watu mzigo unafika hajapata fedha za kulipia mzigo wake na hivyo lazima Bandari iu- store huo mzigo kwa gharama za mteja (demurrage ).

Vijana wa UVCCM hakuna mnachojua kwenye dunia ya uchumi!
Nyie fanyeni kazi za Uchawa mkivizia teuzi basi!
Asante kwa matusi. Pia samahani kwa typing errors.

Sasa turudi kwenye hoja.

Bandari yetu ni ndogo ni kama Mwaro tu. Meli kupakua hadi zisubiriane kule maji marefu. Bandari yetu inakosa ufanisi na Teknolojia ndo maana unaona mambo ya Storage. Meli inapakuliwa mzigo kwa siku nne badala ya siku moja kwa ukosefu wa vifaa. Unaenda kutoa mzigo unaambiwa system ipo down. Au unaenda kutafuta Kontena lako haulioni wala haujui lipo ICD ipi unatumia hata wiki kulitafuta. Halafu ukienda unakuta storage ya kufa mtu watu wanaamua kutelekeza mzigo.

Kingine mifumo ya bandari haisomani. Inafanya mzunguko leo upo TRA kesho upo Bandari kitu kilekile.

Nchi ikasema hapana. Tutafute mtu wa kuendesha ili kuwapunguzia usumbufu watanzania.

Pale Kurasini kuna eneo la EPZ Authority, anapewa na kutengeneza ambapo mizigo yote itachukuliwa pale. Wa Mikoani zipo Bandari kavu zishaanza kujengwa Pwani na Dodoma. Malori hakuna haja ya kufika Dar.

Yaani Kontena ikifika Bandarini kila kitu kinakuwa tayari. Yaani mzigo unapakiwa kwenye meli ukishalipa kila kitu. Yaani ni kushusha na kuchukua mzigo wako. Ni kama mwendo kasi, ikifika ni kupanda sababu tiketi ushalipa mapema. Na pale EPZA utapewa muda wa kutosha wa kuchukua muzigo. Ukichelewa kwa muda ndo utaanza lipishwa storage
 
Salaam Wakuu,

Wote tunaijua Bandari ya Dar Es Salaam.
View attachment 2658109
Watu walidanganya eti kuanzia Geti namba moja hadi namba 8 anapewa DP World kumbe uongo. DP World anapewa kazi ya kupakia na kupakua Makasha kama ilivyokuwa kwa TICTS si kwamba anapewa bandari yote ya Dar, anapewa kijisehemu tu.

Kwahiyo TPA ataendelea na kazi ya kupakua Magari, Mafuta nk.

Pili DP World anakuja na Teknolojia ambayo itawezesha Mifumo ya TRA, TASAC, TPA isomane. Yaani mzigo wako ukifika unachukua hapo hapo hamna mambo Storage wala gharama zimezidi.

Hawa wanaopiga kelele ni watu waliokuwa wanategemea hela za storage hawa wenye bandari kavu. DP World yeye kwenye hatakuwa na mambo ya storage sababu hadi mzigo unafika unakuwa ushalipia kila kitu.

Nimefafanuliwa na Mwanasheria wa bandari baada ya kumtwanga swali.

Nimewapenda bure DP World.

Sasa hawa wanaopotosha wana dhamira gani?

Sema kuna wengine wanapinga sababu walishalishwa matango pori ukizingatia haya makubaliano ya awali yapo kwa lugha ya Kimombo.

Ukweli ni kwamba hadi sasa hakuna Mkataba umesainiwa wala hakina kitu kilicho chukuliwa. Hata huu Mkataba wa Mashirikiano ya Nchi kwa Nchi ambayo wanataka yawe na Ukomo nayo hayajatiwa saini.

Wanasiasa nao washapata sehemu ya kupepetea mdomo.

Natamani kuona Watanzania tukishikamana kwa manufaa ya Watoto wetu. Tuache kuishi kama zamani.

Sasa hivi TPA inapakua Kontena laki 6 kwa Mwaka. Ila DP World watapakua Makontena Mil 2 kwa Mwaka.

Sasa hivi baandali inachnagia pato la taifa kwa 35% lakini DP World wakianza Bandari ya taifa itachangia 97%

Hii itafanya Watanzania wapumue na mambo ya tozo. Nchi inatoza tozo hadi kwenye Miamala sababu hakuna vyanzo vya mapato vya kueleweka na Nchi lazima iendelee.

Ajabu ni kwamba Wanaoongoza kwa kuiponga DP World mitandaoni ni Wakenya sababu wanajua hii ni vita ya Kiuchumi. DP World wakianza bandari za Kenya hawana chao. Hata waliokuwa wanapinga bomba la Mafuta Mafuta Uganda kuja Tanzania ni Wakenya hadi wakaandamana Ulaya huko eti litaharibu Mazingira.

Watanzania tujitafakari na tujielewe.

Kila kitu kina mazuri na Mabaya, kwanini Wakenya wanaona Ubaya wa DP World tu?

Bila uzalendo tutaishia hapa hapa kulaumiana. Sasa hvi Mwarabu ndo mwenye hela ndo maana hata timu za Mpira za Uingereza anapewa Mwarabu. Hata Bandari zao wamempa Mwarabu lakini sisi wabongo Bandari tunataka eti tumpe Singa singa na Kanjibhai.

Tujaribu Waarabu japo miaka 5 tuone.
View attachment 2658110
Serikali iachane na huu mradi,watu wanataka waendee kuwa maskini mnalazimisha kuwatoa Ili iwaje? Acha wawe wanalipa gharama kubwa za usafiri,siku za kusubiria na urasimu kama huo.
 
Mkuu, watu wanapotosha, hakuna Mkataba uliojadiliwa. Wakianza kujadili Mkataba ndio wataweka muda. Haya ya sasa ni Maazimio tu ya kufanya biashara ya bandari kati ya Nchi na Nchi. Hata Bunge limepitisha maazimio. Kama maazimip yakikubalika ndipo mikataba sasa inaanza. Yaani hii ni kama barua ya Posa, bado mwali kuolewa.
Wewe kumbe hakuna kitu kabisa.

MoU ilisainiwa Februari 2022.

Mkataba mkuu ulisainiwa October 2022.

Iliyobakia kusainiwa ni mikataba midogo ya utekelezaji, ambayo kimsingi lazima iongozwe na mkataba mkuu.

Naona hapa JF tuna watu wenye uelewa duni sana kwenye mambo mengi.

Baada ya kusaini mkataba mkuu, hakuna mkataba mwingine wowote utakaoletwa bungeni. Hiyo mjkataba midogo ya kisekta itasainuwa kwa siri na itakuwa mikataba ya siri. Hivyo ndivyo mkataba mkuu unavyoeleza. Mkataba huu ndiyo mwongozo mkuu.

Kama hulijui hata hilo, pole sana. Hatuna namna ya kukusaidia, bakia hivyo hivyo, waache wanaoelewa waendelee kupigania ulindwaji wa rasilimali za nchi.
 
Kuna kikubdi cha wanasiasa ndo wanapotosha na wala hawana utalaamu wa mambo haya...Eti bandari zinauzwa !

Ujinga tu kuleta hofu kwa watu .
Nadhani huu ni muda sahihi kuwaita Wanasiasa wa vyama vya siasa na kuwaelewesha. Walioeleweshwa na Wabunge ambao wote CCM. Mwanasheria wa Serikali waite vyama vya upinzani wawaeleweshe na wajibu maswali yao.

Wengi wanaenda na upepo wa Propaganda za Kenya na wale wasiotakia mema Nchi.

Watanzania wavivu wa kusoma. Wakishasomewa unampa title tu habari anajua mwenyewe. Pia ingekuwa vizuri haya makubaliano yandikwe kwa kiswahili. Watanzania washazoea wanapigwa hivyo kila mkataba wanajua ni wezi. Wangetafsiri kiswahili kila mtu akausoma, wanapropaganda wangekosa sehemu ya kupotosha. Eti bandari yote inauzwa mkataba hauna kikomo sijui DP WORLD ni kampuni ya mfukoni yasingekuwepo. Tatizo kubwa ni lugha ya Makubaliano haya.
 
Acha Kupotosha Poyoyo wewe.
Dpw hawapewi eneo katika bandari Bali wanapewa Bandari yote na nyinginezo katika Nchi Yetu.
Kuna Tofauti Kubwa Kati Mkataba wa Ticts Na Mkataba wa Dpw.
Mkataba wa ticts ulikuwa na ukomo kuanzia eneo la kumiliki mpk muda wakuhudumu.
Huu wa dpw hauna ukomo lkn pia anapewa bandari zote za nchi ya Tanzania Kasoro Zanzibar.
Msituone Tu Watoto Kiasi hicho.
Shida kubwa ni kwamba hawa watu kutokana na akili yao ndogo ya kushindwa kuutambua hata uduni wa akili zao, wanaamini watu wengine ni wajinga, tena kuuzidi ule ujinga wao, kumbe wanataka kuwadanganya watu watu wanaowazidi akili hata zaidi ya mara 10.

Lakini wajue kuwa siku zote mwenye akili atashinda. Hawa washenzi wa majukwaani na wale mahayawani wa bungeni, wataanguka wao, na umma utashinda.
 
Waambie waliokutuma wakagawe bandari za Zanzibar na sio Tanganyika
Mkuu mbona TICTS alipopewa hujaleta mambo ya Zanzibar na amekaa miaka Ishirini? Kwanini huyu anayekuja kufanya kazi za TICTS unaleta Ubaguzi. Sema hii Ishu ya DP World imesaidia kujua kwamba Tanzania bado kuna Ubaguzi. Yaani kuleta muwekezaji ni kugawa? Mbona TICTS alipokuwepo hukusema hivyo.? Nahisi bado umelipotoshwa
 
Narudia tena na tena hoja yangu kwamba "Miaka nenda rudi uchimbaji madini unafanywa na makampuni ya nje kwa mikataba ya aina ya IGA, je, nchi imepiga hatua gani kiuchumi".

Mategemeo hayo unayodai ni ndoto za alinacha.
Ile Mikataba ilikuwa siri. Lakini huu umekuwa wa wazi hadi wewe unapata nafasi ya kutoa maoni. Namshukuru rais Samia kwa Uwazi huu. Iendelee hivi hata mikataba mingine. Tofauti ndo hiyo. Huu hautakuwa na Usiri kama hiyo ya madini, mafuta na Gesi. Je hilo si jambo jema mkataba kuwekwa wazi?
 
Khaaa yani wee ndo unawaimbisha zaidi singeri watanzania unawapeleka kushoto
Kulia ni wapi? Natamani kupata mtu tubishane kwa hoja. Mfano umeona nawapeleka kushoto, unaandika hoja inayo wapeleka kulia then waamue waende kushoto au kulia.
 
Sasa hapa umekosa point. Umetoka kwamba bandari imeuzwa umeanza kusema na nchi imeuzwa. Makubwa haya.
Wewe ni mtoto mdogo? Kuuza Bandari zote ni kuuza nchi. Hivi slaa na vitu vya hovyo haviwezi kupenyezwa kupitia Bandari na nchi kusambaratishwa? Kuwa CCM ni KAZI sana
 
Salaam Wakuu,

Wote tunaijua Bandari ya Dar Es Salaam.
View attachment 2658109
Watu walidanganya eti kuanzia Geti namba moja hadi namba 8 anapewa DP World kumbe uongo. DP World anapewa kazi ya kupakia na kupakua Makasha kama ilivyokuwa kwa TICTS si kwamba anapewa bandari yote ya Dar, anapewa kijisehemu tu.

Kwahiyo TPA ataendelea na kazi ya kupakua Magari, Mafuta nk.

Pili DP World anakuja na Teknolojia ambayo itawezesha Mifumo ya TRA, TASAC, TPA isomane. Yaani mzigo wako ukifika unachukua hapo hapo hamna mambo Storage wala gharama zimezidi.

Hawa wanaopiga kelele ni watu waliokuwa wanategemea hela za storage hawa wenye bandari kavu. DP World yeye kwenye hatakuwa na mambo ya storage sababu hadi mzigo unafika unakuwa ushalipia kila kitu.

Nimefafanuliwa na Mwanasheria wa bandari baada ya kumtwanga swali.

Nimewapenda bure DP World.

Sasa hawa wanaopotosha wana dhamira gani?

Sema kuna wengine wanapinga sababu walishalishwa matango pori ukizingatia haya makubaliano ya awali yapo kwa lugha ya Kimombo.

Ukweli ni kwamba hadi sasa hakuna Mkataba umesainiwa wala hakina kitu kilicho chukuliwa. Hata huu Mkataba wa Mashirikiano ya Nchi kwa Nchi ambayo wanataka yawe na Ukomo nayo hayajatiwa saini.

Wanasiasa nao washapata sehemu ya kupepetea mdomo.

Natamani kuona Watanzania tukishikamana kwa manufaa ya Watoto wetu. Tuache kuishi kama zamani.

Sasa hivi TPA inapakua Kontena laki 6 kwa Mwaka. Ila DP World watapakua Makontena Mil 2 kwa Mwaka.

Sasa hivi baandali inachnagia pato la taifa kwa 35% lakini DP World wakianza Bandari ya taifa itachangia 97%

Hii itafanya Watanzania wapumue na mambo ya tozo. Nchi inatoza tozo hadi kwenye Miamala sababu hakuna vyanzo vya mapato vya kueleweka na Nchi lazima iendelee.

Ajabu ni kwamba Wanaoongoza kwa kuiponga DP World mitandaoni ni Wakenya sababu wanajua hii ni vita ya Kiuchumi. DP World wakianza bandari za Kenya hawana chao. Hata waliokuwa wanapinga bomba la Mafuta Mafuta Uganda kuja Tanzania ni Wakenya hadi wakaandamana Ulaya huko eti litaharibu Mazingira.

Watanzania tujitafakari na tujielewe.

Kila kitu kina mazuri na Mabaya, kwanini Wakenya wanaona Ubaya wa DP World tu?

Bila uzalendo tutaishia hapa hapa kulaumiana. Sasa hvi Mwarabu ndo mwenye hela ndo maana hata timu za Mpira za Uingereza anapewa Mwarabu. Hata Bandari zao wamempa Mwarabu lakini sisi wabongo Bandari tunataka eti tumpe Singa singa na Kanjibhai.

Tujaribu Waarabu japo miaka 5 tuone.
View attachment 2658110
Kwa mkataba upi unao refer?
 
Nimekulia makuzi na madhira na maudhi ya muwekezaji hewa anaitwa Anger trust lmtd asie na ofisi wala anuani. Siwezi kuwa sehemu ya kuunga mkono wawekezaji kutoka bala asia daima dumu.
Pole sana Mkuu. Wasiwasi ndio akili ila hawa sisi sio wa kwanza, ingia Google uangalia. Hapo Rwanda washatengeneza bandari ya Nchi kavu japo Rwanda haina bahari.

Kagame anataka mizigo kutoka Tanzania na Kenya, Nchi za Burundi, Kongo, Malawi Uganda anawasaidia Uwakala inachukuliwa kwake. So wengi wanampinga DPW Tanzania ni Wanyarwand walio bongo. Sababu wanajua akija Tanzania bandari yao ya Nchi kavu kaina kazi.
20230615_091109.jpg
20230615_091120.jpg
 
Mkuu kama kweli itakuwa vizuri lakini hapo umechanganya mhe! Waziri alisema ni 67% wewe umesema 97% yupi yupo sahihi?

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
Inawezekana nipo sahihi au Waziri akawa sahihi pia. Mkuu, kwa sasa Bandari ndo inachangia pakubwa kwenye pato la taifa yaani 35%-37% ambayo ni Trilioni 7 kwa Mwaka. DP World matarajio ni kwamba bandari itaweza kuingiza Trilioni 26 kwa Mwaka ndo maana nikasema 97%.

Kama Trilioni 7 ni 35%) Je, Trilioni 26 itakuwa ni asilimia ngapi? Nimepiga hesabu hivyo nikapata 97% Makadirio

Nimefanya kupiga hesabu. Wanasema ufanisi utakuwa mara 3 ya sasa. Ndo maana nikasema makadilio ya 97% hata mara mbili itakuwa 74% si mbaya.
 
Mim niliyajua haya. Kwanin wakenya ndio wapinge.sisi tulikua twasubir gar imekuja mara ipo sijui icd gan mara icd gan usumbufu mtindo mmoja.mwisho bond.waje dp kwanza middle east huko ndio kuna mapesa kwa sasa,
Hata mimi nashangaa. Wakenya wamefanikiwa kuwashika Masikio Watanzania kwenye hili. Walijaribu kuleta propoganda kipindi cha Bomba la Mafuta la Uganda to Tanga na Bwawa la Nyerere wakashindwa.
 
Inawezekana nipo sahihi au Waziri akawa sahihi pia. Mkuu, kwa sasa Bandari ndo inachangia pakubwa kwenye pato la taifa yaani 35%-37% ambayo ni Trilioni 7 kwa Mwaka. DP World matarajio ni kwamba bandari itaweza kuingiza Trilioni 26 kwa Mwaka ndo maana nikasema 97%.

Kama Trilioni 7 ni 35%) Je, Trilioni 26 itakuwa ni asilimia ngapi? Nimepiga hesabu hivyo nikapata 97% Makadirio

Nimefanya kupiga hesabu. Wanasema ufanisi utakuwa mara 3 ya sasa. Ndo maana nikasema makadilio ya 97% hata mara mbili itakuwa 74% si mbaya.
Sawa mkuu mm binafsi nilikuwa na doubt hii issue mwanzo after kuangalia Bunge nikatolewa tongo tongo atleast kidogo saivi Niko katikati japo sio sana DP world watupe Tu assurance ya ajira Kwa wazawa wasije wakajazana warabu tupu kitu ambacho kitaua ajira Kwa wazawa

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom