DP World kuchukua Eneo la Chuo Cha Polisi Kurasini

DP World kuchukua Eneo la Chuo Cha Polisi Kurasini

Duh, hivi kweli wewe ni Mtanzania? Mbona kila hoja inayoigusa DPW unajitokeza kutetea? Hivi una maslahi gani na hao wageni?

Unakata sana aise
Hawa wa hivi huwa wapo sana. Huwa hawako serious, wanapenda kuleta utani kwa kila jambo, kwao hiyo ni furaha kufanya hivyo. Huwa always wako vizuri tu kwa sababu hawawi na stress.
 
Kweli samia umeamua kushupaza shingo? Sitasema tena juu ya hili ! KWA jiwe tulimshauri abadilike akashupaza shingo mpaka nikaandika hapa menemene tekel na persin!!!! Kwako mama samia sitaandika haya ila mpaka nione kweli dp wamepewa hizo exclusive rights ikitokea hivyo nitanawa mikono juu yako na sitakuwa na hatia juu yako nitakususa na kumuachia Mungu.
Acha mikwara mbuzi wewe.
 
Duh, hivi kweli wewe ni Mtanzania? Mbona kila hoja inayoigusa DPW unajitokeza kutetea? Hivi una maslahi gani na hao wageni?

Unakata sana aise
Hata mimi naona Kuna watu wanajifanya wabongo kumbe sio , lengo lao sio zuri kabisa
 
kama wanachukua hilo eneo, serikali si ndio inatakiwa ilipe kutokana na makubariano ya mkataba, au
 
Bandari ndio mlango wa nchi. Tunawapa wageni funguo, milango ya Tanzania bila sisi kuwasimamia, kuwa na oversight. Madawa, silaha, wanyama, madini, watu watapitishwa jinsi DP World inavyotaka.
Hata kuchuku Twiga, Pundamilia , Simba wote . Kinana atakuwa mratibu.
Serikali bado inaendelea kusimamia bandari na pale wanapewa baadhi ya operations tu sio sehemu yote. Suala la ulinzi na usalama 24/7 lipo chini ya vyombo vyetu msipende kuongea mambo ambayo hayapo.
 
Duh, hivi kweli wewe ni Mtanzania? Mbona kila hoja inayoigusa DPW unajitokeza kutetea? Hivi una maslahi gani na hao wageni?

Unakata sana aise
Hao wameshaambiwa Watajengewa Misikiti akili zao zote zishafiringwa sio wao tena bali ni UTI tupu ndizo zinaongea
 
Shupazeni shingo na kujibu uharo, mama yenu mtampoteza. Na zipo tabiri kwamba anaweza asimalize mihula miwili. Jiwe alishupaza shingo, mdanganyeni macho kumchuzi naye ashupaze shingo.
Tulia wewe huyu mama hana roho mbaya kama yule jamaa . Samia mpaka 2030 hutaki hama nchi.
 
Hayo malori Yao yatasindikizwa na Nani toka bandarini Hadi mpakani?
Watayatafutia barabara Yao au Ni hii hii? Yatapita Iyovya? Haya ya kwetu ya transit yatafanya kazi gani?
Kuna mtu somewhere amechoka kazi.
 
Mambo ya mkataba yameanza utekelezaji haraka sana, huku mipango ikianza kufanyika Ili ndugu zetu DP world waanze kufanya kazi mara moja.

Sijui mambo ya Mikataba, lakini DP world katika mkataba wao watachukua pia Eneo la Chuo Cha Polisi Kurasini Kinachosimamiwa na kamishna Msaidizi Mambo Sasa.
Sijajua kwanini serikali haitagazi hatua mbalimbali zinazoendelea za utekelezaji wa mkataba huu , ambao Umekuwa ukipingwa Kwa nguvu na watu wanna, Mwabukusi, Slaa, Padri kitima na Mdude.

Wataalamu Wa serikali na wawakilishi wa DP world walitembelea maeneo ya chuo Cha Polisi Kurasini na kufanya na kuchua vipimo vya mipaka, huku dp world ikijiandaa kulipa fidia zote za uhamishaji wa chuo hicho Cha jeshi.

Jingine linaloendelea , ambalo silijui rasmi. Ni kuwa DP world ataingiza magari zaidi ya 2000 yaani maroli Kwa ajili ya kisafirisha mizigo nje ya nchi, inavyosemekana DP world ndio atakuwa transporter pekee wa kisafirisha mizigo nje ya nchi, na watanzania watabaki Tanzania.

Hizi ni habari zinaukweli lakini nashangaa kwanini Serikali ya Chama Tawala haitoi maendeleo ya utekelezaji wa mradi huu ambao unaendelea kimya kimya kama alivyosema Mangwea "KIMYA KIMYA"
 

Attachments

  • F6F6765B-1913-45FC-9A24-8A5E42AF5E44.png
    F6F6765B-1913-45FC-9A24-8A5E42AF5E44.png
    84.3 KB · Views: 3
  • IMG_2047.MP4
    1.2 MB
Habari hii kama ni ya kweli basi inasikitisha sana..... ila Malori 2,000 hayatoshi kufanya supply za mizigo ndani na nje ya nchi hii.
 
Back
Top Bottom