DP WORLD: Mkataba wa Bandari kwa Kiswahili (tafsiri isiyo rasmi)

K
Kwa hiyo sasa?. Sisi tunaujua na tumeukubali. Acha kuhangaika.
 
Kwa DP world ni kitu gani na kitu gani kilipitishwa bungeni kuhusiana na DP wolrd na Serikali ya Tanzania wewe bibi kizee mwenye **** chafu?
Soma kisha useme una tatizo na haya:

UTANGULIZI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
iliyowakilishwa ipasavyo na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi (“Tanzania”) na SERIKALI YA DUBAI, iliyowakilishwa ipasavyo na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Bandari, Forodha na Ukanda Huru (“Dubai”);

(Tanzania na Dubai baadaye zinarejelewa kama “Nchi Wanachama” (kila moja kama “Nchi Mwanachama”):

(A) KWA KUZINGATIA ziara ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu, Dubai Expo 2020 na kikao alichofanya na Mtawala wa Dubai Februari 2022 kuhusu fursa za uwekezaji nchini Tanzania;

(B) KWA KUZINGATIA Mkataba wa Makubaliano (MoU) kati ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na DP World (DPW) uliosainiwa katika ziara ya Mh. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Maonesho ya Dubai 2020 (Dubai Expo) tarehe 28 Februari, 2022;

(C) KWA KUZINGATIA matakwa yaliyotolewa katika Mkataba wa Makubaliano kuhusu maeneo ya ushirikiano kati ya TPA na DPW kwa ajili ya kuendeleza na/au kuboresha uendeshaji na usimamizi wa miundombinu ya kimkakati ya Bandari za Bahari na Maziwa Tanzania, kanda maalum za kiuchumi, hifadhi za usafirishaji na ukanda wa kibiashara wa Serikali ya Tanzania;

(D) KWA KUTAMBUA nia ya Serikali ya Tanzania ya kuhimiza uwekezaji ili kuendeleza na kuboresha utendaji na ufanisi wa bandari za bahari na maziwa ili kuendana na dira ya Serikali na mwenendo wa kimataifa wa huduma za usafiri
wa baharini;

(E) KWA KUZINGATIA matakwa ya Serikali ya Tanzania kutumia fursa na kufaidika na eneo lake la kijiografia katika usafiri wa baharini na kufungua uwezo wake wa soko katika ukanda huu kwa kuhudumia nchi zilizounganishwa na ardhi kupitia kuimarisha ushindani wa bandari na kuboresha shughuli za kijamii na kiuchumi;

(F) KWA KUTAMBUA uwekezaji mkubwa wa Serikali ya Tanzania uliofanywa katika kuboresha miundombinu na miundo mikuu ya aina mbalimbali nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na Mradi wa Dar es Salaam Maritime Gateway (DMGP) na Standard Gauge Railway (SGR) na matakwa yake ya kufikia faida katika uwekezaji huo, kuimarisha utendaji wa bandari na kuchochea ukuaji wa uchumi kwa ajili ya ustawi wa watu wa Tanzania na ukanda huu;

(G) KWA KUTHAMINI mabadiliko ya huduma za usafiri wa baharini yaliyofanywa na Serikali ya Dubai kupitia DPW ambayo yalisababisha huduma za usafiri wa baharini kuwa mchangiaji mkubwa wa Pato la Taifa la Dubai (GDP)

(H) KWA KUTAMBUA kwamba DPW ni kampuni yenye uzoefu na yenye sifa na uwezo wa kimataifa katika ukuzaji wa bandari, usimamizi, uendeshaji na mtoaji wa suluhisho la ugavi;

(I) KWA KUZINGATIA mikataba mbalimbali ya miradi inayokusudiwa na Nchi Wanachama kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali itakayokubaliwa kupitia Mikataba ya Serikali Mwenyeji (HGAs), mikataba mahususi ya maafikiano au
mikataba mingine ya miradi kati ya Tanzania na kampuni husika za mradi;

(J) KWA KUZINGATIA kuwa Nchi Wanachama zinataka kuingia katika Mkataba huu ili kuweka mfumo shuruti wa manunuzi na utekelezaji wa Miradi mbalimbali inayokusudiwa katika Mkataba huu.

KWA HIYO SASA, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai zinapenda kuingia katika Mkataba huu ili kuwezesha malengo ya pande zote za Nchi Wanachama kama ilivyoainishwa hapa chini
 
Mijadala hii ni mizuri sana tatizo imegawanya makundi na kila kundi linamashabiki wa kutosha na badala ya kutoa hoja imekuwa ni kuunga hoja kwasababu tu aliyetoa ni kundi lao.

Kwakuwa jambo hili pia Mahakama imefikishiwa ni sehemu sahihi zaidi ili tupate tafsiri nzuri ya hiki kinachoendelea.
 
Sioni shida ya mkataba kwa jumla ila kuna baadhi ya vipengele vinaukakasi hasa kwa upande wetu inabidi kuviweka sawa kabla ya kuingia kwenye HGAs.
 

Kama wameshaingia kwenye huo mkataba hiyo tenda inatangazwa ya nini?
Mbona unajichanganya, na hueleweki.
Utatangazaje tenda ya kitu ambacho umeshaingia na mtu mkataba akifanye?
Huo si utapeli
 
Sioni shida ya mkataba kwa jumla ila kuna baadhi ya vipengele vinaukakasi hasa kwa upande wetu inabidi kuviweka sawa kabla ya kuingia kwenye HGAs.
Hakuna kipengele cha kuwekwa sawa. Kipengele ki[i unakiongelea ambacho hakina jibu kwenye mkabata wenyewe?
 
Linapokuja suala la udini mleta post uko vizuri sana
 
DPW DEAL IS NOT REAL
Ni kundi la watanzania wanataka kujimilikisha biashara ya Bandari kwa mgongo wa DPW

Niliposikia watu wanalalamika kuhusu huu mkataba na kueleza ubaya wake, sikuwaelewa. Nililazimika kuutafuta na kusoma mwenyewe mwanzo mwisho. Baada ya kusoma mara kadhaa na kuelewa, comment yangu ya kwanza niliyoitoa ilikuwa kwamba Rais na Waziri waliwekwa kwenye poisoned room kwa ajili ya majadiliano au walipewa kahawa ilokuwa na sumu ya kufifisha uwezo wao wa akili huku wenzao wa upande wa pili wakiwa na protectives. Sikuelewa kwa nini waliweza saini mkataba huu ambao ni one sided.

Wabunge walinichefua zaidi na kunitafakarisha. Niliwapuuza kwa kuwa ni kawaida yao kuunga juhudi kwa manufaa yao binafsi hasa ya kutetea nafasi zao za kugombea tena.


Nilipomuona Rostam Azizi anajitokeza kuunga mkono tena kwa nguvu zote, ilinifanya nitafakari zaidi nikikumbuka kashfa zake ambazo zilimfanya apotee kabisa kwenye ulingo wa siasa. Katika tafakuri yangu, nilianza kuhisi uwepo wa upigaji mwingine kama wa kipindi kile cha makampuni hewa.

Nimekuwa nikijiuliza, hivi Serikali yetu kweli ni kipofu kiasi hiki kwa vitu vilivyo wazi?
Kwa nini DPW inapewa upendeleo kiasi hiki?
Kwa nini serikali inatumia nguvu nyingi kiasi hiki kuipamba DPW? Kizuri si hujiuza?
Kwa nini serikali inapuuza sauti ya wengi, wataalam, wananchi na kuwapoza kwa kusema itafanyia kazi maoni yao richa ya kwamba wanajuwa kuwa hakuna nafasi ya kufanya hivyo kwa mujibu wa mkataba huu?

Kimsingi, Serikali imeamua kuwapuuza wananchi bila kujali madhara yake. Kuthibitisha hili, Rais kaamua kupeleka hili jambo kwenye kamati kuu ya CCM ili kulipa nguvu zaidi na kulifanya kuwa la chama, siyo la Rais na Serikali yake tu. Hii linathibitisha kupuuza sauti ya wananchi.

Swali linakuja, kwa nini Serikali inapuuza sauti ya wananchi?

Jibu langu kwenye swali hili ni rahisi sana. Hili ni deal la watu wetu wa ndani. Ndo maana wanaomba tuwaamini; kinachotupa hofu kwamba waarabu watamiliki milele haiko hivyo. Ni watanzania wachache ndiyo watakaokuwa wanamiliki, na wamejiwekea ulinzi kupitia huu mkataba ili vizazi na vizazi vyao viendelee kufaidi. Hakika, ni wajanja sana.

Nini kinathibitisha jibu langu?
1. Mkataba kwa ujumla wake kuwa one-sided.
2. Mkataba kutokuwa na thamani halisi ya uwekezaji
3. Mkataba kutokuonesha Tanzania itanufaika kwa kiasi gani
4. Kutokuwepo kwa physibility study ambayo ingeonesha kiasi cha investment kinachohitajika kufikia desired standards na expected profit na mgawanyo wa faida.
5. DPW kuwa kutamkwa kwenye mkataba kuanzisha kampuni au makampuni mengine ambayo yatasajiliwa Tanzania, ambayo yatajulika kama project companies na affiliates zake ambazo pia zitakuwa na hadhi na haki sawa na DPW.
6. Kutambuliwa kwa Investor kama any project company and their affiliates na/au mtu yeyote mwenye hisa kwenye hizo project companies zitakazoanzishwa.
7. Kutamkwa kwenye mkataba Ibara ya 4, kifungu kidogo cha 5, kwamba DPW na washirika wake watakuwa na jukumu la kutafuta fedha kwa ajili ya miradi husika. Hii inamaanisha kwamba DPW tunaeambiwa ni giant kwenye shipping na logistics kajitoa kwenye kufadhili miradi yote. Na huenda ndo maana upembuzi yakinifu na kiasi kitakachowekezwa hakijulikani.
8. Kulazimisha kuwa na IGA na nchi isiyo na mamlaka kamili ili wawe na ulinzi, kwamba Serikali ikiamua kuvunja mkataba na pengine kutaifisha mali zao baada ya kustukia deal, wanaweza tumia huo mwamvuli wa sheria za kimataifa kukomboa mali zao.
9. Kwenye kusaini, mashahidi pande zote mbili hawakuandika majina yao. Huenda hawakutaka kuja kuwa responsible. Kwa nini tusiwajuwe kwa majina?
10. Kutokuhusika kwa Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Africa mashariki ambae ndiye as nahusika na uhusiano wa kimataifa. Mbalawa tungemuona anasaini HGA.
11. Sababu ya kwamba hata kama mahusiano ya kidiplomasia yakivunjika mkataba huu utaendelea kuwepo. Imewekwa hivyo kwa sababu hizo kampuni za miradi zitakuwa ni za wabongo, huo uhusiano wa kidiplomasia hautawahusu.
12. Kulazimisha kufanya marekebisho kwenye sheria ya ulinzi wa raslimali zinazohusisha usafirishaji wa majini na kuruhusu kupitishwa kwa raslimali nyingine asili ambazo hazijavunwa Tanzania. Hii itawapa nafuu ya kupitisha vitu vingine vya kimagendo kwa kuwa mnyororo wote za usafirishaji majini utakuwa chini yao. Unakamata magogo wanakwambia yametoka Zambia. Hatari sana.
13. Nguvu nyingi iliyotumika kulipamba hili jambo ikiwa ni pamoja na kupeleka wabunge na waandishi Dubai; Serikali kuendelea kutetea hadi kulipeleka kwenye kamati kuu na kutoa maazimio ya kuendelea na mchakato.
14. Kutokuwepo kwa commitment ya UAE kwenye mkataba ambao ni wa mahusiano ya Kimataifa, au hata Dubai kama Serikali. Badala yake kampuni ndiyo imekuwa subjected kwenye commitment. Poor we Tanzanians! Yaani unapeleka mkataba kufanya ratification bungeni kama mkataba wa Kimataifa halafu upande wa pili wametuwekea kampuni, seriously?
15. DPW kupewa Gati 0 hadi 7 ambapo tumewekeza kiasi cha tirioni moja, mkopo kutoka World chini ya mradi wa DMGP. Mradi huu umeboresha sana miundombinu. Kwa nini wasiwape kujenga Gati 12 hadi 15 au kule Bagamoyo kama ilivyo kwenye Ilani ya CCM? Ki msingi hawahitaji investment kubwa sana kwenye miradi ya phase 1 kwa kuwa development imefanyika sana. Kinachohitajika ni uendeshaji na usimamizi tu. Mambo ya mifumo kudomana hakuhitaji investment kubwa. After all siku hizi Meli hazizidi siku tatu.

Kimsingi sababu ni nyingi sana kuthibitisha hili.

Jaribu kusoma Article One upate maana ya DPW, Project company, project agreement, investor, entity, person na project activity; ambayo yote yametumika kwenye mkataba. Hawakuwa wajinga kutolea maana.

Tusitegemee kuona kile tunachoelezwa kikitokea kama tutafumba macho na kukubali kushindwa.

Tukatae huu uhuni kwa nguvu zote.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Tanganyika.

C&P
 
Nyagi bapa, napiga glass 2 then narudi tujadili hili Jambo la kitaifa. [emoji125][emoji125]
 

Mkataba upo hapo juu, post #1.

Tuoneshe huo "ukakasi" tuukatie pilipili na ndimu za unga.
 
Mkataba upo hapo juu, post #1.

Tuoneshe huo "ukakasi" tuukatie pilipili na ndimu za unga.
Umekuwa ukipitia hoja nyingi zinazopinga mkataba (ambapo umekuwa ukitoa hoja ya kuwa siyo "mkataba" bali ni "makubaliano") bila kujadili hoja hizo. Unaweka, sasa, tafsiri ya mkataba huo na kudai uoneshwe "ukakasi" uukatie pilipili na ndimu za unga, aluuu! Ebu kuwa mwungwana urejee mijadala hiyo ujibu hoja za wanaoupinga.

Naamini pia, umesikiliza maoni ya viongozi wa vyama vya upinzani kupinga mkataba. Nawaza tu, kwa sauti, kuwa WanaCCM wasipochukua hatua dhidi ya Serikali yao kuitaka irejee yaliyomo kwenye mkataba wa ushirikiano, kabla ya kusaini mikataba ya utekelezaji (HGAs), itawagharimu kisiasa nchini.

Hofu yangu inatokana na ukweli kuwa, wakati wa Awamu iliyopita, upinzani ulipinga utawala waliodai ni wa kidikteta, wapiga kura hawakujali. Utawala wa awamu hii umekuwa ukisifiwa kwa kile upinzani unadai ni utawala wa kidemokrasia. Lakini, lakini, lakini kinachoendelea sasa hivi kuhusu rukhsa inayotolewa na Serikali kwa wageni kuwekeza kwenya rasimali za Taifa, kwa mikataba yenye ukakasi (mkatie pilipili na ndimu za unga) zimewaibua tena viongozi wa upinzani kuipinga Serikali, na wapiga kura wanasikia na kuelewa mbivu na mbichi.

Hivyo basi, tofauti na upinzani dhidi ya Utawala wa Awamu iliyopita, wapiga kura wanasikia na wataamua, siyo tena kuhusu Katiba au maendeleo ya vitu, bali hatima ya rasimali zao.
 
Wewe
Mkataba upo hapo juu, post #1.

Tuoneshe huo "ukakasi" tuukatie pilipili na ndimu za unga.
Sasa Hauaminiki hata kidogo, mwanzo ulikomaa kuwa siyo mkataba hata ulishindwa kusoma hata maneno ya kawaida ya utangulizi sehemu B.

Kwa maana hiyo hata ukioneshwa vifungu vyenye ukakasi hautakubali. Hata hivyo watu wamekuwa wakionyesha mara kwa mara vifungu hivyo ila tu unajifyatua kama hauvioni.

Udhaifu wa mkataba umeekezwa na wengi wakiwemo wataalam wa sheria hasa kwa ujumla wake sasa wewe na wao nani mwenye elimu ya suala husika.
 
Nimeandika mara nyingi sana humu, hakuna maneno ya Kiswahili yanayowea kutafsiri Agreement, unaweza kutafsiri makubaliano unaweza kutafsiri mkataba. Mradi uelewe tu ni mkataba wa nini? Au ,akubaliano ya nini?

Wewe nani alitaka umuamini?

Wewe unapenda mkataba? Sema ni mkataba wa nini?

Mbona mambo myepesi yanawahangaisha nyinyi failures?
 

Hoja nyingi zinafikirisha hasa inayohusu DPW kuanzisha Kampuni za utekelezaji (Project Companies) ambazo mleta mada anahisi ni za WaTz na zitalindwa na IGA


ITAPENDEZA ukijibu hoja za The Burning Spear, bandiko #53 (nimeambatanisha) badala ya majibu ya mkato na matusi, ati nyiyi failures! Kwa nini unajificha nyuma ya majibu ya kitoto?
 
Mtjibu yote tazama video clip ya jana, hakuna kifungu ambacho hakijajibiwa:

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…