DPP amuondolea shtaka Abdallah Zombe

DPP amuondolea shtaka Abdallah Zombe

Felesi siyo Biswalo, angalia ndugu ingawa cheo cha DPP ni kile kile ila watumishi ni tofauti.
Kwa Jaji Dkt Feleshi pale JPM alichemsha, hakuna mtu anaweza muingilia Feleshi eti kwa rushwa, pia jamaa ni mchapakazi balaa, uliza mwanasheria yeyote wa serikali atakuambia bosi wao huyo wa zamani alivyo mwadilifu.
 
Sawa...acha wafarijiane tu hapa duniani kwa kusafishiana majina ila kama kweli alimwaga damu au alishiriki kudhulumu nafsi ya mtu,ataipata adhabu yake siku atakapofunga macho yake.
Mauaji ya wale wafanyanyabiashara yalikikuwa hivi: Kipindi kile walichouawa kulikuwa na wimbi kubwa la ujambazi. Amri ikawatolewa kutoka juu kwenda kwa wakuu wa polisi wa Mikoa yote kuwa ''majambazi washughulikiwe kwa nguvu zote tena ikibidi wauwawe wanapokamatwa bila kufikishwa mahakamani ili kutoa onyo kwa majambazi''. Sasa siku walipokamatwa wale wafanyabiashara kulikuwa kumetokea tukio la ujambazi. Baada ya polisi kuwahisi na kuwakuta na kiasi kikubwa cha fedha wakachukulia (kwa uzembe bila kufanya upelelezi wa kina) ni majambazi. Wale polisi waliowakamata wakawasilina na Zombe kuwa majambazi wamekamatwa. Zombe akatoa amri kuwa ''na wauwawe''. (Kumbuka Zombe alipotoshwa na askari wale waliowakamata wale majambazi na yeye akatoa amri ya kizembe bila kuhakikisha zaidi). Halafu kuna jambo jingine la muhimu ambalo ndilo lililochochea mauaji yao. ie. Polisi waliowakamata waliingiwa na tamaa ya kumega zile fedha walizowakuta nazo. Zile fedha ndizo hasa ziliwapofusha polisi macho ''kuulizia zaidi'' kwani waliona kuwa wakiwaua itakuwa rahisi kwao kumega zile fedha. Hivyo hii kesi si Zombe wala si wale polisi watakaofungwa. Hii ni kwasababu wale waliotoa amri (serikali) wanajua kabisa mauaji yalifanywa kutokana na amri yao japo uzembe ulitumika. Ndio maana siku zote watu wenye weledi wanasisitiza mhalifu yoyote ahukumiwe na mahakama na si vingine.
 
MIMI NILISHASEMA SERIKALI YA RAIS JPM UENDA ITAGONGA MWAMBA NA KUSHINDWA VIBAYA KWENYE VITA VYA UFISADI NA RUSHWA KAMA OFISI YA DPP NA MAHAKAMA WATU WATAKUA WALE WALE.MAFSDI,WAUAJI,MAJAMBAZI WAKISHIKWA NA KUSHTAKIWA OFISI YA DPP NA MAHAKAMA WATAKUA WANAWAACHIA NA KUENDELEA KUPGA HELA,AINGII AKILINI KILA KESI ZA VIGOGO NA ZA PESA NYINGI SERIKALI INASHINDWA WHY?LAKINI KESI YA RUSHWA YA MWENYEKITI WA MTAA KAOMBA RUSHWA YA ELFU KUMI ANAFUNGWA NA MAHAKAMA UTASIKIA INASEMA HILO NIFUNDISHO KWA WENGNE.HAPO HAMNA KITU TUNACHEZEA WAKILI TU.
 
una mshtaki mtu kwa kosa la mauaji, harafu unakuja na rufani ya kosa la kuficha wauaji? DPP anajua anachokifanya kweli?
Hivi ofisi ya DPP kuna wanasheria kweli wanaostahili kuitwa Wanasheria? Rufani ni juu ya kuachiliwa kwenye Kosa la Mauaji halafu unakuja badilisha shitaka hilo katika hatua hii kweli??!! Siyo kosa wala si dhambi kukubali kushindwa katika kesi maana yote ni matokeo. Mwachieni Zombe aendelee na shughuli zake amesumbuliwa vya kutosha sana.
 
Tuna vijana wanasheria wazuri tu wanamaliza vyuo vikuu kila mwaka ingekuwa ni vizuri wapate kazi katika hii ofisi ya DPP.
 
Haki iko mbinguni tu....... ,mnawatia uchungu wanafamilia waliopoteza ndugu zao katika mauaji yale ya kikatili kama kumuachia Zombe mlishamuachia basi muachieni tu atakutana na noma zake siku ya kiama.
 
Hivi ofisi ya DPP kuna wanasheria kweli wanaostahili kuitwa Wanasheria? Rufani ni juu ya kuachiliwa kwenye Kosa la Mauaji halafu unakuja badilisha shitaka hilo katika hatua hii kweli??!! Siyo kosa wala si dhambi kukubali kushindwa katika kesi maana yote ni matokeo. Mwachieni Zombe aendelee na shughuli zake amesumbuliwa vya kutosha sana.

Hivi kumbe hata wao kwa wao wanaweza kubadilishiana kesi???? Nilidhani ni kwa watu wanyonge tuuu!!!!!!!
 
Mwendesha mashataka wa Serikali(DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi MKoa wa Dar, Abdala Zombe.

Amebakiwa na shtaka la kuficha wahalifu.

======================

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na sasa inataka ajibu mashtaka ya kuficha wahalifu.


DPP amefanya mabadiliko hayo kwenye rufaa aliyoikata Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu wa kumuachia huru Zombe, ambaye alikuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) katika mashtaka ya mauaji.

Awali, DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyomwachia huru Zombe na wenzake tisa, katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva mmoja wa teksi wa Manzese jijini Dar es Salaam.

Katika rufaa hiyo, DPP alikuwa anaiomba Mahakama ya Rufani iwatie hatiani washtakiwa hao kwa kosa la mauaji ya kukusudia, kama ilivyokuwa kwenye kesi ya msingi, kosa ambalo adhabu zake ni pamoja na kunyongwa hadi kufa.

Hata hivyo, DPP amebadili msimamo huo dhidi ya Zombe na badala yake anaiomba Mahakama hiyo imtie hatiani kwa kosa la kuwalinda wahalifu ambao walitenda kosa la mauaji ya wafanyabiashara hao na dereva wa teksi.

Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, Timoth Vitalis, ambaye ni Wakili Mkuu wa Serikali (PSA) na Richard Rweyongeza, ambaye ni wakili wa kujitegemea anayemtetea Zombe katika rufaa hiyo, walisema mtu anayepatikana na hatia kwa kosa hilo adhabu yake ni kifungo jela kisichozidi miaka saba.

Kwa maana hiyo, hata kama Mahakama ya Rufani itakubaliana na hoja za rufaa za DPP na kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo jipya ambalo hata hivyo, hakuwa ameshtakiwa nalo kwenye kesi ya msingi, atakuwa ameepuka adhabu ya kitanzi.

DPP alibadili msimamo wake huo dhidi ya Zombe siku ya usikilizwaji wa rufaa hiyo Mahakama ya Rufani mbele ya jopo la majaji watatu, Bernard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage, hivi karibuni.

Mkurugenzi huyo wa mashtaka alifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo la mauaji.

Akizungumzia uamuzi huo wa DPP kumuondoa kwenye shtaka la mauaji kama alivyokuwa akidaiwa tangu awali na sasa kupewa shtaka la kuwalinda wahalifu, Zombe alisema kwanza alikuwa ameonewa kwa kuhusishwa na hatimaye kushtakiwa kwa kosa la mauaji.

Alisisitiza kuwa hakutendewa haki wakati wa kumfungulia shtaka hilo la mauaji kwa kuwa sheria hazikufuatwa.

“Kwanza ni mambo ya ajabu sana. Nimedhalilishwa sana kwa muda wote huo na kuonekana kuwa mimi ni muuaji kila ninakopita, kwa kufunguliwa shtaka ambalo sikuhusika nalo,” alisema Zombe.

“Mimi sikuwapo eneo la tukio na wala nilikuwa siwafahamu watu hao na hata Tume (iliyoundwa na Rais kuchunguza mauaji hayo iliyoongozwa na Jaji Mussa) Kipenka ililiridhika kuwa sikuwepo eneo la tukio. Sasa nilihusikaje na mauaji hayo?”

Zombe aliongeza kuwa washtakiwa wote walihojiwa na kuandika maelezo yao na kwamba huo ndiyo utarartibu wa kisheria.

Zombe alisisitiza kuwa yeye alikuwa mwendesha mashtaka kwa muda mrefu na mkuu wa upelelezi wa mkoa, hivyo anajua taratibu kwa kuwa alikuwa akiandika majalada mengi kwenda kwa Mwanasheria wa Serikali na mengine yalikuwa yakienda mahakamani kama alivyoyaandika.

Kuhusu kosa alilobadilishiwa na DPP wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, Zombe hakuwa tayari kulizungumzia kwa kuwa bado Mahakama haijatoa hukumu.

Kabla ya kumbadilishia shtaka hilo, wakati wa usikilizwaji wa rufaa, DPP alitaka kumuongezea Zombe shtaka hilo kama shtaka mbadala, wakati wa usikilizwaji wa kesi ya msingi.

Hata hivyo, DPP aligonga mwamba baada ya Jaji Massati kumkatalia kwa maelezo kuwa alitakiwa ashtakiwe tangu mwanzo kwa kosa hilo.

Kabla ya kumuondoa Zombe katika kosa la adhabu hiyo ya kunyongwa, kwanza DPP, aliwaondolea washtakiwa wengine watano, baada ya kubaini kuwa ushahidi aliokuwa nao hauwagusi katika rufaa hiyo.

Walioondolewa ni Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abineth Salo na Festus Gwabisabi.

Lakini ameendelea kuwang’ang’ania Zombe na wenzake watatu ambao ni Christopher Bageni, Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.
Hakuna cha ajabu hapo...Huyu DPP ndo jukwaa la maigizo...Hii kesi ilishakwisha..zimebaki stori tu
 
Naandika haya kwa uchungu mkubwa. Ingawa kwasasa sifanyi kazi za kiwakili,nafahamu vyema taratibu za kiwakili kuanzia mahakama ya Mwanzo hadi ya Rufani. Nafahamu kwakuwa nami ni Msomi wa Sheria. Nafahamu kuwa rufaa huchipu,kumea na kujikita kwenye shauri au kesi ya mwanzo. Hakuna nafasi,kwenye rufaa,kuweka mambo au kesi mpya. Hata kama kwasasa nafanya siasa za CCM,hayo nayajua na yamenikaa.

Sasa kuna rufaa katika Mahakama ya Rufani iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini almaarufu kama DPP. DPP anapinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kumwachia huru aliyekuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi Abdallah Zombe na wenzake. Washtakiwa hao ambao sasa ni Warufaniwa walikuwa wakishtakiwa kwa kosa la mauaji. Hakukuwa na shtaka la kuficha wahalifu.

Sasa,zinachomoza ripoti kuwa DPP amewasilisha rufaa yake Mahakama ya Rufani kukiwa na shtaka jipya:kuficha wahalifu. Narudia tena,kama Mwanasheria na kada mbobezi wa CCM,kuwa rufaa haipaswi kuwa na jambo jipya. Kama kinachosemwa ni kweli,DPP must go. Kama kinachoandikwa ni kweli,Zombe na wenzake watashinda kiulaini. DPP sasa ni Ndugu Biswalo Mganga.

Siamini kwanza kisemwacho kwakuwa hakiwezekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Kwani Mzee wangu DPP amekwambia anataka kushinda kesi au anataka HAPA KAZI TU!!!!!!!!!!!!!Ili aonekane anafanya kazi basi hata kesi ya Paka kula panya ataipeleka mahakamani
 
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na sasa inataka ajibu mashtaka ya kuficha wahalifu.

DPP amefanya mabadiliko hayo kwenye rufaa aliyoikata Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu wa kumuachia huru Zombe, ambaye alikuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) katika mashtaka ya mauaji.

Awali, DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyomwachia huru Zombe na wenzake tisa, katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva mmoja wa teksi wa Manzese jijini Dar es Salaam.

Katika rufaa hiyo, DPP alikuwa anaiomba Mahakama ya Rufani iwatie hatiani washtakiwa hao kwa kosa la mauaji ya kukusudia, kama ilivyokuwa kwenye kesi ya msingi, kosa ambalo adhabu zake ni pamoja na kunyongwa hadi kufa.

Hata hivyo, DPP amebadili msimamo huo dhidi ya Zombe na badala yake anaiomba Mahakama hiyo imtie hatiani kwa kosa la kuwalinda wahalifu ambao walitenda kosa la mauaji ya wafanyabiashara hao na dereva wa teksi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Timoth Vitalis, ambaye ni Wakili Mkuu wa Serikali (PSA) na Richard Rweyongeza, ambaye ni wakili wa kujitegemea anayemtetea Zombe katika rufaa hiyo, walisema mtu anayepatikana na hatia kwa kosa hilo adhabu yake ni kifungo jela kisichozidi miaka saba.

Kwa maana hiyo, hata kama Mahakama ya Rufani itakubaliana na hoja za rufaa za DPP na kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo jipya ambalo hata hivyo, hakuwa ameshtakiwa nalo kwenye kesi ya msingi, atakuwa ameepuka adhabu ya kitanzi.

DPP alibadili msimamo wake huo dhidi ya Zombe siku ya usikilizwaji wa rufaa hiyo Mahakama ya Rufani mbele ya jopo la majaji watatu, Bernard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage, hivi karibuni.

Mkurugenzi huyo wa mashtaka alifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo la mauaji. Akizungumzia uamuzi huo wa DPP kumuondoa kwenye shtaka la mauaji kama alivyokuwa akidaiwa tangu awali na sasa kupewa shtaka la kuwalinda wahalifu, Zombe alisema kwanza alikuwa ameonewa kwa kuhusishwa na hatimaye kushtakiwa kwa kosa la mauaji.

Alisisitiza kuwa hakutendewa haki wakati wa kumfungulia shtaka hilo la mauaji kwa kuwa sheria hazikufuatwa.
"Kwanza ni mambo ya ajabu sana. Nimedhalilishwa sana kwa muda wote huo na kuonekana kuwa mimi ni muuaji kila ninakopita, kwa kufunguliwa shtaka ambalo sikuhusika nalo," alisema Zombe.

"Mimi sikuwapo eneo la tukio na wala nilikuwa siwafahamu watu hao na hata Tume (iliyoundwa na Rais kuchunguza mauaji hayo iliyoongozwa na Jaji Mussa) Kipenka ililiridhika kuwa sikuwepo eneo la tukio. Sasa nilihusikaje na mauaji hayo?"

Zombe aliongeza kuwa washtakiwa wote walihojiwa na kuandika maelezo yao na kwamba huo ndiyo utarartibu wa kisheria. Zombe alisisitiza kuwa yeye alikuwa mwendesha mashtaka kwa muda mrefu na mkuu wa upelelezi wa mkoa, hivyo anajua taratibu kwa kuwa alikuwa akiandika majalada mengi kwenda kwa Mwanasheria wa Serikali na mengine yalikuwa yakienda mahakamani kama alivyoyaandika.

Kuhusu kosa alilobadilishiwa na DPP wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, Zombe hakuwa tayari kulizungumzia kwa kuwa bado Mahakama haijatoa hukumu. Kabla ya kumbadilishia shtaka hilo, wakati wa usikilizwaji wa rufaa, DPP alitaka kumuongezea Zombe shtaka hilo kama shtaka mbadala, wakati wa usikilizwaji wa kesi ya msingi.

Hata hivyo, DPP aligonga mwamba baada ya Jaji Massati kumkatalia kwa maelezo kuwa alitakiwa ashtakiwe tangu mwanzo kwa kosa hilo. Kabla ya kumuondoa Zombe katika kosa la adhabu hiyo ya kunyongwa, kwanza DPP, aliwaondolea washtakiwa wengine watano, baada ya kubaini kuwa ushahidi aliokuwa nao hauwagusi katika rufaa hiyo. Walioondolewa ni Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abineth Salo na Festus Gwabisabi. Lakini ameendelea kuwang'ang'ania Zombe na wenzake watatu ambao ni Christopher Bageni, Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.

Source: Mwananchi
Wangeacha kuhangaika tu maana wanapoteza muda na fedha. Ukweli unajulikana nini Zombe na wenzake walifanya lakini udhaifu wa upelelezi na uendeshaji wa mashitaka ndiyo uliofikidha hapo. Ndiyo maaan binafsi nafikiti kuanzidha mahakama maalumu kwa ajili ya makosa fulani ni kuacha uhalisia wa tatizo. Tuwape uwezo hawa, yaani wapelelezi na waendesha mashitaka, na tutashind maovu.
 
rufaa imetupiliwa karibu, unaweza kuiokota na kuirudisha tena kotini
 
Tuna vijana wanasheria wazuri tu wanamaliza vyuo vikuu kila mwaka ingekuwa ni vizuri wapate kazi katika hii ofisi ya DPP.
unaweza kuwalipa?! wanaenda katika makampuni ya sheria yanayolipa vyema.... wana changamoto nyingi za kimaisha, wanafata kwenye mkwanja wa kutosha.
 
Wafanyabiashara waliuawa sinza kwenye ukuta wa posta wakisemekana walikuwa wanatoroka na vile vile hao askari waliofanya mauaji walikubali kuwa walitumwa kufanya hvyo. Mpaka mwaka 2010 askari hao wapatao tisa walikuwa washafariki mmoja mmoja kwa nyakati tofauti wakiwa ktk harakati za kutoa ushahidi nakumbuka alibaki mmoja ambaye hali yake kiafya haikuwa nzuri hvyo kupelekea naye kufariki, na mchezo ukaishia hapo.
 
Mwendesha mashataka wa Serikali(DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi MKoa wa Dar, Abdala Zombe.

Amebakiwa na shtaka la kuficha wahalifu.

======================

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na sasa inataka ajibu mashtaka ya kuficha wahalifu.


DPP amefanya mabadiliko hayo kwenye rufaa aliyoikata Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu wa kumuachia huru Zombe, ambaye alikuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) katika mashtaka ya mauaji.

Awali, DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyomwachia huru Zombe na wenzake tisa, katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva mmoja wa teksi wa Manzese jijini Dar es Salaam.

Katika rufaa hiyo, DPP alikuwa anaiomba Mahakama ya Rufani iwatie hatiani washtakiwa hao kwa kosa la mauaji ya kukusudia, kama ilivyokuwa kwenye kesi ya msingi, kosa ambalo adhabu zake ni pamoja na kunyongwa hadi kufa.

Hata hivyo, DPP amebadili msimamo huo dhidi ya Zombe na badala yake anaiomba Mahakama hiyo imtie hatiani kwa kosa la kuwalinda wahalifu ambao walitenda kosa la mauaji ya wafanyabiashara hao na dereva wa teksi.

Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, Timoth Vitalis, ambaye ni Wakili Mkuu wa Serikali (PSA) na Richard Rweyongeza, ambaye ni wakili wa kujitegemea anayemtetea Zombe katika rufaa hiyo, walisema mtu anayepatikana na hatia kwa kosa hilo adhabu yake ni kifungo jela kisichozidi miaka saba.

Kwa maana hiyo, hata kama Mahakama ya Rufani itakubaliana na hoja za rufaa za DPP na kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo jipya ambalo hata hivyo, hakuwa ameshtakiwa nalo kwenye kesi ya msingi, atakuwa ameepuka adhabu ya kitanzi.

DPP alibadili msimamo wake huo dhidi ya Zombe siku ya usikilizwaji wa rufaa hiyo Mahakama ya Rufani mbele ya jopo la majaji watatu, Bernard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage, hivi karibuni.

Mkurugenzi huyo wa mashtaka alifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo la mauaji.

Akizungumzia uamuzi huo wa DPP kumuondoa kwenye shtaka la mauaji kama alivyokuwa akidaiwa tangu awali na sasa kupewa shtaka la kuwalinda wahalifu, Zombe alisema kwanza alikuwa ameonewa kwa kuhusishwa na hatimaye kushtakiwa kwa kosa la mauaji.

Alisisitiza kuwa hakutendewa haki wakati wa kumfungulia shtaka hilo la mauaji kwa kuwa sheria hazikufuatwa.

“Kwanza ni mambo ya ajabu sana. Nimedhalilishwa sana kwa muda wote huo na kuonekana kuwa mimi ni muuaji kila ninakopita, kwa kufunguliwa shtaka ambalo sikuhusika nalo,” alisema Zombe.

“Mimi sikuwapo eneo la tukio na wala nilikuwa siwafahamu watu hao na hata Tume (iliyoundwa na Rais kuchunguza mauaji hayo iliyoongozwa na Jaji Mussa) Kipenka ililiridhika kuwa sikuwepo eneo la tukio. Sasa nilihusikaje na mauaji hayo?”

Zombe aliongeza kuwa washtakiwa wote walihojiwa na kuandika maelezo yao na kwamba huo ndiyo utarartibu wa kisheria.

Zombe alisisitiza kuwa yeye alikuwa mwendesha mashtaka kwa muda mrefu na mkuu wa upelelezi wa mkoa, hivyo anajua taratibu kwa kuwa alikuwa akiandika majalada mengi kwenda kwa Mwanasheria wa Serikali na mengine yalikuwa yakienda mahakamani kama alivyoyaandika.

Kuhusu kosa alilobadilishiwa na DPP wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, Zombe hakuwa tayari kulizungumzia kwa kuwa bado Mahakama haijatoa hukumu.

Kabla ya kumbadilishia shtaka hilo, wakati wa usikilizwaji wa rufaa, DPP alitaka kumuongezea Zombe shtaka hilo kama shtaka mbadala, wakati wa usikilizwaji wa kesi ya msingi.

Hata hivyo, DPP aligonga mwamba baada ya Jaji Massati kumkatalia kwa maelezo kuwa alitakiwa ashtakiwe tangu mwanzo kwa kosa hilo.

Kabla ya kumuondoa Zombe katika kosa la adhabu hiyo ya kunyongwa, kwanza DPP, aliwaondolea washtakiwa wengine watano, baada ya kubaini kuwa ushahidi aliokuwa nao hauwagusi katika rufaa hiyo.

Walioondolewa ni Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abineth Salo na Festus Gwabisabi.

Lakini ameendelea kuwang’ang’ania Zombe na wenzake watatu ambao ni Christopher Bageni, Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.

Ndo kilichokuwa kimelengwa muda mrefu. Sasa kesi ndo imekuwa lainiiiiiiiii!! . Zombe vs Republic , the accused is going to win smoothly
 
Mwendesha mashataka wa Serikali(DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi MKoa wa Dar, Abdala Zombe.

Amebakiwa na shtaka la kuficha wahalifu.

======================

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amemuondolea kosa la mauaji aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na sasa inataka ajibu mashtaka ya kuficha wahalifu.


DPP amefanya mabadiliko hayo kwenye rufaa aliyoikata Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu wa kumuachia huru Zombe, ambaye alikuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) katika mashtaka ya mauaji.

Awali, DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyomwachia huru Zombe na wenzake tisa, katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva mmoja wa teksi wa Manzese jijini Dar es Salaam.

Katika rufaa hiyo, DPP alikuwa anaiomba Mahakama ya Rufani iwatie hatiani washtakiwa hao kwa kosa la mauaji ya kukusudia, kama ilivyokuwa kwenye kesi ya msingi, kosa ambalo adhabu zake ni pamoja na kunyongwa hadi kufa.

Hata hivyo, DPP amebadili msimamo huo dhidi ya Zombe na badala yake anaiomba Mahakama hiyo imtie hatiani kwa kosa la kuwalinda wahalifu ambao walitenda kosa la mauaji ya wafanyabiashara hao na dereva wa teksi.

Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, Timoth Vitalis, ambaye ni Wakili Mkuu wa Serikali (PSA) na Richard Rweyongeza, ambaye ni wakili wa kujitegemea anayemtetea Zombe katika rufaa hiyo, walisema mtu anayepatikana na hatia kwa kosa hilo adhabu yake ni kifungo jela kisichozidi miaka saba.

Kwa maana hiyo, hata kama Mahakama ya Rufani itakubaliana na hoja za rufaa za DPP na kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo jipya ambalo hata hivyo, hakuwa ameshtakiwa nalo kwenye kesi ya msingi, atakuwa ameepuka adhabu ya kitanzi.

DPP alibadili msimamo wake huo dhidi ya Zombe siku ya usikilizwaji wa rufaa hiyo Mahakama ya Rufani mbele ya jopo la majaji watatu, Bernard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage, hivi karibuni.

Mkurugenzi huyo wa mashtaka alifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani Zombe kwa kosa hilo la mauaji.

Akizungumzia uamuzi huo wa DPP kumuondoa kwenye shtaka la mauaji kama alivyokuwa akidaiwa tangu awali na sasa kupewa shtaka la kuwalinda wahalifu, Zombe alisema kwanza alikuwa ameonewa kwa kuhusishwa na hatimaye kushtakiwa kwa kosa la mauaji.

Alisisitiza kuwa hakutendewa haki wakati wa kumfungulia shtaka hilo la mauaji kwa kuwa sheria hazikufuatwa.

“Kwanza ni mambo ya ajabu sana. Nimedhalilishwa sana kwa muda wote huo na kuonekana kuwa mimi ni muuaji kila ninakopita, kwa kufunguliwa shtaka ambalo sikuhusika nalo,” alisema Zombe.

“Mimi sikuwapo eneo la tukio na wala nilikuwa siwafahamu watu hao na hata Tume (iliyoundwa na Rais kuchunguza mauaji hayo iliyoongozwa na Jaji Mussa) Kipenka ililiridhika kuwa sikuwepo eneo la tukio. Sasa nilihusikaje na mauaji hayo?”

Zombe aliongeza kuwa washtakiwa wote walihojiwa na kuandika maelezo yao na kwamba huo ndiyo utarartibu wa kisheria.

Zombe alisisitiza kuwa yeye alikuwa mwendesha mashtaka kwa muda mrefu na mkuu wa upelelezi wa mkoa, hivyo anajua taratibu kwa kuwa alikuwa akiandika majalada mengi kwenda kwa Mwanasheria wa Serikali na mengine yalikuwa yakienda mahakamani kama alivyoyaandika.

Kuhusu kosa alilobadilishiwa na DPP wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, Zombe hakuwa tayari kulizungumzia kwa kuwa bado Mahakama haijatoa hukumu.

Kabla ya kumbadilishia shtaka hilo, wakati wa usikilizwaji wa rufaa, DPP alitaka kumuongezea Zombe shtaka hilo kama shtaka mbadala, wakati wa usikilizwaji wa kesi ya msingi.

Hata hivyo, DPP aligonga mwamba baada ya Jaji Massati kumkatalia kwa maelezo kuwa alitakiwa ashtakiwe tangu mwanzo kwa kosa hilo.

Kabla ya kumuondoa Zombe katika kosa la adhabu hiyo ya kunyongwa, kwanza DPP, aliwaondolea washtakiwa wengine watano, baada ya kubaini kuwa ushahidi aliokuwa nao hauwagusi katika rufaa hiyo.

Walioondolewa ni Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shonza, Abineth Salo na Festus Gwabisabi.

Lakini ameendelea kuwang’ang’ania Zombe na wenzake watatu ambao ni Christopher Bageni, Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.

Hiv Zombe alisha staafu au?
 
Nasoma hapa na kujiuliza hivi ni kesi mpya ama ileee ya mabwepande?
Zombe Ana matukio!
Zombe huyu huyu ndiyo yule aliohusiswa na wafanya biashara wa madini Morogoro miaka ile na Mauaji mengine 2006 Dar es salaam yaliyoleta utata mwingi akiusishwa na kina Tibaigana enzi zile za mauaji ya watu waliokuja kugundulika hawakuwa majambaz...Na sasa hii tena na zote anachomoa....
 
Kwa taarifa yenu yale yalikuwa majambazi yaliyokubuhu na alichofanya huyu kamanda kilikuwa sahihi kabisa na kinafanyika duniani kote, kosa lake alijichanganya kidogo tuu! Na huu ndo ukweli mchungu, ukitaka meza, ukikataa tema!
Ukishajua mtu ni jambazi wewe kama askari (mtoa comment), unabeba bunduki yako na kuwaua. Ndivyo? [emoji15]
 
haishangazi sanaa labda kama angehukumiwa kifungo cha maisha ndo ningeshangaaa.wakubwa wengi wa wanao patikana na na makosa ya kifungo huwa niwale tu wanao amua kutolewa kama sadaka wa kafara.
 
Nchi hii inatia kinyaa,yani mtu aue watu alafu sasa wanaanza kufanya ujanja wa kumuachia aisee hili ni jipu mkuu magufuli aone hili amtumbue uyo dpp haraka sana haiwezekani mtu aue watu alafu leo wanataka kumuachia hii si haki hata kidogo huu ni mchezo mchafu magu aingilie kati hatuna wanasheria wa serikali kwenye hii nchi ni uozo mtupu
 
Back
Top Bottom