DPP kuridhia mashtaka dhidi ya vigogo kesi za TAKUKURU?

DPP kuridhia mashtaka dhidi ya vigogo kesi za TAKUKURU?

Hamna lolote longo longo tu hadi leo hawajafungwa MAFISADI. Subira yenye heri imekwisha changa la macho la kila siku.
 
UCHUNGUZI dhidi ya tuhuma za ufisadi dhidi ya aliyekuwa Waziri wa Fedha katika Serikali ya awamu ya tatu, Basil Mramba, umechukua sura mpya, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Eliezer Feleshi kukamilisha kazi yake.


Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa tayari jalada la uchunguzi huo limesharejeshwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa ajili ya kufanyika kazi zaidi.


Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini kuwa, Mramba anachunguzwa kutokana na tuhuma za ufisadi katika misamaha ya kodi ambayo ilitolewa kwa mabilioni ya shilingi kwa wafanyabiashara katika mazingira tata.


Feleshi alilithibitishia Mwananchi Jumapili katika mahojiano maalumu ofisini kwake, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kuwa jalada la kesi hiyo lilifikishwa ofisini kwake na amemaliza kulifanyia kazi.


Alisema baada ya kumaliza kulifanyia kazi amewakabidhi Takukuru kwa ajili ya kulifanyia kazi zaidi.


"Tumelirudisha kwao ndiyo wanaojua ambacho wanaedelea nacho, kwa hiyo nini kinafanyika ni bora muwaulize wao," alisema Feleshi.


Alipoulizwa kama ofisi yake imetoa maelekezo ya kufunguliwa mashtaka au kulifanyia kazi zaidi jalada hilo, alisema kwa kawaida taratibu zao haziruhusu kueleza nini ofisi hiyo imeandika katika jalada la uchunguzi.


Feleshi aliongeza kwamba, Takukuru ambao ndiyo wanaochunguza tuhuma hizo ndiyo wenye mamlaka ya kueleza hatua iliyofikiwa.


Mkurugenzi huyo alifafanua kwamba, taratibu za kiutendaji haziruhusu kueleza nini ambacho ofisi hiyo imeandika kwenda kwa mhusika.


Alisema taratibu zote zinazofanyika ikiwamo kama ni mashtaka, mhusika pia anapaswa kupewa taarifa.


"Hakuna kitu kinafanyika kwa siri, hata mhusika (mtuhumiwa) lazima awe anapewa taarifa za mchakato," alisisitiza Feleshi.


Hata hivyo, uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini zaidi kwamba kuna mipango mbalimbali ya chini kwa chini, inayofanywa na serikali ya kutaka kuwafikisha mahakamani baadhi ya vigogo nchini kwa tuhuma za ufisadi.


Taarifa kutoka ndani ya serikali zinaeleza kwamba, majalada mbalimbali ya uchunguzi yameanza kupelekwa katika ofisi ya DPP.


Alipoulizwa taarifa za majalada ya baadhi ya vigogo wengine kuchunguzwa na kupelekwa ofisini hapo, alisema wingi wa majalada katika ofisi hiyo ni kitu cha kawaida.


Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Lilian Mashaka, alisema pamoja na taarifa hizo kuwa za kweli, hawezi kusema chochote kwa kuwa sio msemaji wa taasisi.


Alishauri gazeti hili kuwasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hosea, kwa maelezo ya kina kuhusiana na suala hilo.


Kauli ya Mashaka ilirudiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa taasisi hiyo, Alex Mfungo, aliyesema kuwa taasisi hiyo ina taratibu zake katika kutoa taarifa na kwamba mkurugenzi mkuu ndiye msemaji.


"Nyie mkitaka taarifa hizo njooni ofisini, mfuate utaratibu, sio kila mtu anasema kila kitu. Msemaji wa taasisi ni mmoja tu," alisema Mfungo.


Hata hivyo, Dk Hosea hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake ya mkononi kuita mara kadhaa bila kupokelewa.


Kwa upande wake, Mramba alipotafutwa kwa njia ya simu jana kwa ajili ya kutoa ufafanuzi kuhusiana na suala hilo, alisema hawezi kuzungumzia mambo yaliyopo katika ofisi za watu wengine bila kufafanua zaidi.


Ikiwa mwanasiasa huyo atafikishwa mahakamani, itakuwa ni mara ya pili kwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuwashtaki watendaji wake wa zamani ikianzia na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, anayeendelea kujitetea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam. Profesa Mahalu anatuhumiwa kuiibia Serikali Sh 2 bilioni kutokana na kuongeza bei wakati wa mchakato wa ununuzi wa Jengo la Ubalozi wa Tanzania, mjini Rome.


Pia kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa rasmi kwamba, serikali iko mbioni kuwashtaki watu wanaotajwa kuhusika katika wizi wa mabilioni ya fedha za umma, katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na wale waliohusika kuipa zabuni kwa upendeleo Kampuni hewa ya kufua umeme wa dharura ya Richmond Development LLC.


Rais Kikwete alimuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kuongoza timu ya wataalamu akisaidiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Saidi Mwema na Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hosea kuchunguza na kuwashtaki watu ambao watabainika kuhusika na wizi wa Sh 133 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika BoT.
 
Mwendesha Mashtaka akamilisha uchunguzi kuhusu Basil Mramba
Na Ramadhan Semtawa

UCHUNGUZI dhidi ya tuhuma za ufisadi dhidi ya aliyekuwa Waziri wa Fedha katika Serikali ya awamu ya tatu, Basil Mramba, umechukua sura mpya, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Eliezer Feleshi kukamilisha kazi yake.


Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa tayari jalada la uchunguzi huo limesharejeshwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa ajili ya kufanyika kazi zaidi.


Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini kuwa, Mramba anachunguzwa kutokana na tuhuma za ufisadi katika misamaha ya kodi ambayo ilitolewa kwa mabilioni ya shilingi kwa wafanyabiashara katika mazingira tata.


Feleshi alilithibitishia Mwananchi Jumapili katika mahojiano maalumu ofisini kwake, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kuwa jalada la kesi hiyo lilifikishwa ofisini kwake na amemaliza kulifanyia kazi.


Alisema baada ya kumaliza kulifanyia kazi amewakabidhi Takukuru kwa ajili ya kulifanyia kazi zaidi.


"Tumelirudisha kwao ndiyo wanaojua ambacho wanaedelea nacho, kwa hiyo nini kinafanyika ni bora muwaulize wao," alisema Feleshi.


Alipoulizwa kama ofisi yake imetoa maelekezo ya kufunguliwa mashtaka au kulifanyia kazi zaidi jalada hilo, alisema kwa kawaida taratibu zao haziruhusu kueleza nini ofisi hiyo imeandika katika jalada la uchunguzi.


Feleshi aliongeza kwamba, Takukuru ambao ndiyo wanaochunguza tuhuma hizo ndiyo wenye mamlaka ya kueleza hatua iliyofikiwa.


Mkurugenzi huyo alifafanua kwamba, taratibu za kiutendaji haziruhusu kueleza nini ambacho ofisi hiyo imeandika kwenda kwa mhusika.


Alisema taratibu zote zinazofanyika ikiwamo kama ni mashtaka, mhusika pia anapaswa kupewa taarifa.


"Hakuna kitu kinafanyika kwa siri, hata mhusika (mtuhumiwa) lazima awe anapewa taarifa za mchakato," alisisitiza Feleshi.


Hata hivyo, uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini zaidi kwamba kuna mipango mbalimbali ya chini kwa chini, inayofanywa na serikali ya kutaka kuwafikisha mahakamani baadhi ya vigogo nchini kwa tuhuma za ufisadi.


Taarifa kutoka ndani ya serikali zinaeleza kwamba, majalada mbalimbali ya uchunguzi yameanza kupelekwa katika ofisi ya DPP.


Alipoulizwa taarifa za majalada ya baadhi ya vigogo wengine kuchunguzwa na kupelekwa ofisini hapo, alisema wingi wa majalada katika ofisi hiyo ni kitu cha kawaida.


Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Lilian Mashaka, alisema pamoja na taarifa hizo kuwa za kweli, hawezi kusema chochote kwa kuwa sio msemaji wa taasisi.


Alishauri gazeti hili kuwasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hosea, kwa maelezo ya kina kuhusiana na suala hilo.


Kauli ya Mashaka ilirudiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa taasisi hiyo, Alex Mfungo, aliyesema kuwa taasisi hiyo ina taratibu zake katika kutoa taarifa na kwamba mkurugenzi mkuu ndiye msemaji.


"Nyie mkitaka taarifa hizo njooni ofisini, mfuate utaratibu, sio kila mtu anasema kila kitu. Msemaji wa taasisi ni mmoja tu," alisema Mfungo.


Hata hivyo, Dk Hosea hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake ya mkononi kuita mara kadhaa bila kupokelewa.


Kwa upande wake, Mramba alipotafutwa kwa njia ya simu jana kwa ajili ya kutoa ufafanuzi kuhusiana na suala hilo, alisema hawezi kuzungumzia mambo yaliyopo katika ofisi za watu wengine bila kufafanua zaidi.


Ikiwa mwanasiasa huyo atafikishwa mahakamani, itakuwa ni mara ya pili kwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuwashtaki watendaji wake wa zamani ikianzia na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, anayeendelea kujitetea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam. Profesa Mahalu anatuhumiwa kuiibia Serikali Sh 2 bilioni kutokana na kuongeza bei wakati wa mchakato wa ununuzi wa Jengo la Ubalozi wa Tanzania, mjini Rome.


Pia kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa rasmi kwamba, serikali iko mbioni kuwashtaki watu wanaotajwa kuhusika katika wizi wa mabilioni ya fedha za umma, katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na wale waliohusika kuipa zabuni kwa upendeleo Kampuni hewa ya kufua umeme wa dharura ya Richmond Development LLC.


Rais Kikwete alimuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kuongoza timu ya wataalamu akisaidiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Saidi Mwema na Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hosea kuchunguza na kuwashtaki watu ambao watabainika kuhusika na wizi wa Sh 133 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika BoT
 
msiwe waabishi, wanaweza kumpeleka mahakamani kama vile mchezo wa kuigiza, ili kutengeneza move lingine kama lile la naila kiula, halafu baadaye atshinda kesi, kimchezo mchezo. mafisadi wana njia nyingi za kuhadaa. kama wanaweza kutengeneza filamu kama ya balali hili litawashinda?
 
Hurray! kwa mbali mwanga wa mapambazuko waanza kujitokeza taratibu na kuleta marumaini mapya kwa watanzania, wafikishwe maakamani tuone uzalendo wa majaji kwa mafisadi wanaomaliza nchi yetu.

Mkubwa hamna kitu hapo, kama watu waliweza kutoa kanya boya Richmond iweje washindwe kwa Mramba.

Huyu Banyamulenge (HOSEA) mwenye MWIZI, sasa wewe umeona wapi kesi ya Nyani ukampelekea Tumbili tena ya Mahindi.

Wakubwa hapo tumeliwa. Ila mimi wala sijakata tamaa hawa tutakomaa nao tuu.
 
Asante sana ndugu
Ni watanzania wachache tunaoweza kuona mbali kaka, naomba mungu awafumbulie wote wajue haya mambo
Hii serikali inatudanganya na kwa sababu ishajua kuwa sisi ni wepesi wa kudanganywa na hatuwezi kuoji na niwepesi wa kusahau
Hivyo wanachofanya ni kuja na uongo kila kukicha ili kutusahaulisha yale ya nyumba.

Maskini sie wadanganyika sijui tutaendelea kuwa namna hii mpaka lini


Ama kweli watanzania bwana, hebu ni lini akili zetu zitakuwa na ufahamu? Eti Mramba anashitakiwa, kwa kosa gani jamani? Mramba ni mtu huru ndani ya nchi yake huru, haya mengine ni kelele za chura, tukitaka kumshitaki Mramba kwanza tuanze na .................................., kisha afuate.S..................... Na mwisho hawa mawaziri wengine.

Basi mshitakini muone cha moto, atatoa siri zote, mpaka mchanganyikiewe.
 
Kanyaga boya ili
Kikwete kushinda kwa 80% ni kutokana na pesa za BOT, ambazo mramba alikuwa waziri wa Fedha chini ya Fisadi mkuu Mkapa, hivyo huyu Kikwete hawezi lolote hapa kwani Mramba kashika mpini jamani
Tusahau haya, hata siku moja hakuna litakalotokea Tanzania, kuwapeleka Mafisadi Mahakamani, ni sawa na Bush kukaa meza moja na Osama jamani


BABA H
Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Mimi ni mgumu sana kuamini vipi kesi ya nyani asikilize Ngedere, siamini vipi inawezekana Ngedere aamuru Nyani aliyemletea mahindi akamatwe, lazima kitakuwa ni kiini macho tu. Lakini pamoja na pessmism tuliyonayo tuendelee kusubiri, unaweza kushangaa kuwa inakuwa ni kiini macho kama cha Nalaila Kiula.
 
Kama kungekwua na dhamira ya kuwashitaki, kesi ingekuwa imeshamalizika na mwenye kuwa Segerea angekuwa anakaribia kumaliza kifungo. CHANGA LA MACHO HILO
 
Changa la Macho lingine hilooooooooo... Nimewahi kusema tena kuwa tutapiga kelele weee ila hakuna kitakachofanyika hapa Tanzania.. Ila ni vizuri tujifurahishe tuu huku JF ili kupunguza machungu But nothing will be done in Tanzania regarding MAFISADI. Wana pesa nyingi sana ambazo hata PM wetu anaziogopa, wana mitandao mikubwa sana. Naomba niulize na mwenye data aniambie. Mramba ameweka watu wake wengi sana pale Hazina kila mtu anajua na mkitaka hata majina nitawapatia. Kuna watu wa sehemu fulani waliandikisha majina yao ili wapatiwe kazi serekalini, kama utani vile 2005 aliwaingiza watu kama 4 ninaofahamu mimi waliojiandikisha kwenye hiyo orodha, unafikiri hao watu wataweza kumgeuka leo hii? Hapa tunapigishana kelele tuu.

Tusubirie tuone labda kweli Watanzania wameamka
 
Ama kweli watanzania bwana, hebu ni lini akili zetu zitakuwa na ufahamu? Eti Mramba anashitakiwa, kwa kosa gani jamani? Mramba ni mtu huru ndani ya nchi yake huru, haya mengine ni kelele za chura, tukitaka kumshitaki Mramba kwanza tuanze na .................................., kisha afuate.S..................... Na mwisho hawa mawaziri wengine.

Basi mshitakini muone cha moto, atatoa siri zote, mpaka mchanganyikiewe.

Mkuu isaya heshima mbele
sasa haya mambo ya dash dash mbona hapa hakuna
hapa ni kumwaga vitu

kwani ni kazi kubwa hapo kusena tuanze na MKAPA kusha tufuate na SUMAYE??
 
CCM ipo kimyaaaaaaaaa inatafuta uongo wa kutupatia....
 
hamna kitu hapa! itachukuwa miezi kadhaa hadi ripoti ya tukukuru itoke.....na ikifikishwa mahakani tutaambiwa ushahidi hautoshi!
sitaki kusema, lakini sina imani na serikali yetu
 
munakumbuka hii stori hizi?

http://www.raiamwema.co.tz/08/03/26/index.php

http://www.thisday.co.tz/News/3951.html

Mawaziri kushitakiwa kwa tuhuma za ufisadi

Mwandishi Wetu
Machi 26, 2008



SERIKALI inakamilisha taratibu za kuwashitaki mawaziri wa zamani wawili wanaotuhumiwa kwa ufisadi, Raia Mwema imefahamishwa.

Habari za uhakika zilizopatikana na kuthibitishwa na maofisa waandamizi wa Serikali zinaeleza kwamba mawaziri hao (majina tunayo) walihojiwa na vyombo vya dola kwa mara kadhaa na sasa mchakato wa kuwashitaki uko katika hatua za mwisho.

Wote wawili walipata kuongoza Wizara ya Fedha, chini ya utawala wa Rais Benjamin Mkapa na mmoja aliteuliwa katika serikali mpya ya Rais Jakaya Kikwete kabla ya kuachwa katika mabadiliko yaliyofanyika hivi karibuni.


Mhe. Pesambili Mramba

Kwa mujibu wa habari hizo, mmoja amekuwa akichunguzwa kufanya maamuzi kadhaa yenye utata, ikiwamo kutoa misamaha ya kodi ambayo kisheria hakuwa na mamlaka nayo akiwa anatuhumiwa kuvuka mipaka ya mamlaka yake katika kutoa misamaha.

Mwingine anaelezwa kuchunguzwa kuhusika na maamuzi kadhaa akiwa Waziri katika Wizara ya Fedha na Wizara ya Nishati na Madini, lakini haikuweza kufahamika mara moja ni eneo gani hasa ambalo mwanasiasa huyo mstaafu amechunguzwa.

Mawaziri wote wawili wanatajwa sana kuwa karibu na Mkapa katika masuala kadhaa ya kiutendaji na hata katika masuala kadhaa binafsi na inaelezwa kwamba baadhi ya mambo yaliyochunguzwa yanaweza kumgusa moja kwa moja Rais huyo mstaafu.

Mkapa anatajwa kuhusika moja kwa moja na mradi mkubwa wa mkaa wa mawe wa Kiwira, akiwa na maslahi binafsi katika kampuni ya Tanpower Resources, ambayo iliuziwa hisa za kampuni ya Kiwira Coal Mines Limited iliyokuwa ikimilikiwa na serikali kabla ya ubinafsishaji.



Mhe. Daniel Yona

Pamoja na Mkapa kutajwa katika maeneo mengi, bado kumekuwa na maelezo ya kutaka "aachwe apumzike", huku baadhi wakitumia kinga ya kikatiba ambayo rais mstaafu anakuwa nayo pamoja na kupingwa na baadhi ya wanasheria.

Haikuweza kufahamika mara moja mawaziri hao walichunguzwa katika maeneo gani mengine zaidi lakini kuna uhakika kwamba uchunguzi huo uligusa pia misamaha ya kodi iliyofanywa katika kipindi mawaziri hao wakiwa madarakani.

Miongoni mwa mambo ambayo yaliguswa ni mkataba kati ya Serikali na wakaguzi wa Alex Stewarts waliokuwa wakifanya ukaguzi wa mapato katika sekta ya madini.

Eneo jingine tata ambalo linatajwa kuguswa ni mkataba wa Serikali na kampuni ya Tanzania International ContainerTerminal (TICTS) wa kukodisha eneo la bandari ya Dar es Salaam, mkataba ambao hadi sasa umekuwa ukipigiwa kelele na wadau mbalimbali wa sekta ya bandari.



RAIS Mstaafu Mkapa

Hata hivyo, mawaziri wote wawili walikuwa ama na mahusiano ya karibu na Mkapa kikazi na hata kibinafsi mambo ambayo yanazidi kuonyesha ni jinsi gani Serikali italazimika kumtaja ama kumgusa rais huyo mstaafu katika uchunguzi na hatimaye mashitaka.

Ikiwa wanasiasa hao watafikishwa mahakamani, itakuwa ni mara ya pili kwa Serikali ya Kikwete kuwashitaki watendaji wake wa zamani ikianzia na aliyekuwa Balozi wa Tanzania Italia, Profesa Costa Mahalu, anayeendelea kujitetea katika mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, akituhumiwa kuiibia Serikali Sh bilioni 2 kutokana na ununuzi wa jengo la ubalozi, Rome.

Hata hivyo, kiu kubwa ya Watanzania kwa sasa iko kwa watu wanaotajwa kuhusika katika upotevu wa mabilioni ya fedha za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na wale waliohusika na mradi tata wa umeme wa dharura wa Richmond Development LLC.

Pamoja na Rais Kikwete kuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kuongoza timu ya wataalamu akisaidiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Saidi Mwema na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (Takukuru), Edward Hosea, kulikuwa na kazi iliyokwisha kuanza kufanywa na vyombo hivyo ndani ya BoT na maeneo mengine nyeti kiuchumi.


Revealed: What Mramba is accused of


-Probe zeros in on suspect tax deal with gold audit firm
-His comment: ''I don't know what you�re talking about''


THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

FORMER finance minister Basil Mramba is being investigated for dubious tax exemptions given to US company Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation, which was awarded a controversial gold auditing contract by the third phase government in 2003, it has been revealed.

Mramba, who has already been questioned by investigators from the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB), has declined to make any comment about the allegations, telling THISDAY: ''I have no comment...I don't know what you are talking about.''

Latest findings by THISDAY have confirmed that the PCCB investigation against the veteran Rombo Member of Parliament, who is now in line for formal prosecution, has centred on the tax exemptions issue in relation to Alex Stewart (Assayers).

The US firm signed a two-year renewable contract with the Bank of Tanzania (BoT) on June 14, 2003, to audit production and exports from the country's booming gold mining industry. The contract was renewed for another two years in 2005.

Under the deal, Alex Stewart Assayers was paid by the government a staggering 70bn/- during the duration of the contract, equivalent to two-thirds of the country's total royalty turnover from gold exports.

Although Alex Stewart Assayers was able to uncover much cheating by most of the major gold mining companies in the country through under-declaration of profits and other means, the terms of the company's contract with the government have remained a subject of heavy criticism in various circles, including the National Assembly.

According to our sources, the investigation is zeroing in on a number of controversial tax exemptions that Mramba may have offered to the US company, contrary to government regulations.

There have also been allegations that various individuals related to either Mramba himself or former BoT governor Dr Daudi Ballali were employed by Alex Stewart Assayers in highly suspicious circumstances.

Investigations by THISDAY have already established that the office of the Director of Public Prosecutions (DPP) has given the PCCB a formal go-ahead to file criminal charges against Mramba.

The Director of Public Prosecutions, Eliezer Feleshi, confirmed that his office had processed the PCCB file on Mramba, but declined comment when asked if his office had issued its consent for prosecution.

However, well-placed sources confirmed that the DPP's office had indeed given the formal consent paving the way for PCCB to prosecute the former minister.

''We expect formal charges to be brought against Mramba at the Kisutu Resident Magistrate's Court in Dar es Salaam...it is now just a matter of time,''a source familiar with the issue told THISDAY.

The 68-year-old Mramba served as finance minister for five years from 2000 to 2005, in the second and final term of the third phase government under ex-president Benjamin Mkapa.

Before being appointed finance minister, Mramba served as minister for industries and trade in the Mkapa administration from 1995 to 2000.

From 2006, he served as minister for infrastructure development in the fourth phase government of President Jakaya Kikwete, later being reappointed minister in charge of industry, trade and marketing, before eventually being dropped after the dissolution and re-composition of the cabinet in February this year.
 
..................Alisema baada ya kumaliza kulifanyia kazi amewakabidhi Takukuru kwa ajili ya kulifanyia kazi zaidi.

"Tumelirudisha kwao ndiyo wanaojua ambacho wanaendelea nacho, kwa hiyo nini kinafanyika ni bora muwaulize wao," alisema Feleshi................

kuna mambo mawili yanawezekana katika hili suala

1. PCCB hawakuleta facts za kutosha kwa DPP na hivyo facts zaidi zahitajika ili ku-justfy ufunguliwaji wa mashtaka

2. Kulindana, i.e involves a chain of other prominent figures
 
Hii system inasound kama office ya mganga wa kienyeji bwana, kama DA ameshamaliza kuandaa file kilichotakiwa ni kumburuza mramba mahakamani. I can't wait kusikia Mramba VS United Republic of Tanzania, na kitakachonivutia zaidi ni kusikia kwamba Mramba ahukumiwa miaka 30 jela.
 
Vigogo mafisadi waitisha serikali

Waandishi Wetu Julai 16, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

Kesi zao zakwama kufunguliwa

WATUHUMIWA wakubwa wa rushwa na ufisadi, wanaelezwa kupumua baada ya kufanikiwa kuwatisha viongozi na watendaji wa juu wa Serikali ili kesi dhidi yao zisitishwe, Raia Mwema imebaini.

Habari za ndani ya Serikali zinaeleza kwamba uchunguzi wa kesi kadhaa uliokuwa katika hatua za mwisho na hata zile kesi ambazo zimekamilika 'zimegonga mwamba' na watendaji huenda sasa 'wakageuziwa kibao'.

Kwa mujibu wa habari hizo, taarifa zilizovuja na kuwafikia wahusika zilipenyezwa kutoka ndani ya vyombo vya Serikali na hivyo kuwafanya watuhumiwa hao kuanza kupambana kuhakikisha wanajihami kwa nguvu zote.

"Kesi zote kubwa sasa zimegonga mwamba baada ya watendaji na viongozi wa juu wa Serikali kutishwa na watuhumiwa ambao baadhi wana mahusiano nao kikazi ama waliwahi kufanya kazi pamoja," anaeleza ofisa mmoja wa ngazi ya kati serikalini.

Na mwanasheria mmoja mwandamizi ameiambia Raia Mwema wiki hii kwamba, kwa sasa inabidi Serikali iwe makini maana watuhumiwa wameungana kuhakikisha 'wanajibu mapigo' kwa yeyote ambaye anashiriki 'kuwaangamiza'.

Imeelezwa kwamba hata zile kesi kubwa 10 ambazo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, aliwahi kutamba kwamba ziko katika hatua nzuri, nazo hazitoweza kufikishwa mahakamani na wahusika sasa wanapumua.

Kwa mujibu wa habari hizo, watuhumiwa hao wamefanikiwa kuvivuruga hata vyombo vya dola kwa kuwagawa na kuwachafua watendaji wa vyombo hivyo na sasa wameahidi kutumia nguvu zao zote kupandikiza watu wao ndani ya vyombo hivyo, kimoja kikiwa ni TAKUKURU.

"Hivi sasa wanajitapa kwamba wataweka watu wao TAKUKURU na kwenye vyombo vingine ambavyo wanaamini kwamba kuna watendaji ambao wana nia ya kuwashughulikia, wakidai kwamba watendaji hao wametumwa kuwamaliza," anasema ofisa mwingine ndani ya Serikali aliye karibu na masuala ya kesi hizo.

Hosea alipata kunukuliwa akitangaza hadharani kwamba ofisi yake inachunguza kesi 10 kubwa za ufisadi, akisema kesi tano kati ya hizo ziko katika hatua za mwisho za kufunguliwa mashitaka akiungwa mkono na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ambaye alitaja hata kesi ambazo amekwisha kuzitolea kibali cha kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna hata kesi moja iliyofunguliwa mahakamani na baadhi ya watuhumiwa wamediriki kutamka hadharani kwamba hakuna mwenye 'ubavu' wa kuwafikisha mahakamani.

"Mwaka huu (2008) kufikia Julai tutakuwa tumekamilisha kesi tano za kwanza… hizi ni kesi za rushwa kubwa kubwa. Na tabia ya kesi za rushwa kubwa ni kwamba inakuwa na madhara makubwa kwa uchumi wa nchi, wahusika huwa ni watu wakubwa, kiasi cha rushwa kinachohusishwa ni kikubwa, eneo la uchunguzi wake huvuka mipaka ya ndani na nchi za nje, zinahusisha maandiko mengi, zinahitaji kiasi kikubwa kwa uchunguzi na huvuta hisia za jamii," alinukuliwa Hosea akisema.

Habari zilizochapishwa na vyombo vya habari zimezitaja kesi kumi zinazochunguzwa kuwa kuwa ni pamoja na ile inayohusu mradi wa mgodi wa dhahabu uliopo Kahama wa Buzwagi, kampuni tata za Meremeta, Tangold, Deep Green na Mwananchi Gold ambazo zilichota fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Kesi nyingine zilizotajwa ni pamoja na ile inayohusu kampuni ya ukaguzi wa madini ya Alex Stewarts, tuhuma zinazohusu ujenzi wa majengo pacha ya BoT, mradi wa mkaa wa mawe wa Kiwira, utata katika miradi ya umeme wa dharura na ununuzi wa rada ya kijeshi kutoa kampuni ya BAe Systems ya Uingereza.

Aidha ilipata kuripotiwa kwamba wanasiasa waliopata kushika nafasi za uwaziri wa fedha, walitarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni, taarifa zilizothibitishwa na maelezo ya DPP, Elieza Feleshi aliyenukuliwa akithibitisha kutoa kibali cha mashitaka kuhusiana na mmoja wa wanasiasa, hao lakini hadi sasa hakuna kesi iliyokwisha kufunguliwa mahakamani.

Miongoni mwa kesi zinazotajwa kuwa na ushahidi wa kutosha ni pamoja na ile inayoihusu kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington DC, Marekani iliyopewa kazi ya kukagua mahesabu ya makampuni ya uchimbaji dhahabu.

Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, amewahi kunukuliwa akisema kwamba chini ya mkataba wake na Serikali, kampuni hiyo inalipwa asilimia 1.9 katika ya asilimia 3 za mrahaba inaolipwa Serikali ya Tanzania na makampuni ya madini ya dhahabu.

Dk. Slaa alisema kufuatana na barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, katika mwaka wa fedha 2005/06, Alex Stewart (Assayers) walilipwa shilingi 14,175,753,189.46 kama malipo ya ukaguzi wa mahesabu ya makampuni ya dhahabu, ijapokuwa "hakuna ripoti za ukaguzi zilizowasilishwa na wakaguzi hawa kuhusu ukaguzi uliofanywa katika mwaka 2005/06."

Akimnukuu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Dk. Slaa alisema, "hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisha kwamba wakaguzi hawa wa dhahabu walipatikana kwa kufuata utaratibu wa zabuni ya ushindani."

"Kuna taarifa za kuwapo kwa rushwa na/au ufisadi kuhusiana na mkataba kati ya Serikali na Alex Stewart Assayers. Barua pepe iliyoandikwa na Erwin Flores ambaye ni Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni hiyo ya Novemba 14, 2006 inamtaja mtu mmoja mwenye wadhifa wa Waziri katika serikali ya Jamhuri ya Muungano na kuwa yeye pamoja na wenzake ambao hawakutajwa wana asilimia 12.5 za hisa kwenye kampuni hiyo na kuwa analipwa na kampuni hiyo," alisema Dk. Slaa.

Sehemu kubwa ye kesi hizo, ni mambo yaliyofanyika katika kipindi cha mwisho cha utawala wa awamu ya tatu ambayo ilijitambulisha kwa maofisa waandamizi serikalini kufanya kazi bila kujali kana kwamba walikuwa wakitarajia kuhama nchi.

Matukio kadhaa ya uhalifu kabambe miaka hiyo ya mwisho wa awamu ya tatu yanaonyesha mtiririko wa wizi wa kughushi, rushwa kabambe na maamuzi yasiyozingatia sheria, kanuni na taratibu za utendaji kazi serikalini.
 
Last edited by a moderator:
Serikali yenye vyombo vya dola inatishwa na mafisadi na kufyata mkia!!!! Kweli hapa kuna jambo kubwa sana lililojificha.
 
Back
Top Bottom