Uchaguzi 2020 Dr. Bashiru: Kama Membe anasema tatizo ni Urais agombee kwa chama chochote tukutane uwanjani

Uchaguzi 2020 Dr. Bashiru: Kama Membe anasema tatizo ni Urais agombee kwa chama chochote tukutane uwanjani

Sasa mbona wakiitisha mikutano mnawakamata na kuwafungulia kesi za uchochezi?
Kabisa.

Si lazima agombee kupitia CCM.

Kwanza keshawahi kugombea kupitia CCM na akashindwa.

Aende TADEA akagombee huko kama kweli nia yake ni kugombea urais na si ajenda zingine.
 
Mimi sijui nani kamdanganya, Kati ya watu wanaocheza karata zao vibaya ni Membe, kwanza hawezi kumshinda Magufuli,kama Magufuli alimshinda akiwa hana connections 2015 leo utaweza?,achana na sifa za kudanganywa eti wewe ni shushu mara ohh ni mwana diplomasia nguli watu wanakuingiza chaka mbaya, Tz kwa sasa kuna millions ya wana diplomasia tena wako kitaa tu hawana kazi, jifunze unyenyekevu na kuwa mvumilivu na utafaulu katika ndoto yako ya urais, kikwete alivumilia baada ya kushindwa na mkapa ,akawa mpole wakati ukafika akafanikisha , angekuwa jeuri asingeweza kutimiza ndoto yake, bado una nafasi kubwa kwa miaka ijayo.

Upinzani, mikikimikiki ya upinzani membe hutaweza, upinzani bongo unataka moyo,yaani unatakiwa uwe tayari , na uwe ngangari vya kutosha, yaani ulivyo mayai mayai itakuwa ngumu kwako , sikukatishi tamaa lakini huu ndo ukweli.
 
Traditionally wanamwachiaga incumbent second term, Membe alitaka Kula ubwabwa bila kunawa mikono.. nadhani sio Sawa na ni kukosa heshima na kujiona Bora zaidi...
Sasa kuondoa hayo manung'uniko si hiyo tradition yao si waiweke kwenye katiba ya chama
Au wanataka wajionyeshe wao wanaipenda democrasia kimaandishi lakini kiuhalisia amna demokrasia
 
Bashiru atuambie kilichsababisha Mangula kupata kiharusi
Ugonjwa wa mangula unahusiana nini na story hii?
Ugonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa
Mbona chadema haijatuambia sababu ya kiharusi cha Marando tokea 2015 mpaka leo?
Watu kama wewe ndio mnaompoteza Membe,alidhani ana watu ccm,kumbe ana watu jamii forum na twitter
 
Okay, wameshamtimua sasa. Wewe na yeye mtafanya nini zaidi ya kunung’unika mitandaoni?

Hamjakatazwa na mtu kugombea huo urais.

Nendeni kwingine mkagombee au anzisheni chama chenu halafu mgombee.

Msing’ang’anie ambako hamtakiwi.

Ila, lengo lenu sidhani kama ni kugombea urais.

Lengo lenu ni kuleta vurugu tu ndani ya chama.
Na Rais ajaye ni paul

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli Ni palepale membe kafukuzwa kwa sababu ya kutaka kumpinga magu ndani ya chama.hivyo ndo vyama vyetu..
 
Hili jamaa lilikuwa CUF ya Lipumba..leo anawapangia CCM asilia ..kweli Wanyarwanda wametushika vibaya dawa yao xenophobia tu
 
Nimekuuliza tofauti ya Independent Candidate na Private Candidate, hujanijibu.

Tunaomba source tujifunze.

Mahakama ikiamua kwamba shirika ni mtu, katika muktadha wa sheria, hilo halimaanishi kwamba shirika ni mtu,

"First and foremost let us take the opportunity to correct one thing:
There is nothing like "a private candidate". That is a direct
translation from Kiswahili "mgombea binafsi". But the right
terminology is "an independent candidate", as Prof. Kabudi,
properly pointed out, and in this judgment we shall use that

terminology" Page 7 of The A.G Vs Rev Mtikila, Civil Case no 45 of 2009
 

Attachments

Bashiru unapaswa kufafanua zaidi, mkutane na Membe uwanja upi? Ni huhu ambao waamuzi wooote ni wa kwenu au mpya wenye waamuzi huru?
 
Back
Top Bottom