Dr. Cheni aeleza sababu za kutojihusisha tena na filamu nchini

Dr. Cheni aeleza sababu za kutojihusisha tena na filamu nchini

kinachoiangamiza Bongo Muvi sio suala la mauzo pekee...wajiulize mbona hata umaarufu wa Wasanii wa Muvi umekwisha kwa muda mrefu sasa...Hakuna wasanii wapya wanaoibuka, zaidi ya kubaki na wale wale wa tangu miaka zaidi ya kumi iliyopita ukilinganisha na wenzao wa Bongo flavour, Majina ni yale yale JB, Ray, Aunty, Wolper, Rose Ndauka, Uwoya n.k.

Na kama hizo kazi zingekuwa zinasambaa kwa njia ya uharamia kama anavyojaribu 'kutujaza' Dr Cheni basi bado tungeona Wasanii wengi wapya wanaibuka na umaarufu wa Bongo muvi ungebakia kama sio kuongezeka...labda ambacho mngekosa ni pesa tu.

Hata Wasanii wa Bongo flavour hawauzi CD, lakini kwa nyimbo zao kuchezwa hovyo na kuchomwa hovyo mitaani ndio tunashuhudia kuibuka kwa Wasanii wapya kila siku.

Kilichoiua bongo Muvi ni ubinafsi ulioendekezwa na hao hao wanaojiita 'Waanzilishi' wa Bongo muvi....wao baada tu ya kuona Watanzania wamewapokea vizuri wao wakajifungia kwenye chumba chao kama Wasanii na kuamini kwamba sasa ndio wakati wa kuchuma mihela..walisahau kabisa kwamba sanaa ya filamu ni matokeo ya team work, kwa maana ya Wapiga picha, Waandishi, Waongozaji n.k ndio maana mlishuhudia kina Ray wakijipa majukumu yote ya kuandaa filamu, muandishi yeye, Cameraman yeye, Muigizaji yeye, na wenzake walifuata mkumbo huo huo.....Wao waliamini kuwa Wasanii wangeweza kusafiri kivyao na kufaidi mihela ya Watanzania milele.

Wana kazi kubwa ya kurudisha imani ya Watanzania tena kwani sio kazi rahisi sana...kuna usemi maarufu kuwa 'bahati huwa haiji mara mbili' ila upo uwezekano wa kurudi tena iwapo tu watakaa chini na kutaka kujifunza Filamu ni nini..

.....Sanaa ya Filamu/burudani huwa haifi, bali husinzia au kuwa kwenye coma hata kwa miaka mia moja iwapo kutakosekana ubunifu na uelewa, mpaka hapo watakapojitokeza watu sahihi wa kuirudishia uhai.
 
View attachment 428444Mwigizaji na mtayarishaji wa filamu nchini, Dr Cheni amesema hatatoa tena filamu nyingine kutokana na hali ya kibiashara ilivyo katika tasnia ya filamu hapa nchini

Dr. Cheni alisema hayo alipokuwa akizungumza na E News ya EATV ambapo alisema kuwa kazi zao hazina ulinzi na haiwafaidishi wasanii ndio maana huoni umuhimu wa kuendelea kutoa kazi hizo

Dr. Cheni alisema ukitoa leo filamu mpya baada ya siku moja utaikuta imesambaa nchi mzima ikiwa inauzwa tena kwa bei chee, alipoulizwa hadi lini ndo atatoa filamu, alisema kuwa hadi hapo Serikali itakapoingilia kutatua suala la kazi zao

"Siwezi kutoa tena filamu hadi Serikali itakapo hakikisha kuwa kazi zetu zipo salama, ukitoa filamu leo siku moja ya pili ya tatu unazikuta chini zinauzwa ambazo ni bandia, kilio chetu sisi bongo movie ni kazi zetu zinaibwa, namuomba Rais Magufuli aingilie kati suala hili kwani vijana wengi wamejiajiri kwenye bongo movie "alisema Dr Cheni

Chanzo : Swahilitimes
Aache upuuzi wa kususia kazi kuna sehemu the great marehemu Kanumba alishawahi kususia kazi aseme tu biashara ya ngada inalipa na imemneemesha
 
Kusema ukweli kila alie wapigia sisiemu wacha aumie tu maana akili xitawarudi
 
Hali imezidi kuwa mbaya kila sekta ni vilio tu
Naona wengi mmeamua kutokumuelewa Dr. Cheni, kasema kazi zinaibiwa, wengi naona mnalazisha kuwa JPM na the so called MAISHA MAGUMU.
 
Hebu tuache mboyoyo...kuna uhusiano gani kati ya kudorora soko na kushiriki kampeni za chama?

Basi na mhusianishe mafanikio ya Diamond na kampeni...maana naye si alishiriki?

Nadhani mmekosa tu cha kushauri na sasa mnatafuta njia ya mkato.

Hao Wasanii waliounga mkono upinzani ni wangapi sasa wanakula matunda ya mafanikio kutokana na kufanya hivyo?
Kidogo nimekuelewa ijapo sijajihusisha na CCM
 
wasubiri uchaguzi ujao wakusanywe tena washonewe sare wazungushwe nchi nzima sindano ipenye dawa iingie
 
Back
Top Bottom