DR Congo hali ilikuwa tete sana, tangu mimi nizaliwe sijawahi kuona matendo kama yale ambayo tulikuwa tunafanyiwa sisi

DR Congo hali ilikuwa tete sana, tangu mimi nizaliwe sijawahi kuona matendo kama yale ambayo tulikuwa tunafanyiwa sisi

Kigoma Region Tanzania

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2021
Posts
230
Reaction score
611
Raia 2643 Kutoka kongo-DRC wameingia mkoni kwetu Kigoma kuomba hifadhi kutokana na machafuko ya vita yanayoendelea nchini kwao baina ya jeshi la nchi hiyo na waasi wa M23

#VisangavyaCongo
1-Msafiri Jampiele
-Kule kongo, hali kule ilikuwa tete sana, maana tangu mimi nizaliwe sijawahi kuona matendo kama yale ambayo tulikuwa tunafanyiwa sisi.

Maana watu walikuwa wanatoka porini, watu tusiowajua, kwenye usiku tu mnalala watu wanaingia, bahati mbaya unakuta wazazi wanafariki, bahati mbaya watoto wanafariki, yani wanauwa watu pasipokua na hatia.
Yaani vile vikapeleka vifo sana ndani ya nchi ya kongo, ile sehemu tuliyokuwa tunaikaa nchi ya Goma, vifo vikakua sana sana sana, watu wakaona hapana, tukizidi kukaa hapa au kuishi hapa, tutapata matatizo sana. Watu wakaamua hapana wacha tukimbilie Tanzania, ili angalau wenzetu wataweza kutupokea ili tupate makao mazuri.

Mimi nimeshuhudia rafiki yangu akiuwawa mbele ya macho yangu, ambaye tulikua naye, saa nne za usiku, maana tulikua tumetoka kuangalia TV sehemu fulani, kuangalia kufuatilia mambo ya mpira haya, muda wa kurudi ndo tukaona watu wanatupiga Taa usoni, wakatushika pale, vizuri mimi nikakimbia.

Nilipokimbia nikafichama sehemu fulani, yule ndugu yangu nikashuhudia jinsi wanavyomfanya pale, wanamfunga kwenye uso, wakampiga mapanga na mimi mwenyewe nikaona, nikashuhudia macho yangu nikifichama, wala hawakuniona, lakini nikashukuru MUNGU maana nikafika nyumbani salama.

#VisangavyaCongo
2-Stanley Goliati
Familia yangu, yani shikupata muda ya kufika nyumbani, baada ya kuambiwa na rafiki yangu kua, yaani ni mtoto ya rafiki yake ya bhabha ni mwanajeshi wa M-vingttrois, akaniambia kaka mzee kashakamatwa, mzee alishakamatwa,

Yaani baba yangu na mama yangu walikamatwa wakawafunga kamba kwenye kimti wakachukua Bidoo ya vide, unajuaa Bidoo, ambalo halina maji wakaweka juu wakachukua kibiriti wakachoma, wakafia hapo kwenye mti.

Mimi nikapigiwa simu niko shamba yaani sikupata na muda wa kusema kwamba niende tena nyumbani, ahh nilipatwa kwanza na uwoga, na hata bibi yangu, mke wangu na watoto sijui kwenye wako, kwa hiyo niliokoa nafsi yangu tu ndo nikaja huku hivi.

336466060_136377045803266_6947514292117630813_n.png
 
simple logic
hivi inamaana hao waasi wameshindwa kudhibitiwa kabisa na majeshi yote,inamaana ni wajanja au wana special weapons kushinda majeshi yote ambayo yamejaribu kurejesha amani huko Congo,, KDF,MUNOSCO,Jeshi la Congo etc

poleni sana ndugu wakongo,karibuni sana bongo nchi ya wajuaji na matajiri wa mchongo,,huku hata sijui mtakula nini maana kwetu Ugali ni laana hata bodaboda siku hizi wanajifichaficha maana na wenyewe kazi yao ni kama laana,karibuni bongo
 
Poleni ,ila andika tu kiingereza mkuu umepotezea content kwasababu ya lugha
Wewe uwezo wako wa kufikiri unadhani Kila nchi inatumia lugha ya kigeni ya kiingereza? Wao wanatumia Kifaransa na amejitahidi kuandika hiki ili audience ya waswahili imwelewe. Angetumia Kifaransa ungeelewa hata mstari?
 
Hawa watu wa Kongo hawana militia. Kijiji cha Tanzania watu hawawezi kukimbia kwa sababu mtu amepiga risasi za Blanco angani.
Nimeona video imetoka juzi M-23 wamekung'utwa na nani sijui,wameachia maeneo fulani.
Majeshi ya EAC yanapelekwa kule. I hope they will be effective. What is happening there is not clear. Serikali ya Mobutu iliondolewa na US State Department. Who are the players now?
 
Wewe uwezo wako wa kufikiri unadhani Kila nchi inatumia lugha ya kigeni ya kiingereza? Wao wanatumia Kifaransa na amejitahidi kuandika hiki ili audience ya waswahili imwelewe. Angetumia Kifaransa ungeelewa hata mstari?
Hicho kiswahili ni cha Congo, na ndivyo walivyo ongea
 
Wewe uwezo wako wa kufikiri unadhani Kila nchi inatumia lugha ya kigeni ya kiingereza? Wao wanatumia Kifaransa na amejitahidi kuandika hiki ili audience ya waswahili imwelewe. Angetumia Kifaransa ungeelewa hata mstari?
😂Sasa uwezo wa kufikiri imekujaje mkuu, ifahamike baada ya mother language lugha ya pili kwa nchi nyingi ni kiingereza ndo mana sijasema kifaransa
 
Poleni sana ndugu zetu na majirani zetu,
Hali ya huko ni mbaya na ndugu zako wqmechagua vita mwanzo mwisho kama sisi tulivyochagua kuiba mwanzo mwisho hata umeme tu hatuna

Karibuni sana kwenye nchi ya vichekesho na utapeli
Hiyo idadi uliyoitaja likija suala la kuwahesabu Shirika la wakimbizi ili watoe msaada
Hiyo idadi tutapandisha x10 ili hela zililiwe na wasiokuwa na huruma na nyie

Maturubali na chakula wataiba
Yaani bora nikae na nyani
 
Raia 2643 Kutoka kongo-DRC wameingia mkoni kwetu Kigoma kuomba hifadhi kutokana na machafuko ya vita yanayoendelea nchini kwao baina ya jeshi la nchi hiyo na waasi wa M23

#VisangavyaCongo
1-Msafiri Jampiele
-Kule kongo, hali kule ilikuwa tete sana, maana tangu mimi nizaliwe sijawahi kuona matendo kama yale ambayo tulikuwa tunafanyiwa sisi.

Maana watu walikuwa wanatoka porini, watu tusiowajua, kwenye usiku tu mnalala watu wanaingia, bahati mbaya unakuta wazazi wanafariki, bahati mbaya watoto wanafariki, yani wanauwa watu pasipokua na hatia.
Yaani vile vikapeleka vifo sana ndani ya nchi ya kongo, ile sehemu tuliyokuwa tunaikaa nchi ya Goma, vifo vikakua sana sana sana, watu wakaona hapana, tukizidi kukaa hapa au kuishi hapa, tutapata matatizo sana. Watu wakaamua hapana wacha tukimbilie Tanzania, ili angalau wenzetu wataweza kutupokea ili tupate makao mazuri.

Mimi nimeshuhudia rafiki yangu akiuwawa mbele ya macho yangu, ambaye tulikua naye, saa nne za usiku, maana tulikua tumetoka kuangalia TV sehemu fulani, kuangalia kufuatilia mambo ya mpira haya, muda wa kurudi ndo tukaona watu wanatupiga Taa usoni, wakatushika pale, vizuri mimi nikakimbia.

Nilipokimbia nikafichama sehemu fulani, yule ndugu yangu nikashuhudia jinsi wanavyomfanya pale, wanamfunga kwenye uso, wakampiga mapanga na mimi mwenyewe nikaona, nikashuhudia macho yangu nikifichama, wala hawakuniona, lakini nikashukuru MUNGU maana nikafika nyumbani salama.

#VisangavyaCongo
2-Stanley Goliati
Familia yangu, yani shikupata muda ya kufika nyumbani, baada ya kuambiwa na rafiki yangu kua, yaani ni mtoto ya rafiki yake ya bhabha ni mwanajeshi wa M-vingttrois, akaniambia kaka mzee kashakamatwa, mzee alishakamatwa,

Yaani baba yangu na mama yangu walikamatwa wakawafunga kamba kwenye kimti wakachukua Bidoo ya vide, unajuaa Bidoo, ambalo halina maji wakaweka juu wakachukua kibiriti wakachoma, wakafia hapo kwenye mti.

Mimi nikapigiwa simu niko shamba yaani sikupata na muda wa kusema kwamba niende tena nyumbani, ahh nilipatwa kwanza na uwoga, na hata bibi yangu, mke wangu na watoto sijui kwenye wako, kwa hiyo niliokoa nafsi yangu tu ndo nikaja huku hivi.

336466060_136377045803266_6947514292117630813_n.png
Hivi ni Kwa Nini hayo maeneo ya Goma na kivu serikali ya Kongo isihamishe watu wote kuwapeleka sehemu zingine wakaishi
 
NATAMANI NIANDIKE TUSI ZITO SANA.
WANAUANA WAO KWA WAO.
VITA NI CONGO KWA CONGO.
WEUSI KWA WEUSI.

HII NI LAANA.

WAAFRICA WOOOTE
WAKONGO WOTE NI MA KU
 
Hawa watu wa Kongo hawana militia. Kijiji cha Tanzania watu hawawezi kukimbia kwa sababu mtu amepiga risasi za Blanco angani.
Nimeona video imetoka juzi M-23 wamekung'utwa na nani sijui,wameachia maeneo fulani.
Majeshi ya EAC yanapelekwa kule. I hope they will be effective. What is happening there is not clear. Serikali ya Mobutu iliondolewa na US State Department. Who are the players now?
Mkuu sometimes ukifikiria unahisi there is something behind this scandal hivi kama wanaweza kufukuzwa na watu wachache inawezekanaje serikali ikashindwa? Unajiuliza au Kuna mtu nyuma ya pazia ni kama hawafukuzwi kiukweli EAC wapo pale ni kweli wamewashindwa? Ni kama serikali Huwa haiamui tu kuwatoa


Au ndo Ile jambazi anakamatwa Leo usiku kaachiwa , akifanya tukio polisi wanafika baada ya tukio kuisha
 
Back
Top Bottom