Tetesi: Dr. Dau kufikishwa mahakamani. Yasemekana kahojiwa TAKUKURU

Tetesi: Dr. Dau kufikishwa mahakamani. Yasemekana kahojiwa TAKUKURU

Status
Not open for further replies.
, anatarajiwa kufikishwa mahakamani
wakati wowote kutoka sasa. Anaandika
Pendo Omary…(endelea).

Dk. Dau anatuhumiwa kuingiza NSSF hasara
ya mabilioni ya shilingi, kutokana mikataba
ya kinyonyaji. Amekuwa katika shirika hilo
kwa miaka 15.

Taarifa kutoka serikalini na taasisi nyingine
zinazoshughulikia uchunguzi zinasema, Dk.
Dau ambaye aliong’olewa NSSF 15 Februari
mwaka huu, atafikishwa kwa mahakamani,
kujibu tuhuma za ufisadi zilizoibuliwa ndani
ya shirika hilo.

Tuhuma nyingine ni matumizi mabaya ya
madaraka, uzembe na ukiukwaji wa taratibu
katika miradi ya uwekezaji na vitega uchumi
mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Miongoni mwa miradi hiyo, ni ujenzi wa
daraja la Kigamboni; hoteli ya kitalii jijini
Mwanza, mradi wa ujenzi wa majengo katika
mji mpya wa Kigamboni, uwekezaji kwenye
jengo la biashara la Mzizima na mgodi wa
mkaa wa mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya
Yeees, afikishwe... wako wazalendo walitonya siku nyingi kwamba 'motivation' ya vigogo wa NSSF kuingia/kuanzisha miradi mikubwa sio tija ya miradi ila ni kufisidi shirika. mradi wa milioni mia moja unajengwa kwa bilioni huku zaidi ya nusu ya fedha zikiishia mfukoni kwa hao vigogo. tumeona vigogo wa NSSF wakijitosa hata kuonekana kogombea miradi mikubwa ya kutisha kama daraja la kigamboni huku wananchi wakionyesha mashaka kuhusu ustawi wa NSSF.
 
Dada yangu; ile ikuwa geresha tuu ya kupewa ubalozi, dhamira ya JPM ilikuwa kumtoa pale kama DG wa NSSSF ili wananchi wasishtuke; so ubalozi haupo hapo na JPM lazima ampeleke ndani, kumbuka kauli za JPM alishasema hatangalia sura au title ya mtu ni lazima awekwe ndani

angalia mfano mwingine wa Katibu Mkuu kiongozi aliepita Ombeni Sefue yupo wapi mpaka leo? unataka kuniambia kuwa JPM hawezi kumtafutia kazi nyingine ya kufanya mpaka kwa kipindi hiki? huyo nae ndo kishaachwa.

JPM ana akili sana na anajua how to work na ntazidi kumuombea JPM kwa Mungu ili azidi kumpa Busra na ulinzi.
sipaoni ambapo dr dau atakwepa asiingie mahakamani, bahati mbaya kwake.. fraday kwake yaweza kuanzia au kuishia segerea na huo utakuwa mwanzo wa maisha mapya,
 
Itabidi itungwe sheria mtu akifanya ufisadi zaidi ya bilioni hakuna mjadala nikunyonga tuu kama china watu waeshimu ela za wananchi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom