Dr. Diallo: Katiba inatengenezwa na Wananchi siyo Wanasiasa, 2014 tuliikosa katiba mpya kwa ubinafsi wa wanasiasa CCM ikiwemo!

Dr. Diallo: Katiba inatengenezwa na Wananchi siyo Wanasiasa, 2014 tuliikosa katiba mpya kwa ubinafsi wa wanasiasa CCM ikiwemo!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Dr. Anthony Diallo amesema ni makosa makubwa na hatari sana kuwaachia wanasiasa watengeneze katiba ya nchi.

Diallo amesema wanasiasa ni wabinafsi hivyo lazima wajipendelee ndio maana katiba ni lazima itengenezwe na wananchi wakisaidiwa na Wataalamu kama ilivyofanyika nchini Kenya.

Diallo yuko mubashara Star tv akihojiwa na Aloyce Nyanda.
=======

Dkt. Anthony Diallo: Mimi sio mtaalam sana wa masuala ya katiba lakini naamini kitu kimoja, katiba huwa ni ya watu, ni ya wananchi wa nchi ile. Katiba haiwezi kuwa ya chama, kosa moja tulilofanya wakati ule mwaka 2014 kwamba vyama ndio vilivyotaka kutengeneza katiba, sio katiba ya wananchi.

Kama mlifuatilia utaratibu uliotumika Kenya, wataalam walichukuliwa wakapelekwa kwenye eneo fulani linaitwa Bomas wakachakata wataalam wa Sheria.

Walipomaliza ikapitiwa tena na wataalam wengine, baada yakupitiwa wakapata draft, ile draft ikapelekwa kwa wananchi kwa kura za maoni, haikwenda bungeni straight.

Sisi hapa unasikia wanaopiga kelele wanasiasa, hakuna nchi ambayo katiba yake hata hii ambayo tunaitumia leo ya 77 ilikuwa revised lakini original katiba ni ya Lancaster ya mwaka 60 ambayo ndio ilitengenezwa tukisaidiwa na wataalam wa kiingereza kwa ajili ya uhuru wa Tanganyika.

Katiba wanasiasa tunafanya makosa kujiingiza, ukijiingiza mwanansiasa kwenye katiba, katiba ile itakuwa biased tu, si ntataka kujipendelea.

Pili, nchi za kiafrika tunafanya makosa sana kuona Katiba ndio tatizo, tatizo lipo kwa watu. Mnafanya makosa, mnaweka Rais ambae atakuja kuvuruga hiyo katiba, kwani katiba ya leo inaruhusu mtu anawekwa Magereza bila kupelekwa mahakamani? Yalifanyika, tatizo letu ni mtu wala sio katiba
 
Ameongeza kwa kusema nchi imepita kwenye kiza kinene ktk kipindi cha miaka 5. Rais wa awamu hiyo hakuheshimu utu, haki na alivunja katiba wazi wazi.

Anaomba tuwe tunarejea histori za wagombea kabla ya kuwapa urais. Kamwe tusirejee tuliyoyapitia.

IMG_20210709_222102_934.jpg
 
Arudi kusoma vitabu vya Civics topic ya direct and indirect democracy!
Screenshot_20210709-223013.jpg
 
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Dr Anthony Diallo amesema ni makosa makubwa na hatari sana kuwaachia wanasiasa watengeneze katiba ya nchi.

Diallo amesema wanasiasa ni wabinafsi hivyo lazima wajipendelee ndio maana katiba ni lazima itengenezwe na wananchi wakisaidiwa na wataalamu kama ilivyofanyika nchini Kenya.

Diallo yuko mubashara Star tv akihojiwa na Aloyce Nyanda.

Na amesema tulikuwa na kiongozi mwenye matatizo ya akili. Hivyo tusirudie tena kupata viongozi wa aina ile. Anasema huyo jamaa alikuwa ni mlevi wa madaraka.
 
Na amesema tulikuwa na kiongozi mwenye matatizo ya akili. Hivyo tusirudie tena kupata viongozi wa aina ile. Anasema huyo jamaa alikuwa ni mlevi wa madaraka.
Diallo kama mkristo apewe sakrament 5
Kssema ukweli kabisa,anafaa kuwa mshauri wa Rais na UVCCM
Naenda kulipia kadi ya chama
 
Kwa kauli za Diallo inaonyesha alikuwa amezungukwa na maadui wengi sana ambao walikuwa na hasira naye sema walikuwa wanasapoti kinafiki.!
Diallo amekuwa mbunge na waziri kwa muda mrefu lakini hana legacy yoyote aliyowaachia watanzania kwenye utumishi wake.
 
Na amesema tulikuwa na kiongozi mwenye matatizo ya akili. Hivyo tusirudie tena kupata viongozi wa aina ile. Anasema huyo jamaa alikuwa ni mlevi wa madaraka.
Alichokisema Diallo ni kweli ila kuna watu hawataamini. Marehemu hakuwa sawasawa wakati wote. Kuna wakati, mara kadhaa alionekana yupo kwenye shida ya magonjwa ya akili, japo wengine wanaweza kuchukulia ni dhihaka.
 
Diallo amekuwa mbunge na waziri kwa muda mrefu lakini hana legacy yoyote aliyowaachia watanzania kwenye utumishi wake.
Kama umemuelewa ni hivi"Tatizo ni Chama siyo MTU"
Hata kama alikuwa waziri ningumu kuwa kinyume na mfumo wa chama.
Ambao ni M/kit taifa
Rais wa nchi,anatumia vyombo vya dola ukienda kinyume na anavyofikiri.

DIALLO HOYE!
 
Nasubiri kauli ya katibu mwenezi akimponda Diallo.Kijana hapendi ukweli,Nyanda huo mjadala urushe kama ulivyo unaondoa unafiki wa CCM.
KONGWA mawasiliano ni shida,tusaidiane ujumbe ufike.
 
Back
Top Bottom