Dr. Joyce Ndalichako, Katibu Mtendaji wa NECTA! "It's Time To Go!.


Mkuu Mkodoleaji, Hakuna syllabus ya Uingereza iliyotumika. Kumbuka kuwa Tanzania ni sehemu ya nchi nyingine duniani. Wametunga mitihani kulingana na syllabus inayopaswa kufundishwa Tanzania kwa muda wa miaka mnne. Lakini kama wameifuata watakuwa wametimiza wajibu wao kama Wakala wa Serikali. Sio kazi ya Baraza la Mitihani kwenda kuwauliza Wizara ya Elimu kuhusu walikoishia ili kutunga mitihani kulingana na walivyofundisha kwa lengo la kuwafichia aibu. Kama hakuna walimu, wanafunzi wanababia katika kusoma sio busara kutafuta mbinu za kuwatahini kutokana na kile wanachokipata, hiyo itakuwa ni kuua elimu; watalaam watakapatikana hawatakuwa na uwezo wa kushindana na watalaam kutoka nchi nyingine kwa sabau wamependelewa katika kupata elimu duni.
 
Last edited by a moderator:
Sasa nani bosi wa wanaotunga na wanaosahihisha?

kuna jambo ambalo watu hamlielewi kazi ya Joyce ni kuratibu mitihani tu na sio kuangalia mtahiniwa anajua nini. kinanishangaza sana ni kwamba hata format za mitihani ingawa zinatolewa na NECTA lkn msimamizi wake ni mwl wa somo husika.

sasa mtu format unayo, syllabus unayo kutunga unatunga wewe mwl moderation unafanya wewe mwl NECTA inakuja kuonekana kwenye uchapaji na usambazaji, kusahihisha anasahihisha mwl wa somo husika matokeo ninatumia statiztical package kuyapanga sasa necta anakosa gani hapo??

rudini kwanza mkaulize je vitabu vya kiada vinavyoruhusiwa na ofisi ya mkutubi mkuu vina kidhi viwango?? je sera ya elimu inakidhi mitaala iliyopo?? planning ya utolewaj wa elimu iko perfect?? mwalimu amewezshwa ipasavyo??
 
Eboh, Pasco kuna kitu unataka kusema ambacho sisi hatukielewi? Mitihani migumu? Au maswali nje ya mitaala? What do you exactly mean?
 

hakuna kisasi mkuu, labda utuambie kisasi ni kutunga mtihani standard kwa level yao.. au labda wanatumia mitaala tofauti...lakini kilicho na ukweli ni kuwa elimu yetu ni mbovu sana. Huwez amini nilikuwa wilaya ya Katesh huko Manyara, nimekutana na wanafunz wako form 2 hawajui hata kusoma kwa ufasaha, na kusoma kwenyewe ni kwa kiswahili, je English? unakaa chini na kujiuliza huyu anaenda wapi?kafikaje level hii? katika uchunguzi mdogo nilioufanya, wanafunzi wa hizi shule za kata baadhi yao wanaenda secondary kwa vi-memo vya madiwani na mwenyekiti wa chama (CCM) mwalimu mkuu/afisa elimu anaambiwa hawa waende shule kwani shule tulijenga kwa ajili yao...IMAGINE....mtu ni bonzooo lakin secondary anakwenda.
haya tujiulize ya STD 7, si walishusha wastani wa kufaulu to 70 ili watoto waende secondary? sasa kweli katika total marks za 250 mpaka 70 (28%) kweli halafu unasema amefaulu, hivi mnategemea nini form 4? MIRACLE? au mwataka kuingia kwa maajabu ya dunia?tena secondary wanafundikwa kwa English na shule zisizo na walimu na vitendea kazi vya kutosha...real wafaulu??? we real deserve haya matokeo ndugu zangu..
 



Huwa nasikiaga kuna nguvu ya hoja na pia kuna hoja ya nguvu. Kwa matazamo wangu hii ni hoja ya nguvu.

Hivi pasco umekurupuka toka usingizini? Waliofaulu walifanya mitihani kutoka wapi? non sense jipange. Hili jukwaa la magreat thinker usilete matapishi humu.
 
Suluhisho umeshalisema na litakiwa sehemu zote kwa muda mrefu na mfupi hakuna njia nyingine zaidi maana vyote ulivyovitaja pale ni vya lazima haukna jinsi labda hoja ibaki je ni jinsi gani ya kuvitekeleza1 tuache siasa kwenye maswala ya elimu na vitu viingine vya msingi na tuwe na vipaombele kwa mambo ya msingi kama elimu, nimesema siasa mfano wa mtaokeao ya darasa la 7 na form 2 ukweli wanafunzi wengine hawansifa za kuendelea ila kwa sababu wanatak sifa kwa watu kuwa wanafunzi wengi wamefaulu so wanaamua kufanya mzaha, kumbuka vitu vizuri kama huwa sio kwa wote ila ni kwa wenye sifa hasa pale mtu anapowezeshwa lakni akishindwa hana budi kuachwa
 
Mkuu wangu Pasco,

Heshima yako mkuu! Sikubaliani na wewe katika hili. Kushindwa kwa timu lawama apelekewe kocha na meneja wa timu na sio refarii.

NECTA wana jukumu la kutunga na kusahihisha mitihani kulingana na mtaala uliopo. Wenye dhamana ya elimu ni Wizara ya Elimu, NECTA ikiwa sehemu ndogo tu ya wizara hiyo.

Mimi nawashukuru NECTA kwa kutuonyesha uhalisia wa kiwango cha elimu. Tena nina wasiwasi kwamba uenda matokeo yalikuwa mabaya zaidi wakayapandisha kidogo; huu ni wasiwasi wangu kwani kunawatu siku kadhaa zilizopita wametoa mashinikizo matokeo kutangazwa. Hii inaonyesha kwamba kuna baadhi ya watu walishajua nini kinafuata!
 

Kwa hiyo Dancan unasema tutoe elimu bora kwa wachache na wengine waachwe?
 
Hiv huyu pasco ana elimu gani?yawezekana huyu ni mwanafunz wa kipndi kile cha kapuya,mtihan wa 98 uliovuja. Yawezekana ulipata divisn 1 kumbe kichwan wewe ni garasa.
Mkuu Kajunju, kwa hili la mimi kuwa garasa, linawezekana maana mimi nilisoma kipindi kile cha waalimu wa UPE!, mtihana wa daasa ra saba nilipasi ila baati mbaya sikuchaguliwa hivyo nikajiendeleza na erimu ya watu wazima ila sio kire kisomo cha ngumbaro, bali ni elumu kwa njia ya posta! huko hatuna mambo ya madivisheni!.
Pasco.
 
Kuna kutunga mtihani mgumu na kuna kutunga mtihani ambao sio ili kuwakomoa kina fulani!.

Mkuu Pasco, bila shaka hii mitihani ikitungwa lazima ihakikiwe na Wizara husika kabla ya kuwafikia wanafunzi, kwa maana hiyi kama mitihani ingekuwa siyo kwanini Wizara iliruhusu ifanyike?

Hapo tatizo ni nani, Ndalichako? Niseme tena nampongeza huyu mama kwa kubana kila kona ili mitihani isiibiwe ili tupate wanafunzi wachache lakini wenye viwango stahili.
 
ok tumekuelewa next time tutawashauri necta kila mwanafunzi atunge mtihani wake pamoja na majibu yake yatakayotumika kumsahihishia! na aufanye wao wasimamie kuhakikisha watoto wanapata zote. jambo la msingi ambalo sisi kama wazazi na wadau wa elimu tunapaswa kulifanya ni kujiingiza vyema kwa elimu ya watoto wetu. bado hatujawekeza vizuri katika elimu ya watoto kwa kuwa hatuoni vizuri umuhimu wa shule kwao. hebu chukulia wazazi wanalipa ada shillingi 1,200,000/- kwa shule ya awali ambayo kimsingi mtoto anatakiwa acheze na wenzake na ajifunze kidogo. lakini leo hii ukimwambia mzazi huyo huyo achangie shule ya kata shillingi 300,000/- tuweze kuboresha mazingira ya watoto wetu waweze kusoma vizuri hataki. sasa unategemea nini. lakini wazazi tumekuwa hatutimizi wajibu wetu, watoto wamekuwa hawana displine kabisa na tunawaangalia. hebu fikiri zaidi ya 50% ya wanafunzi muda mwingi wanavaa headphone wanasikiliza muziki na usiku wanaangalia moves saa ngapi wanasoma? shule za binafsi zinafanya vizuri lakini zinachangiwa zaidi na mazingira mazuri kwa kiasi fulani yaliyowekwa ikiwemo spoon feeding hili wanalitegemea sana lakini mimi nauhakika kama jamii tukijitoa kusimamia wajibu wetu tunaweza kubadili picha ya shule hizi muhimu: tujifunze kukubali kuwa sisi ndio chanzo cha uozo uliopo na si kuangalia taasisi zinafanya nini zaidi kila mmoja atimize wajibu wake na nina uhakika tutafanikiwa. wazazi wengi ukiwauliza ni lini walitazama maendeleo ya watoto wao au kwenda shule kuulizia mtoto anaendeleaje hupati majibu ya maana tunaishia kulipa ada na kuhifadhi risiti sasa hili ndilo tulilovuna.(wazazi tunastahili lawama kuzidi wanafunzi waliofanya mtihani)
 
Safi sana kwa haya maelezo, ila like siioni kabisa
 
Pasco umechanganyikiwa wife alikuambia peleka watoto shule nzuri ukang'ang'nia shule za kata. Kubali matokeo mkuu wanao wamepata kile baba yao alichowaandalia na serikali yako ya ccm. Dr joyce hapa hana kosa ulitaka awafanyie wanao mtihani
fikiria njia ya kucorect mistake uliyofanya mkuu
 
NECTA hawana kosa. Wao wametunga mtihani. Wapinzani wakisema bungen mnasema ooh vurugu onen sasa.

Nakuunga mkono Mkuu, Mgosi original, hebu fikiria mfano huu....unaenda kusoma shule ya udereva, mwalimu hakundishi gari, sheria na alama za barabarani zote au alikufundisha wewe hukuzishika. Unapenda kwenye trafic polisi watakuuliza mawaswli na road test kulingana na sheria na alama ulizopaswa kufundishwa, kama ukifeli kwa kuwa mwalimu wako wa driving school hakukufundisha au ulifundishwa lakini hukuelewa sio kosa la traffic polisi aliyekufanyia test bali yule ambaye hakukufundisha au wewe mwenyewe ambaye ulifundishwa lakini hukuelewa na ukakubali kwenda kwenye interview ilhali unafahamu kuwa hukulewa masomo husika.
 
Eboh, Pasco kuna kitu unataka kusema ambacho sisi hatukielewi? Mitihani migumu? Au maswali nje ya mitaala? What do you exactly mean?
Mkuu Takalani Sesame, eboh yako nimeipokea kwa mikono miwili!. Nisome tena na tena labda utanielewa!. Usiponielewa kabisa, then sorry its not me but someday you will, na kitakachokuelewesha sio mimi bali matokeo!.
Pasco.
 
Mkuu licha tu ya kuhakikiwa na wizara kwani hao waliofaulu japo ni wachache walifanya mitihani gani? na tujiulize kwanini ni hizo shule na sio hizo zingine?
 
Mkuu Takalani Sesame, eboh yako nimeipokea kwa mikono miwili!. Nisome tena na tena labda utanielewa!. Usiponielewa kabisa, then sorry its not me but someday you will, na kitakachokuelewesha sio mimi bali matokeo!.
Pasco.
Mkuu matokeo sio kipimo cha kujua ugumu wa mitihani maana kufeli au kufaulu kwa mwanafunzi kunasabishwa na vitu vingi ikiwemo maandalizi ya mwanafunzi mwenyewe
 
@pasco hebu angalia hii.



Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Joyce Ndalichako akionyesha karatasi ya majibu ya mmoja wa watahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2012, Dar es Salaam jana.
 
Pasco UCHOCHEZI JAMII (Public Incitement) una sura nyingi sana.........ikiwemo hii
Huyu ni mtu hatari sana kama anadhani anweza kuchezea akili za Watanzania, nilidhani angeongelea hata madai ya Walimu kulipwa stahili zao na motisha ni moja ya sababu, kwa akili ya Pasco ambayo imezungukwa na ujanjaujanja anadhani James Mbatia ni mpuuzi.

Pasco kwa hili hap JF humpati mtu yeyote makini kukuunga mkono mawazo yako yaliokaa kiujanjaujanja, Haki Elimu kila kukicha kwenye TV zote wamesambaza matangazo ya kukosoa namna watoto wetu wanavyoandaliwa lakini huko kote wewe huoni ila umemuona Ndalichako?

Huu ni msiba mwingine kwa Tasnia ya habari si tu kwa Wanafunzi walioferi, kama mwandishi mwenye Taaluma ya habari anakuja na hoja nyepesi na mfu kama hizi basi Taifa lina msiba mzito kila sekta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…