Dr. Joyce Ndalichako, Katibu Mtendaji wa NECTA! "It's Time To Go!.

Dr. Joyce Ndalichako, Katibu Mtendaji wa NECTA! "It's Time To Go!.

Daima watunga mitaala huwa wanatoa vitabu vya aina mbili; vitabu vya kiada na vya ziada (text books and reference books). Mtunga mitihani anachojali wakati wa kutunga mtihani ni concept iliyopo kwenye syllabus, kama kwenye syllabus watoto wanajifunza osmosis, mtunzi wa mtihani atatafuta sweli linalohusiana na concept ya osmosis kulingana na level ya mtoto. Hatatunga swali la form six akalileta kwa form four. Na uzuri ni kwamba utunzi wa maswali ya mitihani haufanywi na mtu mmoja. Random sample ya walimu kutoka mashuleni plus representative wa TIE huwa wanaparticipate. So mtu kukaa chini na kuanza kumrushia mawe Ndalichako, ni kutafuta visingizio visivyo na maana. Ukweli ni kwamba curriculum implementation haikuwenda sawa, walimu wapo kwenye Mgomo. Pasco asitake kukwepa ukweli. awaambie wakubwa wake kwamba walimu wapo kwenye mgomo, serikali itafute namna nzuri ya kusikiliza matatizo ya walimu.

Lukolo nakubaliana na wewe kwa maelezo uliyoyatoa, lakini kitu kimoja ufahamu matokeo ya mitihani ni zao la Baraza la Mitihani. Matokeo yakiwa mabaya watu watalalamikia Baraza la Mitihani. Kwa nini basi inakuwa ni kwa sababu Baraza ndio linalochagua watungaji, baraza ndilo linachagua wasahihishaji na baraza ndilo linatoa mitihani. Sasa kama syllabus haikutekelezwa yote, mitihani ingetungwa kutokana na kile kilichotekelezwa. Huwezi kutunga nje ya kile kilichofundishwa na kuwaita watoto wamefeli, watu watasema umewafelisha.

Sasa kama ulivyosema kumvagaa Ndalichako peke yake kwa kweli siyo sahihi maana mfumo mzima wa elimu una matatizo na ndiyo maana hata mitaala haikutolewa bungeni. Hivyo kuna haja kabisa ya kuufumua mfumo mzima wa elimu ili kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata elimu iliyo bora
 
Naungana nawewe kamanda ,inashangaza kuona kwamba mtihani huu wa mwisho ndio unapewa uzito mkubwa kuliko maendeleo ya mtoto akiwa darasani na mwalimu
Haingii akilini mwanafunzi afundishwe na mwalimu asiye na vifaa /nyenzo na motisha, halafu mwanafunzi aje apewe mtihani na NECTA (wenye mazingira mazuri ya kazi,vitendea kazi,motisha nk,hata kama watajitetea kua walimu wanaitwa kutunga na kusahihisha mitihani ,something must be wrong)

Hapa kuna tatizo kubwa sana ,uchunguzi wa kina unatakiwa ufanyike kuhusiana na hili swala, la sivyo hivi visasi vya NECTA vitalipeleka taifa shimoni

Kwa nini unaona kumpima mwanafunzi kwa mtihani wa mwisho sio sahihi katika kipindi hiki? Kwa nini sio zama zile ulizokuwa ukisoma wewe? Still NECTA wapo right.
 
Pasco umeongea point ambayo watu wengi hawataki kuiona.
Kwangu Mimi suala si Dr Ndalichako tu, ila hata Waziri Kawambwa na viongozi waandamizi have to go. Hatukatai kuwa kuna watoto ambao hawasomi, hilo tunalijua maaana wote tumesoma sekondari. Sasa sababu za kufeli haiwezi kuwa moja tu ya uzembe wa wanafunzi.

Sababu zinaweza kuwa zifuatazo:
1. Uzembe wa wanafunzi
2. Mfumo mbovu wa elimu
2.1. Kutokuwa na mitaala ya kueleweka
2.2. Kuwa na shule bila walimu
2.3. Kutokufanya ukaguzi wa kutosha
2.4. Kutokuwa na motisha kwa walimu
2.5. Kutoboresha shule za kata n.k.
3. Utendaji mbovu wa Baraza la Mitihani
3.1. Kutunga mitihani ambayo haiendani na mihutasari waliyopewa walimu kufundisha na wanafunzi kusoma (nakumbuka wakati nasoma Sekondari, nilisoma Book-Keeping na kulikuwa na kitabu kinaitwa Book Keeing for Tanzania Secondary Schools kama sikosei ambacho kilikuwa kinatolewa na Wizara ya Elimu, lakini hata siku moja hutapata swali kutoka ndani ya hicho kitabu. Maswali karibu yote yalikuwa yanatoka kwenye Frank Wood-Business Accounting ambacho wakati huo kukipata ilikuwa mbinde)
3.2. Kutokuwa makini katika usahihishaji
4. Kutowajibika kwa nchi (Uzembe wa Viongozi) (viongozi hawajui kuwa wanatakiwa kulijenga taifa hili kwa kupitia elimu). Nakumbuka kuna bwana mdogo ambaye alishindwa kuendelea na shule akiwa Form Three kutokana na uwezo mdogo. Baada ya miaka kadhaa ya kujishughulisha na biashara akapata fedha akataka kurudi shule ili aendelee. Ile shule aliyokwenda ili ajiendeleze kama Private Candidate akaambiwa alete barua toka ile shule aliyokuwa anasoma. Ile shule aliyokuwa anasoma wakampa barua, kwenda kwenye shule mpya wakamwambia aje na matokeo ya Form Two akawajibu kuwa mwaka wao mitihani ya Form Two ilikuwa imefutwa, ili ilikuja kurudishwa baadaye. Wakamwambia nenda baraza la mitihani ukachukue barua kuthibitisha hilo. Kwenda baraza la mitihani wakasema huweza kwenda form three mpaka ufanye mitihani ya Form Two upya. Huyo bwana mdogo akaamua kuachana na masuala ya shule aendelee na maisha yake mengine. Nimetoa huu mfano kuonyesha jinsi viongozi wasivyoona jinsi wanavyojenga taifa la wajinga kwa kutowajibika kwao. Sasa hao watoto 240,000 wanakwenda wapi? Kama siyo kuanza kufuga majambazi na machangu.
Pasco watu wengi, hawataona ulichosema, lakini hawa viongozi lazima waje na maelezo ya kutosha kuhusu sababu hizi zote. Vinginevyo they have to go.

Pia waangalie cha kufanya. Kwangu mimi kuna mambo mawili tu:
1. Mitihani isahihishwe upya
2. Mitihani itungwe upya na wanafunzi wafanye tena. Hili si mara ya kwanza maana mitihani ya Mwaka 1998 (kama sikosei) ilirudiwa mwaka 1999 baada ya kuona kuwa kuna udanganyifu mkubwa.

Samahani wadau nimeandika sana.
Umeeleza kwa umakini mkubwa sana ila sijaona point inayomfanya Ndalichako aachie ngazi,, mitihani ikisahihishwa upya matusi yatakuwa majibu sahihi? au vesi za bongo fleva na wasiojibu je nao watapewa alama gani? hoja zako za hapo juu ndio zilikuwa sahihi kabisa, Kuhusu kurudiwa mitihani mwaka 1998 ilirudiwa kwa sababu wao walishindwa kudhibiti mitihani so ukavuja this time unataka urudiwe kwa sababu zipi?
 
mimi naanza kuwa na mashaka, kama wizara haina mitaala (fake??) hao NECTA wanatumia ipi kutunga mitihani?

Lakini pia hapa tunaona vitu tofauti kutokana na hoja hii, walivyowambia wananchi mwanzoni juu ya elimu watawala (viongozi) wakabuni wazo la St. 'School' na wakadhani ndio ujanja. Hata walivyoambiwa walijipa confidence tu wakisema "hao wengine watajijua" na hata wakaenda mbali zaidi na kutuletea shule za siasa (za kata). Sasa kinachotokea ni dalili za mwazo wa tatizo na wala sio tatizo kamili. Fikiria NECTA wakifanya hivyi, je wakisema East Africa Community (EAC) tu harmonize pia elimu jaribu kufikiria itakuwaje kwa wanafunzi wa Kitanzania!!!
Tulimuhasi Mwalimu Nyerere bila kufikiria njia mbadala kwa kudhani 'rukhusa' inge animate vision ya elimu ya nchi.

LAKINI:
hebu tafakari juu ya hii logo ya NECTA na uhalisia wa elimu ya dunia ya sasa ....angalia symbols kama jembe, koleo, kitabu then ufikirie elimu ilivyobadilika kidunia!
necta.jpg
necta2.jpg
 
Au Pasco umeamua kumsulubisha Kawambwa indirectly? Jicho la tatu lanionesha hivyo. If that is what you meant I like your ingenious approach.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Kutunga mitihani ambayo haiendani na mihutasari waliyopewa walimu kufundisha na wanafunzi kusoma (nakumbuka wakati nasoma Sekondari, nilisoma Book-Keeping na kulikuwa na kitabu kinaitwa Book Keeing for Tanzania Secondary Schools kama sikosei ambacho kilikuwa kinatolewa na Wizara ya Elimu, lakini hata siku moja hutapata swali kutoka ndani ya hicho kitabu. Maswali karibu yote yalikuwa yanatoka kwenye Frank Wood-Business Accounting ambacho wakati huo kukipata ilikuwa mbinde)

Hapa sijakuelewa.......maswali yaoke kwenye kitabu? Sio yatungwe na wataalamu wa NECTA?
 
Kwa nini unaona kumpima mwanafunzi kwa mtihani wa mwisho sio sahihi katika kipindi hiki? Kwa nini sio zama zile ulizokuwa ukisoma wewe? Still NECTA wapo right.
Mimi nilishalipinga hili siku nyingi kamanda, kudhihirishi hilo niliona ni upuuzi na niliacha kufanya mitihani na test za darasani ikiwepo mitihani ya mock nikisubiri hiyo necta yao kwa sababu niliona ni upuuzi kupotweza muda kutengeneza cont. assessment isiyo na kazi.
 
Jamani kwa mtazamo wangu hawa wenzangu ni "Janga la Kitaifa" sana, hivi jamani nani yuko salama? Ndalichako yuko chini ya Kawambwa ambao wote wanaripoti kwa Kikwete,sasa mama wa watu kafanyaje. Mtoa mada hebu anza kwa Kawambwa kwani huyu Shukuru hajui kwa nini wanafunzi wamefeli acha kutafuta mchawi, Mchawi ni wewe mwenyewe. wewe mwenyewe umechukua hatua gani ili kuwafundisha wenzio elimu ni mwanga. Wewe endelea kulalamikia mama Ndalichako mwenzio ni dokta huyo, acha wivu:nono:
 
Umeeleza kwa umakini mkubwa sana ila sijaona point inayomfanya Ndalichako aachie ngazi,, mitihani ikisahihishwa upya matusi yatakuwa majibu sahihi? au vesi za bongo fleva na wasiojibu je nao watapewa alama gani? hoja zako za hapo juu ndio zilikuwa sahihi kabisa, Kuhusu kurudiwa mitihani mwaka 1998 ilirudiwa kwa sababu wao walishindwa kudhibiti mitihani so ukavuja this time unataka urudiwe kwa sababu zipi?

Dancan,
Hiyo mapendekezo kwangu yalitokana na vitu viwili: 1. Kwamba kwa sababu walimu wengi hawana motisha inawezekana hawakusahihisha kwa makini. Hapa utaniuliza je umakini utaongezeka wakisahihisha mara ya pili, naamini kama wakipewa motisha wanaweza kusahihisha kwa makini (lakini hapa hata mimi naona bado pagumu). Na pia kusahihisha upya haina maana hakutakuwa na watakaofeli (kama hao wa bongo fleva).

2. Pia kutokana na matatizo mengi ya wizara ya elimu, kuna uwezokano syllabus hazifundishwi kwa ukamilifu na mitihani ikitungwa kwa kuzingatia kuwa syllabus zilikamilika. Sasa kinachotakiwa kufanywa ni kutungwa mitihani mipya ambayo itawiana na syllabus ambazo zimekamilishwa. Huu ni ufumbuzi wa muda mfupi. Kwa ufumbuzi wa muda mrefu ni kuangalia matatizo yote yanayoikumba sekta ya elimu na kuyarekebisha. Sasa hili litaendana pamoja na kuwafumua viongozi ambao wamekaa lakini hawajayatatua haya matatizo ya elimu.
 
Jamani kwa mtazamo wangu hawa wenzangu ni "Janga la Kitaifa" sana, hivi jamani nani yuko salama? Ndalichako yuko chini ya Kawambwa ambao wote wanaripoti kwa Kikwete,sasa mama wa watu kafanyaje. Mtoa mada hebu anza kwa Kawambwa kwani huyu Shukuru hajui kwa nini wanafunzi wamefeli acha kutafuta mchawi, Mchawi ni wewe mwenyewe. wewe mwenyewe umechukua hatua gani ili kuwafundisha wenzio elimu ni mwanga. Wewe endelea kulalamikia mama Ndalichako mwenzio ni dokta huyo, acha wivu:nono:
 
Mkuu bado nashindwa kulielewa hili Bandiko...
Ila binafsi nikiwa kama mmoja wa wanafunzi wa zamani, nimeyatazama matokeo haya kwa namna tofauti kidogo.
Moja kwa moja ni ngumu kutambua ni nini chanzo cha matokeo mabovu, lakini nadhani kuna mambo mawili matatu ambayo huenda ndio yakawa chanzo.
1. Aina ya utunzi wa mitihani umezingatia uelewa kuliko kukariri (Mwenye kuelimika ndiye ataye faulu).
2. Kuna uwezekano pia mitihani ilikuwa ni migumu (Wanafunzi walikomolewa). Ukijaribu kuangalia idadi ya wafaulu wa daraja la kwanza utaona ni wanatahiniwa wachache mno waliofaulu kwa kiwango hicho.
3. Wapo wanaodhani kuwa mfumo wa utandawazi na teknohama pengine umechangia kwa asilimia kubwa, ila binafsi naamini hiyo sio sababu haswa ya msingi. Jaribu kuangalia matokeo ya shule zilizofanya vizuri Kitaifa mathalani St. Fransic, Marian Girls n.k(Hizi shule wanafunzi wao huwa hawa-interact na outside world)...utagundua kuwa kwa wastani shule hizo zimefanikiwa kufaulisha wanafunzi kwa kiwango kikubwa, lakini sasa kiwango cha ufaulu kwa watahiniwa wa Daraja la Kwanza, ni wa wastani mno...si kama tulivyozoea miaka ya nyuma kuona ufaulu wa Division I zile za "single digit" zikiwa za kutosha.

Kikubwa sana hapo pia wanafunzi wanawekwa kinidhamu ya kishule kama miaka hiyo ya zamani uzuri na wewe ni mtu wa zamani lakini tazama leo maisha ya wanafunzi jinsi yalivyo hakuna utofauti na watoto wa mitaani maana hata kwenye kumbi za starehe unawakuta hakuna wa kuhoji wengine wanaishi na mabwana kabisa ukiachilia mbali na wanaoishi geto kwa ghalama za wanaume,wakati zamani kwenda mjini tu ilikuwa ishu lazima uwe na get pass otherwise huna shule na ndio hizo shule tajwa hapo juu bado wanendeleza mfumo huo. kuhusu ugumu wa mitihani inawezekana ila aliyesoma marks zinapungua kidogo kama ilivyotokea kwa hizo shule ulizotaja, wa A hawezi pata F
 
Ni fikra za kivivu sana kufikiria kuwa eti kufeli kwa wanafunzi hawa kunasababishwa na Necta, pia ni utapiafikra kufikiri kuwa eti sababu za wanafunzi hawa kufeli ni moja au mbili tu, kwangu mimi hoja ya mbatia ndo ulikuwa msingi mzuri wa kuanzia kujadili tatizo hili! lakini je ni serikali gani hii isiyotaka kuwajali walimu kama haitoshi haitaki kujadiliwa bungeni?
 
Kama sylabus imetolewa shule makini zimefundisha kama inavyotakiwa na baadhi ya shule isiyo na maabara kwa mfano haikufundishwa ipasavyo ndalichako aende kuuliza kila shule mmefundishwa nn ili atunge mtihani au atunge kutokana na sylabus inavyotaka? Wale walochora katuni wameongezea watu wa kufeli ndalichako afanyeje?
 
Dancan,
Hiyo mapendekezo kwangu yalitokana na vitu viwili: 1. Kwamba kwa sababu walimu wengi hawana motisha inawezekana hawakusahihisha kwa makini. Hapa utaniuliza je umakini utaongezeka wakisahihisha mara ya pili, naamini kama wakipewa motisha wanaweza kusahihisha kwa makini (lakini hapa hata mimi naona bado pagumu). Na pia kusahihisha upya haina maana hakutakuwa na watakaofeli (kama hao wa bongo fleva).

2. Pia kutokana na matatizo mengi ya wizara ya elimu, kuna uwezokano syllabus hazifundishwi kwa ukamilifu na mitihani ikitungwa kwa kuzingatia kuwa syllabus zilikamilika. Sasa kinachotakiwa kufanywa ni kutungwa mitihani mipya ambayo itawiana na syllabus ambazo zimekamilishwa. Huu ni ufumbuzi wa muda mfupi. Kwa ufumbuzi wa muda mrefu ni kuangalia matatizo yote yanayoikumba sekta ya elimu na kuyarekebisha. Sasa hili litaendana pamoja na kuwafumua viongozi ambao wamekaa lakini hawajayatatua haya matatizo ya elimu.
Ni kweli kaka ila naomba ujue kuwa .Kwa ghalama za usahihishaji hizo hutolewa na NECTA haihisiani na mshahara tena walimu wengi hufurahi wakipata hiyo nafasi maana ni hela ya ziada
Kuhusu silabausi unapozungumzia ubora mara huwa lazima ubora huo ufuatwe tukisema itungwe mitihani kwa mujiwa silabasi zilizokamilka tutakuwa tunajidanganya maana shule zote haziishii pamoja utakuta wengine wako nyuma wengine mbele nk but cha muhimu sababu zote ulizotoa hapo mwanzo zifuatwe ili kukamilisha hizo silabasi maana ndio standard ya elimu kwa inchi nyingi sasa leo ukisema tutunge kulingana na uzembe wetu wa kutomaliza silabasi tutakuwa tunajidanganya wenyewe na tutaaibika huko duniani maana cheti hicho hakitumiki Tanzania pekee
 
Sijawahi tegemea hata siku moja mkuu wangu pasco utaandika kitu usichokielewa kabisa? Sidhani kama unaijua kazi ya necta...kama ungeijua usingelaumu hata kidogo
 
Ni kweli kaka ila naomba ujue kuwa .Kwa ghalama za usahihishaji hizo hutolewa na NECTA haihisiani na mshahara tena walimu wengi hufurahi wakipata hiyo nafasi maana ni hela ya ziada
Kuhusu silabausi unapozungumzia ubora mara huwa lazima ubora huo ufuatwe tukisema itungwe mitihani kwa mujiwa silabasi zilizokamilka tutakuwa tunajidanganya maana shule zote haziishii pamoja utakuta wengine wako nyuma wengine mbele nk but cha muhimu sababu zote ulizotoa hapo mwanzo zifuatwe ili kukamilisha hizo silabasi maana ndio standard ya elimu kwa inchi nyingi sasa leo ukisema tutunge kulingana na uzembe wetu wa kutomaliza silabasi tutakuwa tunajidanganya wenyewe na tutaaibika huko duniani maana cheti hicho hakitumiki Tanzania pekee

Dancan,
Nakubaliana na wewe kabisa nguvu ziwekezwe katika kutoa elimu tushindane na watu wengine duniani. Hilo nimesema ni suluhisho la muda mrefu. Sasa suluhisho la muda mfupi ni lipi kama taifa? Maana tuna watoto laki mbili na ushee ambao wanaenda kuzagaa barabarani na kila mtu anakubali kuwa hili ni tatizo tufanyaje?
 
Back
Top Bottom