Dr. Leakey Abdallah yupo TV 1

Dr. Leakey Abdallah yupo TV 1

Acha kudanganya watu, Liki Abdallah ni mchumi kitaaluma na ana Phd , siyo aliitwa Dr kwa ajili ya mpira.

Nishamuona sana katika makongamano ya uchumi.

Acha utoto wewe..unapokosoa basi utoe na evidence..alisoma phd chuo gani na mwaka gani??..kumuona mtu kwenye makongamano ya uchumi hakumfanyi mtu kuwa PHD holder!..kumbuka huyo jamaa ni mfanyabiashara mwenye makampuni ya kutalii hivyo si ajabu kumuona kwenye makongamano hayo..
 
Labda hiyo PHD kaichukua after 96
watu waliokuwa wanapiga simu DTV akichambua mpira ndo walifananisha jina lake
la Liki ambali ni kifupi cha Malik....na Dr Leackey yule maarufu aliekuwa mvumbuzi wa vitu vya kale
kama binadamu wa kwanza huko Olduvai Gorge...

Ndio chanzo cha jina lake

Achana nae huyo jamaa hamjui Leakey
 
Dr Leakey = soka
Masoud Masoud = music

Jamaa Hawa nawakubali sanaaa.
Nilianza kumcheki Dr Leakey kwenye Euro 96 yaani ilikuwa poa sana kuiangalia DTV enzi zile. Alimfanya Michuzi awe mpokeaji simu tu toka kwa callers.
Pia namkumbuka sana enzi zile za UEFA cup wakati Galatasaray ikiua timu moja hadi nyingine pale Ali Sami Eni stadium hadi wakaotwaa ndoo Ya UEfa cup. Enzi za Hakan Sukur na Arif Edem
 
Eddo ni mmoja wa wachambuz mahir sana kwenye kizaz cha sasa na namkubali sana kwenye upande wa creativity kwangu mimi naona dr leaky ni mzur sana kwenye historia kuliko kuuchambua mchezo wenyewe
 
Dr Leaky ndo alioanzisha hii kazi ya 'uchambuzi wa soka Tanzania'

Yeye ndie pioneer na mtu ambae hata wamama wasiopenda mpira wanafurahia kumtazama
akiongea kuhusu mpira.....

Watu walionza kutazama TV juzi ndo wanauliza 'eti kwa nini anaitwa Dr'

Kumbe wakati jina linaanza kule DTV enzi hizo hamkutazama?

Hakujiita yeye Mwenyewe....aliitwa na watu ..mashabiki wa mpira...
Wengine hawakuwa na luninga enzi hizo mkuu,wengi wameanza kumiliki luninga na visimbusi dtv ishapotea.walokuwa na tv miaka ya 90 mpaka early 2000 walikuwa wakuhesabika mtaani,hasa huku uswahilini
 
Ukimuongelea mwalimu kashasha unanikumbusha jinsi alivyokuwa anachambua world cup kwa weledi wa hali ya juu.
 
Dr Leakey = soka
Masoud Masoud = music

Jamaa Hawa nawakubali sanaaa.
Nilianza kumcheki Dr Leakey kwenye Euro 96 yaani ilikuwa poa sana kuiangalia DTV enzi zile. Alimfanya Michuzi awe mpokeaji simu tu toka kwa callers.
Pia namkumbuka sana enzi zile za UEFA cup wakati Galatasaray ikiua timu moja hadi nyingine pale Ali Sami Eni stadium hadi wakaotwaa ndoo Ya UEfa cup. Enzi za Hakan Sukur na Arif Edem
Umenikumbusha huyu Masoud Masoud, hichi kizazi kinahitaji sana kuwasikia na kujifunza kwao.
Dr. Leakey
Mwl. Kashasha
Eddo Kumwembe
Jeff Leah
 
Back
Top Bottom