Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Mtu yeyote anayechukua posho mara mbili kwa kazi ile ile anafanya makosa bila kujali ni rais wa nchi, waziri, mbunge au diwani wa kata.

Tusitetee mtu hapa na badala yake tutetee sheria. Kama kwa kupambana na mtu mmoja serikali imefungulia mkondo wa maji, hilo ni jambo jema kwa taifa maana ni nafasi ya kuwaumbua wote wanaofanya hivyo.

Nashangaa kuna watu wanakuja hapa na kusema kuchukua posho mbili sio kosa, inaonyesha jinsi Watanzania tunavyoshindwa kuelewa na kuheshimu sheria na maadili.

Hata kama PCCB ni wabovu mno lakini kweli utawalaumu pale wanapoamua kumhoji mtu ambaye amefanya kosa?

Tunajua polisi ni wala rushwa, kweli utawalaumu siku wakiamua kukukamata kwasababu umekula rushwa?

Ukitenda kosa usitafute mchawi na badala yake mchawi ni wewe mwenyewe. Mtu yeyote anayepigania jambo fulani lazima ajiangalia kwenye kioo na kuona yeye mwenyewe ni msafi, vinginevyo wabaya wake watammaliza na hilo ni kila sehemu hapa duniani.
Mkuu hakuna utetezi sana hapa bali utanielewa vizuri zaidi pale mwisho. Maana haya mswala ya posho mbili yameenea sana Serikalini. Ninaimani hakuna atakayepona katika hili si ofisi ya raisi si ofisi ya waziri mkuu. Uchunguzi wa kina ukifanyika double payments zipo za aina nyingi sana! Ni nani atakayekwenda kuchunguza Ofisi ya Waziri Mkuu?, Ikulu? Ni Hosea?? Ndiyo maana watapigana kufa na kupona kisiingie chama kingine kushika usukani wa Serikali. Na kama itatokea tukiwa hai nakuomba ukumbuke hii thread wakati madudu yatakapokuwa yanafumuka.
 
Samwel unashangaza JF yote, maana inaonekana wazi unachuki na hawa wabunge mahiri tena wa kwanza nchini kutoka chama cha mafisadi. Tulia kidogo ungoje watakayoyafanya na kufichua pale TAKUKURU watapomaliza kuwahoji au kuwatishia. Itaanza movement ya aina yake ambayo hizi posho zote zitabidi zianikwe ndipo na Ikulu itakapochafuliwa. Wabunge hapa wamejikuta wameingizwa mjini lazima wote wakubali. Maana walizidiwa ujanja pale walipopitisha mswada wa kuanzisha TAKUKURU lakini hawakujua kuwa wamemwongezea tena mkono mrefu Rasi, hawakuweza kuweka hata kipengele kuwa wao ndiyo wamchague kiongozi wa hiyo taasisi, sasa imewageuka mara ya pili. Ya kwanza ni pale walipojaribu kufukia ukweli wa mambo ya Richmond na sasa kuwahoji kwa nia ya kuwatisha. Wakisha hojiwa wakaja wamepoa wakaacha mapambano kitakuwa kimeeleweka. Na wasipolifanyia kazi swala zima la posho mbili mbili serikalini na nyingine za aina hiyo tutajua kuwa wameshapatiwa kile alichopata mbunge mtegemewa akaanza kutetea Richmond.
.

Mkuu.mbona unaongea pumba.Ninaishangaza JF?Wewe ni kiongozi wa JF?.Umejuaje kama kila mwana Jf anashangaa?.upeo wako mdogo mzee rudia tena kusoma post zangu.
 
Mkuu hakuna utetezi sana hapa bali utanielewa vizuri zaidi pale mwisho. Maana haya mswala ya posho mbili yameenea sana Serikalini. Ninaimani hakuna atakayepona katika hili si ofisi ya raisi si ofisi ya waziri mkuu. Uchunguzi wa kina ukifanyika double payments zipo za aina nyingi sana! Ni nani atakayekwenda kuchunguza Ofisi ya Waziri Mkuu?, Ikulu? Ni Hosea?? Ndiyo maana watapigana kufa na kupona kisiingie chama kingine kushika usukani wa Serikali. Na kama itatokea tukiwa hai nakuomba ukumbuke hii thread wakati madudu yatakapokuwa yanafumuka.
.

Mkuu wangu Mpenda tz.
Heshima mbele.Unashangaza sana mzee wangu.kama posho mbili zimeenea serikalini kwa hiyo dawa ni kuzihalalisha?hehehe.Kwa mtaji huu kweli tutafika?
 
Afadhali amekubali maana angeendelea kubisha yangemkuta yaliyomkuta Sendeka wangempa kesi ya kukataa amri halai ya kuitwa kuhojiwa.

Bravo Mwakyembe umekwepa mtego wa mafisadi
.

Afadhali yaliyomkuta Sendeka.Yaliyomkuta marehemu Kolimba je?
 
Mwakyembe alikataa kuhojiwa na TAKUKURU as a matter of principle kwamba wao walipendekeza kwenye tume yao kuwa Kiongozi wa Takukuru aadhibiwe kwa kupindisha ukweli; sasa kabla ya serikali kutekeleza agizo hilo la bunge wakaja na spin ya kutaka kuwathibiti wabunge kwa kupokea posho mbili mbili!! Sasa kama Mwakyembe amekubali kuhojiwa kabla ya Serikali kutimiza maagizo ya bunge maana yake hakuwaanaamini hoja iliyomsukuma awali kukataa kuhojiwa kabla ya mkuu wa Takukuru kuwajibishwa! Sasa hiyo ni weakness ambayo hapo baadae itamgharimu kwani hawa Takukuru lazima watamtafutia sababu ya kumtia hatiani na kudilute uadilifu ulioomyeshwa na kamati yake; na hilo ndio lengo lA SERIKALI!! He should have stuck to his guns!!
 
Mbunge wa Kyela Dkt Harisson G Mwakyembe alipokataa kuhojiwa na TAKUKURU kuhusu mambo ya posho mbili vyombo vya habari viliandika sana na wengine walimwona kama ni shujaa kwa kitendo hicho cha kukataa! Nilitegemea kwamba baada ya kujisalimisha TAKUKURU au kukamatwa kwa Mwakyembe na TAKUKURU basi vyombo vya habari vingeandika, unless taarifa iliyoandikwa humu JF ilikuwa haina ukweli wowote! Kama ina ukweli basi vyombo vya habari esp magazeti yaleyale yaliyoandika habari za kukataa kuhojiwa yangeandika! Wapambe wa Mwakyembe wanaweza kudai kwamba kuandikwa kwa habari za kuhojiwa kuna maslahi gani kwa nchi? Swali langu kwao ni kwamba kuandika habari za kukataa kuhojiwa kwa Mwakyembe, kitendo cha kuvunja Sheria ya nchi, kuna maslahi gani kwa taifa?
 
Under fair ground they suppose to report the same as they did on the first issue.
 
Jamani,

Kuhojiwa kwa Dk. Mwakyembe kumetangazwa na gazeti la Mtanzania na kichwa cha habari kikubwa kuwa "Mwakyembe ahojiwa", toleo Na. 4960 la Ijumaa Des. 11, 2009. Kwa mujibu wa habari hiyo, Mbunge huyo wa Kyela amehojiwa baada ya kuwekewa bayana hatari itakayomkuta mbele kama atakataa kuhojiwa, kwamba angekamatwa na maofisa wa TAKUKURU na wangemuhoji na kumfungulia shitaka jipya la kukaidi wito halali wa TAKUKURU. Chanzo cha habari hizo kinasema TAKUKURU walikuwa wanatekeleza maelekezo ya Spika aliyetaka Wabunge wahojiwe kwa aibu ya kuchukua posho mara mbili mbili kiwizi! Alisalimu amri akahojiwa. Subirini, labda ataitisha Mkutano wa Waandishi wa habari kuelezea, kama alivyofanya awali wakati anakaidi kuhojiwa!

Bwassa
 
sasa imethibitika na kubainika kua iliandikwa Buchanan ulitaka kutudanganya ?
 
Kwa hiyo kukataa kwake kulikuwa tu geresha! Presha kidogo tu kabend! Ha ha ha ha ha! Ndio kamanda wa vita against ufisadi - my ass
 
Takukuru ikamuhoji pia na mzee wa kagoda na mzee wa kiwira bana,inahoji udaga inaacha jodari😱
 
Back
Top Bottom