Elections 2015 Dr. Pombe Magufuli, Rais mteule wa Tanzania awamu ya 5

Elections 2015 Dr. Pombe Magufuli, Rais mteule wa Tanzania awamu ya 5

Chadema wana wabunge 60 mwaka huu. Unadhani unadhani Hao watakufa namna gani?
 
Mkuu kama hata idadi ya wapiga kura inazidi kila siku unategemea nini tukubali tu mateso Hamna jinsi!
 
Wana JF na Watanzania wenzangu,

Uchaguzi mKUU 2015 ndiyo umemalizika hivo kwa kumpata Rais wa Awamu ya 5 Dr. John Joseph Pombe Magufuli kwa kupata kura 8,892,935 kati ya milioni 13+ waliojiandikisha kupiga kura sawa na asilimia 58 % huku mgombea wa Upinzani Edward Ngoyayi Lowasa akipata kura 6,022,848 sawa na asilimia 39.97% almost 40%.

Kulingana na Takwimu za Tume ya Uchaguzi NEC tuliambiwa Watanzania millioni 22.75 walijiandikisha kupiga kura kati ya Watanzania milioni 48+. Lakini walijitokeza kulingana na matokeo haya ni milioni kama 14.9 tu. Hapa kuna milioni kama 8 hawakupiga kura na milioni nyingine 30+ wala hawakuhangaika na kujiandikisha kupiga kura ukiondoa walio chini ya umri wa miaka 18 kama takwimu hizi ni za kweli!

Rais huyu wa awamu ya 5 lazima aelewe na ajue kuwa ana mzigo mkubwa wa kuliongoza Taifa hili kubwa lenye watu karibia milioni 50. Tunajua wengi waliompa kura ni aidha wafuasi wa CCM au wafuasi wa chama na wasio. Kwa mantiki hiyo Dr. Magufuli hatakuwa Rais wa Watu milioni 8 tu waliompigia kura au wana-CCM pekee wala Wasukuma kabila analotaoka D. Magufuli. Hivo Rais wa awamu hii ya 5 ajue kuwa Watanzania milioni karibia 40 hawakumchagua awe Rais wao na hivo basi hawezi kujisifu wala kujitapa kuwa amepata Ridhaa ya Watanzania wote.

Ushauri kwa Dr. Magufuli ni kwamba lazima afanye kazi kwa unyenyekevu mkubwa kwa kuwaheshimu Watanzania wote waliomchagua na wale ambao hawakumchagua wakiwemo Wapinzani wake Kisiasa. Kama atatumia busara na hekima basi awashirikishe Wapinzani kwa maana ya vyama vya siasa ambavyo wamepata kura zaidi ya milioni 6 kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa itakayo saidia kuondoa manung'uniko, malalamiko na chuki za kisiasa ili nchi isonge mbele kiuchuni, kielimu na kiafya. Tanzania siyo ya Magufuli wala CCM ni ya Watanzania wote milioni 50!

Nawasilisha.

mmeanza kumfundisha kazi,,, hua hamchelewi
 
Hongera JPM kwa ushindi wako, cha msingi sasa ni kuchukua hatua za kuleta maendeleo na kuunganisha waTz wote kama ulivyotuahidi kwenye kampain.
 
alaumiwe aliyewasababishia watanzania ujinga na umasikini maana ndivyo vitu viwili vikuu vinavyowasababisha watanzania waichague ccm
 
Hahahahaaaaaa CCM haihitaji serikali ya mseto maana inajitosheleza mkubwa. Cha mwisho, issue ya madaraka ni ya kikazi zaidi na si kufurahishana au ulaji kama inavyotamkwa na wengi. Hapa ni kazi tu na si kufurahishana wala kujuana. Na Magufuli akitaka afeli basi ni rahisi sana. Atengeneze serikali ya kujuana na si kufanya kazi za watanzania kwa weredi na uaminifu. Namfahamu vyema na naamini hilo halitakuwepo.
 
Hongera hongera...kwanza ukatubu ikiwa umehusika kuwapoka watanzania ushindi wao! Lah kama hukusika basi waepuke wote walikuweka hapo ili wakufaidi. NAKUSA VUNJA HICHO CHAMA ACHANA NACHO KWANZA HUKUKITAJA KABISA KATIKA KAMPENI ZAKO. WAFUATAO NI WATU HATARI KATIKA UTAWALA WA AWAMU YAKO
1.huyu MTU anaekuachia kiti..ni hatari sana uismwamni katukatu..muulize Lowasa alichomfanyia licha ya mema aliyomtendea
2. January Makamba - pandikizi la kuuwa demokrasia..
3. Kinana..ni hodari wa kuuwa viongozi kwa maslahi yake...ni mhimili wa ufisadi na highest profile wa corruption - poacher no. one
4. Nape - kuwadi wa kinana.
5. Mwakiembe, Sita, Samia ...wazikaji wa haki za watanzania
6. Warioba - mchumia tumbo na mbinafsi
7. Wasanii wote waliokushabikia
8. Diallo - mkabila no. 1
9. Wahindi waliowengi - kina manji n.k
10. Raisi Mwinyi na Mkapa usiwategemee sana - hawana sifa kwa sasa kwa wababa wa taifa.
11. teua hata watu toka upinzani wawe katika serikali ijayo
12. Usikubali kuuwa demokrasi kama huyu anaekuachia kiti
13. anzisha chama kingene upesi hili ni suluhisho la kuachana na nguo inayonuka mavi na haraufu mbaya --CCM ni chukizo mbele za Mungu
MWISHO: Mwisho mtegemee YESU MUNGU ALIYE HAI
 
Naomba wale wote waliokuwa wanashabikia kauli ya mzee kingunge kwamba ccm imeishiwa pumzi bado wanaamini kauli ile au wameshafahamu kuwa yule mzee na mgombea wake ndio wameishiwa pumzi

Uko sawa kwa upeo wako. Na huko Zanziber mtasema Seif ameishiwa pumzi.
 
Kama ccm inataka kuongoza (sio kutawala) nchi hii kwa amani lazima wawe waungwana watafute njia ya kupooza zaidi ya roho milioni 6 ambazo zina masononeko na maumivu kutokana na matokeo ya huu uchaguzi yenye utata. Ni busara tu kutafuta namna ya kuonesha watu hawa kwamba hawakupoteza vyote. Watu mil. 6 ni wengi na wakiamua kuihujumu serikali hii mpya kimyakimya serikali na ccm watafeli vibaya. Na asilimia kubwa ya hawa watu ni wasomi na waelewa.
Kiufupi ccm waking'ang'ania kuchukua vyote na kuongoza kwa maguvu na kiburi watapata shida sana ktk uongozi wao.Lazima mtafute namna ya kuwaweka karibu wapinzani wenu ili muongoze nchi smoothly. Kebehi, matusi, ubabe na mengine km hayo yatampa Magufuli wakati mgumu sana!
 
Niliisha andika huko nyuma kwamba CCM ikishinda ktk uchaguzi mkuu wa mwaka huu na Chadema chini ya Lowassa ikashindwa, hakuna kingine kitakachofuata na huo utakuwa ndio mwisho wa Chadema.

Kwa msingi huo itakuwa ni ndoto kwa Chadema kushika dola ndani ya miaka 50. Subirini muone.

I beg to differ, Ingawa nilipenda sana JPM ashinde lakini siombei CDM ife, na si sahihi kusema kinachofuata ni mwiaho kwa CHADEMA. Mi naona kuna mtaji wa kutosha uliopatikana kuweza kujijenga zaidi na 2020 au 2025 kuchukua nchi, cha msingi ni wao kuji evaluate na kutengeneza njia za ku move forward bila ya ku change gia hewani
 
Huu wimbo wa mabadiliko, nimeimbishwa, mpaka nimeshtuka kumbe wimbo wenyewe hauna mashairi wala beat na kumbe mwimbishaji mwenyewe hakujipanga.

Kwa kweli mabadiliko niliyoimbishwa yamepatikana kwa aina yake, na mabadiliko niliyoyapata ndio haya:
1.Nisijiamini kipumbavu, kwa sababu Nina pesa, mwisho wake aibu, fedheha na kulalamika kwamba ninaonewa.

2.Nisifikiri pesa inabadili mioyo na iman za watu, kuhusu Mimi ni Nani?

3.Naalikwa kutafakari kwa kina kile ninachoona, kuamini na kusikia na sio kufuata miemko na hisia za walio wengi.

4.Nisitegemee shortcut/mkato kufanikisha mipango ya kimaisha.

5.Kujitambua na kufanya kazi kwa bidii ni mabadiliko.

6.Nisihofu yajayo, kwani yaliyopo yanatosha kwa hofu.

7.Umoja na Ushirikiano ni jambo la msingi katika kusaka maendeleo.

8. Tamaa mbaya,

9. Tamaa mbaya

10..........?.............

Mabadiliko ya kweli na ukombozi vinaanza na wewe, katika hali yako, nje ya hapo no ushiriki tu.
 
"Ikulu ni mahali patakatifu"~Mwl.JK
Watanzania tungekua wajinga sana kuwakabidhi mafisadi na genge lao la wapiga dili ikulu.Ongereni watanzania kwa kufanya maamuzi sahihi.na ongera JPM kwa kuaminiwa na watanzania.siasa zimekwisha sasa imebaki kazi tu.
 
UKAWA wameisoma namba laivu na Tinga Tinga linaingia Ikulu. Gwajima, Kakobe na Tb Joshua tuliambiwa kuwa wamemtabiria Lowassa kuwa atakuwa rais wa 5 wa Tanzania. Leo unabii wa uwongo wa manabii hawa umedhihirika na MUNGU amewaumbua manabii feki. Niliwahi kuandika humu JF kuwa hawa manabii ni wahuni tu na ni watu wanaotafuta pesa na sio kumtumikia Mungu. Kama kweli hawa wangekuwa ni manabii wa MUNGU basi leo tungeshuhudia Lowassa akitangazwa mshindi. Watu wamekuwa wakimsingizi MUNGU kwa kila kitu. Wengine walikuwa wanasema Lowassa ni chaguo la MUNGU na mimi niliwaambia kama kweli huyu ni chaguo la MUNGU basi atashinda, lakini kama sio chaguo la MUNGU kamwe hawezi kushinda urais.

Ilifika mahali nikauliza humu JF kuwa hivi ni lini mlimsikia MUNGU akiwaambia Lowassa atakuwa rais wa Tanzania?? Hakuna aliyenijibu. Sasa tazama tinga tinga lina tinga Ikulu bila wasi wasi. Wengine wakatuambia kama hatumpendi Lowassa, tukale "malimao" sasa mimi nawaambia hivi hayo "malimao" wale wao.

Wengine wakatuambia Lowassa ni "mafuriko" sasa mafuriko yamezuiwa na kidole na yako wapi hayo "mafuriko"??? Tinga tinga limezuia mafuriko???? Wengine wakatuambia Lowassa ana "intelligence" yake ndani ya Serikali hivyo anajua kila kitu na CCM hawawezi kuiba kura na yeye mwenyewe alisema kura za urais wamuachie yeye sasa mbona leo analalamika na kulia lia eti ameibiwa kura?????

Hah ah ha ha ha mimi leo nacheka sana, hivi yuko wapi Kingunge Ngombale Mwiru? Yuko wapi Fredrick Sumaye?? Yuko wapi Chizi?? Yuko wapi Juma Mwapachu?? Wako wapi hawa jamani, ha ha ha ha ha niambieni wako wapi????

Magufuli Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee CCM Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

#HapaKaziTu, SASA twendeni tukafanye kazi, tufanyekazi kweli kweli. #HapaKaziTu
 
Hili linchi halina maana tena.
Hapa ni kujiunga kwenye kundi la kifisadi.
Kuwanyonya haohao wajinga hadi wapate akili.
 
alaumiwe aliyewasababishia watanzania ujinga na umasikini maana ndivyo vitu viwili vikuu vinavyowasababisha watanzania waichague ccm

Ambaye ni nani.? Usiseme CCM sababu ndivyo jinsi anavyopenda kuona, kwamba tunaendelea kubaki na ujinga wetu ili tuendelee kuichagua
 
Back
Top Bottom