Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
-
- #281
PHP:
Alisema Baada ya kampuni ya Richmond kushindwa kuzalisha umeme, Septemba 2006, Bw. Aziz aliwasiliana naye akimwelezea tatizo la umeme akimshawishi awekeze kwenye umeme, akiamini kuwa mwekezaji anayetakiwa ni mwenye uwezo na anayeweza kufanya shughuli hiyo haraka.
"Mtakumbuka kuwa TANESCO iliomba kupitia kwenye vyombo vya habari mwekezaji mwenye uwezo wa kuzalisha kuanzia megawati 1 kuwasiliana nayo kuzalisha umeme wa dharura. Gridi ya taifa ilikuwa inaishiwa umeme kabisa.
"Hatimaye, Dowans ilifikia makubaliano na Richmond, kuwa kama TANESCO ingekubali kampuni yake ingechukua nafasi ya Richmond kuchukua mkataba wa kuzalisha umeme. Tuliamini kuwa Dowans ingepokewa vizuri na TANESCO, serikali na umma kama shujaa, kinachotushangaza haikuwa hivyo.
Alisema Dowans ililipa dola za Marekani milioni 109 (kwa ajili ya mitambo, vifaa vyake na wahandisi na baadaye kuongeza mtaji wa dola milioni 20.
Al Adawi alisema kuwa watu wasiokuwa taarifa sahihi wamekuwa wakiishutumu kampuni yake wakiita ya mfukoni, lakini yeye anawapa changamoto waoneshe kampuni nyingine ya mfukoni yenye mitambo ya dola za Marekani milioni 109.
Huu ni uongo mtakatifu.........bei ya mitambo ilikuwa ni dola za marekani 7.5 na wala siyo dola 109..............................