Elections 2010 Dr. Slaa kujibu maswali "Live" ITV saa moja Usiku Jumamosi Hii

Mie nitakwenda na family social centre kuwatch maana kuna dalili za mgao wa usiku

Asante Msanii laki usiwashau wale ndugu zako wa kijijini ambao muda huo watakuwa wametune kuangalia michezo ya kuigiza maana sitashangaa leo TBC wakiwarusha akina masanja na Joti muda huo
 
Wakuu
Tanesco wameshaanza kutu-beep huku kinondoni kusini toka asubuhi wanakata kata umeme.

Tuombe Mungu wasirudie haya jioni.
 
muda siyo mrefu nimepokea ujumbe unaosomeka hivi '' tujipange vizuri youthleague wote nchi nzima....wasomi...walimu wa vyuo vikuu...makada...wajumbe wa baraza kuu n.k...kumuuliza maswali ambayo yatamuudhi kwenye mdahalo wa itv jumamosi...yale ya usemasema uongo...ugoni na wake za watu...alivyoacha upadre,kufukuzwa ukatibu chama cha walemavu na sababu zake@n.k jipange vizuri ili chadema wasipate nafasi ya kupiga simu za kumjenga.mdahalo unaanza saa1 jioni.''
aliyeniforwadia ni kada wa chichiEM na ameniambia anayesambaza imean source ni mtoto wa mmoja wa wagombea urais na kiongozi wa umoja wa vijana wa chama kimojawapo kikubwa.

mytake/:
nawashukuru kwa kuwa wanasaidia kusambaza ujumbe ili watu wengi wasikilize mdahalo huo ambao naamini dr atawawin wote watakaompa muda wa kumsikiliza. hoja hizo ni nyepesi sana na ana majibu ya hoja zote hizo. wadau kazeni mwendo wa kusambaza ujumbe watu wasikilize mdahalo huu...mwamko wa mabadiliko ni mkubwa sana nchi nzima,kuchukua nchi ni very possible. Vote dr Slaa.


 
Hawajui kuwa ndo wanampa umaarufu Dr Slaa cha msingi wangemshauri JK nae apande next week
 
Mdahalo wa urais kesho

na Mwandishi wetu

TAASISI ya East Africa Business and Media Training Institute kwa kushirikiana na Vox Media Centre imeandaa mdahalo wa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Mkurugenzi wa Vox Media, Juvenalis Ngowi, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa mdahalo huo utafanyika kesho kuanzia saa 12 jioni na kurushwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha ITV.
Alisema mdahalo huo utafanyika katika Hoteli ya Movenpic na wananchi wataweza kuuliza mashwali moja kwa moja.
Ngowi alieleza kuwa mdahalo huo unatarajiwa kuhudhuriwa na watu 200.
Wagombea urais kwa Tanzania Bara mbali na Dk. Slaa ni Jakaya Kikwete (CCM), Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Peter Mziray (APPT-Maendeleo), Fahmi Dovutwa (UPDP), Mugahywa Muttamwega (TLP) na Hashimu Rungwe (NCCR - Mageuzi).
Huu ni mdahalo kwa pili kuandaliwa na Vox, baada ya ule wa kwanza kufanyika mwanzoni mwa mwaka huu visiwani Zanzibar ambao uliwakutanisha wagombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
WHICH IS WHICH JAMANI?SLAA ALONE AU ATAKUWA NA WENZAKE WA UPINZANI
 
Wamechoka, vichwa vinawauma maana hawashindani na Dr Slaa wanashindana na Poeple power..............................
 
ccm ni chama chenye wanachama wengi mbumbumbu, kwa Dr Slaa sina shaka nae, maana hata kama mdahalo ungeongozwa na Rostam, jamaa anaakili kali, anajua jibu kabla hujamaliza kumuuliza swali, Huyu si Kikwete, ambae anasubiri kushauriwa na makamba ndio ajue nini la kuongea.
 
Hata JK Mwenyewe Ikifika saa moka atatyuni ITV kumcheki Dr. Wa Ukweli
 
Hiyo Mipango nami nimeipata sehemu moja,

wazee wengi tu wamekaa wanasema Chadema wanatuudhi na hiyo wameifanya ndo salamu yao. Kaazi kwelikweli.

lakini na wananchi wa ukweli ambao tumechukizwa na hali hii pia tujipange kuuliza maswali ya maana ya kujenga. maana ccm maji ya shingo na ndo maana wanatafuta kashfa za nguvu kwa chama mbadala hata za kuua, kuleta fujo ili chadema wakireact credit zishuke kidogo

TUSIDANGANYIKE!!!
 

maanake huyu ni dr. Waukwelikweli.
 
Ha! Likizo ulojipa imekwisha? Mbona imekuwa fupi sana? Back to mada, as a background, uliza swali ukijua kuwa CCM iliizuia zanzibar ilipojiunga.
 
ni muhimu mkatupatia huo mjadara na inload ktk chart scane iliwambali tuweze ona
 
swali lako halina maslahi kwa taifa, ndio maana hayo mambo sisiemu waliyaweka kwenye ilana ya 2005 kwa kukurupuka na yakawashinda sasa wameyatoa, Slaa atajikita kwenye ilani zaidi na ninategemea Jenerali atajikita zaidi kwenye yale mambo yenye maslahi zaidi kwa taifa. Hilo la OIC tusubiri JK zamu yake ikifika umuulize
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…