Elections 2010 Dr. Slaa mgombea urais 2010 kupitia CHADEMA

Elections 2010 Dr. Slaa mgombea urais 2010 kupitia CHADEMA

Status
Not open for further replies.
mimi ninamaswala haya kwa dk slaa
1)endapo atashinda uchaguzi na kuwa rais nini atafanya katka kurudisha mahakama ya kadhi
2) vipi kuhusu swla la oic
3) vipi kuzibadilisha kuwa siku za mapumziko kuwa j3 na j4 badala ya j1 na j2 au kuongeza ijumaa?

Hivi huyu jamaa huwa anaandika kwakuwa ana lakusema au anaandika kwakua anataka kuandika?
 
Kwa kila kiwango katika medani ya siasa na uelewa wa mambo, Dr Slaa amempita kwa mbali mno, tena sana, ni kama umbali wa anga na nchi kavu. Tangu Dr. Slaa alipotangaza majina ya watuhumiwa wa ufisadi Mwembe yanga Dar es Salaam, hadi bungeni ambapo ameweka sawa masuala mbalimbali katika vifungu vya sheria na bajeti ya nchi. Hivi karibuni Dr. Slaa ndiye yeye pekee aliyeona madudu katika sheria ya uchanguzi ambayo JK yeye alimwaga wino bila hata kusoma. JK hatilii maanani kusoma katika misitari ndiyo maana ana uelewa mdogo wa mambo ukilinganisha na Dr Slaa. Kituko cha mwaka ni pale JK alipoulizwa akiwa nje ya nchi kwa nini nchi yako ni maskini wakati inamaliasili kibao. Yeye akajibu kwa mbwembwe kwamba hajui anashangaa. Sasa mtu anakuwaje rais kama hajui matatizo ya nchi? Dr. Slaa alishaona tangu mwanzo kwamba nchi yetu inakwamishwa na ufisadi ndio maana yeye na Tindu Lisu wakajitoa mhanga kuwakabili watuhumiwa wa ufisadi 11. CCM msiwe wanafiki, Dr. Slaa yupo juu sana, ameongoza nchi kwa mawazo mazuri japo alikuwa bado Mbunge. Akiwa rais neema imewashukia Watanzania.
 
Mi naamini Chadema pamoja na Dr. Slaa wapo makini na hawajafanya kosa kama watu wengi wanavyofikiria hapa!! kuwa na mgombea Urais ambaye anakubalika hii inachangia sana wananchi kuwa na imani na Chama na kuwachagua wabunge wa chama hicho.....nakumbuka mwaka 1995 ule umaarufu wa Mrema ulikipatia NCCR mageuzi wabunge....lakini toka wakati huo hakuna tena mbunge kutoka chama hicho!! kwa hiyo hoja ya kwamba chaddema itapunguza idadi ya Wabunge siioni mantinki yake kama watu wanafikiria nje ya box!! Go Slaaa Go....
We r not think just for tomorrow meal......................

You are spot on.........mgombea urais ana influence sana kwenye wagombea ubunge.....na mambo yalivyo mwaka huu weneye hela watapiata CCM hivyo CHADEMA ijipange mapema kupick up potential candidates watakaoachwa CCM....my take ni zaidi ya 50.....hatuhitaji tu rais wa upinzani bali idadi ya kutosha ya wabunge kuibana serikali maana sasa JK atakuwa anashuka mlimani (2010-2015) kama atashinda....sadly hiki huwa kipindi kibaya sana maana marais hawana woga tena wa kutochaguliwa....Mwinyi(1990-1995) madudu kibao CHAVDA,CIS,etc....Mkapa(2000-2005) RADA,JET,EPA,KIWIRA,NYUMBA ZA SERIKALI etc.....Kikwete??????
 
Ndugu Wanajamii forum,

Kwanza napenda kumpongeza mheshimiwa Slaa kwa uamuzi wake,

Lakini nimesikitika kwa uamuzi huo kwa hali halisi ya siasa za Tanzania hawezi kushinda na tutakuwa tumempoteza mchangiaji mzuri sana kwenye bunge lijalo,ninani atakuwa na ujasiri wa Dr.Slaa wa kukosoa sera mbovu za CCM na kuibua maovu akiwa nje ya Bunge,na pia atakuwa hajawatendea haki wapiga kura wake wa Karatu,angesubiri mwaka 2015 hapo angekuwa amecheza kete nzuri,

Ninahofia Slaa asije akaja kufilisika kisiasa kama Mheshimiwa Mrema,

Elisante Yona
 
Dk. Slaa kugombea urais


*Kamati Kuu Chadema yampitisha rasmi
*Ndoa yake yazua mjadala katika vikao
dr%20wilbrod%20slaa_thumb.jpg

*Ategemea udini wa Wakatoliki kushinda
*Viti Maalumu navyo vyawaletea kasheshe

Na Maregesi Paul

HATIMAYE Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimemteua Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilibrod Slaa, kuwa mgombea urais wakati wa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31.

Dk. Slaa alichaguliwa jana na wajumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho iliyokaa jijini Dar es Salaam.

Kutokana na hali hiyo, Chadema sasa itakuwa na kazi ngumu kumpata mtu makini
atakayekiwakilisha chama hicho katika Jimbo la Karatu, lililokuwa likiongozwa na Dk. Slaa kwa awamu tatu.

Taarifa za uhakika zilizopatikana kutoka ndani ya kikao hicho zilisema kuwa, uteuzi wa Dk. Slaa ulitawaliwa na mvutano mkali baada ya yeye kutotaka nafasi hiyo, huku akitoa sababu kuu mbili.

Kabla mwanasiasa huyo kupitishwa, mwingine aliyekuwa amependekezwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu, Profesa Mwesigwa Baregu, ambaye hakupitishwa. Baregu mwaka 2005 aliwatosa Chadema saa ya mwisho baada ya kukataa kuchukua fomu, ikabidi Mbowe ndiye ajitose.

Sababu ya kwanza iliyotajwa na Dk. Slaa alipokuwa akipinga kuwania nafasi hiyo, alisema hajafunga ndoa na mkewe, Rose Kamili, kwa kuwa alikosa sifa baada ya kujiondoa katika nafasi ya uongozi wa kiroho wa Kanisa Katoliki miaka mingi iliyopita.

Sababu nyingine iliyotajwa na Dk. Slaa kama kinga yake ya kumnusuru kuwania nafasi hiyo ni kitendo cha mkewe kuwania ubunge katika Jimbo la Hanang kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kutokana na sababu hizo, Dk. Slaa aliwaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa iwapo atakiwakilisha chama katika nafasi hiyo muhimu, jamii haitamwelewa tofauti na chama kinavyofikiria.

"Mwanzoni kulikuwa na mvutano, Dk. alikataa katakata, alijieleza sana, lakini mwishowe wajumbe walimtoa hofu, wakamwambia anazo sifa za kugombea, asiwe na hofu.

"Wajumbe walimwambia kuwa, kama ni suala la ndoa, Katiba haisemi mahali popote kwamba, mgombea urais lazima awe amefunga ndoa.

"Baada ya hoja hizo na nyinginezo, hatimaye akalainika, akakubali kukiwakilisha chama na sasa anasubiri baraka za Baraza Kuu na Mkutano Mkuu wa chama," kilisema chanzo chetu.

Habari za ndani zilisema Dk. Slaa aliingia makubaliano yasiyo rasmi na baadhi ya maaskofu Katoliki alikokuwa kifanya kazi kwenye Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) na anategemea kutumia ukaribu wake na maaskofu hao kupigiwa ndogo ndogo aingie Ikulu.

Mbali na mvutano huo, chanzo hicho kilisema mvutano mwingine ulioonekana kutikisa kikao ulikuwa katika hoja ya namna ya kuwapata wabunge wa Viti Maalumu wa chama hicho.

Katika kikao hicho, inasemekana baadhi ya wajumbe walitaka wajumbe wa mkutano unaowachagua wabunge wa Viti Maalum, wajigharamie nauli kutoka mikoani, wakati wajumbe wengine walitaka chama kiwagharamie wajumbe hao kwa kuwa kimekuwa kikiwagharamia wajumbe wa vikao vingine.

"Baada ya mvutano katika nafasi ya urais, shughuli nyingine ilikuwa kwa wabunge wa Viti Maalumu, kwani baadhi walitaka wajumbe hao wajigharamie na wengine walitaka chama kiwajibike kwao.

"Baadhi walisema iwapo wajumbe watajigharamia, wagombea na na baadhi ya wajumbe wa mkutano huo watashindwa kuhudhuria kutokana na kutokuwa na fedha, jambo ambalo litawapa nafasi wabunge waliokuwa madarakani kushinda kwa urahisi kwa sababu wao wana fedha.

"Mvutano haukuishia hapo, wajumbe wengine walitaka wabunge wa viti maalumu waliomaliza muda wao, wasiruhusiwe kugombea ili kutoa nafasi kwa wengine ili nao wapate uzoefu kisiasa pamoja na fedha kama walivyo wenzao waliomaliza muda wao.

"Pamoja na hayo, wajumbe walitaka chama kitakapopeleka majina ya wagombea wa nafasi hizo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), yapelekwe kwa kufuata uwiano wa kikanda ili kuepuka wabunge hao kutoka kanda moja kama ilivyo sasa," kilisema chanzo chetu.

Dk Slaa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, walipopigiwa simu kwa nyakati tofauti ili kuzungumzia mkutano huo, hawakupokea simu zao.

MTANZANIA ilimwandikia ujumbe mfupi Dk. Slaa uliosema hivi: "Dk. Shikamoo. Hongera nakupigia hupokei… Nimeambiwa maaskofu Katoliki wamebariki uteuzi wako. Tunakwenda mitamboni na ndo habari yetu. Pia na suala la kutofunga ndoa na mvutano wa Viti Maalum uliotokea. Tunaomba maoni yako tuwe balanced. Asante Mhe." Hadi saa tatu usiku alikuwa hajajibu.
Source: Mtanzania
 
habari zilizopatikana sasa hivi zinasema kwamba dk. Slaa ndiye mgombea urais wa chadema mwaka 2010.

9036dj.jpg

kikao kilichomchagua dr. Slaa kuwa mgombea urais wa chadema

more to come
hongera dr slaa kwa maamuzi yaliyo sahii kwa wakati sahii
 
Mimi nazani kadri siku zinavyokwenda Dr Slaa atafafanua yote. Tusubiri tuone
 
Ndugu Wanajamii forum,

Kwanza napenda kumpongeza mheshimiwa Slaa kwa uamuzi wake,

Lakini nimesikitika kwa uamuzi huo kwa hali halisi ya siasa za Tanzania hawezi kushinda na tutakuwa tumempoteza mchangiaji mzuri sana kwenye bunge lijalo,ninani atakuwa na ujasiri wa Dr.Slaa wa kukosoa sera mbovu za CCM na kuibua maovu akiwa nje ya Bunge,na pia atakuwa hajawatendea haki wapiga kura wake wa Karatu,angesubiri mwaka 2015 hapo angekuwa amecheza kete nzuri,

Ninahofia Slaa asije akaja kufilisika kisiasa kama Mheshimiwa Mrema,

Elisante Yona

Slaa kugombea na kushinda au kutoshinda karatu ni matakwa ya wananchi wa karatu.Wananchi wa Karatu wanaweza kuamua kuwa na msimamo uleule na kuwashangazeni.Kinachokuhakikishia karatu kuchukuliwa na CCM ni nini endapo Slaa atagombea Uraisi?

Kuacha kugombea Urais na kubaki kugombea ubunge ili hali wananchi wa Tanzania na wanazuoni wanamwomba agombee Uraisi utakuwa ni ubinafsi na Uchoyo.

Dr. slaa amesikiliza kilio cha watanzania na amechagua fungu lililo jema!

Bila shaka hii siyo habari njema kwa CCM kwa upande wa Urais na Slaa anaweza kuwashangaza wengi kwa kushinda Uraisi, kwani hata uwizi wa kura una kikomo chake!
 
yaani kama kweli viongozi ni chaguo la mungu, basi naamini dr. slaa ndio chaguo sahihi na tumuombe mungu atupe slaa wetu.
 
Lol! kazi ipo hapo Itabidi mama ajivue usisiemu hapo hana jinsi inabidi awe begakwabega nu mumewe....:welcome: CHADEAMA Mama Slaa
 
Ndugu Wanajamii forum,

Kwanza napenda kumpongeza mheshimiwa Slaa kwa uamuzi wake,

Lakini nimesikitika kwa uamuzi huo kwa hali halisi ya siasa za Tanzania hawezi kushinda na tutakuwa tumempoteza mchangiaji mzuri sana kwenye bunge lijalo,ninani atakuwa na ujasiri wa Dr.Slaa wa kukosoa sera mbovu za CCM na kuibua maovu akiwa nje ya Bunge,na pia atakuwa hajawatendea haki wapiga kura wake wa Karatu,angesubiri mwaka 2015 hapo angekuwa amecheza kete nzuri,

Ninahofia Slaa asije akaja kufilisika kisiasa kama Mheshimiwa Mrema,

Elisante Yona

Ndugu Elisante,
Mimi naamini kabisa kuwa kwa hali ya maisha yalivyo sasa, Dr Slaa atakuwa changamoto kubwa, kamwe hajafanya makosa, na wala hajawaangusha wana Karatu, CHADEMA itashinda tena huko. Kwa Slaa kugombea urais kutaongeza idadi ya wabunge wa upinzani Bungeni kwa hiyo chama tawala ccm (kama kitashinda) kitakuwa na wakati mgumu sana bungeni. Na pia tukumbuke ukweli kuwa masuala ya ufisadi yalilipuliwa kwenye viwanja vya Mwembe Yanga na si bungeni, kwa hiyo Slaa anaweza kuwafanyia watanzania akiwa popote. Nenda Slaa! Nenda Watanzaia tuko bega kwa bega, kuibwaga CCM inawezekana hata sasa, wananchi tuamke tuikomboe nchi yetu kutoka kwenye makucha ya ukoloni wa mafisadi. PAMOJA TUTASHINDA
 
Jamani huu ni muda wa dhahabu tuliokuwa tunausubiri,piga simu sasa,kama uko nje piga simu sasa,kama uko humu humu bongo ongea na jamaa na ndugu,kila mpenda mabadiliko tupatie kura 20++ kutoka vijijini,ni muda wa vitendo sasa,waelimishe,wapige kura ya mabadiliko,this is what we have been longing for for a long long time,we are always slow at taking chances but let's take this one!...Go go slaa Go go wind of change!
 
Ndugu Wanajamii forum,

Kwanza napenda kumpongeza mheshimiwa Slaa kwa uamuzi wake,

Lakini nimesikitika kwa uamuzi huo kwa hali halisi ya siasa za Tanzania hawezi kushinda na tutakuwa tumempoteza mchangiaji mzuri sana kwenye bunge lijalo,ninani atakuwa na ujasiri wa Dr.Slaa wa kukosoa sera mbovu za CCM na kuibua maovu akiwa nje ya Bunge,na pia atakuwa hajawatendea haki wapiga kura wake wa Karatu,angesubiri mwaka 2015 hapo angekuwa amecheza kete nzuri,

Ninahofia Slaa asije akaja kufilisika kisiasa kama Mheshimiwa Mrema,

Elisante Yona

Nadhani umefafanua vizuri alipofilisika Mrema akaja Slaa....basi atakuja mwingine kwa hiyo tumwache agombee
 
Source: Mtanzania

Hivi hili gazeti "mtanzania" huwa watu wanatoa hela kulinunua au linatolewa bure???????? Why it is this low?????

Habari za ndani zilisema Dk. Slaa aliingia makubaliano yasiyo rasmi na baadhi ya maaskofu Katoliki alikokuwa kifanya kazi kwenye Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) na anategemea kutumia ukaribu wake na maaskofu hao kupigiwa ndogo ndogo aingie Ikulu

Hivi waziri Mkuchika yuko wapi kwenye hili, je ingeandikwa na gazeti kwamba JK aliingia makubaliano yasiyo rasmi na baadhi ya mashehe kupigiwa ndogo ndogo kuingia ikulu serikali ingekaa kimya????

Kwa nini mitizamo ambayo inaonekana ni binafsi na habariz zisizothibitiswa zenye nia na sumu mbaya kabisa ya udini zinazidi kuwa popular siku hizi????????

SHAME ON YOU "GAZETI LA MTANZANIA"
 
I WISH DR SLAA AWE RAIS WETU,MUNGU MTANGULIE NA AFANYE MIUJIZA, Halafu tufanye yafuatayo:
1. Tuishinikize tume ya uchaguzi kutoa majina ya wapiga kura mapema kwa kila eneo walilojiandikisha ,make wana mchezo wa kupeleka jina sehemu nyingine( hasa sehemu ambazo ni tishio kwa CCM)ukienda kuangalia jina lako unakuta halipo, wanasema watashughulikia mara saa kumi na mbili inafika muda wa kupiga kura unaisha unakuwa umekoswa haki yako ya kupiga kura, hivyo watoe majina mapema na kwa usashihi ili wapiga kura wajue mapema kama majina yao yapo kwenye kituo walichojiandikishia.
2.Serikali iruhusu wanafunzi wa vyuo vikuu wapige kura za kumchagua Rais majumbani kwao kwani wengi wamejiandikisha kwenye vyou vyao( DSM,Morogoro,Dodoma ,Iringa na mahala pengine) lakini Vyuo vitafunguliwa baada ya uchaguzi hivyo watashindwa kupiga kura huko majumbani kwao watakapokuwa likizo.
3.CUF na NCCR Mageuzi viunganishe nguvu na CHADEMA,Lipumba amuachie Dr Slaa kwani kwa sasa nyota ya Dr Slaa inang'ara sana kuliko Lipumba,Dr anakubalika sana kwa sasa, tuachane na vyama vingine waganga njaa( TLP,UDP na vingine vilivyopo tu kwenye orodha ya msajili wa nyama,havijulikani kabisa nchini).
4. Sisi wenye uelewa na machungu ya nchi hii tuwahamasishe ndugu zetu(Kila mmoja ahamasishe ndugu zake huko vijijini )waache woga kwamba vyama vya upinzani vikiongoza nchi kutatokea ukosefu wa amani.Hizo ni propaganda tu za akina makamba na CCM yake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom