Droo ya robo fainali kombe la shirikisho la Azam Sport

Droo ya robo fainali kombe la shirikisho la Azam Sport

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,420
Reaction score
18,298
Droo ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam imechezeshwa leo ambapo mechi za hatua hiyo zimepangwa kuchezwa kwa siku mbili, Juni 27 na Juni 28, mwaka huu

Katika hatua hiyo watetezi, Azam FC imepangwa kuvaana na Simba SC, huku Yanga SC ikiialika Kagera Sugar, Namungo FC itacheza dhidi ya Alliance FC na Sahare All Star itacheza na Ndanda SC

Washindi wa mechi hizo watakutana katika hatua ya nusu fainali ambazo zitachezwa kati ya Julai 11 na Julai 12 mwaka huu

IMG_20200529_115634.jpeg
 
Naiona njia nyeupe kwa Yanga. Ila sijajua Mshindi kati ya Simba na Azam atakutana na nani.
 
Sijajua bado ila mechi ya simba na azam ni ngumu maana simba anataka kombe ,azam naye anataka kwenda confederation cup
Duh. Nimeona Mshindi kati ya Yanga vs Kagera atacheza na Mshindi kati ya Simba vs Azam. Hii ni wazi kuwa Simba itaharibu safari ya Azam na Yanga na kuirahishishia kazi NAMUNGO
 
Duh. Nimeona Mshindi kati ya Yanga vs Kagera atacheza na Mshindi kati ya Simba vs Azam. Hii ni wazi kuwa Simba itaharibu safari ya Azam na Yanga na kuirahishishia kazi NAMUNGO
Indeed
 
nawatamani vyura nusu fainali, watatueleza lile goli la morrison walilipataje ?
 
Back
Top Bottom