DStv badilisheni mtangazaji na utangazaji wa Kiswahili kwenye mechi za Kombe la Dunia

DStv badilisheni mtangazaji na utangazaji wa Kiswahili kwenye mechi za Kombe la Dunia

Huyu mtangazaji wenu anapayukapayuka na hata haieleweki anaongea nini. Kila wakati anapaza sauti na kuongea vitu visivyoeleweka wala kuhusiana na mechi iliyopo mubashara.
Yaani nilivosikia wachambuzi wa bongo tu nkapata kichefu chefu.,uswahili mwingi....ndio maana siku zote naangalia tv yenye wazungumzaji wa kiingereza...jamaa wako vizuri...wanatema reality na facts...ukija wa bongo Sasa no fact ,utumbo mtupu...siasa za Simba na Yanga zimeharibu Sana akili za wachambuzi .

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kiukweli hawa watangazaji wa kiswahili wa DSTV wanaboa mnoo.
Mapungufu makubwa niliyoyaona.

1. Mtangazaji anakuwa nyuma ya tukio, sisi tunaona tukio kwanza (goli au kosa kosa) halafu mtangazaji ndio anaibuka kusema kwa makeke wakati tukio limepita kwa nusu sekunde. Hiyo kitu inaboa sana. Nadhani ni kwa sababu watangazaji hawako live uwanjani, wanafuatilia sambamba na sisi tunaoangalia kwa Tv, hivyo sauti zao zitachelewa kidogo.

2. Hawako katika uhalisia kabisa, hususani huu utangazaji wa Maulid Kitenge (umejaa mbwembwe zisizo na maana) au ule kina Kibwana (wa Clouds Fm) ambao umejaa blah blah za kuiga uzungu, afadhali hata ule utangazaji wa option nyingine ya kiswahili (sijui jamaa wa RTD wale) ambao umekaa kiuhalisia kiasi.


Binafsi mpaka sasa watangazaji wa kiswahili wa Azam Tv kwenye ligi ya ujerumani ndio nawaelewa vizuri. Wale jamaa nawaelewa sana.
Watangazaji walikuwa Radio Tanzania,na External ,idhaa ya nje,
Jocob Tesha,Jurious Nyaisanga,Maria chipungahelo,Aboubakar liongo,nk,
Siku hizi ni kupayuka tu,
Wasafi walikuwa na mpayukaji mmoja,Zembwela,wakaona hatoshi,wakamuajiri Ktenge Ili apayuke zaidi,baade akakimbilia Efm,kwenda kupayuka zaidi!!
Efm pale,Kitenge,Gerald hando,Musa Kipanya,na Mdada mmoja,ukisikiliza Cha maana wanachoongea hakuna,ni utumbo mtupu!!
 
Huyu mtangazaji wenu anapayukapayuka na hata haieleweki anaongea nini. Kila wakati anapaza sauti na kuongea vitu visivyoeleweka wala kuhusiana na mechi iliyopo mubashara.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Tumepigwa
 
Kiukweli hawa watangazaji wa kiswahili wa DSTV wanaboa mnoo.
Mapungufu makubwa niliyoyaona.

1. Mtangazaji anakuwa nyuma ya tukio, sisi tunaona tukio kwanza (goli au kosa kosa) halafu mtangazaji ndio anaibuka kusema kwa makeke wakati tukio limepita kwa nusu sekunde. Hiyo kitu inaboa sana. Nadhani ni kwa sababu watangazaji hawako live uwanjani, wanafuatilia sambamba na sisi tunaoangalia kwa Tv, hivyo sauti zao zitachelewa kidogo.

2. Hawako katika uhalisia kabisa, hususani huu utangazaji wa Maulid Kitenge (umejaa mbwembwe zisizo na maana) au ule kina Kibwana (wa Clouds Fm) ambao umejaa blah blah za kuiga uzungu, afadhali hata ule utangazaji wa option nyingine ya kiswahili (sijui jamaa wa RTD wale) ambao umekaa kiuhalisia kiasi.


Binafsi mpaka sasa watangazaji wa kiswahili wa Azam Tv kwenye ligi ya ujerumani ndio nawaelewa vizuri. Wale jamaa nawaelewa sana.
Hawapo live uwanjani kivipi,si nimeskia wapo qatar jamn kila mechi watakua live au[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Kwa Sasa Kuna Gharib Mzinga wa azam, yule jamaa anajitahidi
Akiwa anatangaza mechi anakua na taarifa za wechezaji wote, sio kama wale WA TBC hawajui hata mchezaji anaeingia sub, shwaini zao
Huyo gharib Yuko well informed yani,dogo anajianda Sana na mechi anayoenda kuitangaza...
 
Kama unatazama DSTV, pale ni VISUAL sasa sauti hata sio lazima.

Hata kwa anayetangaza kupitia TV halazimiki kuelezea kila kitu maana Watu wanaona, hiyo sio Redio.

Kazi ya Mtangazaji sanasana ni kwa ajili ya kufafanua mambo madogomadogo kama sheria za soka ili Mtazamaji asiyejua aelewe baadhi ya maamuzi ya Refa, au mara moja moja kutoa wasifu wa Mchezaji n.k.

Otherwise sio lazima kumsikiliza Mtangazaji.
 
Hawapo live uwanjani kivipi,si nimeskia wapo qatar jamn kila mechi watakua live au[emoji848][emoji848][emoji848]

Quatar ya wapi? Wamejifungia kwenye kachumba hapa hapa na wao wanaangalia kwenye Tv kama sisi.
 
Kiukweli hawa watangazaji wa kiswahili wa DSTV wanaboa mnoo.
Mapungufu makubwa niliyoyaona.

1. Mtangazaji anakuwa nyuma ya tukio, sisi tunaona tukio kwanza (goli au kosa kosa) halafu mtangazaji ndio anaibuka kusema kwa makeke wakati tukio limepita kwa nusu sekunde. Hiyo kitu inaboa sana. Nadhani ni kwa sababu watangazaji hawako live uwanjani, wanafuatilia sambamba na sisi tunaoangalia kwa Tv, hivyo sauti zao zitachelewa kidogo.

2. Hawako katika uhalisia kabisa, hususani huu utangazaji wa Maulid Kitenge (umejaa mbwembwe zisizo na maana) au ule kina Kibwana (wa Clouds Fm) ambao umejaa blah blah za kuiga uzungu, afadhali hata ule utangazaji wa option nyingine ya kiswahili (sijui jamaa wa RTD wale) ambao umekaa kiuhalisia kiasi.


Binafsi mpaka sasa watangazaji wa kiswahili wa Azam Tv kwenye ligi ya ujerumani ndio nawaelewa vizuri. Wale jamaa nawaelewa sana.
Yule mwamba wa TBC anaitwa Nazareth nadhani anajua sana
 
Huyu mtangazaji wenu anapayukapayuka na hata haieleweki anaongea nini. Kila wakati anapaza sauti na kuongea vitu visivyoeleweka wala kuhusiana na mechi iliyopo mubashara.
Atakuwa Juma Nkamia huyo kama siyo Denis Mpagaze
 
Tatizo la watangazaji wa kiswahili wanafanya kazi kwa mazoea, na sio wataalamu

1. Hawana data!
ukisikiliza matangazo ya wazungu huwa wanatoa data za timu na wachezaji
unaeza pata darasa tosha la mpira
watakuambia rekodi ya timu ya mechi zilizopita
watakupa data za mchezaji mmoja mmoja mfano; idadi ya magoli, club anayocheza, historia yake nk
watakupa uchambuzi juu ya kocha na vikorombwezo vingi vingi vinavokupa burudani

mbongo utasikia tu mbungi inawekwa kati piga moja refuuu kule anapokea namba 23
naona mabaliko namba 10 anatoka anaingia namba 19....utopolo mtupu

hwafanyi research ya timu wanazoenda kutangaza, hata majina ya wachezaji hawayajui wanataja namba

2. Hawana lugha nzuri za kutangaza, zaidi ya kelele za kosakosa na mara chache hukaa kimya bila maneno!
wanajisahau sana
Wapo watangazaji wa kiswahili wanaotangaza kwa data na ufundi mkubwa mfano mzuri ni Gharib Mzinga wa Azam tv
 
Kuna wa TBC yeye hutaja tu nchi yoyote

Utamsikia "ni free kick kuelekea Portugal.....anapiga kule unababatiza mabeki wa Brazil unakuwa ni kona...anaenda kupiga kona nambari kumi wa Croatia...anapiga kona go go gooo...la la inatoka juu ya lango...ni goal kick kuelekea Poland...wakati huo huo Wachezaji wa Ecuador wanamlalamikia Refa kwamba Kipa aliugusa mpira ule".
 
Kuna wa TBC yeye hutaja tu nchi yoyote

Utamsikia "ni free kick kuelekea Portugal.....anapiga kule unababatiza mabeki wa Brazil unakuwa ni kona...anaenda kupiga kona nambari kumi wa Croatia...anapiga kona go go gooo...la la inatoka juu ya lango...ni goal kick kuelekea Poland...wakati huo huo Wachezaji wa Ecuador wanamlalamikia Refa kwamba Kipa aliugusa mpira ule".
😂😂😂😂 Huyo jamaa kaua.
 
Back
Top Bottom