DSTV yaondoa chaneli za Urusi kwenye king'amuzi chake Afrika

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Naona Western Bloc wanataka kubaki peke yao wanapiga propaganda vita ya Urusi na Ukraine ambapo Multichoice Afrika maarufu kwa kisimbusi chake cha DSTV imeiondoa chaneli ya Urusi ya Russia Today(RT) ambapo kwenye tamko lake wakisema hatua hiyo wamelazimika kuichukua kutokana na vikwazo vilivyowekwa na umoja wa Ulaya.

Mwanahisa mkubwa Multchoice Afrika ni kampuni mama ya Naspers ambayo asilimia 49 inamilikiwa na waholanzi wa Prosus. Mapema wakati vita inaanza EU ilipiga marufuku RT kuonekana barani Uropa.

DSTV ina visimbuzi milioni 20 vilivyo hai na kulipiwa barani Afrika, hata hivyo inawezekana uono kuwa mkubwa zaidi kutokana na vingi kuangaliwa kwenye ngazi ya familia au jamii kama bar na vibandaumiza.
 
Safi sana, Putin avurugwe kote kote, Warusi wazuiwe kwenye kila kitu hadi wamchukie na kuanza maasi.
Kuna Masheikh wanamsifia Putin kama mtume wamesahau kipodo alichowapa waislamu kule Chechnya.
 
Wacha waondoe tu..
Dikteta put-in abanwe!
 
RT naipenda sana ilinisaidia kubalance story za kina CNN. Nawakumbuka watu kama Murad Gazdiev aliyekuwa anaingia frontline kule Syria kutoa coverage ya mashambulizi ya ISIS. Gayane Chichakyan na mahojiano yake. Larry King (RIP) na uchambuzi wake wa siasa. Vipindi kama Going Underground na Boom or Bust. Miaka hiyo mpaka 2016 nilipoacha day school
 
Alianza Azam, hadi nilishangaa, mimi nilikuwa napenda kuangalia BBC, CNN, Al jazeera, France24 then narukia RT ili kubalance. Sasa wanataka tusikilize kelele za upande mmoja tu. Na ndio maana Russia alikuwa justified kupiga kituo cha TV kwasababu kama wao wanabana media, na yeye abane basi. Wanatunyima haki ya habari.
 
Ili tatizo haliwezi malizwa kwa vikwazo. Ni vyema wapiganao wakae chini wafike malengo yao.

NATO wazuie proceed zozote za nchi kujiunga kwao ili kuleta amani. Bila hivyo tutachelewa
 
Wewe naye unapotosha kweli uhitaji kubance story kwa kupitia RT?!!kama warusi wenyewe wameanza kushituka na kile kinachoonyeshwa kwenye tv yao ya taifa,!!!?Aljazeera tu ndio mtambo wa kweli ukitaka habari za ukakika!!!na ndio maana kote anapigwa vita!!
 
Mrusi kama kweli mbabe kiteknolojia azirudishe hewani jinga kubwa arudishe hata Free To Air yaani FTA kama anajitia babe

Wanaume wanemfungia hana ubavu wa kurudisha hewani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…