Dubai na Tanzania zilikuwa chini ya mtawala mmoja? Ilikuwa nchi moja?

Dubai na Tanzania zilikuwa chini ya mtawala mmoja? Ilikuwa nchi moja?

Nilisoma kitabu Cha tiputipu hakika wazungu wameficha sana historia,pia wameanikiwa kuwafanya waarabu kua watu wabaya na wapenda utumwa wakati ni tofauti na uhalisia was kipindi hiko
Waarabu walikua madalali wa biashara ya utumwa huwezi waondoa katika hilo mana walishiriki kikamilifu kumuumiza mtu mweusi.

Mpaka leo hili liko wazi..

#MaendeleoHayanaChama
 
Waarabu walikua madalali wa biashara ya utumwa huwezi waondoa katika hilo mana walishiriki kikamilifu kumuumiza mtu mweusi.

Mpaka leo hili liko wazi..

#MaendeleoHayanaChama
Muarabu alipata vipi hao watu weusi kama siyo weusi wenyewe kushiriki kikamilifu?

Na mpaka leo hii liko wazi kwa yanayotokea sasa.

Acha lawama za upande mmoja, pande zote zimeshiriki.
 
Waarabu walikua madalali wa biashara ya utumwa huwezi waondoa katika hilo mana walishiriki kikamilifu kumuumiza mtu mweusi.

Mpaka leo hili liko wazi..

#MaendeleoHayanaChama
Mnachotaka kusema kipindi hiko mtu mweusi alikua boya sana hajui lolote.kujitetea,kujiongoza,kujisimamia unataka kuuaminisha watu watu weusi walikua hawajielewi? Tulishiriki kikamilifu kwenye biashara hiyo Kwa kupitia machifu..wakosaji,mateka na vijana wowote chifu aliiona wanafaa aliwauzia waarabu.

Pia ilikua lazima vifaa visafirishwe Kwa kupitia nguvu kazi kwahiyo machifu wakipewa pesa wanatoa vijana wao
 
Wazungu wameandika "edited version "ya history..

Hawataki tujue Empire zingine zilizokuwa powerful...
Omani Empire nasikia ilikuwa powerful kwenye maritime fleet kuliko nchi nyingi za Ulaya..

Mkuu wazungu ni watu wenye wivu sana, Ila ndio wanaitawala hii Dunia kwahiyo wanatupeleka wanavyotaka wao, Hata Jiwe wakilita mkate na sisi tutaishia kulita hivo hivo.

Wakati Wazungu wanagawana Africa Zanzibar ilikua ni tayari nchi kubwa ambayo walishindwa kuingia kiwepesi, walitumia njia za kijanjajanja kuiingia pamoja na kuikatakata himaya Zake, na mwisho waikaizika 1964 kwa Muungano uchwara ili kuizima kabisa pamoja na historia yake.
 
Waarabu walikua madalali wa biashara ya utumwa huwezi waondoa katika hilo mana walishiriki kikamilifu kumuumiza mtu mweusi.

Mpaka leo hili liko wazi..

#MaendeleoHayanaChama

Mkuu unsumbuliwa na chuki za kikabila au za kidini, Ukizungumza kuuzwa kwa watu weusi hata hao watu weusi wenyewe walishiriki kikamilifu katika kuuzana
 
CCM ndio mchawi wa hii nchi, Hii nchi bila ya CCM ingelikua mbali sana. Ni mambo yanayostaajabisha sana na kuacha maswali mengi ukisikia kuwa watu walikua wanazamia Zanzibar au Dar es Salaam kutoka arabuni kuja kutafuta maisha na leo tizama hali ya maisha ilivyo hapa na hao waliokua wanadandia majahazi kuja kutafuta maisha kwetu.
 
History ya nchi zetu inashangaza sana.

Cha ajabu Sisi wenyewe hatuchimbi history vizuri.

Around mwaka 1830 wakati Sultan wa Oman anaamua kuwa Zanzibar itakuwa second capital baada ya Muscat. Na akaweka gavana Mombasa na Dar es Salaam.

Huu utawala wa huyu Sultan huku East Africa ulianzia Somalia Hadi Msumbiji. Pwani yote ya hizi nchi za Tanzania, Kenya, Somalia na sehemu ya Msumbiji alitawala yeye.

Na Oman ilikuwa nchi kubwa Sana huko uarabuni sio Oman ya sasa, yaani UAE yote ilikuwa ndani ya Oman. Hiyo miji ya Abu Dhabi na Dubai ilikuwa haipo kipindi hiko ni vijiji tu vya watu wachovu. Zanzibar ilikuwa mji mkubwa kuliko hivyo vijiji vya Dubai enzi hizo.

Mpaka mwaka 1970 wakati UAE inaundwa Zanzibar ilikuwa Brand kubwa kuliko Dubai. Infact mikoa kama Tabora au Tanga ilikuwa miji mikubwa kuliko Dubai na Abu Dhabi.

Tunapaswa kuchimba Sana history kujua tulikosea wapi.

History yetu inashangaza sana
Tatizo la weusi kila mtu na tumbo lake akishiba anapeleka ulaya kwwnda kuficha ndugu zetu polisi najeshi wanawalinda hao mafisadi
 
Nilisoma kitabu Cha tiputipu hakika wazungu wameficha sana historia,pia wameanikiwa kuwafanya waarabu kua watu wabaya na wapenda utumwa wakati ni tofauti na uhalisia was kipindi hiko
Hapa ndipo mnapoharibu ninyi mabwana. Waarabu hawakuwa watu wema kwa waafrika wazawa. Waliuza watumwa maelfu kwa maelfu, mbaya zaidi waliuza hadi watumwa wa kizungu.

Tukirudi kwenye mada ya The Boss , historia kuhusu Zanzibar ipo wazi na imejaa kwenye vitabu. Tatizo ni kwamba watanzania hatupendi kusoma na kufanya tafiti. Hata kama tukisoma tunasoma ili kukidhi ajenda zetu za kidini, kikabila na kisiasa. Historia haitakiwi isomwe hivyo...

Kuhusu Zanzibar sasa, Sultani hakuishia Dar es salaam na Mombasa, alifikia sehemu nyingi za ndani. Dr Karl Jhulke wa Ujerumani alivyokuja Tanganyika ili kusaini mikataba na Lady Mbumi of Mkondokwa aliambiwa kabisa kwamba eneo lile liko chini ya Zanzibar.

Upande mwingine, Dr Karl Peters wa The Society for Germany Colonization, aliambiwa kwamba maeneo kama Arusscha (Arusha) na Kilimanjaro yalikuwa chini ya Sultani (Under Zanzibar Suzerain) baada ya machifu wa maeneo hayo kufanya mikataba na Sultani.

Ukisoma zaidi, mkataba wa chifu Mangungo unamtambua mangungo kama Sultan, na siyo Traditional Chief. Hivyo inaonesha kabisa utawala uliokuwa unafahamika maeneo hayo ulikuwa ni ule wa kinzanzibari wa kisultani, kwasababu maeneo hayo yalikuwa chini ya Zanzibari.

Ushahidi wa hili ninalolisema uko kwenye barua ambazo Sultani aliwaandikia wafalme wa Uingereza na Ujerumani baada ya mkataba wa Berlin akilalamika kwanini wamegawana maeneo yake bila yeye kushirikishwa. Tafuta hizi barua utazipata...

Binafsi, huwa nasema ni heri waarabu waliingiliwa (thwarted) mapema na wazungu katika kutawala sehemu za huku bara. Kama wasingezuiliwa, mambo mabaya sana yangefanyika huku. Mabaya mno....
 
History ya nchi zetu inashangaza sana.

Cha ajabu Sisi wenyewe hatuchimbi history vizuri.

Around mwaka 1830 wakati Sultan wa Oman anaamua kuwa Zanzibar itakuwa second capital baada ya Muscat. Na akaweka gavana Mombasa na Dar es Salaam.

Huu utawala wa huyu Sultan huku East Africa ulianzia Somalia Hadi Msumbiji. Pwani yote ya hizi nchi za Tanzania, Kenya, Somalia na sehemu ya Msumbiji alitawala yeye.

Na Oman ilikuwa nchi kubwa Sana huko uarabuni sio Oman ya sasa, yaani UAE yote ilikuwa ndani ya Oman. Hiyo miji ya Abu Dhabi na Dubai ilikuwa haipo kipindi hiko ni vijiji tu vya watu wachovu. Zanzibar ilikuwa mji mkubwa kuliko hivyo vijiji vya Dubai enzi hizo.

Mpaka mwaka 1970 wakati UAE inaundwa Zanzibar ilikuwa Brand kubwa kuliko Dubai. Infact mikoa kama Tabora au Tanga ilikuwa miji mikubwa kuliko Dubai na Abu Dhabi.

Tunapaswa kuchimba Sana history kujua tulikosea wapi.

History yetu inashangaza sana
Kwann hizi story zinakuja kipindi cha uongozi huu wa awamu ya 6

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Mwambie huyo sultan atachezea blowjob akituletea mazoea yake....
 
Tujikite zaidi kufundisha watu namna ya kujiokoa kiuchumi na kielimu.

Masuala ya Wazungu na WAARABU walitutawala vipi mpaka wapi hayasaidii kuleta chakula mezani
 
History ya nchi zetu inashangaza sana.

Cha ajabu Sisi wenyewe hatuchimbi history vizuri.

Around mwaka 1830 wakati Sultan wa Oman anaamua kuwa Zanzibar itakuwa second capital baada ya Muscat. Na akaweka gavana Mombasa na Dar es Salaam.

Huu utawala wa huyu Sultan huku East Africa ulianzia Somalia Hadi Msumbiji. Pwani yote ya hizi nchi za Tanzania, Kenya, Somalia na sehemu ya Msumbiji alitawala yeye.

Na Oman ilikuwa nchi kubwa Sana huko uarabuni sio Oman ya sasa, yaani UAE yote ilikuwa ndani ya Oman. Hiyo miji ya Abu Dhabi na Dubai ilikuwa haipo kipindi hiko ni vijiji tu vya watu wachovu. Zanzibar ilikuwa mji mkubwa kuliko hivyo vijiji vya Dubai enzi hizo.

Mpaka mwaka 1970 wakati UAE inaundwa Zanzibar ilikuwa Brand kubwa kuliko Dubai. Infact mikoa kama Tabora au Tanga ilikuwa miji mikubwa kuliko Dubai na Abu Dhabi.

Tunapaswa kuchimba Sana history kujua tulikosea wapi.

History yetu inashangaza sana
ni maili/kilomita 32 tu kutoka ufukwe wa bahari ya hindi kuanzia lamu mpaka pemba msumbiji. Si nchi yote (Tanganika or east africa germany)
 
Hapo uko karibu mnoooo!!! Sikia sasa East African lift valley yooote kuanzia kule middle East ya leo ni Bustani ya Edeni yoooote ile..ilikuwa ni mali yetu weusi...wa africa Mashariki tangu Mababu.. Tumedhurumiwa sasa tunaitaka kwa damu iwayo yeyote!..lazima irudi....omani ni watoto wa juzijuzi tu....waliomo watajua pa kwenda lkn mziki wetu ndo huo....mjiandae kufa kwa kupigana.....vita ni lazimaili tukomboe east african rift valley.
Ungesema ivo...lkn kutulishsa kokoto za ukoloni hatutaki ....weye umetumwa si bure.
Kawaambie tumekataa huo utoporo...weupe wa oman/middle east...hao!! Kawambie watafute pa kwenda. Twaja sie.......
 
History ya nchi zetu inashangaza sana.

Cha ajabu Sisi wenyewe hatuchimbi history vizuri.

Around mwaka 1830 wakati Sultan wa Oman anaamua kuwa Zanzibar itakuwa second capital baada ya Muscat. Na akaweka gavana Mombasa na Dar es Salaam.

Huu utawala wa huyu Sultan huku East Africa ulianzia Somalia Hadi Msumbiji. Pwani yote ya hizi nchi za Tanzania, Kenya, Somalia na sehemu ya Msumbiji alitawala yeye.

Na Oman ilikuwa nchi kubwa Sana huko uarabuni sio Oman ya sasa, yaani UAE yote ilikuwa ndani ya Oman. Hiyo miji ya Abu Dhabi na Dubai ilikuwa haipo kipindi hiko ni vijiji tu vya watu wachovu. Zanzibar ilikuwa mji mkubwa kuliko hivyo vijiji vya Dubai enzi hizo.

Mpaka mwaka 1970 wakati UAE inaundwa Zanzibar ilikuwa Brand kubwa kuliko Dubai. Infact mikoa kama Tabora au Tanga ilikuwa miji mikubwa kuliko Dubai na Abu Dhabi.

Tunapaswa kuchimba Sana history kujua tulikosea wapi.

History yetu inashangaza sana
Yani hii Tabora sasa! Kila mkutano unasikia ulifanyika Tabora enzi hizo! Sijui kilitokea nini maskini ya Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom