Dudubaya amjibu Mwakyembe, azidi kumshukia Ruge Mutahaba

Dudubaya amjibu Mwakyembe, azidi kumshukia Ruge Mutahaba

Binafsi sijaona sheria yoyote iliyovunjwa kiasi cha Mh. Mwakyembe aamuru Dudubaya akamatwe. Si lazima kila mtu amsifie marehemu. Pamoja na hayo manzuri anayosifiwa Ruge, ni ukweli ulio wazi kuwa alikuwa na mapungufu mengine ambayo yaliwakwaza baadhi ya watu. Si sahihi Mwakyembe kutaka kuuaminisha umma kuwa Ruge alikuwa malaika. Rusisahau kuwa ni Ruge huyuhuyu amefariki akiwa amepiga marufuku nyimbo za wasanii wa Wasafi kupigwa Clouds media kisa tu hawa vijana wamegoma kunyonywa. Ni Ruge huyuhuyu ambae aliendesha kampeni kubwa ya kutaka kumpoteza Diamond kwenye ramani ya muziki. Watu kama kina Lady Jaydee wanayajua vinzuri machungu waliyosababishiwa na Ruge. Tufike mahali tuache kuwa wanafiki eti kisa mtu kafa.
 
Kunadilika unamaanisha nini mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kubadilika ni kuendana na soko la muziki kwa kuzingatia wakati na mazingira. Kubadilika kuanzia mavazi, beat, style ya kuimba, , video style na uandishi. Angalia nyimbo za prof Jay, Dully Sykes, Jmo na Lady Jdee za zamani na za sasa hivi ndiyo utaona utofauti.
Afande Sele, Dudu baya na Juma Nature ni wasanii walioshindwa kubadilika kimavazi, kuimba (anaimba style hiyo hiyo), maudhui ya nyimbo ni yale yale, beat ni zile zile. Unategemea nani atamsikiliza?
 
Dudubaya amezidi kumshukia Ruge mutahaba na kusema kuwa alikuwa akiwanyonya wasanii aliokuwa anasema anawainua
Dudubaya ameendelea kusena kuwa Ruge ndio alisababisha Studio ya Bongo Records kuanguka kutokana na kutaka fedha kutoka kwa producer huyo na wasanii aliokuwa akiwarekodia

Amesema yupo tayari kwenda polisi ambako ameitwa kwenda kesho


Unamkamata Dudu Baya unamuacha Cyprian Musiba...wenye akili lazma wakushangae......
 
tulimtakia kheri osama?
Mtu anapoondoka huwa tunamtakia kheri ktk safari yake ya mwisho haijarishi duniani aliishi vipi eidha kwa kheri au kwa ubaya kwani ni mmoja peekee anayetoa hukumu ya haki, vilevile sisi sote ni wadhambi hakuna aliyekamilika bali ni Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema mwenye
Kurehema, let him Rest In Peace

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pengine huu utaratibu umejaa unafiki. Unakuta mtu anamtakia safari njema mara akigeuka anasema maneno ya kashfa kuliko kashfa yenyewe. Huyo marehemu mimi nilikuwa simjui hivyo nisieleweke kuwa naunga mkono watu wanaomlamu. Ila tu nadhani hata huyu waziri Mwakyembe ni kama amekosa kazi ya kufanya kuingia mambo yasiyomhusu! Kwa nini analazimisha anapofariki mtu fulani basi kila mtu asikitike na hata kama anahisi marehemu hakuwa mtu mzuri awe mnafiki asiseme ukweli wake? Mambo ya kijinga namna hii unakuta yanafanywa na hawa viongozi wa nchi yetu waliofilisikika kichwani na wamebakia kudandia ujinga unaotokea mitaani.
Ni heri huyo mnafki anamtakia mema maiti anamzika baada ya hapo ndio anazungumza aliyotendewa, kwanza hata hao viongozi wenu wa dini hawajawaambia kuhusu kumsengenya maiti? marehemu ni marehemu yake yanakua yameshaisha kwa wakati huo hata wewe umtukane vipi hakuna anachosikia wala hawezi kurudi kukujibu zaidi unaowaumiza ni wapendwa wake, unasupport ujinga wa Dudubaya unasahau kua maneno yake yanaumiza wengine,

Hebu vaa viatu vya wazazi wa Ruge au vya watoto wake, umefiwa na baba yako au mama yako au mke wako halafu kabla hujampumzisha unasikia mtu/watu wanamuongelea kwa mabaya je unafurahi?

Hakuna mtu ameambiwa ahuzunike lakini kama huna huzuni kwanini usikae tu kimya kuliko kuanza kumtusi na kumkejeli marehemu?
wewe katika maisha yako umefanya mazuri tu hakuna baya hata moja? ni nani aliyekamilika chini ya jua?

PS; Mwakyembe hajakurupuka ila watu wamemuomba aingilie kati kumdhibiti huyo Dudubaya japo kwa muda tu ili kumaliza msiba.
 
Rest in peace kivipi.....mangapi kayafanya huyu mhaya yasiyo na chembe ata ya Huruma....alimtapeli mpaka Dada yetu Said a karoli...mm kiukweli naungana na Dudu Baya na na hii kwangu haijaanza leo....huyu MTU unadhani ni wangapi aliwaharibia maisha yako kupitia mziki....Ngwea,Hide,Sugu n.k
Huyo dada yako Saida mwenyewe kwa kinywa chake aliweka wazi kua Ruge sie aliyemuibia bali yule meneja wake wa zamani ndio alikua anachukua hati miliki za nyimbo zake,

Ngwear!? lol, kwa hiyo Ruge ndie alikua anamvutisha madawa au?

Haya wewe ungana na Dudubaya mfe mkazikwe ili muende kumsuta vizuri huyo marehemu, maana kupiga kelele huku ni kazi bure, Hawasikiiii.
 
Hivi ile hadithi ya Vinega.... iliishiaga wapi?
 
Huyo DUDU BAYA hajuwi NGUVU ZA MAREHEMU,,anadhani KUFA NI HIYARI,,,afanye afanyavyo WATAKUTANA TU NA RUGE tena soon huko KUZIMU,,,usimdhihaki MAITI,, hujuwi safari yako LINI,,na huko uendako ni WAPI,,na mwenyeji wako ni NANI , Nina uhakika NDANI YA SIKU 90 atapata MAJIBU.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni heri huyo mnafki anamtakia mema maiti anamzika baada ya hapo ndio anazungumza aliyotendewa, kwanza hata hao viongozi wenu wa dini hawajawaambia kuhusu kumsengenya maiti? marehemu ni marehemu yake yanakua yameshaisha kwa wakati huo hata wewe umtukane vipi hakuna anachosikia wala hawezi kurudi kukujibu zaidi unaowaumiza ni wapendwa wake, unasupport ujinga wa Dudubaya unasahau kua maneno yake yanaumiza wengine,

Hebu vaa viatu vya wazazi wa Ruge au vya watoto wake, umefiwa na baba yako au mama yako au mke wako halafu kabla hujampumzisha unasikia mtu/watu wanamuongelea kwa mabaya je unafurahi?

Hakuna mtu ameambiwa ahuzunike lakini kama huna huzuni kwanini usikae tu kimya kuliko kuanza kumtusi na kumkejeli marehemu?
wewe katika maisha yako umefanya mazuri tu hakuna baya hata moja? ni nani aliyekamilika chini ya jua?

PS; Mwakyembe hajakurupuka ila watu wamemuomba aingilie kati kumdhibiti huyo Dudubaya japo kwa muda tu ili kumaliza msiba.
Sikubaliani na wewe. Haijalishi mtu ni mzima au amefariki. Osama Bin Laden alipouawa kuna watu walisikitika na kuna waliofurahi. Sadam Husein naye hivyo hivyo. Mwalimu Nyerere naye hivyo hivyo. Japokuwa ki-moral siyo vizuri lakini hakuna sheria iliyokataza mtu kutoa maoni yake kuhusu mtu aliyefariki hasa kama alikuwa public figure. Kusema ukweli hata mimi siwezi kukaa na kuanza kufuruhia kifo cha binadam mwenzangu. Lakini hili halininyimi kuzungumza ukweli kwa mtu anayeonewa bila kosa kwa sababu ya kiongozi mkurupukaji kama Mwakyembe. Unajua hawa viongozi wetu hawana kazi za kufanya ndiyo maana unaona wanapishana pishana sehemu zenye mazishi na sherehe kama fisi kwenye mzoga. Dudubaya hakufanya kosa lolote. Yeye ametoa maoni yake juu ya marehemu. Kwani ni lazima asifu? Kama Familia ya marehemu inaona kuwa amekashifiwa basi ndiyo wanatakiwa kuchukuwa hatua na si wanasiasa wadandie mambo yasiyowahusu. Halafu mbaya zaidi Mwakyembe Wizara yake haina uhusiano kabisa na jambo aliloamuru lishughulikiwe! Kama anahusika basi ni ruksa waziri wa Kilimo kuamuru mtu anayemkashifu mkulima yeyote aliyefariki akamatwe!
 
Labda huyo felician ndo THE LATE RUGE 😅😅😅
Kumbe wengi mnalaumu hata bila kuwa na ushahidi na mnachanganya mambo. Ruge alimtapeli wapi Saida wakati aliyemtapeli ni Felician yule wa FM studios aliye msainisha mkataba kuwa nyimbo ni mali yake.
 
Kwakuwa marehemu hawezi tena kumnyonya MTU aliyehai, Huwa MTU akifariki tunaachana na maovu yake tunamsindikiza kwa mema. Hata kama marehemu alikuwa mwizi, kiafrika huwa tunamuazima sifa nzuri na kumsindikiza. Dudu jina lako lisikuathiri sana, samehe, songa mbele pambana

Mkuu hayo maneno umeyatoa wapi eti ufanye maovu duniani halafu tukusindikize kwa mema
Yaan uwe mwizi au uuwe watu halafu ukifa tukufanye uwe mwema hiko kitu hakuna
Mnavyoongea muwe mnafikiria kabla ya kusema
Mshahara wa dhambi ni umauti
 
Back
Top Bottom