Wa kwanza kutoka ndo nini? Anaweza kumeinteini pozisheni? Kiba alichemkia pale alipotoka kuimba na R Kely, angenyoosha. Ukizingatia alikuwa na AIRTEL. Mr Nice hakutoka? LEO YUPO WAPI? Hao Daz dundaz si umeona? wapo wapi? wameweza kumeinteini?? Kuna mwana bongo fleva yeyote aloyewahi kufikia alipo Mondi leo?? Acheni mambo yenu... K ni K tu
Kuimba na R Kelly kisha kupotea isiwe kigezo cha kujiaminisha uongo.
Kwa taarifa yako tuu katika wale wanamuziki walioshiriki ile project hakuna ambaye hakuwa na wazo walau la kufanya wimbo mmoja na R Kelly lakini hakuna aliyefanikiwa kwanza ni ratiba ya mwanamuziki pili na kikubwa ilikuwa pesa..
Hata hivyo hiyo kollabo isingekuwa na nguvu labda ingekuwa kwa 2face na R Kelly kwani alikuwa amefanikiwa kuiteka Afrika hivyo ngoma yake ingemfungulia milango nje ya Afrika lakini mtu kama Ally ndo kwanza alikuwa anahangaika kujihakikishia utawala Afrika Mashariki.
Kusini hawajamwelewa, Magharibi hawamjui , Afrika ya kati hawamtambui...
Kumbuka hapo ' social media' bado hazina nguvu ya kumbeba mwanamuziki.
Wakapanga kufanya muziki baina yao ili kuongeza ushawishi kwenye nchi za wenzao.Ilifanikiwa Fally na Ally japo haikutoka.
2face akawa bussy na matamasha huku na huko, Aman na Redsun wakawa mwendo kinyonga yule Mkameruni na wenzake ndo tukawasahau kabisa kwani njia za kuwafuatilia wanamuziki zilikuwa finyu zaidi ya redio na Tv ambazo bado zilikuwa za kitaifa.
Alikiba akapotea kwa miezi si chini ya 10(si miaka mitatu kama anavyodai) kwani My everthing ilitoka 2013 machi na 2014 july akatoa Mwana.
Huku akiendelea kushirikishwa na wanamuziki wachanga mashabiki wake wakataka aimbe wimbo wake na hatimaye akaiachia rasmi Mwana(kumbuka kimasomaso ni project ya Kusaga kama sijasahau, wanamuziki kuzirudia nyimbo za zamani kisasa wimbo mwingine katika project hiyo ulikuwa Yalaiti ya Mwana Fa na Linah).
Matokeo ya mwana wengi mliyaona na ikaja kuwa njia ya Ally kufika alipo huku nyimbo zake zikiongea zaidi...
Wenzake wa one 8 najua tunajua walipo...
Hivyo tusipotoshane kuhusu sijui one 8 sijui hakuitumia vyema lakini ukweli ni kwamba ameweza kutamba nyakati zote tangu hatuijui Instagram hadi leo tuna snapchart Alikiba ameweza kwenda navyo ingaws kutokana na kuwa wa zama zile amejikuta akishindwa kwenda na kasi juu ya matumizi ya ' socia media'....
Kongole kwa Alikiba , amefanya kilichowashinda wengi wa zama zake.