Dunia hii chagua upande, aidha Urusi au Amerika, kamwe usiwe katikati, utalipa gharama kubwa siku moja !

Dunia hii chagua upande, aidha Urusi au Amerika, kamwe usiwe katikati, utalipa gharama kubwa siku moja !

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Kama Kiongozi kamwe usiwe katikati, chagua upande ambao utaona unakufaa na uende mazima siyo nusu nusu, nusu nusu itakufaa tu kama kila kitu kiko sawa, lkn kikinuka hauna msaada wowote na wanakushukia kama mwewe.

Mfano Erdogan wa Uturuki mwaka 2016 kama asingekuwa rafiki wa kweli wa Putin ilikuwa ntolee tayari, aliponea chupu chupu kupigwa coup d’tat Putin akamtip na kumuokoa, juzi kati pia Kazakhstan kilishanuka lkn kwa kuwa nchi za huko zina ushirikiano na Urusi Putin akazima Mapinduzi, Syria pia bila ya urafiki wa ukweli na wa kuaminiana na Urusi sasa hivi Assad asingekuwepo, hata Irani anakingiwa kifua pia.
Mara nyingi USA au Urusi huwa wanajua kinachotokea Dunia nzima hivyo kama ukiwa rafiki yao wa kweli wanakulinda kama umafia unatokea kwa mmoja wao.

Lakini ukiwa nusu nusu huku unataka kule unatamani pia kama, kikinuka uko peke yako, ndicho kilichomponza Gadafi kwa mtazamo wangu alikuwa huku kwa Amerika, Ufaransa na akina Tony Blair anakula hapo hapo pia alijiweka na Urusi, kilivyonuka Putin alikaa pembeni ingawaje walijua kila kitu lkn alikuwa vugu vugu na mtu vugu vugu haaminiki, hata Sadamu Husein pia alikuwa vugu vugu huku anatumika na Amerika hapo hapo pia anajipendekeza kwa Urusi, Amerika ilivyokinukisha Urusi kakaa pembeni.

Hata sijui…
 
Upande wa USA ni salama zaidi na ndio unaendana na Dunia ya sasa
 
Mimi mwananchi wa kolomije nikiwa upande utanisaidia nini
Mwananchi wa Kolomije haya mambo hayakuhusu, ni makubwa kuliko wewe na mimi. Yanawahusu watawala na familia zao (Wenye nchi) ambao wametingwa kuzunguka duniani kuomba pesa na misaada.

Mkuu Kijakazi nadhani sasa hivi siyo Urusi tena, bali ni Uchina. Nguvu ya Urusi haipo kiuchumi na kisiasa kama zamani, iko kijeshi na kiujasusi, tena kwenye baadhi ya maeneo kama Ulaya na Mashariki ya Kati. Ilhali Uchina ndiyo ana ushawishi mkubwa kisiasa, kijeshi na kifalsafa na yuko dunianiani kote kuanzia Marekani, Asia na Afrika.

Lakini, muhimu ni kufahamu kwamba kipindi ambacho tunakipitia kiko tofauti kidogo kwasababu hakuna kitovu kimoja cha nguvu ya dunia (No Single Centre of Power) kama ilivyokuwa miongo michache iliyopita, ambapo aidha uwe Washington au Moscow. Siku hizi vitovu viko vingi na vina nguvu sana: Mfano Washington, Beijing, Moscow, Brussels na Vatican.

Jambo kubwa ambalo linatokea karne yetu ni kuzaliwa kwa vitovu binafsi vya nguvu (Rise of Independent Power Centers) kama makampuni na mashirika makubwa duniani ambayo yamekuwa na nguvu kubwa kisiasa kutoka na ukwasi ambao yameupata. Haya mashirika makubwa ya kimataifa yameanza kabisa kutunga sera na sheria mbalimbali ambazo zimeanza kuathiri mwelekeo mzima wa siasa za dunia.

Hivyo wahusika wakuu siyo mashirika binafsi kama ilivyokuwa zamani (states are no longer independent actors of international politics). Hii kitaalamu tunaita POWER DEVOLUTION. Hebu fikiria leo hii masuala makubwa ya kibenki yanaratibiwa na Society for Worldwide Interbank Financial Telecommunication (SWIFT) au Masuala makubwa ya kiusuluhishi yanaratibiwa na taasisi kama International Centre for Settlement of Investment Disputes (ICSID). Hizi taasisi kama zenyewe zimetunga sheria ambazo nchi mbalimbali imeziinga na kuzifuata.

Mfano mwingine, The Manhattan Chase Bank, The Goldman Sachs, Oxxon Mobil , American Israel Public Affairs Committee (AIPAC), The National Association of Evangelicals (NAE) na International Freemasonry wameweza kushawishi mwenendo mzima wa siasa za nchi kubwa kama Marekani na dunia yote. Hivyo ni lazima tuwe makini, lakini tunapoangalia upande wa kuchagua, karata zetu inabidi zichangwe vizuri mno.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Upande wa USA ni salama zaidi na ndio unaendana na Dunia ya sasa
Dunia imebadilika sana ndani ya kipindi kifupi na itaendelea kubadilika. Hakuna upande salama, hivyo lazima tuchange karata zetu vizuri. Kuna kitu kinatokea kwenye hii karne ambacho hakikuwahi kutokea uko nyuma: The Rise of the Globalists/Internationalists/Global Citizenry who work viciously hard to undermine national sovereignty in favour of a Singular Global Order.

Yaani haya ya kuchagua upande ni kuchagua kifo tu na yamepitwa na wakati, soma hawa wakubwa wa dunia ndiyo utafahamu uchezaje karata zako.
 
Back
Top Bottom