Dunia imeanza kuelewa ni kwanini CHADEMA wanapigania kufa na kupona Katiba Mpya

Dunia imeanza kuelewa ni kwanini CHADEMA wanapigania kufa na kupona Katiba Mpya

Hivi sasa vyombo mbalimbali vya kimataifa vya habari vya nje kama vile vya CNN, Aljazeera, BBC na vingine vingi, "headlines" ya habari zao ni kukamatwa na Jeshi la Polisi nchini kwa Mbowe na "kubambikiwa" kesi ya ugaidi kwa kosa tu la kupigania Katiba mpya ya nchi hivi sasa.

Vile vile mashirika mbalimbali ya dunia kama vile Amnesty International na mengine mengi tu yanashinikiza pia Mbowe aachiwe huru, kwa kuwa ni dhahiri kuwa amefunguliwa kesi ya ugaidi kisiasa.

Ukiangalia hata zile haki za mtuhumiwa zimekiukwa kwa kiasi kikubwa Sana na Jeshi la Polisi Katika kesi hii ya ugaidi wa Mbowe kama vile kumpeleka kisiri siri mahakamani, Bila hata kuwajulisha mawakili wake, wanaomsimamia kwenye kesi yake

Ni kwanini nasema Chadema Wana kila sababu ya kupigania kufa na kupona mabadiliko ya Katiba mpya sasa na siyo wakati mwingine wowote.

Sababu kubwa ni kuwa hii Katiba ya nchi imepitwa na wakati, na ni ya mfumo wa chama kimoja kwa kuwa imempa madaraka ya ki_mungu mtu, Rais wa nchi, ambaye ni wa CCM, kiasi ambacho hakika, inadhoofisha kwa kiasi kikubwa mno kupanuka kwa demokrasia nchini

Rais wa nchi ndiyo kila kitu hapa nchini, anafanya uteuzi wa watendaji wote kwenye nafasi muhimu kwenye serikali hii.

Kwa mfano tumejionea hivi majuzi, akiwateua makada wa CCM, kutoka UV- CCM, vibinti vidogo kabisa kushika nafasi nyeti za u_DED, ambapo hao ndiyo wanategemewa kuwa "marefa" kwenye uchaguzi wa vyama vingi, kwenye maeneo waliyopangiwa!

Baada ya kelele nyingi Sana, zilizopigwa mwaka Jana na wapinzani, kwenye uchaguzi mkuu uliopita, kuwa CCM ilifanya wizi wa waziwazi kwenye uchaguzi huo, kwa kuwatumia makada hao wa CCM kwa kusaidiwa na Jeshi la Polisi, kufanya wizi huo wa kura, ndiyo kwanza anazidi kukoleza kwa kufanya uteuzi huo wa upendeleo kabisa!

Bado Rais Samia Suluhu Hassan anaendeleza teuzi hizo za "kipuuzi" kwa kuendelea kuwajaza makada wa CCM wasiokuwa na ujuzi wowote kwenye hizo nafasi za utendaji Katika majimbo yao, kwa lengo tu la kwenda kufanya "wizi" wa kura kwenye maeneo waliyopangiwa.

Sababu zinazotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan, kuwa suala hilo la uundwaji wa Katiba mpya siyo kipaumbele chake kwa sasa, kwa kuwa hivi sasa, anaujenga uchumi wa nchi, ulioanguka Sana, hazina mashiko.

Hatujasahau namna Rais aliyemtangulia, Hayati Magufuli, namna alivyokuwa akituaminisha watanzania kuwa tutembee vifua mbele, kwa kuwa nchi yetu ni tajiri Sana, hadi tunaweza kuwa "donor country" wa kuweza kuwakopesha hayo mataifa yanayojiita yameendelea!

Swali ambapo wananchi tunapaswa kumuuliza Rais Samia Suluhu Hassan, hivi uchumi wa nchi yetu umeanguka ghafla, baada ya kifo cha Magufuli?

Swali la pili, haoni kuwa uundwaji wa Katiba mpya ya nchi, unapaswa kufanywa sasa, ili kuepuka hii hali ya kumfanya Rais mungu mtu, ambaye yeye ndiye amepewa mamlaka makubwa mno ya kuteua watendaji mbalimbali wa serikali na haulizwi ni vigezo gani anatumia vya kuwateua hao watendaji wake?

Suala la uundwaji Katiba mpya ni hitaji la sasa la wananchi wa nchi hii na hakuna sababu zozote zenye mashiko, za kuendelea kufanya "delaying tactics"
Hivi hata ukitumia akili ndogo tu, hayo mataifa yawasaidieni ninyi kupata katiba kwa manufaa yenu na raia wa nchi ambazo mmeona hata kupitisha sheria ya mageuzi kuhusu maliasili ilikuwa kama kutenda kosa la jinai?

Unapenda mno kupata madaraka kwa nguvu...Na kusema ukweli muombe Mungu isijetokea mimi nikawa Rais wa nchi hii, nitakuwa zaidi ya Hayati JPM....You arw so obsessed na kutwaa madaraka hata kwa gharama za maisha ya watu...Mungu na awahukumu saqasawa na dhamira zenu....I hate even being in one country na watu wa aina yenu; Wasaliti wakubwa!
 
Mawazo yangu finyu yanaona sababu za bunge kujaa wabunge wa NEC CCM ni hii katiba mbovu tuliyonayo. Ukiwa mpinzani sahau nafasi hata ya kuwa kiongozi wa mtaa. Anaeitetea hii katiba ni mmoja kati ya wale wachache wanaonufaika nayo.
Kumbe mnalilia vyeo?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Duniani kurekebisha na kubadilisha katiba ni kitu cha kawaida. Watu wote wanawashangaa CCM kuwa mbogo wakisikia mabadiliko ya katiba.
Kwa kweli inashangaza mno, namna CCM wanavyoshupalia shingo wanaposikia Chadema, wakipigania kufa na kupona uundwaji wa Katiba mpya.

Wananchi tunajiuliza hivi kuna nini hadi hawa maccm yakatae uundwaji wa Katiba mpya, ambapo ni hitaji kuu la wananchi kwa hivi sasa??
 
Kwa kweli inashangaza mno, namna CCM wanavyoshupalia shingo wanaposikia Chadema, wakipigania kufa na kupona uundwaji wa Katiba mpya.

Wananchi tunajiuliza hivi kuna nini hadi hawa maccm yakatae uundwaji wa Katiba mpya??
Tatizo siyo kupata Katiba lakini noa ya hao wanaopigania katiba....Kwao katiba inahusu kuingia madarakani na wala siyo welfare ya watanzania...Wameshakuwa chama kikuu cha upinzani kwa zaidi ya muongo moja watuonyeshe walichowahi kukifanya chenye tija zaidi ya kupinga tu kila kitu na kugeukageuka kama vinyonga katika hoja zao....CCM ikilegea na kukabidhi nchi kwa watu wa jinsi hii, vizazi vyetu havitawasamehe!
 
Hii serikali ya mama imechafuka mapema mno kimataifa sababu ya kutofuata katiba. Mama amefeli kabisa. Urais ni rahisi kabisa kama rais atazingatia katiba na sheria. Lakini awamu ya 5 na 6 zimetia fora kwa uvunjifu wa katiba na sheria na ndiyo chanzo cha matatizo yote
 
Watu ambao wapo radhi kufanya lolote ilimradi wapate wanacho hitaji...HATARI SANA KWA USALAMA WA TAIFA HILI!
 
Acha kulazimisha si wote bali baadhi. Mfano mimi sioni umuhimu wa katiba mpya
Wewe bado unaishi kwa shemeji yako mme wa dadako unashinda sebureni ukiangalia tamthilia na usiku unalala sebureni huku ukisikiliza dadako anavyomkatikia mme wenu chumbani huwezi kujua chochote kuhusu maisha.
 
Tatizo siyo kupata Katiba lakini noa ya hao wanaopigania katiba....Kwao katiba inahusu kuingia madarakani na wala siyo welfare ya watanzania...Wameshakuwa chama kikuu cha upinzani kwa zaidi ya muongo moja watuonyeshe walichowahi kukifanya chenye tija zaidi ya kupinga tu kila kitu na kugeukageuka kama vinyonga katika hoja zao....CCM ikilegea na kukabidhi nchi kwa watu wa jinsi hii, vizazi vyetu havitawasamehe!
Una uhakika gani na una hiki sema? Kama kwa miaka 60 chama tawala kimeshindwa kuisimamia serikali ili hata kupata maji kila kijiji na nyumba bora kwa raia tutegemee ni nini zaidi?
 
Una uhakika gani na una hiki sema? Kama kwa miaka 60 chama tawala kimeshindwa kuisimamia serikali ili hata kupata maji kila kijiji na nyumba bora kwa raia tutegemee ni nini zaidi?
Nina uhakika na zaidi kwakua I was once with these people!
Nilijitolea kwa jasho na damu kukijenga kwa fikra na mawazo kisha sikutaka hata kuwa na nafasi hata moja yakujifaidisha, lakini hata yale mapendekezo ya maana hawakuyataka wala kuyatilia maanani, zaidi ya kugawana vyeo na mapato wasiyoyatolea jasho maarufu kama ruzuku to suit their personal needs!
 
Chama hiki na watu wake wanatumia weakness za raia kupenyeza agenda zake mfu zisizoitakia mema nchi yetu...Vijana amkeni, jiungeni na chama chenye institution iliyojijenga vizuri na chenye misingi imara ya taifa hili ili kuwaondoa wale wachacje wanaotaka kukitumia kwa faida binafsi. Hapo mtakuwa mnaitendea haki nchi hii...Huko mliko mnatumia tu na ole wenu mkishiriki hii dhambi ya kuiuza nchi yetu kwa wageni!
 
Una uhakika gani na una hiki sema? Kama kwa miaka 60 chama tawala kimeshindwa kuisimamia serikali ili hata kupata maji kila kijiji na nyumba bora kwa raia tutegemee ni nini zaidi?
Dawa ni kuingia kwa wingi kukiboresha chama hicho kilichopo ambacho atleast kimeonyesha kubadilika kila awamu...Hii ni our own style of democracy...CCM haijawahi kuwa ile ile unaona trend...Which means ndani ya CCM kuna democracy illa nje ya CCM hakuna chama kinachoweza kuizidi CCM kwa strategies na processes, CCM ni institution imara kabisa naweza kusema imara kuliko hata serikali yenyewe....CCM ilichokosa ni vijana ambao walidanganywa na vyama vilivyoundwa kwa malengo ya kutugawanya na kutu distract kwenye maendeleo hivyo kubakiza wengi ambao ni ma opportunists na wenye kuwa na God fathers...Hata hivyo trend ilibadilika alipoingia hayati JPM na kwa sasa CCM ina vijana wazuri lakini bahati mbaya fulani hivi bado wengi hawajapata strategic positions.
 
Mawazo yangu finyu yanaona sababu za bunge kujaa wabunge wa NEC CCM ni hii katiba mbovu tuliyonayo. Ukiwa mpinzani sahau nafasi hata ya kuwa kiongozi wa mtaa. Anaeitetea hii katiba ni mmoja kati ya wale wachache wanaonufaika nayo.
Very true
 
Back
Top Bottom