Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Endelea kutuelimisha mkuu, tunakushukuru kwa elimu hii njema,

nina mchango kidogo kuhusu viongozi wa dini,
Hawa watu ni watu wenye influence kubwa sana katika jamii yetu na basically ni watu ambao walitakiwa kuwa kama dira na viongozi wa haki kwenye jamii, tatizo lao kubwa wengi wao ni viongozi wa dini ambao wapo kimaslahi zaidi badala ya malengo halisi ya utumishi wao, hawa ukipenyeza rupia kidogo tu umeshawayumbisha na kuvuruga umoja wao, na hapa CCM wanajua kucheza nao vizuri sana.

Mfano dhahiri utaona mathalani makanisa kwa umoja wao walitoa tamko kuupinga uharamia wa katiba na ubabe wa mwenye kiti na walikua na standing zao toka mwanzo, kwa akili ya kawaida nilitegemea huo ndio msimamo wa viongozi wote wa dini hiyo, loooh, lahaula, wakajitokeza wengine tena wapo bungeni kushabikia ule upuuzi kinyume cha viongozi wao walio nje kuupinga, na nikashangaa wengine eti wakienda kusalisha siku ya makabishiano pale Dodoma, nikabaki kujiuliza umoja wao uko wapi, kumbe hawa sio wamoja maslahi yanaweza kuwagawanya kirahisi na kuchanganya waumini wao.

Lakini bado nawapa credit viongozi kadhaa wa kadha wa dini wana msimamo mwanzo mwisho, hawakubaliani na kila upuuzi unaopndekezwa na watawala, wakati wote hukosoa na kuonya pale wanapoona mapungufu, mentioning few ni Shura ya Maimam, Ask. kakobe, Padr. Mapunda,Ask. Ngalalekumtwa na wengineo, hawa japo hawajawa na misimamo ya 100% lakini anagalau wameonyesha guts za kuikosoa serikali kwenye huu mchakato wa bora katiba iliyoandaliwa na ccm na washirika wake.

Ninaamini viongozi wa dini wana impact kubwa sana na watatumika sana kujaribu kuhalalisha haramu hii ya bora katiba ya CCM na washirika wake, na kwa nchi yetu ambapo uelewa wa wa wanchi wake wengi upo chini, udanganyifu mkubwa sana utafanywa na hawa watu, ambao bila aibu watashabikia hii katiba ambayo mwenyekiti wake Sitta aliwatukana viongozi wao na kuwadharau

King Suleiman Mbona umeshasema nilitotaka kueleza? Lazima utakuwa mtabiri wewe ha ha ha! Ahsante sana.

Nitakachofanya ni kuongezea kidogo tu, mengine umeshasema yote.
 
KUNDI LA VIONGOZI WA DINI
Sehemu ya I
Hapo bandiko 21 tueongelea makundi 3 yatakayopewa kazi yapromotion ya rasimu ya CCM.
Waandishi wa habari, kutisha viongozi na viongoziwa dini.


King Suleiman kaeleza vizuri sana. Uwepo wa viongozi wa diniulikuwa na sababu kuu zifuatazo; (1)Kuhakikisha kuwa wao kama sehemu ya taasisina jamii yenye wafuasi wengine inashiriki katika mchakato
(2)Kuhakikisha masilahi ya waumini katika yanalindwa ili katibaisiingilie au kuacha wazi uhuru wa kuabudu
(3) Kuwa wapatinishi kati yawabunge wenyewe au bunge na wananchi

(4) Kuwasikio la wananchi katika kuona haki inatendeka kwa dhamana ya kiroho waliyonayo


Viongozi wa dini wamekuwa wahanga wa wanasiasa. Kilawanapomaliza kutumika, wanasiasa huwasimanga hata kuwatia matatani. Juzi turais alisikika akikemea kuchanganya siasa na dini na dini na siasa.

Huwezi kutenganisha siasa na dini. Chimbuko la siasa niuwepo wa dini na maadili ya kiroho hayatengi jambo la siasa au nje ya siasa.

Hivyo kuwaambia wasichanganye dini na siasa kuna maana pale tu siasaitakapoachwa kuchanganywa na dini.


Inashangaza Rais aliyesema wasichanganye dini na siasa,hakukemea viongozi wa siasa kama waziri wake Lukuvi aliyepeleka siasa ya katibakanisani.

Kwa maneno mengine Rais anaruhusu siasa kuchanganywa na dini na sikinyume chake.

Inashangaza wakati wa maadhimisho ya kidini, viongozi wa kisiasa tunawaona wakihudhuria, iwe Krismas au baraza la Idd. Wakitoka hapo wanakemea kuchanganya dini na siasa.

Yanapotokea matatizo yaliyosababishwa na wanasiasa,utawasikia viongozi wa siasa wakiwaomba viongozi wa dini waombee taifa.

Inakuwaje wanasiasa wanaruhusiwa kushiriki shughuli za dini wakiwa na majoho yao ya kisiasa lakini ni marufuku viongozi wa dini kushiriki siasa?


Viongozi wa dini nao wanasehemu yao ya kulaumiwa. Hivi wanasiasa wanaingiaje katika shughuli za maadhinmisho yanayohusu Imani. Kwanini wanawakaribisha.

Hata wziri Lukuvi naye alikaribishwa kuongea kanisani.
Kwaniniviongozi wa dini wasialike viongozi wenzao kama wanataka mbadala katikashughuli zao?


Kwanini, kwa mfano tu, mwadhama Pengo asimwalike kadinalimwingine kutoka nje katika sherehe za Wakristo?
Kwanini shehe mkuu asimwalike mufti wa taifa jingine katika shughuli za waislam?

Maana hao wageni wana lakusema kuhusu Imani, ukimwalika Sitta atakwambia namna wananvyojipanga kwa kura za facebook, Tango na Whatsup na ataomba umuombee mipango yake inyoke.

Kiongozi wa dini utakataa vipi ili hali umwemwalika katika nyumba yako na unajua hajui wala hana mamlaka ya kiroho (moral authority) kuzinyoosha roho zawaumini akiwayeye I muovu namba moja?

Unamkaribisha tumbili shambani utegemee nini kama si kuvuna mabua?
Hebu turudi katika mchakato tuone ushiriki wao
Inaendelea….
 
Tofauti na Maelezo ya jaji warioba na tume ya katiba, juzi Katika hotuba yake baada ya kukabidhiwa katiba iliyopendekezwa, hatukumsikia rais wa JMT Wala kiongozi yoyote akifafanua maslahi ya Washirika wa pande zote Mbili za muungano - hasa kiuchumi na kimamlaka. Badala yake, tulichosikia kwa lugha nyepesi Kabisa ilikuwa ni maslahi ya upande mmoja tu wa muungano - Zanzibar, huku maslahi kwa upande wa Tanganyika yakipuuzwa Kama vile Tanganyika haipo, lakini muhimu zaidi, Kama vile Tanganyika haitapata athari Zozote chini ya Mfumo ndani ya katiba inayopendekezwa.

Kwa mfano, Zanzibar wameahidiwa mikopo ya nje, uhusiano wa kimataifa, kuendesha rasilimali zao za Mafuta na gesi, na muhimu, tofauti na Huko nyuma, Zanzibar sasa itavuna viongozi watano wenye hadhi ya urais huku Tanganyika ikivuna viongozi wawili tu wenye hadhi ya urais (Tena hadhi ya kinadharia tu), huku kivitendo, Zanzibar wakiwa Ndio walioshika mpini. Tutajadili masuala haya yote - moja baada ya jingine, lakini Katika Bandiko hili, ningependa kujadili suala la madaraka ya urais chini ya katiba inayopendekezwa na jinsi gani mapendekezo husika yatachochea kuvunjika kwa muungano:

Tukumbuke Kwamba hoja za kina Nape Nnauye, MwanaDiwani, chama, Kobello, Gamba la Nyoka, Mtanganyika, ZeMarcopolo, na makada Mbali mbali CCM dhidi ya serikali Tatu ilikuwa ni pamoja na Kwamba serikali Tatu zitaongeza utitiri wa viongozi, hivyo kuongezea mzigo walipa kodi. Makada hawa walikebehi sana hoja zetu juu ya uwepo wa rasimu ya CCM ya mafichoni lakini Ukweli sasa upo wazi - rasimu iliyopotishwa Ina content ambayo ilishafanyiwa kazi na kina Chenge, migiro, Wassira, lukuvi, etc Kabla hata mjadala kamili bungeni haujaanza. Tulisema miezi Sita iliyopita (April 2014), na sasa Ukweli huo umesimama.

Twende moja kwa moja kwenye hoja.

Tume ya warioba ilipendekeza rais mmoja wa muungano na viongozi Wengine wawili wa kuongoza pande Mbili za muungano bila ya kujalisha Viongozi hawa watapewa majina gani ya kiutawala. Pahala ambapo palitarajiwa kuwa suala la title za viongozi wa nchi washirika lingejadiliwa lakini bila ya kuathiri Roho ya rasimu ya wananchi (serikali Tatu) ilikuuwa ni ndani ya bunge maalum la katiba. Lakini tofauti na tume ya warioba, na katiba inayopendekezwa sasa imebariki gharama kubwa zaidi kwa wananchi, hasa watanganyika. Tofauti na rasimu ya tume ya jaji warioba, rasimu ya mafichoni ya CCM Sasa imeweka wazi Kwamba Jamhuri ya muungano wa Tanzania itakuwa na viongozi SABA wenye hadhi ya URAIS. Tukianza na Upande wa Zanzibar, wao watakuwa na viongozi WATANO wenye hadhi ya urais, Kama ifuatavyo:

1. Rais wa Zanzibar (anayepigiwa kura na wazanzibari tu lakini Ana Nguvu hadi kwa wananchi ambao Hawakushirikishwa kumchagua - watanganyika).
2. Makamu wa kwanza wa rais Zanzibar ambae ni msaidizi wa rais wa Zanzibar, hivyo kuwa na mamlaka ya kukaimu mamlaka juu ya watanganyika.
3. Makamu wa pili wa rais Zanzibar (mamlaka sawa na makamu wa kwanza wa rais Zanzibar).
4. Makamu wa kwanza wa rais wa JMT (mgombea mwenza kutoka Zanzibar (Huyu yupo kuwakilisha maslahi ya wazanzibari, sio watanganyika).
5. Makamu wa pili wa rais wa JMT (ambae pia Ana kofia nyingine ya urais wa Zanzibar).

Hapa tusisahau Kwamba katiba ya Zanzibar (2010) imepora mamlaka ya katiba ya JMT.

Kwa Upande wa Tanganyika, wao watakuwa na viongozi WAWILi tu kati ya marais Saba wanaoridhiwa na katiba inayopendekezwa:

1. Rais wa JMT - Huyu tumeshaona jinsi gani katiba ya Zanzibar (2010) ilivyompora mamlaka. Kwa maana nyingine, rais wa JMT chini ya katiba inayopendekezwa atakuwa ni rais wa Muungano kinadharia tu, huku akiwa sio lolote kivitendo. Kwa maana nyngine Rahisi, rais wa muungano will become "a toothless dog" Katika uongozi wake wa jamhuri ya "muungano". Ukweli huu utazidi kujitokeza siku sio nyingi kwani Kama alivyojadili Nguruvi3 Hapa au kwingineko, Zanzibar hawawezi kurudi nyuma na kubadili katiba Yao kwa manufaa ya Tanganyika iliyovaa koti la muungano.

2. Rais wa pili kutoka wa Tanganyika atakuwa ni waziri mkuu wa JMT ambae vituko vya katiba inayopendekezwa vimempa wadhifa wa "makamu wa TATU" wa rais!

Hii inafanya uwepo wa marais SABA Katika mazingira ya katiba inayopendekezwa - Zanzibar ikitoa watano, Tanganyika ikitoa wawili, huku marais wa upande wa Zanzibar wakiwa Ndio wenye mamlaka makubwa zaidi kiutawala (rejea mgongano wa kikatiba) lakini pia kirasilimali (kwani chochote cha Tanganyika ni cha muungano kwa vile haina serikali yake). Hali hii inafanya cha Zanzibar Kiwe cha Kwao, na cha Tanganyika Kiwe cha wote - watanzania. Licha ya soko moto kote hili, bado Gharama zote za kuhudumia marais hawa Saba wakiwa madarakani na wakienda kustaafu zitakuwa ni za mtanganyika. Mwezi Aprili mwaka huu, Hamad rashid alipinga sana rasimu ya tume Kwamba itapelekea uwepo wa marais watatu ambao watakuwa ni mzigo kwa walipa kodi. Katika Hili la marais Saba sijui atakuwa na mtazamo gani. Tatizo letu ni Kwamba hatuna waandishi wa habari Mahiri kufuatilia mambo Kama haya.

Kama alivyojadili Nguruvi3, muungano umefikia Katika hatua ya hatari kuliko kipindi chochote Kile. Kwa mfano Katika suala jamhuri ya muungano, miaka 50 baadae, JMT imekuwa ni nchi Mbili Zenye serikali Mbili, na marais Saba,lakini Watu bado Hawaoni Kwamba hili ni bomu la mtego (timing bomb).

Chini ya Katiba inayopendekezwa, CCM inapendekeza kwamba – Rais wa Zanzibar afanywe kuwa Makamu wa Rais wa Muungano bila ya kujalisha Rais wa Muungano anatokea upande upi wa Muungano. Kwa kufanya hivyo, CCM inadai kwamba – hali hii itamwongezea Rais wa Zanzibar - “madaraka na hadhi” ndani ya serikali ya Muungano na pia nje ya nchi. Huku ni kupandikiza mbegu ya machafuko na hatimaye kuvunjika kwa muungano kwa sababu:

Mkataba wa Muungano (1964) uliweka utaratibu ambao – Rais wa Muungano wa NCHI Moja, alikuwa na wasaidi wake wakuu wawili – Makamu wa Kwanza wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Zanzibar (Marehemu Karume), na Makamu wa Pili wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika (Marehemu Kawawa).

LAKINI chini ya katiba inayopendekezwa, CCM haisemi iwapo Rais ni MMOJA wa nchi MOJA, badala yake Inasema tu kutakuwa na rais wa JMT, na hao Wengine Sita.

Katiba inayopendekezwa haisemi ni kiongozi gani ndiye atakayesimamia Mawaziri watakaokuwa wanasimamia mambo ya Tanzania Bara katika mfumo huu wa serikali mbili “ulioboreshwa”. Katika mikakati yake ya kuuza kwa umma katiba inayopendekezwa, CCM haina Maelezo juu ya ufafanuzi wa masuala muhimu (kiutekelezaji), kwa mfano, - katika mazingira ya Zanzibar kuwa ni “nchi” kamili, yenye “mamlaka” kamili, katiba, amiri jeshi mkuu, Wimbo wa taifa, ikitokea kwamba Rais wa Muungano anatokea upande wa pili wa muungano (Zanzibar), JE:

· Rais huyu kutoka nchi jirani ya “Zanzibar” atasimamia masuala yasiyo ya muungano - ya upande unaoitwa “Tanzania Bara”, ndani ya Jamhuri ya Muungano, kwa mamlaka yepi?

· Iwapo Rais wa Muungano atatokea panapoitwa “Tanzania Bara”, Rais huyu wa Muungano atakuwa na mamlaka yepi ya kusimamia mambo ya “Tanzania Bara” wakati yeye atakuwa amechaguliwa na wananchi wa pande zote mbili za muungano - Tanganyika na Zanzibar?

· Zipo wapi ‘pande mbili’ za muungano bila ya kuwepo kwa Serikali ya Tanganyika?

Katika haya, CCM haina uwezo wa kufafanua Hali ambayo itazidi kuudhoofisha muungano. Kwa vyovyote vile, Katiba inayopendekezwa haitaboresha muungano bali itajenga mazingira ya kuvunja muungano. Tuendelee kufafanua hili:

Kwa mfano, iwapo Rais wa Muungano atatokea upande wa nchi jirani ya “Zanzibar”, ambaye kwa Mujibu wa katiba inayopendekezwa, Rais wa Zanzibar pia atakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano. CCM inapendekeza kuwa rais wa nchi Jirani ya Zanzibar moja kwa moja awe ni makamu wa rais wa muungano (Tanganyika) hata Kama hakuna mtanganyika hata mmoja aliyempigia kura. Kwa maana nyingine, rais wa Zanzibar pia atakuwa ni rais wa watanganyika kwa njia ya uteuzi. Hiki ni kituko cha mwaka - watanganyika kuwa na marais wawili, mmoja waliyempigia kura, mwingine aliyepigiwa kura nchi Jirani (Zanzibar) kisha kuteuliwa kuwa rais wao watanganyika, Tena akiwa na katiba (ya Zanzibar)ambayo Ipo juu kimamlaka kuliko Ile ya watanganyika/muungano.

Mbali ya athari hizi, Ipo nyingine kubwa. kwa mfano, Kitendo cha rais wa Zanzibar kuwa makamu wa rais wa muungano bila kujalisha Rais wa Muungano atatokea upande upi wa Muungano kitatupeleka Katika Hali ifuatayo:

• Siku moja, Rais wa Muungano na Makamu Wa Rais Wa Muungano, wote watakuwa wametokea nchi jirani ya “Zanzibar”. Kwa maana hii, aidha kwa makusudi au bahati mbaya, CCM inajenga mazingira ambayo Zanzibar hawataweza tena kutoa Rais wa Muungano. Hii ni kwa sababu:

Hali hii itaamsha watanganyika kwani kwa maana ya Kwamba - Kama tulivyoona, chini ya rasimu inayopendekezwa na CCM, Rais wa Zanzibar “automatically”, atakuwa pia ni Makamu wa Rais wa Muungano. Sasa ikitokea Siku CCM ikasimamisha mgombea Urais wa Muungano kutokea nchi jirani ya “Zanzibar”, nchi ambayo pia automatically itatoa makamu wa Rais wa Muungano, chini ya mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, wapiga kura kutoka upande wa inayoitwa “Tanzania Bara”, upande ambao una wapiga kura zaidi ya 90% ya wapiga kura wote wa Jamhuri ya Muungano, HAKIKA, wengi ya wapiga kura hawa kutoka “Tanzania Bara”, hawatakubali kumchagua mgombea wa urais (CCM) kutokea nchi ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake pia anatokea huko huko “nchini” Zanzibar. Kwa maana nyingine, wananchi wa tangangika siku moja watakataa mgombea wa aina hii atakayependekezwa na CCM.

Je athari yake ni nini?

Ni kwamba – chini ya katiba inayopendekezwa na CCM, ni muhimu sasa waZanzibari waanze kujiandaa kisaokolojia Kwamba watanganyika Kamwe hawatomchagua kwenye Sanduku la kura mgombea urais mzanzibari kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Watanganyika watakuwa wamefanya uamuzi sahihi lakini Kitachofuatia kwa upande wa Zanzibar ni Kwamba wazanzibari wataanza kulalamika kwamba wanabaguliwa, wanaonewa, wananyimwa haki ndani ya Jamhuri ya muungano, kwahiyo waachwe “Wapumue”. And interestingly enough, watakaongoza katika kutoa hoja hizi ni wale wale wazanzibari ambao Islaml Jusa alisema kwamba walipofika Dodoma “Waliufyata”. Ni wale wale ambao leo wanapinga kwamba wao sio “wasaka tonge”. Katika kundi hili, hatutashangaa kuja kuona viongozi kama Balozi Seif Iddi, Mohamed Seif Khatib, nahodha, kificho,Hamad Rashid Mohamed, na wengine wakija kugeuka na kusema Kwamba Tanganyika inafanya Zanzibar kuwa koloni. Baadae tutaona jinsi gani ruksa kwa Zanzibar kukopa, kuwa na uhusiano wa kimataifa n.k bado hayatamaliza Dhana ya ukoloni.Hakuna mamlaka kamili kwa Zanzibar kwa Jambo lolote bila ya uwepo wa Tanganyika.

• Je kwa upande wa viongozi wa CCM bara, watakuja Lamba matapishi yao?

Kwa upande wa inayoitwa “Tanzania Bara”, iwapo Mgombea Urais wa Muungano atatokea nchi jirani ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake “automatically” pia atatokea Zanzibar, watakaoongoza katika kupinga hali hii haitakuwa watu wengine bali wale wale makada wa CCM ambao ndani ya bunge la katiba walijiita kwa majigambo Kwamba wao Ndio wenye “Maoni ya Walio Wengi”, ambao wamepitisha katiba inayopendekezwa kwa vigele gele na
Vifijo. Fitina zilizomkumba Dr. Salim Ahmed Salim alipokuwa anawania urais hazitafua dafu kwa fitina zitakazojitokeza katika mazingira tunayojadili hapa. Wana CCM ambao watakuwa katika makundi ya kutafuta Rais wa Muungano wataendesha kampeni kubwa kupinga uongozi wa Muungano kwenda kwa “nchi jirani katika kofia zote mbili za juu – Rais wa Muungano na Makamu wa Rais wa Muungano.

Kuna haja ya wazanzibari na watanganyika kuungana kuzuia hatari iliyopo Mbeleni. Ujumbe muhimu kwa wazanzibari ni Kwamba wanachoambiwa na CCM ndani ya rasimu inayopendekezwa ni kwamba:

• "Kuanzia sasa, wazanzibari wajiandae tu kisaikolojia kuwa ni “wasindikizaji” tu wa Uongozi" katika Jamhuri ya Muungano."

Pia CCM nayo ijiandae kutupiwa lawama na malalamiko mapya juu ya Ukoloni wa Tanganyika kwa Zanzibar. Mbegu ya kuvunjika kwa muungano sio tu imeshapandwa, Bali pia imeanza kuchepuka.

Itaendelea ambapo tutajadili athari za katiba inayopendekezwa - athari Katika maeneo mengine ya uchumi, rasilimali, bunge, Mahakama, mikopo, uhusiano wa kimataifa n.k, hoja ikiwa ni jinsi gani maeneo haya yataathirika chini ya katiba inayopendekezwa, na jinsi gani yatazidi kuudhoofisha muungano wa serikali Mbili na hatimaye muungano huo kuvunjika.

Cc Dingswayo, Mag3, EMT, Mkandara, Barubaru, Bongolander, ukwelikitugani, happyfeet, Pasco, Jasusi, JokaKuu, MTAZAMO, Mwigulu Nchemba, Ezekiel Maige, MJINI CHAI, gfsonwin Mimibaba Zakumi

















Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Katiba imeshapitishwa na Bunge. Kilichobaki ni maamuzi ya wananchi. Kila mwananchi ana kura moja. Jumla ya kura zote ndio itaamua hatima ya katiba.

Cha muhimu nikufanya mchakato kwa amani, hakuna sababu ya kutumia nguvu...
 
Huu ni Muungano Wa CCM bara na CCM Zanzibar. Lakini kama utapigiwa kura, nadhani sio Watanganyika wala Wanzinzibar Wanao taka Muungano.

Muungano ni wa watanganyika na wazanzibari; ni mmoja tu kati yao akikataa muungano umekufa, na kama wote wawili wakiukataa ndio unazikwa kabisaaaaaa!!
 
Katiba imeshapitishwa na Bunge. Kilichobaki ni maamuzi ya wananchi.
Kila mwananchi ana kura moja. Jumla ya kura zote ndio itaamua hatima ya katiba.
Cha muhimu nikufanya mchakato kwa amani, hakuna sababu ya kutumia nguvu...

Mkuu Zemarcopolo, unaweza kutusaidia kujibu hoja za mchambuzi angalau kwa ufupi tu na kuanisha kwa hoja ubora wa katiba hii pendekezwa ya CCM na ile ya tume ya warioba, tutajie strenght za hii ya akina Sitta na weakness za rasimu ya akina warioba, japo kwa hoja chache.

Maana ninachokiona unakimbia mjadala kwa majibu mepesi kwamba tusubiri wapiga kura whl hao wapigakura wanatakiwa kupata elimu hii na kuelewa impact ya uchaguzi wao, ni hayo tu
 
Katiba imeshapitishwa na Bunge. Kilichobaki ni maamuzi ya wananchi.
Kila mwananchi ana kura moja. Jumla ya kura zote ndio itaamua hatima ya katiba.
Cha muhimu nikufanya mchakato kwa amani, hakuna sababu ya kutumia nguvu...

Anayeamua matokeo ya kupiga kura sio wale wanaopiga kura bali wale wanaohesabu kura; ndio maana hata kwenye kuhesabu akidi Sitta na genge lake hawakuruhusu wasimamizi wa kuhesabu zile kura na hapo wakapata nafasi ya kuchakachua!!

Nguvu ni lazima itumike kuhakikisha kuwa ccm hawataiba kura wakati wa kuhesabu kura za maoni; ccm na serikali yake ni wapenda kutumia vitisho vya vyombo vya dola kufanikisha uharamia wao!! Wananchi ni lazima wawe vigilant kulinda kura zao ama sivyo haki yao itapokwa na hawa magamba!! This country has that experience of vote rigging!!
 
Wakuu naomba mnisaidie maana nimechanganya kidogo, hivi kwa wananchi ili katiba ipite inahitaji 50% + au ni 2/3 (75%) kama ilivyokua bungeni?


Maana hata kama wananchi wengi hawana uelewa wa kutosha, kwa mchakato ulivyokwenda naona ugumu sana kupitishwa kwa katiba hii kihalali bila hila zozote
 
Katiba imeshapitishwa na Bunge. Kilichobaki ni maamuzi ya wananchi.
Kila mwananchi ana kura moja. Jumla ya kura zote ndio itaamua hatima ya katiba.
Cha muhimu nikufanya mchakato kwa amani, hakuna sababu ya kutumia nguvu...

Niulize tu kama kilichobaki ni maamuzi ya wananchi una maana kuwa katiba inayopendekezwa siyo ya wananchi mpaka pale wananchi watakapoipitisha?

Maana akipokea katiba, Rais alisema kuwa ni katiba ya wananchi kwa ajili ya wananchi.

Kama ni katiba ya wananchi kuna maana gani tena ya wananchi kuipigia kura?
 
Mkuu Mchambuzi nadhani kwanza umekosea sana kuniweka mimi kwenye kundi la ukada wa CCM, wewe unafahamu fika ya kwamba mimi sipo kwenye huo upande. Mimi nazungumzia upande unaitwa hali halisi (reality), naangalia nyakati na kutanabaisha kutokana na nyakati. Nilikataa serikali tatu na nilikataa mbili nikasema ama tuwe na muungano wa serikali moja au kama haiwezekani basi tugawe mbao au tubaki na jini tunalolijua.

Nadhani ukiangalia mdahalo wangu mwingi nilikuwa nasema kwanza Mzee wetu Warioba yeye ndio alianza kutupoteza na kuja na swala lao la serikali tatu, sababu hakusoma nyakati. Mbili, CCM wao wana mtaji wa kisiasa na niliwaambieni hapa kwamba muda ndio adui namba moja wetu, CCM watapitisha katiba ya kukilinda chama chao na mfumo wao. Kama unakumbuka andiko la Kitila Mkumbo kwamba CCM wanayo majority Vote hata UKAWA wakikimbia, na hilo lilikuwa wazi.

Sasa jambo la muhimu ni moja tuu, Jee watanzania wataikataa katiba mpya? Kutokana ninavyoona mfumo wa siasa ya Tanzania Bara, I don't see katiba hii kukataliwa. Naona kwamba hili ndio limekula kwetu, kama kweli tunataka Katiba tukaze mguu upinzani washinde Majority ya bunge by 2025 then tuongeelee katiba mpya. Haya mengine yote mnayongea ni assumption na majority of Tanzanian hawana hata pesa ya kula lunch.
 
Mkuu Mchambuzi nadhani kwanza umekosea sana kuniweka mimi kwenye kundi la ukada wa CCM, wewe unafahamu fika ya kwamba mimi sipo kwenye huo upande. Mimi nazungumzia upande unaitwa hali halisi (reality), naangalia nyakati na kutanabaisha kutokana na nyakati. Nilikataa serikali tatu na nilikataa mbili nikasema ama tuwe na muungano wa serikali moja au kama haiwezekani basi tugawe mbao au tubaki na jini tunalolijua.

Nadhani ukiangalia mdahalo wangu mwingi nilikuwa nasema kwanza Mzee wetu Warioba yeye ndio alianza kutupoteza na kuja na swala lao la serikali tatu, sababu hakusoma nyakati.

Mbili, CCM wao wana mtaji wa kisiasa na niliwaambieni hapa kwamba muda ndio adui namba moja wetu, CCM watapitisha katiba ya kukilinda chama chao na mfumo wao. Kama unakumbuka andiko la Kitila Mkumbo kwamba CCM wanayo majority Vote hata UKAWA wakikimbia, na hilo lilikuwa wazi.

Sasa jambo la muhimu ni moja tuu, Jee watanzania wataikataa katiba mpya? Kutokana ninavyoona mfumo wa siasa ya Tanzania Bara, I don't see katiba hii kukataliwa.

Naona kwamba hili ndio limekula kwetu, kama kweli tunataka Katiba tukaze mguu upinzani washinde Majority ya bunge by 2025 then tuongeelee katiba mpya. Haya mengine yote mnayongea ni assumption na majority of Tanzanian hawana hata pesa ya kula lunch.
Kwanza, nikuambie kuwa tuhuma dhidi ya Warioba ni kumchafua tu ambako CCM wamekuwa anafanya kila uchao na hapa unatekeleza wanachokifanya.
Hivyo sidhani kama Mchambuzi atakuwa amekuonea hata kidogo.

1. Warioba hakupaswa kusoma nyakati, yeye aliongozwa na hadidu rejea alizotoa Rais na ambazo Rais alizikana na juzi amezikubali. Ukiangalia kwa jicho pevu, mchakato ulikwenda vema kwa mujibu wa Warioba hata hivyo, Rais aliamua kuuvuruga baada ya kutishwa na wahafidhina ndani ya CCM.

Mzee Warioba hana tatizo, yeye ni tarishi, unless utueleze kama naye alipaswa kutenda ya yahoo, wahtsup na face book.

2.Kuna ushahidi usio na shaka kuwa hata mtaji wa CCM haukuwa na maana.
Huko Makkha mahujaji hawakupiga kura, wale UKAWA 2 ni maruhani anawajua Sitta peke yake.
Ndani ya chumba cha kuhesabu kura za CCM hakukuwa na uhakiki, kura za Tango, whatsup na facebook hazijulikani zilisimamiwa na nani na kwa utaratibu gani.

Afisa ubalozi Saudia kapoteza kazi kwa kusema ukweli, mwanasheria mkuu wa SMZ kapoteza kazi kwa kueleza ukweli.
Huo ndio mtaji unaotaka watu waelewe kuwa CCM ilikuwa nao? Hukuona mazingaombwe hata kidogo yaliyofanyika.
Udanganyifu wa highschool wa Smawel John Sitta unauita mtaji wa kisiasa! ebo!

Tatu, jambo la muhimu si kurasimisha rasimu haramu. Jambo la muhimu ni Watanzania kujadili uharamu, uharamia na madhara yanayolikabili taifa siku zijazo. Hilo ndilo muhimu hata CCM wanalijua( Gamba la Nyoka), sijui imekuwaje upo out of the inner circle. Anyways unaweza pia kuwa katika kazi, na hivi promotion ya rasimu ya CCM imeanza, watu wapo busy

Nne,ni tatizo kubwa kudhani katiba ni mali ya wapinzani. Nilidhani ungeshauri wananchi wafanye nini. Kama tutaendelea na mwendo mwenye kisu kikali ndiye anayekula nyama, tutaandika katiba kila baada ya miaka 5.
 
Wakuu naomba mnisaidie maana nimechanganya kidogo, hivi kwa wananchi ili katiba ipite inahitaji 50% + au ni 2/3 (75%) kama ilivyokua bungeni??
Maana hata kama wananchi wengi hawana uelewa wa kutosha, kwa mchakato ulivyokwenda naona ugumu sana kupitishwa kwa katiba hii kihalali bila hila zozote
Sina kumbu kumbu, lakini ninadhani ni 2/3. Mchambuzi unaweza kutusaidia kwa hili.
 
Last edited by a moderator:
Anayeamua matokeo ya kupiga kura sio wale wanaopiga kura bali wale wanaohesabu kura; ndio maana hata kwenye kuhesabu akidi Sitta na genge lake hawakuruhusu wasimamizi wa kuhesabu zile kura na hapo wakapata nafasi ya kuchakachua!! Nguvu ni lazima itumike kuhakikisha kuwa ccm hawataiba kura wakati wa kuhesabu kura za maoni; ccm na serikali yake ni wapenda kutumia vitisho vya vyombo vya dola kufanikisha uharamia wao!! Wananchi ni lazima wawe vigilant kulinda kura zao ama sivyo haki yao itapokwa na hawa magamba!! This country has that experience of vote rigging!!
Mimi nadhani kuongelea kura ya maoni ni kutoa uhalali kwa mzoga.
Nilidhani tuongelee uharamia, fraud,forgery, bribery, corruption na ujinga mwingine ulivyotendwa na John Samwel Sitta

Ningefikiri wananchi wakatae kabisa hata kabla. Hilo linawezekana. Mbona mswada wa kwanza ulichanwa kule znz na serikali ikanywea.
Tatizo wananchi tunadhani CCM ndio nchi, ukweli ni kuwa sisi ndio nchi. Tukikubali kila kitu hata hizo kura wataiba tu.
Kwanza tuwaonyeshe kuwa wizi,kughushi n.k. wakiwa hawana wananchi wote(UKAWA) kumeondoa maana ya katiba ya nchi.

Tuwape nafasi waifanye ya Lumumba, si ya Tanzania.
 
Tofauti na Maelezo ya jaji warioba na tume ya katiba, juzi Katika hotuba yake baada ya kukabidhiwa katiba iliyopendekezwa, hatukumsikia rais wa JMT Wala kiongozi yoyote akifafanua maslahi ya Washirika wa pande zote Mbili za muungano - hasa kiuchumi na kimamlaka. Badala yake, tulichosikia kwa lugha nyepesi Kabisa ilikuwa ni maslahi ya upande mmoja tu wa muungano - Zanzibar, huku maslahi kwa upande wa Tanganyika yakipuuzwa Kama vile Tanganyika haipo, lakini muhimu zaidi, Kama vile Tanganyika haitapata athari Zozote chini ya Mfumo ndani ya katiba inayopendekezwa.

Kwa mfano, Zanzibar wameahidiwa mikopo ya nje, uhusiano wa kimataifa, kuendesha rasilimali zao za Mafuta na gesi, na muhimu, tofauti na Huko nyuma, Zanzibar sasa itavuna viongozi watano wenye hadhi ya urais huku Tanganyika ikivuna viongozi wawili tu wenye hadhi ya urais (Tena hadhi ya kinadharia tu), huku kivitendo, Zanzibar wakiwa Ndio walioshika mpini. Tutajadili masuala haya yote - moja baada ya jingine, lakini Katika Bandiko hili, ningependa kujadili suala la madaraka ya urais chini ya katiba inayopendekezwa na jinsi gani mapendekezo husika yatachochea kuvunjika kwa muungano:

Tukumbuke Kwamba hoja za kina Nape Nnauye, MwanaDiwani, chama, Kobello, Gamba la Nyoka, Mtanganyika, ZeMarcopolo, na makada Mbali mbali CCM dhidi ya serikali Tatu ilikuwa ni pamoja na Kwamba serikali Tatu zitaongeza utitiri wa viongozi, hivyo kuongezea mzigo walipa kodi. Makada hawa walikebehi sana hoja zetu juu ya uwepo wa rasimu ya CCM ya mafichoni lakini Ukweli sasa upo wazi - rasimu iliyopotishwa Ina content ambayo ilishafanyiwa kazi na kina Chenge, migiro, Wassira, lukuvi, etc Kabla hata mjadala kamili bungeni haujaanza. Tulisema miezi Sita iliyopita (April 2014), na sasa Ukweli huo umesimama.


Madaraka waliyopewa Zanzibar yapo kwenye draft ya Warioba.na ungeainisha kama Mgombea wa urais angekuwa Prof. Safari au Dr. Shein,mgombea mwenza akatoka Bara, Si ungelia machozi kabisa?

Ainisha mamlaka kutokana na wapiga kura na siyo asili au ukabila wa mtu, hayo ni mambo primitive.

Watanzania kwa ujumla watamchagua Rais na makamu wa Rais wawili (wa kwanza na waziri mkuu).

Waziri mkuu atachaguliwa na watanzania indirectly kutokana na rais aliyepewa nguvu na watanzania kwa ujumla, madaraka yake yapo chini ya uwezo wa bunge la jamhuri ambacho ni chombo cha watanzania kwa ujumla. Kwa hiyo viongozi watatu ni wa watu wa jamhuri. Na viongozi watatu ni wa Zanzibar (makamu wa rais wa Zanzibar waili na rais).

Hakuna katiba ya mafichoni yenye mabunge matatu,huo ni uongo uliouleta JF na inabidi u-apologize( ila kwa sababu hujali, unaonasiyo tatizo kuongopa)
 
CCM NA WASHIRIKA WAO WAWEWESEKA, WAHAMISHA UTETEZI KUTOKA GHARAMA ZA SERIKALI SASA WAJIFANYA KULINDA MUUNGANO,

wadau nimekua nikiwafuatilia sana Nguruvi, Mchambuzi, mag3, bongolander na wengineo kuhusu masuala ya nchi yetu yakijadiliwa hapa katika Duru la Great thinkers na hasa suala hili la katiba ambalo ni hot news kwa sasa, ninwashukuru sana binafsi kwa kunifumbua macho yangu nimeweza kuona zaidi ya maono ya kawaida kupitia mabandiko yenu muhimu yaliyojaa hoja ma tija, for sure kazi yenu sio bure mnatuelimisha wengi, msichoke wala kukatishwa tamaa kwa changamoto na matukano ya watu wenye negative perceptions.


Back to the topic,
wakati mchakato wa katiba kwa hatua ya bunge maalumu la katiba, makada wa CCM waliipinga sana rasimu ya tume kwa kisingizo cha muundo una gharama nyingi na kelele nyingi sana zisizo na justfication hata kidogo. Ukihudhuria midahalo karibu yote na makongangamano walikua wakisema serikali tatu ni gharama na zinamuumiza mlipa kodi, na waliongea bila justification kwakua tu walijua wanaongea na watu wajinga na wanao kubali kila upuuzi unaosemwa.

Nikasitika sana mtu mchumi kama Mwigulu, wasomi kama Prof. Tibaijuka, Mwandosya, Dr. mwayembe, Migiro na wasomi wengi wa chama hicho wakijadili bila justification wala proof za kitaalam walau kidogo kuhusiana na gharama, hapo sijawataja wale ambao elimu zao tu ni doubt kumkosoa Warioba na tume yake kama akina Lukuvi, Lusinde, Komba,Asha baraka na wengine wengi wakawa wanaropoka tu bila aibu kwamba muungano wa serikali tatu ni gharama. Cha kusitisha sana watu wenye vyeo ndani ya chama kama mwenezi wao wakawa wanongea very cheap things " ukiongeza mke mwingine ni gharama" unajiuliza huyu mtu anafikiria sawa sawa kweli au anaongozwa na nn kuongea hayo?? Japo simshangai sana kwenye aproach yake ya siasa za kimihemko, though kiukweli kwa suala kama la katiba uweledi unahitajika zaidi.

Kwa nini walifanya hayo yote kudanganya kuhusu gharama?? Jibu ni rahisi wanawajua watanzania ni wajinga na watadanganyika kirahisi kwani wao ndio wana maisha duni, sasa ukiwaambia unawaongezea mzigo inakua ni shida kwao na kwa hapo wakajua wataungwa mkono( na hasa watanganyika maana ndio wano umia zaidi) Wanachosahau Hapa ni kwamba siku zote sio sawa na watanzania wa leo sio wa jana, miongoni mwao wanauelewa mzuri na watawaelimisha wasioelewa, japo sio wote bt naamini watakuwepo watakaokombolewa


Mungu hamfichi Mnafiki, nini kimetokea baadae? Kama alivyoainisha mchambuzi kwenye bandiko lake # 23 na Nguruvi3 kwenye mada zake za gharama za muungano, CCM wameumbuka ghafla, rasimu yao ya mafichoni inaoneka ni ya gharama kubwa mara dufu ya ile rasimu ya tume ya warioba na wale wooote waliokua wanapiga kelele kwamba serikali tatu ni gharama wapo kimya juu ya hili. Please Mwigulu 1st class economist kama unavyojiita, tunakuomba ujitokeze tena na wenzako akina Nape na wasira mtueleze kwa takwimu ni ipi rasimu yenye gharama kama mlivyopiga kelele mwanzoni mkiwadanganya watu wasio fikiria zaidi ya ukomo wao ( maana nyie ndio mnaaminika katika chama kuset standards za wengine kuongea) kuropoka hovyo na kuwatukana wazee wa tume, vipi Rasimu ya tume na katiba yenu pendekezwa ipi mzigo kwa watanganyika na wazanzubari?? Ni akina nani wanamapenzi mema na nchi yao??


Kiukweli hamuwezi kujibu maswali haya zaidi ya blah blah, maana kwa kuangalia tu kwenye presidential status kutoka watu watatu sasa ni kama saba ( refer; Mchambuzi, bandiko # 23), bunge lenye watu karibu 400 compare na Bunge la watu 75 ( hata ukichukua na bunge la tanganyka na zanziba hawawezi kuzidi 300). Na gharama kubwa zaidi za kuwabenbeleza wazanzibar waukubali Muungano, kweli mna mapenzi mema ya muungano au mnataka tu kuwafurahisha wazanzibar wabaki kwenye muungano? Kila nikiwaza sipati jibu juu ya mtazamo wa hawa watu na ninalilia nchi yangu sana kupata viongozi wenye maono haya.

"Even the magicians can run out of tricks" aliwahi mdau mmoja wa duru, ndicho kinachowatokea sasa, wamebaki kulazimisha mambo na kujifanya eti wanawaenzi waasisis kwa kufanya haya wafanyayo bila kuangalia time effects, mambo yanabadilika na walicho pendekeza tume ndio uhalisia wenyewe wa muda sio kulazimisha mambo. Wote hawazungumzi tena mambo ya gharama za serikali sasa wanapiga kelele tu kwamba tuulinde muungano kwa gharama yoyote.

utawala wa Rumi ulipokaribia kuanguka walilazimisha mambo kwa kujiona wao ni ruler na wengine watawafuata kwa kila wasemacho, lakini muda uliwalazimisha kukubali ukweli. Ninatamani viongozi na wanchi wasome alama za nyakati na kujiadjust accodingly, maana hata huu muungano tunaosema tunaulinda kama ni kwa visions za nmana hii ya akina Viongozi wa chama kuwadanganya na kuwapotosha wanachi kwamba katiba sio muhimu kwao, basi Naliona anguko kubwa sana na ninafadhaika sana hatutaki kuukubali ukweli.

Niishie hapa, maana ninajisikia uchungu sana kwa namna mambo yanavyokwenda kwenye nchi yangu, i feel cryng for my country,kwa nini watu hawafunguki na kuona zaidi ya upeo wa kawaida, zaidi ya wanasiasa wetu zaidi ya wapiga ramli waongi na wapotoshaji??
 
Kwanza, nikuambie kuwa tuhuma dhidi ya Warioba ni kumchafua tu ambako CCM wamekuwa anafanya kila uchao na hapa unatekeleza wanachokifanya.
Hivyo sidhani kama Mchambuzi atakuwa amekuonea hata kidogo.

1. Warioba hakupaswa kusoma nyakati, yeye aliongozwa na hadidu rejea alizotoa Rais na ambazo Rais alizikana na juzi amezikubali. Ukiangalia kwa jicho pevu, mchakato ulikwenda vema kwa mujibu wa Warioba hata hivyo, Rais aliamua kuuvuruga baada ya kutishwa na wahafidhina ndani ya CCM.

Mzee Warioba hana tatizo, yeye ni tarishi, unless utueleze kama naye alipaswa kutenda ya yahoo, wahtsup na face book.

2.Kuna ushahidi usio na shaka kuwa hata mtaji wa CCM haukuwa na maana.
Huko Makkha mahujaji hawakupiga kura, wale UKAWA 2 ni maruhani anawajua Sitta peke yake.
Ndani ya chumba cha kuhesabu kura za CCM hakukuwa na uhakiki, kura za Tango, whatsup na facebook hazijulikani zilisimamiwa na nani na kwa utaratibu gani.

Afisa ubalozi Saudia kapoteza kazi kwa kusema ukweli, mwanasheria mkuu wa SMZ kapoteza kazi kwa kueleza ukweli.
Huo ndio mtaji unaotaka watu waelewe kuwa CCM ilikuwa nao? Hukuona mazingaombwe hata kidogo yaliyofanyika.
Udanganyifu wa highschool wa Smawel John Sitta unauita mtaji wa kisiasa! ebo!

Tatu, jambo la muhimu si kurasimisha rasimu haramu. Jambo la muhimu ni Watanzania kujadili uharamu, uharamia na madhara yanayolikabili taifa siku zijazo. Hilo ndilo muhimu hata CCM wanalijua( Gamba la Nyoka), sijui imekuwaje upo out of the inner circle. Anyways unaweza pia kuwa katika kazi, na hivi promotion ya rasimu ya CCM imeanza, watu wapo busy

Nne,ni tatizo kubwa kudhani katiba ni mali ya wapinzani. Nilidhani ungeshauri wananchi wafanye nini. Kama tutaendelea na mwendo mwenye kisu kikali ndiye anayekula nyama, tutaandika katiba kila baada ya miaka 5.

Nguvu mimi sipo kwenye ukanda wa kujadili hadithi za mfalme njozi na wakeze, nataka tutazame uhalisia. Wewe na mimi hapa tutalalama kwamba kura zimeibwa au zimeibiwa lakini ukweli ni kwamba JK ameshapokea rasimu, sasa tuangalia njia ya mbele ( way forward) ni lazima tukubali wenye mtaji wa kiasiasa (political capital) kwa sasa ni vyama vya upinzani sababu wao wanalo jukwaa la kufikisha ujumbe mbali zaidi ya mimi na wewe.

Cha muhimu ni kwamba UKAWA wajikite kwenye kuainisha uhaini wa katiba hiyo na kuwapa changamoto Watanzania wengi kuikataa. Lakini muhimu zaidi kama tunataka mabadiliko Tanzania lazima tubadili uwezo wa kufukiri wa Watanzania, wengi wetu sisi ni wasaliti na warubuni. Wapo waliokuwa wanasema wanaweza kudhubutu lakini wakati wa kura wote walipiga ndio, na ndio maana nasema hata leo katiba ile ikiwekwa kwenye chumba cha kupigiwa kura majority ya Watanzania watasema hii ndio katiba yetu.

Kuhusu la mzee Warioba mimi nilishasema tangu mwanzo mawazo ya serikali tatu yalikuwa hayana mashiko na sisi watu wazima tulijua kabisa kwa dhati hayawezi kufika hata kibaha na yatakufa.
 
Tofauti na Maelezo ya jaji warioba na tume ya katiba, juzi Katika hotuba yake baada ya kukabidhiwa katiba iliyopendekezwa, hatukumsikia rais wa JMT Wala kiongozi yoyote akifafanua maslahi ya Washirika wa pande zote Mbili za muungano - hasa kiuchumi na kimamlaka. Badala yake, tulichosikia kwa lugha nyepesi Kabisa ilikuwa ni maslahi ya upande mmoja tu wa muungano - Zanzibar, huku maslahi kwa upande wa Tanganyika yakipuuzwa Kama vile Tanganyika haipo, lakini muhimu zaidi, Kama vile Tanganyika haitapata athari Zozote chini ya Mfumo ndani ya katiba inayopendekezwa.

Kwa mfano, Zanzibar wameahidiwa mikopo ya nje, uhusiano wa kimataifa, kuendesha rasilimali zao za Mafuta na gesi, na muhimu, tofauti na Huko nyuma, Zanzibar sasa itavuna viongozi watano wenye hadhi ya urais huku Tanganyika ikivuna viongozi wawili tu wenye hadhi ya urais (Tena hadhi ya kinadharia tu), huku kivitendo, Zanzibar wakiwa Ndio walioshika mpini. Tutajadili masuala haya yote - moja baada ya jingine, lakini Katika Bandiko hili, ningependa kujadili suala la madaraka ya urais chini ya katiba inayopendekezwa na jinsi gani mapendekezo husika yatachochea kuvunjika kwa muungano:

Tukumbuke Kwamba hoja za kina Nape Nnauye, MwanaDiwani, chama, Kobello, Gamba la Nyoka, Mtanganyika, ZeMarcopolo, na makada Mbali mbali CCM dhidi ya serikali Tatu ilikuwa ni pamoja na Kwamba serikali Tatu zitaongeza utitiri wa viongozi, hivyo kuongezea mzigo walipa kodi. Makada hawa walikebehi sana hoja zetu juu ya uwepo wa rasimu ya CCM ya mafichoni lakini Ukweli sasa upo wazi - rasimu iliyopotishwa Ina content ambayo ilishafanyiwa kazi na kina Chenge, migiro, Wassira, lukuvi, etc Kabla hata mjadala kamili bungeni haujaanza. Tulisema miezi Sita iliyopita (April 2014), na sasa Ukweli huo umesimama.

Twende moja kwa moja kwenye hoja.

Tume ya warioba ilipendekeza rais mmoja wa muungano na viongozi Wengine wawili wa kuongoza pande Mbili za muungano bila ya kujalisha Viongozi hawa watapewa majina gani ya kiutawala. Pahala ambapo palitarajiwa kuwa suala la title za viongozi wa nchi washirika lingejadiliwa lakini bila ya kuathiri Roho ya rasimu ya wananchi (serikali Tatu) ilikuuwa ni ndani ya bunge maalum la katiba. Lakini tofauti na tume ya warioba, na katiba inayopendekezwa sasa imebariki gharama kubwa zaidi kwa wananchi, hasa watanganyika. Tofauti na rasimu ya tume ya jaji warioba, rasimu ya mafichoni ya CCM Sasa imeweka wazi Kwamba Jamhuri ya muungano wa Tanzania itakuwa na viongozi SABA wenye hadhi ya URAIS. Tukianza na Upande wa Zanzibar, wao watakuwa na viongozi WATANO wenye hadhi ya urais, Kama ifuatavyo:

1. Rais wa Zanzibar (anayepigiwa kura na wazanzibari tu lakini Ana Nguvu hadi kwa wananchi ambao Hawakushirikishwa kumchagua - watanganyika).
2. Makamu wa kwanza wa rais Zanzibar ambae ni msaidizi wa rais wa Zanzibar, hivyo kuwa na mamlaka ya kukaimu mamlaka juu ya watanganyika.
3. Makamu wa pili wa rais Zanzibar (mamlaka sawa na makamu wa kwanza wa rais Zanzibar).
4. Makamu wa kwanza wa rais wa JMT (mgombea mwenza kutoka Zanzibar (Huyu yupo kuwakilisha maslahi ya wazanzibari, sio watanganyika).
5. Makamu wa pili wa rais wa JMT (ambae pia Ana kofia nyingine ya urais wa Zanzibar).

Hapa tusisahau Kwamba katiba ya Zanzibar (2010) imepora mamlaka ya katiba ya JMT.

Kwa Upande wa Tanganyika, wao watakuwa na viongozi WAWILi tu kati ya marais Saba wanaoridhiwa na katiba inayopendekezwa:

1. Rais wa JMT - Huyu tumeshaona jinsi gani katiba ya Zanzibar (2010) ilivyompora mamlaka. Kwa maana nyingine, rais wa JMT chini ya katiba inayopendekezwa atakuwa ni rais wa Muungano kinadharia tu, huku akiwa sio lolote kivitendo. Kwa maana nyngine Rahisi, rais wa muungano will become "a toothless dog" Katika uongozi wake wa jamhuri ya "muungano". Ukweli huu utazidi kujitokeza siku sio nyingi kwani Kama alivyojadili Nguruvi3 Hapa au kwingineko, Zanzibar hawawezi kurudi nyuma na kubadili katiba Yao kwa manufaa ya Tanganyika iliyovaa koti la muungano.

2. Rais wa pili kutoka wa Tanganyika atakuwa ni waziri mkuu wa JMT ambae vituko vya katiba inayopendekezwa vimempa wadhifa wa "makamu wa TATU" wa rais!

Hii inafanya uwepo wa marais SABA Katika mazingira ya katiba inayopendekezwa - Zanzibar ikitoa watano, Tanganyika ikitoa wawili, huku marais wa upande wa Zanzibar wakiwa Ndio wenye mamlaka makubwa zaidi kiutawala (rejea mgongano wa kikatiba) lakini pia kirasilimali (kwani chochote cha Tanganyika ni cha muungano kwa vile haina serikali yake). Hali hii inafanya cha Zanzibar Kiwe cha Kwao, na cha Tanganyika Kiwe cha wote - watanzania. Licha ya soko moto kote hili, bado Gharama zote za kuhudumia marais hawa Saba wakiwa madarakani na wakienda kustaafu zitakuwa ni za mtanganyika. Mwezi Aprili mwaka huu, Hamad rashid alipinga sana rasimu ya tume Kwamba itapelekea uwepo wa marais watatu ambao watakuwa ni mzigo kwa walipa kodi. Katika Hili la marais Saba sijui atakuwa na mtazamo gani. Tatizo letu ni Kwamba hatuna waandishi wa habari Mahiri kufuatilia mambo Kama haya.

Kama alivyojadili Nguruvi3, muungano umefikia Katika hatua ya hatari kuliko kipindi chochote Kile. Kwa mfano Katika suala jamhuri ya muungano, miaka 50 baadae, JMT imekuwa ni nchi Mbili Zenye serikali Mbili, na marais Saba,lakini Watu bado Hawaoni Kwamba hili ni bomu la mtego (timing bomb).

Chini ya Katiba inayopendekezwa, CCM inapendekeza kwamba – Rais wa Zanzibar afanywe kuwa Makamu wa Rais wa Muungano bila ya kujalisha Rais wa Muungano anatokea upande upi wa Muungano. Kwa kufanya hivyo, CCM inadai kwamba – hali hii itamwongezea Rais wa Zanzibar - "madaraka na hadhi" ndani ya serikali ya Muungano na pia nje ya nchi. Huku ni kupandikiza mbegu ya machafuko na hatimaye kuvunjika kwa muungano kwa sababu:

Mkataba wa Muungano (1964) uliweka utaratibu ambao – Rais wa Muungano wa NCHI Moja, alikuwa na wasaidi wake wakuu wawili – Makamu wa Kwanza wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Zanzibar (Marehemu Karume), na Makamu wa Pili wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika (Marehemu Kawawa).

LAKINI chini ya katiba inayopendekezwa, CCM haisemi iwapo Rais ni MMOJA wa nchi MOJA, badala yake Inasema tu kutakuwa na rais wa JMT, na hao Wengine Sita.

Katiba inayopendekezwa haisemi ni kiongozi gani ndiye atakayesimamia Mawaziri watakaokuwa wanasimamia mambo ya Tanzania Bara katika mfumo huu wa serikali mbili "ulioboreshwa". Katika mikakati yake ya kuuza kwa umma katiba inayopendekezwa, CCM haina Maelezo juu ya ufafanuzi wa masuala muhimu (kiutekelezaji), kwa mfano, - katika mazingira ya Zanzibar kuwa ni "nchi" kamili, yenye "mamlaka" kamili, katiba, amiri jeshi mkuu, Wimbo wa taifa, ikitokea kwamba Rais wa Muungano anatokea upande wa pili wa muungano (Zanzibar), JE:

· Rais huyu kutoka nchi jirani ya "Zanzibar" atasimamia masuala yasiyo ya muungano - ya upande unaoitwa "Tanzania Bara", ndani ya Jamhuri ya Muungano, kwa mamlaka yepi?

· Iwapo Rais wa Muungano atatokea panapoitwa "Tanzania Bara", Rais huyu wa Muungano atakuwa na mamlaka yepi ya kusimamia mambo ya "Tanzania Bara" wakati yeye atakuwa amechaguliwa na wananchi wa pande zote mbili za muungano - Tanganyika na Zanzibar?

· Zipo wapi ‘pande mbili' za muungano bila ya kuwepo kwa Serikali ya Tanganyika?

Katika haya, CCM haina uwezo wa kufafanua Hali ambayo itazidi kuudhoofisha muungano. Kwa vyovyote vile, Katiba inayopendekezwa haitaboresha muungano bali itajenga mazingira ya kuvunja muungano. Tuendelee kufafanua hili:

Kwa mfano, iwapo Rais wa Muungano atatokea upande wa nchi jirani ya "Zanzibar", ambaye kwa Mujibu wa katiba inayopendekezwa, Rais wa Zanzibar pia atakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano. CCM inapendekeza kuwa rais wa nchi Jirani ya Zanzibar moja kwa moja awe ni makamu wa rais wa muungano (Tanganyika) hata Kama hakuna mtanganyika hata mmoja aliyempigia kura. Kwa maana nyingine, rais wa Zanzibar pia atakuwa ni rais wa watanganyika kwa njia ya uteuzi. Hiki ni kituko cha mwaka - watanganyika kuwa na marais wawili, mmoja waliyempigia kura, mwingine aliyepigiwa kura nchi Jirani (Zanzibar) kisha kuteuliwa kuwa rais wao watanganyika, Tena akiwa na katiba (ya Zanzibar)ambayo Ipo juu kimamlaka kuliko Ile ya watanganyika/muungano.

Mbali ya athari hizi, Ipo nyingine kubwa. kwa mfano, Kitendo cha rais wa Zanzibar kuwa makamu wa rais wa muungano bila kujalisha Rais wa Muungano atatokea upande upi wa Muungano kitatupeleka Katika Hali ifuatayo:

• Siku moja, Rais wa Muungano na Makamu Wa Rais Wa Muungano, wote watakuwa wametokea nchi jirani ya "Zanzibar". Kwa maana hii, aidha kwa makusudi au bahati mbaya, CCM inajenga mazingira ambayo Zanzibar hawataweza tena kutoa Rais wa Muungano. Hii ni kwa sababu:

Hali hii itaamsha watanganyika kwani kwa maana ya Kwamba - Kama tulivyoona, chini ya rasimu inayopendekezwa na CCM, Rais wa Zanzibar "automatically", atakuwa pia ni Makamu wa Rais wa Muungano. Sasa ikitokea Siku CCM ikasimamisha mgombea Urais wa Muungano kutokea nchi jirani ya "Zanzibar", nchi ambayo pia automatically itatoa makamu wa Rais wa Muungano, chini ya mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, wapiga kura kutoka upande wa inayoitwa "Tanzania Bara", upande ambao una wapiga kura zaidi ya 90% ya wapiga kura wote wa Jamhuri ya Muungano, HAKIKA, wengi ya wapiga kura hawa kutoka "Tanzania Bara", hawatakubali kumchagua mgombea wa urais (CCM) kutokea nchi ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake pia anatokea huko huko "nchini" Zanzibar. Kwa maana nyingine, wananchi wa tangangika siku moja watakataa mgombea wa aina hii atakayependekezwa na CCM.

Je athari yake ni nini?

Ni kwamba – chini ya katiba inayopendekezwa na CCM, ni muhimu sasa waZanzibari waanze kujiandaa kisaokolojia Kwamba watanganyika Kamwe hawatomchagua kwenye Sanduku la kura mgombea urais mzanzibari kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Watanganyika watakuwa wamefanya uamuzi sahihi lakini Kitachofuatia kwa upande wa Zanzibar ni Kwamba wazanzibari wataanza kulalamika kwamba wanabaguliwa, wanaonewa, wananyimwa haki ndani ya Jamhuri ya muungano, kwahiyo waachwe "Wapumue". And interestingly enough, watakaongoza katika kutoa hoja hizi ni wale wale wazanzibari ambao Islaml Jusa alisema kwamba walipofika Dodoma "Waliufyata". Ni wale wale ambao leo wanapinga kwamba wao sio "wasaka tonge". Katika kundi hili, hatutashangaa kuja kuona viongozi kama Balozi Seif Iddi, Mohamed Seif Khatib, nahodha, kificho,Hamad Rashid Mohamed, na wengine wakija kugeuka na kusema Kwamba Tanganyika inafanya Zanzibar kuwa koloni. Baadae tutaona jinsi gani ruksa kwa Zanzibar kukopa, kuwa na uhusiano wa kimataifa n.k bado hayatamaliza Dhana ya ukoloni.Hakuna mamlaka kamili kwa Zanzibar kwa Jambo lolote bila ya uwepo wa Tanganyika.

• Je kwa upande wa viongozi wa CCM bara, watakuja Lamba matapishi yao?

Kwa upande wa inayoitwa "Tanzania Bara", iwapo Mgombea Urais wa Muungano atatokea nchi jirani ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake "automatically" pia atatokea Zanzibar, watakaoongoza katika kupinga hali hii haitakuwa watu wengine bali wale wale makada wa CCM ambao ndani ya bunge la katiba walijiita kwa majigambo Kwamba wao Ndio wenye "Maoni ya Walio Wengi", ambao wamepitisha katiba inayopendekezwa kwa vigele gele na
Vifijo. Fitina zilizomkumba Dr. Salim Ahmed Salim alipokuwa anawania urais hazitafua dafu kwa fitina zitakazojitokeza katika mazingira tunayojadili hapa. Wana CCM ambao watakuwa katika makundi ya kutafuta Rais wa Muungano wataendesha kampeni kubwa kupinga uongozi wa Muungano kwenda kwa "nchi jirani katika kofia zote mbili za juu – Rais wa Muungano na Makamu wa Rais wa Muungano.

Kuna haja ya wazanzibari na watanganyika kuungana kuzuia hatari iliyopo Mbeleni. Ujumbe muhimu kwa wazanzibari ni Kwamba wanachoambiwa na CCM ndani ya rasimu inayopendekezwa ni kwamba:

• "Kuanzia sasa, wazanzibari wajiandae tu kisaikolojia kuwa ni "wasindikizaji" tu wa Uongozi" katika Jamhuri ya Muungano."

Pia CCM nayo ijiandae kutupiwa lawama na malalamiko mapya juu ya Ukoloni wa Tanganyika kwa Zanzibar. Mbegu ya kuvunjika kwa muungano sio tu imeshapandwa, Bali pia imeanza kuchepuka.

Itaendelea ambapo tutajadili athari za katiba inayopendekezwa - athari Katika maeneo mengine ya uchumi, rasilimali, bunge, Mahakama, mikopo, uhusiano wa kimataifa n.k, hoja ikiwa ni jinsi gani maeneo haya yataathirika chini ya katiba inayopendekezwa, na jinsi gani yatazidi kuudhoofisha muungano wa serikali Mbili na hatimaye muungano huo kuvunjika.

Cc Dingswayo, Mag3, EMT, Mkandara, Barubaru, Bongolander, ukwelikitugani, happyfeet, Pasco, Jasusi, JokaKuu, MTAZAMO, Mwigulu Nchemba, Ezekiel Maige, MJINI CHAI, gfsonwin Mimibaba Zakumi

















Sent from my iPhone using JamiiForums

Kila jambo ni wakti na siku zote wakti ukifika huwezi kuzuia jambo kuwa.

Hapa namaanisha kuwa WATANGANYIKA bado hawako tayari kuanzisha sirikali yao ima kwa kukhofia namna ya kuiendesha na kutojiamini.

Lakin kubwa hapa ni suala la UDINI. Nafikiri mmeona suala la mahakama ya kadhwi ilivyosumbua Bunge la katiba a Mh sitta.

Mimi nashauri Tgk jipangeni na muone changamoto zenu na kuzitafutie majawabu kabla kuanzisha sirikali yenu.

Ahsantum

 
Kuhusu la mzee Warioba mimi nilishasema tangu mwanzo mawazo ya serikali tatu yalikuwa hayana mashiko na sisi watu wazima tulijua kabisa kwa dhati hayawezi kufika hata kibaha na yatakufa.

Mawazo ya serikali Tatu yalikuwa ni mawazo ya Nani?

Na ni Nani aliyefanya mawazo ya serikali Tatu yasivuke kibaha?



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hakuna katiba ya mafichoni yenye mabunge matatu,huo ni uongo uliouleta JF na inabidi u-apologize( ila kwa sababu hujali, unaonasiyo tatizo kuongopa)[/FONT][/SIZE][/COLOR]

Mtaendelea kuyaita "uongo" Yale yote ambayo fahamu zikiwarudia huwa mnaona Kwamba kumbe hayafai.

Ni hivi - hoja ya kuwepo kwa baraza la wawakilishi la Tanzania bara litakaloshughulikia masuala ya Tanzania bara chini ya Mfumo wa muungano wa serikali Mbili, hata ziboreshwe vipi, ni Jambo ambalo lisingewezekana. Hatua yenu ya kujaribu kuja na mkakati wa kuzuia wabunge kutoka visiwani kushiriki mjadala usio husu mambo ya muungano ingekuwa ni kuchochea tu mgogoro. Hii ni kwa sababu mmepata ufahamu na Kugundua Kwamba hakuna "mambo ya Tanzania bara peke yake" yatakayopatikaba chini ya Mfumo wa serikali Mbili hata mkiziboresha vipi, mwisho wake kutakuwa na mambo ya Zanzibar na mambo ya muungano tu, kwisha.

Mlipopata fahamu mkagundua Kwamba ndani ya serikali Mbili, hauwezi kuwa na bunge la Tanzanka bara na bado Mkazunguka kwa wananchi na katiba mnayopendekeza Kwamba bunge Hilo litakuwa ni la wananchi. Ndani ya serikali Mbili hata mziboreshe namna gani hakuwezi kuwa na msimamizi wa mambo ya Tanzania bara kwa sababu serikali ya kufanya hivyo ni serikali ya Tanganyika ambayo hamuitaki licha ya wananchi kuzidi kuitaka. Fahamu zenu zikarudi na mnaona kuleta Bunge la Tatu ndani ya serikali Mbili - hakuna atakayewajibika pale aliyeagizwa atashindwa kutekeleza alichoagizwa.

Fahamu zilipowarudia, mmegundua Kwamba duniani kote, bunge ni moja ya mihimili mitatu ya dola, mingine ikiwa ni Mahakama na serikali. Mligundua Kwamba hakuwezi kuwepo mabunge mawili ndani ya bunge la muungano - bunge la TANZANIA bara bila ya kuwepo baraza la mawaziri la Tanzania bara, bila rais au waziri mkuu.

Na kuhusu hoja yako nyingine hapo juu kuhusu uwepo wa marais Saba, hoja ambayo imezurura zurura bila
tija, hoja ya Kujibu ambayo mlikuwa mpo busy bungeni mkipotosha umma huku pia kina nape wakizunguka nchi nzima kuijenga ni Kwamba nanukuu:

"Serikali Tatu ni kuongeza gharama na kuifanya nchi kuwa na marais watatu, suala ambalo pia litaleta mgongano wa madaraka".

Je marais Saba ndani ya serikali Mbili ni nafuu zaidi kwa walipa kodi kuliko mapendekezo ndani ya rasimu ya tume? Je, marais Saba hakutaleta mgongano wa madaraka?



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Madaraka waliyopewa Zanzibar yapo kwenye draft ya Warioba.na ungeainisha kama Mgombea wa urais angekuwa Prof. Safari au Dr. Shein,mgombea mwenza akatoka Bara, Si ungelia machozi kabisa?
Ainisha mamlaka kutokana na wapiga kura na siyo asili au ukabila wa mtu, hayo ni mambo primitive.
§ Watanzania kwa ujumla watamchagua Rais na makamu wa Rais wawili (wa kwanza na waziri mkuu).
§ Waziri mkuu atachaguliwa na watanzania indirectly kutokana na rais aliyepewa nguvu na watanzania kwa ujumla, madaraka yake yapo chini ya uwezo wa bunge la jamhuri ambacho ni chombo cha watanzania kwa ujumla. Kwa hiyo viongozi watatu ni wa watu wa jamhuri. Na viongozi watatu ni wa Zanzibar (makamu wa rais wa Zanzibar waili na rais).
§ Hakuna katiba ya mafichoni yenye mabunge matatu,huo ni uongo uliouleta JF na inabidi u-apologize( ila kwa sababu hujali, unaonasiyo tatizo kuongopa)
Katiba iliyopo ni ya mafichoni. Hapa duru kuna uzi huu https://www.jamiiforums.com/great-t...-za-ccm-kuingiza-katiba-yao-ya-mafichoni.html Unaongelea na kuwataja wahusika wa katiba ya mafichoni.

Hilo lilikuwa ni miezi 4 iliyopita. Wote waliotajwa ndio waandishi wa rasimu hii ya CCM

Ni kutokana na rasimu ya mafichoni, mwanasheria mkuu wa znz alishangaa kila siku rasimu inakamilika bila hata mjadala.

Akauliza namna vipengele vitakavyopingana na ile ya znz na ugumu mbele ya safari. Yaliyompataunayujua.

Yule Afisa wa ubalozi aliyesema mahujaji hawawezi kupigakura, yaliyompata unayajua.

Muhimu Zaidi, rasimu ya Warioba ilisema viongozi 3, Rais waJMT na kila mshirika na kiongozi wao.
Kwa maneno mengine kila mshirika atahudumia viongozi wake isipokuwa yule wa JMT ambaye obvious atahudumiwa naTanganyika kwa jina la Tanzania.


Kwa rasimu ya CCM, viongozi 7 anaosema Mchambuzi au 6 unosema wewe ni mzigo wa Mtanganyika.
Makamu wa rais ambaye ni Rais wa znz atalipwa kwa wadhifa wa makamu wa Rais wa JMT

. Na hao wengine kwa kutambuliwana rasimu ya CCM na kutokuwepo kwa Tanganyika, watahudumiwa na Tanganyika kwajina la Tanzania.


Swali usilotaka kujibu ni hili, ukilinganisha na rasimu yaWarioba, hii ya CCM unayoipigia debe imepunguza vipi gharama ulizowahi kusema S3 itaongeza?
 
Back
Top Bottom