Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Mkuu kinachoongelewa hapa ni hoja. Tumekujibu hoja zako na pengine ungettuelewesha kama hatuelewi.

Hatuwezi kukaa kimya hata pale tunapoona unapotosha. Unaposema mfano wa Canada na Tanzania ni sawa, tutasema hapana! Unaposema issue siyo uchumi, wakati madai ya wznz ni kuhusu kuonewa kiuchumi nawe ukiwasadidia katika mikopo na misaada, tuakwambia no, uchumi ndilo tatizo.

Ukitaka tuamini kuwa znz inaonewa, tutakuonyesha haionewei.
Ukisema S2 ni nafuu kuliko 3, tutakuuliza, tuonyeshe unafuu ulipo.

Nashangaa kukuuliza utuonyeshe unafuu wa S2 unakuwa mbogo. Ni hoja mkuu, matusi na kashfa hazina nafasi.

Unataka kubabaisha umma kuwa unaishi Canada, wakati mfumo wenyewe huelewi. Hakuna wabunge wa majimbo wanaoingia federal gov na hakuna wa fed wanoingia majimboni. Tanzania si Canada, mfumo upo tofauti na hakuna mwingine kama huu duniani.

Ulipokuja na hoja ya bima ya afya, tuliweka sawa hata pale usipopajua ingawa unatumia bima hiyo.Tunausaidia umma dhidi ya wapotoshaji na wababaishaji.

Tunakwenda kwa hoja. 'If you can't take the heat get out of the kitchen'
nasema kulumbana na wewe ni sawa na kumfukuza kichaa nikiwa uchi kwa sababu hata ukioa leo lengo la ndoa ni upendo na kuwa na familia yako ikitokea maswala ya mkeo kudai fedha au mali haina maana ndoa yenu ilitokana na malengo ya kifedha na mali. Unashindwa vipi kuelewa kwamba haya ya siasa na uchumi yamekuja baada ya muungano. Hata Mchambuzi kasema muungano wetu ulikuwa wa kisiasa na sio kiuchumi wewe umekazania tu uchumi. Mimi nimewakosoa nyote na kuwambai muungano wetu ulikuwa wa WATU yaani jamii yetu kuwa moja, haya madai mengine yapo na yataendelea kuwepo na ndio maana Wazanzibar hawaelewi wanapoambiwa Zanzibar sio nchi ni kutokana na fikra za kisiasa na kiuchumi baada yaa.

Sasa wewe unakuja namaswala ya Ethiopia na Eretria ambao waliungana lakini Ukabila ukawatenganisha, sijui Syria na Egypt sielewi unazihusishaje. Somalia na Ogaden wakati Ogaden ipo Ethiopia ilhali wakazi wake ni Wasomali bado huelewi kwamba muungano wa WATU huondosha ukabila na unaposhindwa kuondoa hilo lolote linaweza tokea. Maswala ya kiuchumi yapo EU kweli na unaweza kusoma mkataba (TREATY) Waloandaa toka mwaka 1958 kuundwa kwa jumuhiya hiyo na wakaja unda mwaka 1992. EU was Originally signed in Rome as the Treaty establishing the European Economic Community.Na ukija soma Artical of Union yetu hakuna mahala popote siasa wala Uchumi umehusishwa hata ktk functions zake (mambo 11) siasa na uchumi havikuwemo lakini wewe bado unalazimisha vilikuwemo, kuna haja gani mimi kuendelea kumfukuza kichaa!
 
nasema kulumbana na wewe ni sawa na kumfukuza kichaa nikiwa uchi kwa sababu hata ukioa leo lengo la ndoa ni upendo na kuwa na familia yako ikitokea maswala ya mkeo kudai fedha au mali haina maana ndoa yenu ilitokana na malengo ya kifedha na mali. Unashindwa vipi kuelewa kwamba haya ya siasa na uchumi yamekuja baada ya muungano. Hata Mchambuzi kasema muungano wetu ulikuwa wa kisiasa na sio kiuchumi wewe umekazania tu uchumi. Mimi nimewakosoa nyote na kuwambai muungano wetu ulikuwa wa WATU yaani jamii yetu kuwa moja, haya madai mengine yapo na yataendelea kuwepo na ndio maana Wazanzibar hawaelewi wanapoambiwa Zanzibar sio nchi ni kutokana na fikra za kisiasa na kiuchumi baada yaa.

Sasa wewe unakuja namaswala ya Ethiopia na Eretria ambao waliungana lakini Ukabila ukawatenganisha, sijui Syria na Egypt sielewi unazihusishaje. Somalia na Ogaden wakati Ogaden ipo Ethiopia ilhali wakazi wake ni Wasomali bado huelewi kwamba muungano wa WATU huondosha ukabila na unaposhindwa kuondoa hilo lolote linaweza tokea. Maswala ya kiuchumi yapo EU kweli na unaweza kusoma mkataba (TREATY) Waloandaa toka mwaka 1958 kuundwa kwa jumuhiya hiyo na wakaja unda mwaka 1992. EU was Originally signed in Rome as the Treaty establishing the European Economic Community.Na ukija soma Artical of Union yetu hakuna mahala popote siasa wala Uchumi umehusishwa hata ktk functions zake (mambo 11) siasa na uchumi havikuwemo lakini wewe bado unalazimisha vilikuwemo, kuna haja gani mimi kuendelea kumfukuza kichaa!
Mkuu ,noma nipo katika rekodi nikisema kuwa muungano wa awali ulikuwa wa kisiasa, lakini, kutokana na mabadiliko ya kiuchumi duniani kwasasa muungano wowote unaangaliwa kiuchumi.

Ndio msingi wa madai ya wazanzibar kuonewa katika muungano. Wznz hawajalalamika kubaguliwa katika jamii yetu.

Tena ndio wanafaidika na muungano wa 'WATU' kwa ukweli kuwa hakuna taifa lililobeba wazanzibar wengi kama Tanganyika.
Na kama ni hivyo, malalamiko yao ya nini?

Jibu,wanataka fursa za kiuchumi na hapo huwezi kukwepa ukweli kuwa sasa hivi ni uchumi.

Malalamiko ya wznz kuhusu mamlaka kamili hayapo katika undugu na Watanganyika.
Vinginevyo wasingehitaji mamlaka kamili. Malalamiko yao ni ya kiuchumi.

Wamefika mahali wanapoteza hata fahamu kwa maelezo ya ajabu.
Kuna video katika bandiko hili ambalo Jusa anasema, taasisi za muungano zote zipo bara na hivyo kuwanyima wzn fursa za ajira na yatokanayo. Bila kuangalia jiografia au gharama, bado wanataka kuongeza mzigo kwasababu tu hoja yao ni ya kiuchumi

Kwavile suala ni uchumi na hilo halikwepeki kwa mtazamo wa wznz, Watanganyika waliokuwa kimya muda mredu wameamaka na kuchachamaa. Wanajiuliza, faida za kiuchumi wanazodai wenzao ndani ya muungano, wao wanafaidika na kitu gani.

Huwezi kuwa na muungano wa watu, huku wengine wakidai uchumi na upande mmoja ukililia undugu.
Huo utakuwa ni upuuzi wa kiwango kziuri tu.

Hivyo wanaotaka muungano wa uchumi ni wznz baada ya Watanganyika kukaa kimya, kuitwa wakoloni, waporaji na wezi wa rasilimali za znz. Watanganyika, wameona hakuna sababu za kuvunja muungano wa 'watu' kwa malalamiko ya wznz.

Njia rahisi yawepo mambo ya pamoja yanayotuwezesha kuishi kama jamii ya 'watu' unayosema.
Yale yasiyo na masilahi kwa upande wowote yawe ya washirika. Ndivyo Warioba na tume walivyoona.

Bila kuchukua hatua za lazima za kuweka sawa uweiano wa uchumi, huu muungano utakufa soon.
Watanganyika waliobeba muungano wamechoka na malalamiko yasiyoisha. Watanganyika wanatumia muda mwingi kujadili namna ya kusihi na wznz badala ya kujadili matatizo yao mengi waliyo nayo. Hili lifike mwisho, wznz wana hiari ya kubaki au kuondoka.

Wznz hawana haki ya kudai aina ya muungano wanaotaka wao, au mambo ya muungano yawe yapi. Wana haki ya kujadiliana na Watanganyika si kuamuru nini wanataka. Hilo tu linawachefua Watanganyika, kwamba ni kwa faida gani hasa wanaamriwa hivyo

Nafuu si wznz kuchangia kodi zao, bali kupunguza utegemezi wa wznz kwa Tanganyika ikiwa ni pamoja na kupanda mbegu za ubora. Haiwezekani znz inayotoa mchango sifuri ipewe kipaumbele kuliko wanaochangia muungano. Hapo ndipo tunaona muungano kuvunjika kama glass.

Kuwalaumu Watanganyika wanaoamka ni makosa. Kw miaka 48 Watanganyika wamekubali kuishi kwa muungano wa watu. Sasa inatosha, inatosha kwasababu wznz wamefika hatua hawataki kufanya lolote zaidi ya kudai tu hata misaada tena kwa lazima. Watanganyika wanahitaji nafuu, mzigo ni mzito.
 
Sasa wewe unakuja namaswala ya Ethiopia na Eretria ambao waliungana lakini Ukabila ukawatenganisha, sijui Syria na Egypt sielewi unazihusishaje. Somalia na Ogaden wakati Ogaden ipo Ethiopia ilhali wakazi wake ni Wasomali bado huelewi kwamba muungano wa WATU huondosha ukabila na unaposhindwa kuondoa hilo lolote linaweza tokea. Maswala ya kiuchumi yapo EU kweli na unaweza kusoma mkataba (TREATY) Waloandaa toka mwaka 1958 kuundwa kwa jumuhiya hiyo na wakaja unda mwaka 1992. EU was Originally signed in Rome as the Treaty establishing the European Economic Community.Na ukija soma Artical of Union yetu hakuna mahala popote siasa wala Uchumi umehusishwa hata ktk functions zake (mambo 11) siasa na uchumi havikuwemo lakini wewe bado unalazimisha vilikuwemo, kuna haja gani mimi kuendelea kumfukuza kichaa!
Nimetoa mifano ya nchi hizo kukuonyesha kuwa tayari zilikuwa na muungano ya 'watu' na sababu za kuparaganyika ni uchumi.

Eritrea waliona wanakuwa marginalized na Ethiopia, kwa mfno mmoja tu. Ndivyo ilivyo kwa south Sudan.
Katika EU, kuna tatizo usiloliona sasa hivi. Muungano wa EU haukusema uchumi kwa upanda wake, lakini uskiusoma vema na kwa utulivu, maana nzima ilikuwa ni kuwa na nguvu ya kicuhumi dhidi ya emergening markets.
Ni kuwa na nguvu za kiuchumi kuchukua nafasi ya NATO ambayo imekuwa dominated na Marekani kiuchumi na kiusalama.

Uingereza imekataa pound sterling kuondolewa. Wajerumani kwasasa wanataka 'dochi' irudi.
Kuna suala la greece, Italy na Spain zinazotishia EU. Nchi kama Ujerumani ndiyo imekuwa ina bail out nchi zingine ambazo zipo katika EU lakini kiuchumi ni tatizo.

Kunaandaliwa kura ya maoni UK kuhusu hatima yao ndani ya EU. Kuna vurugu Ujerumani za kuwataka wajitoe.
Wafaransa wanawanyooshea vidole wengine kwa kuwa mzigo.

Ukiangalia yote hayo si kisiasa, au usalama. Ni uchumi unaoleta tabu.

Hivyo, inategemea umeseoma treaty yao ukiwa unaangalia nini.
Kama ni maandishi upo sahihi, kama ni maudhui na dhana nzima nakusishi urudi kusoma ukiwa umetulia.
 
MALALAMIKO NI YA ZNZ DHIDI YA MUUNGANO
NANI ANAWASEMEA WATANGANYIKA?

Kila mara tumesikia riwaya iliyopigwa photocopy ya Chenge ikinanadiwa kujibu mamalalamiko ya wazanzibar.
Inavyoelekea katiba haikuandikwa kwa ajili ya mambo ya kitaifa likiwemo suala la muungano.

Imeandikwa mahususi kujibu malalamiko ya waznz

Swali la haraka linalojitokeza ni hili, je malalamiko ya Watanganyika yanashughulikiwa na nani?
Jibu la swali hilo ni gumu kwasababu kilichopo ni malalamiko ya wznz dhidi ya muungano.

Muungano unaohusisha znz na hivyo Watanganyika wanavalishwa koti la muungano, huku wakiendelea kujitoa kama Watanzania.
Hapo ndipo mtego ulipo, kwamba ni malalamiko ya wznz dhidi ya muungano ni si Tanganyika.

Kiuhalisia na hata wakisisilizwa, wznz wanasema ni malalamiko dhidi ya Tanganyika.
Muungano wanauita Tanganyika ingawa wanauita Tanzania pale wanapotaka kunyoosha mkono na kuchota

Jambo wasilojua viongozi wetu au wanalopuuza ni uwepo wa washirika wa muungano.
Mbele ya safari Watanganyika watataka kuona kero zao zinaisha.

Kero za Watanganyika ni uzito walioubeba katika muungano wakiwa hawana sauti.
Hawana sauti kwasababu wamefungwa midomo na jina Tanzania

Utamaduni wa kufanya mambo kwa mazoea ni mbaya sana.
Kwa mfano, tumeuliza asilimia 4.5 wanayopata wznz inatoka wapi na inahusu nini. Hakuna jibu.

Tunauliza nani alipewa nguvu ya kisheria ya kuongeza 4.5% hadi 7% ? Hakuna jibu.
Ni utaratibu gani umetumika kufikia kiwango husika ?Hakuna jibu.

Watanganyika watajiuliza, ile 21% ya ajira imekokotolewa kutokana na sheria gani, kanuni zipi zimetumika.
Hapa si suala la ajira tu, bali ni suala kubwa zaidi.

Kwamba, 21% ndiyo inayotumiwa kupata 1.75Bilioni kwenda znz kila mwezi.
Watanganyika watajiuliza kwanini waadhibiwe kwa nafasi ambazo nyingi hazihusiani na muungano

Watanganyika watajiuliza, kwanini wawajibike kwa taasisi zilizoanzishwa kwa sheria ya znz katika kuhudumia?

Kwa mfano, kwanini Tanganyika iwe accountable kwa makosa yanyofanywa na Zanzibar maritime kwa kusajili na kuchukua pesa za nje. Kwanini image ya Tanganyika iharibike kwa kitu kisishcowasadia wao.

Na hilo la kuwasikiliza wao ndilo limetoa nguvu isiyojulikana wznz wanaipata wapi!!
Aghalabu utawasikia, tunataka muundo kadhaa wa muungano
Tunataka mambo kadhaa yawe ya muungano, na kadhaa yasiwe

Nguvu hiyo inatokana na ukweli, katika muungano wao wapo kama nchi, Mtanganyika hajulikana nafasi yake.

Ni aina hiyo ya znz dhidi ya muungano ndiyo inaondoa haki ya Watanganyika katika muungano.
La kujiuliza, haki ya kumua aina na mambo ya muungano, znz wamepewa na nani na kwa gharama gani katika huu muungano?

Orodha ni ndefu, na kwa mifano kama hii, ipo siku Watanganyika watasema ‘enough is enough' na hapo ndipo kifo cha ghafla cha muungano kitakapotokea.

Kikitokea kifo hicho, hakuna njia tena ya kuaminiana au kuwa na mahusiano mengine.

Tayari msingi wa chuki utakuwa umejijenga, kwamba kila mtu kivyake.

Hilo litatokea kwasababu Watanganyika watajihisi si sehemu ya muungano, hawasikilizwi na kwamba muungano ni kwa ajili ya kuwafariji wznz kama viongozi wanavyodai sasa hivi.

Tusemezane
 
Mchambuzi,Sababu ulizobainisha za kushindwa kuanzishwa kwa JFC ni sababu za kitoto sana na hazina mashiko hata moja

Sasa katika kaanun za fedhwa tunajiuliza.
1. Je Znz achangie katika mfuko gani pesa zake za muungano? Je Tgk anachangia katika mfuko gani pesa za muungano?
2. Je Znz au Tgk kila nchi inatakiwa ichangie kiasi gani katika muungano?
3. Je nani atakuwa mdhibiti mkuu wa mapato na matumizi ya fedhwa hizo zikijumuishwa na mikopo na misaada?.

Jibu la masuala hayo hapo juu ambayo ndio yanayoleta mtafaruku mkubwa sana wa kutoaminiana, kutuhumiana na kulalamikiana solution yake ni kuundwa kwa Joint Finance Commission (JFC)

Suala lipo pale pale JMTz inapata wapi kiburi cha kutotekeleza sharia hii iliyopitishwa na Bunge? wanakhofia nini kutekeleza sharia hii ya kuanzishwa JFC?
Kwa kukusaidia, Suala la TRA nimelijibu vilivyo kabisa. Nimesema hivi TRA inakusanya kodi zote za JMTZ na makusanyo hayo yanawakilishwa katika wizara ya fedhwa Muungano.

ZRB inakusanya mapato yote ya Znz na makusanyo hayo yanapelekwa hazina Znz.

Kwa nyongeza zaidi pesa wanazokusanya TRA zitaonekana katika bajeti ya muungano wa JMTz na pesa wanazokusanya ZRB zitaonekana katika bajeti ya nchi ya Znz.


Kwa kukusaidia zaidi mfumo wanaotumia TRA na ZRB katika kukusanya mapato katika Znz ni sawa kabisa na mfumo unaotumiwa na Halmashauri za JMT


Kwa jibu fupi pesa inayokusanywa na TRA znz inapelekwa hazina JMTz na kwa mwaka 2014/2015 TRA wanakusudia kukusanya Mapato ya kodi Tsh 11,318,222/= kwa mujibu wa makadirio ya bajeti ya 2014/15.
!!!! ???
Kwa muungwana kama kitu hafahamu basi anasema bayana SINA Ujuzi nalo hilo.
Thank you
 


ZNZIWAJIBIKE KWA MAMBO YANAYOIHUSU

KUPUNGUZAMZIGO SI KUCHANGIA TU, NI KUJIHUDUMIA


Tumeona mambo yasiyo na majibu kama gharama za kuendesha muungano,adhabu wanazopewa Watanganyika kulipia waafanyakazi wa muungano, asilimia 7 isiyo na maelezo, na gharama za taasisi zisizo na kanuni

Kwa ufupi,mambo yanayotatiza ni mengi na hakuna anayetueleza kwa kina mambo hayoyamefikiwaje, na akina nani kwa sheria na kanuni ganui.

Ipo hoja yaMkandara kuwa znz haiwezi kuchangia muungano. Kama hoja yake ni kweli, basi haina sababu za kudai muungano wa usawa na haki. Vitu hivyo huambatana nakuwajibika.

Endapo znz haiwezi kuwajibika, wapi inapata nguvu za kudai haki na usawa?
Wapi inapata nguvu za kuamua aina ya muungano?
Wapi inapata nguvu zakupanga nini kiwe katika muungano na nini kiondolewe?


Watanganyika kipato chao ni kidogo ukilinganisha na znz kama alivyosema Mchambuzikwa namba.
Lakini bado Watanganyika wamebeba asilimia 100 ya muungano.

Hapa nilazima znz iwajibike kwa kutoa sehemu ya mapato yake kuhudumia muungano.
Mfano,kama Tanganyika itatoa asilimia 40 ya pato lake, znz itoe kiasi hicho cha pato lake.


Ni ajabu kusikia wznz wakidai nafasi katika muungano bila kujua zinagharamiwa vipi na kwa gharama ya nani.

Kwavile hawawajibiki katika muungano, uchungu na thamaniya muungano hawaioni. Ndio chanzo cha kutukana kila mara!


Tunaposema znz wachangie, tuna maana nyingi. Moja ikiwa ni znz kupunguza gharama za utegemezi

Mfano, znz ihudumiwe wabunge wake wanaokuja Dodoma kwa ajili ya znz.

Znz ilipe misharaha wafanyakazi wake wa muungano na ichukue kodi za wafanyakazi hao.

Znz ipewe taasis ihudumie kwa mapato yao.Mfano, wznz wanaoingia katika taasisi za muungano zikiwemo bodi za mashirika,walipwe na SMZ


Znz ichukue jukumu kla kuelelimisha watu wake kwa kutumia chombo chao cha ZHESLB.

Na znz ilipie mashirika yake yaliyojiondoa
katika muungano kwa ada zake


Kwa kufanyahivyo, si kuwa itachangia muungano, bali pia itawajibika na kupunguza mzigo kwaTanganyika.

Na hapo znz itaweza kusimama na kudai usawa wa muungano japo kwa kuvumiliana.

Kwa hali ya sasa ya utegemezi wa asilimia 100,Watanganyika wanapaswa kujiuliza, mzigo huo wataubeba hadi lini na kwa masilahi gani.


Tusemezane
 
!!!! ??? Thank you

Nguruvi3,

Siku zote ukitaka kumNUKUU 'quote' mtu chukua mada nzima na colour pale kwenye au unapoona kuna mash'kira lakin SIO hicho unachofanya cha kukata baadhwi ya maneno na kugeuza mengine.

Hiyo ni dalili ya KUFILISIKA KIMANTIKI.

Kuwa MUWAZI KAMA UNA suala lolote lile una mush'kira nalo uliza mchana kweupeeee nitakupa BAYANA ZAKE na sio kujificha nyuma ya PAZIA.

Kumbuka Nia na kusudi ya Barza hii ni KUPASHANA HABARI, KUILIMISHANA na wakti mwingine KUBURUDISHANA.

Sasa kama una suala basi Bismillah ULIZA tutakusaidia kuliko kujibanza na kunung'unika pekee hakukusaidii. Hapa tukupa ILMU ya bureeeee kabisaaaaa.

Karibu.



 
ZNZ INAWEZAJE NJE, ISHINDWE YA NDANI?

Znz wanadai wapewe haki ya kushiriki katika shughuli zakikanda, kimataifa kama nchi nje ya JMT.

Huko ni maeneo kama EAC, SADC na taasisi nyingine ambazo huhitaji uratibu pamoja na ada ya ushiriki


Kwa maneno mengine znz ipo tayari kujiharamia katika jumuiya kama EAC, SADC n.k.

Ushiriki katika maeneo hayo una gharama za unedeshaji. Hivyo ndivyo riwaya ya Chenge inavyosema.

Riwaya haikuanisha kama znz itajihudumia au itadhaminiwa na JMT kama inavyodhaminiwa katika mikopo


Znz itakuwa na haki ya kudai udhamini wa JMT kama sehemu yaJMT.

Ndivyo ilivyo na haki ya kukusanya kodi zake au kukopa kutoka eneo jingine na mwisho kuzipitisha gharama hizo kwa Mtanganyika kwa jina la JMT


JMT itajikuta ikibeba mzigo mwingine wa kuhudumia znz katika ushiriki wa mambo ya nje au kudhamini znz ili iweze kupewa haki katika mashirika na taasisi za kikanda.

Ndivyo inavyosemwa kuwa , pale znz itakapohitaji udhamini basi JMT itabeba mzigo


JMT ni Tanganyika, na hapo Watanganyika wawe tayari kubeba mzigo mwingine.

Jambo Watanganyika wanapaswa kujiuliza, kama znz inaweza kushiriki katika taasisi za kimataifa na mashirika hayo, vipi znz ishindwe kuhudumia sehemu ya wawakilishi wake katika JMT. Kwanini znz isilipe gharama zawabunge wao?


Kwanini znz hiyo yenye kupewa uwezo huo, isiweze kulipia wafanyakazi wa zanz ndani ya JMT?

Na mwisho, ni kujiuliza,je znz inaweza kusimama pamoja naTanganyika katika kutetea masilahi yake huko katika taasisi na mashirika ya nje. Tumeona mfano, waliposikia kuna mafuta na gesi wamekimbia kuondoa katikamambo ya muungano.

Je, pale patakapokuwa na masilahi ambayo znz inaona yana manufaa kwao wataweza kusimama pamoja na Tanganyika
dhidi ya wapinzani?


Tunaweza kuona kuwa unapoipa znz madaraka bila uwepo waTananyika, ni kuihujumu Tanganyika kwa jina la Tanzania.

Vipi znz iweze kujisimamia nje, ishindwe kuchangia au kutoa msaada ndani ya muungano.


Znz inasimama vipi yenyewe kimataifa, ikiwa bado ni mzigo katika muungano?

Tusemezane
 
Nguruvi3, Haya ni maelezo tuloanza nayo ktk malumbano ya kuwepo Muungano na kila mmoja wetu kajieleza hivi. Sasa wewe soma yote halafu nambie nani kasema Muungano wetu ulikuwa wa WATU. Nasisitiza tu ya kwamba, haya ya Muungano wa Kisiasa na Kiuchumi ni ya kimwongozo wa mfumo utakao tutumika kujenga nchi.
Tuliandika hivi:-

Mkandara
:- mkuu niliyasema haya nitarudia tena kuyasema ya kwamba mnatafuta sababu za kisiasa na kiuchumi zaidi kuzungumzia Muungano wetu ilihali tayari imeshaelezwa kwamba muungano wetu ni wa WATU na kwa vile ardhi ni eneo la watu hao wanamoishi ndio maana tumekuwa na nchi mbili. Sababu hizi zimeelezwa katika vitabu kibao lakini nyie hamtaki isipokuwa mnachotaka wenyewe.

Mchambuzi
:-
Muungano uliopo ni muungano wa KISIASA, sio muungano wa KIUCHUMI. Mfumo wa Muungano wa sasa unaichukulia Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sio moja ya nchizi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala la uchumi halipo katika masuala ya muungano.

Nguruvi3
:- M
uungano wa watu unaweza kuwepo bila kuwa serikali. Zanzibar na Tanganyika zilikuwa na mahusiano miaka dahari. Kilichosababisha muungano ni sababu za kiuchumi na kisiasa. Otherwise tunaweza kuishi bila muungano na watu wakawemo katika ardhi husika bila matatizo.

Kama sababu ya Muungano ingelikuwa ni siasa mbona chama cha TANU na ASP walikuja ungana mwaka 1977, miaka 13 baada ya muungano, badala ya siku ile ile a muungano? na kama ilikuwa ni za kisiasa na kiuchumi mbona Katiba ya kudumu ilikuja kuandikwa pia mwaka 1977 badala ya 1964 - Maana katiba na muundo wa vyama ndio mwongozo wa nchi kisiasa na kiuchumi. Muungano wa EU ni wa kiuchumi from the start, to the end ndio watafikiria kuuunganisha watu!

Bado hamkubali Karagabaho!
 
Nguruvi3, Haya ni maelezo tuloanza nayo ktk malumbano ya kuwepo Muungano na kila mmoja wetu kajieleza hivi. Sasa wewe soma yote halafu nambie nani kasema Muungano wetu ulikuwa wa WATU. Nasisitiza tu ya kwamba, haya ya Muungano wa Kisiasa na Kiuchumi ni ya kimwongozo wa mfumo utakao tutumika kujenga nchi.
Tuliandika hivi:-

Mkandara
:- mkuu niliyasema haya nitarudia tena kuyasema ya kwamba mnatafuta sababu za kisiasa na kiuchumi zaidi kuzungumzia Muungano wetu ilihali tayari imeshaelezwa kwamba muungano wetu ni wa WATU na kwa vile ardhi ni eneo la watu hao wanamoishi ndio maana tumekuwa na nchi mbili. Sababu hizi zimeelezwa katika vitabu kibao lakini nyie hamtaki isipokuwa mnachotaka wenyewe.

Mchambuzi
:-
Muungano uliopo ni muungano wa KISIASA, sio muungano wa KIUCHUMI. Mfumo wa Muungano wa sasa unaichukulia Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sio moja ya nchizi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala la uchumi halipo katika masuala ya muungano.

Nguruvi3
:- M
uungano wa watu unaweza kuwepo bila kuwa serikali. Zanzibar na Tanganyika zilikuwa na mahusiano miaka dahari. Kilichosababisha muungano ni sababu za kiuchumi na kisiasa. Otherwise tunaweza kuishi bila muungano na watu wakawemo katika ardhi husika bila matatizo.

Kama sababu ya Muungano ingelikuwa ni siasa mbona chama cha TANU na ASP walikuja ungana mwaka 1977, miaka 13 baada ya muungano, badala ya siku ile ile a muungano? na kama ilikuwa ni za kisiasa na kiuchumi mbona Katiba ya kudumu ilikuja kuandikwa pia mwaka 1977 badala ya 1964 - Maana katiba na muundo wa vyama ndio mwongozo wa nchi kisiasa na kiuchumi. Muungano wa EU ni wa kiuchumi from the start, to the end ndio watafikiria kuuunganisha watu!

Bado hamkubali Karagabaho!
Mkandara , nimekuuliza huko nyuma, kwani malalamiko ya wazanzibar ni kuhusu nini ?
Hujajibu

Nikupe dondoo pengine unaweza kutuongoza katika hili

1. ZNZ wanataka mamlaka kamili ili
  • Waweze kujikombo kiuchumi kwa maneno yao
  • Wawe na udhibiti wa uchumi wao
  • Waondokane na kunyonywa kicuhumi na Watanganyika
  • Wawe na uwezo wa kushiriki uchumi wa dunia
-Wapewe fursa sawa za uchumi katika muungano

Hayo yote ndiyo yanapeleka yafuatayo
-Kudai 4.5% iongezwe na sasa 7% (Ni uchumi)
- Kudai kodi za wafanyakazi wa muungano wapewe(Uchumi)
-Kukwepa kulipia ada na huduma za muungano kwa mapato yao(Uchumi)
-Kudai misaada na mikopo (Uchumi)
- Kusukuma gharama za kuendesha muungano kwa Watanganyika(uchumi)
-Kutaka kodi za bidhaa zao ziondolewe zikiingia Tanganyika(uchumi)
-Kudai nafasi za ajira zisizo wahusu (uchumi)

2. Tueleze kama wnz wana malalamiko yoyote ya kisiasa

3. Tueleze kama wazanzibar wamebaguliwa kama watu katika JMT. Ingawa wao ni wabaguzi wakubwa wakitekeleza sera hiyo chafu dhidi ya Mtanganyika kuliko raia mwingine wa eneo la ukanda huu
 
Mkandara , nimekuuliza huko nyuma, kwani malalamiko ya waznz ni kuhusu nini ?
Hujajibu

Nikupe dondoo pengine unaweza kutuongoza katika hili

1. ZNZ wanataka mamlaka kamili ili
- Waweze kujikombo kiuchumi kwa maneno yao
- Wawe na udhibiti wa uchumi wao
- Waondokane na kunyonywa kicuhumi na Watanganyika
- Wawe na uwezo wa kushiriki uchumi wa dunia
-Wapewe fursa sawa za uchumi katika muungano

Hayo yote ndiyo yanapeleka yafuatayo
-Kudai 4.5% iongezwe na sasa 7% (Ni uchumi)
- Kudai kodi za wafanyakazi wa muungano wapewe(Uchumi)
-Kukwepa kulipia ada na huduma za muungano kwa mapato yao(Uchumi)
-Kudai misaada na mikopo (Uchumi)
- Kusukuma gharama za kuendesha muungano kwa Watanganyika(uchumi)
-Kutaka kodi za bidhaa zao ziondolewe zikiingia Tanganyika(uchumi)
-Kudai nafasi za ajira zisizo wahusu (uchumi)

2. Tueleze kama wnz wana malalamiko yoyote ya kisiasa

3. Tueleze kama wznz wamebaguliwa kama watu katika JMT. Ingawa wao ni wabaguzi wakubwa wakitekeleza sera hiyo chafu dhidi ya Mtanganyika kuliko raia mwingine wa eneo la ukanda huu
Umeniuliza kuhusu zanzibar wanataka nini na sikukujibu wa sababu majibu huyaweka wewe mwenyewe sasa mimi nijibu kipi?

Pili sababu za Wazanzibar kudai hazihusiani na kuundwa kwa Muungano isipokuwa ni matukio ndani ya Muungano, na ndio sababu nikakupa mfano wa ndoa - wewe kama mume na mkeo. Hamkuona kwa sababu ya kiuchumi japo inaweza tokea mikwaruzo na kero ndoa yenu ikavunjika kwa sababu za kiuchumi. Ama mkeo anaweza kudai una mu abuse! haina maana ndio chimbuko la ndoa. Hivyo kuhusisha ndoa na Uchumi ama tukio lolote lile ndani ya ndoa kuwa ndio chanzo cha kufunga ndoa hili ndilo nalopinga miye na kusema ni mahusiano baina yenu wawili ndio yalifikia maamuzi ya ndoa

Twende mbele, umesema madai ya Wazanzibar ni:-
1.ZNZ wanataka mamlaka kamili ili
- Waweze kujikombo kiuchumi kwa maneno yao
- Wawe na udhibiti wa uchumi wao
- Waondokane na kunyonywa kicuhumi na Watanganyika
- Wawe na uwezo wa kushiriki uchumi wa dunia
-Wapewe fursa sawa za uchumi katika muungano

Sasa wewe umeisha orodhesha haya, inakuwaje unaniuliza mimi tena maswali ya Kisiasa wakati nimesha kwambia kuwa Siasa haihusiki na kuundwa kwa Muungano? Ama unataka kunivuta katika imani yako badala ya kuzungumzia nilichosema mimi? Na hata hivyo, kuhusu Siasa, hivi kweli hujasoma madai ya Zanzibar kisiasa wakitaka mamlaka zaidi ndani ya Muungano? Cheo cha makamu wa rais itambuliwe pia kuwa ni rais wa Zanzibar? Hujasikia wakilalamika kuhusu nafasi zao ktk uwakilishi wa balozi wetu nje, Hujasikia kuhusu kutomtambua waziri mkuu wetu na kadhalika! Wenye asili ya bara kutogombea uongozi Zanzibar ilihali wao (Wazanzibara) wanagombea bara toka udiwani, wenyeviti wa serikali za mitaa hadi ubunge?

Kwa nini tuendelee na ubishi ktk mambo ambayo yapo wazi na yamekuja tokea ndani ya Muungano? na sio kweli jmimi nawapa support kwa kila madai yao. Halafu unauliza Wazanzibar wanabaguliwa vipi? ilihali wewe mwenyewe umeorodhesha madai yao (kiuchumi) sasa yatazame wewe madai hayo kisha wape majibu wao na sii kuniuliza mimi maana mimi sii Mzanzibar aloweka madai uloorodhesha ila naufahamu muundo wa serikali mbili una manufaa yapi na mapungufu gani ambayo kati yake ndimo kuna utata.

Mwisho kuhusu Tanganyika, mimi nadhani sisi bara tungejifunza toka Uingereza (England) wao wamewezaje kulitumia jina la Uingereza ndani ya serikali mbili. Binafsi sioni umuhimu wa kuwa na Tanganyika kama jina badala ya Tanzania au Bara, kwa sababu jina ni jina tu. Hata wakazi wa Kagera hujitambulisha kama wanatoka Bukoba kuliko kulitaja jina la Kagera toka zamani ikiitwa mkoa wa ziwa magharibi. Bukoba imechukua nafasi kubwa ya kujitambulisha wao kuliko Kagera ama Ziwa magharibi na haipotezi maana yoyote wala hawapungukiwi na lolote. Wachagga na Moshi hata atoke kona gani, hii Kilimanjaro ipo tu kimandishi.

Maasalaam.
 
Hivi kweli hujasoma madai ya Zanzibar kisiasa wakitaka mamlaka zaidi ndani ya Muungano?

Cheo cha makamu wa rais itambuliwe pia kuwa ni rais wa Zanzibar?

Hujasikia wakilalamika kuhusu nafasi zao ktk uwakilishi wa balozi wetu nje,

Hujasikia kuhusu kutomtambua waziri mkuu wetu na kadhalika! Wenye asili ya bara kutogombea uongozi Zanzibar ilihali wao (Wazanzibara) wanagombea bara toka udiwani, wenyeviti wa serikali za mitaa hadi ubunge?

Na sio kweli jmimi nawapa support kwa kila madai yao.

Halafu unauliza Wazanzibar wanabaguliwa vipi? ilihali wewe mwenyewe umeorodhesha madai yao (kiuchumi) sasa yatazame wewe madai hayo kisha wape majibu wao na sii kuniuliza mimi maana mimi sii Mzanzibar aloweka madai uloorodhesha ila naufahamu muundo wa serikali mbili una manufaa yapi na mapungufu gani ambayo kati yake ndimo kuna utata.

Mwisho kuhusu Tanganyika, mimi nadhani sisi bara tungejifunza toka Uingereza (England) wao wamewezaje kulitumia jina la Uingereza ndani ya serikali mbili. Binafsi sioni umuhimu wa kuwa na Tanganyika kama jina badala ya Tanzania au Bara, kwa sababu jina ni jina tu. Hata wakazi wa Kagera hujitambulisha kama wanatoka Bukoba kuliko kulitaja jina la Kagera toka zamani ikiitwa mkoa wa ziwa magharibi. Bukoba imechukua nafasi kubwa ya kujitambulisha wao kuliko Kagera ama Ziwa magharibi na haipotezi maana yoyote wala hawapungukiwi na lolote. Wachagga na Moshi hata atoke kona gani, hii Kilimanjaro ipo tu kimandishi.Maasalaam.
Nianze na aya ya mwisho kuhusu Uingereza. Napenda kukutaarifu kuwa Uingereza haijatumia jina la muungano wao. Nafahamu watu wengi wanachanganya hili jambo kwasababu ya lugha ya kiswahili inayotambua Uingereza kama Great Britain.

Kwa lugha yetu ya kiswahili, hatujaweza kutofautisha kati ya England, Great Britain na United Kingdom. Zote tunaita Uingereza kwa ujumla wake. Kwa mantiki hiyo, Uingereza siyo England kwa kiswahili ni jumuisho la yote.

Hata kibubusa busa tukikubaliana nawe, bado kuna hoja inayorindima kuhusu England ambayo kwa mfumo wa sasa inaonekana kufanana na Tanzania bara. England wanadai kutambuliwa zaidi na kupewa mamlaka kama washiriki wao wa Scotland, Wales na Ireland. Kura ya maoni ya Scot imefungua ukurasa mpya, nadhani unalielewa hilo.

Pili, madai ya wznz kuhusu nafasi za ubalozi si ya kisiasa ni ya kutaka ajira.

Balozi hufanya kazi kwa niaba ya nchi. Awe Mtanganyika au mzanzibar waote wataongozwa na miongozo ya nchi na si maeneo wanayotoka. Hoja ya mabalozi ni sehemu ya kujazia madai ya wznz mengine yakiwa hayana maana

Hivi balozi akiwa mznz inasaidia nini. Balozi akiwa Mbondei inasaidiaje.
Hili ni jambo la hatari na kipuuzi kwasababu ipo siku wasukuma watadai wapewe nafasi za ubalozi.
Kwa taarifa yako, wasukuma peke yao wakiamua wanaweza kumchagua rais wa JMT seuse watu laki 5 wa znz!

Nchi haihitaji mabalozi wa kujenga matabaka. Na zaidi ya hapo mabalozi na balozi hizo znz na SMZ haina mchango wa aina yoyote. Hatutengenezi balozi za kuajiri wznz.

Tayari wana 21% ya ajira zisizo wahusu na wanalipwa Bilioni 1.75 kwa mwezi kama adhabu ya kuwajiri wznz nchini Tanganyika. Nafasi za ubalozi ni chache (30)ulkilinganisha na nyingi tu wanazopata zisizowahusu.
Hivyo hoja ya ubalozi ni ya kitoto,nashangaa wapo wznz wenye elimu wanaozungumzia hili

Tatu, madai ya PM kutotambuliwa znz si ya wznz. Ni Watanganyika wanahoji huyu waziri mkuu wa Tanzania kwanini hawezi kufanya kazi znz hadi apate kibali cha uzanzibar ukaazi.

Na waziri mkuu huyo huyo wasiyemtambua ndiye mwajiri wa wznz katika halmashauri na taasisi nyingine zilizo chini yake.
Mbona wznz hawakatai hilo.

Cheo cha umakamu wa Rais nalo ni dai la kipuuzi. Rais wa znz anapokuwa makamu wa Rais, tayari anaondolewa nguvu yake kama Rais. Huyu atakuwa ni kiongozi wa muungano ambaye ni balozi tu kule znz.

Ndivyo Jumbe alivyofanywa, alipOkwenda kinyume na matakwa ya Dodoma aliitwa na kuwekwa pembeni.
Hivyo kudai nafasi hiyo ni upeo finyu wa kuona matatizo mbeleni.
Ni hao hao wanadai mamlaka kamili, mamlaka kamili yanaywezekanaje ikiwa Rais wa znz anaripoti Dodoma?

Lakini pia upuuzi wa hoja ya makamu wa rais Unakuja na malalamiko ya wznz ya kupata nafasi za kujiunga na taasisi za kimataifa. Kwamfano, makamu wa Rais akiwa Rais wa znz na znz ikawa mwanachama wa SADC, Rais wa JMT hayupo, Rais wa znz atakwenda kwa niaba ya Tanganyika, halafu nchi yake anayosimamia itawakilishwa na Rais huyo huyo.

Hapo kutakuwa na conflict of interest na lazima aatakubaliana na Tanganyika kwasababu za nguvu zake.
Nani ana lose kama si wznz. Na huo ndio msingi wa kusema hoja hiyo hawajaingalia, ni ya kipuuzi kwa upande wao.
Wana shoot miguu yao wenyewe.

Nne, kuhusu madai yao, tumeonyesha kila dai na siku hizi husikii tena wznz wakiongelea hilo.
Znz kama nchi na vyombo vyao sasa ni wakati wahudumie watu wao ndani ya muungano.

Wachukue dhamana ya kusomesha watoto wao, walipe mishahara wafanyakazi, wasipewe pesa zisizo na audit kama Bilioni 1.75 ambayo haijulikani imepatikana kwa utaratibu gani, wasipewe 7% ya mikopo na misaada bali waende kukopa na kupata misaada yao, wasidai 21 ya ajira kwasababu haziwahusu na hata wasipokuwepo nafasi hizo zitajazwa na Watanganyika, wasilete watu wa kulala pale Dodoma kwa jina la wabunge. Kama wanawaleta walipie gharama zao

Na kubwa zaidi lazima wawajibike katika muungano.
Muda wa free ride umekwisha, Tanganyika haihitaji kuvaa koti la muungano lililojaa adha kutokana na kunguni mmoja.

Kunguni haondoki hadi pale koti jipya la Tanganyika litakaposhonwa
 
Nguruvi3,
Mkuu ndio maana nasema kuendelea kulumbana na wewe ni sawa na kumfukuza kichaa nikiwa uchi. Mimi nimeandika hivi, sisi bara tujifunze hao Uingereza wamewezaje wao kutumia jina lao ktk muundo wa serikali 2?. Sikusema Uingereza wanatumia jina la Muungano na hakuna mahala mtu hata mmoja alojichanganya kati ya Uingereza na Great Britain. Huu ni ukumbi wa great thinker na sidhani kuna mtu haelewi hilo. swala ama hoja yangu ni;- Uingereza (yenye mamlaka ya shughuli za serikali 2 kama bara) wamewezaje kutumia jina la nchi yao ktk muundo wa serikali 2 - kigumu kipi hapo?..

Kama unakumbua enzi ya mwalimu Sisi tulituma jna la Tanzania bara, tukawa na timu zetu za Mpira, riadha na kadhalika hii ikatupa kufahamika duniani kama Tanzania bara.Uingereza vile vile wameendelea kutumia jina lao japo wapo ktk serikali 2 kwa hiyo madai ya Tanganyika ni jukumu letu ssi wala sio Wazanzibar kuliendeleza na wala sii lazima tuwe na serikali 3 kwa sababu Uingereza wameweza.

Haya unaposema madai ya Wazanzibar kuhusu balozi sio ya kisiasa ila wanataka ajira. Mkuu balozi huteuliwa na rais wa chama kilichopo madarakani ambaye ni mwakilishi wa chama tawala. sawa na RC au DC hawa wote ni wateule wa rais toka chama tawala na hivyo ukiyatazama madai mengi ya Wazanzibar yanatoka vyama vya upinzani kina Jussa ambao wewe unakubaliana nao ktk mengi ila unakuwa kigeugeu pale unapotazama maslahi ya Tanganyika.

Mara sasa umeanza kusema kuna madai ya kipuuzi, kumbe unaelewa kuna madai mengine zaidi ya hayo ya Kiuchumi eeeh!..sasa kwa nini muungano wetu usitokane na madai hayo ya kipuuzi ila Kichumi!.Je, Mchambuzi naye kudai muungano ni wa kisiasa pia hajui kwa sababu wewe huoni sababu zake za kisiasa!. Mkuu unaona taabu gani kusoma na kuelewa mwenzako anapotoa hoja! unakurupuka na majibu yanayokwepa ukweli ili mradi tu ubishane..

Unachosha sana mkuu kwakheri
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara , usiwachanganye wasomaji. Na kwa hilo la kuchanganya watu hakika wewe ni mzuri sana.

1. Hatuwajawahi kufahamika duniani kama Tanzania bara.
Hata tulipokuwa na timu za michezo, hakuna mahali tuliwahi kujulikana kama Tanzania bara. Tumejulikana kama Tanzania.

2. Unpoasema Uingereza inawezaje kutumia mfumo wa S2, hapa napo unachapia chapia
Mfumo wao ni tofauti na huu wa S2 za Tanzania. Hata CCM watanitetea kwani wao husema muungano wetu ni wa kipekee duniani.
Na hakika ni wa kipekee maana Uingereza unakosema, Malkia ndiye mwenye jeshi, Union jack, na God save the queen.

Hapa kwetu tuna maamiri jeshi wakuu wawili, mdogo anayeishi znz na mkubwa anayeishi magogoni.
Tuna bendera za Tanzania na Zanzibar, na tuna wimbo wa Tanzania na znz.
Hadi hapo huwezi kulinganisha apple na avocado. Huu muungano wetu ni wa kipekee

3. Unaposema tuige mfano wa Uingerezam, ni bahati mbaya upo nyuma ya wakati kidogo.
Baada ya kura ya Scotland, Waingereza ambao ni Engalnd sasa wanadai nao wapewe mamlaka kama washirika.

David Cameron atanitetea kwa hoja yake siku ya referendum.
Sasa unataka tuige kile wenzetu wanachobadili, huoni copy and paste ni tatizo Mkuu wangu!!!

4, Kuhusu Balozi, ni suala la ajira tu kwa wznz. Hakuna hoja yoyote ya maana wanayoijenga kwa kuwa na mabalozi wznz.

Tunafahamu mabalozi huchaguliwa na kufanya kazi zao kwa miongozo.
Ni wateuliwa wa Rais kama walivyo wakuu wa mikoa, lakini masharti ya kazi zao hayahusiani na shughuli za kisiasa isipokuwa tu kwa mablozi wapuuzi wa nchi kama zetu. Hatuelewi endapo mabalozi ni wznz hiyo kisiasa ina play vipi labda ututanabaishie

Nikupe kionjo kidogo cha upuuzi wa mabalozi. Hawa hawazidi 40 kwasasa.

Kama znz wanataka kulifanya hilo la kisiasa, mbona hawaangalii maelfu ya wznz waliojazana halmshauri na taasisi zisizo za muungano. Lakini pia hao mabalozi hawaishi kwa solar energy, wanahudumiwa.

SMZ na znz kwa ujumla hazina mchango katika muungano, vipi waone mabalozi ni haki yao, lakini huduma za mbalozi hao si tatizo lao. Hapa ni ajira tu, na si vema shughuli nyeti kama za kibalozi kufanywa shamba la ajira kwa wznz

5. Tumewahi kusema kuwa muungano kwa siku za nyuma uliongozwa na siasa.
Zama za sasa uchumi una nguvu zaidi kuliko siasa. Na muungano huangaliwa katika mukatadha huo.

Ni kwa jicho la uchumi ndio maana madai ya wznz si kukosa tabasamu au bashasha kutoka Tanganyika, bali ni kupewa zaidi kutoka Tanganyika. Hakuna dai la znz lisilo na masilahi kiuchumi. Nitajie moja nikueleze

Ni kwa msingi wa jicho la uchumi, Tanganyika wanasema, wao kama nchi masikini wana matatizo na wajibu kwa watu wao.

Haiwezekani sehemu ya watu laki 5 ambao laki 5 nyingine wanaishi Tanganyika, ipewe fadhila kuliko mkoa mmoja masikini sana Tanzania. Hakuna sababu za Tanganyika kubeba mzigo wa SMZ.

Kwa mfano, katika mapesa yanayokwenda znz, zipo zinaohudumia utitiri wa makamu wa Rais.

Hilo la makamu wa Rais wa znz ni matatizo yao, ni dhambi kumbebesha mlipa kodi wa mlimba, Utete au Ngujini mzigo wa kuhudumia makamu 2 wa Rais wa znz wanaopataikana kwa matatizo yao. Hata katiba ya JMT haiwatambui leo kwanini tuhwahudumie?

SMZ ina katiba na vyombo vyake, leo wanaleta watu Dodoma kwa ajili ya nchi yao gharama anazibeba mkazi wa Mbagala rangi tatu, Buguruni kwa mnyamani na Tangi bovu. Insane!
Wabunge wa znz wahudumie na SMZ.Taasisi za znz kama ZMO ihudumie na SMZ

Kinachouma sana ni pale wznz waliokaa kikao cha wznz kwa jina la muungano, wakapjipangia 21% ya ajira, halafu wakaweka adhabu kwa Mtanganyika kuwa lazima alipe Bilioni 1.75 kwa mwezi kwa kumwajiri mznz katika halmashauri au taasisi isiyo na muungano.
Hili lazima likomeshwe na Watanganyika waamke sasa, wasisubiri.

Kwa hesabu rahisi kama tuna mikoa 30, ina maana ili tuweze kupeleka znz Bilioni 1.75 kwa mwezi, kila mkoa lazima uchangie takribani milioni 50 kwa mwezi kutoka katika mapato yake.

Kwamba, Watanganyika wanaadhibiwa kwa kutoa ajira kwa wznz.

Ni halmashauri gani ya Tanganyika inayopata milioni 50 kwa mwezi kama ruzuku.
 
Last edited by a moderator:
MAMBOYA MUUNGANO YANAPOFICHWA

KATIBA YA CHENGE NI KUMTWISHA MTANGANYIKAMZIGO ZAIDI

mambo mengi ya muungano haya nutaratibu wala kanuni, na ni mzigo mzito anaoubeba Mtanganyika anapolala na kuamka. Mtanganyika amebeba SMZ na muungano kwa ujumlawake

Usiri wa mamboya muungano ni chanzo cha Tanganyika kuumia.Kwa mfano, uendeshaji wa JMT na ruzuku kwa SMZnijukumulaTanganyika, wznz wakitumia jina la Tanzaniakama liability na sio asset

Kuendelea na muundo wa sasa kuna tatizo kubwa .Watanganyika wanajua uzito wa muungano waliobeba,gharama zisizowahusu walizobeba n.k. Kwa bahati mbaya yote ni siri na yanazidi kutia hasira dhidi ya znz.

Tuangalie jambo moja linalohusiana na hoja yetu. Tunafahamu wakazi wa znz kwa wakati mmoja si zaidi ya laki 6.
Wengi wao kati ya 1.2 milioni wanaishia Tanganyika na kwingeneko. Tunafahamu, SMZ haina ajira zaidi ya 10,000


JMT kwa njia zisizoeleweka zilizotokana na vikao vya wznz, imetoa 21% ya ajira kwa wznz.
Kwa minajili ya mjadala, endapo JMT ina wafanyakazi laki 1, hiyo ni sawa na 21,000kwa wznz.


21,000 huduma zao zinatokana na gharama za JMT ambayo ni Tanganyika peke yake.
Upo ushahidi SMZ haichangii chochote katika JMT.


Hivyo,21,000 ya wznz watapatikana kwa uzanzibar waona si sifa .
Hapa, Watanganyika wamebaguliwa kwasababu nafasi zao hazipatikani kwa mikoa au wilaya bali ushindani.

Lakini pia,wafanyakazi hao kutoka znz wengine hawana sifa kama yule Jaji wa mahakama kuu ambaye elimu yake haikumruhusu, alipewa nafasi kwa uzanzibar tu.

Katikanafasi 21,000 znz inapewa Bilioni 1.75!
Kwamba,wamepewa nafasi zizisowahusu, wamechukua nafasi za Watanganyika,wametengenezewa ajira na Zaidi ya hapo wanalipwa Bilioni 1.75 kwa mwezi kutokakodi za Watanganyika kwa kuwasaidia wzn katika suala la ajira.

Kwasasa haya hayapo wazi na ilivyo yanaendelea kufichwa.
Katiba yaChenge imezidi kushindilia msumari wa moto kwa Watanganyika.
Inaeleza wazi ,suala la znz kukopa ni haki yao na udhamini kutoka Tanganyika ni haki yao kikatiba.

Maana yakeni kuwa wznz watakopa, watagoma kulipa na Mtanganyika atalipa deni hilo kama anavyolipa 7% ya pato la Tanganyika kwenda znz, Bilioni 1.75/mwezi kama adhabuya kuajiri wznz, kulipia mashirika ya SMZ yasiyo ya muungano, kugharamia muungano wote kwa ujumla.

SMZ itakuwana jukumu la kusambaza huduma nzuri za maji, elimu ya bure, kutokusanya kodi,na utitiri wa viongozi n.k. kwasababu gharama zote za huduma znz zinalipwa na Tanganyika.

Haya Watanganyika wanayabaini kila siku. Kwamba huduma za watu 600,000 na rasilimali wanazopata ni kubwa ukilinganisha na huduma za watu milioni 5 na rasilimali wanazopata wa mkoa wa Dar es Salaam, Mwanza au Arusha.

NaWatanganyika watajiuliza, nini hasa mchango au huduma au thamani inayoletwa na znz katika muungano huu kiasi cha watu laki 6 kupewa rasilimali kiasi hicho !!!

Siku Watanganyika watakapoamua, ndio itakuwa siku ya mwisho wa muungano.

Tusemezane
 
WATANGANYIKA WAMEN'GAMUA

WAZANZIBAR NJIA PANDA

KATIBA YA CHENGE NI MWIBA KWA PANDE ZOTE

Sehemu ya I

Mchakato wakatiba umesaidia kufahamu utete na utata wa muungano.
Malalamiko ya wazanzibar dhidi ya muungano yamekosa mashiko.
Malalamiko ya Watanganyika yaliyokuwa mioyoni sasa yapo hadharani

Tume yaWarioba ilisikia kutoka kwa wananchi, ikatoa mapendekezo ya wananchi iliyokea.
Tume ilifahamu njia ya kunnusuru muungano. Kinyume chake ipo siku yatatoka
mioyoni na muungano kufikia hatima.


Kwa mfano,inaeleweka hakuna dhulma inayofanywa dhidi ya znz katika uchumi.
Inaeleweka, madai ya wznz haya kujengwa katika msingi wa hoja za mashiko.


Watanganyikawametambua mzigo wa muungano ni wao.Kwamba, wanagharamia shughuli zisizo za muungano kuliko gharama zinazoelekea eneo jingine la Tanganyika.

Watanganyika wana maswali yasiyo na majibu. Hawajui kwanini znz ipate 7% ya pato lisilojulikana.
Wametambua dhulma kama vile ajira 21% iliyotengewa Bilioni 1.75 kwa mwezi bila kanuni.

Pia wametambua znz kama sehemu ya Tanzania ina kipaumbele
kama viti maalumu pasi kuwa na mchango ndani ya muungano


Katiba yaChenge imewapa mzigo Watanganyika. Kuna vipengele vinavyoilazimu Tanganyika kubeba mzigo usioihusu.

Mathalan,kipengele cha katiba kinachoipa znz uhakika wa kudhaminiwa ikikopa.
Hilo Watanganyika hawalioni kama ni tatizo kubwa wanalokabidhi kizazi chao

KudhaminiZanzibar katika mikopo

Katiba yaChenge imetoa fursa ya znz kukopa nje. Rasimu ya Warioba ilitoa fursa kwa nchi washirika, yaani Tanganyika na Zanzibar kupata udhamini wa JMT. Haikutoa haki kwa upande mmoja na kuhamisha mzigo upande wa pili.

Hili nitatizo kwasababu, katika muundo wa sasa znz imepitisha madeni yake kwa JMT.
Suala hilo likiwekwa kikatiba maana yake ni kuwapa haki ya kufanya chochote kwamujibu wa katiba.
Watakopa
watakavyo hata kama ni hovyo, watakataa kulipa na deni atalipa Mtanganyika.


Mwaka 2012 znz ilikusanya bili za umeme kwa kutumia shirika la zesco zipatazo Bilioni20.
Kiasi hicho kililiwa na wajanja wznz. Mwisho wa siku deni la znz kwaTanesco likafikia takribani Bilioni 67.

Deni hilo limehamishiwa JMT kwasababu znz walikataa kulipa wakisema umeme wanaouziwa ni ghali.
Hakukuwa na ughalibali walikataa tu kwa kujua JMT itabeba mzigo.

Deni likapitishwa kwaWatanganyika kwa kuongezewa bili za umeme ili kuendesha Tanesco.


Hapo ni bila ya kuwa na kipengele cha katiba. Kwa mujibu wa katiba ya Chenge, znz itakuwa na haki ya kukopa ndani na nje na deni hilo kulihamishia JMT ambayo Tanganyika ndiyo mwendeshaji peke yake.

Mzigo huo utakwenda kwa mkulima na mfanyakazi wa Tanganyika.

Inaendelea sehem ya II
 
Inaendelea… II

Rasimu ya Warioba iliruhusiwa kujiunga na mashirika na taasisi za kimataifa kama itakavyokuwa Tanganyika.
Rasimu ya Chenge imetoa nafasi kwa Zanzibar tu.

Swali ni kuwa kama znz itajiunga na taasisi na mashirika hayo, nani atakayewajibika katika gharama zake?


Jibu rahisi ni JMT itagharamia. Hoja ya znz ni kuwa, JMT inasimamia mambo ya kimataifa, na znz ni mshirika wa JMT. Kikatiba znz inapaswa kudhaminiwa na JMT. Mzigo huo ataubeba Mtanganyika kwa mbeleko ya JMT.

Znz imeruhisiwa kukopa na misaada kutoka nje. Mikopo na misaada hiyo itatumika znz na si Tanzania, ingawa kila kinachopatikana kwa jina la JMT ambalo kimsingi ni Tanganyika, znz inapaswa kupata

Swali la kujiuliza, kama znz inakopa kwa ajili ya wazanzibar, kwanini dhamana ya mkopo huo aibebe Mtanganyika ikiwa hana faida nayo?

Na kwamba znz inapokwenda kukopa ina uwezo, kwanini wakati wa kudhaminiwa jukumu hilo alibebe mwananchi wa Singida, Kigoma au Mtwara?


Katiba ya Chenge inachukua matatizo ya znz na kuyaleta Tanganyika bila sababu.

Wakati huo huo Tanganyika imenyimwa haki ya kujitambua ili kutoa urahisi wa znz kujificha katika chaka chafu la JMT.
Ni chafu kwasababu ni chaka linalotumiwa kuiba na wala si kusaidiana. Tuna mfano hapa chini


ZNZ wameondoa mafuta na gesi katika muungano ili kinachopatikana kiwe kwa faida ya wazanzibar.
Mafuta na gesi ya Tanganyika, inatumika kwa ajili ya muungano.
Gesi inayozalishwa sasa kodi yake ndiyo inayohudumia muungano


Katiba ya Chenge haina sehemu inayowawajibisha waznz ndani ya muungano.
Ina sehemu inayowapa fursa wznz bila kujua gharama za fursa hizo au muungano


Kwa watanganyika, kukubali kujadili katiba ya Chenge ni kukubali kitanzi cha kuihudumia znz katika miaka mingine 50.

Kwa miaka 50 imekuwa hivyo na sasa znz inahakikishiwa na katiba ya Chenge ubwete mwingine kikatiba


Nje ya katiba ya change, Watanganyika wajiulize gharama wanazobeba kwa znz zina manufaa gani mbele ya safari?

Tunauliza hivyo kwasababu kile wznz wanachoona kina manufaa wamekiondoa katika muungano.
Yale wanayoona yana gharama sasa wanataka yawekwe kikatiba, kwamba kuhudumiwa ni haki yao


Kwa Watanganyika katiba ya Chenge ni kukalia msumari wa moto watakaojutia maishani mwao.
Ni katiba inayowapa mzigo wa znz kisheria. Ndio maana tunasema katiba ya Chenge ni mwaiba mkali.



Tuangalie upande wa znz



Inaendelea III
 
Sehemu III


Kwa upandewa znz, yapo makundi mawili.Kundi la CCM wanaofahamuznz ni tegemezi na utegemezi utawezekana iwapo itajificha katika chaka la jina Tanzania.

Kundi linataka mgawanyo wa madaraka na fursa zinazotokana muungano bila kufikiria wajibu wa znz kwa muungano.

Wajibu wameuacha kwa Mtanganyika kwa jina la Tanzania.Kundi linamtazamo finyu kwa kuzingatia mabadiliko ya kisiasa

Hoja za wznzz inajibika vema kwa hoja za Watanganyika, hivyo,madai yao hayasimami bila kujibu swali la Watanganyika, ni kwa nini na faida gani!

Kwa mfano,kundi hilo limeshinikiza 7%,21% namabilioni yasiyo na utaratibu kisiasa.
Uelewa wa muungano kwa Watanganyika wa leo unaongezeka na hawatakubali mazoea kama yalivyo .


Muundo wa serikali na uwakilishi unabadilika, utegemezi wa CCM kama nguzo yao unapungua kadri unavyosonga mbele

Na ili znz iendelee kunufaika kwa kjificha, ni lazima ikubali kutoa mamlaka yake

Ndio msingiwa kundi hilo kutaka serikali ya umoja wa kitaifa ifutwe kama ilivyokuwa hojaya marehemu Salmini A

Inaeleweka,ili katiba ya Chenge ifanye kazi, ni lazima yawepo mabadiliko ya katiba ya znz 2010 yenye utata ndani ya muungano. Mabadiliko yanahitaji 2/3 kura ya maoni isyoweza kupatikana.

Hoja yakuvunja GNU inalenga kurudisha mamlaka kwa CCM, waweze kufanya mabadiliko yatakayoendana na katiba ya Chenge.

Bila kufanya hivyo, Watanganyika watachachamaa. Kwa maneno mengine kundi hili la CCM lipo radhi kutoa kwa ajili ya uwepo wa S2 ili znz iendelee kuwa chini ya kivuli cha JMT

Kundi laPili
Hili linataka muungano, Tanganyika na znz zikiwa washirika. Nalo linatafuta maeneo ya kujibanza katika muungano.

Tofauti ni kutaka mamlaka kamili kamailivyopendekezwa na tume ya Warioba.

Msimamo wao ni znz inayomiliki katiba ya 2010 iliyonyofoa mamlaka za muungano, jambo linalotazamwa na Watanganyika kama hatua za kuvunja katiba ya JMT na muungano.

Kwa hali yoyote katiba ya Chenge haiwezi kujibu hoja za makundi hayo mawili bila kuleta mtafaruku mkubwa wa kisiasa Zanzibar. Katiba haiwezi kuridhisha CCM kwa kutoweza kufuta katiba ya znz, na wala kuwaridhisha waaotaka S3 kwa vile imehodhi mamlaka ya znz. ZNZ ipo njia panda

Inaendelea sehemu ya mwisho
 
Sehemu ya IV
Rasimu yaWarioba ilieleza kwa umakini matatizo na suluhu.
Ilitenga shughuli za nchiwashirika, kutoa uhuru wa kujiamulia hatima zao na kubeba muungano japo kwa ulinganifu kama si kuopunguza mzigo kwa upande mmoja.


Rasimu yaWarioba ilitunguliwa na CCM kwa hoja zinazojibiwa na katiba ya Chege

1)Hoja yaCCM Gharama za muungano zitaongezeka
- Tume Warioba:Gharama zitapungua kwa kujihudumia miongoni mwa washirika(mambo7)
- KatibaChenge; Gharama zitaongezeka kwa kuwa na serikali kubwa(mambo 16)

2) CCM; Hakuna vyanzo vya kuaminika vya mapato vya serikali ya muungano
- Tume:Vyanzo vitatokana na kodi za serikali washirika
-KatibaChenge: Vyanzo vya uhkika vitatoka JMT ambayo ni Tanganyika kama ilivyo sasa

3)CCM: Kutakuwa na gharama za viongozi na wastaafu kutoka S3
- Tume :Washirika watahudumia viongozi wao, na wastaafu watakuwa wachache
-KatibaChenge: Kutakuwa na viongozi 7 wa kitaifa, watahudumiwa na Tanganyika

4) CCM: Lengoni kuondoa kero za muungano
-Tume: Kuwena mambo 7 kutoka 22 , 7 yatahudumiwa na Tanganyika kwa unafuu
-KatibaChenge: Mambo yatakuwa 16 ikiwa ni pamoja na kurudisha waliyoondoa wznz Kwa gharama za Tanganyika


Hojazinaendelea kwa wingi katika mfano huo.

S2 hazitairidhisha znz na muda si mrefu malalamiko yatarudi.

Lakini pia S2 zinamshusha mzanzibar kama raia daraja la 2 kutokana na ukweli, znz haiwajibiki katika muungano na ni tegemezi . Viongozi waznz wataonekana kundi la ‘akina mama viti maalumu' na wznz hawatakuwa na sauti, thamani yao ndani yamuungano haionekani ukiachilia utu.

Na kwavileWatanganyika wanaelewa vema nguvu yao ndani ya muungano, hilo litawapa uwezo wakuwaburuza wznz si kwa uonevu, bali haki waliyo nayo kutokana na gharama wanazobeba.
Mfano, Rais wa znz akikaimu Urais wa JMT, waziri mkuu wa Tanganyikaatamwamrisha afanye jambo gani.


Katiba yaChenge ni mwiba kwa znz, rasimu ya Warioba iliwapa mamlaka na hadhi kama mshirika wa muungano.

Na kwavile yapo manung'uniko ya Watanganyika vifuani na yasiyojibiwa, ipo siku watachukua hatua

Katika mazingira ya sasa, wznz wameshapoteza sauti na hadhi ndani ya muungano.
Hojazao zimekosa mashiko, na wameanikwa kwa utegemezi usio na uwajibikaji.


Hatua inayofuata ni Watanganyika kutema ya moyoni, na muungano uatafikia hatma mapema na katika mazingira ya kusitisha na kutisha

Tusemezane
 
Kama tunakubaliana kuwa mgogoro wa Muungano ni suala la ki-uchumi,kisiasa na kidugu kwa nyakati hizi. Nadhani kuna haja ya kufunguliwa uzi uliofungwa na Moderator juu ya chimbuko la madai ya 11.5% ya hisa za wazanzibar huko BOT ( Maxence Melo ). Kwenye uzi huo kuna maswali mengi ya mantiki ambayo hayakujibiwa hasa yale yaliyoko kwenye mabandiko marefu ya Mchambuzi na EMT. Kama tungepata majibu ya maswali yale ingesaida sana kutatua mgogoro huu. Moja ya nukuu kutoka mandiko hayo ni hii

EMT said:
.....Kwa mujibu wa swali la nyongeza la Hamad Ali Hamad (CUF), records zinaonyesha kuwa Zanzibar ilikuwa na asilimia 11.5 ya shares kwenye EACB. Wakati BOT inaanzishwa, shares hizo zilihamishiwa BOT. Katika swali lake, Hamad Ali Hamad (CUF), alitaka kujua zilipo hizi shares ambazo zilihamishiwa kutoka EACB kwenda BOT.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Fedha alikubali kuwa asilimia 11.5 ya shares za Zanzibar EACB zilihamishiwa BOT wakati wa kuanzishwa kwa benki hiyo. Kuhusu zilipo shares hizo, Naibu Waziri huyo alisema it is still unclear na kwamba ni moja ya controversial issues za muungano ambazo zinafanyiwa kazi kwa sasa na serikali za pande zote mbili......

Uzi uko kwenye link hii >>>https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/334157-hisa-za-zanzibar-katika-benki-kuu-je-smz-imewahi-kuipa-ruzuku-bot-3-print.html


 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom