Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Kuna suala la msingi sana umelibainisha katika manung'uniko yako NALO NI HILI LA MFUKO WA JIMBO KWA WABUNGE WA ZNZ.

Hakika suala hili niliwahi kutanabaisha wakti tunajadili kupitishwa kwa SHARIA YA KUANZISHWA KWA MFUKO WA JIMBO hapa barzani. Nakumbuka niliwahi kuhoji kuwa fedhwa hizi zinatoka katika mfuko mkuu wa Hazina. Na CAG wa JMtz ndio atakae kuwa mdhibiti wa matumizi ya fedhwa hizi yaani yeye ndie atakae kagua pesa matumizi ya fedhwa hizi.

Nakumbuka niliuliza JE KWA WALE WABUNGE WA ZNZ WALIOPEWA FEDHWA HIZI ZA JIMBO WATAKAGULIWA NA NANI? Wakti CAG wa JMTz hana mamlaka hayo ya kufanya ukaguzi Znz? nakumbuka nilipewa jibu kuwa CAG JMTz atamkaimisha madaraka hayo kwa CAG Znz aweze kufanya kazi hiyo na kumletea ripoti.

Niliguna sana kwani kwa lugha ya kiuhasibu kupokea nyaraka bila kuzithibitisha kwa macho kwa utekelezaji wa jambo hilo ni mtihani mzito sana.

Ok all in all Bunge la JMTz lilipitisha kwa kauli moja NA SASA WABUNGE WA ZNZ WANAJINOMA.

Hakika cha mjinga uliwa na mwerevu!!!.

Laiti kama wabunge wa Tanganyika na wawakilishi kutoka TGK wangesimama kidete katika Bunge la Katiba kuitetea RASIMU ya WARIOBA kama walivyofanya wawakilishi na wabunge na wajumbe kutoka Znz basi hayo MANUNG'UNIKO yangefika ukingoni.

Binafsi nawapa pole waTgk kupoteza bakhati adhwiim.


kwanza nakuomba usijibu tena hoja yangu kwenye bandiko #320 , hapo juu.
hakika hiki ndicho nilichokuwa nakitetea toka tuanze hii mada kwamba Chenge na wenzie wametuingiza mkenge ili wapate mwanya wa kutunyonya vizuri.

nionavyo mimi huu ni mpango mwingine wa hawa wenye meno yasochoka kutafuna kuendelea kuchota fedha ilihali siye wengine tunaambiwa zimepelekwa kwenye mfuko wa jimbo.

sasa najua kwann inawezekana mambo kama sherehe kubwaaa za uhuru na muungano zinazogharimu serikali hela nyingi zinawezekana ilihali tukiambiwa kwamba serikali haina hela hata ya dawa hosp.

ofc nyingine utakuwa hata OC hazijaja kwa karibu nusu mwaka sasa, lkn mambo yasiyokuwa ya umuhimu yanafanyika unajiuliza kwan fedha zilizopatikana kwenye hili zimetoka wapi??

apa sasa ndo napata jibu kwamba kuna mwanya ulioachwa wazi ambao pia hakuna anayeweza kuuhoji ndiko zinavujishiwa hizi hela. No wonder kila mbunge wa zbr anapitishiwa bakuli kuchangia yajapo masherehe, ama safari za ambazo hazikuwa kwenye ratiba.

sitashangaa siku kusikia kwamba hata fedha hizo za mfuko wa jimbo wabunge hao wa zbr hawazitumii manake zinawekwa kama amana tu ambapo siku mwenyewe anapoitaka basi huenda kuichukua. sitashangaa hata kidogo
 
hapa naomba kwamba tuanze kwa kuulizana maswali na ninaomba Mkandara na Barubaru waanijibu.

Je wabunge wanaotoka zanzibar kuingia kwenye BLMT wanapatikana akwa vigezo gani?
Je wabunge hao wakiingia kwenye BLMT wanaingia kama wawakilishi wa majibo yao ama kama wawakilishi wa zbr?
1. Wabunge wa Zanzibar hupatikana kwa vigezo sawa kabisa na wabunge wa bara.

2. Wabunge wa Zmz wanaingia kwenye BLMT kama wawakilishi wa majimbo yao Kitaifa. Hata nchi zenye serikali 3 huwa na wabunge wa aina hii japo wana wabunge wanaowakilisha majimbo yao ndani ya serikali yao. Pengine basi labda ungeuliza wabunge wa bara je?. Hawa kwa ni wawakilishi wa majimbo yao Kitaifa vile vile kwa sababu mgeni anapokuja nyumbani kwako yeye humwakilisha hata mkeo ama watoto wake lakini wewe mwenyeji ni mkarimu wao.

Kifupi, tunachanganywa sana na muundo wa serikali 2 lakini ukisha uelewa vizuri tunaweza kuweka mfumo utakao fichua vijimambo vilivyofichwa ndani yake maana tunapozungumzia swala la fedha. Tanganyika ambayo haitumii tena jina lake ila la ubini wake ndiye mwenye kuweka fedha. Za bara huziweka mfuko mmoja wa suruali na za JMT huziweka mfuko wa pili wa suruali yake. Tofauti na serikali 3 ambapo inakuwa kama bwana mwenye wake wawili. Humpa mke mmoja fedha za matumizi na mwingine fedha za matumizi kisha yeye huangalia swala gani zaidi atalishughulikia ili kukuza utajari wa familia na hivyo Utajiri huo utakuwa kwa wote!

Tatizo linalokuja hapa ni katika kugawana, kuna madai ya huyu mke wa pili mwenye mtoto mmoja anadai sawa na mke wa pili japo mke wa pili ndiye mwenye watoto wengi. Hii mimi naikataa kwa sababu hatutazami kugawa utajiri kulingana na hesabu ya watoto isipokuwa uwekezaji mzuri kwa kizazi hiki maana wote ni wana Ubin mmoja. Tunagawana utajiri kwani hii mirathi baba kisha kufa? kwa nini fedha hizo zisiwekezwe kwa watoto wanotaka kusoma Elimu ya juu wenye nafasi zaidi ya kufanikiwa kuliko kutazama wingi?

Fedha za kujikimu kila mmoja hupewa ama hukusanya kulingana na uwezo wake, hivyo swala la kubishania sio fedha za kujikimu bali fedha za bwana ambazo malengo yake ni kuwekeza katika jamii hiyo ili ipate kutajirika zaidi.

Kwa hiyo utaona kwamba ubishani wangu haupo kwenuye kugawana mirathi ambao wengi wetu wanautumia kama vile Tanganyika na Zanzibar tutagengana kesho ma akuna hatari ya baba kutoa talaka kwa wake zake. Hii habari ya JMT kugawa fedha za maendeleo kwa asilimia ndio sikubaliani nalo maana uwekezaji nchini hauwezi kuwa na uuwiano maana kila mkoa una maliasili na rasilimali zake na nyingine ni muhimu zaidi ktk kukuza uchumi kuliko sehemu nyinginezo.

Leo tunawekeza zaidi Dar kwa sababu services imechukua nafasi kubwa ya ujenzi wa mfuko wa mapato lakini sii haramu tukakarabati na kupanua bandari za Tanga na Mtwara ili kesho mikoa hiyo pia iweze kuchangia mfuko wetu na na kupunguza muda wa upokeaji na usafirishaji mizigo ya nje. na kwa kufanya hivyo nchi jirani zingetumia zaidi bandari zetu kutokana na uwezo mkubwa wa kusafirisha na kupokea kwa haraka.

Zanzibar, sioni sababu ya kutokuwa na Free port ambayo ingekuwa Dubai ya Africa. mashirika toka China, Maleysia, Japan na India yakasogezwa soko lake ktk ufuko wa Afrika kiasi kwamba nchi za jirani hawana haja ya kwenda Dubabi ama China kutafuta mali. Na mizigo ikishatoka Zanzibar italipiwa ushuru wa kupitia bara ama usafiri kwa mashirika yetu ya ndege kupata mizigo na hivyo ATC kuboreka.

haya ni mawazo yangu tu ambayo yanatazama jinsi ya kujiendeleza na sio kugawana kidogo ambacho kingeweza kuwa mtaji wa kesho ili kila mmoja ajitafutie mwenyewe. Sijui nikuite dada au Kaka, Hata katika familia zetu ukiona biashara yoyote ambayo pato la biashara hiyo hugawanywa badala ya kuufanya mtaji basi ndugu hao hawataendelea kamwe. Kulipana mishahara haipotezi haki ya miliki na wala sii vizuri kuanza kuulizana hiyo mishahara hiyo ya kujikimu huyu mwenzetu amefanya nini kwa sababu ni sisi tulompangia kazi yake. kaifanya vizuri tumsifie kaifanya vibaya tutazame wapi asaidiwe maaa utajiri ni wetu sote.
 
WABUNGE WA ZNZ NI WA TAIFA NA NCHI YA ZNZ
UWPO WAO DODOMA NI MZIGO KWA WALIPA KODI

WANAWAKLISHA ZNZ, NA SMZ INAAJIBU WA KUWAHUDUMIA


Mkuu Mkandara
, kwanza nisema umekwepa hoja za msingi na swali la gfsonwin

Tuweke kumbukumbu sawa. Tumeuliza tuonyeshwe wapi wazanzibar wanaonewa?


Hakuna jibu, nalililopo ni la misaada na mikopo.Tumeuliza4.5%, 1.75Bilioni, gharama za uwizara husika na taasisi zake nanianayegharamia? Hakuna jibu, tunaambiwa ni 94.5% ya JMT.

Tumeuliza, iweje 95.4 igawanywe hadi znz ili hali znzinapata 4.5% tofauti kabisa na eneo jingine?
Hakuna jibu.
Tumeuliza, kwavile ni mikopo wapi bajeti ya znz inaonyeshakupia deni? Hakuna jibu.
Tukauliza gharama za muungano zinatolewa na nani?


Hakuna jibu, lililopo ni misaada na mikopo. Tumeuliza kwasasawahisani wamesitisha, je muungano umekufa? Hakuna jibu

Turudi kwenye maswali ya gfsonwin.Si kweli kwamba sisi ni taifa moja.
Ushahidi ni wzn kudai utaifawao. Kwa mantiki hiyo wabunge waznz ndani ya JMT si wa taifa la Tanzania, ni wabunge wanaowakilisha znz, hebupitia hoja hizi


1 Kuna tume ya uchaguzi ZEC inayosimamia shughuli za uchguzina upatikaji wao.
2 Wapowabunge kutoka BLW wasiowakilisha jimbo lolote bali BLW.
3 Ndaniya bunge la JMT, wznz wana 2/3 inayosimamia masilahi ya znz na si Tanzania. Hakunambunge au wabunge wengine wenye nguvu ya 2/3 isipokuwa wao tu kwa kutambua uzanzibarwao na si
utaifa

4 Uwepo wao Dodoma ni kwa wizara zisizodi
5.Mambo mengine hayawahusu kama yasivyotuhus yao.
6
Mfuko wa jimbo ni pesaza JMT, na znz tayari imeshachukua 4.5% unless useme 94.5 ni ya wote 4.5 ni yao.


Kwa kuzingati hayo wabuge wa znz, kwanza hawapaswikuzungumzia mambo yasiyo ya muungano. Hatuna upungufu hadi kuwaazima.
Kuzungumzia ni kufanya kazizisizo wahusu.


wzn hawamtambui waziri mkuu wa JMT, wapi wanapata mamlaka yakumhoji akiwa nchini kwake. Kwa kifupi wabunge wa taifa la znz ni mamluki,wakae kimya na si kuongelea mambo wasio na ufahamu nayo, yasiyo wahusu nayasiyo na masilahi kwao

Hoja kubwa ni kuwa, kwavile wanakuja kwa masilahi ya znz,hatuna sababu za kulipia gharama zao.
Ni wakati sasa, SMZ iwahudumie kwa kuwani wawakilishi wa nchi yao


Mfuko wa jimbo hawana haki, waende SMZ iliyopokea 4.5% naBilioni 1.75 kila mwezi kupewa huko huko.
Kugharamiwa na JMT ambayo hawanamchango,wameshachukua chao ni wizi na uharamia.

Hilo ndilo tunataka lifike mwisho, ni moja yay ale yaliyopovifuani mwa Watanganyika.

Inaendelea …… (hoja zingine)
 
MFUMO WA S2 HAUNA MFANO DUNIANI
WABUNGE WA ZNZ NI WA TAIFA LA ZNZ
WABUNGE WA JMT HAWAELEWEKI NI WA TANGANYIKA AU TANZANIA!


Mkandara
Kwanza,kuna mambo maatatu nayaona kwako. Moja, ima huelewi mfumo uliopo na matatizo yake, unaelewa umeamua kupotosha au una jingine tusilolielewa

Pili,hakuna nchi yoyote duniani yenye mfumo wa muungano tulio nao. Kuchukua mifano ya sehemu nyingine usizozitaja nikujenga hoja kwa kutumia dhana yako, na wala si ufahamu unaodai hatuuelewi

Tatu, mfano wako wa znz kuchukua pesa na kuweka mfukoni mwake na JMT kuweka mfuko mwingine ni mfu na irrelevant. Tumeonyesha kuwa zile za JMT zinatumiwa na znz na hivyo znz ina mifuko miwili, wake na wa JMT

Nne, mfuko unaosema ni JMT na Tanganyika imechukua jina la ubini nao ni mfu.
Kama unatumia ubini wa Mkandara, huo si wako ni wa jamii ya akina Mkandara.

Hivyo, huwezi kuwa na umiliki wake mwenyewe ukizuia wengine kutumia haki hiyo. Ndivyo znz inavyotumia ubia
ni

Tano, malalamiko ya znz ni Tanganyika kuvaa koti la muungano kwa kuwa na jina la Tanzania.

Malalamiko ya Watanganyika ni kuvaa koti hilo likitumiwa na wznz katika wizi


Sita, Mfumo unaozungumzia wan chi zingine huuelewi.
HukoCanada unapokuishi kuna mabunge ya majimbo yenye wabunge wake(Member ofprovincial parliament) wakiongozwa na waziri mkuu anayeitwa Premier.

Haya ni mabunge yenye uwezo wa kutunga sheria zao na haupo uhusiano na bunge la shirikisho


Wabunge wa shirikisho wanaitwa MP kama hapa kwetu.

Wabunge wa majimbo hawaingii katika shirikisho Ottawa wala hawana uwakilishi.

Wabunge wa shirikisho hawaingii katika majimbo. Hii nitofauti na sisi ambapo kuna wabunge wa znz na wale wanaotoka kutoka BLW.

Wabungewa Tanganyika hawapo wapo wabunge wa taifa ambalo halijulikani kama ni Tanganyika au ni Tanzania.


Kwa mantiki hiyo mfumo wetu hauelezeki. Huwezi kuwa na wabunge wa znz wanaowakilisha znz na kupewa 2/3 ukawaita wa taifa. Hao ni wznz,na wala huwezi kuwa na wabunge wa majimbo wanaowakilisha kisichojulikana kamani Tanganyika au Tanzania ukawaita wataifa

Hoja ya wabunge wa znz kuwa wa taifa ni njia ya kuwahalalishaili waendelee na ufisadi.

Ni ufisadi kuwasababu, kwanza hawamtambui kiongozi wa serikali bungeni.(PM), wanatambua pesa tu

Pili, serikali ya JMT haina mamlaka nao, tatu, uwepo wao nikupata 2/3 kwa mambo yasiyozidi 5 kwa hali ya sasa.


Sisi tunasema, znz hata kama wataleta wabunge 600, ilimradi wanawahudumia wao hakuna tatizo.

Tusichotaka kukiona ni wao kuleta watu wao halafu gharama abebe Tanganyika

Tangnyika haihitaji wabunge wa znz kwa mambo ya Tanganyika kwasababu, hayawahusu, na wala hawana ufahamu wa matatizo ya Tanganyka

Uwepo wao nimzigo na hilo ndilo Tanganyka wanasema, sasa basi, SMZ ihudumie watu wao kama inavyochukua 4.5%, 1.75Bilioni na makando kando mengine. Hawa ni wabunge wataifa la znz, Tangayika haihusu.


Inaendelea …..
 
HOJA YA BANDARI HURU ZNZ

Mkandara , sijuihoja ya znz kuwa na bandari huru imeingiaje. Hadi sasa znz ina bandari huru.

Kilichowafanya waondoe bandari katika mambo ya muungano ni kuwa na bandari huru. Sijui kama hilo una ufahamu nalo au

Pili, unaposema znz iwe kama Dubai nadhani unadakia mambo bila kufanyia utafiti wa kutosha.
Angalia Dubai na washirika wanaoizunguka halafu angalia znz na majirani


Znz inachukua mapato na kukataa kuyaingiza katika muungano kunaeleza kwanini Tanganyika haipaswi kuwa responsible kwa mambo ya wznz ikiwa ni pamoja na failure zao

Chukulia mfano, mafutana gesi ambayo hayatoka hata tone wamekimbia kuyandoa.
Lengo lao ni kuhakikisha mapato yao hayavuki bahari ingawa yetu ni halali kuwafikia.


Ukifanya znz k bandari huru hakuna manufaa kwa Tanganyika.

Znz itatumia jina la Tanzania kufanya uchochoro wa bidhaa na kukosesha taifa mapato.

Walipoanzisha bandari huru walipewa hiyo fursa, kilichotokea wafanyabiashara wote wakawa wanapitisha bidhaa zao znz wasikokusanya kodi. Tanganyika ikaumia, ndio sababu ya kuachana na upuuzi huo.


Ukiruhusu znz kuwa bandari huru, maana yake ni kumbebesha mzigo Mtanganyika aliye elemewa na mzigo wa znz kwa sasa. Itabidi tulipekodi Zaidi kwa vile znz watakuwa uchochoro.

Kuruhusu bandari huru ni kuongeza gharama za miundo mbinu bila kuchukua mapato ya kujenga na kukarabati.
Kodi zote zitabaki znz kamailivyo mafuta na gesi n.k.


Znz ana hiari ya kuwa bandari huru, lakini hilo si sharti lamuungano. Tanganyika nao wanahiari kuifanya bandari ya Mtwara au Tanga huru kubaliana na ushindani wa majirani kama Beira na Malindi.

Kuona haya kunaumiza Watanganyika.
Wznz wanapodai kuwa taifa na uchumi wao ni haki yao.

Haki ya Watanganyika kuamua hatma yao ipo wapi?


Kwa taarifa, narudia, znz wana bandari huru na ni haki yao kwa faida yao. Hilo lisiongeze mzigo mwingine Zaidi ya huu Watanganyikawanaohangaika nao. Na wala lisizuie Watanganyika kufanya maendeleo kwa kuogopa znz.
 
Last edited by a moderator:
Muungano uliopo ni muungano wa KISIASA, sio muungano wa KIUCHUMI. Mfumo wa Muungano wa sasa unaichukulia Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sio moja ya nchizi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala la uchumi halipo katika masuala ya muungano, hivyo basi kila kila upande unatakiwa uwe na mawaziri wake wanaosimamia na kutekeleza sera za uchumi na mipango na kila upande ulitakiwa uwe na bajeti yake. Suala la Bandari ni suala la kiuchumi, linahitaji sera ya mipango, uchumi, lakini muhimu Zaidi, mikakati ya kibajeti kupitia sekta husika (Fedha, Miundo Mbinu, Biashara n.k). Ni kwa mantiki hii, naunga hoja ya Nguruvi3 hapo juu.
 
Last edited by a moderator:
Muungano uliopo ni muungano wa KISIASA, sio muungano wa KIUCHUMI. Mfumo wa Muungano wa sasa unaichukulia Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sio moja ya nchizi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala la uchumi halipo katika masuala ya muungano, hivyo basi kila kila upande unatakiwa uwe na mawaziri wake wanaosimamia na kutekeleza sera za uchumi na mipango na kila upande ulitakiwa uwe na bajeti yake. Suala la Bandari ni suala la kiuchumi, linahitaji sera ya mipango, uchumi, lakini muhimu Zaidi, mikakati ya kibajeti kupitia sekta husika (Fedha, Miundo Mbinu, Biashara n.k). Ni kwa mantiki hii, naunga hoja ya Nguruvi3 hapo juu.
Mkuu
Karibu sana jamvini, uliadimika kwa muda sasa. Tunaambiwakuwa mawaziri wa JMT ndio hao hao wanatakiwa wawe wa Tanganyika( Mkandara) ilikupunguza gharama.
Mkandara huyo huyo anasema waziri wa JMT hana kazi kule znz anashughulikia ya bara. Katika halikama hiyo wazo lake la Dubai halikuzingatia hali ya kisiasa au kiuchumi, niyale yale ya kuamua 4.5% na Bilioni 1.75kwa mwezi bila kuwa na kanuni
Huu muungano unatakiwa uwe wa kiuchumi, na katika angle hiyoznz haionekani kuwa na msaada Zaidi ya kuwa tatizo. Hawawezi kulalamika nakudai haki zisizo zao! Hawawezi kuwa mzigo mzito kuliko engine ya economy i.eDar es Salaam. Na ziaid ya hapo znz imekuwa distractions tu katika kujadilimatatizo ya taifa
 
Last edited by a moderator:
MAMBO YASIYO YA MUUNGANO
WABUNGE, WATUMISHI WA ZNZ NI ‘ZIGO TARAJIWA'

Kamati ya serikali za mitaa Tanganyikayaongozwa na mgeni kutoka znz

Rasimu ya Warioba iliweka washirika wa muungano ili kuleta utangamano na kuondoa sintofahamu

Katiba yaChenge/CCM ni mfanano wa 1977, penye mabadiliko ni kwa ajili yakuwafurshisha wznz na si kutafuta kiini na suluhu ya tatizo. Kukwepa tatizo kwa njia za kupulizia utuli ‘perfume' ni kuficha uvundo, na mwisho wake ni funza kutjitokeza

Katiba hiyoya Chenge inasemwa tu bila kuonyesha wapi imetoa majibu ya matatizo na malalamiko ya pande husika. Inavyoonekana ,Tanganyika imevalishwa koti la muungano na kufungwa mdomo kwa kuwa muungano.

Tumeangalia maeneo Tanganyika inayabeba kama muungano na si mshirika. Yapo ya muda mfupi na muda mrefu yasiyoonekana.

Mfano,Wabunge wa znz ni kwa ajili ya znz. Wana turufu ya 2/3, kukubali au kukataa jambo ka niaba ya znz.
Inategemewa, wabunge hao kusimamia masilahi ya znz na si Tanganyika katika mambo ya muungano tu.


Ukisoma taarifa za bunge, kamati ya serikali za mitaa inaongozwa na mzanzibar na wajumbe wengine ni wazanzibar(Mohamed R Mbaruku-Mwenyekiti, na IssaMajaliwa-mjumbe) . Serikali za mitaa si jambo la muungano na halijawahi kuwa.

Uchaguzi uliomalizika wa serikali za mitaa ulihusu Tanganyika chini ya usimamizi wa ofisi ya waziri mkuu nasi tume ya uchaguzi ya taifa. Hilo ni jambo la waziri mkuu ambaye Zanzibar hatambuliki kikatiba, kisheria au kiitifaki.

Hivi ,inakuwaje kamati inayohusu Tanganyika iwe chini ya mbunge wa znz ambaye:

  • Uwepo wake ni kwa ajili ya Zanzibar
  • Kamati isiyo katika mambo ya muungano
  • Mbunge asiyejua habari za serikali za mitaa zaTanganyika

Juzi, kamati ikiwakilisha taarifa ya uchunguzi ilishangaza kidogo.
Bwana Mbaruku na Majaliwa wanaandika taarifa ya serikali za mitaa ya Tanganyika inawahusu nini?


Walikwendaje kufanya uchunguzi au kupata taarifa kutoka ofisi ya waziri mkuu wasiyemtambua?
Uzalendo wao katika Tanganyika ni upi, ikiwa wao wapo kutetea 2/3 ya znz na sivinginevyo?


Inaendelea..
 
Inaendelea..

Huko nyumatuliona utata wa mfuko wa jimbo. Kwamba, wazanzibar hawap[aswi kupewa fedha zajimbo.
Hizo si za muungano, wao wanazao kupitia 4.5% na Bilioni 1.75 kwa mwezi kama kodi ya wafanyakazi.


Hawa wanaongia katika kamati za bunge ni tatizo jingine. Hawana uelewa wa mambo yaTanganyika, na hivyo taarifa zao zinakosa uaminifu'integrity' kwasababu wanafanyakazi kwa malipo na si utaifa.

Wznzw amelalamika kuhusu kuongezwa mambo ya muungano kinyemela.
Hili la wizara au taasisi zisizo za muungano ni la kinyemela. Lakini, Wznz hao hao wanaolalamika unyemela wanadai fursa kwa lazima kwa kutumia asilimia 21 ya ajira za muungano.


Ndivyo ilivyo kwa taasisi za umma na watumishi wake. Zanzibar inapewa 21%isiyojulikana imepatikana kwa formula gani. Gharama za watumishi hao 21% SMZ haijui na wala haihusiki. Tatizo la muda mfupi!

Tatizo lamuda mrefu ni kuwa, wznz hao waliopata ajira kwa 21% hata kama hawana sifa,bado Tanganyika italazimika kuwalipia mafao yao ya utumishi na pensheni zaohadi mwisho wa maisha yao.
Hili ni deni lisiloonekana alilobeba Mtanganyika bila kujijua.


Mitirirko mzima unaanza pale mzanzibar anapomaliza highschool.

Elimua juu ana upendeleomaalumu na mikopo isiyorudishwa.

Ajira ana 21 isiyojulikana, kodi zinapelekwaznz kule kule walikopata upendeleo kwa kiasi cha Bilioni 1.75 kila mwezi.


Gharama za 21% anazilipia Mtanganyika. Mafao ya uzeeni ya 21% ya wznz anazilipia Mtanganyika.

Hapa ndipo wanatakiwa wajiulize, je, wanatendea haki kizazi chaocha leo na kijacho?


Inaendelea…
 
MUUNGANOWA HAKI NA USAWA-WZNZ

Moja yakauli mbiu za wznz ni muungano wa haki na usawa.

Hakuna anayeelewa ni haki gani wanadai. Inaeleweka sasa, Watanganyika wanaopaswa kuda ihaki na usawa.


Haki na usawa kwa mtanganyika ni kupata Tanganyika liyo nje ya Tanzania ili kujiamulia mambo yake bila kuidhulumu znz na bila kudhulumiwa na znz.

Utamduni wakuficha mambo unahtAarisha hatima ya muungano kuliko kuimarisha.

Njia muafaka ni kuwa na mambo machache kama yalivyopendekezwa na tume ya Warioba.

Na makubaliano yakiwepo, mambo hayo machache yajadiliwe kwa uwazi nini ushiriki, na mchango wa kila mshiriki.


Huu utaratibu wa kufanya mambo kwa mazoea, kupendezana na kufurahishana utapelekeakifo cha ghafla cha muungano. Kwa mfano, leo Watanganyika wamebaini kuwa huu muungano wameubeba vichwani mwao wenyewe.

Watanganyika wamebaini waliyokuwa hawajui. Wanadai kuonyeshwa haki ya znz upewa 4.5 ? Na zip habarikuwa sasa ni 7% kama hatutakosea. Tunamwalika mwenzetu Ngongo mwenye uzi uliothibitisha ongezeko kutoka 4.5% hadi 7%

Watanganyika wanadai, 21% ya ajira inapatikana kwa utaratibu gani?
Wanadai kuonyeshwa mchango wa znz katika muungano (si vyeo au misaada)
Watanganyika wanajiuliza, iweje deni la znz liwe la Tanzania?

Orodha ni ndefu sana

Wamebaini kutokuwepo na haki katika taifa linalojiita ni moja.

Mtanganyika akilipa kodi kujenga daraja Mtimbira, barabara Magoroto au kisima cha maji Kaliua anauhakika kufanya hivyo ni wajibu wake.

Ipo siku atakuwa na fursa za kwendamaeneo tofauti na kufaidika na fursa bila ubaguzi wa aina yoyote


Mtanganyikaanapotumia gharama na fursa zake kwa znz si haki.

Si haki kwasababu ili aweze kufaidika na fursa za znz ni lazima awe na ZanzID.
Kitambulisho hicho ni mahususi kumtenga Mtanganyika awapo znz katika fursa zote

Mtanganyika anapokuwa znz ni sawa na mnigeria au mkongo. Wote ni wageni na hawana fursa kama wznz wenye ZanzID.

Inapotokea kodiya Mtanganyika inatumika kwa mambo yasiyo ya muungano au ya muungano akiwa peke yake si haki na usawa.

Kwanini Mtanganyika apelike 1.75Bilioni znz? SMZ haikusanyi kodi kiasi hicho, iweje iwe haki kwa Mtanganyika kufanya hivyo na znz ilalamike kuhusu haki na usawa?

Ni usawa na haki gani ambayo mzanz anaweza kusimama hapa jamvini na kutuonyesha kadhulumiwa?


Ni haki nausawa gani unaowapa wznz nguvu ya kusema hili liwe la muungano, lile hapana.
Muungano uwe kadha wa kadha na si vinginevyo!


Funika kombe inayofanywa na CCM ni hatari sana kwa mustakabali wa muungano.

Prof Kabudikaonya, Watanganyika wana yao vifuani na siku wakiytaoa muungano utafikiamwisho.

Tusemezane
 
Last edited by a moderator:
.......

Hivi ,inakuwaje kamati inayohusu Tanganyika iwe chini ya mbunge wa znz ambaye:

  • Uwepo wake ni kwa ajili ya Zanzibar
  • Kamati isiyo katika mambo ya muungano
  • Mbunge asiyejua habari za serikali za mitaa zaTanganyika

Juzi, kamati ikiwakilisha taarifa ya uchunguzi ilishangaza kidogo.
Bwana Mbaruku na Majaliwa wanaandika taarifa ya serikali za mitaa ya Tanganyika inawahusu nini
?


Walikwendaje kufanya uchunguzi au kupata taarifa kutoka ofisi ya waziri mkuu wasiyemtambua?
Uzalendo wao katika Tanganyika ni upi, ikiwa wao wapo kutetea 2/3 ya znz na sivinginevyo?


Inaendelea..
Hili lilinisikitisha sana...na kudhihirisha kuwa Hawa wapo kwa maslahi ya Zanzibar na hawana uchungu na Tanganyika; akiitimisha maelezo ya kamati yake(Mh. Mbaruku, M.R.), kwa kinywa chake nilimsikia akitolea maelezo kisa cha kukataliwa na Mzungu kuingia kwenye majengo yanayomilikiwa kwa ubia kati ya Manispaa ya Kinondoni na 'mwekezaji'. Alisema (mh. Mbaruku) mzungu aliwakatalia kuingia kwenye majengo hayo na yeye kama mwenyekiti (mzanzibar) hakufanya chochote zaidi ya kunung'unika na kutusikitikia watanganyika (msisitizo wa kwangu) kwa kumruhusu Mzungu kuwa na kiburi kiasi hicho. Ni kwa uchungu na uzalendo alionao Mh. K. Lugola(mtanganyika) aliamua kumvaa mzungu huyo na ndipo mwenyekti aliamua kuita polisi kuingilia kati na baadaye wakaruhusiwa kuingia kwenye majengo hayo. Kama mwenyekiti alitakiwa achukue hatua kama alivyofanya Zitto (pamoja na matatizo yake) wakati wakutafuta mikataba ya Gesi inayofanywa siri, kiasi cha kuwasweka ndani wafanyakazi wa TPDC.

Jambo lingine ni utaratibu wa kupitisha miswada inayohusu fedha kwa kupigiwa kura kwa uwiano wa 2/3 kutoka Zanzibar ili iweze kupitishwa/kubaliwa. Hili lilizungumzwa na Mh. Cheyo (mtanganyika). Mh. Cheyo alilalamika kanuni hii ambayo inaweza kukwamisha miswada yenye maslahi wa kwa Tanzania (Tanganyika for this case), kisa Zanzibar haijaridhishwa na mambo fulani, mfano wakiondolewa kupelekewa 4.5% ambayo sasa inasemekana ni 7% ya pesa makusanyo ya Tanzania(mfano nimeutoa mimi).

Hivyo, kwa mambo hayo mawili niliyoeleza kuna athari ambazo zinawapata watanganyika kwa kukubali kuongozwa na watu wa nchi jirani ya Zanzibar ama kukubali wao waamue mambo yanayohusu Tanganyika (wanayoita nchi jirani).
 
Mkuu
Karibu sana jamvini, uliadimika kwa muda sasa. Tunaambiwakuwa mawaziri wa JMT ndio hao hao wanatakiwa wawe wa Tanganyika( Mkandara) ilikupunguza gharama.
Mkandara huyo huyo anasemawaziri wa JMT hana kazi kule znz anashughulikia ya bara. Katika halikama hiyo wazo lake la Dubai halikuzingatia hali ya kisiasa au kiuchumi, niyale yale ya kuamua 4.5% na Bilioni 1.75kwa mwezi bila kuwa na kanuni
Huu muungano unatakiwa uwe wa kiuchumi, na katika angle hiyoznz haionekani kuwa na msaada Zaidi ya kuwa tatizo. Hawawezi kulalamika nakudai haki zisizo zao! Hawawezi kuwa mzigo mzito kuliko engine ya economy i.eDar es Salaam. Na ziaid ya hapo znz imekuwa distractions tu katika kujadilimatatizo ya taifa

Shukrani Nguruvi3.

Majuzi nilikuwa nimekaa sehemu na mtu mmoja (kada wa CCM) ambae alikuwa ni mjumbe wa tume ya warioba akitokea Zanzibar. Nikamuuliza swali rahisi tu kwamba, je Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana mamlaka gani Zanzibar? Jibu lake likawa ni rahisi sana tena hapo kwa papo kwamba "Huyo Waziri Mkuu ni wenu wabara, sisi wazanzibari hatumtambui huyo". Kumbuka kwamba anajibu haya juu ya Kiongozi ambae ndiye kiongozi mkuu wa shughuli za kila siku za serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Nikamuuliza tena, Rais amemteua kijana mwenzako kuwa naibu waziri ofisi ya makamu wa wa rais (muungano), huyu kijana kazi yake ni nini hasa katika suala zima la muungano? Kwa swali hili, pia akajibu bila kusita kwamba huyo ni wa kwenu, sisi tunae mama suluhu. Nikauliza, mama suluhu mnaye akifanya nini? Hilo hakujibu.

Ni bora kofia hii ya waziri wa muungano sasa ianze kuitwa "Balozi wa Zanzibar" Tanganyika ili na upande wa Tanganyika nao uteue balozi wake kwenda kusimamia maslahi ya Tanganyika nchini Zanzibar.
 
Last edited by a moderator:
Shukrani Nguruvi3.

Majuzi nilikuwa nimekaa sehemu na mtu mmoja (kada wa CCM) ambae alikuwa ni mjumbe wa tume ya warioba akitokea Zanzibar. Nikamuuliza swali rahisi tu kwamba, je Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana mamlaka gani Zanzibar? Jibu lake likawa ni rahisi sana tena hapo kwa papo kwamba "Huyo Waziri Mkuu ni wenu wabara, sisi wazanzibari hatumtambui huyo". Kumbuka kwamba anajibu haya juu ya Kiongozi ambae ndiye kiongozi mkuu wa shughuli za kila siku za serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Nikamuuliza tena, Rais amemteua kijana mwenzako kuwa naibu waziri ofisi ya makamu wa wa rais (muungano), huyu kijana kazi yake ni nini hasa katika suala zima la muungano? Kwa swali hili, pia akajibu bila kusita kwamba huyo ni wa kwenu, sisi tunae mama suluhu. Nikauliza, mama suluhu mnaye akifanya nini? Hilo hakujibu.

Ni bora kofia hii ya waziri wa muungano sasa ianze kuitwa "Balozi wa Zanzibar" Tanganyika ili na upande wa Tanganyika nao uteue balozi wake kwenda i maslahi ya Tanganyika nchini Zanzibar.

The question is why this position exists at first place? Once the country decided that the president should be the chief executive and the head of state, the prime minister position should have disappeared.
 
The question is why this position exists at first place? Once the country decided that the president should be the chief executive and the head of state, the prime minister position should have disappeared.

The position was set to meet political ends, not economic ends. Hakuna la maana kiuchumi linalofanywa na ofisi ya waziri mkuu. Tazama mchango wa ofisi hii kwa uchumi wa Tanzania. Angalau basi tume ya mipango, au kitengo alichokuwa nacho Wassira ikulu kabla ya mabadiliko ya juzi, zingekuwa kwa waziri mkuu. Waziri mkuu ana tawala za mikoa na serikali za mitaa, na hizi zinafanya kazi kisiasa zaidi kuliko kiuchumi. Haiwezekani Halmashauri zitegemee zaidi ya 60% ya matumizi yake kutoka serikali kuu kama ruzuku. Haiwezekani. Ni utamaduni huu huu wa cash transfer ndio unatumika chini ya serikali mbili kwenda Zanzibar. Mwisho wake ni a lot of leakages and wastage of public funds.
 
The position was set to meet political ends, not economic ends. Hakuna la maana kiuchumi linalofanywa na ofisi ya waziri mkuu. Tazama mchango wa ofisi hii kwa uchumi wa Tanzania. Angalau basi tume ya mipango, au kitengo alichokuwa nacho Wassira ikulu kabla ya mabadiliko ya juzi, zingekuwa kwa waziri mkuu. Waziri mkuu ana tawala za mikoa na serikali za mitaa, na hizi zinafanya kazi kisiasa zaidi kuliko kiuchumi. Haiwezekani Halmashauri zitegemee zaidi ya 60% ya matumizi yake kutoka serikali kuu kama ruzuku. Haiwezekani. Ni utamaduni huu huu wa cash transfer ndio unatumika chini ya serikali mbili kwenda Zanzibar. Mwisho wake ni a lot of leakages and wastage of public funds.

That's correct. The position was created as a buffer to protect the president from bad execution of government policies. It has created another layer of bureaucracy which wasn't supposed to exist and it's a waste of money.
 
Mchambuzi
Ukisomarasimu ya Warioba, mambo yote yalipatiwa ufumbuzi. Kwamba, kurakuwa nawawakilishi wa kila upande kuhusu mambo ya muungano.

Huyoaliyekwambia wana mama Samia Suluhu, yupo sahihi.
Kwenyemkutano(video ipo bandiko za nyuma) Samia kama waziri hakuongea katika capacityhiyo. Aliongea kama mzanzibar akionyesha kuwapigania wzn kama waziri wamuungano. Alisema, nafasi za uongozi(kama kawaida ya wzn ) sasa zinatfutiwaformula ya kugawanywa.

Samiaakasema, nafasi hizo ni kama kule BoT na TPDC. Hapa kuna maswali sana, kuleBoT, Gavana Ndulu na waziri wa fedha SMZ wamesema znz haina mchango kwa miaka 30.

TPDC, ni sualala mafuta na gesi. Wzn wameondoa katika mambo ya muungano.
Swali ,katika taasisi hizo wazanzibar wanafanya kazi gani?

Ni kama bodiza bandari, mashirika kama TBS.
Huko wznzwameshaondoa, wanatafuta nafasi za kuongoza kitu gani?

Hoja ya jitegemee ina mashiko. Uwepo wa wzn katika bunge una athari kubwa sana.
Kwa mfano,wzn wapo kwa 2/3 ya mambo ya muungano.

Lakini wanapigakura kwa mambo yasiyo wahusu. Kwa mfano, ukiwepo mjadala wa miradi kati yawizara ya afya, maliasi na ujenzi, ikipigwa kura, zile za wznz zinawezakubadili mwelekeo .Haya si mambo yanayowahusu lakini wamepewa nguvu ya kuamua.

Ndilo hilila serikali za mitaa. Akina Mbaruku wamepewa hadi uenyekiti.
Hili sijambo la muungano, na hawana uwezo wa kumhoji waziri Ghasia au PM Pinda.
Znzhaitambui Pinda, wsanafanyaje kazi ndani ya ofisi ya Pinda?

Katiba yaChenge inawapa hadi nafasi ya lazima ya Uspika. Hili bunge asilimia Zaidi ya 90linaloongelea mambo ya Tanganyika, mzanzibar anapataje nafasi ya kusimamiashughuli zake. Wzbz wapo kwa kutumikia 2/3 iliyowapeleka znz na si kuingilia nakusimamia mambo ya Tanganyika. Ndivyo ilivyo katika wizara na idara.

Ujira wake,ni wznz kulalamika wanaonewa, mambo yameongezwa kinyemela, muungano haunamanufaa na Mtanganyika ni mkoloni mweusi.

KwaniniWatanganyika wasiwape nafasi wnz kwenda kushughulika na mambo yao?
Na hapa pa kuanzia ni kuhakikisha mambo yasiyowahusu wasiyaguse, na wala wasishiriki

HakunaMtanganyika ndani ya BLW wala anayekagua serikali za mitaa Zanziba
Hakunamtanganyika wizara ya ujenzi, afya, miundo mbinu znz. Na ni busara kuwapawatumishi wao waende kusaidia taifa lao, na Watanganyika wahangaike na yao.
 
TAASISI NA MASHIRIKA YASIYO YA MUUNGANO
YASIYOYA MUUNGANO, KILA UPANDE UBEBE MZIGO WAKE

WZNZ WAPEWE NAFASI YA KUHUDUMIA NCHI YAO.

Zipo taasisi zinazojulikana kama za muungano.Kiuhalisia taasisi na mashirika yamepoteza sura ya muungano.
Ni
wakati wakuyatenga na kila upande uyasughulikie


Tumeona suala la wabunge wa znz na athari zao katika gharamana maamuzi ya mambo yasiyowahusu.
Tatizo ni
kubwa Zaidi katika mashirikana taasisi.


Kwa mfano,shirika la bandari, viwango(TBS), Tanzania Maritime, Sumatra, TPDC, shirika la mambo ya anga(IATA) na shirika la anga (ICAO), yote yana ‘wenza kwa upande waznz''

Kwa mantiki hiyo mashirika au taasisi kama hizo sasa ni za Tanganyika.Hivyo kuna haja ya kuyaacha mikononi mwa Watanganyika, wayahudumie kwa kuendeleza au kuua na Zanzibar wahudumie mashirika na taasisi zao.


Zanzibar iliondoa bandari ili kuweza kunufaikakwa mtazamo wao. Hatuoni kuna sababu gani za wazanzibar kuwa wajumbe wabodi ya bandari Tanzania au waajiriwa wa shirika hilo.

Kama itabidi, bas inafasi hizo zitangazwe na raia wa nchi kama Rwanda na Kenya wapewe fursa sawa na wznz kwasababu si suala la muungano.


KunaTanzania Maritimes org. Zanzibar wa ZMO. Meli zinazoandikishwa na ZMZ hutumiajina la Tanzania-Zanzibar. Makusanyo ya ada za meli hizo huchukuliwa na znz nawala si JMT.

Lakini, ada za ZMO kule International maritimes org(IMO)zinalipwa na Tanganyika kwa jina la Tanzania.
Hili sasa lifike mwisho, ZMO ibebe majukumu yake kama taasisi huko znz


Hatuoni sababu za TBS kuwa na wajumbe kutoka znz. Haya ni maeneo yaliyotengewa 21%yakiwa yamepoteza sifa za muungano. Ipo ZBS isiyoingiliana na TBS, na ni vemaTBS ikabaki kuwa ya Watanganyika

Tukirudi kwenye wizara na idara, ni wakati pia wa kuangali maeneo yenye muungano.
Yale yasiyo ya muungano, Watanganyika waachwe wayahudumie.


Mfano, znz wana wizara yao ya utalii. Inapotokea waziri wa utalii wa JMT akawa mzanzibar, allegiance yake si kwa JMT ni kwa znz. Waziri, mkurugenzi au katibu mkuu huyo yupo likely kuhujumu Tanganyika kwasababu uwepo wake ni kutokana na nafasi ya upendeleo wa asilimia 21, mapenzi yake yapo znz kama tulivyomuona Samia Suluhu akihutubia mkutano na kueleza jinsi wanavyoitetea znz na si waziri wa JMT

Watanganyika hawapaswi kukabidhi taasisi na mashirika kwa raia wan chi jirani.
Kama litatokea , kwanini isitangazwe kwa raia wengine wa Afrika mashariki?


EndapoWatanganyika hawatafunguamacho, katiba ya 1977 iliyopigwa photocopy naChenge 2014 itaendelea kuwaumiza miaka mingi ijayo.

Watabeba lawama za wznz na matusi kwa gharama zao wenyewe.

Ni wakati wznz wapewe nafasi ya kwenda kuhudumia taifa lao.

Yale ya muungano yazungumzwe si kwa misaada na mikopo,bali ni vipi tunayahumia?



Tusemezane
 
Muungano uliopo ni muungano wa KISIASA, sio muungano wa KIUCHUMI. Mfumo wa Muungano wa sasa unaichukulia Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sio moja ya nchizi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala la uchumi halipo katika masuala ya muungano, hivyo basi kila kila upande unatakiwa uwe na mawaziri wake wanaosimamia na kutekeleza sera za uchumi na mipango na kila upande ulitakiwa uwe na bajeti yake. Suala la Bandari ni suala la kiuchumi, linahitaji sera ya mipango, uchumi, lakini muhimu Zaidi, mikakati ya kibajeti kupitia sekta husika (Fedha, Miundo Mbinu, Biashara n.k). Ni kwa mantiki hii, naunga hoja ya Nguruvi3 hapo juu.

Mchambuzi,

Ulichonena ni sahihi kabisa japo kuna yaani yaani kidogo.

USAHIHI NI KWA SIRIKALI JMTz ITEKELEZE SHARIA YA UANZISHWAJI WA JOINT FINANCE COMMISSION (JFC) iliyopitishwa na bunge lake la JMTz ili kila nchi ujulikane inachangia nini katika muungano na uratibu wa fedhwa hizo.

JFC ndio itakayounganisha nchi hizo mbili kwa maana ya Znz na Tgk kiuchumi na kukata mzizi wa fitna.

Tujiulize kwanini Serikali ya JMTz inasita na kupata kigugumizi kutekeleza sharia hii ya kuanzishwa kwa JFC?.


 
J
Mchambuzi,

Ulichonena ni sahihi kabisa japo kuna yaani yaani kidogo.

USAHIHI NI KWA SIRIKALI JMTz ITEKELEZE SHARIA YA UANZISHWAJI WA JOINT FINANCE COMMISSION (JFC) iliyopitishwa na bunge lake la JMTz ili kila nchi ujulikane inachangia nini katika muungano na uratibu wa fedhwa hizo.

JFC ndio itakayounganisha nchi hizo mbili kwa maana ya Znz na Tgk kiuchumi na kukata mzizi wa fitna.

Tujiulize kwanini Serikali ya JMTz inasita na kupata kigugumizi kutekeleza sharia hii ya kuanzishwa kwa JFC?.

Barubaru,

Katiba ya JMT (1977) inatambua uwepo wa AKAUNTI YA PAMOJA, kama sehemu ya mfuko mkuu wa hazina ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusema kwamba - kutawekwa fedha yote itakayochangiwa na serikali mbili kwa kiasi kitakachoamuliwa na tume ya pamoja (Joint Commission). Serikali mbili zinazotajwa hapa ni ile ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine ya Tanzania Bara. Utata unakuja kwa sababu serikali ya Tanganyika haipo, badala yake iliyopo ni serikali ya Tanzania ambayo nayo haipo kivyake kama ilivyo kwa serikali ya Zanzibar kwani chini ya serikali mbili, serikali ya Tanzania Bara remains to be synonymous to serikali serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akaunti ya pamoja haitekelezeki kwa sababu mfumo wa serikali mbili hauruhusu mazingira hayo. Tuangalie kwa undani zaidi. Tume ya pamoja (JFC) ipo kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977) katika ibara ya 133, lakini ipo pia ndani ya riwaya ya andrew chenge. Majukumu yake yanaainishwa kama ifuatavyo:

1. Kuchambua mapato na matumizi yanayohusu utekelezaji wa mambo ya muungano na kutoa mapendekezo kwa serikali mbili juu ya mchango na mgao wa kila serikali.
Swali: Ni mambo yepi hayo ya muungano ambayo yametenganishwa na yale ya Tanganyika (ukipenda Tanzania Bara)?Bila ya kuyatenganisha masuala husika, jukumu #1 la JFC hapo juu haliwezi kutekelezeka.

2. Jukumu la pili la JFC - Kuchunguza wakati wote mfumo wa shughuli za fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na uhusiano wa kifedha baina ya serikali mbili.
Swali: Mfumo wa shughuli za fedha chini ya mfumo wa serikali mbili unachunguzwa vipi bila ya kutenganisha masuala ya muungano na yale yasiyo ya muungano kwa pande zote mbili za washirika wa muungano?

Huku ni kupoteza tu muda na fedha za walipa kodi kwani JFC inajikuta ikifanya kazi ndani na chini ya mfumo wa muungano wenye wizara/taasisi zenye sura kuu tatu:

1. Mambo ya muungano pekee yake.
2. Mambo ya Tanzania bara.
3. Mambo mchanganyiko.

Tuangalie mifano hai:

a) Ofisi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina mamlaka Zanzibar kasoro kwenye "Suala la Usajili wa vyama vya siasa", kitengo ambacho kipo chini ya waziri mkuu, na ni moja ya masuala ya muungano. Kwa maana hii, ofisi kubwa kama ya waziri mkuu ina mchanganyiko wa masuala ya muungano (Vyama vya siasa) na mengineyo ambayo ni ya bara tu. Katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

b) Wizara ya katiba ya sheria, wizara hii ni ya Tanzania bara peke yake lakini ina idara ambazo ni za ki-muungano, kwa mfano idara ya mahakama (inayokusanya mapato mengi tu), Katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

c) Wizara ya uchukuzi chini ya Samuel Sitta, wizara hii ni ya Tanzania bara tu lakini ina idara ambazo zina sura za ki-muungano kama vile TCAA, TMA, TPA, ATC (zinazokusanya mapato mengi tu). Katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

d) Wizara ya Sayansi na Tekinolojia kwa Mbarawa na mwenzake Makamba, hii ni wizara ya Tanzania bara tu, lakini ina idara ya TCRA ambayo ni ya muungano, idara ambayo inakusanya mapato mengi tu, katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

e) Wizara ya Viwanda na biashara, hii nayo ni ya Bara tu lakini ina idara za kimuungano kama vile Brela na TBS, na idara hizi zinakusanya mapato mengi tu, katika hali hii, JFC itafanya vipi kazi zake?

f) Wizara ya fedha, kuna NMB, CHC, NIC, na humu yapo ya muungano na yasiyo ya muungano.

g) Wizara ya mambo ya ndani ya nchi, humu pia kuna mchanganyiko. Faini anayopigwa mtanganyika kwa kuvuka taa nyekundu kwenye taa mpya pale Mianzini arusha, faini hiyo inavuka kwenda Zanzibar kwa sababu ni wizara ya muungano, lakini faini za zanzibar, hizi hazivuki kuja Tanganyika.

h) Wizara ya Nishati na Madini, hii ni ya Tanzania Bara pekee lakini TPDC inafanya kazi kimuungano.
Kumbuka, vyanzo vya mapato ya kuendesha muungano yamegawanyika katika makundi mawili:

1. Mapato yatokanayo na kodi. Humu kumejaa utata mwingi sana juu ya makusanyo ya wapi yanapelekwa wapi.
2. Mapato yasiyotokana na kodi. Haya tumejadili hapo juu, faini za polisi, mahakama, brela, etc.

Awali tuliona majukumu ya JFC kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977). Kama tupo pamoja hadi hapa, je JFC itaweza vipi kuchambua mapato na matumizi yanayohusu utekelezaji wa masuala ya muungano wakati yapo mapato chini ya wizara zisizo za muungano bali za Tanzania Bara lakini wizara hizi zina sura ya ki muungano? Mapato ya aina hii yanazidi shilingi Trilioni moja kila mwaka.

Natumaini Barubaru umepata majibu kwa swali lako ambalo huwa unalirudia sana. Ningeomba kuanzia sasa tusaidiane kuyaweka haya wazi, lakini muhimu zaidi, kuhimiza juu ya haja ya Tanganyika kuzinduka.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi ahsante sana kwa ufafanunuzi. Hoja ya JFC inatumiwa kufidia mapungufu na kukwepa ukweli.
Tumeuliza sana, kama znz haichangii kwasababu hakuna JFC,ni mfuko gani unaoiwezesha kupata 4.5% ambayo sasa imepanda na kuwa 7%. Hakuna anayekuja na jibu, wanarudia hoja ile ile dhaifu

Tumeuliza, kwasasa znz inapata Bilioni 1.75 kwa mwezi. Je, zinatoka mfuko gani wa pamoja? Hakuna jibu, wanarudi na hoja ile ile isiyo na maana kwasababu hawana majibu.

Tumeuliza, watimishi wa muungano wanalipwa na frdha kutoka mfuko gani wa pamoja? Hakuna jibu, wanarejea hoja wanayojua haina mashiko.

Tunauliza, zile pesa za kusaidia bajeti ya znz kutoka JMT zinatoka mfuko gani? Hakuna jibu, wameshikilia pale wasipo na jibu

Inapofika wakati wa kudai masilahi wznz ni wazuri sana wa kuumba na kudai. Wakati wa kuwajibika, hukimbilia hoja za kipuuzi kama hii ya JFC.

Kwa mtu mwenye akili angejiuliza

Na mwisho, tumewauliza formuala gani zinatumika kwa znz kupata mafao ya muungano, ambazo haziwezi kutumika katika kuchangia muungano? Hakuna jibu, wanasema misaada na mikopo. Tumewaonyesha ni kiasi gani znz inapata kutoka muungano bila kujua kwanini na kwa njia gani. Hawana jibu, wanaturudisha kule kule kule wasiko na mjibu

Ni kwa msingi huo, utawasikia wznz wakizungumzia kugawana vyeo, kupata nafasi zaidi kwasababu mentally wanaaamini kuwa huu muungano unajiendesha kwa solar energy, na wajibu wa kuhudumia hiyo solar system ni wa Tanganyika.
Wao wanawajibu wa kukusanya tu.

Kwa sasa tunawaambia Watanganyika lazima mambo yatenge, na shughuli zishsughuikiwe na nchi husika. Tanganyika irudi, znz ikae kama mshirika mwenza katika kuzungumzia nafasi yake ndani ya muungano na si nani anakuwa spika, waziri au vyeo. Lazima znz wawajibike katika muungano katika kuuendeleza, si kufanya Tanganyika shamba la mavuno.

Hakuna haki isiyo na wajibu, na waznz sasa ni wakati watambue kuwa Watanganyika wamechoka si kuudumia muungano peke yao bali pia uzito walioubeba ambao return yajke ni questionable
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom