Duru: UKAWA njia panda, CCM maji ya shingo

Mkuu Mag3
Takribani mwezi mmoja, Jaji Warioba alisimama na kusema zoezi halitawezekana.

Alitoa sababu za kisheria, kwamba muda wa elimu ya umma na kampeni havitafuata sheria.
Hilo ni baada ya kulazimishwa kura ya maoni


Jaji Lubuva alipaswa kumsikiliza Jaji mwenzake. Hapana! Akaamua kufuata maagizo tu hata pale ukweli ulipodhihiri.

Akaacha kutumia hekma za taaluma yake, au hesabu za kawaida na kubaki kusema ‘ndiyo mzee'


Makundi ya wazee kama akina Bomani yalimuonya kwa njia mbalimbali yakisema mchakato ulishavurugwa.
Jaji Lubuva hakuwasikiliza


Mwezi uliopita, ilikuwa wazi hakuna kura ya maoni kwaababu zaidi ya 100.

Jaji alisimama mbele ya kusema ‘zoezi linakwenda vema, tumemaliza Njombe kwa mafanikio,tumejifunza.
Tunategemea vifaa Zaidi na ikifika April 30 zoezi litakamilika'

Jaji Lubuva hakufikiria mfumo huo mpya unahitaji uhakiki, alifikiri kumfurahisha ‘mfalme'

Ni jaji Lubuva aliyepanda ndege kwenda Kenyana Nigeria kuazima BVR.

Masikini Jaji hakujua BVR ni kitu na mfumo endelevu, kwamba unahitajika kila siku.

Jaji hakuweza kupata habari kuwa Nigeria walikuwa na uchaguzi na walihitaji BVR


Hilo tu linaonyesha Jaji Lubuva alivyo out of touch na duniaya leo.

Wenzake wakamchagiza kisiasa,mambo ni mazuri. Kila wakati mtoa taarifa alikuwa Rais, Jaji akipokea maagizo

Kimenuka wenzake wamemkimbia, wanamwachia zigo atangaze jinsi alivyofeli, na kweli akatangaza

Na si kufeli tu bali jinsi asivyojua kazi wala anachokifanya.

Haiwezekani wiki mbili tatu zilizopita asema ‘kwa mafanikio, kisha anakuja kusema tumefeli'
Hakuna aibu kubwa kama hiyo.

Jaji anapaswa kuangalia jinsi alivyoburuzwa, heshima ilivyopotea na kama anasababu za kuendelea kulitumikia taifa tena


Haiwezekani mtu aliyeonyesha udhaifu, ubutu na uwezo kama wa Jaji kuendelea kusimamia tume ya uchaguzi.

Hivi hata matokeo ya kuchagua kiranja mkuu wa sekondari, Jaji anaweza kutangaza watu wakamwamini tena!!
Seuse Uchaguzi mkuu Oktoba


Rai yetu kwa Jaji , wenzake wamemtosa na amebeba mzigo asiostahili . Jaji ameshindwa na taifa limefeli mikononi mwake.

Hana sababu za kuendelea na uenyekiti wa tume ya uchaguzi.

Tayari ni felia hatuwezi kusubiri felia nyingine inayoweza kulitumbukiza taifa katika hali ya hatari

Jaji Lubuva ni wakati sasa ‘pack and go' Unless una dhiki nyingine, hatuamini kama unasababu za kuendelea na kazi

Aibu na fedheha iliyokukumba inatosha, ni muda sasa ulinde heshima ya wajukuu wako watakaotumia jina lako.

Hutawatendea haki wajukuu, ikiwa jina lako litaendelea kunasibishwa na uchafu, dhalili na fedheha inayokukabili sasa.

Jaji ondoka, umelitia taifa aibu ya BVR na sasa aibu nyingine! Tulindie heshima ya taifa letu. Umefeli kikamlifu



 
MAAZIMIO YA KMATI KUU YA CHADEMA

MAPUNGUFU YA TAMKO LAO NA HATARI INAYOWAKABILI

sehemu ya I

Jana kamati kuu ya Chadema imetoa tamko baada ya kkao chao. Pamoja na mambo mengine, kamati kuu imeongelea suala la katiba inayopendekezwa kuahirishwa hadi baada ya uchaguzi.

Kauli hiyo ima haikuandaliwa kifundi au imetolewa kama sehemu ya kuwa njia panda kama bandiko linavyosema.
Turejee tamko hilo kwanza



KWANINI TUNAONA TATIZO KATIKA TAMKO HILI?

Inaendelea sehemu ya II

 
Sehemu ya II

Kama inavyumbukwa, UKAWA wakiwemo Chadema walitoka nje ya bunge maalumu la katiba kama hatua ya kupinga na kutoshiriki mchakato uliovurugwa na CCM.

Hiyo ililazimisha katiba ya CCM kususiwa na wananchi, uandikishaji kusuasa sua na mwisho kuahirishwa

Hoja kubwa ya wapinzani ni kudharauliwa kwa maoni ya wananchi, na kuingizwa katiba ya CCM.
Pia, ni kushinikiza CCM warudi katika ramani 'map' iliyokusudia katiba ya wananchi na si kikundi cha watu

Tume ya Warioba na wananchi wamesimama kidete katika rasimu, kutetea msimamo wa kurudi kwenye rasimu

Tunakumbuka pia, UKAWA walihamasisha ususiaji wa katiba pendekezwa ya CCM, wito uliotikiwa na wananchi

Hadi sasa katiba pendekezwa imekosa hamasa, msisimko na kupoteza maana nzima ya uandikaji wa katiba

Hayo yamewezekana kwasababu wananchi wapo nyuma ya UKAWA wakiamini kwa dhati, katiba inayopendekezwa si yao ni ya wana CCM na kwamba mchakato mzima ulivurugwa.

Tunakumbuka sheria ya mchakato imeeleza hatua na muda wa shughuli za zoezi ikiwemo elimu kwa umma, uandikishaji na upigaji kura. Pamoja na kuvurugwa kuna sababu za kisheria zinazozuia mchakato haramu usiendelee

Kwa maana nyingine 'haramu' imezidi kuwa haramu kwasababu kisheria hakuna jambo linaloweza kufanyika bila kubadili sheria. Muda wa rais kutangaza kura ya maoni iumepita, elimu ya umma na uandikishaji umepita. Hii maana yake ni kuwa haramu imezidi kuwa 'haramu'

Hakuna uwezekano wa 'haramu' ya katiba kuendelea kwasababu kisheria haikubaliki.


TATIZO LA KAULI YA KAMATI KUU YA CHADEMA

Zipo njia za kuifanya 'haramu' iwe 'haramu' kidogo

1. Kurudi katika bunge la JMT na kurekebisha sheria ili muda wa kura ya maoni utangazwe,uandikishaji umalizwe,muda wa elimu ya umma utangazwe.

Hapo ni kurudi katika ubao kuanza upya hata kama haramu itapendekezwa kwa nguvu.

2. Kufuta kabisa katiba pendekezwa na kurudi kwenye rasimu

3. Kufuta zoezi zima na kuliandaa upya

Katika hayo matatu, hakuna hata moja linalotambua katiba pendekezwa.

Inaendelea.....
 
Sehemu ya II


KATIBA PENDEKEZWA NI 'OFF THE TABLE ab initio''

Tunaweza kusema kwa dhati kuwa nia ya UKAWA NA CDM wakwemo ilikuwa
1. Kususia mchakato mbovu
2. Kutotambua katiba pendekezwa
3. Kususia zoezi zima litalozaa katiba mbovu, isiyo ya wananchi na iliyoandaliwa na CCM

Kwa mantiki hiyo suala la katiba pendekezwa ni kando ya meza ya agenda (off the tabel) kwa kuanza hapo tu

KAMATI KUU CHADEMA

Ukisoma tamko la kamati kuu ya Chadema hapo juu, linasema katika vipengele kama ifuatavyo
1. Kichwa cha habari 'Kuhusu kura ya maoni''

Inashangaza kuwa suala la katiba pendekezwa limeweza kuwa katika agenda ya kikao cha kamati kuu yao

Kwa kuanzia , hiyo haikuwa agenda yao kuanzia walipotoka katika BMLK, waliohamasisha wananchi kususia na walipokuwa na msimamo na UKAWA kwa pamoja.

Ni makosa makubwa kwamba suala la katiba pendekezwa lilipewa hata nafasi na suala la kura ya maoni lilijadiliwa. Kura ipi ya maoni?

2. ''Mwendendo wa kisiasa na kiuchumi hauruhusu kura ya maoni ya katiba inayopenekezwa''

Maana yake ni kuwa kama hali ingekuwa nzuri kidogo kisiasa na kicuhumi, Chadema wangefikiria kura ya maoni ya katiba pendekezwa, kura ya kile walichosema ni haramu!

Kura ya maoni ya katiba ipi penekezwa CDM walioshiriki?

3. ''...Isipokuwa hadi baada ya uchaguzi mkuu wa Oktober 2015 kwa mujibu wa katiba''
Yaani wanapendekeza katiba ya Cheng' ifikiriwe baada ya uchaguzi mkuu.
Kwamba, sasa wanaanza kufikiria katiba ya CCM kwa kuipa uhalali taratibu.

Ni makosa makubwa sana
Hivi uchaguzi ukiisha na CCM wakaja na katiba yao kama watakuwa madarakani, wakisema wanafuata mapendekezo ya kamati kuu ya CDM, Kamati kuu ya CDM na CDM watajibu nini

4, Kamati kuu imeazimia kwenda na msimamo wa UKAWA kuwa kura ya maoni isifanyike na uchaguzi mkuu

Ni makosa kutaja kura ya maoni, na ni makosa makubwa kufikiria kuwa pamoja na uchaguzi mkuu.

Pengine wangesema kura ya maoni haipo, uchaguzi mkuu ufanyike wenyewe.
Kwamba hawakubali kura ya maoni kwanza, na hivyo isiunganishwa na uchaguzi mkuu.

5. ''Lakini kwa vyovyote vile kura ya maoni iwe baada ya uchaguzi mkuu''

Hapa ina maana tayari wameshaanza kuikubali katibapendekezwa, tatizo lao ni muda tu.


Inaendelea....
 
Sehemu ya IV

Hoja:

Tamko la kamati kuu ya CDM linatia shaka. Haieweki kwanini suala la kura ya maoni na katiba pendekezwa, waliosusia wakiwa ndani ya UKAWA liwe agenda ya kikao cha kamati kuu

Agenda ingekuwa rahisi, hawaitambui katiba pendekezwa na hawatambui hatua zote zinazofuata za kuhalalisha katiba hiyo.

Katika kipengele hicho, CDM hawaonekani kuwa makini

Kitendo cha kutosimama eneo moja, kinatoa fursa kwa CCM kuendelea na katiba ikiwa tayari walishakubali kuwa zoezi hilo limekosa uhalali wa kisiasa kwa kigezo chochote kile

Bandiko hili tulisema CCM maji ya Shingo, na sote tumeona maji yalivyokuwa marefu hadi kukubali kuacha zoezi lililolazimishwa na mzee wa Urambo na wenzake kwa rushwa, na kila aina ya uhalifu

Tulisema wapinzani wapo njia panda. Kwamba hawaoni mitego wanayotegewa.
Hili la tamko la CDM ni moja ya njia panda tulizoeleza

Katika mazingira haya, Chadema watoke mbele na kufafanua kuhusu tamko lao katika kipengele cha kura ya maoni.

Hilo litawasaidia na kusaidia upinzani kwa ujumla kujua wanasimama wapi na wanaelekea wapi

Kinyume chake, tutashuhudia Rais Mwingine akija na kuwaita kunywa juice ya maembe na baada ya hapo watatoka na msimamo wa Rais huyo kama atakuwa si wa upande wao.

Kamati kuu ya Chadema, kauli yenu ni tata tokeni mbele mueleze umma nini mlifikiria
Tamko lina mapungufu mengi na mazito

Tusemezane
 
Ndiomana Tunasema CDM ni walaghai tu,mfano wao walisema wamesusia kura ya maoni,sababu mchakato haramu,lakini wamekuwa wanajadili Tarehe ya kura ya Maoni,mfano Hotuba ya Mbowe katika bunge la bajeti tarehe 12 May 2015
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…