Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #61
Mkuu Mag3
Takribani mwezi mmoja, Jaji Warioba alisimama na kusema zoezi halitawezekana.
Alitoa sababu za kisheria, kwamba muda wa elimu ya umma na kampeni havitafuata sheria.
Hilo ni baada ya kulazimishwa kura ya maoni
Jaji Lubuva alipaswa kumsikiliza Jaji mwenzake. Hapana! Akaamua kufuata maagizo tu hata pale ukweli ulipodhihiri.
Akaacha kutumia hekma za taaluma yake, au hesabu za kawaida na kubaki kusema ‘ndiyo mzee'
Makundi ya wazee kama akina Bomani yalimuonya kwa njia mbalimbali yakisema mchakato ulishavurugwa.
Jaji Lubuva hakuwasikiliza
Mwezi uliopita, ilikuwa wazi hakuna kura ya maoni kwaababu zaidi ya 100.
Jaji alisimama mbele ya kusema ‘zoezi linakwenda vema, tumemaliza Njombe kwa mafanikio,tumejifunza.
Tunategemea vifaa Zaidi na ikifika April 30 zoezi litakamilika'
Jaji Lubuva hakufikiria mfumo huo mpya unahitaji uhakiki, alifikiri kumfurahisha ‘mfalme'
Ni jaji Lubuva aliyepanda ndege kwenda Kenyana Nigeria kuazima BVR.
Masikini Jaji hakujua BVR ni kitu na mfumo endelevu, kwamba unahitajika kila siku.
Jaji hakuweza kupata habari kuwa Nigeria walikuwa na uchaguzi na walihitaji BVR
Hilo tu linaonyesha Jaji Lubuva alivyo out of touch na duniaya leo.
Wenzake wakamchagiza kisiasa,mambo ni mazuri. Kila wakati mtoa taarifa alikuwa Rais, Jaji akipokea maagizo
Kimenuka wenzake wamemkimbia, wanamwachia zigo atangaze jinsi alivyofeli, na kweli akatangaza
Na si kufeli tu bali jinsi asivyojua kazi wala anachokifanya.
Haiwezekani wiki mbili tatu zilizopita asema ‘kwa mafanikio, kisha anakuja kusema tumefeli'Hakuna aibu kubwa kama hiyo.
Jaji anapaswa kuangalia jinsi alivyoburuzwa, heshima ilivyopotea na kama anasababu za kuendelea kulitumikia taifa tena
Haiwezekani mtu aliyeonyesha udhaifu, ubutu na uwezo kama wa Jaji kuendelea kusimamia tume ya uchaguzi.
Hivi hata matokeo ya kuchagua kiranja mkuu wa sekondari, Jaji anaweza kutangaza watu wakamwamini tena!!
Seuse Uchaguzi mkuu Oktoba
Rai yetu kwa Jaji , wenzake wamemtosa na amebeba mzigo asiostahili . Jaji ameshindwa na taifa limefeli mikononi mwake.
Hana sababu za kuendelea na uenyekiti wa tume ya uchaguzi.
Tayari ni felia hatuwezi kusubiri felia nyingine inayoweza kulitumbukiza taifa katika hali ya hatari
Jaji Lubuva ni wakati sasa ‘pack and go' Unless una dhiki nyingine, hatuamini kama unasababu za kuendelea na kazi
Aibu na fedheha iliyokukumba inatosha, ni muda sasa ulinde heshima ya wajukuu wako watakaotumia jina lako.
Hutawatendea haki wajukuu, ikiwa jina lako litaendelea kunasibishwa na uchafu, dhalili na fedheha inayokukabili sasa.
Jaji ondoka, umelitia taifa aibu ya BVR na sasa aibu nyingine! Tulindie heshima ya taifa letu. Umefeli kikamlifu
Takribani mwezi mmoja, Jaji Warioba alisimama na kusema zoezi halitawezekana.
Alitoa sababu za kisheria, kwamba muda wa elimu ya umma na kampeni havitafuata sheria.
Hilo ni baada ya kulazimishwa kura ya maoni
Jaji Lubuva alipaswa kumsikiliza Jaji mwenzake. Hapana! Akaamua kufuata maagizo tu hata pale ukweli ulipodhihiri.
Akaacha kutumia hekma za taaluma yake, au hesabu za kawaida na kubaki kusema ‘ndiyo mzee'
Makundi ya wazee kama akina Bomani yalimuonya kwa njia mbalimbali yakisema mchakato ulishavurugwa.
Jaji Lubuva hakuwasikiliza
Mwezi uliopita, ilikuwa wazi hakuna kura ya maoni kwaababu zaidi ya 100.
Jaji alisimama mbele ya kusema ‘zoezi linakwenda vema, tumemaliza Njombe kwa mafanikio,tumejifunza.
Tunategemea vifaa Zaidi na ikifika April 30 zoezi litakamilika'
Jaji Lubuva hakufikiria mfumo huo mpya unahitaji uhakiki, alifikiri kumfurahisha ‘mfalme'
Ni jaji Lubuva aliyepanda ndege kwenda Kenyana Nigeria kuazima BVR.
Masikini Jaji hakujua BVR ni kitu na mfumo endelevu, kwamba unahitajika kila siku.
Jaji hakuweza kupata habari kuwa Nigeria walikuwa na uchaguzi na walihitaji BVR
Hilo tu linaonyesha Jaji Lubuva alivyo out of touch na duniaya leo.
Wenzake wakamchagiza kisiasa,mambo ni mazuri. Kila wakati mtoa taarifa alikuwa Rais, Jaji akipokea maagizo
Kimenuka wenzake wamemkimbia, wanamwachia zigo atangaze jinsi alivyofeli, na kweli akatangaza
Na si kufeli tu bali jinsi asivyojua kazi wala anachokifanya.
Haiwezekani wiki mbili tatu zilizopita asema ‘kwa mafanikio, kisha anakuja kusema tumefeli'Hakuna aibu kubwa kama hiyo.
Jaji anapaswa kuangalia jinsi alivyoburuzwa, heshima ilivyopotea na kama anasababu za kuendelea kulitumikia taifa tena
Haiwezekani mtu aliyeonyesha udhaifu, ubutu na uwezo kama wa Jaji kuendelea kusimamia tume ya uchaguzi.
Hivi hata matokeo ya kuchagua kiranja mkuu wa sekondari, Jaji anaweza kutangaza watu wakamwamini tena!!
Seuse Uchaguzi mkuu Oktoba
Rai yetu kwa Jaji , wenzake wamemtosa na amebeba mzigo asiostahili . Jaji ameshindwa na taifa limefeli mikononi mwake.
Hana sababu za kuendelea na uenyekiti wa tume ya uchaguzi.
Tayari ni felia hatuwezi kusubiri felia nyingine inayoweza kulitumbukiza taifa katika hali ya hatari
Jaji Lubuva ni wakati sasa ‘pack and go' Unless una dhiki nyingine, hatuamini kama unasababu za kuendelea na kazi
Aibu na fedheha iliyokukumba inatosha, ni muda sasa ulinde heshima ya wajukuu wako watakaotumia jina lako.
Hutawatendea haki wajukuu, ikiwa jina lako litaendelea kunasibishwa na uchafu, dhalili na fedheha inayokukabili sasa.
Jaji ondoka, umelitia taifa aibu ya BVR na sasa aibu nyingine! Tulindie heshima ya taifa letu. Umefeli kikamlifu