Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #41
KATIBA: CCM YABANWA KULIA KUSHOTO
TAMKO LA JUMUIYA YAKIKISTO LINA WALAKINI
SERIKALI IMEFUNDISHA''WANAFUNZI WANAJIBU''
Sehemu ya I
Jumuiya za dini ya Waislam zilitoa matamko kuhusu katiba. Zilisemasuala la kadhi lisipokuwepo kikatiba, watahamasisha waumini wasusie kura yamaoni ya katiba ya Chenge
Jumuiya ya kikrsito imetoa tamko likihimiza kuikataa katibaya Chenge wakati wa kura za maoni
Wapo takaolaumu viongozi wa dini kuchanganya dini na siasa.
Serikali ndio iliyo asisi msemo huo. Ni makosa kuzilaumujumuiya za dini kutoa maoni.
Inapotokea waziri katika serikali yupo kanisaniakizungumzia katiba, hatutegemei waumini wakae kimya.
Tamko la jumuiya zakikristo ni majibu ya mafunzo yaliyotolewa kanisani na akina Lukuvi
CCM wanapotoa ahadi za mahakama ya kadhi ili kupata kura,hatutarajii waumini wakae kimya.
Matamko ya jumuiya za kiislam ni majibu kutokana na mafunzo ya CCM
Hivyo, ni vema kusema, serikali imewafundisha na sasawanafunzi wanajibu somo.
Waziri mkuu
Katika kuhaha ili katiba iungwe mkono, waziri mkuu amesema suala la mahakama ya kadhi linarudi tena bungeni.
Hii ni baada ya kubanwa upande mmoja. Kabla halijarudi bungeni wengine wanaona ni suala la kuligawa taifa.
Ni haki kusema, serikali imebanwa kulia na kushoto. Haina pakutokea na ujanja na ubabe wa katiba sasa unaiumiza. Imebanwa kulia na kushoto
TAMKO LA JUMUIYA ZA KIKRISTO
Tamko la jumuiya limekuja miezi mingi baada ya katiba yaChenge kusukumizwa kwa hila na mbinu.
Katika tamko, jumuiya zinasema hakukuwa na uadilifu, nchi imegawanyika hasa likisisitiza kuhusu mahakama ya kadhi.
Jumuiya inasema, serikali inalitumia suala hilo kama hongo na mchakato mzimaulikosa uadilifu
Tamko hilo linaendelea kusisitiza kuwa wananchiwajiandikishe, washiriki mchakato mzima, wasome katiba na kuielewa na mwisho wapige kura ya hapana
Kwa maoni ya duru za siasa, tamko la jumuiya za kikristo lina walakini.
Kwanza, jumuiya haikuunga mkono wapinzani wakati uhuni wa mswadawa sheria ya kuanzisha mchakato ilipoanza.
Wapinzani walisema, bunge la katibaliwe na wabunge watakaochaguliwa kutoka katika makundi ya jamii na si 201watakaoteuliwa na Rais
Lengo la wpinzani lilikuwa kuhakikisha makundi ya jamii yanachagua watu watakao simamia masilahi yao kwa upana Kilichotokea, sheria ikampa Rais kuchagua wabunge.
Kwa muda wote huo si jumuiya ya wakristo auwaislam walioonyesha kukerwa na hilo.
Kwa uoande wa waislam, walikuwepo masheikh wa jumuiya ziizonje ya Bakwata na wale wa Bakwata.
Kwa upande wa wakristo nako walikuwepo wa jumuiya kubwa yawakatoliki na wale wa kiprotestant
Makundi yote mawili hayana uadilifu wa kuhoji uadilifu wabunge wakati yalikaa kimya wakati uadilifu unachakachuliwa!
Makundi yote mawili yaliungana kuandika waraka wa kulaani UKAWA na kuunga mkono mchakato.
Hakuna taasisi ya nje si ya waislam au wakristo iliyowakemea kwa kununuliwa.
Leo matamko yanahusu nini? Hawa watu wa dini hawakuona ukosefu wa maadili kuanzia mwanzo
Inaendelea II
TAMKO LA JUMUIYA YAKIKISTO LINA WALAKINI
SERIKALI IMEFUNDISHA''WANAFUNZI WANAJIBU''
Sehemu ya I
Jumuiya za dini ya Waislam zilitoa matamko kuhusu katiba. Zilisemasuala la kadhi lisipokuwepo kikatiba, watahamasisha waumini wasusie kura yamaoni ya katiba ya Chenge
Jumuiya ya kikrsito imetoa tamko likihimiza kuikataa katibaya Chenge wakati wa kura za maoni
Wapo takaolaumu viongozi wa dini kuchanganya dini na siasa.
Serikali ndio iliyo asisi msemo huo. Ni makosa kuzilaumujumuiya za dini kutoa maoni.
Inapotokea waziri katika serikali yupo kanisaniakizungumzia katiba, hatutegemei waumini wakae kimya.
Tamko la jumuiya zakikristo ni majibu ya mafunzo yaliyotolewa kanisani na akina Lukuvi
CCM wanapotoa ahadi za mahakama ya kadhi ili kupata kura,hatutarajii waumini wakae kimya.
Matamko ya jumuiya za kiislam ni majibu kutokana na mafunzo ya CCM
Hivyo, ni vema kusema, serikali imewafundisha na sasawanafunzi wanajibu somo.
Waziri mkuu
Katika kuhaha ili katiba iungwe mkono, waziri mkuu amesema suala la mahakama ya kadhi linarudi tena bungeni.
Hii ni baada ya kubanwa upande mmoja. Kabla halijarudi bungeni wengine wanaona ni suala la kuligawa taifa.
Ni haki kusema, serikali imebanwa kulia na kushoto. Haina pakutokea na ujanja na ubabe wa katiba sasa unaiumiza. Imebanwa kulia na kushoto
TAMKO LA JUMUIYA ZA KIKRISTO
Tamko la jumuiya limekuja miezi mingi baada ya katiba yaChenge kusukumizwa kwa hila na mbinu.
Katika tamko, jumuiya zinasema hakukuwa na uadilifu, nchi imegawanyika hasa likisisitiza kuhusu mahakama ya kadhi.
Jumuiya inasema, serikali inalitumia suala hilo kama hongo na mchakato mzimaulikosa uadilifu
Tamko hilo linaendelea kusisitiza kuwa wananchiwajiandikishe, washiriki mchakato mzima, wasome katiba na kuielewa na mwisho wapige kura ya hapana
Kwa maoni ya duru za siasa, tamko la jumuiya za kikristo lina walakini.
Kwanza, jumuiya haikuunga mkono wapinzani wakati uhuni wa mswadawa sheria ya kuanzisha mchakato ilipoanza.
Wapinzani walisema, bunge la katibaliwe na wabunge watakaochaguliwa kutoka katika makundi ya jamii na si 201watakaoteuliwa na Rais
Lengo la wpinzani lilikuwa kuhakikisha makundi ya jamii yanachagua watu watakao simamia masilahi yao kwa upana Kilichotokea, sheria ikampa Rais kuchagua wabunge.
Kwa muda wote huo si jumuiya ya wakristo auwaislam walioonyesha kukerwa na hilo.
Kwa uoande wa waislam, walikuwepo masheikh wa jumuiya ziizonje ya Bakwata na wale wa Bakwata.
Kwa upande wa wakristo nako walikuwepo wa jumuiya kubwa yawakatoliki na wale wa kiprotestant
Makundi yote mawili hayana uadilifu wa kuhoji uadilifu wabunge wakati yalikaa kimya wakati uadilifu unachakachuliwa!
Makundi yote mawili yaliungana kuandika waraka wa kulaani UKAWA na kuunga mkono mchakato.
Hakuna taasisi ya nje si ya waislam au wakristo iliyowakemea kwa kununuliwa.
Leo matamko yanahusu nini? Hawa watu wa dini hawakuona ukosefu wa maadili kuanzia mwanzo
Inaendelea II