Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #321
gfsonwin
Suala la kwenda mahakamani linawezekana, lakini pia uangalie mfumo uliopo unatoa nafasi?
Jitihada za kuzima sauti si suala la bahati mbaya, ni suala lenye mkakati mkubwa kimfumo
Kama utakumbuka, bunge lilizuiliwa kuoneyshwa na Nape Nnauye kwa maagizo ya serikali ambayo leo anaweza kutazama nyuma na kubaini alichofanya kilikuwa na athari kiasi gani katika jamii
Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi katika chombo huru wanakamatwa katika mazingira ya kusikitisha, wanaandamwa waliko ilimradi tu kuhakikisha kuna kuogofya
Hata dhamana , jambo la kawaida kisheria limechukua mwelekeo wa kisiasa. Mahakama!
Ikaja kwa wanasheria wakiambiwa uwakili unafanywa kwa 'baadhi' mengine ni tatizo
Tukasikia hoja kuhusu mambo ya sheria zilizoleta utata sana
Ukabakia mhimili usio rasmi wa medium. Huu umeonekana ni mwiba kwa kusema yasiyotakiwa
Ikatukumbusha zama hizo ukifungua Kenya (KBC) habari ni za mtukufu Rais Moi
Na zama za RTD, Uhuru na Mzalendo. Kwamba, habari ni mambo mazuri tuu kila kitu sawia
Tukakwenda mbali kidogo kwa kuingia vituo vya matangazo kushinikiza habari tunazotaka
Hilo linaonekana ''kukubalik'' Waziri alipochukua hatua hakuchukua muda akaondolewa
Waziri aliyeingia anasema hana habari kuhusu tukio, na hawezi kuliongelea
Tumemsikia akiongelea video ya Ney wa Mitego na kwamba kauli imetoka aachiwe
BASATA wenye jukumu walipiga marufuku, Polisi walimkamata kwa kutenda kosa
Unaweza ona, kwamba, waziri anaweza kushughulikia Ney na hana 'habari' kamili za Clouds
Habari za clouds ni nzito, ni tukio la kwanza , hatukuzoea na lilitisha tasnia ya habari
Medium zimeonywa ziandike habari za maendeleo, hatujui hili la Ney ni sehemu yake au la
Ukitazama kwa undani, mfumo mzima hautoi nafasi kwa taasisi kufanya kazi.
Unategemea maelezo.Unaposema watu waende mahakamani factors zingine unaziangaliaje?
Bila kubadili mfumo wa sasa unaotoa nguvu zaidi ya kipimo, popote panapofikiriwa, nguvu ina nguvu
Tusemezane
Suala la kwenda mahakamani linawezekana, lakini pia uangalie mfumo uliopo unatoa nafasi?
Jitihada za kuzima sauti si suala la bahati mbaya, ni suala lenye mkakati mkubwa kimfumo
Kama utakumbuka, bunge lilizuiliwa kuoneyshwa na Nape Nnauye kwa maagizo ya serikali ambayo leo anaweza kutazama nyuma na kubaini alichofanya kilikuwa na athari kiasi gani katika jamii
Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi katika chombo huru wanakamatwa katika mazingira ya kusikitisha, wanaandamwa waliko ilimradi tu kuhakikisha kuna kuogofya
Hata dhamana , jambo la kawaida kisheria limechukua mwelekeo wa kisiasa. Mahakama!
Ikaja kwa wanasheria wakiambiwa uwakili unafanywa kwa 'baadhi' mengine ni tatizo
Tukasikia hoja kuhusu mambo ya sheria zilizoleta utata sana
Ukabakia mhimili usio rasmi wa medium. Huu umeonekana ni mwiba kwa kusema yasiyotakiwa
Ikatukumbusha zama hizo ukifungua Kenya (KBC) habari ni za mtukufu Rais Moi
Na zama za RTD, Uhuru na Mzalendo. Kwamba, habari ni mambo mazuri tuu kila kitu sawia
Tukakwenda mbali kidogo kwa kuingia vituo vya matangazo kushinikiza habari tunazotaka
Hilo linaonekana ''kukubalik'' Waziri alipochukua hatua hakuchukua muda akaondolewa
Waziri aliyeingia anasema hana habari kuhusu tukio, na hawezi kuliongelea
Tumemsikia akiongelea video ya Ney wa Mitego na kwamba kauli imetoka aachiwe
BASATA wenye jukumu walipiga marufuku, Polisi walimkamata kwa kutenda kosa
Unaweza ona, kwamba, waziri anaweza kushughulikia Ney na hana 'habari' kamili za Clouds
Habari za clouds ni nzito, ni tukio la kwanza , hatukuzoea na lilitisha tasnia ya habari
Medium zimeonywa ziandike habari za maendeleo, hatujui hili la Ney ni sehemu yake au la
Ukitazama kwa undani, mfumo mzima hautoi nafasi kwa taasisi kufanya kazi.
Unategemea maelezo.Unaposema watu waende mahakamani factors zingine unaziangaliaje?
Bila kubadili mfumo wa sasa unaotoa nguvu zaidi ya kipimo, popote panapofikiriwa, nguvu ina nguvu
Tusemezane