Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

Mkandara,

Ulichoongea ni sawia kabisa ila NILICHOTAKA UJUE KUWA HATA ULE MKATABA WA MUUNGANO ILIBIDI URIDHIWE NA BLM WAKTI ULE ILI UWE SHARIA KULE ZNZ. Sasa kwa vile mpaka leo haujaridhiwa hivyo ni batili kisharia kutumika Znz.

Hivyo Znz wana haki kamili kufanya chochote kile bila kuogopa muungano. na hawapaswi kulipia muungano kwani wao SI MIONGONI MWENU. vile vile

Lakin kumbuka mahakama ya rufaa ni sehemu ya mvungano wenu.








Balaza la Mapinduzi mwaka 1964 walikuwa na wajumbe wangapi na kina nani? Naomba majina yao kisha nambie ktk hawa nani hakushirikishwa!

Jambo moja kubwa sana nimeligundua ni kwamba kumbe Watanzania wengi pamoja na viongozi wa leo hawafahamu kabisa mfumo wa Muungano wetu. Na ndio maana hukwaza na hili la Nchi 1 serikali 2. Hili pekee ni Catch 22 kwao. Hawajui tofauti zilizopo kati ya shughuli za JMT na shughili za Serikali ya Mapinduzi na kwa nini ilikuwa hivyo. Hawajui mapana ya serikali ya Muungano wa Tanzania, hili ni somo jipya kwa viongozi na wananchi kwa ujumla.
 
SAMUEL SITTA NA UFUFUO WA TANGANYIKA

SEHEMU YA PILI

Katika sehemu ya kwanza, tulijadili kwamba hoja ya G55 ilikuja katika versions tatu tofauti na sio moja kama wengi wanavyofikiri. Ufahamu juu ya ukweli huu ni muhimu ili kujua jinsi gani serikali ilifanikiwa kuidhibiti hoja hii (tofauti na mkakati wa ccm uliotumia hoja kwamba serikali tatu haikuwa ni sera ya ccm).

Baada ya kujadili hizi versions za Hoja ya G55,ni muhimu kujikumbusha matukio kadhaa yaliyojiri kipindi kile:
Kati ya tarehe 30 july siku ambayo hoja ya G55 ilipoibuliwa kwa mara ya kwanza, na tarehe 24 agosti 1994 ilipokuwa adopted na bunge, zanzibar ilijitoa OIC. Pakatokea pia makubaliano kwamba rais wa znz ataacha kuwa makamo wa rais wa jmt na badala yake kutakuwa na makamu rais ambae atakuwa running mate wa urais wa muungano na atatokea pande tofati wa muungano na ule anaotokea rais; Mwalimu nyerere alihutubia wabunge huku waziri wa sheria na katiba, samuel sitta akiahidi kuandaa chapisho la government white paper juu ya muungano kwa mujibu wa version ya tatu ya hoja ya G55 ambapo umma ungekaribishwa kuchangia mawazo juu ya mfumo wa muungano, hasa suala la kuirudisha Tanganyika; mikakati yote hii ililenga kuanza ipunguza nguvu motion ya G55 lakini ni dhahiri kwamba kuna Limit ya kiwango cha viongozi kuweza chakachua historia. Umma ukifikia sehemu ukasema "sasa imetosha", suala ambalo chama kiliweza dhibiti kwa miaka hamsini kinaweza badilika kwa nguvu ya umma ndani ya siku chache tu;ushahidi wa hili kwa nchi za wenzetu upo wazi;

Tutazame implications za hoja ya G55:

Professor shivji katika kitabu chake titled "let the people speak: Tanzania down the road to neo-liberalism" anasema kwamba:

Ili kuelewa vyema version ya tatu ya G55, kuna haja ya kujadili kwanza versions 1&2. Shivji anasema kwamba version ya kwanza ambayo ililenga kuanzisha serikali ya tanganyika ilikuwa na unresolvable constitutional and political problems; constitutional problem ya kwanza ni kwamba ile motion ilikuwa ni motion binafsi iliyohoji mfumo wa muungano; kwa maana hii, chini ya ibara ya 98(1) ya katiba ya JMT (1977), ingehitajika robo tatu ya kura ya wabunge wote ili kupitishwa, na possibly robo tatu ya wabunge wa znz na bara (rejea ibara ya 98(1b) ya katika ya JMT 1977, kwa vile motion ililenga marekebisho ya katiba ya nchi(jmt). Katika mazingira yale, shivji anasema kwamba hoja isingeweza kupita kwani kura zisingetosha.

Tatizo la pili la version ya kwanza ni kwamba - kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ingelazimu zaidi ya 70% ya katiba ya JMT (1977) kuandikwa upya; hili lisingewezekana kwani ingekuwa ni karibia sawa na kuandika upya katiba kwani moja ya nguzo kuu za katiba ya jmt (1977) ni mfumo wa serikali mbili, na isitoshe, bunge lile halikuwa na mamlaka ya kufanyia mabadiliko katiba ya jmt kiasi cha kugusa its basic structure (hasa mfumo wa muungano);

Na tatu, mabadiliko ya makubwa ya katiba hasa kuirudisha Tanganyika yangewezekana tu kwa kupitia uandikishaji wa katiba mpya ya JMT; na bunge la jmt (pamoja na rais) halikuwa na nguvu za kikatiba kuandika katiba mpya, nguvu hiyo ingetakiwa itokane na bunge la katiba ambalo mamlaka yake na nguvu zake inatakiwa zitoke moja kwa moja kwa wananchi; katika hili shivji anasema kwamba:

In a republic, the people are the ultimate sovereign and possess the powers to constitute a government for themselves. A constituent assembly therefore is a higher body than the parliament

Kwahiyo, hoja inayofuatia ni kwamba - attempt yoyote ya kubadilisha mfumo wa muungano kwa kufanyia marekebisho katiba ya JMT ingekuwa unconstitutional kwa vile ni kinyume na mkataba wa muungano (1964).

Kulikuwepo tatizo lingine la kisiasa kuhusiana na version ya kwanza ya hoja ya G55. Kwa mfano, je nani aliwapa wabunge mamlaka ya kubadilisha mfumo wa jamhuri ya muungao? Kwani wakati wanachaguliwa, walichaguliwa kwa misingi ya katiba ya katiba ile ile ya 1977. Kwa maana hii, iwapo walikuwa wanahisi katiba ile ilikuwa na mapungufu kimfumo, basi utaratibu wa kikatiba wa kufanikisha hili ulihitaji kuhusisha wananchi ili watumie mamlaka waliyonayo kufanya mabadiliko haya kwani sio serikali wala bunge la JMT vilikuwa na mamlaka makubwa zaidi ya wananchi katika kufanikisha jambo lile; hali hii ikapelekea adoption ya Version ya pili na ya tatu;

Ni dhahiri kwamba wabunge walibaini mapungufu tajwa hapo juu ambayo yalikuwepo ndani ya version ya kwanza; kwahiyo wakaja na version ya pili kurekebisha tatizo hili (rejea huko juu), hasa kwa kuja na nyongeza juu ya kura ya maoni/referendum; hivyo version ya pili ikakatua tatizo pungufu la version ya kwanza na sasa kuwa hoja ambayo inasimama na ipo sahihi "legally and politically"; version hii ya pili kimsingi ilikuwa na mambo muhimu yafuatayo:

Wabunge kama wawakilishi wa wananchi wanaona kwamba kuna mapungufu ya kimsingi ya mfumo wa serikali mbili ambao umezaa malalamiko ya pande zote za muungano na kwamba njia sahihi ya kurekebisha tatizo hili ni kwa kurudisha serikali ya Tanganyika, hivyo kuufanya muungano kuwa ni wa serikali tatu - ya muungano, na mbili zinazosimamia masuala je ya muungano katika kila nchi shiriki - serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar. Kwahiyo wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi wanapendekeza kwa wananchi hoja hii ili wao ndio wawe na maamuzi ya mwisho; kwa mantiki hii, hoja ya G55 ikaelekeza serikali kuandaa "referendum" ambapo, serikali ingeleta bill bungeni na kuipa serikali mamlaka ya kufanya referendum na kuweka sawa mchakato wa kufanikisha zoezi hili;

Bunge na BILL ya referendum:

Simple majority kwa kanuni za wakati ule zingepitisha version ya pili ya G55 na ingekuwa haijaenda kinyume na mkataba wa muungano, 1964; hivyo kisheria hali ingekuwa sawa; kisiasa - pia hali ingekuwa sawa kwani kimsingi, kilichokuwa kitokee ni wawakilishi wa wananchi (wabunge) kurudisha suala hili fundamenta back to the people/demos;

Katika hali hii, issa shivji alipata kuandika kwamba:

...Now many people have misunderstood and others have deliberately mispresented, the significance and content of a referendum. The kind of referendum on the union structure proposed in the second version of necessity is inseparable from a number of other constitutional questions.

...As I have already argued, if three governments are accepted, we would require a new Constitution. The new constitution clearly couldn't stop at simply providing for three governments. The principles which guide the government or governments;its powers; and structure, etc, all would have to be discussed; all this would have to be done afresh in the light of our history; the current circumstances;the utter legal inadequacy of the present constitution and its doubtful political legitimacy and so on; in short we would have to discuss the whole issue of crystallising a national consensus and establishing a new constitutional order.

The most democratic way of doing it would ofcourse be by a process of national debate preceeding a national referendum; this would mean we would have to consider seriously the calling of a national conference followed by a constituent assembly followed by a referendum on the new draft constitution;

For these reasons, for the powers-that -be, the issue of referendum is an opening up of a "Pandora's Box. No wonder the word had an electric effect on the party (CCM) and state machinery. And no wonder too that some compromises had to be made so long as a "referendum" was kept out.

Mikakati ya kuua hoja ya kura ya maoni ikapelekea kuzaliwa wa version three ya G55 huku mchakato ukiratibiwa kikamilifu na ccm na serikali yake, na waziri wa sheria na katiba wa wakati huo, akiwa ni Samuel Sitta.

Itaendelea...



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mchambuzi,

Binafsi yangu nimemsikiliza sana JK na pia kumsoma Warioba. Kisha nimekusoma wewe vizuri tu na kugundua ya kwamba sasa hivi Tanzania ina mgogoro mkuwa zaidi ya vile nilivyofikiria. Na labda niliweke hvi ili tupate pa kuanzia mjadala huu. Kutokana na changamoto zote zilizopo, migogoro na kero zote za muungano kuwepo hakuna mahala hata pamoja ambapo kero hizo zimeorodheshwa kwa fikra na kutupa majibu ya pande zote mbili iwe ya Xanzibar au ya Tanganyika.

Kwa mfano, rais leo kazungumzia Tanganyika kuvaa koti la Muungano. Hili ni kero la muungano lakini je ina maana gani? No vitu gani vilivyotokea kufuatia kero hii huko nyuma. Tanganyika kuvaa koti la Muungano haikujieleza vya kutosha kiasi kwamba wasomi waweze kujua unapolivua koti unafanya nini, hili koti linaathari zipi. Ni bahati ktk hotuba hiyo hiyo nikaja gundua swala moja hasa JK alipozungumzia swala la reli, akisema hili sio swala la Muungano - maana Zanzibar hawana reli, hawaihitaji. Pale pale ikanigusa vizuri kumbe Tanganyika inapoingia mkataba wowote wa limataifa kwa kukopa fedha za kigeni ama kuomba msaada mvji za nje hutumia jina la Tanzania kwa sababu Tanganyika haipo wala haina creditline kimataifa. Hapo ndipo akili ikanipa picha ya Tanganyika kuvaa koti la Muungano. sasa sielewi kama hii ndio maana haswa ya kero za Wazanzibar au kuna zaidi ya haya maana hatujapewa maelezo kamili.

Pili, Nikakumbuka swala la Usajili wa vyombo vya moto. Zanzibar walisajili meli ya Iran kwa jina la Tanzania na bendera ya Taifa. Tukakwaruzana sana humu JF na mh. Membe kukabiriwa na maswali chungu nzima toka nchi za nje. Tuseme mathlan meli ile ingekiuwa imebeba Uranium ingekuwaje? Hivyo Swala la Usalama wa Taifa linaingilia shughuli zote za Jamhuri na hivyo usajili lazima ufuate sheria luu ya kaitba ua Jamhuri, athari zake tumeziona.

Tatu, katika Hotuba ya JK leo nimegundua kuwa Zanzibar tunayoilaumu kuvunja katiba ya Muungano, sii kweli ni wao maana JK alizungumzia swala la katrume na Seif Sharrif Hamaf. Nikakumbuka ule mufaka baina ya CCM na CUF ambao Karume na Hamad Sharrif walifikia muafaka na baada ya hapo tuliona baadhi ya maswala ya Muungano yakihamia ktk maswala yasiyokuwa ya Muungano, japo ukiisoma katiba yetu yale mambo 22 baadhi mamlaka yake yameisha rudishwa Zanzibar, ndio Kinyemela kwenyewe huko. Hivyo sisi tunagugumia na maswali kumbe majibu yake ni kwamba utawala uliopo madarakani wamefanya mageuzi haya kama hatua ya kuondoa kero za Muungano pasipo ridhaa ya wananchi wala kufanya marekebisho ktk katiba ya Muungano.

Tupende tusipende haiwezekani mamlaka kamili yakatolewa kwa nchi moja moja kutokana na kero za muungano itakuja haribu kabisa umuhimu wa kuwepo serikali 2 na ndio maana Warioba alisema zile serikali 2 tulizoachiwa na waasisi wetu hazipo tena na hii ndio hatari kubwa zaidi ya Muungano kuliko kero zenyewe.

Sasa ebu, tutazame mataifa, mengine hufanya nini? Kwanza hakuna swala lolote ndani ya katiba linaloipa nchi mamlaka kamili kama dola, isipokuwa mamlaka ya ki-nchi (republic) ambayo mara nyingi inahusiana na mgawanyo wa kazi na sheria. Zipo sheria ambazo zinaweza zisitumike upande wa pili lakini kwa kifupi Katiba ya Muungano ni katiba mama hakuna jambo ambalo lisilokuwa na Muungano kwa sababu maswala yote ya wizara zote za Jamhuri husika yanahusiana kwa namna moja ama nyingine.

Wenzetu wamekuwa na mfumona utaratibu mzuri sana wa kukusanya mapato kwa kila State au Province zao ambapo kuna asilimia ya pato la kila serikali huenda ktk mfuko wa Taifa. Na inaposemwa shughuli za kila nchi haina maana hata mapato yake ni 100% ya nchi (State) ila mfumo huu huzigawa kazi ktk majimbo hayo ili kupata ufanisi zaidi oyekelezaji lakini kugawana shghuli haina maana ndio kugawana hadi mapato yake kwa sababu tu ya state moja.

Katika mfumo wa wenzetu walokuwa na miungano ya nchi, kila nchi huchangia mfuko wa TAIFA tokana na ushuru, forodha, kodi na kadhalika yaani pato lolote la serikali lazima asilimia fulani iende kwenye mfuko wa Taifa japo nchi husika ndio ina mamlaka ya kushughulikia. Na kila mwaka wa bajeti serikali kuu (federal) huzi fund states na wizara zote ili kutimiza majukumu yake ktk mipango ya maendeleo. Hivyo ni jukumu la mawaziri wa kila state kupangiwa fedha hizo zitatumikaje baada ya kupewa na serikali kuu maana kila states ina mahitaji yake. Tulivyo sasa hivi ni sawa kabisa na kuwa na serikali 3 ambazo Tanganyika imejificha ndani ya Tanzania na kutumia nafasi hiyo kukidhi mahitaji yake.

Hivyo basi ikiwa ushuru ni asilimia 30, automatically 20% inakwenda Federal na 10% inabakia ktk mfuko wa nchi husika. Lakini kwa jinsi tunavyokwenda leo Utagundua kwamba ni kweli Tanganyika imejificha ndani ya Tanzania na vigumu sana kujua mchango wake ktk mfuko wa taifa zaidi ya Tanganyika yenyewe kuwa ndio serikali kuu ya Tanzania (ya muungano). Tumeliwa ktk swala la Reli ya kati na wahindi na hilo deni linahesabika kama ni deni la Taifa zima hivyo Znz wameubeba mzigo wetu ambao hauwahusu. Correct me if am wrong!

Kutokana na hotuba ya JK na ile ya Warioba imenijengea hofu zaidi na kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kuondoa kero hii kubwa ya Tanganyika kuvaa koti la Muungano, na haitawezekana zaidi ya Tanganyika kuwa na serikali yake, ina maana serikali ya 3. Kuwepo kwa serikali ya 3 kunaondoa hoja hii moja kubwa ya kuvaa koti, laa sivyo ndani ya serikali 2 ni muhimu iwe wazi kabisa Tanzania inapochukua mikopo ama misaada ni lazima Zanzibar wafaidike na mikopo ama misaada hiyo kwa sababu tunalitumia jina la Muungano, tutasemaje hili swala sii la Muungano wakati mdhamana ni serikali ya muungano?.

JK amewapa kazi hii kubwa sana kamati ya bunge la katiba na sidhani kama wataiweza kwa sababu Kero zimebakia pale pale na sina hakika kama wanaelewa how deep kero hizi zimefikia. Na sidhani kama wengine wanaelewa hata maana ya msemo huu wa kwamba Tanganyika imevaa koti la muungano una maana gani? sasa tutegemee nini kutoka kwa watu ambao kwanza hawana mwanga mkubwa juu ya migogoro yote ya Katiba. Imebakia 6 ndiyo lakini waanze na kero ipi?
Na kama nilivyokwisha sema toka awali ya kwamba Katiba mpya huandikwa na watalaam sio kundi la watu ambao sii wawakilishi wa wananchi. Huu mpango wa kura badala ya kuweka meza kuu ya wataalam ambao watachuja michango ya hawa wajumbe na kuuliza maswali ni kuwakabidhi jisu la samurai au Jitsu wajitoe mhanga wa Kijapan. Hii ni kuyafutiana lawama hali wengine wameosha mikono.

Hayo mambo 6 yalobakia unategemea kweli hili bunge la katiba litaweza kuyamudu maana uamuzi wa serikali 3 unaweza tu kujibu swla moja lakini pia unaharibu maswala mengine yalokwisha rudishwa ktk maswala yasokuwa ya muungano na yale ya muungano. Ni vigumu sana kutenganisha wizara za serikali na kuzifanya za Muungano na zingine sii za muungano ila unaweza kutenganisha majukumu ya shughuli za Muungano.

Ni kosa kubwa sana kugawana wizara na idara za serikali badala ya shughuli za serikali kuwa shughuli za nchi(state). Huku majuu kwetu wizara zote ni wizara za serikali kuu (TAIFA) isipokuwa zimegawiwa majukumu kwenye nchi zake kama ilivyo nyumbani mikoani na kuna mahusiano makubwa kati ya wizara hizo na serikali kuu aidha kwa kutumaini funds ama mipango ya maendeleo ambayo hayaingiliani na majukumu ya Kitaifa.

Nitaendelea kesho inshaallah!
 
Last edited by a moderator:
Msingi imara wa muungano wowote ni uchumi,iwe ni muungano wa n.g.o,au muungano wa ushirika wa jambo lolote,katu,muungano unaosimama sababu ya msingi wa kupata madaraka,uongozi ,au aina nyingine ya kupeana haki za kiuongozi uimara wake hauchukui mda mrefu,ni hapo naona haja na hoja pana sana ya kuujadili muungano wa tanganyika na zanzibar katika muundo ambao msingi wa uchumi utaamua muundo upi wa serikali ni muafaka,hoja kuu iwe ni msingi wa kiuchumi ,kuliko msingi wa kisiasa ambao mtaji wake mkuu ni kuweka uwiano wa madaraka,kama hatukuweka msingi imara katika uchumi,muundo wa serikali tatu katika muungano utapata shida sana,unless kama tunatafuta diplomasia ya kuvunja muungano bila kuhitaji bughudha .tupime kila nadharia,tupime kila hisia,ni kwa namna gani vitawiana na uhalisia katika utekelezaji .
 
Balaza la Mapinduzi mwaka 1964 walikuwa na wajumbe wangapi na kina nani? Naomba majina yao kisha nambie ktk hawa nani hakushirikishwa!

Jambo moja kubwa sana nimeligundua ni kwamba kumbe Watanzania wengi pamoja na viongozi wa leo hawafahamu kabisa mfumo wa Muungano wetu. Na ndio maana hukwaza na hili la Nchi 1 serikali 2. Hili pekee ni Catch 22 kwao. Hawajui tofauti zilizopo kati ya shughuli za JMT na shughili za Serikali ya Mapinduzi na kwa nini ilikuwa hivyo. Hawajui mapana ya serikali ya Muungano wa Tanzania, hili ni somo jipya kwa viongozi na wananchi kwa ujumla.

Mkandara,

Member wa Baraza la Mapinduzi (MBM) wa kwanza walikuwa 10. ndani yake alikuwemo Yusuf Himid, Seif bakari na wengine.

Lakin kubwa katika kadhia hii ni WAPI MAANDISHI ILI KUKAMILISHA ILE TARATIBU YA MKATABA WA KIMATAIFA WA KUUNGANISHA NCHI MBILI HURU?

Mimi binafsi napenda kukwambia kisharia tunasema MUUNGANO wenu ni wa TANGANYIKA KWA ZNZ, na sio TGK na ZNZ




 
Mkandara,

Member wa Baraza la Mapinduzi (MBM) wa kwanza walikuwa 10. ndani yake alikuwemo Yusuf Himid, Seif bakari na wengine.

Lakin kubwa katika kadhia hii ni WAPI MAANDISHI ILI KUKAMILISHA ILE TARATIBU YA MKATABA WA KIMATAIFA WA KUUNGANISHA NCHI MBILI HURU?

Mimi binafsi napenda kukwambia kisharia tunasema MUUNGANO wenu ni wa TANGANYIKA KWA ZNZ, na sio TGK na ZNZ




Sijakuelewa unataka maandishi gani? Hivi kuna maandishi gani ktk Union baina ya Great Britain na Ireland ambayo wewe unayapa mfano nasi hatuna.
 
Balaza la Mapinduzi mwaka 1964 walikuwa na wajumbe wangapi na kina nani? Naomba majina yao kisha nambie ktk hawa nani hakushirikishwa!
Mkuu Mkandara,

Wajumbe wa baraza la mapinduzi 1964 walikuwa wafuatao:

1. Karume - Rais wa znz
2. Abdulla Kassim Hanga - makamu wa rais
3.Abdurahaman babu
4.Hasnu makame
5.Aboud Jumbe
6.Salehe Saadalla
7.Idris abdul wakil
8.Othman shariff
9.Abdulah aziz twala
10. Hassan Nassor Moyo
11. Field Marshall John Okello
12. Kamishna wa polisi - Edington Kisassi
13. Yusuf Himid
14.Seif bakari
15. Ramadhan Haji
16. Abdalah Natepe
17. Pili khamis
18.Khamis hemedi
19.Said idi bavuai
20. Said wa shoto
21. Muhammed abdulla
22. Abdulla mfaranyaki
23.Hafidh suleiman
24. Khamis darwesh
25.Khamis abdulla ameir
26. Muhammed mfaume omar
27. Muhsin bin ali
28. Mohammed juma
29. Daud mahmoud
30. Hamid ameir ali

Source: issa shvji

Pia Kwa mujibu wa memorandum ya CIA dated 1968 kama nilivyowasilisha awali, ratification ilifanywa na only one third ya hawa 30, which means wajumbe 10; nikajenga hoja kwamba kwa vile haikufikia 2/3, pengine ni sababu kwanini Karume hakuruhusu iende on official records ingawa kwa karume, yeye aliamua one third imetosha;

Nikipata muda nitajadili kwa undani zaidi;

Pia kwenye bandiko lako #203 nafarijika kwamba angalau unaanza kuona mantiki ya kuizindua Tanganyika; ntakurudia baadae katika hili pia;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Msingi imara wa muungano wowote ni uchumi,iwe ni muungano wa n.g.o,au muungano wa ushirika wa jambo lolote,katu,muungano unaosimama sababu ya msingi wa kupata madaraka,uongozi ,au aina nyingine ya kupeana haki za kiuongozi uimara wake hauchukui mda mrefu,ni hapo naona haja na hoja pana sana ya kuujadili muungano wa tanganyika na zanzibar katika muundo ambao msingi wa uchumi utaamua muundo upi wa serikali ni muafaka,hoja kuu iwe ni msingi wa kiuchumi ,kuliko msingi wa kisiasa ambao mtaji wake mkuu ni kuweka uwiano wa madaraka,kama hatukuweka msingi imara katika uchumi,muundo wa serikali tatu katika muungano utapata shida sana,unless kama tunatafuta diplomasia ya kuvunja muungano bila kuhitaji bughudha .tupime kila nadharia,tupime kila hisia,ni kwa namna gani vitawiana na uhalisia katika utekelezaji .
Mbona muungano umeshavunjwa tayari kabla ya serikali 3! Rejea katiba ya znz iliyofanyiwa marekebisho 2010

1. Zanzibar ni nchi na mipaka yake
2. Ina bendera, wimbo wa taifa na vyombo vya uwakilishi
3.Kuna majeshi yanyoitwa vikosi maalumu
4. Kama kuna jambo nje ya BLW maamuzi ya BLW yatakuwa ya juu. Ndiyo maana tukitaka kupitisha sheria ya kujenga vyoo au nyumba za walimu lazima BLW likubali
5. Znz ina Amir jeshi mkuu

Unataka muungano gani zaidi. Wabunge wa znz wanaokuja Dodoma wanakuja kukusanya pesa. Hawana lolote la kutenda au kujadili kwasababu ni watalii tu ambao hawahitaji visa. Muungano upo wapi hapo
 
Mkuu Mkandara,

Wajumbe wa baraza la mapinduzi 1964 walikuwa wafuatao:

1. Karume - Rais wa znz
2. Abdulla Kassim Hanga - makamu wa rais
3.Abdurahaman babu
4.Hasnu makame
5.Aboud Jumbe
6.Salehe Saadalla
7.Idris abdul wakil
8.Othman shariff
9.Abdulah aziz twala
10. Hassan Nassor Moyo
11. Field Marshall John Okello
12. Kamishna wa polisi - Edington Kisassi
13. Yusuf Himid
14.Seif bakari
15. Ramadhan Haji
16. Abdalah Natepe
17. Pili khamis
18.Khamis hemedi
19.Said idi bavuai
20. Said wa shoto
21. Muhammed abdulla
22. Abdulla mfaranyaki
23.Hafidh suleiman
24. Khamis darwesh
25.Khamis abdulla ameir
26. Muhammed mfaume omar
27. Muhsin bin ali
28. Mohammed juma
29. Daud mahmoud
30. Hamid ameir ali

Source: issa shvji

Pia Kwa mujibu wa memorandum ya CIA dated 1968 kama nilivyowasilisha awali, ratification ilifanywa na only one third ya hawa 30, which means wajumbe 10; nikajenga hoja kwamba kwa vile haikufikia 2/3, pengine ni sababu kwanini Karume hakuruhusu iende on official records ingawa kwa karume, yeye aliamua one third imetosha;

Nikipata muda nitajadili kwa undani zaidi;

Pia kwenye bandiko lako #203 nafarijika kwamba angalau unaanza kuona mantiki ya kuizindua Tanganyika; ntakurudia baadae katika hili pia;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Naona hapo ahali yangu na hiyo source yako imewapuruchuka, MBM wa kwanza kabisa baada mapinduza walikuwa kumi tu na wote wamefariki.

Hao ulio ongeza walikuwa wanaongezeka mpaka leo .lakin wale 10 wa kwanza ninaowajua mimi wakti ule wa mapinduzi walikuwa hawa.

Karume
Edington Kisassi
Hasnu makame
Abdulah aziz twala
Salehe Saadalla
Yusuf Himid
Seif bakari
Said idi bavuai
Said wa shoto
Khamis darwesh.

Tukumbuke historia ya Znz imepotoshwa sana kama yalivyopotoshwa ya Tgk.



 
Mbona muungano umeshavunjwa tayari kabla ya serikali 3! Rejea katiba ya znz iliyofanyiwa marekebisho 2010

1. Zanzibar ni nchi na mipaka yake
2. Ina bendera, wimbo wa taifa na vyombo vya uwakilishi
3.Kuna majeshi yanyoitwa vikosi maalumu
4. Kama kuna jambo nje ya BLW maamuzi ya BLW yatakuwa ya juu. Ndiyo maana tukitaka kupitisha sheria ya kujenga vyoo au nyumba za walimu lazima BLW likubali
5. Znz ina Amir jeshi mkuu

Unataka muungano gani zaidi. Wabunge wa znz wanaokuja Dodoma wanakuja kukusanya pesa. Hawana lolote la kutenda au kujadili kwasababu ni watalii tu ambao hawahitaji visa. Muungano upo wapi hapo

Nguruvi3,

Ahali yangu kama tulivyobainisha huko juu kuwa utaratibu wa kisharia wa kimataifa wa kuunganisha nchi mbili huru kwa upande wa Znz haukukamilika hivyo kuufanya uwe batili na tunaweza sema kuwa MUUNGANO ULIOPO KUWA WA TGK KWA ZNZ. Na sio wa TGK na ZNZ.

Kigezo hicho kinaipa Znz nguvu za kisharia kufanya lolote bila kuvunja katiba ya JMTz.



 
Sijakuelewa unataka maandishi gani? Hivi kuna maandishi gani ktk Union baina ya Great Britain na Ireland ambayo wewe unayapa mfano nasi hatuna.


Labda nikuulize JE unajuwa kwanini NYERERE alimzuia JUMBE kuandaa Hati ya Maombi ya kuhoji na kutaka ufafanuzi kwenye Mahakama Maalum ya Kikatiba juu ya muundo sahihi wa Muungano kwa kutumia ibara ya 125 ya Katiba ya JMTz?.
 
Labda nikuulize JE unajuwa kwanini NYERERE alimzuia JUMBE kuandaa Hati ya Maombi ya kuhoji na kutaka ufafanuzi kwenye Mahakama Maalum ya Kikatiba juu ya muundo sahihi wa Muungano kwa kutumia ibara ya 125 ya Katiba ya JMTz?.

Muoman wewe haya hayakhusu! Ulishakimbia ukaikana Mlandege na Tabora wayatakiyani yetu??? Kula tende na halua tuache na Tanzania yetu; usipandikize chuki kati yetu wazinzibar na watanganyika waungwana tutapata tu muafaka!
Cc gombesugu
Tafadhwali tuondolee hii tafrani ya kiOman mwarabu mzima mambo ya wabantu yamkhusu vipi?? Mbona sisi hatuhoji ya Oman??
 
Last edited by a moderator:
Naona hapo ahali yangu na hiyo source yako imewapuruchuka, MBM wa kwanza kabisa baada mapinduza walikuwa kumi tu na wote wamefariki.

Hao ulio ongeza walikuwa wanaongezeka mpaka leo .lakin wale 10 wa kwanza ninaowajua mimi wakti ule wa mapinduzi walikuwa hawa.

Karume
Edington Kisassi
Hasnu makame
Abdulah aziz twala
Salehe Saadalla
Yusuf Himid
Seif bakari
Said idi bavuai
Said wa shoto
Khamis darwesh.

Tukumbuke historia ya Znz imepotoshwa sana kama yalivyopotoshwa ya Tgk.
Naona Field Marshall John Okelo unamkwepa!
 
Naona Field Marshall John Okelo unamkwepa!
Huyo hasemwi maana atabadili historia inayotakiwa. Niliwahi kumsikia (tarehe 6 oct 2012 pale bwawani) Nosr Moyo akisema yeye ni mwana baraza la mapinduzi la kwanza kabisa. Sijui hili nalo lipoje.

Kuna Mzee thabiti Kombo, hawa sijui walijiunga lini na BLM.
 
Labda nikuulize JE unajuwa kwanini NYERERE alimzuia JUMBE kuandaa Hati ya Maombi ya kuhoji na kutaka ufafanuzi kwenye Mahakama Maalum ya Kikatiba juu ya muundo sahihi wa Muungano kwa kutumia ibara ya 125 ya Katiba ya JMTz?.
Lini, wapi na ushahidi gani uliopo kuhusu hilo? Kuna nyaraka!
 
Nguruvi3,

Ahali yangu kama tulivyobainisha huko juu kuwa utaratibu wa kisharia wa kimataifa wa kuunganisha nchi mbili huru kwa upande wa Znz haukukamilika hivyo kuufanya uwe batili na tunaweza sema kuwa MUUNGANO ULIOPO KUWA WA TGK KWA ZNZ. Na sio wa TGK na ZNZ.Kigezo hicho kinaipa Znz nguvu za kisharia kufanya lolote bila kuvunja katiba ya JMTz.
Mamlaka kamili wanayotaka wznz ni yapi iwapo wana nguvu hizo kisharia?
 
Sijakuelewa unataka maandishi gani? Hivi kuna maandishi gani ktk Union baina ya Great Britain na Ireland ambayo wewe unayapa mfano nasi hatuna.
Ndiyo maana nimemuuliza atupe maandishi ya kuonyesha jinsi Nyerere alivyomzuia Jumbe kuhoji muungano katika mahakama maalumu ya katiba.
Kama hana, anapata wapi ushujaa wa kuomba maandishi kwa wenzake?
 
Mkuu Mkandara,

Wajumbe wa baraza la mapinduzi 1964 walikuwa wafuatao:

1. Karume - Rais wa znz
2. Abdulla Kassim Hanga - makamu wa rais
3.Abdurahaman babu
4.Hasnu makame
5.Aboud Jumbe
6.Salehe Saadalla
7.Idris abdul wakil
8.Othman shariff
9.Abdulah aziz twala
10. Hassan Nassor Moyo
11. Field Marshall John Okello
12. Kamishna wa polisi - Edington Kisassi
13. Yusuf Himid
14.Seif bakari
15. Ramadhan Haji
16. Abdalah Natepe
17. Pili khamis
18.Khamis hemedi
19.Said idi bavuai
20. Said wa shoto
21. Muhammed abdulla
22. Abdulla mfaranyaki
23.Hafidh suleiman
24. Khamis darwesh
25.Khamis abdulla ameir
26. Muhammed mfaume omar
27. Muhsin bin ali
28. Mohammed juma
29. Daud mahmoud
30. Hamid ameir ali

Source: issa shvji

Pia Kwa mujibu wa memorandum ya CIA dated 1968 kama nilivyowasilisha awali, ratification ilifanywa na only one third ya hawa 30, which means wajumbe 10; nikajenga hoja kwamba kwa vile haikufikia 2/3, pengine ni sababu kwanini Karume hakuruhusu iende on official records ingawa kwa karume, yeye aliamua one third imetosha;

Nikipata muda nitajadili kwa undani zaidi;

Pia kwenye bandiko lako #203 nafarijika kwamba angalau unaanza kuona mantiki ya kuizindua Tanganyika; ntakurudia baadae katika hili pia;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Naomba hiyo link ya Issa Shivji maana nijuavyo kwenye list hii naona ame include members wa Afro Shiraz Youth league ambao walijulikana kama the committee of 14.

1. Sasa ebu tujiulize hivi, Ikiwa Okello alifukuzwa kabla ya Muungano imekuwaje naye awe kwenye list ya Revolution Council walotakiwa kupiga kura kuunga ama kukataa Muungano?

2. Je, Inaingia akilini ASP na Umma Party kuwashirikisha Youth league wake ktk makubaliano ya Muungano wake maana ikumbukwe tu pia kuna tofauti baina ya Baraza la Mapinduzi kabla ya Muungano na baraza hilo baada ya Muungano.

List yangu kabla ya Muungano ni 1. Abeid Karume, 2. Abdallah Kassim Hanga, 3. Abdul Aziz Twala, 4. Abdulrahman Babu, 5. Aboud Jumbe, 6. Hasnu Makame, 7. Othamn Sharrif, 8. Saleh Saadalla, 9. Abdul Wakil na 10. Hassan Nassoro Moyo.

Sasa inasemekana kuwa hii ni 1/3 kutokana na majina yote ya washirika including hawa wa Youth league (upotoshaji) ili kuunda watu 30 walokuwa na dhamana ya kupitisha Muungano ambavyo sii kweli. Kuwa member of the revolution ama kushiriki ktk Mapinduzi haikupi mamalaka ya kuwa Member of revolution Council wakati wa makubaliano baina ya nchi 2.

Naomba kusahihishwa kwa ushahidi maana hizi hadithi nazisikia kila siku lakini hakuna mtu alokuja na kunipa List ya Revolution Council kabla ya makubaliano ya muungano tofauti na hii niijuayo mimi.
 
Naona Field Marshall John Okelo unamkwepa!

Mag3,

Labda nikwambie tu siku ya mapinduzi 1964 mimi niliku kijana mdogo na ufahamu wangu nikiwa hata madrasa nimeanza kusoma kwa maalim Bakhathiri shanghani,

Hivyo najua mengi sana ingawa sipendi kuyajadili kwa sasa.

Lakin Okelo enzi zile akijiita Masho hajapata kuwa MBM hata dakika moja pale ZNZ. Kumbuka na ukuu wa majeshi aliteuliwa YUSUF HIMID na msaidizi wake alikuwa SEIF BAKARI.

Tuyaache haya kwani yana machungu ndanimwe.



 
Nguruvi3,
Kwa miaka 50 hukuidai Tanganyika, na hiyo Zanzibar kama nchi ilikuwepo kwa miaka 50, ni kitu gani kilichowasukuma nyie mdai Tanganyika ilihali mnajua fika kwamba kuna ukweli mkubwa ktk madai ya Wazanzibar, moja ni kuwa Tanganyika imevaa koti la Muungano?. Na sii sababu ya jina la Tanzania bali Tanganyika kutumia Tanzania kama Taifa, tumeomba mikopo na misaada kwa Jina la JMT kwa manufaa ya bara, tena kibaya zaidi misaada hiyo viongozi wameifisadi hivyo leo tuna deni la Taifa kubwa kutokana na sisi. Kwa nini hatulizungumzii hili kwanza halafu taratibu tupande juu hadi tufike kwa kero zetu.

Unajua kuna hadithi moja (ya kweli) ambayo nitakusimulia, Kuna mama mmoja (jina lake kapuni) alirithi nyumba ya vyumba sita Kinondoni. katika maisha akafunga ndoa na mume ambaye baadaye kwa kutumia NDOA na mama huyo, alienda benki na kukopesha fedha nyingi tu na akaweka ile nyumba kama rehani. Baada ya muda mzee wa watu akashindwa kurudisha deni ikabidi benki waje kuikamata nyumba.

Siku walofika wakamkuta yule mama ambaye ndiye haswa mrithi wa nyumba. Wakamwambia kilichotokea na kinachafuata. Yule mama akasema hana taarifa yoyote kuhusu nyumba ile kuwekwa rehani na wala mume sii yake, yeye ndiye haswa mwenye nyumba. . Yamekwenda wee ikaonekana hata yule mama hakuwahi kubadilisha jina la mirathi ya nyumba, yule mzee pia sijui hati ya nyumba aliipata vipi hadi benki ikamkubali.

Yamekwenda wee, ikaonekana kuna mtu aloinunua nyumba ile kupitia Utaifishaji wa Benki na kalipa deni lilokuwa. Kesi mahakamani, imekwenda weee leo miaka sijiui 20 lakini yaonyesha wazi mama yule kisha liwa maana hana uwezo wa kushindana na benki wala huyo mnunuzi. Kifupi wameliwa wote kilichobakia ni lawama ndnai ya nyumba ndoa haishikiki tena. Kuna ile kesi ya Bakwata na maeneo ya Ardhi za waislaam na kadhalika. Ni usanii unaoendelea ambao sii kwa watu binafsi tu nimekuwa hadi Taifa tunapiga magoli ya visigino. Hii ndio hulka yetu, toka watu binafsi hadi viongozi na wapambe, tunafanya makosa lakini hatutaki kukubali makosa ila humrudishia victim kuwa yeye ndiye mwenye makosa tena tunakuwa wakali ajabu.

Hivyo basi kwanza sisi bara tunatakiwa kukubali makosa. Tukubali ni kweli sisi tumelitumia jina la Muungano kuchukua mikopo na misaada inayoiendesha mambo yasokuwa ya muungano. Mfano wa reli ya kati. Kisha baada ya kuyakubali makosa sasa ndio itafutwe njia nyepesi ya kuondoa tatizo hilo.

Hii kutokubali makosa na kuanza kunyoosheana vidole haitatufikisha popote na nina hakika hata hilo bunge la katiba watafika mahala watakwama kutokana na kwamba huko Bungeni kwenyewe Tayari kuna Utanganyika na Uzanzibar hakuna muungano hapo. Hatua hizi zinachukuliwa kutokana na jazba, hasira na karaha mlozidumisha kwa miaka 50.

Lakini ukiingia ndani zaidi utagundua kwamba hizo serikali 3 zinazoombwa mfumo wake ni wa ajabu kabisa. Haiwezekani serikali za nchi ziwe juu ya serikali kuu, ama rais wa Muungano awe ni ceremonial sasa unafikiri kuna muungano hapo kweli. Hakuna Taifa hata moja lenye muungano wake halafu serikali za nchi zipo juu ya serikali kuu. na ndio maana JK akasema mnalikaribisha jeshi kuchukua nchi akijua makosa yalofanyika ktk mapendekezo yenu. Pande mbili zisipokubaliana na kuingia uhasama hili Jeshi litakuwa upande gani? JK ametishia tu kutokana na makosa mnayoyafanya kupendekeza serikali 3 wakati hamjui mamlaka yapi hutengeneza muungano wa nchi

Tukubali kwanza makosa walotupa, tuyatazame na kukubali sii swala la Zanzibar inatutegemea sisi zaidi ya sisi kuwateemea wao. Muungano wetu haukuwa wa kutegemeana ama nani anamtegemea mwenzake. Hii kunyoosheana vidole kusema kweli mimi Kwanzasiiafiki. NI mwanzo wa kiburi cha kutokubali makosa yalokwisha fanyika.
 
Back
Top Bottom