Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

Duru za siasa: Bunge la Katiba, upotoshaji na kiwewe cha kuzinduka Tanganyika

Hiki kitu kinachoitwa legal foundation wengi hawataki kukijadili kwasababu kinaondoa dhana ya serikali 2. Lakini basi tukiuliza kama legal foundation ni dhana mbaya, watuambie msingi wa serikali 2 ni upi. Hakuna jibu, wanataka tuamini tu kuwa ilikuwa serendipity hivyo tuendelee tu kibubusa kama ilivyotokea.

Serikali 1 imeshindikana, 2 zina matatizo yasiyo na suluhu. Where do we go from here!
Serikali 3, in worst case scenario vunja jahazi
Mkuu nasubiri majibu yako kwanza maana upotoshaji wako bado kabisa hauwezi kujenga hoja ya msingi.

Nilisema na nitasema tena Artical of Union ni legal foundation ya kuundwa kwa TAIFA moja na sio NCHI moja. Na Nikaendelea kusema Leo hii Tanganyika sio nchi tena baada ya kuliacha jina hilo kisheria na kutumia neno Tanzania kwa kuongeza mapana ya eneo lake ikijumuishwa na Zanzibar. Na sababu ya pili nikasema Tanganyika sio nchi kwa sababu kila nchi ina mihimili mitatu. 1. Serikali, 2 Mahakama na 3. Bunge lake hivyo Tanganyika haipo na haina vitu hivyo isipokuwa Zanzibar ni nchi kwa sababu ina mihimili hiyo. Tanganyika ilikwisha kufa, leo hii tuna Taifa moja tu lijulikanalo kama Tanzania na ukitaka kuiua Tanzania ni kuirudisha Tanganyika na tutakuwa tumekiuka sheria vie vile za katiba tuloapa kuilinda kama walivyofanya Wazanzibar na katiba yao ya mwaka 2010. Hivyo kosa moja haliwezi kupatiwa ufumbuzi kwa kufanya kosa jingine kinyume cha katiba na makubaliano ya Muungano.

Nirudi ktk KERO ZA MUUNGANO - Hizi kero zilikuwepo toka zamani na kwa hatua tofauti, Nilishakueleza huko nyuma hivyo tuliposhindwa kuzitatua na hasa kasheshe lilianza baada ya kutoka mfumo wa Kijamaa na kuingia Ubepari. Tanzania bila kujiandaa tuliingia mfumo huo pasipo kufanya amendments za kichumi ktk katiba yetu ya JMT na katiba ya Zanzibar, hapo ndipo Tanganyika iliyokufa ikaanza kujitokeza maana tuliyatazama kero zile kwa maslahi ya Bara na sii kwa maslahi ya Zanzibar au Tanzania.

Kwa hiyo Wazanzibar wakajiona wao kama ni koloni la Tanganyika. Na nadhani unajua maana ya koloni au territorial government ambayo haina mamlaka kamili. Hivyo toka tumeunda muungano wetu Zanzibar ilikuwa na mihimili yake mitatu kulingana na katiba ya JMT lakini ktk utendaji na utekelezaji wa vitu hivi kulingana na na madai ya WaZanzibar ni kuwa hawakuwa na mamlaka kamili ktk uendeshaji nchi yao. Nadhani pia unaelewa mamalaka kamili walokuwa nayo states za Marekani au Province za Canada au zile za Uingereza na kadhalika, kwa nini kero zao sisi tumeziingiza ktk mamlaka ya JMT pasipo ridhaa ya Wazanzibar(mambo mengine 11 yaloongoezeka)ama yale ya muungano kuinufaisha bara tu.

Hivyo, ilichotakiwa ni viongozi wetu kukaa na kuyapanga mamlaka hayo wazi ili yawe ya Zanzibar au ya JMT bila kuingiliana. Na kwa hekima yangu nilojaaliwa najua fika kwamba kwa wale wanaoitaka tanganyika mpya hawataishia hapo. Wataanza kuweka masharti kwa Wazanzibar na Wazanzibara, kumbuka kuna walalahoi wanaosubiri tu mchafuko huu na hakika Usalama wa Wazanbara utakuwa matatani.

Hivyo basi kama kweli tunaitafuta suluhu ya Muungano wetu tulitakiwa kuzitazama hizo kero za Muungano kabla ya Zanzibar hawajaandika katiba yao mpya ya mwaka 2010. Kila kilichobadilishwa mle (katiba ya Zanzibar) ni kero zilizokuwepo ambazo tulizipuuza na sasa ndizo sababu ya kuzaliwa kwa katiba hiyo na kumezaa Kero mpya kwa Bara. Kero juu ya kero.
Hivyo kero za muungano zimehamia Bara na sasa, nasi tunatafuta dawa yake, jino kwa jino huku tukifanya makosa yale yale waloyafanya Zanzibar ya kukiuka katiba ya Muungano. Kuirudisha Tanganyika itakuja na katiba yake ili kutoa sare kwa katiba ya Zanzibar na sii Muungano. Did we solve our problems? bila shaka ni hapana, ila tumeongeza matatizo yaani sasa sote tumekiuka Katiba ya JMT, hivyo hakuna hata sababu ya bunge hilo la katiba kuwepo.

Kitakacho fuata sasa hivi ni Zanzibar wabadilishe katiba yao ili tukubaliane nao (mjadala mwingine), Tanganyika nao waandike katiba yao halafu ndio Katiba ya JMT iundwe hii itachukua miaka 5 hadi 10 ijayo. Je tumefanikisha lipi - HAKUNA maana hata tukiwa na serikali 3 bvado swala la OIC litakuwa ktk mambo ya nje na serikali kuu (3) bado italizuia kwa sababu zile zile walizotoa tulipokuwa na serikali 2. Tunashindwa kutazama kero zenyewe badala yake tunajitazama sisi kutokana na hii kitu UBEPARI na hatukuwa tayari kuandaa mwongozo unatuwezesdha sote ktk ushirika wa JMT.
 
MKANDARA,

Naona unajiviringisha na kukatataa kutoa historia ya Tanganyika iliyomfanya Nyerere aende Znz kuomba muungano.

LABDA KWA AKILI YA KAWAIDA KABISA INAWEZEKANA VIPI NCHI YENYE UKUBWA WA 885,800 SQ KM NA WATU ZAIDI YA MILIONI 18 WAKTI HUO KUUNGANA NA NCHI YENYE UKUBWA WA 2,000 SQ KM NA WATU CHINI YA LAKI MBILI. MUUNGANO WA 50/50
?

JE NCHI hiyo kubwa inanufaika nini hapo?

Je unataka tuiweke hadhwarani kilichomsukuma Nyerere kwenda Znz kuomba Muungano?

Pole sana lakin kumbuka historia HAIFICHIKI IPO KAMA PEMBE LA NG'OMBE. ATHARI ZAKE NADHANI SASA ZIMEANZA KUCHOMOZA HUKO TGK.

JE unajuwa kwanini Bunge lenu la Katiba limejaa khofu kubwa sana na kutoaminiana linapojadili MUUNGANO?

ZNZ HURU ILEEEEEEEEEEE NA TGK HURU ILEEEEEEEE. pOLE SANA

Barubaru hapo nyuma nilidhani ungeelewa maana ya mjadala, nikaona unaharibu uzi nikakupuuza.
Kadri tunavyokwenda mbele naona unaharibu zaidi kwasababu huna mantiki zaidi ya ushabiki.

Labda nikumbushe kuwa suala la muungano kwa Nyerere halikuanza na Zanzibar.
Mwaka 1963 wakati huo znz ikiwa chini ya Sultan Nyerere alikuwa na wazo la kuungania Afrika mashariki (EAF).

Katika miaka ya 60 Nyerere alihitilifiana na swahiba wake Nkrumah kwasababu ya Pan Africanisim.
Kumbuka jitihada hizo hazikuanza mwaka huo, huko nyuma kulikuwa na PAFMECA kule mwanza.
Ingawa PAFMECA ilikuwa na malengo ya ukombozi zaid,i hiyo ni dalili kuwa Nyerere alipenda muungano ever since.

Kuanzishwa kwa frontline states ndiko kumeacha legacy ya SADC hadi leo.
Na SADC imeondoka katika objectives za mwanzo na sasa kulekea katika ushirikiano wa kiuchumi.
Mwaka 1967 ikaundwa EAC licha wazo hilo kupigwa chini mwaka 1963.

Ilipoanzishwa EAC ya sasa na akina Mwinyi, Moi na Museveni Nyerere alikuwepo na wala hakusema lolote baya kuhusu hilo ikiwa ni ishara ya kuunga mkono mashirikiano. Hayo yote yanaonyesha jinsi alivyokuwa anapenda mashirikiano ya watu beyond Berlin conference philosophy

Kwa uchache huo unaweza kuona jinsi Nyerere alivyopenda watu kuwa kitu kimoja.
Katika mkutano wa Pan Africanism, moja ya mambo yaliyojadiliwa ilikuwa ni umuhimu wa umoja kuelekea katika uchumi mkubwa.

Lakini pia lazima ufikiri kama mtu mzima aliyewahi kutembea tembe eneo la shule.
Huwezi kuongelea muungano wa mwaka 1964 kwa kuangalia mazingira ya mwaka 2014.
By that time dunia ilikuwa na mwelekeo tofauti kukiwa na nguvu pinzani za mashariki na magharibi.
Katika miaka ya 1960, 1970 hadi 1980 Mapinduzi yalikuwa kitu cha kawaida redioni.


Unaposema Znz na Tanganyika zimeungana 50/50 ni upotoshaji wa mambo.
Kama ni hivyo kelele za znz kuonewa zinatoka wapi?
Na wala ukiulizwa hiyo 50/50 uionyeshe sijui kama utaweza. Tumekueleza kila jambo kwa takwimu lakini huonekani kuelewa.

Ningekuomba kama huna hoja zinazolingana na mada iliyopo ni busara ukikaa kimya kuliko kuvuruga uzi.
Nadhani ustaarab ni jambo jepesi na heshima haiombwi, tafadhali sana rudi katika mada ama sivyo kaa kimya.
 
MCHAMBUZI

Kumfananisha Dourado na al marhum Prof Haroub Othman Miraji ni sawa na kufananisha chumvi na sukari.

Dourado alikuwa mwanasharia mkuu wa Znz wakti wa Mvungano ambapo mchakato huo wa muungano ulimruka na kumuweka pembeni japo alikuwa mwanasharia mkuu.

Prof Haroub yeye alikuwa mwanazuoni maarufu lakin hakuwa na a madaraka yoyote ya kiserikali kule Znz.

sasa kila mtu ana uzito wake hapo LAKIN DOURADO ANA UZITO ZAIDI KATIKA KADHIA HII.

JE UNAWEZA KUNIAMBIA KWANINI DOURADO HAKUSHIRIKISHWA KATIKA MCHAKATO WA MUUNGANO?


Hatumfananishi dourado na haroub bali tunaangali hoja ya haroub dhidi ya dourado kwamba dourado alikuwa ni mjumbe wa tume ya nyalali ambayo iliridhia kwamba Baraza la mapinduzi lilishirikishwa vilivyo katika ratification ya muungano. Dourado alisimamia hoja hiyo chini ya tume ya nyalali, kwanini tusihoji unduminakwili wa dourado? Tutajuaje kama 1983 kwenye paper yake kwa tanganyika legal society alisema uongo lakini chini ya tume akaamua kusimamia ukweli?

Ni muhimu pia ukafahamu kwamba ni viongozi wa znz ndio wa kulaumu kwa kutotekeleza matakwa ya mkataba juu ya ratification kikamilifu kwani hakuna sehemu yenye ushahidi kwamba Tanganyika iliwabana juu ya hilo; Tanganyika kwa upande wao walifanya kama mkataba unavyoelekeza; moja ya sababu kwanini Baraza la mapinduzi halikufanikisha matakwa ya muungano per se ni kwamba baraza hili lilikuwa limegawanyika sana juu ya mkataba, hasa content, na mgawanyiko huu ulitokana na debate kali iliyojitokeza ndani ya baraza, kwahiyo kimsingi, baraza la mapinduzi lilijadili suala la mkataba, na Kassim hanga alitoa hoja nzito sana kuunga mkono muungano na kuweza kuwashawishi wajumbe wengi kuunga mkono hoja; shivji alifanya mazungumzo na mmoja wa wajumbe wa baraza hilo wa wakati ule, Khamis Abdullah Ameir ambae kwa mujibu wa shivji:

Khamis abdulla ameir confirmed that once karume brought the articles to the revolutionary council and gave then to salim rashid to read, rashi said (although as a secretary he was not supposed to say anything) that how come all the importnant ministries were in the hands of the union? I said, this is an important question, why not a referendum? Karume became very angry, stood up and said "if you don't want I will do it myself. So we kept quite.
Kwa maana na ushahidi huu wa shivji, suala la mkataba lilijadiliwa kwenye baraza la mapinduzi lakini ratification ilikuwa kwa kulazimishana sana na ndio maana leo mjadala una evolve around mkataba kuwa ratified na baraza la mapinduzi vis a vis mkataba kuwa debated na baraza la mapinduzi. All that said and done, Tanganyika na nyerere had less to do with kilichojiri ndani ya baraza la mapinduzi kwa hatua ile. Karume alikuwa anaishi kwa uwoga kutokana na factions za kisiasa zanzibar hivyo akabariki mambo kwa mamlaka yake. Hii ni moja ya sababu kwanini Nyerere alisita mchakato wa katiba ya JMT ambapo mchakato ulitakiwa uwe umeanza kabla ya Mei Mosi 1965, na badala yake tunasoma kwenye historia nchi kuingia katika katiba ya muda kwa miaka 12 na ushee. Kwa maana nyingine, mapungufu ya karume na baraza la mapinduzi justified uchakachuaji wa mkataba wa muungano but that is a different debate.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu nasubiri majibu yako kwanza maana upotoshaji wako bado kabisa hauwezi kujenga hoja ya msingi.

Nilisema na nitasema tena Artical of Union ni legal foundation ya kuundwa kwa TAIFA moja na sio NCHI moja. Na Nikaendelea kusema Leo hii Tanganyika sio nchi tena baada ya kuliacha jina hilo kisheria na kutumia neno Tanzania kwa kuongeza mapana ya eneo lake ikijumuishwa na Zanzibar.

Na sababu ya pili nikasema Tanganyika sio nchi kwa sababu kila nchi ina mihimili mitatu. 1. Serikali, 2 Mahakama na 3. Bunge lake hivyo Tanganyika haipo na haina vitu hivyo isipokuwa Zanzibar ni nchi kwa sababu ina mihimili hiyo.

Tanganyika ilikwisha kufa, leo hii tuna Taifa moja tu lijulikanalo kama Tanzania na ukitaka kuiua Tanzania ni kuirudisha Tanganyika na tutakuwa tumekiuka sheria vie vile za katiba tuloapa kuilinda kama walivyofanya Wazanzibar na katiba yao ya mwaka 2010. Hivyo kosa moja haliwezi kupatiwa ufumbuzi kwa kufanya kosa jingine kinyume cha katiba na makubaliano ya Muungano.

Nirudi ktk KERO ZA MUUNGANO - Hizi kero zilikuwepo toka zamani na kwa hatua tofauti, Nilishakueleza huko nyuma hivyo tuliposhindwa kuzitatua na hasa kasheshe lilianza baada ya kutoka mfumo wa Kijamaa na kuingia Ubepari.

Tanzania bila kujiandaa tuliingia mfumo huo pasipo kufanya amendments za kichumi ktk katiba yetu ya JMT na katiba ya Zanzibar, hapo ndipo Tanganyika iliyokufa ikaanza kujitokeza maana tuliyatazama kero zile kwa maslahi ya Bara na sii kwa maslahi ya Zanzibar au Tanzania.

Kwa hiyo Wazanzibar wakajiona wao kama ni koloni la Tanganyika. Na nadhani unajua maana ya koloni au territorial government ambayo haina mamlaka kamili. Hivyo toka tumeunda muungano wetu Zanzibar ilikuwa na mihimili yake mitatu kulingana na katiba ya JMT lakini ktk utendaji na utekelezaji wa vitu hivi kulingana na na madai ya WaZanzibar ni kuwa hawakuwa na mamlaka kamili ktk uendeshaji nchi yao.

Nadhani pia unaelewa mamalaka kamili walokuwa nayo states za Marekani au Province za Canada au zile za Uingereza na kadhalika, kwa nini kero zao sisi tumeziingiza ktk mamlaka ya JMT pasipo ridhaa ya Wazanzibar(mambo mengine 11 yaloongoezeka)ama yale ya muungano kuinufaisha bara tu.

Hivyo, ilichotakiwa ni viongozi wetu kukaa na kuyapanga mamlaka hayo wazi ili yawe ya Zanzibar au ya JMT bila kuingiliana
. Na kwa hekima yangu nilojaaliwa najua fika kwamba kwa wale wanaoitaka tanganyika mpya hawataishia hapo. Wataanza kuweka masharti kwa Wazanzibar na Wazanzibara, kumbuka kuna walalahoi wanaosubiri tu mchafuko huu na hakika Usalama wa Wazanbara utakuwa matatani.

Hivyo basi kama kweli tunaitafuta suluhu ya Muungano wetu tulitakiwa kuzitazama hizo kero za Muungano kabla ya Zanzibar hawajaandika katiba yao mpya ya mwaka 2010. Kila kilichobadilishwa mle (katiba ya Zanzibar) ni kero zilizokuwepo ambazo tulizipuuza na sasa ndizo sababu ya kuzaliwa kwa katiba hiyo na kumezaa Kero mpya kwa Bara. Kero juu ya kero.

Hivyo kero za muungano zimehamia Bara na sasa, nasi tunatafuta dawa yake, jino kwa jino huku tukifanya makosa yale yale waloyafanya Zanzibar ya kukiuka katiba ya Muungano. Kuirudisha Tanganyika itakuja na katiba yake ili kutoa sare kwa katiba ya Zanzibar na sii Muungano. Did we solve our problems? bila shaka ni hapana, ila tumeongeza matatizo yaani sasa sote tumekiuka Katiba ya JMT, hivyo hakuna hata sababu ya bunge hilo la katiba kuwepo.

Kitakacho fuata sasa hivi ni Zanzibar wabadilishe katiba yao ili tukubaliane nao (mjadala mwingine), Tanganyika nao waandike katiba yao halafu ndio Katiba ya JMT iundwe hii itachukua miaka 5 hadi 10 ijayo. Je tumefanikisha lipi - HAKUNA maana hata tukiwa na serikali 3 bvado swala la OIC litakuwa ktk mambo ya nje na serikali kuu (3) bado italizuia kwa sababu zile zile walizotoa tulipokuwa na serikali 2. Tunashindwa kutazama kero zenyewe badala yake tunajitazama sisi kutokana na hii kitu UBEPARI na hatukuwa tayari kuandaa mwongozo unatuwezesdha sote ktk ushirika wa JMT.
Mkuu Mkandara nimejaribu sana kukurudisha katika bandiko la Mchambuzi uelewe tofauti ya nchi, serikali,taifa n.k. na umegoma. Matokeo yake unajichanganya sana ni bahati mbaya.

Mihimili mitatu haiundi nchi hata siku moja. Nchi ipo tu kila siku provided ina mipaka, eneo na vilivyomo.
Mihimili ni nguzo za kuiwezesha serikali kutimiza majukumu. Serikali ni chombo kinachoongoza siyo nchi.
Na taifa linaundwa na mambo mengine ambayo kwa pamoja yanatengeneza nchi na kuunda serikali. Naachi hapo

Unaposema Tanganyika si nchi kwa kuachia jina kuwa Tanzania kwa kuongeza mipaka, hii maana yake tuna nchi moja yenye mipaka yake. Kuwa na nchi moja hakuzuii kuwa na serikali kama vyombo vya utawala, tuna ya znz.
Swali linakuja hii nchi iliyoongeza mipaka na kuitwa Tanzania ikimaanisha znz imo inakuwaje ndio Tanganyika tena mkuu?

Kama unakubali znz ni nchi kwakuwa na serikali, nchi hiyo ya znz imeungana na nchi gani?
Usituambie JMT! Hapana,tusingependa kuwachanganya vijana wanaotusoma tena, pengine watatucheka.

Uhalali wa znz kuwa nchi unapatikana wapi wakati tuna Tanzania yenye mipaka mipana hadi znz?
Unakuwaje na li nchi likubwa likiwa na ka nchi kadogo.
Unaweza kuwa na nchi kubwa ikiwa na serikali tofauti ndani ya nchi hizo. Hapa uelewe serikali hata za miji ni serikali.

Umesema wazanzibar hawana mamlaka kamili ya kuendesha nchi yao. Kwanini usiungane nasi kuwapatia malaka kamili kadri wanavyotaka? Je serikali 2 ndizo zitawapa mamlaka baada ya kushindwa miaka 50?

Unakubali kero zilikuwepo zikapuuza. Nani amepuuza kama si CCM na serikali 2?tume ya Amina ilikuja na mapendekezo, hayajafanyiwa kazi miaka 12. Mkandara anasema ni marekebisho kidogo tu tuendelee na mfumo ule ule anaoulalamikia umepunguza nguvu za nchi pendwa ya znz na siyo kuua Tanganyika.

Tume ya AMINA iiondoa mambo 11 ikiwemo Anga na Bandari. Wznz wakaondoa mafuta na gesi kwakusikia tu. Kila walipofanya hawakuhitaji kushauriana na JMT. Walifanya kwasababu wana kiburi.

Mwaka 2010 wakakamilisha kiburi,leo tunawajibika kupeleka mapendekezo ya kujenga vyoo vya shule yetu kwa BLW .
Huu uhuni, Tanganyika haiwezi kuendelea nao. Vipi unaona eti Tanganyika kujitafutia nafasi ni kuvunja katiba, wakati huo huo unatetea znz ilikuwa na haki kwaasababu ya kupuuzwa. Mkuu unaeleweka hapa kweli.

Usalama wa wznz baada ya serikali 3 hauna tatizo. Wznz wana nchi yao , wana hiari ya kubaki Tanganyika kwa taratibu za Tanganyika au wana hiari ya kurudi nyumbani.Wasi wasi ulio nao Mkandar ni kuhusu ubaradhuli wa kuchoma Watanganyika moto.
Hilo halitatokea,Watanganyika wamevuka kiwango. Kama tumehifadhi Wanyarwanda wanaotutukana leo seuse wznz.

Kuhusu mambo 11 yaliyoongezwa, nimekuuliza uniatjie moja tu linaloinufaisha Tanganyika hukuwez,hukuwa na jibu wala mstari mmoj. Ukanitaka nikakupa mifano 5 ya haraka haraka. Kwanini bado unazungumzia kitu usicho na ushahidi nacho?

Kuhusu OIC hilo litakwisha kwasababu znz itakuwa na uwezo wa kujiunga na taasisi au mashirika ya kimataifa au kikanda.
Tanganyika sijui kama itakuwa na kikwazo na kwasababu gani.

Kwasasa ambapo Tanganyika ndiyo Tanzania itakuwa ni ujinga na upuuzi kuacha jina kutumiwa kwa namna isiyoeleweka.
Tumeona jina likitumika kusajili meli za watu binafasi wa Iran, sidhani kama linakubali kwa mantiki tu.
Hivyo jiunge nasi kuitakia znz mambo mema, malaka kamili.
 
Mkandara.

Wachumi wanasema hakuna Muungano pasipo manufaa kwa wanao ungana. Hata katika ndoa tunaambiwa tunapata manufaa ya mapenzi na kuhurumiana baina ya wanandoa.

Je katika muungano huo wa 50/50 Tgk inanufaika kwa lipi?



Mkuu wangu swala lako swadakta tena limeingia ktk Uislaam na hakika Uislaam ndio way of life. Swali langu linakuja hivi:-
Umejaaliwa kuoa wake wawili, mmoja kakupa watoto 10 wa kiume, na mke wa pili kakupa watoto wawili wa kiume, Je mirathi yako utaigawa kwa 50/50 kutokana na matumbo ya mama zao? ama utazigawa kulingana na asilimia sawa kwa hao watoto wako wote 12?
 
Mkuu Mkandara nimejaribu sana kukurudisha katika bandiko la Mchambuzi uelewe tofauti ya nchi, serikali,taifa n.k. na umegoma. Matokeo yake unajichanganya sana ni bahati mbaya.

Mihimili mitatu haiundi nchi hata siku moja. Nchi ipo tu kila siku provided ina mipaka, eneo na vilivyomo.
Mihimili ni nguzo za kuiwezesha serikali kutimiza majukumu. Serikali ni chombo kinachoongoza siyo nchi.
Na taifa linaundwa na mambo mengine ambayo kwa pamoja yanatengeneza nchi na kuunda serikali. Naachi hapo

Unaposema Tanganyika si nchi kwa kuachia jina kuwa Tanzania kwa kuongeza mipaka, hii maana yake tuna nchi moja yenye mipaka yake. Kuwa na nchi moja hakuzuii kuwa na serikali kama vyombo vya utawala, tuna ya znz.
Swali linakuja hii nchi iliyoongeza mipaka na kuitwa Tanzania ikimaanisha znz imo inakuwaje ndio Tanganyika tena mkuu?

Kama unakubali znz ni nchi kwakuwa na serikali, nchi hiyo ya znz imeungana na nchi gani?
Usituambie JMT! Hapana,tusingependa kuwachanganya vijana wanaotusoma tena, pengine watatucheka.

Uhalali wa znz kuwa nchi unapatikana wapi wakati tuna Tanzania yenye mipaka mipana hadi znz?
Unakuwaje na li nchi likubwa likiwa na ka nchi kadogo.
Unaweza kuwa na nchi kubwa ikiwa na serikali tofauti ndani ya nchi hizo. Hapa uelewe serikali hata za miji ni serikali.

Umesema wazanzibar hawana mamlaka kamili ya kuendesha nchi yao. Kwanini usiungane nasi kuwapatia malaka kamili kadri wanavyotaka? Je serikali 2 ndizo zitawapa mamlaka baada ya kushindwa miaka 50?

Unakubali kero zilikuwepo zikapuuza. Nani amepuuza kama si CCM na serikali 2?tume ya Amina ilikuja na mapendekezo, hayajafanyiwa kazi miaka 12. Mkandara anasema ni marekebisho kidogo tu tuendelee na mfumo ule ule anaoulalamikia umepunguza nguvu za nchi pendwa ya znz na siyo kuua Tanganyika.

Tume ya AMINA iiondoa mambo 11 ikiwemo Anga na Bandari. Wznz wakaondoa mafuta na gesi kwakusikia tu. Kila walipofanya hawakuhitaji kushauriana na JMT. Walifanya kwasababu wana kiburi.

Mwaka 2010 wakakamilisha kiburi,leo tunawajibika kupeleka mapendekezo ya kujenga vyoo vya shule yetu kwa BLW .
Huu uhuni, Tanganyika haiwezi kuendelea nao. Vipi unaona eti Tanganyika kujitafutia nafasi ni kuvunja katiba, wakati huo huo unatetea znz ilikuwa na haki kwaasababu ya kupuuzwa. Mkuu unaeleweka hapa kweli.

Usalama wa wznz baada ya serikali 3 hauna tatizo. Wznz wana nchi yao , wana hiari ya kubaki Tanganyika kwa taratibu za Tanganyika au wana hiari ya kurudi nyumbani.Wasi wasi ulio nao Mkandar ni kuhusu ubaradhuli wa kuchoma Watanganyika moto.
Hilo halitatokea,Watanganyika wamevuka kiwango. Kama tumehifadhi Wanyarwanda wanaotutukana leo seuse wznz.

Kuhusu mambo 11 yaliyoongezwa, nimekuuliza uniatjie moja tu linaloinufaisha Tanganyika hukuwez,hukuwa na jibu wala mstari mmoj. Ukanitaka nikakupa mifano 5 ya haraka haraka. Kwanini bado unazungumzia kitu usicho na ushahidi nacho?

Kuhusu OIC hilo litakwisha kwasababu znz itakuwa na uwezo wa kujiunga na taasisi au mashirika ya kimataifa au kikanda.
Tanganyika sijui kama itakuwa na kikwazo na kwasababu gani.

Kwasasa ambapo Tanganyika ndiyo Tanzania itakuwa ni ujinga na upuuzi kuacha jina kutumiwa kwa namna isiyoeleweka.
Tumeona jina likitumika kusajili meli za watu binafasi wa Iran, sidhani kama linakubali kwa mantiki tu.
Hivyo jiunge nasi kuitakia znz mambo mema, malaka kamili.
Mkuu wangu rudia tena kujisoma wewe mwenyewe maana unajichanganya wewe na sio mimi.

Nimesema hivi NCHI ina mihimili mitatu 1.Serikali, 2. Mahakama na 3. Bunge. Sasa wewe unaposema mihimili ni kuiwezesha tu SERIKALI ambayo ni mhimili mmoja ktk nchi sijui hii imekaaje? nisome vizuri...

Nyie na wanasiasa hao uchwara mnataka kutuaminisha kwamba kinachoundwa hapa ni serikali 3 kwa nchi moja, jambo ambalo ni uongo kwa sababu huwezi kuirudisha serikali ya Tanganyika pasipo kuzirudisha pia Bunge lake na mahakama yake, hivyo tayari umeisha unda Nchi ya Tanganyika. Wadanganyeni tu hao wajinga wanaodhania kinachoundwa hapa ni serikali 3 sijui tutachangia Bunge moja na mahakama moja au vinginevyo mnavyofikiria nyie. hakuna kitu kama hivcho ni lazima nchi ya Tanganyika irudi na mihimili yake yote, serikali ikiwa moja wapo.

Ukweli ni kwamba mfumo huu unaosemwa kuwa na serikali 3 una maana moja tu. Tutakuwa na nchi 2 huru ndani ya Taifa moja (JMT), kama ilivyo Marekani, Canada na kadhalika. Muundo wa muungano huo utakuwa hivi:- Kila nchi ina serikali yake, mahakama yake na bunge lake. Kisha ile inayosemwa serikali ya 3 ni serikali kuu ya TAIFA (nation) Tanzania. Hii pia litakuwa na serikali yake, mahakama yake na bunge lake kama Federal Government. Hivi vitu haviwezi kuepukika ila ktk mijadala ili kuwaweka watu sawa wadhanie kwamba kinachobadilika hapa ni ujio wa serikali tu, hapana tunaunda nchi zetu upya na kuunda muungano upya!.

Maadam Zanzibar ni nchi yenye serikali, bunge na mahakama nina hakika Tanganyika pia itakuwa na serikali bunge na mahakama yake ndio maana waraka umeacha kutaja muundo wa NCHI hizi, ukitumia tu neno serikali husika zitaamua muundo wake lakini ukweli ni kwamba NCHI (republic) husika zitaamua muundo wa serikali, bunge na mahaka zao kulingana na mamlaka walokabidhiwa. Kinachoundwa hapa ni nchi ya Tanganyika ambayo ilikufa mwaka 1967, hivyo inarudishwa na kupewa mamlaka yake kama ilivyo NCHI ya Zanzibar kwa kutumia ujanja ujanja wa kusema tunataka serikali 3. Hapo sisi pia tutakuwa tunaibvunja katiba ya Muungano kama walivyofanya Zanzibar na sio suluhisho la kero bali ubishi na jeuri kama walokuwa nayo wao bila kujali katiba wala makubaliano....

Kufuatia maamuzi haya ya kijinga ya serikali 3, ndio maana nasema hao wajumbe wa kuandika katiba mpya sielewi wanafanya nini hapo Dodoma maana inatakiwa kwanza tuizae Tanganyika yenye katiba yake, iunde serikali yake, bunge lake na mahakama yake kama ilivyokuwa kabla ya mwaka 1967. Kisha Zanzibar nao waondoe maswala ya muungano kama itakavyokubalika ktk katiba yao hiyo mpya kuleta uuwiano wa kimkataba. Na baada ya hapo ndipo tutaweza kuandika katiba ya jamhuri ya Muungano hiyo ni miaka mitano kama sio 10 ijayo.

Kinyume cha hapo ni upotoshaji na ufisasdi mkubwa unafanyika hapa maana kilichotuleta Dodoma ni kuandika katiba mpya ambayo inalingana na mazingitra tulokuwepo leo, ile ya mwaka 1977 imepitwa na wakati, haikidhi maswala ya demokrasia, haki za binadamu, soko huria na Utandawazi, haihusiani kabisa na swala la serikali 1, 2 wala 3. Maoni ya wananchi kuhusu serikali ngapi, ni maoni tu yasiyoangalia athari zake bali ni fikra za za mwamba ngoma ktk ubepari.

Matatizo na kero za muungano zitabakia pale pale, na matokero yake ni kuuvunja Muungano maana kutoka 2 kwenda 3 ni utenganishi zaidi ya kutoka 2 kwenda 1. Kuwepo kwa serikali 2 ilikuwa hatua ya kwanza kufikia serikali 1 na sii 3. Hizi kero zingeweza kabissa kutatuliwa kabla na bado kuna muda na nafasi ya kuzitatua wakati katiba mpya ikiandikwa ili tuwe na katiba mpya kabla ya 2015, maana nina hakika Zanzibar wanaweza kabisa kuondoa zile kero zao ktk maswala yote ya Ushuru, bandari na elimu ikiwa sisi tutakuwa wasikivu na tufanye japo kama nilivyopendekeza.

Kinachowauma Zanzibar ni njaa tu, ndio nikasema sii vizuri kwa mama mjamzito kula kwa ajili yake tu maadam kabeba kiumbe tumboni ni muhimu afahamu anapokula hula kwa ajili ya viumbe wawili na kuzingatia baby nutrition haiondowi mamlaka yake. Kauli ya Pinda, warioba ku deny kuwepo kwa Zanzibar kama nchi ilihali wanadai kuwepo kwa nchi ya Tanganyika ni sawa na kumnyima yule mtoto Uhai wake kwa sababu tu ni mimba ambayo kaibeba Mama. Sasa ikiwa mnaona tunaumia cha kujiuliza nikwa nini tulikubali kubeba mimba hii na sii kusikilizia machungu ya mtoto huyo anavotupiga mateke kwa sababu ana njaa yake! Je ni busara kuitoa mimba hiyo kwa sababu tu inatuumiza wakati sisi wenyewe ndio tulipenda kuibeba!

Bado hunielewi mkuu wangu?
 
Katika eneo tunalokubaliana ni moja tu, kwamba mchakato ulikuwa na matatizo.
Kabla ya hapo kulitakiwa kwanza maoni ya wananchi kama wanataka 1,2,3 au vinginevyo. Hilo nakubaliana nawe na wala sina wahka. Uhuni huo umefanywa na CCM kwa kile wanachoamani na unachoamini ni matatizo kidogo tu, yanarekebishika ingawa miaka 50 hakuna lolote.

Nisipokubaliana nawe ni pale unapoaminisha kuwa serikali 2 zinawezekana kuna matatizo madogo madogo. Kuvunja katiba ya nchi ni tatizo dogo!!!!!
Na kwanini lionekane kubwa Watanganyika wanapoamua kuweka mambo sawa sawa ili wznz wasiteseke kujificha na kubadili mambo.

Nisipokubaliana nawe ni pale unaposhauri wznz wanaweza kubadili katiba yao kukidhi masharti ya katiba ya JMT. Hawa watu wameonyesha kiburi kwa muda mrefu na wala hawaonekani kujifunza kutoka na na viburi vyao.
Leo tukae tena tunawabembeleza, kwa lipi kwanini na kwa faida gani.

Nisipokubaliana nawe ni pale unapotaka tuwe na serikali 1. Wznz watashauriwa na nani waache ubora na kuwa Watanzania. Hawa watu hawataki hata kuitwa Watanzania, leo watakuwaje wamoja na Watanzania. Myth

Nisichokubalina nawe ni kusema Tanganyika imekufa mwaka 1967. Kama imekufa znz imeungana na nani. Na kwanini mmoja wa wazazi afariki halafu tubaki tukiamini kuwa mama ana ndoa na kaburi. Kwamba mtoto amechukua nafasi ya baba! Mkandara, mkuu wangu wapi na wapi.
 
SAMUEL SITTA NA UFUFUO WA TANGANYIKA

SEHEMU YA KWANZA

Samuel sitta ni mtu muhimu sana katika nyakati na harakati hizi za kuizindua Tanganyika kwa sababu kuu mbili:

*Kwanza, yeye ndiye mwenyekiti wa bunge la katiba, nafasi aliyoishinda kwa kura nyingi, almost in a bipartisan fashion katika bunge lenye wajumbe wa vyama vingi vya siasa.

*Pili, Sitta ni kiongozi ambae ana practical experience na suala zima la Tanganyika kupitia sakata la G55 mwaka 1994 ambapo yeye alikuwa ndiye waziri wa katiba na sheria.

Sababu hizi mbili ni tosha kwa umma kuwa na kila sabab ya kuamini kwamba - kuzinduka kwa Tanganyika au kuendelea kufunikwa kwa Tanganyika chini ya zulia, kwa kiasi kikubwa sana kutatokana na sitta kama kiongozi lakini pia sitta kama kiongozi wa serikali ya ccm.

Siku kadhaa zilizopita, vyombo vya habari viliripoti kwamba sitta ametoa mapendekeza binafsi kwamba litakapokuja suala la kura ya siri vis a vis wazi, yapo masuala ambayo yatahitaji kura ya wazi na yale yatayojitaji kura ya siri. Katika hili la siri inasemekana alikuwa akilenga suala la mfumo wa muungano. Sio ajabu sana kwa sitta kuja na mtazamo huu kwani kama alivyojadili Nguruvi3, sitta yupo upande wa serikali mbili na pia serikali tatu kutokana na wakati uliopo mbele yake. Kwa wale wanaohitaji Tanganyika yao, sitta comes in two versions: sitta as a threat and sitta as an opportunity kwa watanganyika na ndoto yao ya muda mrefu juu ya uzinduzi wa Tanganyika.

Sehemu nzuri zaidi ya kuanza kumjadili sitta iwapo he offers threat or opportunity kwa watanganyika na ndoto yao, pengine ni kwa kumtazama katika kioo cha historia, hasa kuanzia kwenye sakata la G55 - msimamo wake, mtazamo wake na maamuzi yake. Hivyo ndivyo nadhani tutaweza mtabiri sitta kuelekea mjadala wa muundo wa muungano bungeni dodoma wiki kadhaa zijazo.

Ili kuweza kumchambua sitta vizuri, ni muhimu tukaanza kwa kuijadili hoja ya G55 ambayo iliishi kwa muda wa wiki tatu tu huku sitta akiwa ni kiongozi muhimu sana wa serikali katika kuisimamia hoja hiyo.

Tukumbuke kwamba kamati ya wabunge wa ccm chini ya waziri mkuu malecela na chama cha mapinduzi chini ya mtendaji mkuu wa chama - katibu mkuu horace kolimba waliridhia hoja hii kutokana na uzito na pia timing yake hivyo kumshauri rais mwinyi kuikubali.

Hoja ya Tanganyika iliishi kwa wiki tatu tu, lakini muhimu zaidi ni kwamba tuelewe hoja hii ilipitia versions kuu tatu katika maisha yake:

Version ya kwanza ilitiwa saini na wabunge 44 (sio 55), na vilivyokuwa muhimu katika version hii ya kwanza ni kwamba:

Ilikuwa na paragraphs nane in its preamble huku hoja kuu ikielekeza serikali ya JMT kuandaa na kuwasilisha a bill bungeni to amend muungano (hivyo katiba ya jmt ya 1977) ili kuanzisha serikali ya Tanganyika kufuatia hatua ya serikali ya zanzibar kujiunga na oic, hatua ambayo ilikuwa ni kukiuka katiba ya jmt 1977. Katika preamble hiyo hoja ya msingi ikawa kwamba watanzania bara wengi hawaridhishwi na mfumo wa serikali mbili ambapo znz wao wana serikali yao inayofanya maamuzi yao huku tanganyika ikiwa haina serikali ya aina hiyo ndani ya muungano, na hoja ikaendelea to argue kwamba - mapungufu haya yatavunja muungano, hivyo njia pekee ya kulinda muungano ni kuanzisha serikali ya Tanganyika ndanni ya muungano, hivyo kuleta mfumo wa serikali tatu.

Version ya pili ikazaliwa siku chache baadae na tofauti na ya kwanza iliyosainiwa na wabunge 44, ya pili ilisainiwa na wabunge 55. Katika sehemu ya utangulizi ilirudia yale yale ya version ya kwanza lakini ikaja na nyongeza moja muhimu sana kwamba- suala la mfumo wa muungano ni suala basic and fundamental hivyo linahitaji ushirikishwaji wa wananchi kwani wao ndio wenye mamlaka ya mwisho juu ya aina ya muugano wanaoutaka. Kwahiyo version hii ya pili ikaelekeza serikali kuandaa kura ya maoni (referendum) kabla ya december 1995 ili kupata maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa serikali ya Tanganyika ndani ya muungano. Motion hii ikawa circulated kwa wabunge ijumaa ya tarehe 20, august 1994.

Kwa mujibu wa issa shivji, wikiendi hii ya august 20-22, 1994 ilikuwa ni moja ya wikiendi ngumu sana za uongozi wa ccm na serikali yake; neno "referendum" lilikipa chama woga mkubwa sana na kukitikisa vilivyo, na tofauti na kipindi cha nyuma (kabla ya mageuzi ya kiuchumi) ambapo chama kilikuwa na uwezo wa kuzima hoja za aina hii (mfano sakata la jumbe), mwaka 1994 ilikuwa ni kipindi cha joto la mageuzi ya kisiasa nchini (tume ya nyalali ikiwa tayari imefanya kazi yake), kwahiyo kuzima hoja ya Tanganyika haikuwa ni jambo rahisi. Kwahiyo chama kililazimika kuja na mbinu nyingine.

Jumamosi ya tarehe 21 august 1994, ccm ikajifungia na wabunge wake kama kamati na baadae chama kikaja na tamko kwa umma kwamba "muafaka/maridhiano" juu ya tanganyika umeshapatikana; suala hili halikuleta kizaa zaa sana kwenye umma kwani tofauti na nyakazi za leo, umma ule haukuwa na uelewa na pia mwamko sana juu ya Tanganyika. Hali hii ikaipa ccm nafasi nzuri kuendelea na mikakati yake ya kuizima hoja ya G55;

Maridhiano husika yakazaa version ya tatu ya motion ya G55 ambayo iliwasilishwa bungeni jumatatu ya tarehe 23 august 95 na kupitishwa na majority ya wabunge (2/3);

Versio ya tatu ya motion ya G55 ilikuwa tofauti na version 1 & 2 ambapo version 3 ilipunguzwa paragraph kuwa sita kwenye preamble tofauti na paragraph tisa kwenye version ya pili; katika version three, kulikuwa na two main shifts:

1. Ilihamisha mkazo kutoka ule wa version two kwamba ni wabara ndio walikuwa wamechoshwa na mfumo wa serikali mbili, na kusema kwamba malalamika ni ya pande zote mbili za muungano;

2. Tofauti na version za awali ambazo zilisema serikali moja haitekelezeki tena, versio ya tatu ilikaa kimya juu ya nini kinatekelezeka, nini hakitekelezeki.

Ni muhimu tuone issa shivji anasema nini juu ya mabadiliko haya:

Kwa mtazamo wake, the first shift hapo juu ilikuwa ni sahihi kwani iliakisi historia ambapo anasema:

Sisi wabara tuna tabia ya kusahau
Kwamba wazanzibari wakati wote wakipinga serikali mbili. Pia anajadili kwamba hoja ya serikali tatu haikutokana na G55 bali ilijengwa siku nyingi na wasomi (always ignored na CCM) lakini pia na kina jumbe et al. Muhimu pia anasema kwamba "hoja ya Tanganyika has been a demand for democracy";ukweli huu unasimama hadi leo; kuna quote muhimu pia toka kwa shivji ambapo anasema:

So the people of zanzibar in a sense struggled and sacrificed for our right to have our own government (right to self determination) long before the Mtikila of this world rediscovered Tanganyika

Muhimu katika version ya tatu pia ni kwamba ilielekeza serikali ya muungano to organize and supervise mchakato utakaohusisha wananchi katika maamuzi ya kuzindua Tanganyika na kupelekwa bungeni mapendekezo juu ya mfumo unaofaa wa muungano, lakini muhimu, suala zima la serikali tatu, kabla ya aprili 1995.


Itaendelea ambapo tutaangalia involvement ya samuel sitta katika sakata zima la ufufuo wa Tanganyika 1994-5 akiwa waziri wa sheria na katiba.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Katika eneo tunalokubaliana ni moja tu, kwamba mchakato ulikuwa na matatizo.
Kabla ya hapo kulitakiwa kwanza maoni ya wananchi kama wanataka 1,2,3 au vinginevyo. Hilo nakubaliana nawe na wala sina wahka. Uhuni huo umefanywa na CCM kwa kile wanachoamani na unachoamini ni matatizo kidogo tu, yanarekebishika ingawa miaka 50 hakuna lolote.

Nisipokubaliana nawe ni pale unapoaminisha kuwa serikali 2 zinawezekana kuna matatizo madogo madogo. Kuvunja katiba ya nchi ni tatizo dogo!!!!!
Na kwanini lionekane kubwa Watanganyika wanapoamua kuweka mambo sawa sawa ili wznz wasiteseke kujificha na kubadili mambo.

Nisipokubaliana nawe ni pale unaposhauri wznz wanaweza kubadili katiba yao kukidhi masharti ya katiba ya JMT. Hawa watu wameonyesha kiburi kwa muda mrefu na wala hawaonekani kujifunza kutoka na na viburi vyao.
Leo tukae tena tunawabembeleza, kwa lipi kwanini na kwa faida gani.

Nisipokubaliana nawe ni pale unapotaka tuwe na serikali 1. Wznz watashauriwa na nani waache ubora na kuwa Watanzania. Hawa watu hawataki hata kuitwa Watanzania, leo watakuwaje wamoja na Watanzania. Myth

Nisichokubalina nawe ni kusema Tanganyika imekufa mwaka 1967. Kama imekufa znz imeungana na nani. Na kwanini mmoja wa wazazi afariki halafu tubaki tukiamini kuwa mama ana ndoa na kaburi. Kwamba mtoto amechukua nafasi ya baba! Mkandara, mkuu wangu wapi na wapi.
Mkuu wangu sijui kama unanisoma vizuri ama laa.

Mimi sikubaliani na serikali 3 kutokana na sababu za maana kabisa nazo zimezitaja. kwanza sio wakati wake na pili serikali 3 ni kuirudisha Tanganyika ---- majibu ya katiba hasi ya Zanzibar. Hii ni kuendelea kuivunja katiba ya Jamhuri iliyopo (jino kwa jino)kama vile Kenya wakiondoa Ubalozi wao kwetu kwa sababu nasi tunaondoa Ubalozi kwa kujibu mapigo lakini hatutaki kutazama kwa nini Kenya wamemfukuza balozi wetu.

Pili, tulichoomba sisi wananchi wote ni katiba mpya ambayo inakwenda na wakati sio swala la Muungano, Kero za Muungano tulizipuuza miaka yote 50, na tukitumia maguvu kuulinda, hivyo nguvu hizo zingeendelea kuwepo. (dhidi ya viongozi wanaokiuka Kiapo)Sasa kutokana na uzushi wa hizi serikali 3 kama suluhisho.

Katiba mpya haiwezi kupatikana na sijui kama hao wajumbe wameliona hili, maana huwezi kutunga katiba mpya ya Jamhuri wakati hakuna nchi ya 2 tayari. Tanganyika yenye katiba yake, bunge lake na mahakama yake. Hivyo nawauliza nyie hao wabunge wa hilo bunge la katiba wanafanya nini Dodoma maana huwezi kuitunga katiba ya Taifa mbele ya zile za nchi. Kifupi tunapoteza mabillioni ya kodi za wananchi kwa usanii huu mpya na watu mnao ushangilia.

Labda sasa niwageukie Wazanzibar, ni hivi muundo wa nchi yetu ni wa kipekee kabisa kiasi kwamba tuliipoteza Tanganyika na kuyapa mamlaka kamili TAIFA la TANZANIA ambalo lina viongozi toka pande zote 2. Hivyo Zanzibar kama nchi ilikuwa tu na mamlaka ktk maswala yasokuwa ya Muungano ambayo kulingana na culture zao, Identity yao viliachwa wazi kwao na ndio maana wao wana Kadhi mkuu, sisi bara hatuna.

Huku bara hatukuwa na tatizo infact tulipoteza sio Identity yetu pekee bali hadi culture zetu na tukachagua Utanzania ambao kiswahili ndio ikiwa lugha yetu. Maswala ya culture na imani yakawekwa kuwa ni haki ya kila mtu kuabudu anachokiamini hata kama unaamini mizimu japo wachawi walikuwa wakiuawa kimakosa. hahah hahah haha!

Zanzibar hawawezi kuwa na mamlaka kamili isipokuwa ya republic na ktk maswala yasokuwa ya muungano. Ikiwa kweli kuna mambo yaloingizwa Kinyemela ilitakiwa yatazamwe na yarudiwe upya kutazamwa na bunge la TAIFA ili kukidhi mahitaji ya sehemu zote. Na ikiwa kero zao zipo ktk mambo yale ya muungano ikiwa ni pamoja na ugawanaji wa pato la taifa au uwekezaji ktk miundombinu ya Taifa hili linaweza kabisa kutatuliwa maana kama tumeweza kugawa madaraka ya viongozi wa pande mbili na wakaridhika kusiwe na tatizo tunashindwa vipi ktk hili? ina maana katiba yetu haikidhi muundo wa kiuchumi ktk makusanyo na ugawaji wa pato la Kitaifa.

Tunashindwa vipi kujenga Bandari ya freeport Zanzibar na Airport ya kimataifa wakati tuna taifa moja?..lakini wepesi kukubali ijengwe Bagamoyo na sii Mtwara au Tanga ilihali Ushuru wake unaingia mfuko wa Taifa ijengwe zanzibar au bagamoyo. Zanzibar ilikuwa central of business kwa karne, kwa nini tusitumie nafasi hiyo ambayo kijiographia imekuwepo toka karne ya kwanza? jibu lake ni UBINAFSI wa sisi bara.

Maana Tax zote zinazokunywa kwa mauzo toka kwa wateja mbalimbali walokuja Znz kununua mali hizo linaenda mfuko wa Taifa bila kujali limezalishwa wapi na Wazanzibar wataona maendeleo, wataona ajira zikipatikana pasipo kuja bara na kadhalika, pia wabara wataingia Zanzibar pasipo choyo maana riziki zipo. Kwa Zanzibar kuwa na bandari ya freeport kinachoondoka hapo ni Import duty tu ili kuyavuta mashirika ya nje kuwekeza ktk uuzaji wa jumla na mataifa mengine wapate nafuu ya kuja Tanzania badala ya Dubai na China. Na pia nafuu kwa Watanzania wote iwe bara au visiwani.

Tungejengea University ya Kimataifa Znz, Hospital ya kimataifa Znz kwa sababu wapo Watanzania bara wanaoishi huko wakiitumikia serikali kuu ama wafanya biashara kwa nini kila kitu kijengwe bara?. Na maadam hivi vitu vipo ktk mambo ya muungano pato lake linakwenda ktk mfuko wa Taifa. Hivyo Zanzibar itaonekana ikichangia vizuri ktk mfuko wa Taifa na kutuwezesha kujichanganya zaidi badala ya kugawana umaskini.

Leo hii Mtwara inaonekana haichangii vizuri ktk mfuko wa Taifa na mkoa maskini wakati wana gas ni kwa sababu uuzaji wa gas umepelekwa Dar. Kodi za mapato zinahesabika ni dar imechangia, kama tungekuwa na madaraka mikoani na kuzinufaisha sehemu kama hizi tungeona mchango wao na pia wananchi wengi wangehamia Mtwara kupata ajira na sii kila mtu kukimbilia Dar. Haya ndio mawazo yangu mkuu wangu na pasipo hili swala la serikali 1,2,au3 tungekuwa na katiba mpya kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015, lakini kwa jinsi tunavyokwenda sasa hivi tusahau kabisa Katiba mpya.
 
Mchambuzi.
Mkuu wangu kuna sehemu umeandika hivi:-

"Ilikuwa na paragraphs nane in its preamble huku hoja kuu ikielekeza serikali ya JMT kuandaa na kuwasilisha a bill bungeni to amend muungano (hivyo katiba ya jmt ya 1977) ili kuanzisha serikali ya Tanganyika kufuatia hatua ya serikali ya zanzibar kujiunga na oic, hatua ambayo ilikuwa ni kukiuka katiba ya jmt 1977. Katika preamble hiyo hoja ya msingi ikawa kwamba watanzania bara wengi hawaridhishwi na mfumo wa serikali mbili ambapo znz wao wana serikali yao inayofanya maamuzi yao huku tanganyika ikiwa haina serikali ya aina hiyo ndani ya muungano, na hoja ikaendelea to argue kwamba - mapungufu haya yatavunja muungano, hivyo njia pekee ya kulinda muungano ni kuanzisha serikali ya Tanganyika ndanni ya muungano, hivyo kuleta mfumo wa serikali tatu."

Sasa nakuuliza upya tukiunda serikali ya 3, je hiyo serikali kuu haitakataa tena swala la OIC kwa sababu zile zile? maana walichoomba Znz mwanzoni ilikuwa OIC kwa ajili yao wenyewe yaani lisiwe swala la muungano. Tulishindwa nini kuliondoa swala hilo kuwa lisiwe la Muungano ila tunafikiri kesho tukiwa na serikali 3 halitakuwa la muungano maana sababu ziko pale pale hazitaondoka.

Hofu kubwa ya viongozi wa bara ni Uislaam hili halina kificho na tunajua wazi, sasa ikiwa vichwa vitakavyo ongoza nchi hizi ni vile vile, akili zile zile, unafikiri hizo serikali 3 zitabadilisha kitu gani ambacho leo hakiwezi kubadilishwa ndani ya serikali mbili.
- Nawakilisha.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi.
Mkuu wangu kuna sehemu umeandika hivi:-

"Ilikuwa na paragraphs nane in its preamble huku hoja kuu ikielekeza serikali ya JMT kuandaa na kuwasilisha a bill bungeni to amend muungano (hivyo katiba ya jmt ya 1977) ili kuanzisha serikali ya Tanganyika kufuatia hatua ya serikali ya zanzibar kujiunga na oic, hatua ambayo ilikuwa ni kukiuka katiba ya jmt 1977. Katika preamble hiyo hoja ya msingi ikawa kwamba watanzania bara wengi hawaridhishwi na mfumo wa serikali mbili ambapo znz wao wana serikali yao inayofanya maamuzi yao huku tanganyika ikiwa haina serikali ya aina hiyo ndani ya muungano, na hoja ikaendelea to argue kwamba - mapungufu haya yatavunja muungano, hivyo njia pekee ya kulinda muungano ni kuanzisha serikali ya Tanganyika ndanni ya muungano, hivyo kuleta mfumo wa serikali tatu."

Sasa nakuuliza upya tukiunda serikali ya 3, je hiyo serikali kuu haitakataa tena swala la OIC kwa sababu zile zile? maana walichoomba Znz mwanzoni ilikuwa OIC kwa ajili yao wenyewe yaani lisiwe swala la muungano. Tulishindwa nini kuliondoa swala hilo kuwa lisiwe la Muungano ila tunafikiri kesho tukiwa na serikali 3 halitakuwa la muungano maana sababu ziko pale pale hazitaondoka.

Hofu kubwa ya viongozi wa bara ni Uislaam hili halina kificho na tunajua wazi, sasa ikiwa vichwa vitakavyo ongoza nchi hizi ni vile vile, akili zile zile, unafikiri hizo serikali 3 zitabadilisha kitu gani ambacho leo hakiwezi kubadilishwa ndani ya serikali mbili.
- Nawakilisha.

Mkuu Mkandara,

Sina jibu la uhakika juu ya swali lako na hoja yako nzima hapo juu, pengine wapo wenye uelewa zaidi watasaidia. Nilichowasilisha hapo juu ilikuwa ni uchambuzi juu ya jinsi gani hoja ya Tanganyika ilibuka bungeni na kuishi kwa wiki tatu kupitia three different versions; ingawa nilitaja suala la OIC, lakini nadhani pia umenisoma pia kwamba hoja ya Tanganyika haukuzaliwa na OIC/G55 bali ilishaibuliwa na wasomi, jumbe et al in the context of democracy and right to self determination;

Nia yangu katika bandiko nililoanzisha ni kujaribu kujenga mjadala juu ya umuhimu wa samuel sitta katika safari ya kuelekea kwa uzinduzi wa Tanganyika na pia juu ya kwanini hoja ya Tanganyika inaendelea kupumua hadi leo hii licha ya juhudi nyingi na za muda mrefu za kuifukia chini ya zulia la "kijani";

Kama nilivyosema, sina majibu kwa maswali yako lakini iwapo unatafuta my opinion, basi ni hii:

Suala la znz na oic lilivutia hisia za watu wengi kwa vile lilikuwa ni suala la kikatiba zaidi lakini pia pakiwa na hoja juu ya madhumuni ya oic ya wakati ule yalikuwa ni nini na kama yalikuwa yanaendana na Tanzania as a secular state kwa mujibu wa katiba ya jmt 1977; katiba ya 1977 inasema kuwa:

shughuli zote za dini zitafanywa nje ya mamlaka ya nchi.

Tufahamu pia kwamba OIC ya sasa na ile ya 1992 hazifanani kwa maana ya kwamba OIC ya sasa haiongozwi na itikadi za kidini bali za ushirikiano wa kiuchumi zaidi; marekebisho ya jumuiya hii yalifanyika baada ya wahusika kubaini kwamba jumuiya ilikuwa na mapungufu katika agenda yake ya kukuza ushirikiano baina ya mataifa mbalimbali; kwa mfano, wakati ule (miaka ya tisini), katiba ya JMT (pamoja na mapungufu yake) iliweka wazi kwamba tanzania ni nchi moja, na pia ni a secular state; katika mazingira haya, zanzibar kujiunga na oic ya wakati ule ilikuwa kinyume na katiba ya jmt 1977 pamoja na ubovu wa katiba kwa wakati ule, na pia zanzibar kupitia katiba yake haikuwa inajitambulisha kama moja ya nchi shiriki za muungano bali "sehemu ya muungano"; kwa mantiki hii, zanzibar kama "sehemu ya jamhuri muungano", kujiunga na jumuiya ya kimataifa pia ilikuwa ni kinyume cha katiba;

Katika mazingira ya sasa ambapo znz ni nchi inayoelekea kwenye mamlaka kamili, kazi kubwa mbele yao ni kuipigania Tanganyika izinduliwe kwanza la sivyo suala la mamlaka kamili kwa znz itaendelea kuwa na vikwazo vingi, including suala la kujiunga na OIC, FIFA n.k; kwa maana nyingine, tusaidiane kirudisha Tanganyika ili kila mmoja awe na uhuru wa kujiamulia wanataka kujiunga wapi, na hata kuvunja muungano iwapo umma wa pande zote utaamua hivyo; kwa misingi hii, suala la znz kwenda oic litakuwa sawa na la uganda ambalo haliathiri kabisa uhusiano na ushirirkiano baina yake na Tanzania;

Nadhani focus yetu kwa sasa iwe pana zaidi kwa kujadili mapungufu ya katiba ya JMT (1977), na haja ya katiba mpya ya jmt lakini pia na ya tanganyika ( suala la serikali tatu) ambapo kila nchi itakuwa na mambo kadhaa ya kujiamulia kwa uhuru wake iwe ikiwa iwe ni OIC, FIFA, COMESA n.k, na ushirikiano ubakie kwenye mambo machache, na kama haiwezekani, tuvunje jahazi kuliko kufanyia repair baharini jahazi linalovuja;




Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
SAKATA LA JUMBE NA SERIKALI TATU

SEHEMU YA KWANZA

Mbali ya kuwasilisha involvement ya sitta na Tanganyika wakati wa sakata la G55, hoja za Barubaru #155 pia zimenisukuma niwasilishe yale yaliyyojiri katika kesi ya Jumbe mwaka 1984 kwani ni katika sakata hili ndio hoja ya Tanganyika iliibuliwa, miaka 17 baada ya Tangayika kututwa kwa mujibu wa sheria namba 24 ya mwaka 1967. Nadhani kufanya hivi itakuwa ni kwa manufaa ya jukwaa/mjadala.


Kwa mujibu wa issa shivji (2006), kawawa alifungua kikao maalum na summary ifuatayo kutoka kamati kuu ya chama juu ya hali ya kisiasa znz:

*Kwanza, kawawa alijadili kwamba kulikuwa na watu ambao walikuwa wanaeneza taarifa kwamba zoezi la kufanyia mabadiliko katiba ya JMT (mfano kuibadili jina znz kuwa Tanzania visiwani, kuongeza orodha ya muungano n.k) zilikuwa ni njama za kuimeza zanzibar, na wazanzibari walianza kuamini taarifa hizi;

*Pili, kwa upande wa bara, kulikuwa na watu walioamini kwamba kutokana na woga wa znz kumezwa, wazanzibari walikuwa wanajiandaa kuvunja muungano;

*Tatu, watu fulani fulani wenye ukaribu na serikali ya znz had openly challeged muungano, kejeli basis ya umoja wa kitaifa na pia siasa ya ujamaa na kujitegemea; mbaya zaidi ni kwamba taarifa hizi hazikuwa zimekanushwa na wahusika hawakuwa wamekamatwa;

*Nne, shughuli hizi na maadui hawa wa muungano zili raise concern sio tu kwa majirani bali pia mataifa ya nje pamoja na marafiki wa Tanzania ambao walikuwa na wasiwasi juu ya future ya muungano;

*Tano, ilikuwa bayana kwamba hali ile ingeliingiza taifa katika hatari na machafuko;
Hoja hii ilijengwa katika mazingira ya maadhimisho ya miaka 20 ya muungano (1964-84) kipindi ambapo pia palikuwepo tetesi kwamba usalama wa znz ulikuwa hatarini; hali ile iliweza dhibitiwa lakini ikaonekana kwamba machafuko ya kisiasa pamoja na mgogoro mkubwa wa kiuchumi ungeweza kutumiwa na maadui kuivuruga nchi;

Baada ya hoja hizi za Kawawa, kwa mujibu wa shivji, kiongozi wa kwanza kuchangia hoja akawa sio mwingine bali Seif Sharrif Hamad ambae alizungumza kwa kirefu akijikita zaidi kuishambulia serikali ya jumbe na kusema wazi kwamba jumbe ndiye mhusika mkuu wa machafuko yale; akaendelea kuonyesha kwamba jumbe ndiye aliyeanzisha na ku encourage mjadala visiwani ulio question uhalali wa muungano na kejeli juu ya supremacy ya chama (ccm) na kuchochea hoja ya serikali tatu; hamad akaendelea kutoa ushahidi mbalimbali juu ya hoja zake; pia akajadili kwamba serikali ya znz ilifanya mambo kinyume na taratibu zilizowekwa na ccm NEC, na akamalizia na maneno makali sana kwamba (shivji):

Ndugu chairman, these actions are contrary to our nation's vision and objectives. Indeed they endanger our security. In other words, they are treasonous. I pray the national executive committee to consider carefully the allegations and all those found responsible should be punished by this meeting

Shivji anasema kuwa wazanzibari karibia wote waliozungumza kwenye kikao hiki cha dharura (ukimuacha Seif Bakari-mmoja wa wajumbe wa kwanza wa baraza la mapinduzi mwaka 1964) aidha walimkana jumbe kihoja huku wengine wakiwa hawaeleweki wanasimamia wapi; seif bakari ambae alikuwa ni mmoja wa walioitwa karumeists aliomba kuzungumza kidogo na kusema kwamba yeye binafsi wakati wote amekuwa akipinga muungano wa tanu na asp (sio muungano wa tanganyika na znz) na kwamba alimuonya sana jumbe juu ya athari za ndoa baina ya tanu na asp; akamalizia kwa ushauri kwamba kuna haja ya viongozi kukaa chini na kumaliza mgogoro ule kwa amani na utulivu; Shivji anasema kwamba mjumbe mwingine - shaban mloo, ambae nae alipata nafasi ya kuongea akiwa ni mfuasi mkubwa wa seif hamad akamshambulia sana jumbe bila kumumunya maneno; mloo alijenga hoja kwamba tangia mwaka 1980, nafasi ya Jumbe ndani ya chama ilikuwa imedhoofika na kupoteza nguvu kubwa ndani ya chama na kwamba hiyo ndio ilikuwa ni sababu ya jumbe kupinga mfumo wa muungano na siasa za chama ndani ya muungano;

Shivji anaendelea kusema kwamba - siku ya tano ya kikao kile, jumbe akapewa fursa ya kujitetea na akazungumza kwa karibia masaa matatu; akaanza kwa kuelezea alivyojiunga na ASP, alivyoshiriki mapinduzi na pia jinsi gani maisha yake hayakuwahi kulenga kujinufaisha binafsi bali kutumikia umma; jumbe akajadili kwamba muungano una matatizo yenye vyanzo vikuu vinne:

*moja, ni tofauti ya kimtazamo juu ya asili ya muungano, na akatoa maoni kwamba shirikisho la serikali tatu ndilo lililokusudiwa ndani ya mkataba wa muungano (1964); katika hili, kimtazamo akawa ametofautiana na mwenyekiti (nyerere) na akadai kwamba kitendo cha viongozi kukataa kujadili hoja hii kwa uwazi na kukubaliana ilikuwa ni moja ya sources za misunderstanding;

*pili, jumbe akasema kwamba kukataa kujadili na kutekeleza mkataba wa muungano ambao kwa mtazamo wake ndio ulikuwa ni cheti cha kuzaliwa cha muungano ilikuwa ni source nyingine ya confusion. Katika hili, shivji anamnukuu jumbe kwa maneno ndani ya kikao kwamba:

We insist on discussing the union superficially without touching on the articles. Why shouldn't we discuss the articles of the union? This is the formal document which was signed by the presidents of Tanganyika and zanzibar. This is the document which lends legality to the union and which is the fundamental basis and source of the constitution. But it has become a sin to mention the articles, why? The source of confusion is the refusal to discuss the articles of the union. Let us lift the taboo from the articles of the union. This is the document of the union's birth - birth certificate of the union. But it can not be discussed

*tatu, shivji anasema kwamba - jumbe aliashiria kwamba kulikuwa na dissatisfaction hata wakati wa karume kutokana na jinsi katiba ya jmt ilivyofanyiwa marekebisho na kuifanya katiba ya tanu kuwa ni sehemu ya katiba ya jmt huku katiba ya asp ikiachwa; jumbe akahimiza msimamo wake kwamba the fact kwamba Tanganyika ilikuwa ime surrender masuala yake kwa muungano haikuwa na maana kwamba Tanganyika ilikufa kwani suala hili lilikuwa ni kwa ajili ya kipindi cha mpito tu wakato taifa linaelekea kwenye mchakato wa katiba mpya kabla ya 1st May, 1965;

*nne, na mwisho, kwa mujiu wa shivji, jumbe akajenga hoja kwamba "the treatment accorded to the revolutionary council's paper on the proposed amendments was both disappointing and inappropriate; hoja yake ikawa kwamba katiba ya jmt ilikuwa imefanyiwa marekebisho mengi sana na maamuzi wakati wote yalikuwa yanatokea bara; hii ilikuwa ni mara ya kwanza sasa na wao kuja mapendekezo ya mabadiliko ya katiba mapendekezo ambayo yakakataliwa bila mjadala; hii haikuwa sahihi kwani NEC CCM ilitakiwa ijadili suala hili kabla ya kupeleka mjadala kwenye umma;

Baada ya hoja hizi, jumbe akaanza kujibu tuhuma juu ya masuala mbalimbali kama vile kwanini hakumchukulia dourado hatua pale aliposhambulia muungano, kumpa special treatment na kumkaribisha znz "bashiri swanzy", wakili mghana aliyepewa jukumu na jumbe kuandaa mabadiliko ya katiba, na pia kutowachukulia hatua wale wote waliokuwa wanatishia uhai wa muungano; katika utetezi wake jumbe akasema kwamba kutokana na ushauri wa kisheria, hakuwa na sababu ya kufanya lolote au kuzuia mjadala juu ya mfumo wa muungano; akasema kwamba kuzuia mjadala kungepelekea kuibuka kwa oppositio chini kwa chini; kwa mujibu wa shivji, jumbe pia akakataa kwamba alihoji supremacy ya chama (ccm) akisema kwamba ilikuwa ni tuhuma iliyohitaji ushahidi. Shivji anasema haya juu ya hoja hii ya mwisho ya jumbe:

This was perhaps jumbe's weakest defense. He could not obviously challege party's supremacy because he himself had been so instrunmental in bringing it about; accepting party supremacy while at the same time expecting autonomy for the zanzibar government was like squaring the circle. It was an irresolvable dilemma, which struck jumbe's political death knell

Jumbe akahitimisha majibu yake in a dramatic fashion (shivji):
Ndugu chairman I have explained the whole truth on this issue as I understand it. But these allegations are serious. Should NEC believe, or even have a doubt, on the truth of these allegations or that either me or the revoltionary government were in any way involved, even if you have any doubt, I give you the benefit of the doubt; you can do me a favour; allow me to relinquish all the responsibilities you have given me; I say this with a clear conscience, without arrogance or humiliation, o anger or joy

Baada ya hapo kikao kika hairishwa kuwapa wajumbe wa kikao kile maalum kulala na kutafakari maelezo ya jumbe;

Itaendelea ambapo nitawasilisha response ya Nyerere kesho yake, word by word pamoja na mengine yaliyojiri;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi.
Mkuu wangu kuna sehemu umeandika hivi:-

"Ilikuwa na paragraphs nane in its preamble huku hoja kuu ikielekeza serikali ya JMT kuandaa na kuwasilisha a bill bungeni to amend muungano (hivyo katiba ya jmt ya 1977) ili kuanzisha serikali ya Tanganyika kufuatia hatua ya serikali ya zanzibar kujiunga na oic, hatua ambayo ilikuwa ni kukiuka katiba ya jmt 1977. Katika preamble hiyo hoja ya msingi ikawa kwamba watanzania bara wengi hawaridhishwi na mfumo wa serikali mbili ambapo znz wao wana serikali yao inayofanya maamuzi yao huku tanganyika ikiwa haina serikali ya aina hiyo ndani ya muungano, na hoja ikaendelea to argue kwamba - mapungufu haya yatavunja muungano, hivyo njia pekee ya kulinda muungano ni kuanzisha serikali ya Tanganyika ndanni ya muungano, hivyo kuleta mfumo wa serikali tatu."

Sasa nakuuliza upya tukiunda serikali ya 3, je hiyo serikali kuu haitakataa tena swala la OIC kwa sababu zile zile? maana walichoomba Znz mwanzoni ilikuwa OIC kwa ajili yao wenyewe yaani lisiwe swala la muungano. Tulishindwa nini kuliondoa swala hilo kuwa lisiwe la Muungano ila tunafikiri kesho tukiwa na serikali 3 halitakuwa la muungano maana sababu ziko pale pale hazitaondoka.

Hofu kubwa ya viongozi wa bara ni Uislaam hili halina kificho na tunajua wazi, sasa ikiwa vichwa vitakavyo ongoza nchi hizi ni vile vile, akili zile zile, unafikiri hizo serikali 3 zitabadilisha kitu gani ambacho leo hakiwezi kubadilishwa ndani ya serikali mbili.
- Nawakilisha.
Niendelee alipoachia Mchambuzi , Mkandara wakati ule na hadi leo suala la mambo ya nje si kuwa ni la kikatiba na secular bali pia lilihusisha ushiriki wa nchi kwa ujumla katika taasisi za kikanda na kimataifa.
Leo Znz haiwezi kujiunga na taasisi au mashirika mengine kwasababu za kikatiba.

Na wala halikuwa suala la OIC tu, unakumbuka mgogoro wa FAT na ZFA. Pamoja na FAT kuisaidia ZNZ hadi leo utambulisho wake FIFA ni utata mtupu kutokana na utambulisho wa Tanzania kimataifa. Ndivyo ilivyo timu ya taifa n.k.

Lakini pia kumbuka Znz iliamua kwenda International Maritime Organization(IMO) kwa mwendo ule ule wa OIC.

Huko walikataliwa kwasababu za taratibu za kimataifa. Hilo hulalamiki kwasababu Zanzibar kwa kutumia ZMO inanufaika kwa kulipiwa ada na Tanzania, ikikusanya mapato.

Rasimu ya katiba(sina uhakika kama umeipitia) au unajaribu kupotosha imeweka wazi kuwa nchi washiriki zitakuwa huru kushiriki katika mambo kama taasisi za kikanda, kimataifa pamoja na mashirika.

Kwa mtazamo huo serikali kuu imeelezwa kusaidia pale itakapohitajika. Kwa mfano znz wakienda IMF na kuombwa mdhamini wa mikopo hapo ina uwezo wa kurudi katika serikali ya shirikisho. Hivyo dhana ya kuwa serikali kuu itapinga hoja ya OIC(ambayo kwakweli inatumika tu lakini haina mantiki) halipo

Kuendelea na serikali 2 kutasababisha historia kujirudia kwa maana nzuri kabisa. Huwezi kuwa na nchi yenye rais mmoja, wimbo wa taifa na bendera halafu ukawa na kanchi kengine ndani ya nchi.

Nafahamu unaliongelea suala la OIC kwasababu linavuta hisia na kujaribu kuficha ukweli mwingine unaofanana na huo.Ningekushauri uwashauri wznz wakubali serikali 3, ili wawe na yao na kujiunga na taasisi yoyote watakayo.
 
Last edited by a moderator:
HOJA NAMBA 1: Mimi sikubaliani na serikali 3 kutokana na sababu za maana kabisa nazo zimezitaja. kwanza sio wakati wake na pili serikali 3 ni kuirudisha Tanganyika ----

HOJA NAMBA 2: tulichoomba sisi wananchi wote ni katiba mpya ambayo inakwenda na wakati sio swala la Muungano, Kero za Muungano tulizipuuza miaka yote 50, na tukitumia maguvu kuulinda, hivyo nguvu hizo zingeendelea kuwepo. (dhidi ya viongozi wanaokiuka Kiapo)Sasa kutokana na uzushi wa hizi serikali 3 kama suluhisho.

HOJA NAMBA TATU:
Katiba mpya haiwezi kupatikana na sijui kama hao wajumbe wameliona hili, maana huwezi kutunga katiba mpya ya Jamhuri wakati hakuna nchi ya 2 tayari. Tanganyika yenye katiba yake, bunge lake na mahakama yake. Hivyo nawauliza nyie hao wabunge wa hilo bunge la katiba wanafanya nini Dodoma maana huwezi kuitunga katiba ya Taifa mbele ya zile za nchi. Kifupi tunapoteza mabillioni ya kodi za wananchi kwa usanii huu mpya na watu mnao ushangilia.

HOJA NAMBA NNE:
Labda sasa niwageukie Wazanzibar, ni hivi muundo wa nchi yetu ni wa kipekee kabisa kiasi kwamba tuliipoteza Tanganyika na kuyapa mamlaka kamili TAIFA la TANZANIA ambalo lina viongozi toka pande zote 2. Hivyo Zanzibar kama nchi ilikuwa tu na mamlaka ktk maswala yasokuwa ya Muungano ambayo kulingana na culture zao, Identity yao viliachwa wazi kwao na ndio maana wao wana Kadhi mkuu, sisi bara hatuna.

Huku bara hatukuwa na tatizo infact tulipoteza sio Identity yetu pekee bali hadi culture zetu na tukachagua Utanzania ambao kiswahili ndio ikiwa lugha yetu. Maswala ya culture na imani yakawekwa kuwa ni haki ya kila mtu kuabudu anachokiamini hata kama unaamini mizimu japo wachawi walikuwa wakiuawa kimakosa. hahah hahah haha!

HOJA NAMBA 5
Zanzibar hawawezi kuwa na mamlaka kamili isipokuwa ya republic na ktk maswala yasokuwa ya muungano. Ikiwa kweli kuna mambo yaloingizwa Kinyemela ilitakiwa yatazamwe na yarudiwe upya kutazamwa na bunge la TAIFA ili kukidhi mahitaji ya sehemu zote.

HOJA NAMBA 6
Na ikiwa kero zao zipo ktk mambo yale ya muungano ikiwa ni pamoja na ugawanaji wa pato la taifa au uwekezaji ktk miundombinu ya Taifa hili linaweza kabisa kutatuliwa maana kama tumeweza kugawa madaraka ya viongozi wa pande mbili na wakaridhika kusiwe na tatizo tunashindwa vipi ktk hili? ina maana katiba yetu haikidhi muundo wa kiuchumi ktk makusanyo na ugawaji wa pato la Kitaifa.

HOJA NAMBA SABA
Tunashindwa vipi kujenga Bandari ya freeport Zanzibar na Airport ya kimataifa wakati tuna taifa moja?..lakini wepesi kukubali ijengwe Bagamoyo na sii Mtwara au Tanga ilihali Ushuru wake unaingia mfuko wa Taifa ijengwe zanzibar au bagamoyo. Zanzibar ilikuwa central of business kwa karne, kwa nini tusitumie nafasi hiyo ambayo kijiographia imekuwepo toka karne ya kwanza? jibu lake ni UBINAFSI wa sisi bara.

HOJA NAMBA NANE
Maana Tax zote zinazokunywa kwa mauzo toka kwa wateja mbalimbali walokuja Znz kununua mali hizo linaenda mfuko wa Taifa bila kujali limezalishwa wapi na Wazanzibar wataona maendeleo, wataona ajira zikipatikana pasipo kuja bara na kadhalika, pia wabara wataingia Zanzibar pasipo choyo maana riziki zipo. Kwa Zanzibar kuwa na bandari ya freeport kinachoondoka hapo ni Import duty tu ili kuyavuta mashirika ya nje kuwekeza ktk uuzaji wa jumla na mataifa mengine wapate nafuu ya kuja Tanzania badala ya Dubai na China. Na pia nafuu kwa Watanzania wote iwe bara au visiwani.

HOJA NAMBA TISA
Tungejengea University ya Kimataifa Znz, Hospital ya kimataifa Znz kwa sababu wapo Watanzania bara wanaoishi huko wakiitumikia serikali kuu ama wafanya biashara kwa nini kila kitu kijengwe bara?. Na maadam hivi vitu vipo ktk mambo ya muungano pato lake linakwenda ktk mfuko wa Taifa. Hivyo Zanzibar itaonekana ikichangia vizuri ktk mfuko wa Taifa na kutuwezesha kujichanganya zaidi badala ya kugawana umaskini.
Mkandara nijibu hoja zako kama nilivyoziwekea namba ili kutoruka hata moja.

Hoja namba 1:
Hujatuonyesha wakati muafaka wa kurudisha serikali 3 ni lini. Halafu hutaki serikali 3 kwasababu Tanganyika itarudi. Mkataba wa 1964 ulikuwa kati ya Tanganyika na Zanzibar. Tanganyika hairudi inazinduka. Tuonyeshe mkataba wa muungano wa Zanzibar na JMT kama ulivyowahi kudai

Hoja namba 2:
Kero zimeanza miaka zaidi ya 30. Rais Jumbe alipoteza nafasi yake. Tume 5 zimeundwa, za JMT na SMZ.Hakuna hata moja iliyokuja na suluhu. Uamsho wapo barabarani, CUF wapo viungani bila kusahau G55. Rais JK aliahidi kumaliza tatizo. Leo unatushawashi tuendelee kuvumilia kwasababu muda wa malaika kuja kutusaidia ikiwa ni pamoja na kurudisha Tanganyika bado.

Hoja namba 3. Umesema wabunge walioko Dodoma hawawezi kutunga katiba ya taifa mbele ya nchi husika. Ni nchi zipi hizo? Zanzibar ipo na hiyo nyingine husika usiyoitaja ni ipi.
Upo katika rekodi ya kusema tumeungana Zanzibar na JMT, sasa tatizo lipo wapi kama nchi mbili huru zinaandika katiba. Otherwise eleza jamvi hiyo nyingine ni ipi.

Hoja namba 4: Prof Humphrey kasema znz haijachangia muungano isipokuwa miaka 3 ya mwanzo. Kwa miaka 5 iliyopita hakuna mchango, yaani ni sifuri. Warioba kaonyesha TRA inakusanya mapato na kuyaacha znz. Hoja ya Tax haipo ni uzushi wa maskani tu.
Kodi ya znz ni ya znz haivuki bahari, ikivuka ni kwa kutumia midomo na hadithi.

Hoja namba 5:
Katika hoja namba 1 umesema hutaki Tanganyika irudi na kusisitiza ilikufa mwaka 1967 na haipo. Hoja nmaba 5 unasema kuna mambo yasiyo ya muungano. narudia tena kukuuliza hayo yasiyo ya muungano yashughulikiwe na nani?

Tanganyika haipo sasa tutayaweka wapi? Hili swali hujibu na hivyo kutumia mambo yasiyo ya muungano ni kupotosha. Huwezi kuwa na SMZ na JMT halafu ukawa na mambo yasiyo ya muungano. Usitumie hilo neno kwasababu unajichanganya sana.
Kama hujichanganyi tuambie yasiyo ya muungano yawekwe wapi.

Hoja namba 6:
Hatuwezi kugawana pato ambalo znz inachangia sifuri Mkandara.
Miaka 5 imepokea tu sasa unataka tugawane nini.

Labda useme pato la linalokusanywa Tanganyika ligawanywe sawa na znz.
Huwezi kuchangia sifuri halafu ukadai mgao.
Mishahara inatoka hazina, madeni yanalipwa, mambo 22 wanadandia, hata umme wa bure leo unataka wagawiwe nini tena?

Kuhusu miundo mbinu, SMZ inapaswa kuendeleza miundo mbinu.
Afya na hospitali si suala la muungano ni hisani.Elimu ni hisani, ujenzi ni hisani n.k.
Bandari wameondoa wenyewe, tuchangie nini? Mafuta na gesi wamekimbiza haraka tuwasaidije

Hayo mambo yaliyoingizwa kinyemela yamewanufaisha wznz siyo Mtanganyika.
Nimekuuliza hii mara ya tano, andika mstari mmoja tu ukionyesha jambo moja la kinyemela lililoinufaisha Tanganyika.

Mimi ninayo 22 yaliyoinufaisha znz ukitaka nitakupa licha ya ukweli kuwa nikupa 5.

Hatuwezi kuacha kujenga banadari zetu kwasababu ya znz, huo ni uzezeta.
Hatuwezi kuacha kujenga vyuo kwasababu ya znz huo ni ututusa.

Bagamoyo itajengwa, Mwambani Tanga itakuwa bandari huru, Mtwara itaibuka kutokana na gesi na tutasonga mbele. Tusipoangalia utatushauri tuwapelekee ndoo bafuni. Mbuga ya Saadan itaendelezwa zikiwemo beach. Unataka tujenge miundo mbinu nchi jirani. Sisi wewe umesem ni nchi na serikali yake.

Kama wanahisi wanonewa njia nyeupe, mbona wamekwama Dodoma nawewe hutaki Tanganyika. Kwamba tuache kufanya maendeleo yetu kisa watu laki 5 na wengine laki 5 wakiishi kwetu.
Hawa wznz ni nani!!! unadhani wana ubora gani na kwa faida gani kwetu kiasi unataka hospitali isijengwe Singida eti ijengwe znz kwa pesa za kodi za Mtanganyika.



 
Barubaru hapo nyuma nilidhani ungeelewa maana ya mjadala, nikaona unaharibu uzi nikakupuuza.
Kadri tunavyokwenda mbele naona unaharibu zaidi kwasababu huna mantiki zaidi ya ushabiki.

Labda nikumbushe kuwa suala la muungano kwa Nyerere halikuanza na Zanzibar.
Mwaka 1963 wakati huo znz ikiwa chini ya Sultan Nyerere alikuwa na wazo la kuungania Afrika mashariki (EAF).

Katika miaka ya 60 Nyerere alihitilifiana na swahiba wake Nkrumah kwasababu ya Pan Africanisim.
Kumbuka jitihada hizo hazikuanza mwaka huo, huko nyuma kulikuwa na PAFMECA kule mwanza.
Ingawa PAFMECA ilikuwa na malengo ya ukombozi zaid,i hiyo ni dalili kuwa Nyerere alipenda muungano ever since.

Kuanzishwa kwa frontline states ndiko kumeacha legacy ya SADC hadi leo.
Na SADC imeondoka katika objectives za mwanzo na sasa kulekea katika ushirikiano wa kiuchumi.
Mwaka 1967 ikaundwa EAC licha wazo hilo kupigwa chini mwaka 1963.

Ilipoanzishwa EAC ya sasa na akina Mwinyi, Moi na Museveni Nyerere alikuwepo na wala hakusema lolote baya kuhusu hilo ikiwa ni ishara ya kuunga mkono mashirikiano. Hayo yote yanaonyesha jinsi alivyokuwa anapenda mashirikiano ya watu beyond Berlin conference philosophy

Kwa uchache huo unaweza kuona jinsi Nyerere alivyopenda watu kuwa kitu kimoja.
Katika mkutano wa Pan Africanism, moja ya mambo yaliyojadiliwa ilikuwa ni umuhimu wa umoja kuelekea katika uchumi mkubwa.

Lakini pia lazima ufikiri kama mtu mzima aliyewahi kutembea tembe eneo la shule.
Huwezi kuongelea muungano wa mwaka 1964 kwa kuangalia mazingira ya mwaka 2014.
By that time dunia ilikuwa na mwelekeo tofauti kukiwa na nguvu pinzani za mashariki na magharibi.
Katika miaka ya 1960, 1970 hadi 1980 Mapinduzi yalikuwa kitu cha kawaida redioni.


Unaposema Znz na Tanganyika zimeungana 50/50 ni upotoshaji wa mambo.
Kama ni hivyo kelele za znz kuonewa zinatoka wapi?
Na wala ukiulizwa hiyo 50/50 uionyeshe sijui kama utaweza. Tumekueleza kila jambo kwa takwimu lakini huonekani kuelewa.

Ningekuomba kama huna hoja zinazolingana na mada iliyopo ni busara ukikaa kimya kuliko kuvuruga uzi.
Nadhani ustaarab ni jambo jepesi na heshima haiombwi, tafadhali sana rudi katika mada ama sivyo kaa kimya.

Nguruvi3,

Awali ya yote napenda uwe muwazi sana na kuacha tarbia ya kutaka ku dominate mjadala kiasi cha kutaka mawazo yako japo mengine potovu watu tuyakubali bila kuyakhoji au hata kukupa bayana zake.

Naomba ujue uzuri wa mnakasha ni kuhishimiana na kutoa lugha za kistaharabu zisizo za kutishana wala kuudhiana kinachotakiwa ni KUTOA HOJA ZENYE MASHIKO.

KAMA KWELI HUU MSEMA KWELI TAFADHALI NIELEZE NI WAPI NIMEHARIBU MNAKASHA HUU? na utoe sababu kama huu msema kweli.

Baada ya huo utangulizi napenda Nikubaliane na wewe kwa 100% japo nina mashaka makubwa kuwa Nyerere alipenda Muungano sana na nchi nyingine.

SUALA LANGU HAPA KWANINI NYERERE HUYO ASIUNGANE NA KENYA AU UGANDA AMBAZO ZILIPATA UHURU KABLA ZNZ NA KUZIFANYA NCHI MOJA MPAKA AKAENDA KUUNGANA NA ZNZ NA KUUWA UTAIFA WA TANGANYIKA?

Lakin suala lingine hapa naona mnaliruka JE MNAFAHAMU SABABU ZA NYERERE KUFUNGA SAFARI KWENDA ZNZ KUOMBA WAUNGANISHE NCHI HIZO NA KUWA JMTz? je ni nini kilimsukuma kufanya hivyo?

Tanganyika na Znz zimeungana 50/50 KATIKA CHOMBO KIKUU CHA MAAMUZI. Labda nikudadavulie namna hiyo KATIBA YENU YA JMTz ya MWAKA 1977 ILIVYOTUNGA NA UTAONA ILIKUWA NA MEMBERS 20 TU YAANI KILA NCHI ILITOA WAJUMBE 10. Je hiyo sio 50/50.

Hebu nikupe kidogo hapo kwa faida ya wasomaji wengine.

Kuna utata namna Katiba ya 1977 ilivyotungwa. Utaratibu unaotajwa katika Mkataba wa Muungano na Sheria ya Muungano unaelekea ulivunjwa kidogo, kwamba badala ya kuundwa Tume huru mahsusi kwa ajili ya kupendekeza Katiba, Tume ya vyama vya TANU na ASP ya watu 20 kwa maana 10 kutoka kila upande wa muungano (ambayo haikuwa na Mwanasheria hata mmoja, bali wakereketwa wa siasa watupu), iliyoundwa mahsusi kuunganisha vyama hivyo viwili, iligeuzwa kuwa ndiyo Tume ya Katiba ya Chama na kupendekeza Katiba.

Mapendekezo ya Tume hiyo na ya Bunge la Katiba kama ilivyotakiwa, badala yake yaliwasilishwa na kujadiliwa kwenye Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama na baadaye kwenye Bunge la kawaida. Pamoja na hayo, Bunge hilo halikuyajadili mapendekezo ya “Tume” kwa sababu alizozitaja Waziri Mkuu wa wakati huo, Rashidi Kawawa, kwamba “Kwa kuwa NEC ilikuwa imeijadili, Bunge halikuwa na mamlaka ya kujadili wala kubadili kitu”.

Utata wa Muundo wa Muungano ulijitokeza tena kama hoja wakati wa Tume ya Jaji Nyalali na kupatiwa suluhisho kwa njia ya mapendekezo ya kurekebisha Katiba. Lakini badala ya mapendekezo ya Tume hii makini kufanyiwa kazi, yalitiwa kapuni na hivyo kupoteza nafasi nyingine nzuri ya kutibu ugonjwa unaousumbua Muungano wetu.
Lakini, kwa nini Tume ya Katiba haikuundwa kwa mujibu wa Mkataba na Sheria ya Muungano? Moja ya sababu ni kwamba waasisi wa Muungano huo, Nyerere na Karume, walianza kugundua kwamba walikuwa tofauti mno kwa kila hali; kuanzia maumbile, kitabia na kifikra, elimu na mtazamo juu ya Muungano waliotia sahihi.

Na hili ndilo linaloleta khofu mpaka leo Rais wa JMtz anaogopa kuzomewa ndani ya bunge la Katiba. Na Bunge enyewe limejaa lhofu tupu na kutoaminiana miongoni mwa wajumbe wake.

Je una ziada hapa.

CC; Kakke, Big Show, Ritz, gombesugu, Bobuk
Baada ya Utangu
 
Hatumfananishi dourado na haroub bali tunaangali hoja ya haroub dhidi ya dourado kwamba dourado alikuwa ni mjumbe wa tume ya nyalali ambayo iliridhia kwamba Baraza la mapinduzi lilishirikishwa vilivyo katika ratification ya muungano. Dourado alisimamia hoja hiyo chini ya tume ya nyalali, kwanini tusihoji unduminakwili wa dourado? Tutajuaje kama 1983 kwenye paper yake kwa tanganyika legal society alisema uongo lakini chini ya tume akaamua kusimamia ukweli?

Ni muhimu pia ukafahamu kwamba ni viongozi wa znz ndio wa kulaumu kwa kutotekeleza matakwa ya mkataba juu ya ratification kikamilifu kwani hakuna sehemu yenye ushahidi kwamba Tanganyika iliwabana juu ya hilo; Tanganyika kwa upande wao walifanya kama mkataba unavyoelekeza; moja ya sababu kwanini Baraza la mapinduzi halikufanikisha matakwa ya muungano per se ni kwamba baraza hili lilikuwa limegawanyika sana juu ya mkataba, hasa content, na mgawanyiko huu ulitokana na debate kali iliyojitokeza ndani ya baraza, kwahiyo kimsingi, baraza la mapinduzi lilijadili suala la mkataba, na Kassim hanga alitoa hoja nzito sana kuunga mkono muungano na kuweza kuwashawishi wajumbe wengi kuunga mkono hoja; shivji alifanya mazungumzo na mmoja wa wajumbe wa baraza hilo wa wakati ule, Khamis Abdullah Ameir ambae kwa mujibu wa shivji:


Kwa maana na ushahidi huu wa shivji, suala la mkataba lilijadiliwa kwenye baraza la mapinduzi lakini ratification ilikuwa kwa kulazimishana sana na ndio maana leo mjadala una evolve around mkataba kuwa ratified na baraza la mapinduzi vis a vis mkataba kuwa debated na baraza la mapinduzi. All that said and done, Tanganyika na nyerere had less to do with kilichojiri ndani ya baraza la mapinduzi kwa hatua ile. Karume alikuwa anaishi kwa uwoga kutokana na factions za kisiasa zanzibar hivyo akabariki mambo kwa mamlaka yake. Hii ni moja ya sababu kwanini Nyerere alisita mchakato wa katiba ya JMT ambapo mchakato ulitakiwa uwe umeanza kabla ya Mei Mosi 1965, na badala yake tunasoma kwenye historia nchi kuingia katika katiba ya muda kwa miaka 12 na ushee. Kwa maana nyingine, mapungufu ya karume na baraza la mapinduzi justified uchakachuaji wa mkataba wa muungano but that is a different debate.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi,

Ahali yangu NAONA UNAANDIKA MAMBO MENGI SANA ambayo yanajaribu kukwepa uhalali wa suala langu kwako.

Suala langu ni fupi sana NA NAOMBA ULIJIBU.
Tunajuwa kuwa Dourado alikuwa mwanasharia mkuu wa Znz wakti wa Muungano. Suala hapa
1. Je inawezekana vipi nchi ikaingia katika mkataba wa muungano bila kumshirikisha Mwanasharia mkuu wa Serikali?
2. Je unajuwa TGK iliwakilishwa na mwanasharia gani katika mkataba huo waMuungano ?

Naomba tuanzia habo kabla kuja hayo mambo ya akina Shivji.

 
Mkuu wangu swala lako swadakta tena limeingia ktk Uislaam na hakika Uislaam ndio way of life. Swali langu linakuja hivi:-
Umejaaliwa kuoa wake wawili, mmoja kakupa watoto 10 wa kiume, na mke wa pili kakupa watoto wawili wa kiume, Je mirathi yako utaigawa kwa 50/50 kutokana na matumbo ya mama zao? ama utazigawa kulingana na asilimia sawa kwa hao watoto wako wote 12?

Mkandara,

Naona huko kwenye Uislaam umekwenda wewe, KWANI MIMI NIMEZUNGUMZIA FAIDA ZINAZOPATIKANA KATIKA NDOA YOYOTE ILE bila kujali itikadi au imani yake.

Lakin kwa Kukusaidia HAKUNA MIRATHI BILA KIFO. Na utaratibu wa mgawanyo umebainshwa wazi kwa waislaam.

Lakin suala la msingi hapa umelikimbia nimekuuliza Katika hali yoyote ya Muungano LAAZIMA KUWE NA WIN TO WIN SITUATION. Sasa suala langu je TGK mnanufaika nini na Znz?

nasubiri jibu hapo.

 
SAKATA LA JUMBE NA SERIKALI TATU

SEHEMU YA PILI

Inaendelea tokea bandiko #172

Kwa mujibu wa Issa Shivji, baada ya wajumbe kwenda kulala kwa nia ya ku digest hoja za Jumbe kwenye kikao, siku iliyofuatia, Nyerere alianza kikao kwa maelezo marefu huku akikiri kwamba hakuwa amewahi kuwa kwenye kikao kigumu kama kile. Kwa juu juu akaelezea historia ya muungano akisisitiza kwamba katika kipindi cha miaka 20 ya muungano, amekuwa rais wa Tanganyika kwa miaka chini ya mitatu, na kwamba 60% ya idadi ya watu walizaliwa kama watanzania; kisha akauliza:
Nani anataka kuirejesha Tanganyika? Nani anataka kirejesha Zanzibar?
Nyerere akaendelea kwa kutilia mkazo msimamo wake kwa ilikuwa ni Karume, na sio yeye Mwalim ambae ndiye alikuwa mhusika mkuu wa kuleta muungano. Akaeleza yafuatayo (Shivji):

Between the late karume and me the person who deserves greater credit for the union is Karume. I and Nkrumah were the big advocates of africa unity. I had discussed the formation of east african federation with obote and kenyatta. But inspite of my advocacy to this day there is no federation. After the revolution karumme had come to dar-es-salaam, not to discuss about the union but to discuss Okello. After the discussion about Okello, I told him, "Sheikh, I have told obote and kenyatta that when they are ready, we should unite. I am telling you the same. He replied "we are ready;call the press right away, we announce. One country, one government, and you the leader

Nyerere akaendelea kueleza kwamba baada ya mapinduzi ya znz alitofatiana na karume juu ya masuala mawili (shivji):

"continued killings and forced marriages with arab girls, but not the union;

Shivji anaendelea kujadili:

"Once he was invited to the revolutionary council meeting of fourteen people where a number of persons were sentenced to death".

Nikimnukuu Shivji juu ya Mwalimu:

"Today is it easy to kill people whom you know to be you enemies but tomorrow you will start butchering among yourselves. And that's exactly what happened to people like salehe saadalla, hanga and othman shariff."

Shivji anasema kwamba Nyerere alipinga kwa nguvu sana" forced marriages of leaders to arab girls. Suala hili lilimtia aibu sana katika anga za kimataifa. Kuna wakati alijadili hili kwenye baraza la mapinduzi lakini karume alitetea sana ndoa za aina hii akisema kwamba (shivji):
"We should reduce these enemies. If we don't reduce them, they will multiply".

Kisha shivji anamnukuu mwalimu akisema haya kwa karume ndani ya kikao hiki cha kumjadili jumbe:

I told them since when did this business of marrying enemies start? He asked me, why I loved these people so much. I replied that it was him who was marrying them, not me

Nyerere akaendelea kwa kumumwagia sifa nyingi Jumbe kwa kwa mstari wa mbele katika kuimaisha muungano wa nchi hizi mbili na pia kufanikisha muungano wa TANU na ASP. Kwa ufahamu wa mwalimu, jumbe alikuwa ni strong advocate wa party supremacy na hakuwahi kumsikia hata siku moja akilipinga hili; kisha nyerere went on to identify three groups ambazo zilikuwa zinapinga muungano (shivji):

First there were the Hizbu. These were known; for them the union was a bulwark against thei designs to bring about instability in zanzibar. They were a spent force and need not be bothered about. The second group was anti-jumbe;they did not like Jumbe to be in power and after jumbe was elected, they began to oppose the union associating jumbe with the union. Some of them were dropped when jumbe appointed his revolutionary council. The third group was anti-democratic which had felt that their power was being reduced by jumbe adopting the constitution and bringing in younger people. These groups had come together and formed an anti-union front.

Kwa mujibu wa Shivji, Nyerere akaendelea kwa kumjibu Jumbe juu ya hoja zake kuhusiana na sources za machafuko ya kisiasa zanzibar (rejea bandiko la awali). Nyerere akaelezea kwamba ni kweli kwamba wakati walipokuwa wanajadiliana kuhusu muungano kwenye ngazi ya afrika mashariki, walikuwa na wazo la shirikisho vichwani mwao ili kuzua nchi shiriki zisihizi kumezwa na muungano. Alipinga serikali moja kwenye muungano na znz kwa sababu kufanya hivyo kungeharibu utambulisho wa znz. Nyerere anaendelea kusema kwamba -Wakati huo huo, hawakuona haja ya kuwa na serikali tatu kwani kwa upande wa mshirika mkubwa zaidi - yani Tanganyika, hapakuwa na uwoga wa kumezwa na muungano, tofauti na kwa mshirika mdogo - zanzibar. Kwahiyo hofu ya zanzibar ingeweza tatuliwa kwa kuipatia znz serikali yake na kwamba hayo ndio yakawa makubaliano;

Kwa miaka 20 ya muungano, nyerere aliendelea, kila mtu alikuwa anajua kwamba Tanzania ilikuwa ni muungano wa serikali mbili, kwahiyo akashangaa kumsikia Jumbe, kama Dourado wakifuata msimamo kwamba mkataba ulilenga serikali tatu. Hoja zikaendelea kwamba - It was one thing kudai serikali tatu kama ilivyofanywa na baraza la mapinduzi 1981 kupitia mapendekezo yake lakini it was quite anothe kujadili kwamba kulikuwa na serikali tatu. The former position kama ikikubaliwa na chama, suala ambalo lingehitaji kujadiliwa kwanza lingemaanisha kurekebisha katiba suala ambalo lingehitaji robo tatu ya kura toka pande zote za muungano. The latter position ingemaanisha pangetokea mgogoro wa kikatiba ambao suluhu yake ingepatikana mahakamani peke yake. Nyerere akaendelea kujenga hoja kwamba in actual fact, hoja ya Jumbe na ile ya Dourado kwamba serikali tatu zilikuwa zimeanzishwa ndani ya muungano, (shivji) "was a subterfuge to take away the matter from the political arena, and therefore within the party's purview, and to turn it into an issue of legal interpretation and therefore within the jurisdiction of a constitutional court."

Kilichofuatia, (shivji) Nyerere 'dropped the bombshell' to use hamad's phrase:

Now the difference of opinion has already risen. The vice chairman is saying there are three governments; I am saying there are two; it is an issue of the articles of the union; and the case has already been prepared - to send it to court. (At this stage the chairman showed the delegates the case file which had been prepared

Vice chairman (Jumbe): "I have not seen this case file";

Delegates: "Ahaaaaa"

Nyerere went on:

The case is ready. Here it is. The case has been prepared for the revolutionary government to prosecute the union government in the constitutional court. And all tje charges we are discussing are there. Articles of the union. Party supremacy. For what wrong is the zanzibar government to prosecute the union government? This has two fold importance: 1+1= 3 and 1+1 = 2. So we should prepare ourselves to go to court. I guess this is the work that the likes of Dourado and Swanzy have been doing

Shivji anajadili kwamba, kuibuliwa ghafla kwa nyaraka ile na Nyerere kulimshtua sana Jumbe. Jumbe alimweleza shivji baadae kwamba mara ya mwisho kuiona nyaraka ile ilikuwa pale alipomuonyesha waziri kiongozi ambae alishauri itafsiriwe kwa kiswahili kwa ajili ya kujadiliwa kwenye baraza la mapinduzi na Waziri kiongozi aliondoka na nakala ambayo ilikuwa bado haijatiwa saini.

Hapo nyuma nilisahau kusema kwamna Kwa mujibu wa shivji, katika trial dock alikuwepo Jumbe na waziri wake kiongozi Ramadhani Haji Fataki while main accusers walikuwa ni kundi dogo la young zanzibais wakiongozwa na 'seif sharrif hamad, na wafuasi wake Hamad Rashid, Shabaan Mloo na Khatibu Hassan.

Shivji anasema kwamba katika mahojiano yake kwa nyakati tofauti na seif shariff hamad na khatibu hassan, afisa usalama mstaafu na mmoja wa wafuasi wa seif sharrif hamad admitted kwamba walihusika na kuifikisha nyaraka ile mikononi mwa Nyerere. Kwa mujibu wa maelezo ya khatibu hassan kwa shivji, hassan alifanikiwa kuipata nyaraka kutoka kwenye ofisi ya Jumbe kupitia his security contacts. Hii ilikuwa ni wakati wa mapumziko ya siku tatu ya kikao cha kamati kuu na NEC. Shivji anaeleza kwamba baada ya kufanikisha kuzichukua kutoka ofisini kwa jumbe, Nyaraka hizi akapewa Waziri Mkuu Sokoine. Anazidi kueleza kwamba Nyerere alizitumia kikamilifu huku Jumbe akishindwa kuzisimamia na kuishia kutoa tu maelezo kwamba alikuwa na taarifa juu ya maandalizi yake lakini hakuwa na version iliyokuwa mikononi mwa nyerere; haya ndio yalikuwa majibu ya jumbe yaliyonukuliwa kwenye minutes za kikao na kuchapishwa na shivji; baadae katika mahojiano yake na Jumbe, Jumbe alimweleza shivji kwamba "Nyerere was reading selectively from the document and Jumbe told him to read the whole. He wouldn't."


Itaendelea ambapo tutaona jinsi gani Nyerere alimaliza kikao in a dramatic fashion.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mchambuzi,

Ahali yangu NAONA UNAANDIKA MAMBO MENGI SANA ambayo yanajaribu kukwepa uhalali wa suala langu kwako.

Suala langu ni fupi sana NA NAOMBA ULIJIBU.
Tunajuwa kuwa Dourado alikuwa mwanasharia mkuu wa Znz wakti wa Muungano. Suala hapa
1. Je inawezekana vipi nchi ikaingia katika mkataba wa muungano bila kumshirikisha Mwanasharia mkuu wa Serikali?
2. Je unajuwa TGK iliwakilishwa na mwanasharia gani katika mkataba huo waMuungano ?

Naomba tuanzia habo kabla kuja hayo mambo ya akina Shivji.


Suala la zanzibar nilishalijadili huku nikikupa ushahidi kwamba mkataba ulijadiliwa na baraza la mapinduzi, kilichojaa controversy ni suala la ratification, sio suala la BLM kupata fursa ya kujadili mkataba, kisha nikakuuliza mtazamo wako juu ya hoja ya prof haroub othman kwamba dourado akiwa mjumbe wa tume ya nyalali aliafiki kwamba baraza la mapinduzi kufanya ratification, nikahoji, je, inawezekana kwamba dourado alidanganya kwenye paper presentation yake kwa Tanganyika Legal Society conference 1983 lakini akasema ukweli chini ya tume ya nyalali? Haujajibu na badala yake you have become a spinner;

Kwa upande wa Tanganyika, taratibu zote zilifuatwa kama ilivyoelekezwa na mkataba wa muungano, lakini kujibu swali lako kuhusu legal team ya Tanganyika juu ya hili, walikuwa ni:

*Mark Bomani akisaidiwa na Roland Brown na P. Fifoot;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom