Duru za Siasa: Kuelekea bunge la katiba,Je, katiba itatokana na wananchi?

Duru za Siasa: Kuelekea bunge la katiba,Je, katiba itatokana na wananchi?

Kilichotokea kwenye Bunge la katiba hakina tofauti sana na hekaya za kesi ya Ngedere. Hii wamekabidhiwa "Nyani" wazoefu, aka makada wa CCM wa muda mrefu.

Kuwa na matumaini kuwa Tanzania itapata katiba nzuri kutokana na hawa watu ni sawa na kuwaza timu yetu ya taifa itaifunga barcelona and the likes. It's statistically no an imposibillity but we both know where everyone will bet for.

Mimi ni mfuasi wa tulipofikia sasa kama taifa, tuendelee kubomoa hadi ifikie hatua hakuna pa kuficha uovu wetu. ififkie hatua tuchoke,wananchi wachoke. hapo ndio kuna la maana litakapofanyika.

Hivi kuna mtu yoyote humu anafikiria kuwa Kikwete atateua Baraza la Mawaziri kutoka kwenye pool ya watu aliowapendekeza kwenye nafasi za uongozi ambao wanaweza kufanya maajabu au kufanya ambacho CCM imekifanya kwa miaka 50 na kufeli?

hii katiba ya sasa hivi naiona kama "stopgap" . somehow a knee jerk reaction just because katiba mpya is the popular thing around. I am saying this and i wlil say this again. unless they vote for three governments of which we will surely make CNN front page as a nation with 3 damn presidents, this new constitution will not move a needle as far as geopolitics or economics are concerned. This is just satisfying a few over-sized egos.

Siku wananchi wakitaka katiba yao, wakachoka kutungiwa katiba, wataitafuta tu.Na msishangae siku hiyo ikifika raisi asipokuwa mchagua majina, na wabunge wakaambiwa wakae pembeni. siku hiyo kwa nchi yetu bado sana.
 
Kimweri
Mfano wako wa taifa stars kuifunga Barcelona unachekesha sana ingawa ndio ukweli usiohitaji diploma au cerificate.Ni kubaliane nawe kuhusu ubovu nikiamini ipo siku wananchi wataona umuhimu wa kusimamia haki na nchi yao

Tangu mchakato ulipotangazwa wengine tuliwaonya Watanzania kuwa yalikuwa ni mazingaombwe

CCM iliyokaa madarakani miaka 50 ilisema haina mpango wa kuandika katiba, iliyopo inatosha.
Hoja ya katiba ilikuwa ya wapinzani, JK akaamua kuichukua juu juu. Haikuwa sera ya CCM.

Sababu kubwa zilikuwa ni kukwepa suala la muungano lisije likatekwa na mchakato unaotokana na wananchi na ambao ungeliangalia kwa jicho la suluhu zaidi.

Mswada wa kwanza ulipinga kujadili kwa muungano. Baada ya kushindikana JK akachukua njia rahisi za kuandika katiba za kumwezesha kufanya anavyotaka na si wananchi wanavyotaka.

Katika bandiko #17 EMT kaeleza vema kuhusu njia mbili kuu za kuandika katiba.
JK akachukua madaraka ya wananchi kuandika katiba.

Mchambuzi #19 na mara nyingi sana 'has been walking us along the path of history' tuone wapi tulijikwaa. Ameongelea kwa undani mkataba wa 1964, bunge la 1965 na 1977 na impact kwa katiba iliyopo.
Makada akina Nape Nnauye hawajitokezi kujibu hoja wanakimbia vijijini kuwalaghai wananchi.

JK katangaza mchakato watu wakashangilia kwasababu watanzania ni watu wa matukio na si issue(s). Hivi tunaanza vipi kuandika katiba bila kuwa na dira ya taifa, bila kuwa na ramani ya taifa na bila kuwa na utashi wa kitaifa kuhusu mambo kama muungano.

Tulihoji mamlaka ya JK kuanzisha mchakato alipewa na nani.
Wapo wanaosema kapewa na bunge, huo ni uongo!

JK alipeleka mswada apewe mamlaka. Kilichotakiwa ni bunge kumpa mamlaka ya yeye kupeleka mswada wa kutafuta muafaka wa pamoja ikijemga mazingira mazuri na si kusimamia.

Matokeo ya kumpa mamla JK yamempa JK kuamua bunge la katiba liwe na wajumbe wa CCM na BLW ili kujenga wingi wa wana CCM katika kupitisha maamuzi yao.

Makosa yakaendelea pale mswada wa kumpa rais kuteua majina ulipofikiwa.
Again, tulionya hivi kwanini chama cha wagfanyakazi kifanye mkuatano wa wajumbe 200 wapeleke majina 20 na JK achague 5. Kwanini wasipeleke majina 5 ya mwisho bila kubadilishwa.
Hapo ikampa JK na CCM nguvu ya kuaongea wajumbe.

MwanaDiwani na Kobello wanasema rais amechaguliwa na wananchi na hivyo anapewa uwezo huo. That being the case kwanini basi asiandike katiba na kuridhiwa na bunge la JMT?
Kwanini aliunda tume na kwanani tume ilichukua maoni ya wananchi.
Ni kwanini iwepo kura ya maoni endapo Rais ana uwezo huo mkubwa aliopewa na wananchi.

Hoja kwamba CCM haitateka mjadala ni dhaifu. Hadi sasa halmashauri kuu imekutana kuweka msimamo. Moja ya mambo wanayotaka ni serikali 2 huku wakiwa na maoni jinsi ya kuboresha serikali w kwa ufanisi. Huu ni aina ya wendawazimu ambao Watanzania tumeukubali

1. Inawezekanaje baada ya miaka 50 ya kukataa kuandika katiba na baada ya tume 5 za kushughulikia muungano kushindwa kutoa jibu, leo CCM wana jibu la haraka kiasi hicho.

2. Ni kwanini CCM kama chama kiweke msimamo katika katiba ya wananchi wote. Hii ni njama ya kupitisha agenda zao kuwa katiba ya wananchi ingawa ni ya CCM hadi sasa wanapoelekea Dodoma

Tuendelee kuanisha njia zitakazotumika kuandika katiba ya CCM kwa jina la katiba ya Tanzania
1. Tayari wana wabunge wa CCM wa kutosha kutoka mabunge yote mawili na wakuteuliwa na JK

2. Tauyari wameshaondoa nguvu ya tume ya Warioba kwa kukataa wasiwemo katika bunge kutetea hoja za rasimu ili waweze kuzipindua wanavyotaka

3. Tayari akina Nape wanahubiri mambo kinyume na utaratibu. Rasimu haipaswi kufanyiwa mabadiliko zaidi ya kuboresha. Wao wameshajivika nguvu za kubadili rasimu kana kwamba bunge la katiba linaandika katiba na rasimu ya Warioba haina maana.

4. Wanaenda kumpata mwenyekiti au Spika wa bunge la katiba kwa kutumia wingi wao
a) Kuzuia hoja na pengine kukandamiza demokrasia kwa masilahi ya CCM
b) Kupenyeza agenda za CCM na kuzuia zinazopingana na hizo(Kupanga wasemaji)
c)Kutoa nafasi kwa CCM inayoandika katiba mafichoni kuwa mbadala wa tume ya Warioba

c) Kuweka utaratibu utakaohakikisha 'waasi' wa CCM wanashughulikiwa
i) Kura itakuwa ya wazi ili kuwabaini wasiokubaliana na CCM
ii) Kupitisha vifungu kwa nguvu za kura na si nguvu za hoja.

CCM wana plana A,B, C katika suala hili.
Plan A ni kama ilivyoelezwa hapo juu
Plan B ni kutumia plana A kulazimisha katiba yao iende kupigiwa kura ya maoni
Plan C ni kutibua mchakato ili uchaguzi ufanyike kwa katiba iliyopo au muda uongezwe

Plan B inaweza kukumbana na nguvu ya wananchi na Plan C itajenga hasira zaidi kwa wananchi.
Kwa plan zote A, B, C kuna jambo zuri sana linalojitokeza.

Mafanikio yanaweza kupatikana kwa CCM lakini ni kwa muda mfupi sana.
Ni kupitia plan hizo wananchi watafupisha muda wa kuvumilia ubovu(Kimweri) na kuharakisha hatua.

Yes, CCM watatengeneza katiba yao lakini ni risk kubwa sana wanaoichukua, ni njia nzuri sana ya kuharakisha mabadiliko yatakayotokana na wananchi kuelemewa na uchovu.
 
WASIOKUBALIANA NA HILA ZA CCM WAFANYE NINI?

Hadi sasa ni wazi katiba itakuwa ni ya CCM kwa jina la wananchi.
Kwa utaratibu uliotumika hakuna namna tunayoweza kusema wananchi wana nguvu nyingine ya kubadili nguvu kubwa ya CCM ambayo makamu wa rais ameisema 'kura'

Ndani ya CCM wapo wasiokubaliana na hali ya mambo yalivyo kwa dhati kabisa.
Kuna kundi la wapinzani na kundi la wale waliteuliwa ambao hawana lolote la kupoteza kutokana na hatima ya katiba zaidi ya mafao yao tu.

Kundi lenye wakati mgumu ni la wabunge wa JMT na BLW ambao matarajio yao ni kurejea bungeni iwe kwa katiba itakayoandikwa au ya zamani.

Kundi hili linatatizika kwa mambo mawili
1. Kukubaliana na CCM wahafidhina ili wapate kuteuliwa tena kutetea nafasi zao
2. Kukubaliana na umma na wapoteze nafasi zao za kuteuliwa na CCM

Kama yupo mtu anayetaka kubaki upande wa wananchini lazima ajitokeze wazi bila kificho na apinge nguvu zote za CCM kwa uwazi.

Ni bahati mbaya sana wapinzani wanavurugana wenyewe si Chadema/CUF au NCCR.
Hii ilikuwa nafasi nzuri sana kutumia uandikaji mbovu wa katiba kama kiboko cha kuwatandika wabunge wa CCM wa mabunge yote mawili.

Katika kipenge (c) tumeeleza kuwa CCM watatumia kura ya wazi ili kujua msimamo wa wabunge wao.

Hapa wapinzani na wapenda mabadiliko wakubaliane na CCM kwa hilo na wapinge kura ya siri. Itaonekana kama tuna 'contradict' kile tulichosema awali kuhusu mbinu ya CCM.
Hakuna contradictions bali ni mkakati mzuri, tufafanue:

Kura ya wazi itawaanika wale wote walioshiriki kuvuruga zoezi hilo hata kama lilishavurugwa kuanzia mwanzo.
Msimamo wa mbunge utajulikana wazi na hiyo takuwa ni bakora nzuri katika sanduku la kura.

Ukisoma maoni ya tume ni dhahiri shahiri wananchi wanataka kitu kingine nje ya kile CCM inachohubiri

Kwa wale watakaopambana na wabunge wa CCM mwakani endapo kura ya wazi itapigwa, basi hawatakuwa na haja ya kuongopa kuhusu 'kuleta' maendeleo au kujenga madaraja n.k.

Itakuwa ni jambo rahisi kuwakumbusha wapiga kura kuwa katika wale waliovuruga mchakato mbunge Mr au Mrs A wa CCM alipiga kura ya kukubaliana na CCM.

Hiyo tu itamweka mbunge huyo katika kujihami na si kushambulia na ndio utakuwa mwisho wa mbunge huyo.

Hii ni nafasi adhimu sana kwa wapinzani na wapenda mabaliko kuitumia ili kuhitimisha muda wa miaka 50 ya CCM na ulaghai na pengine kuwapeleka mapunzikoni kama UNIP na KANU.

Vyama hivyo vilikwenda mapunzikoni na sasa vipo katika 'Coma' kutokana na ukaidi kama unao onyeshwa na CCM.

Rai yetu ni kuwa wakubaliane na matakwa ya CCM ya utaratibu wa kura ya wazi kwasababu ni silaha nzuri sana mbele ya safari.

Kura ya siri inaweza isitoe matokeo wanayotaraji na ikawa haina nguvu kama kiboko mbele ya safari.

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3,

Nakubaliana na hoja zako zinazopingana na hoja za MwanaDiwani na Kobello kwamba Rais (na hata wabunge) walichaguliwa na wananchi, hivyo mandate ya Rais Kikwete kuteua wajumbe wa bunge la katiba is a mandate derived from the people/wananchi;

Nilishajadili elsewhere kwamba - ukifuatia historia ya nchi yetu katika muktadha tunaojadili, literally and practically, kwa katiba mpya za nchi kwa 1962 na ya sasa (1977), Rais na wabunge wa CCM derived mandate from each other na tukumbuke kwamba leo hii msimamo wa ccm juu ya muungano ni ule ule wa 1977, na kwa jinsi chama kilivyojipanga kuendelea kusimamia sera yake ya muungano, huu ni msimamo wa 1977 hivyo mandate inayojadiliwa na MwanaDiwani na Kobello lazima itazamwe kwa sura ya 1977; Kwanini nasema hivi?

Nani aliwapa mandate wabunge kuketi and adopt katiba ya sasa ya JMT (1977) ambayo ndiyo inayokinga serikali mbili kama sera ya ccm? Jibu ni kwamba mandate hiyo ilitoka kwa Rais wa JMT; je, nani alimpa rais wa JMT mandate ya kuwapa mamlaka wabunge kutunga katiba mpya (1977)? Rais alipata mandate hiyo kutoka kwenye Mkataba wa muungano (1964) licha ya suala hili kupigwa dana dana na TANU kwa karibia miaka 13 huku nchi ikiingizwa katika katiba ya muda kwa miaka 12 (1965-1977); solution ikapatikana baada ya kuunganisha vyama vya siasa - TANU na ASP, wakati vyama vya siasa hakuna sehemu vinatajwa kwenye mkataba wa muungano (1964); je, nani alipitisha mkataba wa muungano ambao ndio legal foundation ya muungano, ambao ndio ulizaa Katiba ya 1977 baada ya uchakachuajia muhimu kukamilika kwa miaka 12? Jibu ni kwamba aliyepitisha mkataba huo ni wabunge wa Tanganyika na Zanzibar; kwa akili nyepesi tu, ni rahisi kubaini kwamba tofauti na mtazamo wa MwanaDiwani ambae kama nilivyosema ni bingwa wa kukimbia mijadala ikishapamba moto kwani hoja zake zimejaa inconsistence, contradictions and incongruity, kumbe anatetea kitu sicho kuhusiana na mandate kwani iwapo tupo pamoja line by line:

Rais na Wabunge derived their respective mandate from each other. It is as clear as the summer sky that the said mandate wasn't derived from the people. Its just that the likes of Mwanadiwani, Nape and others have chosen to live the dark age over the enlightment age. What a misfortune.

Mkuu nguruvi3, wenzetu hawa MwanaDiwani, Nape Nnauye na wenzao wanasahau kwamba "even magicians run out of tricks";

Nitarejea tena kujadili tricks zilizotumika kwenye sakata la G55 halafu niunganishe na mtazamo wako juu ya scenario zinazoweza ku unfold Dodoma ili tuone CCM and her magicians watachomoka vipi katika kipindi hiki;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Siku wananchi wakitaka katiba yao, wakachoka kutungiwa katiba, wataitafuta tu.Na msishangae siku hiyo ikifika raisi asipokuwa mchagua majina, na wabunge wakaambiwa wakae pembeni. siku hiyo kwa nchi yetu bado sana.
Ni sentensi kama hizi zinazonifanya nihitimishe kwa kusema kuwa Wananchi wengi wala hawakuwa na haja ya katiba mpya na asilimia karibu 75 hawajahudhuria, hawajui kinachoendelea na hawatajali katba itakuwaje. Ni asilimia ndogo ndiyo wanashurutisha haya mambo.

By that simaanishi kuwa ni jambo baya, au watanzania wako backwards. Are the Chinese politically backwards? Compared to lets say Kenyans? Tuache kukariri mambo yasiyo ya ukweli.
 
MwanaDiwani na Kobello wanasema rais amechaguliwa na wananchi na hivyo anapewa uwezo huo. That being the case kwanini basi asiandike katiba na kuridhiwa na bunge la JMT?
Kwanini aliunda tume na kwanani tume ilichukua maoni ya wananchi.
Ni kwanini iwepo kura ya maoni endapo Rais ana uwezo huo mkubwa aliopewa na wananchi.

Hoja kwamba CCM haitateka mjadala ni dhaifu. Hadi sasa halmashauri kuu imekutana kuweka msimamo. Moja ya mambo wanayotaka ni serikali 2 huku wakiwa na maoni jinsi ya kuboresha serikali w kwa ufanisi. Huu ni aina ya wendawazimu ambao Watanzania tumeukubali

1. Inawezekanaje baada ya miaka 50 ya kukataa kuandika katiba na baada ya tume 5 za kushughulikia muungano kushindwa kutoa jibu, leo CCM wana jibu la haraka kiasi hicho.

2. Ni kwanini CCM kama chama kiweke msimamo katika katiba ya wananchi wote. Hii ni njama ya kupitisha agenda zao kuwa katiba ya wananchi ingawa ni ya CCM hadi sasa wanapoelekea Dodoma

Si kutakuwa na referrendum?
Mkuu huwezi kukataa mandate valiyopewa rais na wananchi, Kikwete alimshinda Slaa kwenye uchaguzi na Alimgaragaza Mbowe vibaya sana kwenye general elections pia.

Kwa karibu robo karne, CCM imekuwa ikipata zaidi ya robo tatu ya bunge. Achilia mbali enzi za chama kimoja.

Kikao cha Zanzibar in the early 90s kilikuwa ni kama kikao cha wapinzani na walikuja na msimamo wa kutoshiriki uchaguzi kwa katiba iliyopo. Wakashindwa (NCCR-Mageuzi).

Vitu kama hivi, vitaifanya CCM ijione bado ina mandate ya kutawala. Chama kiwe na zaidi ya robo tatu ya bunge??? Nipe mfano wa nchi nyingine yenye demokrasia ya vyama vingi North of us yenye legislative composition kama TZ. Hakuna!

Halafu unategemea wakuamini kuwa hawana mandate ya wananchi? They'd be gone a long time ago.

Rais amepewa mandate ya kufanya hivyo na Bunge LA JMT, huu ubishi mwingine ni overexaggeration. Rais ni sehemu ya bunge, he's more like a senator apart from being an Executive. Ana mamlaka ya ku-introduce a bill that can be voted down na ana mamlaka ya kutosaini bill yeyote. Hii ipo nchi nyingi tu zilizoendelea.

Mamlaka aliyo nayo Rais Kikwete ndiyo aliyo nayo Hollande, Obama, MASIRE, Dos santos, Uhuru etc... Sometimes even less than others. Halafu unauliza kwanini asingeandika katiba mwenyewe, hehehe .... are you serious?

Kuhusu CCM kuja na msimaamo wao, poa tu na CDM mje na msimamo wenu, wananchi wataamua. Sioni ajabu hapo.
 
Nguruvi3,
ningependa kuchangia katika maeneo kadhaa ya hoja zako hapo juu. Kama ulivyojadili mkuu Nguruvi3, CCM ilikataa katakata kukubali wazo la katiba mpya na umejadili vizuri sana suala hili hivyo nisingependa kuingia kwa ndani sana; lakini ningependa kusema hivi, bearing in mind kwamba kuna uwezekano wa katiba ya 1977 kuendelea kutumika per scenarios ulizojadili hapo juu:

CCM walikuwa wanapinga hoja ya katiba mpya kwa hoja zifuatazo:

1. Katiba iliyopo (1977) ilikuwa properly adopted, mchakato ulifuata njia zote sahihi ambapo wawakilishi wa wananchi enacted the constitution, hivyo katiba hiyo ni legitimate na taifa halihitaji katiba mpya;

2.Serikali ya ccm imechaguliwa na wananchi na ni serikali halali kwahiyo hakuna haja ya kuwa na transitional government itakayosimamia mchakato wa katiba mpya kufuatia mageuzi ya kisiasa nchini;

3. Chama kilipinga mapendekezo ya national constitutional conferences kwa hoja kwamba such conferences are held only when kunakuwa na transfer of power kutoka kwa serikali ya mkoloni kwenda kwa serikali huru;

4. Pia ccm ilijenga hoja kwamba haja ya katiba mpya inakuja pale tu kama taifa lipo clearly divided into political groupings zenye strong support in the electorate suala ambalo linapelekea chama tawala kupoteza credibility;

Vyama vya siasa wakati ule (miaka ya mwanzo ya tisini) vikajibu hoja kwamba wao kama vyama vilivyosajiliwa vina wanachama ambao ni watanzania kama ilivyokuwa kwa ccm kwahiyo hata wao wana haki ya kushiriki katika kutengeneza katiba mpya ya nchi. Hoja nyingine ya upinzani ilikuwa kwamba - katiba iliyopo only carters for partisan interests (CCM) na sio national interests. Majibu ya CCM kwa hoja hii yakawa kwamba: suala la vyama vya upinzani kwamba na wao vinawakilisha matakwa ya wananchi kama ilivyo kwa wana ccm, suala hili litakuwa determine wakati wa chaguzi kuu ndani ya mfumo wa vyama vingi; kwahiyo vyama vya upinzani wajibu wao ni to walk the talk-to prove themselves kwenye sanduku la kura kama kweli vinaungwa mkono hivyo vinastahili kushirikishwa katika mchakato wa kutunga katiba mpya; CCM ikaenda mbali zaidi na kusema kwamba: usajili wa vyama husika unavitambua tu kama taasisi halali za kisiasa na ruksa kwa vyama hivi ni katika kujitengenezea sera zao, itikadi, establish their positions on various issues na kujipigia kampeni mbele ya umma; kitendo cha kuvisajili kama vyamma vya siasa, ccm argued further, doesn't necessarily mean kwamba vina haki ya kushiriki let alone kuwa consulted katika maamuzi muhimu ya kitaifa;

Hizi ndio zilikuwa ni hoja za msingi za CCM kwa miaka karibia 20 kabla ya Rais Kikwete kukubali kuanzisha mchakato wa katiba mpya; validity of such arguments ni kitu that we can spare for later, lakini kwa sasa kilicho muhimu ni uwezekano wa taifa kuendelea na katiba ya sasa kwa hoja ya wana ccm kwamba ni katiba halali;

Kama nilivyojadili hapa and elsewhere, hoja juu ya legitimacy ya katiba ya JMT (1977) is full of fallacious (not true/accurate); hoja hii ni lazima ipingwe kwa nguvu zote na kwa ushahidi wote kwamba the 1977 Constitution isn't a people's constitution; at no point, katiba hii ilihusisha wananchi; katiba hii ilikuwa drafted na kamati ya chama (CCM), ikapata baaka za NEC-CCM, ikawa enacted na bunge la katiba lenye wajumbe walioteuliwa na rais, ambao literally walikuwa ni wana ccm wote; kati ya wajumbe 212, ni wajumbe 101 tu (chini ya nusu) walitokana na uchaguzi majimboni! Wengine wote waliteuliwa moja kwa moja kwenda kuwakilisha the interest of the "executive branch"; hakuna tofauti kubwa sana na kilichotokea katika mchakato wa sasa na Nguruvi3 amejadili hili vyema; kwa kifupi, hata kwa standard za CCM tu, bunge lile wasn't a real representation of the people;

Tuseme basi hoja juu ya uhalali wa katiba ya 1977 inapita kwa kuzingatia mazingira ya wakati ule, hii haina maana kwamba taifa halihitaji katiba mpya; katiba mpya ni muhimu kama tunataka kuwa na a peaceful transition na kama tunataka kubakia na amani na utulivu; vinginevyo hatari za umwagaji wa damu na taifa kuwa categorically listed as a failed state ni dangers that are imminent; Kobello katika mjadala wetu mwingine anasema hatari hizi hazipo;pengine ni kwa mtazamo huu, ccm inaendelea kujiamini kwamba inaweza kuendelea kuwaendesha wananchi kwa jinsi inavyotaka;

Iwapo ccm italazimisha turudi kwenye katiba ya 1977, ni muhimu itambue kwamba katiba ya sasa haifai in practice and in principle:

Kwanza, na hii ni on purely practical level, katiba ya sasa is unworkable! Hii ni kwa sababu, licha ya mapungufu tajwa hapo juu and elsewhere, katiba hii msingi wake ni nguzo kuu mbili: one party monopoly system and two government union structure. Nguzo zote hizi mbili no matter how much ccm is trying to hold, these two pillars are crumbling if not crumbled already; kama alivyojadili Nguruvi3 hapa and elsewhere, chama na bunge lake vimekaa vikao vingi na kuunda tume kadhaa kujaribu kutatua mgogoro wa muungano bila mafanikio; ndio maana Nguruvi3 anauliza, je haya maneno ya ccm kupitia Nape Nnauye kwamba msimamo ni serikali mbili kwa nia ya kuboresha mfumo uliopo, ccm itakuja ni kipi kipya? Isitoshe, ccm ilishindwa wakati ule zanzibar bado ni sehemu ya JMT kwa mujibu wa katiba ya znz na ya JMT, lakini sasa znz ni moja ya nchi zinazounda JMT kwa mujibu wa katiba ya sasa ya znz; all in all, the ongoing crisis of the union should be (to any reasonable person) a sign that the 1977 constitution isn't workable;

Pili, ni katika suala la principle; katiba ya nchi isn't simply a legal document or technical document, bali its a "political document"; ili document hii ipate political legitimacy na istahili obedience and loyalty ya watawala na watawalwa, lazima iwe na national consensus (iridhiwe kitaifa), sio iridhiwe kichama (ccm) kama nape et al wanavyojaribu kulazimisha; katiba ambayo haina national consensus, moja kwa moja looses its political legitimacy;
MwanaDiwani, Nape Nnauye, Kobello and others of the same vein:

Katiba genuine ni ile yenye political legitimacy, kitu ambacho hakipo katika aina ya katiba mnayotaka kutulazimishia wananchi; katiba inayokosa political legitimacy kwa kawaida huwa imposed on the populace na hakuna mtu ambae huijali, both ruled and rulers alike; sasa ndugu zangu, pengine mnapojichanganya ni hapa:

Kuwa na katiba ya aina hii haina maana kwamba serikali ya ccm hasa miaka ya nyuma didn't have legitimacy kwa kutawala chini ya katiba ya 1977. Ukweli ni kwamba it had legitimacy lakini such legitimacy was derived from other sources, the source of its legitimacy wasn't the 1977 constitution; utawala wa chama kimoja wakati wa ujamaa ulikuwa na legitimacy iliyokuwa derived from:
1. Ujamaa
2. Historia ya harakati za uhuru.
3.Na kutoka kwa a popular and charismatic leader (Nyerere).

Je, yepi kati ya haya mnaweza kuyatumia kuhalalisha uhalali wenu wa kutawala chini ya katiba ya 1977 endapo hiyo ndio njama yenu?

Kumbukeni, kupitia sources hizi tatu za legitimacy chini ya Mwalimu, umma haukujali sana juu ya katiba na content yake na wengi hawakujali sana iwapo katiba ilikuwa inaheshimiwa au lah; lakini leo hii mazingira sio kama yale ya awali mnayojaribu kulazimisha:

*Historical legitimmacy ya TANU na ASP kama independent movements imeshachuja;
*hatuna tena charismmatic leaders ndani ya ccm;
*itikadi ya ujamaa imechinjiwa baharini na viongozi wa ccm (bila kushirikisha wanachama wake); maswali yanayofuatia ni je:

Karika hali hii, ni kitu gani kitatusaidia kuleta maridhiano ya kitaifa? Jibu ni katiba mpya ambayo inatokana na wananchi regardless of their political orientations and persuasions;

Je, ni kitu gani kitaleta uaminifu kwa upande wa watawala na upande watawalwa kwa taifa lao? Jibu ni hilo hilo hapo juu - yani Katiba Mpya;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
\Pili, ni katika suala la principle; katiba ya nchi isn't simply a legal document or technical document, bali its a "political document"; ili document hii ipate political legitimacy na istahili obedience and loyalty ya watawala na watawalwa, lazima iwe na national consensus (iridhiwe kitaifa), sio iridhiwe kichama (ccm) kama nape et al wanavyojaribu kulazimisha; katiba ambayo haina national consensus, moja kwa moja looses its political legitimacy;
MwanaDiwani, Nape Nnauye, Kobello and others of the same vein:

Katiba genuine ni ile yenye political legitimacy, kitu ambacho hakipo katika aina ya katiba mnayotaka kutulazimishia wananchi; katiba inayokosa political legitimacy kwa kawaida huwa imposed on the populace na hakuna mtu ambae huijali, both ruled and rulers alike; sasa ndugu zangu, pengine mnapojichanganya ni hapa:

Kuwa na katiba ya aina hii haina maana kwamba serikali ya ccm hasa miaka ya nyuma didn't have legitimacy kwa kutawala chini ya katiba ya 1977. Ukweli ni kwamba it had legitimacy lakini such legitimacy was derived from other sources, the source of its legitimacy wasn't the 1977 constitution; utawala wa chama kimoja wakati wa ujamaa ulikuwa na legitimacy iliyokuwa derived from:
1. Ujamaa
2. Historia ya harakati za uhuru.
3.Na kutoka kwa a popular and charismatic leader (Nyerere).

Je, yepi kati ya haya mnaweza kuyatumia kuhalalisha uhalali wenu wa kutawala chini ya katiba ya 1977 endapo hiyo ndio njama yenu?

Kumbukeni, kupitia sources hizi tatu za legitimacy chini ya Mwalimu, umma haukujali sana juu ya katiba na content yake na wengi hawakujali sana iwapo katiba ilikuwa inaheshimiwa au lah; lakini leo hii mazingira sio kama yale ya awali mnayojaribu kulazimisha:

*Historical legitimmacy ya TANU na ASP kama independent movements imeshachuja;
*hatuna tena charismmatic leaders ndani ya ccm;
*itikadi ya ujamaa imechinjiwa baharini na viongozi wa ccm (bila kushirikisha wanachama wake); maswali yanayofuatia ni je:

Karika hali hii, ni kitu gani kitatusaidia kuleta maridhiano ya kitaifa? Jibu ni katiba mpya ambayo inatokana na wananchi regardless of their political orientations and persuasions;

Je, ni kitu gani kitaleta uaminifu kwa upande wa watawala na upande watawalwa kwa taifa lao? Jibu ni hilo hilo hapo juu - yani Katiba Mpya;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Like we discussed before, legitimacy ya katiba ya 1977 imetokana na wananchi through their president and their parliament and was cemented by local and general election results kwa zaidi ya robo karne.

The same applies to the new constitution, tofauti ni kuwa kutakuwa na referrendum. Pia kutakuwa na local and general elections soon, so no matter what wananchi wataamua kwa kutumia kura. There will be no bloodshed!, please refrain yourselves from such ideas and understand your people!

Hatuna charismatic leaders, hatuna struggle for freedom na hatuna ujamaa. Ila usisahau kitu kimoja muhimu sana ... HATUNA UPINZANI.

Katibva mpya itapatikana na katiba yeyote lazima itakuwa na kasoro kutegemeana na mawazo ya mtu. Mfano,rasimu hii inatoa uhuru wa utafiti wa sayansi .... does that endorse stem cell research in Tanzania?
Pia inakataza viongozi kupelekwa ICC, are we out of ICC? WHY? Ni asilimia ngapi walitoa maoni haya?

Lets just calm down.
 
Pamoja na kuwaunga mkono Mdau Nguruvi3 na Mchambuzi kwa kukumbushia licha ya ajenda ya Katiba Mpya kuvaliwa njuga na Chadema na baadhi ya vyama vya upinzani, lakini kulikuwa na shinikizo kutoka nchi wahisani wanachangia gharama za uendeshaji uchaguzi Mkuu hasa nchi za Umoja wa Ulaya kushauri Kikwete juu ya hilo. Pengine kelele toka upinzani tu zisingesaidia sana, ila woga wa kukosa anachokitazamia toka kwako ndicho kilicholegeza moyo wa Farao.

Pamoja na CCM kujenga hoja kwamba suala la Katiba Mpya si ilani yao ya uchaguzi na kumshinikiza Kikwete aiondoe kisha kushindikana, kilichofanyika ni kuiteka itokee kadiri ya matakwa yao, ndio maana hatushangai kuona idadi kubwa ya wanasiasa na makada wa CCM walioingizwa kwa mlango wa nyuma kwa tiketi za kuwakilisha wa makundi nafasi ambazo zilipaswa ziwakilishwa na raia wasio wanasiasa kwa vile wanasiasa wameshawakilishwa tayari.

Dalili ninazoziona dhahiri iwapo wataweza kuheshimu sheria na miongozi ya muundo wa Katiba mpya hasa kifungu cha 25 ambacho kinataka wajumbe ambao ni wabunge wa bunge maalum la Katiba wasibadilishe vifungu vya rasimu bali kuviboresha kwa vile hayo ni jumla ya maoni ya wananchi. Itakuja kutia aibu siku kura za wananchi zikikataa katiba kwa vile baadhi ya vifungu walivyopendekeza ndani ya Rasimu hiyo kunyofolewa na wabunge. Hilo haliko wazi lakini dalili zipo tokana na CCM ilivyojipanga.
 
Like we discussed before, legitimacy ya katiba ya 1977 imetokana na wananchi through their president and their parliament and was cemented by local and general election results kwa zaidi ya robo karne.

The same applies to the new constitution, tofauti ni kuwa kutakuwa na referrendum. Pia kutakuwa na local and general elections soon, so no matter what wananchi wataamua kwa kutumia kura. There will be no bloodshed!, please refrain yourselves from such ideas and understand your people!

Hatuna charismatic leaders, hatuna struggle for freedom na hatuna ujamaa. Ila usisahau kitu kimoja muhimu sana ... HATUNA UPINZANI.

Katibva mpya itapatikana na katiba yeyote lazima itakuwa na kasoro kutegemeana na mawazo ya mtu. Mfano,rasimu hii inatoa uhuru wa utafiti wa sayansi .... does that endorse stem cell research in Tanzania?
Pia inakataza viongozi kupelekwa ICC, are we out of ICC? WHY? Ni asilimia ngapi walitoa maoni haya?

Lets just calm down.

Hali halisi ya Katiba hii ya sasa 1977 wananchi hawakushirikishwa kama inavyofanyika sasa, walioifanyia kazi ni baraza la wawakilishi na wabunge wa bunge la Muungano. Mchakacho uliofanyika safari hii ni mpana sana na watu po pote wanajua nini kinaendelea kuhusu katiba mpya. Hiyo ya mwaka 1977 nilikuwa na akili za kutosha lakini sikusikia cho chote toka kwa wazazi wangu au shuleni wakiongelea hilo, ilikuwa ni mambao ya ndani serikalini huko. Si mbaya njia waliyotumia maana kipindi hicho mwamko wa wananchi usingeweza kuwa kama wa leo, walichojua kuchagua wabunge huoni sura ila wanawakilishwa jembe na nyumba, ukichagua nyumba umechangua Mchambuzi na ukichagua jembe umemchagua Kobello ndio mazingira ya wakati huo na ilibidi kurahizisha hivyo kwa watu wa vijijini. Leo ni kizazi kingine kimejaa walioelimika hata kama hawakupata elimu ya kutosha. Kinachoendelea na mfumo wa serikali ni kushindana na wakati bila kusoma ishara za nyakati hatima ni kuishia mbio ukingoni.
 
Hali halisi ya Katiba hii ya sasa 1977 wananchi hawakushirikishwa kama inavyofanyika sasa, walioifanyia kazi ni baraza la wawakilishi na wabunge wa bunge la Muungano. Mchakacho uliofanyika safari hii ni mpana sana na watu po pote wanajua nini kinaendelea kuhusu katiba mpya. Hiyo ya mwaka 1977 nilikuwa na akili za kutosha lakini sikusikia cho chote toka kwa wazazi wangu au shuleni wakiongelea hilo, ilikuwa ni mambao ya ndani serikalini huko. Si mbaya njia waliyotumia maana kipindi hicho mwamko wa wananchi usingeweza kuwa kama wa leo, walichojua kuchagua wabunge huoni sura ila wanawakilishwa jembe na nyumba, ukichagua nyumba umechangua Mchambuzina ukichagua jembe umemchagua Kobellondio mazingira ya wakati huo na ilibidi kurahizisha hivyo kwa watu wa vijijini. Leo ni kizazi kingine kimejaa walioelimika hata kama hawakupata elimu ya kutosha. Kinachoendelea na mfumo wa serikali ni kushindana na wakati bila kusoma ishara za nyakati hatima ni kuishia mbio ukingoni.
Ah! .... ngoja niende MMU naona hapa mnafosi kingi.
 
Kuna jambo halieleweki katika bunge la Katiba.
Uchaguzi wa wawakilishi wa makundi ya kijamii umelenga kuhakikisha wawakilishi hao wanayaangalia mambo yanayogusa makundi yao kwa namna moja au nyingine.


Halafu kuna wabunge wa bunge la JMT na BLW.

Hawa ni wawakilishi wa wananchi bila kujali itikadi zao za kisiasa.

Uwepo wao bungeni si chama ni kwa masilahi ya kundi la jamii kwa ujumla wake.


Upatikanaji wa wabunge(JMT) na wawakilishi(BLW) unapitia mifumo ya chama, lakini kazi yao ya kwanza ni kuwakilisha wananchi na si vyama vyao.


Kwa vile utaratibu ulishaharibiwa toka mwanzo matatizo yanayotokea sasa ya misimamo ya vyama ni zao la ubovu tangu awali.


Laiti misingi ya uandikaji katiba ingefuatwa bunge la katiba lisingekuwa na sehemu kubwa ya wabunge vyama.


Hapo kungekuwa na mijadala ya maana na endelevu kwasababu hakuna ambaye angefungwa mikono na minyororo ya vyama.


Tunasisitiza kuwa zoezi zima liliratibiwa hovyo na kwa ni ovu.

Hii ni katiba itakayotokana na wananchi?


Tusemezane

 
Nguruvi3
Kwenye baadhi ya vyombo vya habari leo, baadhi ya wabunge wa CCM wameonekana kushtukia deal kuingizwa kichakichwa kinyume cha matakwa ya wananchi waliowatuma bungeni, mmojawapo ni Mbunge Kangi Lugola ameelezea wazi katika kifungu kinachohusu mfumo wa serikali ndani ya Muungano wa Tanzania, yeye yuko tayari kueleweka vibaya kwa Chama chake CCM lakini hayuko tayari kwenda kinyume cha matakwa ya wananchi waliomchagua na kumtuma kwamba wao wanataka mfumo wa serikali tatu.

Baadhi ya wabunge wameenda mbali zaidi kwamba wabunge wa bunge la Muungano kutoka visiwani ambao wana serikali yao utakuta wanaingizwa bara kwenye kamati ambazo haziihusu serikali ya visiwani kama Serikali za Mitaa, hilo lina utatanishi na mipaka haiko wazi, bora kuwe na bunge la Muungano na bara/visiwani kuwa na mabunge yao kama ilivyo visiwani. Nisingependa kwenda mbele zaidi katika hili maana mengi yanayolalamikiwa wabunge wa Visiwani kuingia ndani ya mambo ya bara yanajulikana na mipaka haiko wazi.

Pengine Wabunge wa bara wamekosa zaidi uzalendo katika kutetea wananchi wa bara kama itokeavyo wa visiwani wanaposhikamana kutetea haki za wa visiwani. Visiwani licha ya kutetea yanayowahusu hawako tayari kuachia advantages wanazozipata wawakilishi katika nafasi ya Muungano.

Kuhusu wabunge wa kuteuliwa kutoka makundi kuwakilisha makundi yao naona lisingeweza kuepukika, vinginevyo bila kfuanya hivyo wangekuwa wamesahaulika. Kwa vyo vyote kama alivyosema
Mchambuzi kumekuwepo na loop hole ambamo serikali na CCM wametumia kuongeza idadi ya wajumbe kutetea wanachokitaka, hata hivyo nionavyo kwa baadhi ni sawa na kumlazimisha punda kwenda kisimani lakini kuyanywa maji itabaki hiari yake.
 
Candid Scope;8744289]
Nguruvi3
Kwenye baadhi ya vyombo vya habari leo, baadhi ya wabunge wa CCM wameonekana kushtukia deal kuingizwa kichakichwa kinyume cha matakwa ya wananchi waliowatuma bungeni, mmojawapo ni Mbunge Kangi Lugola ameelezea wazi katika kifungu kinachohusu mfumo wa serikali ndani ya Muungano wa Tanzania, yeye yuko tayari kueleweka vibaya kwa Chama chake CCM lakini hayuko tayari kwenda kinyume cha matakwa ya wananchi waliomchagua na kumtuma kwamba wao wanataka mfumo wa serikali tatu
Mkuu hili tumelieza mapema sana.
Kwa kutambua kuwa suala la Tanganyika lina unyeti na hisia kwa Watanganyika, wabunge wameamua kufanya kura kuwa ya siri.

Tumewashauri wapinzani kuwa ili wawe katika nafasi nzuri wangekomalia kura ya wazi.
Hilo lingewaweka wabunge wasaliti hadharani na kutoa nafasi ya wananchi kuwajua mmoja mmoja wakiwemo wagombea urais watarajiwa. In other words ni kuwaweka katika spot kwa masilahi ya Tanganyika
Baadhi ya wabunge wameenda mbali zaidi kwamba wabunge wa bunge la Muungano kutoka visiwani ambao wana serikali yao utakuta wanaingizwa bara kwenye kamati ambazo haziihusu serikali ya visiwani kama Serikali za Mitaa, hilo lina utatanishi na mipaka haiko wazi, bora kuwe na bunge la Muungano na bara/visiwani kuwa na mabunge yao kama ilivyo visiwani. Nisingependa kwenda mbele zaidi katika hili maana mengi yanayolalamikiwa wabunge wa Visiwani kuingia ndani ya mambo ya bara yanajulikana na mipaka haiko wazi
Hili nalo tumeliongelea kwa undani kuwa wznz ni wazuri sana wa kudai haki hata zisizokuwa zao.

Kwa mfano, mjumbe wa kamati ya bunge la JMT kutoka znz kwanini awe katika kamati za bunge kwa mambo yanayohusu Tanganyika.

Hivi ni kwanini mkurugenzi wa maendeleo wa wilaya ya Tanganyika atoke znz.
Hivi ni kwanini waziri wa afya na watumishi wengine watoke znz huku SMZ ikiwa na watu wake.

Hivi karibuni wameanzisha baraza la mitihani, utashangaa wajumbe wa bodi ya NECTA robo ni wznz. Kwanini wawepo katika chombo kisichowahudumia wao na wasichokitambua?

Kilichopo hapa ni kukosa uzalendo kwa Watanganyika, na ndio hoja kuu kuwa Watanganyika watanufaika zaidi na kurejea Tanganyika kuliko ilivyo.

Ni kwa utegemezi uliopo wznz wanataka mamlaka kamili lakini hawathubutu, narudia tena hawathubutu wala hawana uwezo wa kupanua vinywa na kusema vunja muungano.
Wanataka mambo ya mikataba n.k. kwa kutambua wananufaika na Tanganyika.
Mtanganyika jiulize unanufaika nini kutoka znz zaidi ya kuchomwa moto!!!

Wanamnyonya Mtanganyika kwa kutumia falsafa ya 'CHANGU CHANGU, CHAKO CHANGU'.
Kosa hili Watanganyika hawalioni na kama wataendelea na mambo ya serikali 2 litawaumiza zaidi.

Kwasasa Mtanganyika analipa kodi lakini mtoto wake hapati mkopo kwasababu kuna nafasi za upendeleo kwa wznz ambao mwisho wa siku hawarudishi mikopo.

Kwa mwaka mmoja wznz 1000 wanasoma kwa kodi za Watanganyika.
Tujiulize hivi kwanini tuvunje migongo kwa kulipa kodi kwa hisani ya watoto wa jirani?
Ni lini mtoto wa Tanganyika atapewa mkopo znz kama hawezi kupewa hata leseni ya udereva kama Mtanzania ila foreigner?

Ninyi vijana wa Tanganyika amkeni sasa na kudai Tanganyika.
Kurudi kwa Tanganyika kutuwapa nafasi ya kuamua hatim na fursa zenu kimaendeleo bila kuminywa
Pengine Wabunge wa bara wamekosa zaidi uzalendo katika kutetea wananchi wa bara kama itokeavyo wa visiwani wanaposhikamana kutetea haki za wa visiwani. Visiwani licha ya kutetea yanayowahusu hawako tayari kuachia advantages wanazozipata wawakilishi katika nafasi ya Muungano.
Tunawataka wabunge wa bara waelewe kuwa wapo kwa ajili ya Tanganyika. Tanzania ilishakataliwa na znz kwa kubadili katiba wapendavyo. Hatuwezi kuendelea kuwabeba mgongoni ili wanufaike na fursa za muungano wakati hawamtaki Mtanganyika asilani.

Znz wametengeneza sheria za kumbagua Mtanganyika wala si mkenya, Mganda au Mmalawi.
Sheria hiyo imewekwa katika ajira ambapo Mtanganyika hajulikani yupo kundi gani.
Wameondoa mafuata na gesi kwa sababu wanamchukia Mtanganyika na wameenda mbali kumpiga kiberiti na mafuta ya petrol.

Tutaendelea kurithisha watoto wetu upuuzi huu hadi lini. Kuna nini rutakosa tukiwa na Tanganyika yetu. Ni muda wa kurudi Tanganyika sasa hilo mkae mkifahamu.


 
KURA ZA BUNGE LA KATIBA(SIRI /WAZI)
OPTION ZINAZOWEZA KUPATIKANA KUTOKANA NA BUNGE

Wana duru siku za karibuni tulizungumzia vema sana kuhusu kura katika BLK.
Mzozo uliozuka leo ni sehemu ya mjadala mpana tuliouona wiki iliyopita.

Tuaendelea kuangalia kwanini imetokea sasa, CCM ina nafasi gani, wapinzani wana nini na suala hilo.

Kisha tutaangalia zile option tulizosema bunge la katiba linaweza kuzichomeka kwa kutumia CCM katika mabandiko ya nyuma. Tayari kuna wazo la serikali 1 n.k. tutaangalia hatima ya bunge kwa siku zijazo.

Na mwisho tutaangalia umuhimu wa kurudi kwa serikali ya Tanganyika.
Licha ya ubovu wa mchakato bado Watanganyika wana fursa ya kupunguza maumivu na machungu yanayotokana na muungano.

Saty tune
 
wakuu Nguruvi3 , Mchambuzi tunawasoma sana na darasa linatuingia sawasawa, binafsi nakosa chakuchangia maana mlishatukatisha tamaa kitambo kuwa katiba mpya itakayotokana na wananchi kuipata chini ya CCM ni ndoto na danganya toto, hata hivyo huu mjadala wa kura ya wazi au ya siri una ukakasi mkubwa,, kwa ufupi WANAOTAKA KURA YA WAZI WANA AGENDA YA SIRI, NA WANAOTAKA KURA YA SIRI WANA AGENDA YA WAZI...
 
Last edited by a moderator:
Kilichotokea kwenye Bunge la katiba hakina tofauti sana na hekaya za kesi ya Ngedere. Hii wamekabidhiwa "Nyani" wazoefu, aka makada wa CCM wa muda mrefu.

Kuwa na matumaini kuwa Tanzania itapata katiba nzuri kutokana na hawa watu ni sawa na kuwaza timu yetu ya taifa itaifunga barcelona and the likes. It's statistically no an imposibillity but we both know where everyone will bet for.

Mimi ni mfuasi wa tulipofikia sasa kama taifa, tuendelee kubomoa hadi ifikie hatua hakuna pa kuficha uovu wetu. ififkie hatua tuchoke,wananchi wachoke. hapo ndio kuna la maana litakapofanyika.

Hivi kuna mtu yoyote humu anafikiria kuwa Kikwete atateua Baraza la Mawaziri kutoka kwenye pool ya watu aliowapendekeza kwenye nafasi za uongozi ambao wanaweza kufanya maajabu au kufanya ambacho CCM imekifanya kwa miaka 50 na kufeli?

hii katiba ya sasa hivi naiona kama "stopgap" . somehow a knee jerk reaction just because katiba mpya is the popular thing around. I am saying this and i wlil say this again. unless they vote for three governments of which we will surely make CNN front page as a nation with 3 damn presidents, this new constitution will not move a needle as far as geopolitics or economics are concerned. This is just satisfying a few over-sized egos.

Siku wananchi wakitaka katiba yao, wakachoka kutungiwa katiba, wataitafuta tu.Na msishangae siku hiyo ikifika raisi asipokuwa mchagua majina, na wabunge wakaambiwa wakae pembeni. siku hiyo kwa nchi yetu bado sana.
Maneno haya yanazidi kubeba uzito kadri tunavyosikia Dodoma hali ilivyo.
 
wakuu Nguruvi3 , Mchambuzi tunawasoma sana na darasa linatuingia sawasawa, binafsi nakosa chakuchangia maana mlishatukatisha tamaa kitambo kuwa katiba mpya itakayotokana na wananchi kuipata chini ya CCM ni ndoto na danganya toto, hata hivyo huu mjadala wa kura ya wazi au ya siri una ukakasi mkubwa,, kwa ufupi WANAOTAKA KURA YA WAZI WANA AGENDA YA SIRI, NA WANAOTAKA KURA YA SIRI WANA AGENDA YA WAZI...
Zumbe hatukutakitisha tamaa tulikuwa tunaeleza mwelekeo, nadhani unaona ukweli ulivyo ndugu yangu
 
Kuna jambo halieleweki katika bunge la Katiba.
Uchaguzi wa wawakilishi wa makundi ya kijamii umelenga kuhakikisha wawakilishi hao wanayaangalia mambo yanayogusa makundi yao kwa namna moja au nyingine.


Halafu kuna wabunge wa bunge la JMT na BLW.

Hawa ni wawakilishi wa wananchi bila kujali itikadi zao za kisiasa.

Uwepo wao bungeni si chama ni kwa masilahi ya kundi la jamii kwa ujumla wake.


Upatikanaji wa wabunge(JMT) na wawakilishi(BLW) unapitia mifumo ya chama, lakini kazi yao ya kwanza ni kuwakilisha wananchi na si vyama vyao.


Kwa vile utaratibu ulishaharibiwa toka mwanzo matatizo yanayotokea sasa ya misimamo ya vyama ni zao la ubovu tangu awali.


Laiti misingi ya uandikaji katiba ingefuatwa bunge la katiba lisingekuwa na sehemu kubwa ya wabunge vyama.


Hapo kungekuwa na mijadala ya maana na endelevu kwasababu hakuna ambaye angefungwa mikono na minyororo ya vyama.


Tunasisitiza kuwa zoezi zima liliratibiwa hovyo na kwa ni ovu.

Hii ni katiba itakayotokana na wananchi?


Tusemezane

Yalisemwa na sasa yanatokea
 
.Wananchi wamepigwa chenga kwasababu kuna eneo ambalo hawana 'say'.

Rais amechaguliwa na wananchi hiyo haimpi nguvu za kutenda kila jambo.
Ingalikuwa ni hivyo basi kusingekuwa na haja ya kutaka NGO au asasi zingine zichague wabunge. Rais angekuwa na nguvu ya kuchagua tu.

Kitendo cha kusema watu walete majina halafu yeye anayachekecha hakina uaminifu ndani yake.
Kwa mfano, katika mapendekezo ya wajumbe 10 kutoka majina 200 jina la Kobello limeongoza kwa kuwa nambari 1.Katika final list ya rais Kobello hayupo.

Hapa inapeleka ujumbe gani kwa waliochagua na Kobello.
Ni kigezo gani alichotumia rais ambacho wajumbe 200 walishindwa kukiona.

Na je kulikuwa na sababu za kupendekeza majina kama rais alikuwa na power ya kuchagua amtakaye? Hivi huoni hiyo ni loop hole ya rais kupenyeza interest zake akilindwa na sheria?

Nakubali kuwa tume ingepewa nguvu zaidi za kuchagua angalau ingeleta maana.
Tatizo ni kuwa tume yenyewe haiaminiwi.
Mfano, wajumbe wa tume si wajumbe wa bunge la katiba. Nani atafanua yaliyotokana na rasimu?

Ukiangalia matatizo yote yanatokana na short cuts ambazo rais amezifanya.
Hakufuata utaratibu kwasababu tu aliogopa hoja zingine zisiligawe taifa.
Hata hivyo hoja hizo zitarudi kwa mlango wa nyuma na kuliumiza taifa.

Mfano, ilitakiwa kwanza kura ya maoni kwa wznz kama wanataka muungano au la.
Baada ya hapo tugeweza ima kuwa na muungano na wa aina gani na kuteneza dira ya taifa au kuvunja kila mmoja kivyake.

Rais aliogopa hilo ndio maana mswada wa kwanza ulisema muungano usijadiliwe.
Matokeo ya hayo ni kuwa na mapendekezo ya serikali 3. Lakini wapo wanaotaka 2 na wengine kuvunja kabisa. Suala linabaki kama tume haikuweza kuja na muafaka unaokubaliwa, watu 600 watawezaje?

Suala la muungano litaendelea kujitokeza na pengine rais atakosa control kwasababu hakukuwa na consensus from the very begining. Sijui kama atakuwa ame solve tatizo.
..........
 
Back
Top Bottom