Duru za Siasa: Kuelekea bunge la katiba,Je, katiba itatokana na wananchi?

Duru za Siasa: Kuelekea bunge la katiba,Je, katiba itatokana na wananchi?

Mkuu Mkandara, katika kujibu swali lako, naomba nikurudishe nyuma kidogo...hivi kwa kusema kweli mfumo tulio nao sasa ni wa serikali ngapi? Mimi naamini kiuhalisia tayari tunazo serikali tatu. Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu kwa upande wa nchi ya Zanzibar kuna serikali mbili na kwa nchi ya Tanzania pia tunazo serikali mbili; sasa swali ni je, ndani ya hizi nchi mbili tuna jumla serikali ngapi? Kama tunazo serikali mbili nchini Tanzania, hizo serikali bila shaka moja inashughulikia mambo ya Muungano na nyingine inashughulikia mambo ya Tanzania bara (Tanganyika) na kama nchi ya Zanzibar pia ina serikali mbili, ni wazi moja inashughulikia mambo ya Muungano na nyingine mambo ya Zanzibar. Je mpaka hapo niko sahihi?

Sasa basi kwa kuwa kuna mambo ya Tanzania bara, mambo ya Zanzibar na mambo ya Muungano, je kiuhalisia tunazo serikali ngapi? Ni kipi kipya kimeletwa na Rasimu ya Katiba kama ilivyosomwa na Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba kwa wajumbe wa Bunge la Katiba? Tunaye Kiongozi wa serikali bungeni ambaye eneo lake la kujidai linaishia Chumbe. Tunaye kiongozi wa serikali ndani ya Baraza la Wawakilishi ambaye eneo lake la kujidai halivuki bahari. Halafu tunayo serikali ambayo mamlaka yake hayana mpaka ndani ya Jamhuri, au nakosea? Si tumeaminishwa yapo mambo ya Muungano? Kwa kujibu swali lako; Naamini tayari tunazo serikali tatu ila kwa uhuni tu tukaamua kuziita mbili, sasa Rasimu inasema uhuni sasa basi! Koleo liitwe kwa jina lake! Uswahili sasa basi!

Muundo na taratibu za serikali 3 tayari tunao kwani Rasimu ya Jaji imewasha taa tuongee tukionana na siyo kuendelea kuendesha mambo gizani. Kwa kukaa gizani katiba ilivunjwa, hakuna aliyeweza kuona; uhaini ulifanywa, hakuna aliyeona na kukekemea; mambo ya kipuuzi hayakuhitaji kufumbiwa macho kwani giza nene tayari lilitamalaki mbele ya macho yetu. Rasimu imetuletea mwanga, waliozoea kufanya mambo gizani sasa wanajifungia kwenye semina wakipanga watakavyohujumu mwanga usiwamulike (masikini CCM!). Hapana Mkuu Mkandara, wamechelewa! It was just a matter of time and the right time has arrived, it is here and it wont go away that easily. Kikwete beware!
Hizi serikali 2 kila Upande umezipata vipi maanake sikuelewi. Nachojua mimi tuna serikali 2 tu nazo n serikali ya Mapinduzi ya zanzibar na Serikali ya Muungano kama ilivyoelezwa ktk katiba ya Jamhuri ya Tanzania. Nje ya hapo inabidi inefahamishe vizuri maanake yaonyesha mattatizo tunayo sisi wananchi hatujui majukumu ya shghuli za serikali zote mbili. Kikatiba hakuna mambo ya serikali ya bara hakuna ila tumeyafanya yapo. Wabara wote ni Watanzania kwa uananchi na Uraia hakuna Ubara ila ktk misemo ya kutofautisha tu sehemu hizi mbili na sii kikatiba. Kama ndivyo Mzanzibara utamweka ktk kundi gani?

Tanganyika haipo, na hakuna mfuko wa Tanganyika hivyo hakuna mambo ya Tanganyika au bara, na ndio maana tunaitaka serikali ya 3 ili nayo ishughulikie mambo ya bara. Kama Tanganyika ipo basi bila shaka pia serikali yake pia ipo! sasa mnaitaka serikali ya 3 ni ipi hiyo? na ndipo hapo tunapokwaruzana na Wazanzibar. Tunapoiomba Tanganyika iwe na serikali ina maana hatujui kuwa gharama za kuiunda hiyo serikali zitatoka wapi kwa sababu mfuko wa fedha uliopo ni wa JMT.

Hivyo basi Ili Tanganyika iwe na serikali yake inabidi tuanze upya kuchagua kiongozi wa nchi (rais ama waziri kiongozi wetu),Wabunge na madiwani wa hii nchi Tanganyika ili rais au waziri mkuu huyo aunde serikali maana ktk hao wabunge ndio tutapata viongozi wa serikali yetu kama tutafuata mfumo wa zamani yaani mawaziri watatokana na Ubunge. Baada ya hapo ndipo tutaipata serikali ya Tanganyika. Hiyo sijii itakuwa lini tukianza kufikiri leo?

Sasa swali langu linakuja hivi, ni mfuko gani utakao gharamia kuundwa kwa hiyo serikali ya Tanganyika maana Tanganyika haina mfumo wake isipokuwa tuna mfuko wa Taifa na Zanzibar wanao wa kwao. Pili ni muda gani utachukua kufanya uchaguzi wa rais (waziri kiongozi),wabunge, madiwani wa nchi hii ya Tanganyika ili tupate kuunda serikali (wizara zake) ambazo hadi sasa hazifahamiki kutokana na kuwepo na kero za Muungano. Warioba na wasomi wametoa tu maoni yao kwa idadi ya wizara hizo lakini je washiriki wameafikiana kuwa na wizara hizo ktk shughuli za Muungano na zisizo za muungano? Na kama wameafiki tuneshindwa nini kuafikiana leo ktk mfumo huu kwani pingamizi liko wapi kama sio kero zennyewe?

Tatu, kutokana na pande zote mbili kutokubaliana na mamlaka ya mambo ya Muungano na yale yasiyokuwa ya muungano, hatuwezi kuunda serikali ya Tanganyika pasipo kumaliza tatizo hilo kwanza ili tukubaliane ni mambo gani yatakuwa ya Muungano na yapi hayatakuwa ya Muungano. Hapo ni sawa kabisa na kurudi nyuma hapa hapa tulipofikia leo, jana au mwaka jana. Hoja kubwa ilotuweka hapa kwa miaka 50 ni kero za Muungano. Sidhani kama itakuwa rahisi tena kufikia muafaka ktk mambo ya Muungano na yasokuwa ya Muungano.

Ama tuchukulie tumefikia muafaka sijui kwa kupitia bunge hili la katiba au bunge ka JMT au tume nyingine, binafsi sielewi ni muda gani swala hilo pekee litachukua na wala tusiliombee. Tukisha kubaliana ktk mambo yasokuwa ya Muungano hapo ndipo Tanganyika itaweza kutunga mimba kwa kuunda kwanza bunge lake, kisha serikali yake na mahakama yake na sielewi serikali ipi itagharamia uchaguzi huo - Tanganyika haina mfuko. (mfano ule wa Nassoro Moyo na embe 3 ktk mifuko miwili) Lakini kumbe hata kama leo tukifikia muafaka ktk maswala ya kero hizi za Muungano tunaweza kupata katiba mpya inayolenga mapungufu ya Kikatiba kulingana na mazingira tuliyopo maana tumeshamaliza kero zetu.

Kinachotuweka hapa na kukwama ni kutokubaliana mamlaka na shughuli za Muuungano na zile zisokuwa za muungano basi, hakuna kitu kingine hizi habari za kujitenga, Kuomba Uhuru na mamlaka kamili, kuunda serikali 3 ni hasira na majibu ya kijeuri kwa pande zote mbili pasipo kukaa chini na kuzitazama kwanza kero zenyewe kwa sababu huko mbele tutakutana nazo tena ili kuunda serikali ya JMT.

Nitarudia kusema kuunda serikali ya Tanganyika ni mbinu tu inatumiwa na wanasiasa kutufumba macho maana ukweli upo wazi kabisa ya kwamba hatukubaliani ktk mfumo mzima wa serikali 1,2 wala 3 kutokana na kero zilizopo. Tumalize kero kwanza japo wananchi wengi hawazijui isipokuwa wanasikizia tu magazetini na mitandaoni. Kero, kero, kero zimekuwa kero!
 
Last edited by a moderator:
Nitashangaa kama kuna mtu atakuwa anashangaa kwa Rais Kikwete kutoa hotuba inayojenga kutetea muhimili wa serikali anayoiongoza na kikubwa kabisa, kutetea sera kuu ya chama chake kinachoongoza taifa. Kama kuna mtu anadhani Rais Kikwete asingetetea hoja ya serikali mbili, basi huyo hayuko kwenye uharisia wa mambo ya siasa za Tanzania.

Ninashukuru sana kwa tume ya Jaji Warioba kuja na hoja ya serikali tatu. Kama tume ya Jaji Warioba ingekuja na hoja ya serikali mbili, ninaamini tusingezisikia taasisi kuu za Tanzania na CCM zikijitahidi kutushawishi na kuelezea chanzo cha matatizo na njia zinazofanya au zinavyotaka kuzifanya katika kukabiliana na wimbi la watu wanaotaka njia nyingine mbadala za kuondoa kero za muungano.

Hoja ya kuwepo kwa serikali tatu imezitingisha taasisi kuu za Tanzania kwa maana kuwa serikali ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano bila kusahau, CCM katika kujiangalia na kufahamu mapungufu katika muungano kutokana na msukumo kutoka kwa wananchi walioitikia na kukubaliana na hoja za serikali tatu.

Ninafahamu kuwa CCM watakuja na rasimu mbadala lakini pia kutokana na kutingishwa na hoja za serikali tatu kutoka kwenye Kamati ya Jaji Warioba, lazima hiyo mbadala iwe kweli ni mbadala kutokana na political trends zinazochipuka huku zimebeba mawazo ya kukubaliana na serikali tatu. Political actions za serikali mbili na CCM kwa sasa ndizo zitakazo determine their political fate katika uwepo wa serikali mbili.

Siyo kwamba wananchi wanaotaka serikali tatu hawataki muungano, la hasha. Matatizo ya muungano ndiyo yamepelekea watu kuja na aina nyingine ya muungano wakitegemea ndiyo utakuwa mwarobaini wa matatizo ya muungano. Hii imesababishwa na matokeo ya kushindwa au kusua sua kuziondoa kero kuu za muungano kwa zaidi ya miaka 35.

Ninafahamu wale wanaotaka serikali za mkataba wana mantiki ya kuvunja muungano hasa ukiziangalia component za serikali inayoingia kwenye mkataba katika mantiki ya serikali za Tanganyika na Zanzibar.

Ngoma ya muungano iko kwa serikali za Muungano kwa sasa ambazo zinaongozwa na CCM.
 
Hizi serikali 2 kila Upande umezipata vipi maanake sikuelewi. Nachojua mimi tuna serikali 2 tu nazo n serikali ya Mapinduzi ya zanzibar na Serikali ya Muungano kama ilivyoelezwa ktk katiba ya Jamhuri ya Tanzania. Nje ya hapo inabidi inefahamishe vizuri maanake yaonyesha mattatizo tunayo sisi wananchi hatujui majukumu ya shghuli za serikali zote mbili. Kikatiba hakuna mambo ya serikali ya bara hakuna ila tumeyafanya yapo. Wabara wote ni Watanzania kwa uananchi na Uraia hakuna Ubara ila ktk misemo ya kutofautisha tu sehemu hizi mbili na sii kikatiba. Kama ndivyo Mzanzibara utamweka ktk kundi gani?

Tanganyika haipo, na hakuna mfuko wa Tanganyika hivyo hakuna mambo ya Tanganyika au bara, na ndio maana tunaitaka serikali ya 3 ili nayo ishughulikie mambo ya bara. Kama Tanganyika ipo basi bila shaka pia serikali yake pia ipo! sasa mnaitaka serikali ya 3 ni ipi hiyo? na ndipo hapo tunapokwaruzana na Wazanzibar. Tunapoiomba Tanganyika iwe na serikali ina maana hatujui kuwa gharama za kuiunda hiyo serikali zitatoka wapi kwa sababu mfuko wa fedha uliopo ni wa JMT.

Hivyo basi Ili Tanganyika iwe na serikali yake inabidi tuanze upya kuchagua kiongozi wa nchi (rais ama waziri kiongozi wetu),Wabunge na madiwani wa hii nchi Tanganyika ili rais au waziri mkuu huyo aunde serikali maana ktk hao wabunge ndio tutapata viongozi wa serikali yetu kama tutafuata mfumo wa zamani yaani mawaziri watatokana na Ubunge. Baada ya hapo ndipo tutaipata serikali ya Tanganyika. Hiyo sijii itakuwa lini tukianza kufikiri leo?

Sasa swali langu linakuja hivi, ni mfuko gani utakao gharamia kuundwa kwa hiyo serikali ya Tanganyika maana Tanganyika haina mfumo wake isipokuwa tuna mfuko wa Taifa na Zanzibar wanao wa kwao. Pili ni muda gani utachukua kufanya uchaguzi wa rais (waziri kiongozi),wabunge, madiwani wa nchi hii ya Tanganyika ili tupate kuunda serikali (wizara zake) ambazo hadi sasa hazifahamiki kutokana na kuwepo na kero za Muungano. Warioba na wasomi wametoa tu maoni yao kwa idadi ya wizara hizo lakini je washiriki wameafikiana kuwa na wizara hizo ktk shughuli za Muungano na zisizo za muungano? Na kama wameafiki tuneshindwa nini kuafikiana leo ktk mfumo huu kwani pingamizi liko wapi kama sio kero zennyewe?

Tatu, kutokana na pande zote mbili kutokubaliana na mamlaka ya mambo ya Muungano na yale yasiyokuwa ya muungano, hatuwezi kuunda serikali ya Tanganyika pasipo kumaliza tatizo hilo kwanza ili tukubaliane ni mambo gani yatakuwa ya Muungano na yapi hayatakuwa ya Muungano. Hapo ni sawa kabisa na kurudi nyuma hapa hapa tulipofikia leo, jana au mwaka jana. Hoja kubwa ilotuweka hapa kwa miaka 50 ni kero za Muungano. Sidhani kama itakuwa rahisi tena kufikia muafaka ktk mambo ya Muungano na yasokuwa ya Muungano.

Ama tuchukulie tumefikia muafaka sijui kwa kupitia bunge hili la katiba au bunge ka JMT au tume nyingine, binafsi sielewi ni muda gani swala hilo pekee litachukua na wala tusiliombee. Tukisha kubaliana ktk mambo yasokuwa ya Muungano hapo ndipo Tanganyika itaweza kutunga mimba kwa kuunda kwanza bunge lake, kisha serikali yake na mahakama yake na sielewi serikali ipi itagharamia uchaguzi huo - Tanganyika haina mfuko. (mfano ule wa Nassoro Moyo na embe 3 ktk mifuko miwili) Lakini kumbe hata kama leo tukifikia muafaka ktk maswala ya kero hizi za Muungano tunaweza kupata katiba mpya inayolenga mapungufu ya Kikatiba kulingana na mazingira tuliyopo maana tumeshamaliza kero zetu.

Kinachotuweka hapa na kukwama ni kutokubaliana mamlaka na shughuli za Muuungano na zile zisokuwa za muungano basi, hakuna kitu kingine hizi habari za kujitenga, Kuomba Uhuru na mamlaka kamili, kuunda serikali 3 ni hasira na majibu ya kijeuri kwa pande zote mbili pasipo kukaa chini na kuzitazama kwanza kero zenyewe kwa sababu huko mbele tutakutana nazo tena ili kuunda serikali ya JMT.

Nitarudia kusema kuunda serikali ya Tanganyika ni mbinu tu inatumiwa na wanasiasa kutufumba macho maana ukweli upo wazi kabisa ya kwamba hatukubaliani ktk mfumo mzima wa serikali 1,2 wala 3 kutokana na kero zilizopo. Tumalize kero kwanza japo wananchi wengi hawazijui isipokuwa wanasikizia tu magazetini na mitandaoni. Kero, kero, kero zimekuwa kero!
Mkuu, hata kama itachukua miaka 5 kubadili mfumo ni bora kuliko kuendelea na donda tulilo nalo.
Pili, kuunda serikali ya Taanganyika si jambo kubwa kama unavyodhani. Ni kiasi tu cha kuondoa mambo mawili matatu tunakuwa na serikali kwasababu kwasasa Tanzania ndiyo Tanganyika

Tatu, kila siku unaongelea mambo yasiyo ya muungano yaondolewe katika muungano.
Hujaweza kutujibu yapelekwe wapi kwasababu Tanganyika haipo
Unatushauri tuondoe mambo yasiyo ya muungano halafu tuyatupe baharini.

Nne,kila mara unaongelea kero za muungano. Hujaongelea uvunjaji wa katiba, sijui hilo unalitazama kwa ukubwa gani

Tano,kuunda serikali 3 si hasira. Tutakaa chini tuangalie nini tena Mkandara? Miaka 50 haikuwezekana leo tukae tunajadili kitu gani kipya mkuu.

Sita,tuonyeshe kero kwa pande zote, siyo kutuambia tuache kujenga mahoteli, bandari na sehemu za mikutano ili znz wafurahi. Kwako wewe kutatua kero ni kumridhisha na kumfurahisha Mzanzibar. That is a history now.
 
Nitashangaa kama kuna mtu atakuwa anashangaa kwa Rais Kikwete kutoa hotuba inayojenga kutetea muhimili wa serikali anayoiongoza na kikubwa kabisa, kutetea sera kuu ya chama chake kinachoongoza taifa. Kama kuna mtu anadhani Rais Kikwete asingetetea hoja ya serikali mbili, basi huyo hayuko kwenye uharisia wa mambo ya siasa za Tanzania.

Ninashukuru sana kwa tume ya Jaji Warioba kuja na hoja ya serikali tatu. Kama tume ya Jaji Warioba ingekuja na hoja ya serikali mbili, ninaamini tusingezisikia taasisi kuu za Tanzania na CCM zikijitahidi kutushawishi na kuelezea chanzo cha matatizo na njia zinazofanya au zinavyotaka kuzifanya katika kukabiliana na wimbi la watu wanaotaka njia nyingine mbadala za kuondoa kero za muungano.

Hoja ya kuwepo kwa serikali tatu imezitingisha taasisi kuu za Tanzania kwa maana kuwa serikali ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano bila kusahau, CCM katika kujiangalia na kufahamu mapungufu katika muungano kutokana na msukumo kutoka kwa wananchi walioitikia na kukubaliana na hoja za serikali tatu.

Ninafahamu kuwa CCM watakuja na rasimu mbadala lakini pia kutokana na kutingishwa na hoja za serikali tatu kutoka kwenye Kamati ya Jaji Warioba, lazima hiyo mbadala iwe kweli ni mbadala kutokana na political trends zinazochipuka huku zimebeba mawazo ya kukubaliana na serikali tatu. Political actions za serikali mbili na CCM kwa sasa ndizo zitakazo determine their political fate katika uwepo wa serikali mbili.

Siyo kwamba wananchi wanaotaka serikali tatu hawataki muungano, la hasha. Matatizo ya muungano ndiyo yamepelekea watu kuja na aina nyingine ya muungano wakitegemea ndiyo utakuwa mwarobaini wa matatizo ya muungano. Hii imesababishwa na matokeo ya kushindwa au kusua sua kuziondoa kero kuu za muungano kwa zaidi ya miaka 35.

Ninafahamu wale wanaotaka serikali za mkataba wana mantiki ya kuvunja muungano hasa ukiziangalia component za serikali inayoingia kwenye mkataba katika mantiki ya serikali za Tanganyika na Zanzibar.

Ngoma ya muungano iko kwa serikali za Muungano kwa sasa ambazo zinaongozwa na CCM.
Mkuu , katika suala la katiba Rais anakuwa kiongozi wa nchi anayetegemewa kuiongoza nchi. Kikwete hakutetea serikali mbili, alichokifanya ni kumdhalilisha Warioba ili kuwaondoa watu katika hoja muhimu.

Nasema hakutetea kwasababu hakuonyesha kwanini serikali 2 ni muafaka.
Kusema Nyerere na Karume walianzisha na hivyo tuendelee kama walivyofikri si utetezi ni kukariri mistari tu ya maneno ya watu.

Kumsema Warioba hana takwimu za kuridhisha yeye akiwa na vyombo vyote bila yakwimu tena kutumia maneno 'tunasikia' si uetetezi ni kumnanga mzee Warioba na wenzake.

Kasema matatizo yametafutiwa ufumbuzi na kupungua kutoka 26 hadi 6 bila kueleza yametafutiwa ufumbuzi upi na kwa upande gani.

Kuwaridhisha wznz kwa kuwapa Rasilimali za Tanganyika, kuwapa kodi za Watanganyika na kuwaacha wavunje katiba si kupunguza matatizo.

Kikwete hakupunguza matatizo kwasababu tatizo kubwa la kuvunjwa kwa katiba hakulizungumzia.
Na hata alipoponda serikali 3 hakufanya hivyo kwa mantiki yoyote bali hisia tu na ulaghai.

Ukiangalia wasomi wengie na watu wa kati wanaojielewa hawakufurahishwa na hotuba yake.
Ukimfikiria Nyerere au watangulizi wa JK magogoni unaweza kudhani JK ana ofisi eneo lingine.

Hotuba yake haikuwa na dira bali kuwananga wapianzi. Si kazi ya Rais kugombana na wana siasa, ni kazi ya Rais kulileta taifa pamoja. Kikwete kafeli sana licha ya udhaifu wake wa kila siku.

Kuhusu mkataba, hilo siafiki kwasababu hatuhitaji mkataba na zanzibar. Hakuna chochote cha maana kinachotulazimisha kuwa na mkataba na wznz. Tunaweza kuwa na MoU kati yao si mkataba.

Kuhusu Tanganyika hakuna shaka kuwa uvumilivu umefika mwisho.
Uhuni, kiburi dharau na jeuri ya wznz ni kwa kujua kuwa hakuna serikali ya Tanganyika hivyo wanaweza kufanya watakalo kama kuvunja katiba bila kukemewa.

Jana waziri wa sheria Abubakary Hamisi Bakar amesema hakuna namna wanaweza kubadili katiba yao kwasababu ime define znz na status yake.
Akasema hawakubaliana na hoja yoyote ya kurekebisha katiba iliyoopo.

Kibaya zaidi kasema Nyerere aliua Tanganyika na hilo ni jukumu la Watanganyika kuirejesha Tangayika yao.
Ikifika hapo hakuna namna, wznz hawataki muungano, kama wanataka uwe wa kiuchumi.

Kiuchumi maana yake ni wao kuwa sehemu ya muungano kwa mambo 7 tena wakichangia na si kusuburi kupewa wakiwa wamepunzika katika mabusati eti kwasaababu ni wznz.

Hilo litawezekana ikiwepo Tanganyika itakayoshughulikia mambo ya Tanganyika kwa ajili ya Watanganyika.
Yale 7 ndiyo yatatuunganisha, na kama ulivyosema hii haina maana kuvunja muungano.
 
SITTA AENDELEA NA KAZI YA KUCHAKACHUA
RASIMU YA KATIBA ILIYOANDIKWA MAFICHONI YAWASILISHWA

Jana mwenyekiti wa bunge Sitta ameeleza kuhusu kamati kupitia vifungu cha kwanza na sita na kamati husika ili 'kutengeneza' muundo wa serikali kabla ya mjadala.

Bila kujadili rasimu ya Tume ya Warioba na wabunge tayari kamati zimeshapitia namna ya muundo wa muungano.
Kamati hizo zimeundwa na wabunge wa CCM

Sitta akaeleza kuwa kamati zimepokea maoni kutoka kwa wajumbe na kuzifanyia kazi. Katika hali ya kujitetea Sitta akadai ni haki kamati hizo kupokea mawazo na maoni ya Wajumbe. Akasema eti wapo wanaosema Rasimu ya katiba ya CCM iliyoandikwa mafichoni si kweli kuwa inaingizwa katika kamati.

Kwanza tusema, kuanza kuangalia mfumo wa muundo wa muungano kabla ya rasimu kufikishwa japo kwa mjadala wa mwanzo ni kichekesho cha usanii wa Sitta na wenzake. Hivi unawezaje kujadili rasimu katika kamati kabla ya wajumbe kuanza kuipitia japo kwa haraka haraka.

Kinachofanyika katika vifungu kwanza na sita ni kamati hizo kuja na mawazo kuwa mfumo wa Warioba haufai na wao wanapendekeza mfumo wa CCM ambao ni serikali mbili. Wakifanikiwa kwa hilo kitakachofuata ni mjadala wa rasimu ya CCM na ile ya Warioba ndio itatiwa kapuni.

Katika ujanja watajifanya wamechukua maoni ya tume ya Warioba kwa mambo kama haki za wazee ili ku justify kuwa katiba ni ile ile iliyofanyiwa maboresho.

Sitta anasema wapo waliopeleka maoni katika kamati. Hiki nacho ni kituko na dalili kuwa mzee huyu amefikia mwisho wa upeo wa kufikiri. Sijui hata kama anaweza kufikiriwa kwa nafasi yoyote mbele ya safari.
Tume ilimaliza kupeleka maoni, hayo yanayopelekwa pembeni ni yapi na kwanini hayakutolewa mbele ya tume?

Huo ndio ushahidi kuwa rasimu ya CCM sasa inaingizwa. Yote hayo yakitokea, wznz waliokuwa wanalalamika kuhusu katiba iliyopo wapo kimya, ndio wenyeviti wa kamati. Hata CUF ya Hamad Rashid nayo ipo kimya ikihalalisha uhalifu.

Mzee Sitta hana sababu za kutafuta kusema uongo au kuudanganya umma. Kwa umri wa miaka 71 jambo kubwa analopaswa kulifanyia taifa hili ni ukweli na busara. Huko sitta hayupo yupo katika kuongoza mbinu chafu za CCM katika mambo ya kitaifa.

Katika mchakato huu kama kuna mtu wa kulaumiwa leo na vizazi vijavyo si yule alishika shoka, bali mpini unaotumiwa na shoja kukata mti, ambaye ni Samwel Sitta.

Mkumbuke Sitta alishatoa kauli za kuwashughulikiwa watakaohoji muungano, akaapa kuulinda muungano kwa nguvu zake zote. Kazi hiyo anaitekeleza kwa bidii baada ya ile ya kwanza ya kuwadhalilisha akina Warioba kukamilika.a

Watacheza a kila aina ya mbinu lakini siku moja tutawauliza ilikuwaje. Tutawauliza wakiwa na bakora zao mikononi.

 
Jitihada zainaendelea ili kuandika katiba ya CCM
Maswali yanazidi kuongezeka
1. Mbunge V.Nyerere anauliza kama maoni ya serikali 3 si ya wengi kwanini serikali ina haha kuzuia suala hilo kabla hata rasimu haijapigiwa kura?
3. Mwingine amehoji kama sample size ya Warioba ni ndogo, wale 600 Dodoma ni sample size kubwa kwa milioni 43?
 
Sasa ni rasmi kwamba katiba haitatokana na wananchi. Inasikitisha sana jinsi gani makada wa ccm na wafuasi wao bungeni wanavyoisigina rasimu ya katiba na kumwandama warioba bila ya kujua kwamba wanawakejeli wananchi. Lakini tujiulize - tangia lini katiba ya nchi imewahi kutokana na wananchi? Katiba iliyopo (ya 1977) ililetwa kama muswada bungeni asubuhi, ikajadiliwa na wachangiaji watatu, na kabla ya saa kumi na moja jioni, ikapitishwa na wabunge wa ccm. Haya ni maneno ya shivji in Let the people speak:Tanzania down the road to neoliberalism (2005). Shivji anazidi kusema kwamba bunge lile la jamhuri (1977) ambalo liligeuzwa kuwa bunge la katiba, zaidi ya nusu ya wajumbe wake walitokana na uteuzi wa moja kwa moja wa rais, chini ya nusu ya wajumbe ndio walitokana na wabunge waliopigiwa kura na wananchi majimboni.

Licha ya haya, kwa muda mrefu sana serikali ya ccm ilipinga hoja ya katiba mpya kwa madai mengi yasiyo na mashiko ya hoja (tutayajadili baadae ili tubaini siri na mkakati wa ccm ambao haujabadika). Kwahivyo basi, ccm haina utamaduni wa kusikiliza wananchi, hivyo tusishangae mchakato huu ukafuata mkondo huo huo. Swali linalofuate ni je:

*ili kupata katiba iayokidhi matakwa ya wananchi, nini kifanyike?
-Wananchi waanze wenyewe kudai katiba yao? Au kazi hiyo ifanywe na Vyama vya upinzani kwa niaba yao? Nini nafasi ya tume katika hili?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Sasa ni rasmi kwamba katiba haitatokana na wananchi. Inasikitisha sana jinsi gani makada wa ccm na wafuasi wao bungeni wanavyoisigina rasimu ya katiba na kumwandama warioba bila ya kujua kwamba wanawakejeli wananchi. Lakini tujiulize - tangia lini katiba ya nchi imewahi kutokana na wananchi? Katiba iliyopo (ya 1977) ililetwa kama muswada bungeni asubuhi, ikajadiliwa na wachangiaji watatu, na kabla ya saa kumi na moja jioni, ikapitishwa na wabunge wa ccm. Haya ni maneno ya shivji in Let the people speak:Tanzania down the road to neoliberalism (2005). Shivji anazidi kusema kwamba bunge lile la jamhuri (1977) ambalo liligeuzwa kuwa bunge la katiba, zaidi ya nusu ya wajumbe wake walitokana na uteuzi wa moja kwa moja wa rais, chini ya nusu ya wajumbe ndio walitokana na wabunge waliopigiwa kura na wananchi majimboni.

Licha ya haya, kwa muda mrefu sana serikali ya ccm ilipinga hoja ya katiba mpya kwa madai mengi yasiyo na mashiko ya hoja (tutayajadili baadae ili tubaini siri na mkakati wa ccm ambao haujabadika). Kwahivyo basi, ccm haina utamaduni wa kusikiliza wananchi, hivyo tusishangae mchakato huu ukafuata mkondo huo huo. Swali linalofuate ni je:

*ili kupata katiba iayokidhi matakwa ya wananchi, nini kifanyike?
-Wananchi waanze wenyewe kudai katiba yao? Au kazi hiyo ifanywe na Vyama vya upinzani kwa niaba yao? Nini nafasi ya tume katika hili?
Mkuu , katiba haitatokana na wanachi. Historia inaonyesha CCM ndivyo wanavyotaka na ndivyo wamefanya miaka mingi sana.

CCM imeunda tume zake yenyewe zaidi ya 8, hakuna iliyokuja na jibu la tatizo. Makundi kama G55 na watu kama Jumbe wamejaribu na kuzuiwa. Hata hivyo Zimwi la katiba lipo mtaani na linaibuka kila mara ngoma za zikipigwa.

Hili ni tatizo kubwa sana ambalo CCM inaliandaa kwa taifa hili.
1. Kutakuwa hakuna maridhiano, na hadi sasa suala la muungano limewatenga wananchi.

2. Muungano utavunjika kwa wananchi kuelewa kuwa CCM haiwezi na ndio kikwazo.
Zitatumika short cut, Kwa mfano, huko znz ambako ukisoma mazingira tu utaona uwezekano wa kukamilisha uvunjaji wa muungano sasa ni asilimia zote, walishaanza 2010 na wameapa kutobadili katiba yao!

Huku bara kutatokea chuki kubwa sana dhidi ya wznz kwasababu ya uzanzibar na ubaguzi wa kizanzibar.
Bara kutakuwa na kuhoji mzigo wa muungano mwisho wa kuubeba ni lini.

Hayo yote yata trigger short cut na muungano utakufa. Kabla ya JK hajaondoka kuna uwezekano wa hayo kutokea
a) Vurugu kubwa sana na watu kupoteza maisha. Yale ya 2001 yaliyoharibu image ya nchi yatajirudia tu, matter of time
b) Wananchi kuamua kwenda solo bila kutegemea political process na hapo muungano unafikia kikomo.

Muungano ni maridhiano na hakuna ndoa inayolindwa kwa bunduki au mabomu ya machozi?
Udanganyifu wa CCM una kikomo, hata sasa wnaapohamia makanisani ni dalili za kuishiwa hoja.

Lini nguvu ya umma iliwahi kushindwa?
Hii inajibu hoja kuwa, wananchi wachukue ownership ya suala la muungano na katiba.
Ikishindikana political process basi nguvu ya umma inachukua nafasi.
 
Sasa ni rasmi kwamba katiba haitatokana na wananchi. Inasikitisha sana jinsi gani makada wa ccm na wafuasi wao bungeni wanavyoisigina rasimu ya katiba na kumwandama warioba bila ya kujua kwamba wanawakejeli wananchi. Lakini tujiulize - tangia lini katiba ya nchi imewahi kutokana na wananchi? Katiba iliyopo (ya 1977) ililetwa kama muswada bungeni asubuhi, ikajadiliwa na wachangiaji watatu, na kabla ya saa kumi na moja jioni, ikapitishwa na wabunge wa ccm. Haya ni maneno ya shivji in Let the people speak:Tanzania down the road to neoliberalism (2005). Shivji anazidi kusema kwamba bunge lile la jamhuri (1977) ambalo liligeuzwa kuwa bunge la katiba, zaidi ya nusu ya wajumbe wake walitokana na uteuzi wa moja kwa moja wa rais, chini ya nusu ya wajumbe ndio walitokana na wabunge waliopigiwa kura na wananchi majimboni.

Licha ya haya, kwa muda mrefu sana serikali ya ccm ilipinga hoja ya katiba mpya kwa madai mengi yasiyo na mashiko ya hoja (tutayajadili baadae ili tubaini siri na mkakati wa ccm ambao haujabadika). Kwahivyo basi, ccm haina utamaduni wa kusikiliza wananchi, hivyo tusishangae mchakato huu ukafuata mkondo huo huo. Swali linalofuate ni je:

*ili kupata katiba iayokidhi matakwa ya wananchi, nini kifanyike?
-Wananchi waanze wenyewe kudai katiba yao? Au kazi hiyo ifanywe na Vyama vya upinzani kwa niaba yao? Nini nafasi ya tume katika hili?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

haya yanayotokea nitashangazwa sana na viongozi wa upinzani wakijifanya hawakuyatarajia, huu mziki wanaucheza wa kikwete na timu yake, wanategemea wao ndio wachague spidi ya marimba?au uzito wa besi?

katiba ya wananchi Tanzania bado sana, ukweli mchungu ni kuwa Wananchi wa Tanzania hawajaidai kikamilifu katiba yao, ndio maana hadi sasa mambo makuu yaliyozungumzwa ni jinsi gani maslahi ya wachache yatatunzwa, kuanzia issue ya serikali 2,3 hadi kura za siri na wazi.

Wananchi wa Tanzania ukiwauliza hii katiba itabadilisha nini kwenye mtazamo na kwenye maisha yao ya miaka 50 mbele, si ajabu watakumbuka vioja na self promotions zinazoendelea DODOMA.

Hakuna nayemfikira mwananchi, kila mmoja yuko busy kuona maslahi yake yatashinda kwa kiasi gani, And CCM is the only winner here.
 
Tanzania kama ilivyo system yote ya utawala, hawako siriasi na jambo lolote. Kazi ni kupiga domo halafu wanaacha upepo utapita tu, au wanasubiri mfadhili awasaidie. Katiba mpya hakuna, ila tunaweza kupata katiba viraka.

Hongera zaao majirani zetu wa Kenya ambao hawakuwa na utani kwenye swala la Katiba. Hata kama katiba yao mpya ina mapungufu, hawakuiandaa kiushabikishabiki na kiubabebubabe kama siye; iliandaliwa kitaalamu kabisa. Utaratibu wa fanya hivi ama sivyo hupati posho, yaani kununua matakwa ya mtu kwa kutumia posho ambayo ni pesa ya walipa kodi, siuoni kama una mantiki yoyote. Sijapata kuuona duniani kote. Hata Marekani ambako waliwahi kuwa na government shutdown huwa hawawatishi wabunge kwa kutumia poshoi! Ninasubiri nione itakuwaje Tanzania.

Kwa utaratibu huu itabidi Tanzania tuwe pia tunaedit michango ya wabunge halafu malipo ya posho zao yaendane na michango yao bungeni. Mbunge anayelala au ambaye kazi yake ni kupongeza bila kuchangia chochote bungeni naye asilipwe posho. Posho ya wabunge iendani na productivity yake; kuanzia sasa. na ningependa jambo hilo liwe ndani ya katiba mpya.
 
haya yanayotokea nitashangazwa sana na viongozi wa upinzani wakijifanya hawakuyatarajia, huu mziki wanaucheza wa kikwete na timu yake, wanategemea wao ndio wachague spidi ya marimba?au uzito wa besi?

katiba ya wananchi Tanzania bado sana, ukweli mchungu ni kuwa Wananchi wa Tanzania hawajaidai kikamilifu katiba yao, ndio maana hadi sasa mambo makuu yaliyozungumzwa ni jinsi gani maslahi ya wachache yatatunzwa, kuanzia issue ya serikali 2,3 hadi kura za siri na wazi.

Wananchi wa Tanzania ukiwauliza hii katiba itabadilisha nini kwenye mtazamo na kwenye maisha yao ya miaka 50 mbele, si ajabu watakumbuka vioja na self promotions zinazoendelea DODOMA.

Hakuna nayemfikira mwananchi, kila mmoja yuko busy kuona maslahi yake yatashinda kwa kiasi gani, And CCM is the only winner here.
Nitashangaa kama kuna mtu mwenye upeo mpana alidhani kama Mchakato wa Katiba kwa jinsi ulivyoanza ungekuwa ni "mteremko".

Kwanza ieleweke kuwa Mchakato wa Katiba ulikuwa unarithi Muungano wenye utata kuanzia siku ambayo viongozi wetu waliamua kuungana na kuziunganisha nchi. Hadidu za rejea zilikuwa zimeifunga tume ya Jaji Warioba ndani ya Muungano ambao una utata kuanzia mwanzo.

Pili, Kuandika Katiba inayohusisha nchi mbili ambazo zina tofauti kubwa sana kiuchumi, kisiasa na kijamii kwanza ni kazi ngumu. Inakuwa ni kazi ngumu zaidi kama kunakosekana pia political legitimacy.

Kuna watu mpaka wameanza kulinganisha Mchakato wa Katiba ya Kenya na Tanzania huku wakisahau kuwa Katiba ya Kenya ilihusisha nchi moja wakati ya kwetu inahusisha nchi mbili zenye muungano wenye maswali mengi zaidi ya majibu.

Kiuhalisia, walioshinikiza mpaka serikali kuridhia Mchakato wa Katiba siyo wananchi kama baadhi ya wanasiasa wanavyotaka kutuaminisha. Walioshinikiza mchakato wa Katiba ni wanasiasa kwa maslahi yao ya kisiasa, ndiyo maana hata njia ya kuwahusisha wananchi haikuwa kama inavyopaswa kama wananchi ndiyo wameshinikiza Mchakato wa Katiba.

Ifahamike kuwa, wananchi wanaposhikiza Mchakato wa Katiba, lazima kwanza Mchakato upewe baraka za political legitimacy kwa njia ya kura ya maoni. Ninaamini kama wananchi wangekuwa wameshinikiza mchakato wa Katiba wanayoitaka, basi tungekuwa tumepiga kura ya maoni kwanza kuundoa mchakato wa Katiba mikononi mwa wanasiasa ambapo wananchi wangejenga msingi wa dira ya taifa/mataifa yao kwanza kabla ya maoni mengine kuanza kukusanywa. Kwa sasa katika Mchakato huu kinachofanyika ni kinyume nyume!.

Kwa sasa utaona kuwa hata idadi ya wananchi waliojihusisha na zoezi hili ni ndogo sana ukilinganisha na idadi ya Watanzania. Kibaya zaidi ninaamini kuna wananchi kwa mamilioni hawafahamu hata connection ya maisha yao na katiba achilia mbali Muungano. Sishangai pale ninaposikia baadhi ya Wabunge wa Bunge Maalum wanaposema na kupaza sauti kuwa muundo wa Muungano hauna connection yoyote na maisha ya wananchi wengi nchini. Kwamba eti wananchi wanachotaka ni huduma za jamii kama maji, shule nzuri na hospitali zenye madawa na madaktali wazuri. This is nonsense!.

Wabunge kama hawa ndiyo tunategemea wataweza kutuletea Katiba tuipigie kura. My foot.

My motto is One Government.

Sijasikia au kusoma hoja mbadala inayoweza kuufanya Muungano uimarike katika serikali mbili au serikali tatu katika hoja zinazotolewa kwa sasa. Kwa hoja za sasa, zinadhihirisha kuwa Muungano utavunjika tu bila kujali kama ni serikli mbili au tatu. Mantiki ya majadiliano katika serikali mbili na tatu siyo nyimgine bali muda utakaochukua mpaka Muungano uvunjike kwa sababu msingi wa mchakato ni matakwa ya wanasiasa.
 
Back
Top Bottom