Duru za Siasa: Kuelekea bunge la katiba,Je, katiba itatokana na wananchi?

Duru za Siasa: Kuelekea bunge la katiba,Je, katiba itatokana na wananchi?

Sehemu ya IV

Wapinzani na wale waisokubaliana na mfumo wa sasa kwa idadi yao ni ngumu kupata 2/3 ya kuunga au kukataa mapendekezo. Nafasi waliyo nayo ni katika yafuatayo
1. Waungane kwa pamoja na liswepo kundi litakalounga mkono 'katiba ya mafichoni ya CCM'
2. Wasikubali majadiliano na serikali nje ya ukumbi wa bunge kuepuka kulaghaiwa tena
3. Watumie makundi machache yaliyobaki kuwavuta kwa hoja
4. Watumie ushawishi wa baadhi ya wanaCCM wanaoona lipo tatizo linalohitaji utaifa
5. Kuhakikisha maamuzi yanakuwa kwa kura za siri

Ufafanuzi;
-Kupoteza mpinzani hata mmoja ni pigo kwao kwasababu idadi yao inahitaji zaidi na si kupoteza

-Penye ugumu na rais atawaita kwa ahadi kama za siku za nyuma, wakiondoka mambo yanafanyika kinyume. Walikubaliana kutosainiwa mkataba, walipoondoka rais akasaini tena baada ya kusitisha maandamano. Hakuna ushahidi makubaliano na serikali yamewahi kufanyiwa kazi.
Kukubaliana na JK halafu kwenda kupingana na Lukuvi au Wasira ni kuamini kuwa JK na mawaziri wake ni vitu tofauti. Wakati huu lazima majadiliano yawe ya wazi na si juu ya glasi za juisi za maembe.

-Katika makundi yaliyopendekezwa yapo machache yanayoweza kuungana nao.
Wapinzani watumie fursa hiyo kuyavuta kwa hoja.
Mfano, waeleze ni kwanini serikali 3 zitapunguza gharama kwa takwimu.

Wahoji, ni kipi ambacho CCM haijakifanya kwa miaka 50 ambacho inataraji kufanya kuondoa kero.
Waoyeshe ni jinsi gani muungano ulivyotegemezi na matarajio ya siku za usoni
Na waonyeshe kwa namba na takwimu faida za serikali 3 ukilinganisha na 2.


-Ndani ya CCM si wote wanounga mkono serikali 2. Wapo wazee wenye ushawshi na uzoefu wanaoelewa matatizo ya muungano na kwamba imeshindikana hadi mbadala upatikane.
Mfano, viongozi hao wameachwa makusudi ili kutotibua dili linalopangwa nyuma ya pazia na rais na CCM.

Tunafahamu msimamo wa Warioba kupitia tume ni serikali 3.
Msimamo wa Malecela kupitia G55 ni serikali 3
Msimamo wa Msuya ni serikali 2 na msimamo wa Sumaye ni serikali 3.
Msimamo wa EL ni serikali 2 kupitia 'katiba ya mafichoni'

Viongozi hawa wana ushawishi wa makundi na viongozi wenzao kupitia uzoefu wao.
Japo wapo nje ya bunge (Kwasababu tu ya JK kutoona umuhimu wa utaifa) wapinzani wanaweza kuungwa mkono kupitia hao. Si rahisi lakini inaweza kusaidia kukabiliana na wingU zito la 'katiba ya CCM'

-CCM wanajipanga kumpata Spika atakayeendesha mambo kwa utaratibu 'wao'.
Katika kuhakikisha kila mmoja anakuwa na uhuru wa kuamua anachokiona ni sahihi bila kufungwa na minyororo ya chama maamuzi yawe kwa njia ya kura na si 'ndiyo' au hapana.
Kinyume chake mazingaombwe tunayoyaona bunge la JMT yataendelea.

Lakini pia kuwepo na utaratibu wa kuzungumza utakaotoa nafasi kwa pande muhimu za mjadiliano vinginevyo kutakuwa na kuchaguana kwa mpangilio ili kukidhi haja iliyokusudiwa ambayo sasa tunaiona ikiwa na mkono wa mwenyekiti wa CCM.

Kuna mwenzetu kaniuliza na bila shaka hataki kutambulika au kutambulishwa.
Swali ni, kwanini mjadala unahusu sana muungano? Je, katiba ni muungano tu bila mambo mengine?

Jibu ni kuwa makosa aliyofanya JK ya kuandika katiba bila kupata ridhaa na dira ya taifa ndiyo yanayotufikisha hapa. Ukifungua rasimu kuanzia kifungu cha kwanza hadi cha miwsho hutaweza kuvijadili hadi utakapokuwa na uhakika unajadili nini.

Kwa mfano, kifungu cha kwanza kabisa kinasema katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Swali linakuja, kuna ushahidi gani kuwa wananchi waliulizwa na kukubali muungano hadi neno hilo litumike.

Bunge la katiba litafanya makosa ya JK kama wakianza kujadili vifungu vya katiba kwanza.
Utajadili vipi vifungu bila kujua structure ya serikali unayokusudia?
Kuna kifungu gani ambacho hakigusi serikali. Na je, serikali inayoguswa ni ipi.
Haya ni marudio ya mambo tuliyojadili wiki 4 zilizopita.

Hali iliyopo Dodoma inaashiria kutokuwepo kwa muafaka wa kitaifa.
Mtu wa kubeba lawama hizo ni Rais, kila jambo lilikuwa wazi kuanzia mwanzo. Maonyo yalitolewa kuhusu utaifa na si uchama.

Rais badala ya kuangalia utaifa amekjikita katika uchama.
Jana kaita kamati kuu ikaja na msimamo wa kushindilia kuhusu kura za wazi.
Ni kwanini CCM imekwama eneo hilo? Tujadili.

Huko nyuma tumeeleza dhana ya rais kuteka mchakato ilikuwa kudhibiti maoni ya wananchi kwa kutumia tume ya Warioba.

Kwa bahti nzuri na mbaya kutegemea upande uliopo tume imefanya kazi kutokana na matakwa ya wananchi. Hapo serikali ikakwama.

Njia ya pili ilikuwa kutumbukiza maoni kupitia mabaraza, nako imekwama.
Njia ya tatu ilikuwa rasimu mbadala nayo imeshatunguliwa kabla haijawasilishwa.
Njia ya nne ilikuwa kujaza wabunge wengi wa CCM kwa makundi yasiyo na maana kwa mfano wa malengo yanayofanana.
Kuchagua makada wa CCM kwa vigezo vya makundi. Nako wamekwama

Njia ya tano ni hii ya kura ya wazi inayowagawa wajumbe.

Kwanini CCM ina haha?
Jibu ni kuwa ndani ya CCM wapo wabunge walio tayari kusimamia masilahi ya nchi.Wapo waliochoshwa na ubabaishaji wa akina Nape na hao wapo tayari kusimama na kuitetea nchi yao dhidi ya uhuni uliokithiri wa CCM.

Ili kuwafunga mikono na midomo CCM inataka kura ya wazi kama kigezo cha kuwatambua. Wamekuja na njia ya kusema watakaokiuka maagizo wataanyang'anywa kadi.

Katika mchezo huo mchafu CCM wamemrubuni mwenyekiti wa BMLK aingie katika vikao vyao akijua wazi hapaswi kuchukua upande.

Huko alikwenda kupewa maagizo ya nini kifanyike ili katiba wanayoitaka CCM itimie. Ndivyo watakavyofanya kama wakifananikiwa kuvuka vikwazo, kwamba wanataka maoni yao na si ya wananchi.

Kuna mambo mawili yaliyopo mbele.
Bunge kuvunjika kabla ya wakati na bila muafaka. Hali ilipofikia inaweza kuwafikisha wabunge wa CCM wenye uzalendo kusema liwalo na liwe nchi kwanza CCM baadaye. Hapo CCM itaanza safari ya kulekea kule UNIP na KANU walipo.

Au, CCM watafanikiwa kufanikisha mambo yao kwa njia za hila.
Haitachukua muda suala la Tanganyika litarudi upya kwa kupitia wabunge wa kama ilivyokuwa kwa G55 na safari hii kwa nguvu zote tena wajumbe wakiwa wengi zaidi.

Tatu, kuna uwezekano wajumbe wa znz wakaamua kuondoka na kuwaacha wachache. Hadi sasa CCM znz ndiyo imegawanyika kuliko bara na hakuna namna ya kuziba ufa uliopo. Hilo likitokea basi muungano utakuwa umehitimishwa haraka sana.

Kwa hali yoyote iwavyo hadi sasa CCM wana wakati mgumu kwa wakati huu na siku za mbeleni.

Ni dhahiri kukwama kwa bunge ni matokeo ya CCM kushinikiza hoja zao na si za wananchi. Hapa maana yake ni kuwa wapinzani na wale wasio na makundi wanazidi kuungwa mkono na wananchi.
CCM wanaweza kutoliona hili mapema lakini mbele ya safari linagharama kubwa.

Njia ya kura ya wazi nayo pia ni mwiba siku zaijazo.
Wanachokifanya ni kuwa expose wabunge kinyume na matakwa yao.

Wananchi wataona nani alikuwa upande wa CCM bila kujali nini ilikuwa dhamira yake.Adhabu itatolewa si kwa CCM bali kwa mbunge binafsi kutokana na kura yake kwa maana kuwa alishiriki uhuni wa CCM.

Adhabu hizo zitawanufaisha sana wapinzani kama watajipanga. Ni silaha nzuri mbele ya safari ya kuwaelezea wagombea wa CCM kama wasaliti wa umma.

Vyovyote iwavyo CCM ipo katika wakati mgumu sana na kifo chake kinaweza kutokea mikononi mwa JK.

Inaweza isiwe kifo cha kupelekwa kaburini lakini kifo cha CCM kupelekwa nyumba ya kuhifadhi wafu kinaonekana dhahiri kama KANUna UNIP

Watatumia ubabe lakini itakula kwao. Hadi sasa ni CCM dhidi ya wananchi na sijui lini nguvu ya umma iliwahi kushindwa na dola au chama cha siasa.
Labda CCM watakuwa wa kwanza kutudhihirishia hilo!

Tusemezane

 
Sehemu ya IV

Wapinzani na wale waisokubaliana na mfumo wa sasa kwa idadi yao ni ngumu kupata 2/3 ya kuunga au kukataa mapendekezo. Nafasi waliyo nayo ni katika yafuatayo
1. Waungane kwa pamoja na liswepo kundi litakalounga mkono 'katiba ya mafichoni ya CCM'
2. Wasikubali majadiliano na serikali nje ya ukumbi wa bunge kuepuka kulaghaiwa tena
3. Watumie makundi machache yaliyobaki kuwavuta kwa hoja
4. Watumie ushawishi wa baadhi ya wanaCCM wanaoona lipo tatizo linalohitaji utaifa
5. Kuhakikisha maamuzi yanakuwa kwa kura za siri

Ufafanuzi;
-Kupoteza mpinzani hata mmoja ni pigo kwao kwasababu idadi yao inahitaji zaidi na si kupoteza

-Penye ugumu na rais atawaita kwa ahadi kama za siku za nyuma, wakiondoka mambo yanafanyika kinyume. Walikubaliana kutosainiwa mkataba, walipoondoka rais akasaini tena baada ya kusitisha maandamano. Hakuna ushahidi makubaliano na serikali yamewahi kufanyiwa kazi.
Kukubaliana na JK halafu kwenda kupingana na Lukuvi au Wasira ni kuamini kuwa JK na mawaziri wake ni vitu tofauti. Wakati huu lazima majadiliano yawe ya wazi na si juu ya glasi za juisi za maembe.

-Katika makundi yaliyopendekezwa yapo machache yanayoweza kuungana nao.
Wapinzani watumie fursa hiyo kuyavuta kwa hoja.
Mfano, waeleze ni kwanini serikali 3 zitapunguza gharama kwa takwimu.

Wahoji, ni kipi ambacho CCM haijakifanya kwa miaka 50 ambacho inataraji kufanya kuondoa kero.
Waoyeshe ni jinsi gani muungano ulivyotegemezi na matarajio ya siku za usoni
Na waonyeshe kwa namba na takwimu faida za serikali 3 ukilinganisha na 2.


-Ndani ya CCM si wote wanounga mkono serikali 2. Wapo wazee wenye ushawshi na uzoefu wanaoelewa matatizo ya muungano na kwamba imeshindikana hadi mbadala upatikane.
Mfano, viongozi hao wameachwa makusudi ili kutotibua dili linalopangwa nyuma ya pazia na rais na CCM.

Tunafahamu msimamo wa Warioba kupitia tume ni serikali 3.
Msimamo wa Malecela kupitia G55 ni serikali 3
Msimamo wa Msuya ni serikali 2 na msimamo wa Sumaye ni serikali 3.
Msimamo wa EL ni serikali 2 kupitia 'katiba ya mafichoni'

Viongozi hawa wana ushawishi wa makundi na viongozi wenzao kupitia uzoefu wao.
Japo wapo nje ya bunge (Kwasababu tu ya JK kutoona umuhimu wa utaifa) wapinzani wanaweza kuungwa mkono kupitia hao. Si rahisi lakini inaweza kusaidia kukabiliana na wingU zito la 'katiba ya CCM'

-CCM wanajipanga kumpata Spika atakayeendesha mambo kwa utaratibu 'wao'.
Katika kuhakikisha kila mmoja anakuwa na uhuru wa kuamua anachokiona ni sahihi bila kufungwa na minyororo ya chama maamuzi yawe kwa njia ya kura na si 'ndiyo' au hapana.
Kinyume chake mazingaombwe tunayoyaona bunge la JMT yataendelea.

Lakini pia kuwepo na utaratibu wa kuzungumza utakaotoa nafasi kwa pande muhimu za mjadiliano vinginevyo kutakuwa na kuchaguana kwa mpangilio ili kukidhi haja iliyokusudiwa ambayo sasa tunaiona ikiwa na mkono wa mwenyekiti wa CCM.

Kuna mwenzetu kaniuliza na bila shaka hataki kutambulika au kutambulishwa.
Swali ni, kwanini mjadala unahusu sana muungano? Je, katiba ni muungano tu bila mambo mengine?

Jibu ni kuwa makosa aliyofanya JK ya kuandika katiba bila kupata ridhaa na dira ya taifa ndiyo yanayotufikisha hapa. Ukifungua rasimu kuanzia kifungu cha kwanza hadi cha miwsho hutaweza kuvijadili hadi utakapokuwa na uhakika unajadili nini.

Kwa mfano, kifungu cha kwanza kabisa kinasema katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Swali linakuja, kuna ushahidi gani kuwa wananchi waliulizwa na kukubali muungano hadi neno hilo litumike.

Bunge la katiba litafanya makosa ya JK kama wakianza kujadili vifungu vya katiba kwanza.
Utajadili vipi vifungu bila kujua structure ya serikali unayokusudia?
Kuna kifungu gani ambacho hakigusi serikali. Na je, serikali inayoguswa ni ipi.
Haya ni marudio ya mambo tuliyojadili wiki 4 zilizopita.

Hali iliyopo Dodoma inaashiria kutokuwepo kwa muafaka wa kitaifa.
Mtu wa kubeba lawama hizo ni Rais, kila jambo lilikuwa wazi kuanzia mwanzo. Maonyo yalitolewa kuhusu utaifa na si uchama.

Rais badala ya kuangalia utaifa amekjikita katika uchama.
Jana kaita kamati kuu ikaja na msimamo wa kushindilia kuhusu kura za wazi.
Ni kwanini CCM imekwama eneo hilo? Tujadili.

Huko nyuma tumeeleza dhana ya rais kuteka mchakato ilikuwa kudhibiti maoni ya wananchi kwa kutumia tume ya Warioba.

Kwa bahti nzuri na mbaya kutegemea upande uliopo tume imefanya kazi kutokana na matakwa ya wananchi. Hapo serikali ikakwama.

Njia ya pili ilikuwa kutumbukiza maoni kupitia mabaraza, nako imekwama.
Njia ya tatu ilikuwa rasimu mbadala nayo imeshatunguliwa kabla haijawasilishwa.
Njia ya nne ilikuwa kujaza wabunge wengi wa CCM kwa makundi yasiyo na maana kwa mfano wa malengo yanayofanana.
Kuchagua makada wa CCM kwa vigezo vya makundi. Nako wamekwama

Njia ya tano ni hii ya kura ya wazi inayowagawa wajumbe.

Kwanini CCM ina haha?
Jibu ni kuwa ndani ya CCM wapo wabunge walio tayari kusimamia masilahi ya nchi.Wapo waliochoshwa na ubabaishaji wa akina Nape na hao wapo tayari kusimama na kuitetea nchi yao dhidi ya uhuni uliokithiri wa CCM.

Ili kuwafunga mikono na midomo CCM inataka kura ya wazi kama kigezo cha kuwatambua. Wamekuja na njia ya kusema watakaokiuka maagizo wataanyang'anywa kadi.

Katika mchezo huo mchafu CCM wamemrubuni mwenyekiti wa BMLK aingie katika vikao vyao akijua wazi hapaswi kuchukua upande.

Huko alikwenda kupewa maagizo ya nini kifanyike ili katiba wanayoitaka CCM itimie. Ndivyo watakavyofanya kama wakifananikiwa kuvuka vikwazo, kwamba wanataka maoni yao na si ya wananchi.

Kuna mambo mawili yaliyopo mbele.
Bunge kuvunjika kabla ya wakati na bila muafaka. Hali ilipofikia inaweza kuwafikisha wabunge wa CCM wenye uzalendo kusema liwalo na liwe nchi kwanza CCM baadaye. Hapo CCM itaanza safari ya kulekea kule UNIP na KANU walipo.

Au, CCM watafanikiwa kufanikisha mambo yao kwa njia za hila.
Haitachukua muda suala la Tanganyika litarudi upya kwa kupitia wabunge wa kama ilivyokuwa kwa G55 na safari hii kwa nguvu zote tena wajumbe wakiwa wengi zaidi.

Tatu, kuna uwezekano wajumbe wa znz wakaamua kuondoka na kuwaacha wachache. Hadi sasa CCM znz ndiyo imegawanyika kuliko bara na hakuna namna ya kuziba ufa uliopo. Hilo likitokea basi muungano utakuwa umehitimishwa haraka sana.

Kwa hali yoyote iwavyo hadi sasa CCM wana wakati mgumu kwa wakati huu na siku za mbeleni.

Ni dhahiri kukwama kwa bunge ni matokeo ya CCM kushinikiza hoja zao na si za wananchi. Hapa maana yake ni kuwa wapinzani na wale wasio na makundi wanazidi kuungwa mkono na wananchi.
CCM wanaweza kutoliona hili mapema lakini mbele ya safari linagharama kubwa.

Njia ya kura ya wazi nayo pia ni mwiba siku zaijazo.
Wanachokifanya ni kuwa expose wabunge kinyume na matakwa yao.

Wananchi wataona nani alikuwa upande wa CCM bila kujali nini ilikuwa dhamira yake.Adhabu itatolewa si kwa CCM bali kwa mbunge binafsi kutokana na kura yake kwa maana kuwa alishiriki uhuni wa CCM.

Adhabu hizo zitawanufaisha sana wapinzani kama watajipanga. Ni silaha nzuri mbele ya safari ya kuwaelezea wagombea wa CCM kama wasaliti wa umma.

Vyovyote iwavyo CCM ipo katika wakati mgumu sana na kifo chake kinaweza kutokea mikononi mwa JK.

Inaweza isiwe kifo cha kupelekwa kaburini lakini kifo cha CCM kupelekwa nyumba ya kuhifadhi wafu kinaonekana dhahiri kama KANUna UNIP

Watatumia ubabe lakini itakula kwao. Hadi sasa ni CCM dhidi ya wananchi na sijui lini nguvu ya umma iliwahi kushindwa na dola au chama cha siasa.
Labda CCM watakuwa wa kwanza kutudhihirishia hilo!

Tusemezane

 
WAPINZANI WA CCM WAMEINGIA MKENGE
WAMEUZA SILAHA KAMA WALIVYOUZA WAKATI WA KUANZISHWA MCHAKATO

Kwa wiki 3 suala la kura za siri na wazi la vifungu 37 na 38 limekwama.
CCM wanamsimamo wa kura ya wazi kudhibiti wanachama wao ili kulinda muungano wa serikali 2 wenye masilahi kwao na si kwa nchi.

Wapinzani wanataka kura 3 ili kuwa huru kwa kila wajumbe wakitegeme kuvuna baadhi ya CCM wasiokubaliana na chama chao.

Imekubaliwa vifungu hivyo viachwe ili bunge lizunduliwe na rais halafu muafaka utafutwe.
Wapinzani wamekubaliana na kama alivyosema Mbatia nchi kwanza na makundi baadaye

Ukiacha Mtikila na Mkosamali, wengine wameafiki wakitumaini kupata muafaka baada ya uchaguzi wa mwenyekiti.

Uchaguzi wa mwenyekiti, ni wazi utatoa mtu wa CCM ambao walikuwa na kikao cha kamati kuu na kusisitiza msimamo wa kura ya wazi. CCM haikuona umuhimu wa nchi kwanza kama Mbatia alivyosema hivyo ni ujinga kudhani kuwa wana nia njema na nchi.

Malalamiko ya Mtikila na Mkosamali yalihusu kutopewa nafasi za kuzungumza. Hilo limefanyika makusudi kwa kumtumia mwenyekiti wa muda ambaye alihudhuria kikao cha CC ya CCM.

Wapinzani wamepotoka kukubaliana na hoja. Hakuna nchi kwanza kwa upande mmoja.
Nchi kwanza ni kwa pande mbili tena CCM wenye madaraka ya nchi waongoze si Mbatia na wenzake.

Mbinu zimeshaandaliwa na CCM kwa kutambua kuwa kura ya wazi ndiyo karata yao ya mwisho katika kulinda muungano wa serikali 2

Kwa mtazamo wa duru haya ndiyo wapinzani watarajie

1. Hotuba ya JK itajenga hoja kuwaonyesha wao hawataki katiba mpya na hawaitakii nchi mema

2. Mwenyeikiti wa kudumu atapewa nguvu kwa kutumia kiti chake
a) Kuhakikisha wanaopangwa kuongea na kuzuliwa ni kwa mamlaka yake kwa kanuni zilizopitishwa

b) Itapendekezwa kura ya wazi kuamua ile 2/3 ya pande mbili za muungano iwe 1/2 kwa kujua CCM watapata watu wa kutosha kutokana na wingi wao

c) Wataamua kanuni kwa kutumia 1/2 ya wajumbe na si 2/3 wakisaidiwa na nguvu ya mwenyekiti

d) Wazungumzaji watapangwa, wa upinzani watapangwa hafifu wasio na hoja.

Bunge litakuwa chini ya udhibiti wa CCM na kila hoja itaangaliwa kwa mtazamo wa ki CCM

2. Mbinu ya pili ni kuwavuruga wapinzani.
Katika kipindi ambacho vifungu 37 an 38 vipo kiporo pesa zitatembezwa, fitna itapitishwa ili kuwafarakanisha wajumbw wa UKAWA na kununua wale wasio na uelekeo ambao ni 201

Hivyo rushwa itafanya kazi na pesa itaembea sana ili kuweka mambo sawa

3. Kuwatisha wajumbe wa CCM wenye msimamo mkali.
Kutakuwa na mikutano ya vyama Caucus ya kutishiana hasa CCM
Njia itakayotumika ni kuwaaminisha kura zao ziwe elektonic au vyovyote bado CCM itakuwa na uwezo wa kuwatambua. Wajumbe watalegea na kukubaliana na msimamo wa chama

Wapinzani akina Lipumba, Mbowe, Mbatia na wengine hawaonekani kujifunza kitu hata kidogo. Mchakato ulipoanza tuliwaambia kuhusu kuaminika kwa serikali ya JK .

Kila walipoitwa Ikulu waliambiwa jambo moja wakitoka mambo yanafanywa tofauti.
Bado hainonekani kama wamejifunza na haijulikani kama watajifunza.

Walipokuwa na maandamano kuhusu katiba JK aliwaita Ikulu na kusitisha mswada usipitishwe hadi marekebisho yatakapofanyika. Majadiliano hayo yakazuia maandamano ya wapinzani.
Siku waliyozuia maandamano JK akasaini mswada kinyume na makubaliano yao.
Wapinzani wakawa hawana pa kutokea.

Bado hawaonekani kumwelewa JK na serikali ya CCM kwa ujumla.
Hili la kukubali kuahirisha vifungu litawagharimu,ni uamuzi wa ajabu usio na fikra.
Wapinzani wamedanganywa kama watoto wajiandae kupewa peremende

Baada ya wiki moja kuanzia sasa wanaduru tutajadili bandiko hili na kuona kama yaliyojadiliwa ilikuwa kuwaonea wapinzani au kuwaambi ukweli.

Wapinzani wameuza ghala la silaha na sasa watulie, CCM imefanikiwa kuuteka mchakato huu.
Pengine waangalie the way forward kuzuia rasimu ya mwisho , ndani ya bunge wameshapoteza.

CCM haiwezi kukataa ndani ya CC ikaja na hoja tofauti nje ya CC.
Roho ya CCM kulinda muungano ni serikali 2 ni kura ya wazi na hilo halitazuilika kwa sasa kwasababu wapinzani wameingia mkenge

Swali la endapo katiba itatokana na wananchi bado linabaki!

Tusemezane
 

SITTA ATAMALIZA KAZI YA CCM
NI MSUMARI WA MWISHO KATIKA HARAKATI ZA WAPINZANI
KATIBA MPYA SASA MASHAKANI, SERIKALI 3 KITENDAWILI

Bandiko lililotangulia(#43) tumeeleza mbinu zitakazotumika kupitisha vifungu kwa utashi wa CCM. Tumeeleza kosa la wapinzani na watarajie nini mbele ya safari

Mh Sitta amechaguliwa, Mwenyekiti na Spika wa bunge la katiba.
Kuchaguliwa kwake si bahati mbaya kama inavyodhani.Sitta anataka kulitumia BMLK kama mtaji wa uchaguzi mkuu akiwa mgombea watarajiwa

Sitta anakabliwa na mambo mawili yatakayoamua hatima yake kwa siku za usoni ndani ya chama na kwa wananchi.

1. Kwa wananchi, anataka athibitishe uwezo wa uongozi wa nchi kwamba yupo tyari kwa prime time

2. Sitta atapendelea kutowaudhi CCM ambao ndio wana kadi ya mwisho kuhusu mbio za Urais

Mtihani uliopo ni kama ule wa uchaguzi wa Spika ambapo CCM walimuondoa kwa kutumia makundi na udhaifu wa mwenyekiti. Hapa ni pagumu sana kwa Sitta.

Ikumbukwe wakati wa uchaguzi wa Spika bunge la JMT, kundi lililomuondoa Sitta kwa kigezo cha wakati wa akina mama ni la EL na Andrea lililokuwa na ushawishi

Na ni Andrea aliyeandika rasimu mbadala ya CCM ya serikali 2 kwa manufaa ya kundi analowakilisha. Nguvu za Sitta kuzuia kundi hili ni kujitafutia kigingi mbele ya safari.

Kamati kuu imekaa na kuamua ni serikali 2, kamati kuu hiyo hiyo itaamua hatima ya Sitta katika mbio za Urais.Ni jambo la kushangaza kutegemea Sitta kuja na kitu nje ya maagizo ya CC

Lakini pia Sitta yupo katika rekodi akiwa muumini wa serikali 2.
Kumbu kumbu za bunge zinaonyesha akitetea hilo kwa nguvu zote na kwenda mbali kwa kusema ni haki kwa wznz kumiliki ardhi na haki hiyo hapaswi kuwa nayo Mtanganyika.

Mchango wake katika mambo ya muungano umelalia sana upande wa znz.
Suala la serikali 3 kama lilivyopendekezwa na tume linaanza kuwa ni ndoto.

Ndoto zitaanza kwa mbinu zilizoelezwa katika bandiko 43 hapo juu.
Kwa vile sasa Sitta ni Spika hilo linampa nguvu ya kutumia kiti katika baadhi ya maamuzi.

Ni sitta aliyeasisi neno kiti kwa kuwanyima wapinzani fursa za kuzungumza na hata kukataa hoja kwa mbinu za kiti kimeamua.

Kiti sasa kina nguvu na wapinzani watarajie maumivu makali sana kutoka kwa Sitta.
Sitta anasema yeye ni chura anayerudi katika maji akimaanisha ana uzoefu.
Uzoefu wa Sitta unaonyesha kuwa alizima hoja ya Richmond hadi leo kwa njia za nguvu ya kiti.

Sitta ameshindwa kusimamia kasfa nyingine ambazo zimebaki kuwa viporo hadi leo.

Si mintaarafu ya duru za siasa kumhukumu Sitta kabla ya kuanza kazi, ukweli unabaki kuwa Sitta tunayemjua,matumaini ya katiba ya wananchi yanazidi kupotea, kosa la wapinzani kuwagharimu tena.

Sitta hawezi kuacha interest zake za kuwa rais kwa kuangalia masilahi ya wananchi.
Kwa sasa anatakiwa aende kamati kuu ya CCM kupokea magizo ya nini kitakuwemo katika katiba.
Sitta anaenda kusimamia uandikwaji wa katiba ya CCM na si wananchi.

Wajumbe wa BMLK wangekuwa na macho wangemchagua mtu asiye na masilahi na CCM.
Pandu hana masilahi ndiyo maana busara zake zimeonekana.
Sita ana interest na hizo zitafunika na kuzima ndoto za wananchi kuhusu katiba.

Sitta hatakubali mchakato usimamishwe ili kupisha serikali ya Tanganyika kuzinduliwa.
Hatakubali, si muumini wa serikali,anategemea maagizo ya CC ya CCM na hana nguvu ya kuyapinga.

Alijaribu kitumbua kikaingia mchanga, nani asiyeogopa nyoka baada ya kugongwa?

Tusemezane


cc Skype
 
Mfumo wa upigaji kura ndani ya BLK unaendelea kuwa kitendawili. Hii sio ishara nzuri hasa ikizingatiwa kwanza, bunge lipo kwenye wiki ya nne sasa (sawa na karibia theluthi moja ya muda ambao bunge linatarajiwa kukaa), na pili,vifungu husika ndio vitakavyopelekea upatikanaji wa katiba ambayo itapelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kura ya maoni. Katika mazingira haya, mwenyekiti wa kudumu ameshapatikana na makamu wake yupo njiani kupatikana, huku pia wajumbe wa BLK wakiwa tayari kula viapo vyao na Rais wa JMT akiwa anakaribia kulizindua rasmi bunge hilo. Mazingira haya yanatuacha na maswali mengi, huku baadhi ya majibu yakiwa yamejadiliwa na Nguruvi3 hapo juu.

Kimantiki, the fact kwamba kanuni ya 37 na 38 bado hazijapata ufumbuzi maana yake ni kwamba shughuli za kuteua mwenyekiti na makamo, kuapisha wajumbe na bunge kuzinduliwa rasmi na rais - shughuli hizi zote hizi sio tu kwamba hazina maana bali pia hazina uhalali wa kuendelea. Swali linalofuatia ni - Kwa vile ccm ilishaamua kufa kiume na msimamo wake wa serikali mbili, je:

1. CCM ipo tayari bunge la katiba livunjike na fedha za walipa kodi ziwe zimeteketea bure kwa ajili tu ya msimamo wake serikali mbili ambao inataka kuulinda kupitia kura ya wazi?

2. Ni kitu gani kimewafanya wajumbe wa BLK waendelee na michakato mingine - kuchagua mwenyekiti wa kudumu na makamo wake, kuapisha wabunge wiki ijayo na rais kuzindua bunge?

Majibu kwa swali la kwanza hapo juu sio black and white lakini kilichodhahii ni kwamba ccm imeshaamua kwamba bora bunge livunjike kuliko chama kupata aibu ya kushindwa kusimamia sera yake ya serikali mbili iwapo kura ya siri itatumika. Ccm haipo tayari kwenda uchaguzi mkuu mwakani katika hali hiyo kwani ni dhahiri kwamba agenda ya muungano itakiangusha chama kwenye majukwaa ya kampeni za siasa.

Majibu kwa swali la pili nayo sio black and white lakini kutokana na hoja alizotoa nguruvi3 hapo juu kuhusiana na makosa ya upinzani katika mchakato huu, kwa mtazamo wangu, wapinzani wamechangia sana kuhakikisha kwamba mpango wa kulivunja bunge la katiba wakati huu haufanikiwi kwani itakuwa ni ushindi kwa ccm kuliko upinzani katika hatua ya sasa. Kama ni kuvunjika, basi hilo lifuate wakati wa majadiliano yaliyojaa hoja za kuivua ccm nguo hasa juu ya serikali mbili. Kwa maana nyingine, Bunge likivunjika katika hatua ya majadiliano juu ya mfumo wa muungano, huo ndio utakuwa ni ushindi wa upinzani, lakini lingevunjika kwa sababu tu kanuni zilizobakia hazifapatiwa ufumbuzi hivyo hatua zilizobakia kutofanyika - ya kuchagua mwenyekiti wa kudumu, kaimu, kuapisha wabunge na rais wa jmt kuzindua rasmi bunge, huu ungekuwa ni ushindi mnono wa ccm kuelekea 2015 kwani hoja kwamba upinzani umevuruga bunge, kodi za umma zimepotea, ni hoja ambazo zingekuwa na mashiko kwa wananchi wa kawaida. Kwahiyo huu inawezekana ulikuwa ni mtego wa ccm lakini umeshtukiwa. Haya ni maoni yangu tu, naweza nisiwe sahihi.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mchambuzi

CCM walikusudia kuvunja bunge kwavile wanataka kuhakikisha sera ya serikali 2 wanayoitaka wao (kikundi cha wachache) inafanikiwa baada ya mbinu za awali kushindwa kama nilivyojadili siku za nyuma.

Mpango wao ulikuwa bunge livunjike ili Rais a design muundo mwingine utakavyovunjilia mbali tume ya Warioba na maoni yake.

Kwamba, iundwe tume nyingine ikipewa hadidu rejea nyingine huku mabadiliko ya vifungu kadhaa yakifanyika kama lile la 2/3 kwenda 1/2.

Kuhakikisha 'waasi' wa CCM wanashughulikiwa ili kwenda bunge lingine kukiwa na watiifu.

Wapinzani wamekosea kwa mtazamo wangu.
Walikuwa na hoja nzito mbele ya wananchi kuhusu umuhimu wa kupiga kura ya siri. Walikuwa na hoja muhimu kwa umma juu ya CCM kunyima uhuru wabunge wake na walikuwa na hoja ya nguvu kwanini mchakato mzima ulikuwa makosa.

Wangeweza kujenga hoja juu uwepo wa kura ya maoni kwanza, halafu upataikanaji wa wawkilishi wa Tanganyika kama alivyojadili Mwanakijiji kabla ya hatua zingine.

Umma ungewaelewa kwasababu si CCM wote wanakubaliana na mbinu za CC au mawaziri 2 , 3 wanaoropoka hovyo.

Ikumbukwe kuwa maoni ya tume ya Warioba ni ya wananchi hivyo wapinzani walikuwa na nguvu ya umma nyuma yao.

Ninasema wamekosea kwasababu kitendo cha kuendelea kupitisha vifungu vingine na kanuni kwa ujumla si halali na wala haivikukidhi haja ya demokrasia au mantiki kama ulivyosema.

Huu ni mtego kwasababu sasa amepatikana mwenyekiti wa kudumu mwenye nguvu za kiutendaji na kisheria kuliko Kificho Pandu.

Jana Sitta amesikika TBC akisema atalinda muungano kwa nguvu zake zote. Unaweza kuona kuwa ameanza kutumia mamlaka yake si ku moderate bunge bali kupokea maagizo ya CC ya CCM.

Hapo ndipo watu watachaguliwa kwa namna fulani kama walivyoachwa akina Mtikila na Mkosamali.Kutawekwa mipango ya kupitisha hoja kwa nguvu kama tulivyomzoea Sitta.

Ni Sitta ambaye alikiuka kanuni za bunge la JMT na kuzima hoja za bunge hadi leo hatuna majibu.

Sasa wapinzani wasitegemee Sitta kwenda kinyume na maagizo ya CC.
Hapo watajikuta wakitupwa nje ya bunge na kupakwa kila aina ya ubaya huku CCM wakipitisha rasimu ya katiba yao.

Mfano mzuri ni pale JK alipocheza dana dana na wapinzani.
Na wao kwa kuamini taifa kwanza wakaukbaliana naye.
Bunge likapitisha mswada likiwa na wabunge 100 kati ya 320. Kwa CCM hiyo ni sawa kwasababu CCM haina haramu ilimradi mambo yake yanyooke.

Mchezo huo wapinzani wautegemee sana na ndipo mtego ulipo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3, kwa kulingana na sheria husika za sasa zilivyo, je rais anaweza kuvunja bunge la katiba tuseme hata kesho au lazima ujanja ujanja utatengenezwa kisheria muda sio mrefu kumpa mamlaka hiyo? Nini mtazamo wako, nauliza kwani mbeleni naona rais kuaibika kama hawatakuwa waangalifu.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3, kwa kulingana na sheria husika za sasa zilivyo, je rais anaweza kuvunja bunge la katiba tuseme hata kesho au lazima ujanja ujanja utatengenezwa kisheria muda sio mrefu kumpa mamlaka hiyo? Nini mtazamo wako, nauliza kwani mbeleni naona rais kuaibika kama hawatakuwa waangalifu.
Mkuu sina uhakika na sheria zilizounda BMLK zinasemaje kuhusu kuvunjwa kwake.

Nina uhakika kuwa kama itatokea basi CCM watavunja na si JK. Hata kama sheria inamtaka JK, ujanja ujanja utatumika ili kuokoa jahazi. Katika masuala magumu kama haya JK hapataikani.

Mbele ya safari ni kugumu sana. JK alifanya makosa kuruhusu misimamo ya vyama badala ya misimamo ya wananchi.Hili bunge kingefanikiwa kama lingekuwa la wananchi bila kuwa na influence ya kisiasa.

Kwasasa kuna Simba na Yanga, na kila jambo linaangaliwa kutoka kona tofauti. Kwavile kuna preamble ya CCM kuteka mjadala hata halali ya CCM itaonekana haram. Kuna mistrust ya hali ya juu sana.

Kuna suala la Uzanzibar lililozaa Utanganyika. Wale wabunge waliokuja kuitetea Znz na si Tanzania wameunda kundi lisilotarajiwa la Tanganyika. Kwamba wapo wanaosema wao ni nani ndani ya bunge na wanatokea wapi.

Maamuzi mengine yatazingatia upande wa wabunge zaidi kuliko utaifa wa Tanzania.

Kuna mipasuko ndani ya vyama. Kuna CCM, mapande makubwa 2, CCM znz yenye mapande makubwa 3.
Mnyukano huo utazaa upinzani wa tatu ambao utakuwa bega kwa bega na wapinzani hadharani au kwa siri.

Nikiangalia scenario zote naona mwisho mbaya sana wa hili bunge.
 
TLIYOSEMA BANDIKO # 43 YAMEANZA KUTIMIA
SITTA KAANZA KAZI ALIYOTUMWA
JK KWENDA KUBOMOA HOJA ZA TUME YA WARIOBA.


Wanaduru, naomba kwa utulivu kabisa mpitie tena bandiko #43 #44 kama nilivyolinukuu hapa chini.
Naliwaahidi kuwa baada ya wiki moja, ima wanajamvi mnisute kwa uzushi au mkubaliane nami kuhusu wapinzani kuuza silaha.

WAPINZANI WA CCM WAMEINGIA MKENGE
WAMEUZA SILAHA KAMA WALIVYOUZA WAKATI WA KUANZISHWA MCHAKATO

Kwa wiki 3 suala la kura za siri na wazi la vifungu 37 na 38 limekwama.
CCM wanamsimamo wa kura ya wazi kudhibiti wanachama wao ili kulinda muungano wa serikali 2 wenye masilahi kwao na si kwa nchi.

Wapinzani wanataka kura 3 ili kuwa huru kwa kila wajumbe wakitegeme kuvuna baadhi ya CCM wasiokubaliana na chama chao.

Imekubaliwa vifungu hivyo viachwe ili bunge lizunduliwe na rais halafu muafaka utafutwe.
Wapinzani wamekubaliana na kama alivyosema Mbatia nchi kwanza na makundi baadaye

Ukiacha Mtikila na Mkosamali, wengine wameafiki wakitumaini kupata muafaka baada ya uchaguzi wa mwenyekiti.

Uchaguzi wa mwenyekiti, ni wazi utatoa mtu wa CCM ambao walikuwa na kikao cha kamati kuu na kusisitiza msimamo wa kura ya wazi. CCM haikuona umuhimu wa nchi kwanza kama Mbatia alivyosema hivyo ni ujinga kudhani kuwa wana nia njema na nchi.

Malalamiko ya Mtikila na Mkosamali yalihusu kutopewa nafasi za kuzungumza.
Hilo limefanyika makusudi kwa kumtumia mwenyekiti muda aliyehudhuria kikao cha CC ya CCM.

Wapinzani wamepotoka kukubaliana na hoja.
Hakuna nchi kwanza kwa upande mmoja.
Nchi kwanza ni kwa pande mbili tena CCM wenye madaraka ya nchi waongoze si Mbatia na wenzake.

Mbinu zimeshaandaliwa na CCM kwa kutambua kuwa kura ya wazi ndiyo karata yao ya mwisho katika kulinda muungano wa serikali 2

Kwa mtazamo wa duru haya ndiyo wapinzani watarajie

1. Hotuba ya JK itajenga hoja kuwaonyesha wao hawataki katiba mpya na hawaitakii nchi mema
2. Mwenyeikiti wa kudumu atapewa nguvu kwa kutumia kiti chake

a) Kuhakikisha wanaopangwa kuongea na kuzuliwa ni kwa mamlaka yake kwa kanuni zilizopitishwa

b) Itapendekezwa kura ya wazi kuamua ile 2/3 ya pande mbili za muungano iwe 1/2 kwa kujua CCM watapata watu wa kutosha kutokana na wingi wao

c) Wataamua kanuni kwa kutumia 1/2 ya wajumbe na si 2/3 wakisaidiwa na nguvu ya mwenyekiti

d) Wazungumzaji watapangwa, wa upinzani watapangwa hafifu wasio na hoja.

Bunge litakuwa chini ya udhibiti wa CCM na kila hoja itaangaliwa kwa mtazamo wa ki CCM

2. Mbinu ya pili ni kuwavuruga wapinzani.
Katika kipindi ambacho vifungu 37 an 38 vipo kiporo pesa zitatembezwa, fitna itapitishwa ili kuwafarakanisha wajumbw wa UKAWA na kununua wale wasio na uelekeo ambao ni 201

Hivyo rushwa itafanya kazi na pesa itaembea sana ili kuweka mambo sawa

3. Kuwatisha wajumbe wa CCM wenye msimamo mkali.
Kutakuwa na mikutano ya vyama Caucus ya kutishiana hasa CCM
Njia itakayotumika ni kuwaaminisha kura zao ziwe elektonic au vyovyote bado CCM itakuwa na uwezo wa kuwatambua. Wajumbe watalegea na kukubaliana na msimamo wa chama

Wapinzani akina Lipumba, Mbowe, Mbatia na wengine hawaonekani kujifunza kitu hata kidogo. Mchakato ulipoanza tuliwaambia kuhusu kuaminika kwa serikali ya JK .

Kila walipoitwa Ikulu waliambiwa jambo moja wakitoka mambo yanafanywa tofauti.
Bado hainonekani kama wamejifunza na haijulikani kama watajifunza.

Walipokuwa na maandamano kuhusu katiba JK aliwaita Ikulu na kusitisha mswada usipitishwe hadi marekebisho yatakapofanyika. Majadiliano hayo yakazuia maandamano ya wapinzani.
Siku waliyozuia maandamano JK akasaini mswada kinyume na makubaliano yao.
Wapinzani wakawa hawana pa kutokea.

Bado hawaonekani kumwelewa JK na serikali ya CCM kwa ujumla.
Hili la kukubali kuahirisha vifungu litawagharimu,ni uamuzi wa ajabu usio na fikra.
Wapinzani wamedanganywa kama watoto wajiandae kupewa peremende

Baada ya wiki moja kuanzia sasa wanaduru tutajadili bandiko hili na kuona kama yaliyojadiliwa ilikuwa kuwaonea wapinzani au kuwaambi ukweli.

Wapinzani wameuza ghala la silaha na sasa watulie, CCM imefanikiwa kuuteka mchakato huu.
Pengine waangalie the way forward kuzuia rasimu ya mwisho , ndani ya bunge wameshapoteza.

CCM haiwezi kukataa ndani ya CC ikaja na hoja tofauti nje ya CC.
Roho ya CCM kulinda muungano ni serikali 2 ni kura ya wazi na hilo halitazuilika kwa sasa kwasababu wapinzani wameingia mkenge

Swali la endapo katiba itatokana na wananchi bado linabaki!

Tusemezane
Juzi mjumbe wa kamati ya kanuni Tindu Lissu alihoji kuvunjwa kwa kanuni kwa kumwalika Jaji Warioba kwanza halafu Rais.

Kanuni zilizokubaliwa na wabunge wakiwemo akina Lipumba, Mbatia(nchi kwanza), Mbowe na wengine zinasema Rais atakukwenda kuhutubia halafu Jaji Warioba atawasilisha rasimu.

Tindu alipotaka mwongozo, Samwel Sitta tuliyewahi kusema hapa duru kuwa ni mnafiki mkubwa na hana nguvu zaidi ya CC ya CCM alimjibu kuwa
'' KANUNI ZINANIRUHUSU KUTUMIA BUSARA YANGU KUAMUA BAADHI YA MAMBO NAMNA NINAVYOONA INAFAA HIVYO NIMETUMIA MADARAKA YANGU KUAMUA HIVYO ILI WAJUMBE WAWE NA MJADALA MPANA KABLA YA KWENDA KWENYE KAMATI''

http://habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/22911-sitta-adaiwa-kukiuka-kanuni

Wanaduru, rudi bandiko #44, 43 lililoandikwa wiki moja iliyopita likiwausia wapinzani kuwa wameuza silaha. Tumeeleza wazi kuhusu Sitta kutumia nguvu ya kiti chake siku za nyuma kuficha uhalifu bungeni. Tukaaeleza alitumia nguvu ya kiti kufanya hivyo na ndivyo atatumia katika kuwamaliza wapinzani na kuendesha agenda za CCM.

Sitta yupo katika rekodi ya kupinga mawazo ya tume ya Warioba kwa kusema anataka serikali 2. Hivyio kitendo cha kumwalika Rais baada ya Jaji Warioba maana yake ni kumpa nafasi ya kujibu hoja za Warioba kabla ya kujadiliwa, kumpa nafasi ya kuweka msimamo wa chama chake kuwatisha wanachama wake.

CCM wameshatishwa (Bandiko 43) na katibu mkuu Kinanan aliyesema wana majina ya watu 15 wanaopingana nao. Hii ni kuwapa hofu wabunge wa CCM kuhusiana na misiamamo yao.

Hivyo duru za saiasa tunasimama na kusema wazi tena tukiwa na ushahidi usio na chembe ya shaka kuwa, Wapinzani wameuza ghala la silaha, hwajifunzi kutokana na juisi za maembe, wanadanganyika kwa hoja dhaifu na ni wepesi wa kukubali kilicho hovyo bila tafakuri.

Wananchi, hili suala la katiba ni jukumu lenu mkiacha hawa akina Mbowe, Lipumba na Mbatia wanaoweza kudanganywa na juisi za maembe nchi hii itateketea.

Ni bora kuzuia kuliko kuponya. Bado ipo nafasi ya kukataa uhuni na udhalimu wa CCM.
Mchezo wa CCM ni maafa kwetu, tunaendelea kucheka nyani tusbiri siku ya mavuno.

Tusemezane.


Kwahisani ya gazeti la Habri leo


http://habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/22911-sitta-adaiwa-kukiuka-kanuni
 
Mkuu Mchambuzi

Nadhani umeona mantiki niliyosema wapinzani waliuza silaha wenyewe.
Yale ya bandiko 44 na 43 sasa yapo wazi.

Mbinu zinazotumika ni nyingi. Sasa hivi kumekodiwa watu kutoka Kenya kuja kueleza historia ya Tanzania. Tuna Manguli akina Shivji hawaalikwi kwasababu watatibua 'dili'.

Nimesema katika bandiko 44 kuwa 'mwisho wa bunge hili ni mbaya' nadhani tulipaswa kusema bunge hili halina mwisho, litavunjika tu.

Kilichotokea Dodoma ni kumpinga Sitta kutumia maguvu na nguvu za kiti kama tulivyojadili huko nyuma.
Makundi yaliyounganisha nguvu ni wapinzani, wateuliwa wa rais wasio na mrengo na wjumbe kutoka Zanzibar wasiotaka kuingiliwa kwa tume ya Warioba.

Huko nyuma tulieleza kuwa CCM ililazimisha mswada wa kukataa tume ya Warioba isiingie bungeni. Njia tulizosema ilikuwa ni kuwazuia wasije haribu mipango ya CCM. Leo unaona jinsi walivyoapatwa na taharuki baada ya kuona wajumbe wamekataa Warioba asianze kwanza.

Ukweli unabaki kuwa Rais anapaswa kuzindua bunge na baada ya hapo mipango mingine iwe ya bunge na si vinginevyo kutokana na kanuni za bunge hilo.

Kitendo cha Sitta ambaye basically ana unafiki kutumia mabavu kimeudhi Wananchi.

Hata hivyo kuna makosa ambayo wapinzani bado wanaendelea kuyafanya.
Baada ya makosa ya kanuni, hili la kuzomea linafanyiwa spinning kuwa wajumbe hawataki serikali 3.

Natoa raia kama wanasoma kuwa lazima awepo msemaji wa kuueleza ulimwengu nini kimetokea na kwasababu zipi.
Kuliacha liandikwe linavyojadiliwa sasa hivi kutawapotosha wananchi waamini kuwa kinachokataliwa ni maoni ya tume, kumbe kinachokataliwa ni ukiukaji wa kanuni.

Hapa tulipofikia kuna kila dalili bunge litavunjika. Kuvunjika kwa bunge kuna maana moja, Rais ameshindwa kuongoza nchi.
Madhara yanayofuata ni muungano kufia mitaani na viungani, na legacy ya JK kwa hili itabaki kuwa hiyo.
Kama walidhani wanalinda muungano kwa mbinu, wame calculate muda mbaya, Sitta anaondoa heshima aliyoa nayo kabisa. Anafunga njia za kuelekea 2015 na ni ishara nzuri kuwa hawezi uongozi wa Tanzania ya leo.

Tusemezane
 
KWANINI CCM WAMESHIKILIA MSIMAMO WA WARIOBA KUANZA
WAPINZANI KARATA YA MWISHO


Jana bunge liliahirishwa kutokana na wapinzani kutotaka Jaji Warioba awasilishe rasimu.
Hii inafuatia kuvunjwa kwa kanuni za bunge zilizotaka rais azindue bunge kwanza.
Spika Sitta alisema kwa busara zake na nguvu aliyopewa na kiti aliona ni vema rais akahutubia baada ya kuwa na agenda.

Katika hali ya kushangaza, Sitta aliona ni vema avunje kanuni zilizochukua siku 22 kuandikwa na jopo la wanasheria na watu wengine wenye weledi kwa vile anaamini busara zake zaidi kuliko wenzake. Hii ni mwanzo wa dharau kubwa sana kwa kamati ya kanuni na bunge kwa ujumla.

Leo imesemwa kuwa ratiba ya Rais haimruhusu kuja kuzindua bunge tofauti na hoja za Samwel Sitta. Kubadilika kwa kauli ni dalili njema sana kuwa jambo lililokusudiwa na akina Sitta ni njama na wala halina mantiki.

Hata kwa kutumia akili za kawaida, bunge la katiba ni jambo muhimu sana kwa taifa kiasi kwamba si rahisi Rais akose saa moja ya kulihutubia tu na wala si majadiliano.

Rais anaweza kusafiri kwenda Dodoma na katika saa 2 akamaliza kazi kubwa ya kitaifa na kurudia katika ratiba zake. Lakini pia kuna Ikulu pale Dodoma anapoweza kuendelea na kazi zake za kawaida. Hilo la ratiba halina maana wala mantiki, ni maneno ya ulaghai tu.

Lengo kubwa la CCM ni kuhakikisha hotuba na rasimu ya Warioba inasomwa kwanza ili Rais ambaye ni CCM namba moja aje kuzijadili hoja za Warioba na wakati huo Warioba akiwa hana nafasi ya kutetea hoja za tume yake.

Mbinu za kuwazuia wajumbe wa tume kuhudhuria vikao ililenga katika kufanikisha mpango huo.

Wapinzani waelewe kuwa njia iliyobaki kwa CCM kuteka hoja na bunge ni kupitia ushawishi wa mwenyekiti wa CCM.

Mbinu hizo ni kama zile zilizotumika kuzuia maandamano ya Wapinzani na Rais akawageuka na kusaini mswada uliopitishwa na wabunge 100 kati ya 320 bila kujali akidi.

Wapinzani waelewe kuruhusu ratiba ya Warioba kuhutubia kabla ya Rais kuna maana zifuatazo

1. Kuruhusu kuvunjwa kwa kanuni na mtu mmoja kwa busara zake, leo na siku zijazo
2. Kuruhusu kuburuzwa kwa vile wataonekana si tishio wala hawana impact katika mchakato
3. Kumpa Rais kupenyeza hoja zake na kuruhusu mchakato kutekwa na CCM

Endapo wapinzani na wale wanapenda demokrasia watakubaliana na ratiba ya Sitta basi ni vema wakarudi kulala vyumbani wakiamka wapokee posho zao.
Mchakato utakuwa umehitimishwa na CCM na wananchi wasubiri rasimu ya CCM

CCM wanakazania ratiba ibadilishwe kwasababu hiyo ndiyo karata yao mkononi kwa sasa.

Wapinzani na wana demokrasia waaingia mkenge huo tena kama walivyoingia siku zilizotangulia? Wakikubali leo basi wakubali kila siku yaishe.

Tusemezane
 
HOTUBA YA WARIOBA IMEPITA
HOTUBA YA RAIS IJUMAA. JE MBINU ZITAFANIKIWA?

Wana duru za siasa kama mjuavyo Rais Kikwete atazindua bunge kesho. Uzinduzi wake umegubikwa na utata wa kisheria kuhusu kanuni zilziotumika na jinsi zilivyovurugwa.

Lengo la kuvuruga kanuni ni kutoa nafasi kwa Rais kuja kujibu hotuba ya Warioba. Tunafahamu kwanini anataka kujibu hotuba hiyo.

Kesho Ijumaa tarehe 24, kabla ya hotuba ya rais tutakuwa na bandiko maalumu hapa kuelezea mwelekeo wa hotuba hiyo kwa ujumla.

Tutaeleza kwa mapana maana ya uzinduzi, tutaeleza alichokusudia, na mbinu atakazotumia kuwashawishi wabunge kukubaliana na hoja nje ya zile alizopewa na tume.

Tutaeleze namna atakavyomjibu Warioba, namna atakahangaika na Wapinzani, jinsi atakavyouzngumzia habari ya Zanzibar. Pia tutaonyesha mtatizo na changamoto zinazomkabili ikiwemo kuvunjika kwa bunge na mbinu atakazotumia ambazo zitamtia matatani zaidi katika chama chake

Tafadhali sana ungana na duru kupata unyeti ambao fukunuku zimeudaka kutoka katika kethchup kama si source.


Nape Nnauye Mwigulu Nchemba Anna Tibaijuka zumbemkuu platozoom Kimweri Mkandara AshaDii Tuko Mag3 Bongolander @Dr Faustine Ndugulile Mchambuzi Skype Mzee Mwanakijiji Mkandara JokaKuu Jasusi Mimibaba GHIBUU Pasco Invisible Skype
 
Last edited by a moderator:
HOTUBA YA WARIOBA IMEPITA
HOTUBA YA RAIS IJUMAA. JE MBINU ZITAFANIKIWA?

Wana duru za siasa kama mjuavyo Rais Kikwete atazindua bunge kesho. Uzinduzi wake umegubikwa na utata wa kisheria kuhusu kanuni zilziotumika na jinsi zilivyovurugwa.

Lengo la kuvuruga kanuni ni kutoa nafasi kwa Rais kuja kujibu hotuba ya Warioba. Tunafahamu kwanini anataka kujibu hotuba hiyo.

Kesho Ijumaa tarehe 24, kabla ya hotuba ya rais tutakuwa na bandiko maalumu hapa kuelezea mwelekeo wa hotuba hiyo kwa ujumla.

Tutaeleza kwa mapana maana ya uzinduzi, tutaeleza alichokusudia, na mbinu atakazotumia kuwashawishi wabunge kukubaliana na hoja nje ya zile alizopewa na tume.

Tutaeleze namna atakavyomjibu Warioba, namna atakahangaika na Wapinzani, jinsi atakavyouzngumzia habari ya Zanzibar. Pia tutaonyesha mtatizo na changamoto zinazomkabili ikiwemo kuvunjika kwa bunge na mbinu atakazotumia ambazo zitamtia matatani zaidi katika chama chake

Tafadhali sana ungana na duru kupata unyeti ambao fukunuku zimeudaka kutoka katika kethchup kama si source.


Nape Nnauye Mwigulu Nchemba Anna Tibaijuka zumbemkuu platozoom Kimweri Mkandara AshaDii Tuko Mag3 Bongolander @Dr Faustine Ndugulile Mchambuzi Skype Mzee Mwanakijiji Mkandara JokaKuu Jasusi Mimibaba GHIBUU Pasco Invisible Skype

Nitasikitika sana, na kwa mara nyingine nitamdharau raisi kama ataingilia mchakato huu wa katiba. "Kwa utashi wake" mwenyewe aliamua kuruhusu mchakato huu akijua kabisa kitakachoandikwa ni kwa manufaa ya taifa litakalokuwepo kwa miaka nenda miaka rudi, sio kwa vikundi vya siasa ambavyo leo vipo, kesho havipo.
Kikwete akifanya kosa kubwa la kwanza kwenye mchakato huu pale alipotia saini sheria yenye mapungufu, kubwa likiwa kukoma kwa mamlaka ya tume ya Warioba mara baada ya kuwasilisha hotuba bungeni. Baada ya hapo alijitahidi kuwa neutral, hata siku alipotoa hotuba baada ya kuwasilishwa kwa rasimu ya pili, hakuonyesha dhahiri kuegemea upande wowote. Atafanya makosa makubwa endapo ataingia kwenye mtego wa chama chake wa kupingana na wananchi wa Tanzania kwa kupinga maoni halali yaliyotolewa na tume.
Kikwete atambue tu kwamba ultimate outcome ya hotuba yake ipo juu ya hadhi yake. Nina uhakika kwa namna yeyote hotuba yake hiyo ambayo kwangu ni ceremonial, haitabadilisha chochote kwa maoni ya wala mtizamo wa Watanzania. Alichowasilisha Warioba ni maoni ya mamilioni Watanzania, atakachoongea Kikwete ni maoni yake binafsi; vitu hivyo viwili haviwezi kushindanishwa, wala kufananishwa.

Ninamshauri Kikwete asimame na ahutubie bungeni kama raisi, kiongozi wa wanaotetea serikali mbili na wanaotetea serikali tatu, wa wanaotetea uraia wa nchi moja, na wanatetea uraia wa nchi mbili. Kiongozi wa wanaotaka serikali ndogo na wasiotaka hivyo. Kiongozi wa Watanzania wote. Atenganishe sasa uraisi na uenyekiti wa CCM, japo kwa hotuba yake kesho...

NB; Mkuu Nguruvi3 pengine utapenda kupaangalia hapo penye red...
 
Last edited by a moderator:
HOTUBA YA WARIOBA IMEPITA
HOTUBA YA RAIS IJUMAA. JE MBINU ZITAFANIKIWA?

Wana duru za siasa kama mjuavyo Rais Kikwete atazindua bunge kesho. Uzinduzi wake umegubikwa na utata wa kisheria kuhusu kanuni zilziotumika na jinsi zilivyovurugwa.

Lengo la kuvuruga kanuni ni kutoa nafasi kwa Rais kuja kujibu hotuba ya Warioba. Tunafahamu kwanini anataka kujibu hotuba hiyo.

Kesho Ijumaa tarehe 24, kabla ya hotuba ya rais tutakuwa na bandiko maalumu hapa kuelezea mwelekeo wa hotuba hiyo kwa ujumla.

Tutaeleza kwa mapana maana ya uzinduzi, tutaeleza alichokusudia, na mbinu atakazotumia kuwashawishi wabunge kukubaliana na hoja nje ya zile alizopewa na tume.

Tutaeleze namna atakavyomjibu Warioba, namna atakahangaika na Wapinzani, jinsi atakavyouzngumzia habari ya Zanzibar. Pia tutaonyesha mtatizo na changamoto zinazomkabili ikiwemo kuvunjika kwa bunge na mbinu atakazotumia ambazo zitamtia matatani zaidi katika chama chake

Tafadhali sana ungana na duru kupata unyeti ambao fukunuku zimeudaka kutoka katika kethchup kama si source.
@Nape Nnauye Mwigulu Nchemba Anna Tibaijuka zumbemkuu platozoom Kimweri Mkandara AshaDii Tuko Mag3 Bongolander @Dr Faustine Ndugulile Mchambuzi Skype Mzee Mwanakijiji Mkandara JokaKuu Jasusi Mimibaba GHIBUU Pasco Invisible Skype
Mkuu Nguruvi3, nilipanga kesho nifanye shanting to and fro Dodoma, kidala dala ninachotumia ni kile cha sky link, wananiambia naweza kupata nafasi kwenda tuu ila kurudi ni issue!. Nikiconfirm kwenda, na mimi ninawapatia live from Dodoma ila yatakayojiri nje ya ukumbi, maana ya ndani wote mtayashuhudia live!.

Kwa maoni yangu, hotuba ya JK ya kesho ndio the most important hotuba ever!, its a do or die for muungano!. Wasoma nyakati wa ile ofisi ya wenye kazi hiyo watakuwa waliishamwaga kila kona ya Dodoma kupima upepo!, mimi sitashangaa kama atajiepusha kabisa kumjibu Warioba asije akalikoroga!, hivyo kuwaachia CCM waicheze hii ngoma kwa kuitumia advantage ya wingi wao!.

Lets way and see!.
Pasco
 
Kwa wale mnaopongeza hotuba ya Warioba, Je swala la serikali 3 likipita mnafikiri ni hatua gani zitafuata? maana yaonyesha wengi hamfahamu muundo na taratibu za serikali 3 unatokanaje na hatua zipi lazima zifuatwe.
 
Kwa wale mnaopongeza hotuba ya Warioba, Je swala la serikali 3 likipita mnafikiri ni hatua gani zitafuata? maana yaonyesha wengi hamfahamu muundo na taratibu za serikali 3 unatokanaje na hatua zipi lazima zifuatwe.
Mkuu Mkandara, katika kujibu swali lako, naomba nikurudishe nyuma kidogo...hivi kwa kusema kweli mfumo tulio nao sasa ni wa serikali ngapi? Mimi naamini kiuhalisia tayari tunazo serikali tatu. Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu kwa upande wa nchi ya Zanzibar kuna serikali mbili na kwa nchi ya Tanzania pia tunazo serikali mbili; sasa swali ni je, ndani ya hizi nchi mbili tuna jumla serikali ngapi? Kama tunazo serikali mbili nchini Tanzania, hizo serikali bila shaka moja inashughulikia mambo ya Muungano na nyingine inashughulikia mambo ya Tanzania bara (Tanganyika) na kama nchi ya Zanzibar pia ina serikali mbili, ni wazi moja inashughulikia mambo ya Muungano na nyingine mambo ya Zanzibar. Je mpaka hapo niko sahihi?

Sasa basi kwa kuwa kuna mambo ya Tanzania bara, mambo ya Zanzibar na mambo ya Muungano, je kiuhalisia tunazo serikali ngapi? Ni kipi kipya kimeletwa na Rasimu ya Katiba kama ilivyosomwa na Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba kwa wajumbe wa Bunge la Katiba? Tunaye Kiongozi wa serikali bungeni ambaye eneo lake la kujidai linaishia Chumbe. Tunaye kiongozi wa serikali ndani ya Baraza la Wawakilishi ambaye eneo lake la kujidai halivuki bahari. Halafu tunayo serikali ambayo mamlaka yake hayana mpaka ndani ya Jamhuri, au nakosea? Si tumeaminishwa yapo mambo ya Muungano? Kwa kujibu swali lako; Naamini tayari tunazo serikali tatu ila kwa uhuni tu tukaamua kuziita mbili, sasa Rasimu inasema uhuni sasa basi! Koleo liitwe kwa jina lake! Uswahili sasa basi!

Muundo na taratibu za serikali 3 tayari tunao kwani Rasimu ya Jaji imewasha taa tuongee tukionana na siyo kuendelea kuendesha mambo gizani. Kwa kukaa gizani katiba ilivunjwa, hakuna aliyeweza kuona; uhaini ulifanywa, hakuna aliyeona na kukekemea; mambo ya kipuuzi hayakuhitaji kufumbiwa macho kwani giza nene tayari lilitamalaki mbele ya macho yetu. Rasimu imetuletea mwanga, waliozoea kufanya mambo gizani sasa wanajifungia kwenye semina wakipanga watakavyohujumu mwanga usiwamulike (masikini CCM!). Hapana Mkuu Mkandara, wamechelewa! It was just a matter of time and the right time has arrived, it is here and it wont go away that easily. Kikwete beware!
 
Last edited by a moderator:
Kumradhi wanaduru, naomba kutoka nje kidogo ya mjadala kwa minajili ya kuweka kumbukumbu sawa kuhusu suala la Warioba na Jakaya.

Mwanzo kabisa wakati wa kupitishwa kwa kanuni za bunge maalum la katiba ndugu Lissu alitoa maelezo kuhusu suala la nani atangulie na nani afuatie. Katika kufafanua alisema kua suala la Jakaya kuhutubia bunge maalum la katiba halipo kikanuni bali kamani ya kanuni waliona ni busara wamwalike kwa kua ni mkuu wa nchi na ni tukio la kihistoria. Utata ukaja baada ya baadhi ya wajumbe kulazimisha kua katika mpangilio aanze Warioba kisha Jakaya kinyume na kanuni lakini Lissu akafafanua kwa kusema kua endapo atatangulia Warioba basi ingeonekana kama Jakaya anakuja kumjibu kama itakavyokua kesho.

Tukirudi katika taratibu za mabunge 'nadhani' ili bunge lianze shughuli zake ni lazima lizinduliwe na rais kinyume na ilivyofanyika na kwa hali hiyo ni wazi Warioba aliwasilisha rasimu ktk mkusanyiko wa watu na si bunge kwa kua mpaka sasa bado halijazinduliwa. Matokeo yake ndo hayo Jakaya kuja na mipasho kesho.

Sasa nirudi kwenye hoja ya Nguruvi3 hapo juu. Sitajadili chochote ila napenda kumsihi Nguruvi3 atuletee uchambuzi aliouahidi kuuleta kesho na badala yake iwe leo ili tupate muda wa kuuona mwelekeo wa Jakaya na mipango dhalimu ya kichama iliyoandaliwa. Natanguliza shukrani.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara, katika kujibu swali lako, naomba nikurudishe nyuma kidogo...hivi kwa kusema kweli mfumo tulio nao sasa ni wa serikali ngapi? Mimi naamini kiuhalisia tayari tunazo serikali tatu. Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu kwa upande wa nchi ya Zanzibar kuna serikali mbili na kwa nchi ya Tanzania pia tunazo serikali mbili; sasa swali ni je, ndani ya hizi nchi mbili tuna jumla serikali ngapi? Kama tunazo serikali mbili nchini Tanzania, hizo serikali bila shaka moja inashughulikia mambo ya Muungano na nyingine inashughulikia mambo ya Tanzania bara (Tanganyika) na kama nchi ya Zanzibar pia ina serikali mbili, ni wazi moja inashughulikia mambo ya Muungano na nyingine mambo ya Zanzibar. Je mpaka hapo niko sahihi?

Sasa basi kwa kuwa kuna mambo ya Tanzania bara, mambo ya Zanzibar na mambo ya Muungano, je kiuhalisia tunazo serikali ngapi? Ni kipi kipya kimeletwa na Rasimu ya Katiba kama ilivyosomwa na Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba kwa wajumbe wa Bunge la Katiba? Tunaye Kiongozi wa serikali bungeni ambaye eneo lake la kujidai linaishia Chumbe. Tunaye kiongozi wa serikali ndani ya Baraza la Wawakilishi ambaye eneo lake la kujidai halivuki bahari. Halafu tunayo serikali ambayo mamlaka yake hayana mpaka ndani ya Jamhuri, au nakosea? Si tumeaminishwa yapo mambo ya Muungano? Kwa kujibu swali lako; Naamini tayari tunazo serikali tatu ila kwa uhuni tu tukaamua kuziita mbili, sasa Rasimu inasema uhuni sasa basi! Koleo liitwe kwa jina lake! Uswahili sasa basi!

Muundo na taratibu za serikali 3 tayari tunao kwani Rasimu ya Jaji imewasha taa tuongee tukionana na siyo kuendelea kuendesha mambo gizani. Kwa kukaa gizani katiba ilivunjwa, hakuna aliyeweza kuona; uhaini ulifanywa, hakuna aliyeona na kukekemea; mambo ya kipuuzi hayakuhitaji kufumbiwa macho kwani giza nene tayari lilitamalaki mbele ya macho yetu. Rasimu imetuletea mwanga, waliozoea kufanya mambo gizani sasa wanajifungia kwenye semina wakipanga watakavyohujumu mwanga usiwamulike (masikini CCM!). Hapana Mkuu Mkandara, wamechelewa! It was just a matter of time and the right time has arrived, it is here and it wont go away that easily. Kikwete beware!
Ahsante, pengine kwa lugha hii na hoja zako nzito Mkandara atakuelewa.
 
Kumradhi wanaduru, naomba kutoka nje kidogo ya mjadala kwa minajili ya kuweka kumbukumbu sawa kuhusu suala la Warioba na Jakaya.

Mwanzo kabisa wakati wa kupitishwa kwa kanuni za bunge maalum la katiba ndugu Lissu alitoa maelezo kuhusu suala la nani atangulie na nani afuatie. Katika kufafanua alisema kua suala la Jakaya kuhutubia bunge maalum la katiba halipo kikanuni bali kamani ya kanuni waliona ni busara wamwalike kwa kua ni mkuu wa nchi na ni tukio la kihistoria. Utata ukaja baada ya baadhi ya wajumbe kulazimisha kua katika mpangilio aanze Warioba kisha Jakaya kinyume na kanuni lakini Lissu akafafanua kwa kusema kua endapo atatangulia Warioba basi ingeonekana kama Jakaya anakuja kumjibu kama itakavyokua kesho.

Tukirudi katika taratibu za mabunge 'nadhani' ili bunge lianze shughuli zake ni lazima lizinduliwe na rais kinyume na ilivyofanyika na kwa hali hiyo ni wazi Warioba aliwasilisha rasimu ktk mkusanyiko wa watu na si bunge kwa kua mpaka sasa bado halijazinduliwa. Matokeo yake ndo hayo Jakaya kuja na mipasho kesho.

Sasa nirudi kwenye hoja ya Nguruvi3 hapo juu. Sitajadili chochote ila napenda kumsihi Nguruvi3 atuletee uchambuzi aliouahidi kuuleta kesho na badala yake iwe leo ili tupate muda wa kuuona mwelekeo wa Jakaya na mipango dhalimu ya kichama iliyoandaliwa. Natanguliza shukrani.
Skype ahsante kwa hili. Nichangie kidogo kuwa baada ya kanuni kuandikwa zilikubalika na Sitta alikuwepo katika kuziandika. Kurudi nyuma na kusema ametumia busara zake ni kudharau kanuni na kamati husika pamoja na bunge lote kwa ujumla wake.
Mbinu zinazofanyika ni zile tulizojadili katika mabandiko yaliyopita na hakika wapinzani wataburuzwa sana kama hawatakuwa macho.

Hoja yako ya pili tunaifanyia kazi. Ahsante
 
Skype ahsante kwa hili. Nichangie kidogo kuwa baada ya kanuni kuandikwa zilikubalika na Sitta alikuwepo katika kuziandika. Kurudi nyuma na kusema ametumia busara zake ni kudharau kanuni na kamati husika pamoja na bunge lote kwa ujumla wake.
Mbinu zinazofanyika ni zile tulizojadili katika mabandiko yaliyopita na hakika wapinzani wataburuzwa sana kama hawatakuwa macho.

Hoja yako ya pili tunaifanyia kazi. Ahsante

Sawa mkuu nimekuelewa.
 
Back
Top Bottom