Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Naona Donald Trump ameamua kukomaa na kukataa ushauri alopewa. Inasemekana hiyo ndiyo ilisababisha hotuba yake kuchelewa kwa kiasi Fulani.

Kwa hotuba yake hii nadhani njiani ataendelea kukwaa visiki...haya Ni maoni yangu Tu ndugu zangu na niko tayari kukosolewa.
Mkuu, Trump ni Ushindi, hashindwi yule!! He is so smart! Though there's a risk of leading US into another military failure if he, Trump, insist the No Fly Zone in Syria as well as continue to molest China and Russia!
 
SIASA ZA KIMATAIFA

Inaendelea...

Hakuzungumzia mengi au plan yake kuhusu siasa za kimataifa.

Aliwataka washirika wa nchi hasa za kiislama kufanya naye kazi pamoja.
Tatizo ni kuwa kauli hiyo ilishatanguliwa na ile ya islamic terrorist ambayo sehemu kubwa ina walakini

Kuhusu NATO, Trump ameahisi commitment, kinyume na kauli za awali kuwa NATO ni obsolete
Hakuongelea mengi kuhusu mahusiano ya US na dunia kwa ujumla

Katika immigrations amejaribu sana kuepuka kauli kali na kuonyesha kuwa serikali yake na mpango wa kuwawakaribisha immigrants kwa kutumia mfumo wa merits badala ya green card

Mpango mzima ulikuwa uwekwe wazi kesho, lakini kwa kuchelea kuvuruga hotuba umeahirishwa

Pamoja na hayo hakuacha kumshambulia Obama akisema ame inherit mess, na kwamba deni aliloacha Obama ni kubwa kuliko Marais wote combine. Hakusema wangapi na deni lilianzia wapi

Kauli hii haitapokelewa vema na Dems na itakapofika wakati wa infrastructure au gharama zitazotokana a ku repeal and replace obamacare, kutakuwa na tatizo

Hotuba yake haikuwa na specifics kama za mambo makubwa kama immigration, Obamacare, tax cut

Ililenga kulileta taifa pamoja.Between the lines, kuna maeneo alilenga 'wapiga kura wake' kama coal mining, halafu akawalenga Republican kwa hoja zao huku akiwafariji Dems kwa baadhi ya mambo

Kuna eneo alilosema 'maadui' zetu sasa ni marafiki. Kauli hii itaibua suala la Russia kwani ndivyo inavyotafsiriwa. Kwa Rep kunabaadhi hawakubaliani na suala hilo na hapo kutakuwa na tatizo

Nchi za Uropa zinazoona Russia kama tatizo hazitajisikia salama kwa kuona adui wao sasa ni Rafiki wa mshirika wao US.Kuna mixed message hapo

Katika kutafuta balance ya makundituliyosema kuna sehemu atapata mtihani

Tatizo lingine ni ile picha ya protectionism kwa kulenga hotuba kwa America na hivyo kuwaacha washirika hasa wa Ulaya katika kutafakari nini kinafuata.

Protectionism inawapa China na Russia leverage katika ku mobilize nchi kama BRICKS na za Asia

Trump anasema America inataka ku lead dunia tena, wakati akisema yeye si Rais wa Dunia

Kauli nyingine ni ile iliyozungumzia ugaidi ikizituhumu nchi za Ulaya kutokana na mashambulizi
Alichotaka kuonyesha hakina tatizo, chaguo la kauli na uzito wake haukupendeza EU kwa uhakika

Kuna nchi kama Ufaransa na Ujerumani zenye uchaguzi, ilionekana kama anachahiza uchaguzi ufuate mrengo wa siasa zake. Kwa sehemu fulani Merkel akishinda uhusiano hautakuwa wa kuaminiana

Tunaendelea ku digest hotuba na tutawaletea kwa jinsi muda unavyosonga mbele

Tusemezane
 
Mkuu, Trump ni Ushindi, hashindwi
Mku hapa nisaidie kidogo. Si alisema NATO ni obsolete! Je ni obsolete?
Si alisema Obamacare atafuta siku ya kwanza! Je, amefuta siku ya kwanza?

Sina maana hawezi au hashindi, ningependa unipe ufafanuzi kidogo kuhusu hayo mawili
 
Mkuu Nguruvi3, ziko tetesi kwamba hotuba ya Trump imebidi ifanyiwe mabadiliko baada ya washauri wake wa karibu kumshauri aendelee tu na kauli zake kama ilivyokuwa kwenye kampeni. Walidai kwamba kufanya vinginevyo iitaonekana kama vile amesalimu amri na hivyo kuwa na hatari ya kuwapoteza wapenzi wake hasa wale wenye mwelekeo wa Tea Party. Kwa hiyo wakamtaka akomae na msimamo wake ule ule na mengine anaweza kufanya kwa Executive order tu. Nikipata habari kamili nitaileta.
 
Breaking News!

Mtego wa panya waanza kunasa waliomo na wasiokuwemo...Je Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Donald Trump, Jeff Sessions, ataponyoka? Stay tuned!

Sidhani kama atapona na kashfa hii lazima atakwenda na maji kama ilivyokuwa kwa General Flyn.

Moja ya makosa makubwa sana aliyofanya Trump ni kutangaza vita na baadhi ya media kubwa kwa kuziita "fake news"... kwa kufanya hivyo amezidi kuwapa ari ya kumchimba zaidi ili kuibua madudu yake. Yaleyale ya kuanzisha ugomvi wa mawe huku anaishi nyumba ya udongo!
 
Sidhani kama atapona na kashfa hii lazima atakwenda na maji kama ilivyokuwa kwa General Flyn.

Moja ya makosa makubwa sana aliyofanya Trump ni kutangaza vita na baadhi ya media kubwa kwa kuziita "fake news"... kwa kufanya hivyo amezidi kuwapa ari ya kumchimba zaidi ili kuibua madudu yake. Yaleyale ya kuanzisha ugomvi wa mawe huku anaishi nyumba ya udongo!
Kitanzi kinaanza kubana taratibu...Manafort, Flynn na sasa Sessions? Hawa ni makandokando tu, target is isolation by elimination... Sessions hana namna, uamuzi wowote atakaochukua utazidi kumweka tu pabaya yeye na walengwa wengine. He is stuck between a rock and a hard place and no matter which way he goes, it is going to be hard to do. Lenye nafuu kidogo kwake ni kukomaa na kugoma kujiuzulu kwa utetezi wa kisheria kwamba kwa kufanya hivyo hajavunja sheria. Lakini akijiuzulu amejipalia mkaa wa moto pamoja na bosi wake aliyemteua...

Marekani watu hawakurupuki...tuvute subira!
 
He is stuck between a rock and a hard place and no matter which way he goes, it is going to be hard to do. Lenye nafuu kidogo kwake ni kukomaa na kugoma kujiuzulu kwa utetezi wa kisheria kwamba kwa kufanya hivyo hajavunja sheria. Lakini akijiuzulu amejipalia mkaa wa moto pamoja na bosi wake aliyemteua...Marekani watu hawakurupuki...tuvute subira!
Mkuu tulisema, Wamarekani hawatupi jambo katika media bila sababu

Washington Post walipoambiwa ni fake news walikaa kimya kama vile wanafunga kampuni

CNN nao walipoambiwa waliendelea kusisitiza tu kuwa wapo sahihi

The W.Post wameanza kutoa dose na wana dossier kubwa, wanavuta kamba kidogo kidogo mtu akitisika, kitanzi kinabana chenyewe

Katika senate hearing, Sessions aliulizwa kama kulikuwa na mawasiliano aliyojua
Akasema hakuna kwa kadri anavyojua. Tayari swali lile lilikuwa na 'mtego'

Jana anasema ni kweli alizungumza na Balozi wa Russia na kwamba ni kawaida kwa member wa senate katika kamati zao kuzungumza na viongozi wa mataifa

Na huo ni ukweli kwani wenzake katika kamati wamethibitisha ni kawaida

Kwa namna isiyoeleweka, mwezi wa 10 alizungumza tena na Balozi huku wenzake hao hapakuwepo aliyezungumza na Balozi huyo.

Hii ilikuwa ni wakati Utawala wa Obama ulikuwa na taarifa za hacking kutoka intel community, hivyo alikuwa katika 'rada'

Kama umemsikiliza Seneta Lindsey Graham na McCain jana, ni kama vile walijua kitu fulani na hoja ni kuwa Sessions anaweza kuwa hakufanya jambobaya, lakini katika mazingira yaliyopo wanataka kujua alizungumza nini

Leo Republican baadhi wanasema Sessions afanye recuse, yaani ajitoe katika kushughulikia uchunguzi wa Russia kama Mwanasheria. Dems wanataka ajiuzulu

Hii maana yake akiji recuse suala linabaki hewani na anaweza kuitwa kwa mahojiano.

Aking'ang'ana analirefusha na hapo kutakuwa na chimba chimba.
Gen Flynn aliona ni vema ajiondoe ili kuepusha 'fukunyua fukunyua'

Washington Post na Media zilizoitwa 'fake' zinataka ku prove kuwa si fake.

Kitendo cha kumtaja Sessions kuna jambo nyuma. Wanataka watu waingie kichwa kichwa

WH wamegundua jambo, jana wamesema hizo ni jitihada za Dems katika kuvuruga mantiki ya hotuba ya Trump katika congress.

Hapa hawakusema Media au IC au Leak
Wanajitahidi kutafuta mchawi Dem kwasababu wanajua kuna 'mzigo' wa nondo

Kama mtakumbuka tulisema , ugomvi wa Trump na IC na Media utaishia pabaya.

Hizi zote ni katika kuhakikisha wana m-prove wrong na wanatafuta ushahidi

Trump alisema hakuna afisa wake aliyejihusisha, hili la Sessions kama mshauri wa kampeni linamweka mahali pagumu

Katika kufunika habari, leo au kesho utasikia WH ikitangaza jambo 'controversial' kama EO ya wahamiaji. Itakuwa kuahirisha tatizo maana tayari 'upele umempata mwenye kucha'

Tusemezane
 
Mkuu tulisema, Wamarekani hawatupi jambo katika media bila sababu...
Mkuu Nguruvi3, mambo ni hivi...wapo watu humu wananisikitisha sana; mtu kama hujui mambo ni heri kunyamaza tu na kusoma yanayojiri. Kujaribu kutazama mambo ya Marekani kwa jicho la Kitanzania ni kosa kubwa sana na ndiyo maana kuna wakati niliwaomba tuyajadili haya mambo katika anga zao na si anga zetu.

Ingekuwa Urusi, Putin anazo nguvu kabisa za kuweza kuzima uchunguzi kama huu kitu ambacho kwa Marekani hakiwezekani, Putin ana nguvu za kuweza kufungia hata vyombo vya habari kitu ambacho kwa Marekani ni ndoto. Ukitaka kuungua vidole nchini Marekani, gombana na vyombo vya habari, utakiona cha moto.
Katika kufunika habari, leo au kesho utasikia WH ikitangaza jambo 'controversial' kama EO ya wahamiaji. Itakuwa kuahirisha tatizo maana tayari 'upele umempata mwenye kucha'
Katika hotuba yake Trump alikuwa amepanga kulegeza kamba katika maswala mengi tu ili kujaribu kulainisha upinzani lakini washikaji wake wa karibu wakamzuia. Ziko tetesi kwamba hotuba aliyoisoma, haikuwa aliyoiandika ila alilazimika kuisoma kwa ushauri potofu kwamba wale wapenzi wake die hard wangemruka.

Hapa ndipo linapokuja swala la popular votes kama tulivyowahi kudokeza...ni kweli alishinda Urais lakini pia ni kweli walio wengi hawakumpa kura. Alipanga kutoa hotuba kwa kuangalia maslahi ya walio wengi lakini kafanya kosa la kuwasikiliza wachache wa karibu.

Kwa sasa hata akitoa EO ya kuwasamehe wahamaiaji wote, kachelewa kwani ataendelea kupata upinzani kutoka kote kote; kwa watu wake na kwa wapinzani wake. Linalosikitisha zaidi ni kwamba hata miezi miwili hajamaliza ofisini.

Sessions akijiuzulu makubwa zaidi yatafuata...ziko data kibao zinasubiri na ni mwitikio wa WH (response) unaosubiriwa. Wahusika walijua mbinu zinazoweza kutumika kuharibu ushahidi hivyo walihakikisha umehifadhiwa mahala salama. Kwa sasa unatolewa taratibu kulingana na response.

Asipojiuzulu yatakayofuata yanaweza yakamtoa nyoka pangoni...tuvute subira!
 
Mkuu Mag3 siasa za Washington ni next level kama ulivyonena

Republican wanahaha wakimtaka Sessions afanye recuse katika Russia investigation

Suala la connections za Russia, hacking ana waliosaidia linachunguza na DOJ
Uchunguzi unafanywa na FBI na Sessions akiwa AG anawajibika

Republican wana hofu, Sessions akikataa kujiuzulu, investigation haitakuwa na maana na matokeo yoyote hatyatakubaliwa.

Hoja ni kuwa Sessions hawezi kusimamia suala ambalo mwenyewe anachunguzwa

Hii maana yake ni kuwa kutakuwa na 'independent investigation' ambayo Republican hawatakuwa na control na kurudisha kumbu kumbu za ''Nixon au Bill Capitol hill''

Ni kwa msingi huo, Dems wamekaa kimyaa wakimwacha Pelosi na Schumer waongee. Wanataka Rep wajichanganye iundwe tume huru

Kuzima huu moto itakuwa tabu kidogo.

Media alizozogoa Trump zinafanya uchunguzi, IC FBI zinafanya uchunguzi.
Katika utatu huo kila mmoja ni 'watch dog' wa mwenzake

Ukitaka kuona ugumu wa sakata fikiria hivi, ilianza kusemwa 'maafisa' wa kampeni.
Halafu akatajwa Manorf, kisha Flynn akabeba msalaba, na Sasa sessions

Media zinakuwa makini kuunda mzunguko mzima, lakini wanapokwenda kunaonekana

Tusemezane
 
Mkuu Mag3 siasa za Washington ni next level kama ulivyonena...
Nakuambia...! Kila watch dog ni independent, sasa hapo. Ndio maana Mkulu alifanya makosa makubwa alipoanza kwa kuziponda INTEL na MEDIA bila kujua anachochea moto.
Ukitaka kuona ugumu wa sakata fikiria hivi, ilianza kusemwa 'maafisa' wa kampeni. Halafu akatajwa Manafort, kisha Flynn akabeba msalaba, na sasa Sessions
Kwa kila anayetajwa na kujiuzulu Mkulu anavuliwa kipande cha nguo na asipoangalia si muda mrefu atabaki bila nguo.
Media zinakuwa makini kuunda mzunguko mzima, lakini wanapokwenda kunaonekana. Tusemezane
Hao wanafanya kinachoitwa investigative journalism na tofauti yake na wa kwetu ni kwamba ukiwachokoza wanajibu mapigo ila hawafanyi hivyo kwa kukurupuka, hapana, wanachukua time na siku muafaka wanatupa mkuki kwa kulenga penyewe!
 
Breaking News: U.S. Attorney General Sessions recuses himself from Russia investigations!

Hatimaye Mwanasheria Mkuu (AG) wa Serikali ya Donald Trump, Jeff Sessions, asalimu amri na kutangaza kujiweka kando (recuse himself) katika uchunguzi unaotarajiwa kufanyika kuhusu tuhuma za Urusi kuingilia mchakato wa uchaguzi wa Marekani. Kabla ya kutangaza uamuzi huo bosi wake, akijibu swali aliloulizwa, alisema bado ana imani kubwa naye na kwamba hakuwa na taarifa yoyote kuhusu mkutano wa AG wake na balozi wa Urusi. Je huu ndio mwisho au kuna zaidi? Tuzidi kuvuta subira...!
 
Breaking News: U.S. Attorney General Sessions recuses himself from Russia investigations!

Hatimaye Mwanasheria Mkuu (AG) wa Serikali ya Donald Trump, Jeff Sessions, asalimu amri na kutangaza kujiweka kando (recuse himself) katika uchunguzi unaotarajiwa kufanyika kuhusu tuhuma za Urusi kuingilia mchakato wa uchaguzi wa Marekani. Kabla ya kutangaza uamuzi huo bosi wake, akijibu swali aliloulizwa, alisema bado ana imani kubwa naye na kwamba hakuwa na taarifa yoyote kuhusu mkutano wa AG wake na balozi wa Urusi. Je huu ndio mwisho au kuna zaidi? Tuzidi kuvuta subira...!
Kwa sehemu fulani amemuokoa bosi wake na pressure kutoka senate and house

Kwa upande mwingine, sasa amefungua 'Pandora's box'
1. Atakuwa subject wa investigation
2. Ataungana na Flynn kutengeneza 'team' iliyosemwa iliwasiliana na Russia
3. Media zitaendelea na curiosity kumhusu na Flynn
4. Uchunguzi wa Russia utapamba moto kwasababu umepata miguu

Kwa muda mambo yataonekana kupoa, mbele ya safari itakuwa tatizo
 
Kwa sehemu fulani amemuokoa bosi wake na pressure kutoka senate and house

Kwa upande mwingine, sasa amefungua 'Pandora's box'
1. Atakuwa subject wa investigation
2. Ataungana na Flynn kutengeneza 'team' iliyosemwa iliwasiliana na Russia
3. Media zitaendelea na curiosity kumhusu na Flynn
4. Uchunguzi wa Russia utapamba moto kwasababu umepata miguu

Kwa muda mambo yataonekana kupoa, mbele ya safari itakuwa tatizo
Haya mambo yanaendelea kuwa mambo...!

Breaking News: President's son-in-law, Jared Kushner also met with the Russian Ambassador!

03kushner-master768.jpg

Jared Kushner, Mr. Trump’s son-in-law and now a senior adviser, also participated in the meeting at Trump Tower with Mr. Flynn and Sergey I. Kislyak, the Russian ambassador. But among Mr. Trump’s inner circle, it is Mr. Flynn who appears to have been the main interlocutor with the Russian envoy — the two were in contact during the campaign and the transition, Mr. Kislyak and current and former American officials have said.
 
UPDATE

Kama mnavyosoma hapo juu , 'mkwe' wa Trump bw Jared aliyemuona Ivanka naye alikuwa na mikutano na balozi wa Russia ndani ya Trump tower.

Kuna maneno kadhaa muhimu hapo, kwanza ni mkutano ikizingatiwa kuwa Flynn na Sessions walikuwa nayo na balozi huyo wa Russia. Halafu kuna Trump tower kama eneo la mkutano.

Kisha Jared ambaye sasa ni mshauri wa Rais, na wakati huo akiwa confidant mkubwa katika kampeni

Swali linalozunguzuka, Ji Trump hakujua mawasiliano ya maafisa wa kampeni na Russia?

Kujitoa 'recuse' kutoka katika uchunguzi unaohusu Russia kumeleta hoja tuliyoijadili mapema jana
Kwamba, Dems watasema DOJ haiwezi kuwa huru ikiwa deputy ndiye anamchungumza Bosi Sessions

Hoja ya kuwa na 'independent special prosecutor' kuliangalia suala zima inazidi kupata nguvu
Dems wanahoja kuwa uchunguzi gani utafanyika ikiwa anyechunguzwa ana madaraka na yumo ndani?

Tatizo la Sessions si kukutana na Balozi, maseneta wengi wakiwemo wa Dems wanakutana na viongozi
Hoja ni wakati aliokutana na balozi wa Russia hasa baada ya kubainika kuna hacking inaendelea
Pili,imesemwa alikutana na balozi katika 'undisclosed place' ambayo definite waandishi wanaijua
Tatu, uhusika wa balozi wakati wa convention, kampeni na tranistions

Hivyo, utatu unazidi kuongezeka Mannorf, Flynn, Sessions, Gordon na Jared
Waandishi si kuwa wamemamaliza, midhali wamegusia Trump Tower tutasikia mengi

WH na Rep wanageukia Dems kwamba inafanya meddling katika suala hili.
Hoja inapoteza nguvu kutokana na kauli za mashambulizi za Trump dhidi ya media na intel community

Ukitazama, media zinapotoa taarifa zina uhakika wa kila detail iwe siku tarehe, muda mahali na nani alikuwepo nani hakuwepo. Hili ni katika kuepuka hoja ya fake news na kushikilia kijinga cha moto

Tazama timing ya habari hii, ilikuwa ni baada ya hotuba ya Trump katika congress

Na angalia timwili lingine lililozuka linalo mhusu Mike Pence (VP) na emails kama za Clinton

Mengi yanakuja na yata derail sana WH na mipango. Mkakati wa ku delegitimize media una backfire

Tusemezane
 
Hoja ya kuwa na 'independent special prosecutor' kuliangalia suala zima inazidi kupata nguvu
Huyo anayeitwa Independent Special Prosecutor, ISP, ndiye anawatia Republicans hofu na hivyo wanajaribu kumkwepa kwa kuing'ang'ania DOJ, Department of Justice, kuendesha uchunguzi. Kwa Sessions kujitoa, itabidi uchunguzi usimame hadi msaidizi wake aapishwe.

Tatizo la ISP ni kwamba anapewa nguvu zisizo na mpaka ikiwemo ya kumwita na kumhoji mtu yeyote ikiwa ni pamoja na Rais mwenyewe bila kuingiliwa na chombo chochote.

Wasiwasi wa Republicans ni Trump...hawajui atastahimili vipi kikaango cha hicho kamati. Hakuna longo longo wala mambo ya uongo uongo hapo la sivyo unajiongezea tu matatizo.
Dems wanahoja kuwa uchunguzi gani utafanyika ikiwa anyechunguzwa ana madaraka na yumo ndani?
Hofu ya Democrats ni uchunguzi kusimamiwa na DOJ, au mtu yeyote yule anayeteuliwa na Rais, hawaamini kama mtu huyo anaweza kuwa huru na ndiyo maana tayari wanamtaka Independent Special Prosecutor ndiye aongoze uchunguzi.
Mengi yanakuja na yata derail sana WH na mipango. Mkakati wa ku delegitimize media una backfire
Ikitokea uchunguzi ukawa mikononi mwa ISP hakutakuwa tena na namna na mipango ya WH lazima iwe derailed.
 
"Mag3, post: 19960916, member: 10873"]Independent Special Prosecutor, ISP, ndiye anawatia Republicans hofu wanajaribu kumkwepa kwa kuing'ang'ania Department of Justice, kuendesha uchunguzi. Kwa Sessions kujitoa, itabidi uchunguzi usimame hadi msaidizi wake aapishwe.
Hapa kuna kitu sijaelewa, Deputy ataapishwa kusimamia DOJ au uchunguzi peke yake na role ya Sessions katika DOJ itakuwaje

Republican hawataki kusikia ISP. Trump alisema suala la emails atatafuta ISP.
Hoja inazuka kwanini ilikuwa ''fair'' wakati huo na sasa ni ''unfair''
Tatizo la ISP ni kwamba anapewa nguvu zisizo na mpaka ikiwemo ya kumwita na kumhoji mtu yeyote ikiwa ni pamoja na Rais mwenyewe bila kuingiliwa na chombo chochote.
Hapo ndipo mtihani ulipo maana kila aliyekuwa na mkono ataitwa na kujieleza alishiriki vipi, alijua nini na kwa vipi
Hofu ya Democrats ni uchunguzi kusimamiwa na DOJ, au mtu yeyote yule anayeteuliwa na Rais, hawaamini kama mtu huyo anaweza kuwa huru na ndiyo maana tayari wanamtaka ISP aongoze uchunguzi.Ikitokea uchunguzi ukawa mikononi mwa ISP hakutakuwa tena na namna WH lazima iwe derailed
Kuna pande kadhaa katika hili

WH hawakuta Flynn ajiuzulu, kilichpelekea wakubali ni kauli za VP Pence kumtetea

Kwa maana kuwa kama angeliitwa kuhojiwa VP angeweza kuwa shahidi kwa utetezi lakini pia credibility ya VP ilikuwa katika majaribu makubwa. Hawakuwa na njia bali kukubali

Kukubali kujiuzulu kunaondoa 'executive privilege' .
Kwa exec privilege anaweza kuitwa na kamati na kula kiapo na usiseme lolote, inakubalika

Kwasasa hana hiyo na ni vulnerable katika kuitwa popote

Ndivyo ilivyo kwa Sessions, kwamba ame recuse ili ku maintain exec privilege
Democrats wameliona hilo

Upande wa Dems, wanajua advantage ya sessions akiwa sec wa DOJ na exec privilege

Wanataka ajiuzulu ili naye awe kama Flynn wakiweza kuitwa na kuhojiwa

Tatizo,nafasi ya Sessions ni ya kuteuliwa hakuna shinikizo linaloweza kumuondoa

Kumwacha abaki DOJ akiwa na recuse uchunguzi utakuwa na influence yake

Democrats hawamwamini Comey kwani amekwenda Capitol hill mara 3 na zote anaonekana kutaka kuzima suala zima.

Ukizingatia ya nyuma na alivyo handle emails za Clinton, Democrat wanaona ISP ndiyo njia

Sehemu ya tatu ni Intel community:
Republican wanataka suala liwe handled na IC.

Wanajua ukweli unaweza kujulikana lakini habari zote ni classified na inaweza kuchukua miaka 20 kuwekwa mbele ya public. Hapo Trump atakuwa amepeta

Democrats wanaliona hilo ndiyo maana hawataki njia hiyo isipokuwa ISP

Equation inakuwa complicated kwa ukweli kuwa kuna kamati ya bunge, kuna IC, kuna media na kunaweza kutokea independent investigations nyingine na ku reveal jambo

Suala litafunikwa vipi au litabumbuliwa vipi ni la muda na ''drip drip 'zinazoendelea
 
WIKI HII KATIKA SIASA ZA US

Sakata la Russia linaendelea kuchukua habari na kufunika kila kinachoeandelea WH

Orodha ya 'watuhumiwa' inaongezeka, habari ikiwa ndani ya Tower
Kwa kiasi imeshagusa nyumba nyeupe kwa 'mkwe' kutajwa katika wahusika

VP pence kakutana na nguvu ya media baada ya kubainika alitumia email binafsi katika mawasiliano ya ofisi. Email ilikuwa hacked na habari zipo zikisubiri muda

Mambo mawili, kwanza, matumizi ya email binafsi kwa sheria za Jimbo la Wisconsin alipokuwa gavana inaruhusiwa. Kilichotakiwa ni kutoa emails hizo wakati anaachia ngazi

Tofauti na Hillary Clinton, Pence hakutumia server binafsi bali email account binafsi
Pence alikuwa mstari wa mbele kumlaani HRC kwa kuweka usalama hatarini akiwa SOS

Ingawa hakuna ulinganifu kwa maana ya email, server na nyadhifa, jambo moja linafanana,wote wawili walizembea na kuweka maeneo katika hali tata kiuslama

Katika suala la Russia, juzi tulisema Trump admin itatupa jambo ili kufanya distractions

WH ilijaribu kutumbukiza suala la information zilizopatikana katika shambulio la Yemen. Media zimeshang'amua janja na suala halikupewa uzito zaidi ya Russia

Katika kuhakkisha habari ya Russia inafifia asubuhi ya Jumamosi Trump ka tweet jambo
Anasema Obama aliweka ving'amuzi Trump tower ili kubaini mawasiliano yake

Hizi ni tuhuma nzito ambazo msemaji wa Obama amezikanusha vikali
Seneta Lindsey Grahm naye kasema ikiwa ni kweli basi akiwa seneta atafutailia

Jambo la kushtua, maafisa wa WH hawakuwa na habari kama 'mzee' ata tweet
Hakuna uhakika kama Obama alifanya au hakufanya hadi habari zitakapoendelea kujiri

Kuna mambo ya kujiuliza kidogo kuhusu hili jambo wakati tukisubiri habari zaidi

1. Timing ya tweet haina tofauti na zingine zilizokuwa na lengo la distrations kubadili maongezi
2. Akiwa Rais na vyombo vyote Trump alitakiwa kuja na ushahidi au kuagiza uchunguzi na si tweet
3. Kuna madai ya wapiga kura milioni 3-5 ambayo hadi leo hajayatolea ushahidi wowote
4. Habari za Attack sweden zlizipata katika media, hizi za wire tap amezipata Breitbart ya Bannon

Sheria za US zinasema Rais hawezi kuruhusu wire tap isipokuwa FBI kwa taratibu za kisheria

Suala la Russia linaitafuna sana WH, kukiwa na jitihada za kulisukuma.
Tatizo ni kuwa tayari kuna media ambao ana mgogoro nao, kuna Intel comm na Congress
Katika mazingira hayo Russia itaendelea kwa muda mrefu

Tusemezane
 
Trump katika kutapatapa sasa anamtuhumu mtangulizi wake Obama kwa kufanya udukuzi kwenye jengo lake la trump tower wakati wa kampeni, lakini kama kawaida hajatoa ushahidi wowote zaidi ya kutuhumu tu ndani ya twiter.
 
Nguruvi3 na Mag3 kwa mfano mambo haya yakiselelea mpaka kwenye Impeachment ya Trump je Dems wapo tayari kuzihimili athari zake? Na kwenye uchaguzi ujao nafasi ya Dems itaongezeka ama ndiyo itapotea kabisa?
 
Back
Top Bottom