Taarifa zilizopo Trump alimtuma WH counselor Don Mcgahn kumuagiza AG amfukuze Mueller. Don alikataa, hakuona sababu na anajua nini kilitokea kwa Nixon
Hizo ni taarifa kutoka anonymous source.
Njia inayotumika kwasasa ni kama ya kumuondoa Andrew McCabe kwanza
Anayefuata ni Roseinstein ambaye ni deputy AG anayemsimamia Mueller
Kwanini McCabe anaondolewa siku moja baada ya Wray (Director FBI) kwenda Capital Hill na kuona kilichomo ndani ya memo? Kama Roseintain anahusika na matumizi ya kisiasa ya vyombo vya usalama kwanini asiondolewe? Au ukishakuwa Deputy AG ndio huwezi kupatikana na hatia?
Huyu McCabe anayetetewa hapa ndiye aliwaagiza maafisa wa FBI kutochunguza Foundation ya Hillary Clinton. Mke wake alipokea $700,000 kutoka kwa Super Pac ya Hillary. Halafu bado DOJ ya Obama ilimuweka kama mmoja wa wachunguzi wa Hillary kwenye sakata ya e-mail za Hillary, wala hakuji-recuse. Si ajabu Hillary alikuwa exonerated hata kabla ya kufanyiwa interview na FBI!!
Hayo yanafanyika kwasababu mbinu za kum 'frustrate' Sessions ajiuzulu zimeshindikana
Kumuondoa Roseinstein kutawezesha kumteua mtu 'loyal' atakayemfukuza Mueller
Mueller kama ataondolewa sio kwa sababu mtu loyal kwa Trump ameteuliwa kuwa Deputy AG, hapana! Ni kwa sababu huyu mtu ana 'conflict of interest' zilizo so clear ambazo zinamfanya asiwe mtu sahihi kufanya huo uchunguzi anaoufanya kwa sababu ya biasness.
Kuanzia sasa utasikia Roseinstein akiandamwa na tayari kuna 'memo' iliyoandikwa na Republican ambayo Nunes ameridhia itolewe hadharani.
Kwanini Democrats wote walio kwenye House Intel. Committee walikataa hiyo memo isitolewe hadharani? Umemsikiliza Rep. Adam Schiff (Top dem kwenye House Intel committee) sababu alizotoa kuhusiana na hiyo memo-release iliyoidhinishwa na House Intel Committee?
Kwani kuna wasiwasi gani ikitolewa hadharani?
Roseintain ndiye aliye approve FISA warrant kwa ajili ya kum-spy Carter Page.
Roseintain kama alitumika vibaya kisisasa dhidi ya Trump na team yake kwanini asiandamwe?
Mchakato mzima una ukakasi wame 'cherry pick' page 4 kutoka katika lundo la pages
Kwanini wanafanya hivyo? Ni kuonyesha FBI ni biased katika FAISAL warrant iliyomweka Carter page matatani
Kama wana-cherry pick kurasa nne umesikia Democrat (Senator au Representative) akisema zitolewe hizo lundo zote? Hata hizo chache zenyewe hawataki zitoke.
Biasness ya FBI inakuja baada ya FBI kupotosha Mahakama ya Foreign Intelligence Surveillance Act (FISA) kwa kutotoa taarifa kuwa ushahidi waliotumia kudai FISA warrant kwa Carter Page ulitokana na dossier za Steele (aliyepewa kazi na Fusion GPS ambao nao walipewa kazi na chama cha Democrat kuchunguza uhusiano wa Trump na Russia).
Haya mambo ya vyombo vya ulinzi na usalama kutumika kisiasa wenzetu hawajazoea, haya mambo yapo sana nchi za dunia ya tatu. Rais Obama alitumia kila njia kumzuia Trump kuingia ikulu, DOJ na FBI ilitumika sana kisiasa. Na Obama ana historia hiyo toka kipindi IRS (Internal Revenue Service) walipotumika ku-target conservatives.
Hilo litajenga uwezo wa mambo mawili.
Kwanza, public iamini kuna tatizo katika uchunguzi mzima wa Mueller
Pili, kutoa mwanya wa kumfukuza Mueller
Hapa sio suala la Public kuamini, hapa ni suala la Public kuchunguza Facts halafu waone nani anastahili kuwajibishwa.
Kama Je, ni wale wa Trump-Russia collusion (hoax) au ni wale waliotumia madaraka yao na vyombo vya usalama na taasisi za nchi kisiasa?
Hii itatupa picha kamili hasa kinachochunguzwa na Mueller, kama ni kitu ambacho kimetengenezwa au sio, na kama kimetengenezwa kunakuwa hakuna haja ya kuendelea na uchunguzi hewa chini ya Mueller badala yake wahusika wa hoax wanawajibishwa.
Hata hivyo, hiyo ni miscalculation. FBI wamesema hakuna tatizo katika memo
Director wa FBI, Christopher Wray alitoka Capital Hill kuchunguza kilichomo kwenye Memo, masaa machache baadae Deputy Director wake Andrew McCabe anaondolewa. Hapo unasemaje FBI wamesema hakuna tatizo?
Nunes amekataa kushirikisha vyombo vingine kwasababu issue nzima itakuwa Debunked
Memo itakuwa de-classified kila mtu ataweza kuona ina nini ndani yake. Rais Trump anayo siku tano (5) kutoa approval ya kuachia memo hadharani. Nadhani isingekuwa 'State of the Union' angeiachia hata leo.
Hofu iliyopo sasa hivi inatengenezwa na vitu viwili au vitatu.
Kwanza, kuna kila dalili ya Obstruction of justice kama ilivyotokea kwa Comey
Bahati mbaya Trump alithibitisha kumfukuza Comey kwa Russia
Ikishathibitika kuwa uchunguzi wa Trump-Russia collusion ni hoax na ilitengenezwa kisisasa, kunakuwa hamna hicho kinachoitwa 'obstruction of justice' kwa Trump. Hiyo memo inasemekana kuna watu wengi humo walitumika kisiasa dhidi ya Trump, Comey mwenyewe, McCabe, Roseinstein n.k. Kwa kifupi uchunguzi utafungwa rasmi na waliotumika kisiasa watawajibishwa.
Pili, washirika akina Flynn wanashirikiana na FBI. Kitendo cha wanasheria wa Flyyn kuwaandika wa Trump kwamba wamekata mawasiliano kina maana ana cooperate na FBI
Mkuu, hivi kweli unadhani washirika wa Flynn na Trump hawawasiliani?
Tatu, idadi ya wanaotoa ushirikiano FBI ni kubwa wakiwemo maafisa wa WH na kampeni. Trump na wanasheria wake hawaelewi hao wanaotoa ushirikiano wanaeleza nini. Wakati huo huo Mueller anaelekea kumhoji Trump 'deposition'
Big news hapa ni kuwa uchunguzi wa Mueller ni hoax. Wakati unawaza 'deposition' ya Trump inabidi uangalie Facts tu mpaka hapa tulipofikia.
Democrats wengi tu wanasema hamna evidence ya Russia collusion. Of course, then wakarukia 'obstruction of justice' ambako nako wanaona giza, sahivi wanazungumzia tax returns na 'money laundering'. I hope huu uchunguzi feki utasitishwa ili kuokoa fedha za walipa kodi zinazoenda bure.
Kuna mswada unaandaliwa ili kumlinda Mueller asifukuzwe na Trump.
Kama mswada huo utapita basi hakutakuwa na namna bali kusubiri matokeo
Hata kama huo muswada utapita kama Democrats wanavyotaka, kama Mueller anafanya uchunguzi hewa haitamsaidia maana hakutakuwa na haja ya kumzuia 'asifukuzwe na Trump' kwa sababu kutakuwa hakuna uchunguzi.
Kosa linalofanyika la kuwatimua akina Comey na McCabe litavujisha habari nyingi
Unachokiona ni 'obstruction of justice' peke yake katika suala zima la Comey na McCabe kuondolewa? Hauoni mengine? Ila nadhani baada ya memo kuwekwa hadharani utaweza kuona mengine.
Swahiba wake Steve Banno alieleza hili katika mahojiano juu ya Comey
Steve Bannon leo ni credible source kwa liberals? Unafiki hauwezi kuisha! Kwa kumponda kote huko kabla hata hajateuliewa kuwa WH Chief Strategist, leo hii anaonekana mtu wa maana? Ama kweli adui wa adui yako ni rafiki yako!
Katika wiki au mwezi utasikia media zikiwa na breaking news, subiri
Breaking News zitatokana na ukweli kwamba uchunguzi wa Mueller ni hoax na watu watajiuzulu wengi tu, Andrew McCabe kaanza wengi tu watamfuata. Ila mwishowe atakaeumbuka kuliko wote ni Rais mstaafu Obama.
Trump ana hofu si kwa Russia investigation. Pengine hakuna ushirika kati yake na Russia wenye uhalifu 'conspiracy' ingawa ushahidi wa collusion wanasheria wanasema si 'crime'
Ohh kumbe sasa hivi kuna uwezekano 'hakuna ushirika kati ya Trump na Russia na ushahidi wa collussion si crime'? Hii kauli inatoka kwa waliobebea bango suala zima la Trump-Russia collusion toka lilipoanza!!
Mlianza na Russia wali-hack vifaa vya uchaguzi katika majimbo ya Wisconsin, Michigan and Pennsylvania, mkatoka kapa. Leo Russia Collusion ishaonekana chenga, mmerukia wapi sasa?
Kuna hofu ya obstruction of justice, kauli na tweet za Trump zinaipa hoja nguvu
Ile draft ndani ya Air force one kuhusu Don Jnr na utata wa mkutano Trump Tower ni sehemu tu
Mmerukia 'obstruction of justice'. Kimsingi, hivi sio vitu viwili tofauti, kwa sababu hiyo justice inayodhaniwa kuwa imekuwa obstructed inatokana na investigation ambayo ishaonekana chenga!! Swali la msingi ni kuwa Trump anawezaje ku-obstruct justice kwa kitu ambacho kimetengenezwa?
Kuna hofu ya money laundering ambayo inaweza kuibua deal za Trump ikiwemo uhusiano wa investment zake Russia, tax return n.k.
Mmerukia na huku kwenye 'money laundering na tax returns'? Ama kweli Trump anatafutiwa kosa lolote sasa!! Hii yote kisa Hillary (mwanasiasa mzoefu) alishindwa uchaguzi na mtu ambaye hajawahi kufanya kazi serikalini na akalia machozi!
Je, mkimkosa huko kwenye money laundering na tax return, mtarukia wapi? Au popote tu ili mradi uchunguzi uwepo?
Steve Bannon katika kitabu cha fire and fury alieleza kuhusu Don Jr atakavyokaangwa kama mayai. Banno anaelewa jambo gani kuhusu pesa?
Unawezaje kutumia kitabu cha 'white Supremacist' kama Steve Bannon kutetea hoja yako? Ukizingatia kitabu chenyewe kiliandikwa na Michael Wolff ambaye Democrats wengi tu akiwemo Obama walimponda na kum-discredit?
Pamoja na hayo bado kuna makosa ya kifundi, kwa mfano, vikwazo dhidi ya Russia vilivyopitishwa na congress kwa wingi,Trump amekataa kuvitekeleza. Ndipo maswali yanakuja, ni kwanini amekuwa laini kwa Russia? Kuna quid pro quo?
The last time Rais Obama alikuwa soft kwa Russia alikutana na Republicans na Democrats waliomuambia hayupo strong kwa Russia. The same way Rais Trump anakutana na Congress inayomuambia yale yale. Swali ni Je, kipindi Obama alivyokuwa analalamikiwa kuwa yupo weak kwa Russia kulikuwa na quid pro quo?
Bado hujagundua kuwa suala la Russia linatumika sana kisiasa US?
Kitu kikipitishwa na Congress kwa wingi hakimaanishi kuwa Rais naye anatakiwa kukipitisha bila kukiangalia kwa undani kwa mda wake!! Ndio maana Rais ana uwezo wa ku-veto au kukataa kutekeleza jambo.
Kudharau maamuzi ya congress kunaweka wakati mgumu wa kumfukuza Mueller
Moderate Republican wanaungana na Dems kuiona dharau na shaka ya uswahiba na Russia
Mueller hatafukuzwa na Trump, ajajifukuzisha mwenyewe, itakapobainishwa hadharani kuwa anachunguza hoax au hafai kufanya uchunguzi dhidi ya Trump.
Wakati Trump akiwa moto kwa North Korea, wiki hii meli za Russia zimezengea fukwe za US Trump akiwa kimya. Yote ukiyaweka katika kapu yanpunguza kuungwa kwake mkono
Yaleyale, 'anatakiwa awe strong kwa Russia'. Obama aliimbiwa sana huu wimbo mwanzoni mwa utawala wake. Hivi kwani Russia nao wamesema wanataka kushambulia US?
Hizo habari za Meli za Russia zimetoka Pentagon na State Dept walisha-respond. The same way leo Ndege ya Russia imekaribia ndege ya Navy ya US futi tano juu ya Black Sea kwenye anga za kimataifa na State Dept wametoa onyo. Kesho unaweza kusikia manowari ya US imekaribia Crimea then Russia wanatoa onyo. Russia hawezi kushambulia US.
Rais Trump hayupo kimya, anaandaa State of the Union atakayoitoa leo.
Moderate Rep wanaondoka kambi ya Trump taratibu kutokana na mtiririko wa matukio
Moderate Republicans wamesaidia kupitishwa kwa bill ya mabadiliko ya kodi, na wapo pamoja na Trump kwenye Immigration reform proposal ambayo Trump ameweka mezani. Pia kuna Democrats wanaenda kwenye mid election mwaka huu, wengi wao wanatiririka kwa Trump.
Salama ni kumfukuza Mueller, investigation ikiisha hasa ya Mueller itaibu japo jambo
Ili kumfukuza Mueller lazima dept of justice ihusike, bila kumuondoa Roseintein, ni ngumu
Mueller atajiondoa mwenyewe kwenye huu uchunguzi wala hamna atakayemuondoa. Roseinstein naye atajipima then atafanya maamuzi sahihi, ambapo anaweza kujiondoa pia.
Suala la matumizi ya vyombo vya ulinzi na usalama kisiasa ni suala ambalo linapaswa kukemewa na watu wote wanaopenda demokrasia na haki. Hasa pale ambapo chama tawala kinafanya hivyo dhidi ya chama cha upinzani kama ambavyo Obama (Democrat) alivyofanya kwa Trump (Republican) ili kujaribu kumsaidia Hillary kushinda uchaguzi.